The Chant of Savant

Wednesday 21 March 2012

Mpayukaji alizwa hotelini akitanua na totos



Najua wengi hapa wameishaanza kupiga ramli kuwa huenda naongelea maeneo ya Beverly hills au New York kwa matajiri. Kwa waliowahi kuishi New York watakuwa wanajua maeneo kama Westbury, Brigdehampton, Sands Point na kwingineko ambako wenye nazo ima huishi au kwenda kutanua hata kwa kufanya mambo ya kipuuzi.
Pia wapo wanaodhani kuwa napanga kwenda kwa walevi wa Bongosalama kuwashitakia walioniibia kama siyo kutafuta kuhurumiwa kwa uzembe na sababu ya kweli iliyosababisha nilizwe. Mmenoa! Sikuibiwa New York wala siandiki kuomba kukutana na waze sorry walevi wa Dalasalama.
Mwenzenu juzi nilitinga kule Ngorongoro kwenye hoteli ambayo jina lake siri yangu kutanua na dogodogoz baada ya kumuacha bi mkubwa solemba. Baada ya kuwa amenichosha kutokana na kunenepeana ukiachia mbali kuwa bize kutumia nafasi yangu kutafuta ulaji binafsi yeye na ndugu zake, nilijihisi kumchoka. Hivyo, niliamua kutafuta vidosho lau nijiburudishe. Niliamua kwenda kufanyia ufuska wangu sehemu iliyojificha ili asininase. Nilijua nimepata kumbe sikujua nilikuwa nimepatikana. Nilijiona bonge ya mjanja nisijue mwisho wa yote nitaonekana fala haswa! Uliwahi kusikia stori ya paka mrembo yaani mama anayerembua mimacho kama hururaini la jamaa zangu fulani?
Baada ya kutinga zangu Ngorongoro nikijifanya nilikuwa kule kikazi, niliingia mitaani kuwasaka ndogondogoz bila kujua ni hatari. Ama kweli yule jamaa aliyeimba kuwa ndogondogo kwa pesa ni hatari hakukosea hasa mwenye kuwa nazo anapokuwa kigogo kama mimi. Hivyo basi, baada ya kutega nyavu zangu na kunasa kidosho cheupe, tuliamua kwenda zetu chumbani kwangu kujivinjari. Tulijivinjari kweli kweli hadi nikachoka sana. Kabla ya kulala tulipata kanywaji ili kuamsha mwenembago. Kumbe kale kanywaji kalikuwa kamewekewa bwimbwi kiasi cha kunifanya nilale kama kichanga. nilipokuwa nakoroma kama gogo, si dogodogo aliamka na kusanya kila nilichokuwa nacho kuanzia laptop zangu nne, dolari 80,000 nilizokuwa nimehongwa na jamaa waliotaka niwape tenda ya kusambaza kahawa kijiweni, madafu 20,000,000 ambayo yalitokana na msaada wa shirika moja ambalo sitaki kulitaja na hata god father yangu yaani pupi yangu. Nilipokagua vitu vyangu nilikuwa kuwa briefcases mbili zimekwenda, Sanduku la silaha ya kujikinga na umeme au kondoo muu nalo limekwenda. Inaonekana huyu manzi hataki kufa kwa miwaya. Yaani anaondoka hata zana zangu ili nisiwanonihino wengine siyo?

 
God father imekwenda, suruali, viatu, saa hata leso yangu vyote vimekwenda. Changu huyu alijua kukomba usiambiwe! Yote tisa. Hivi bi mkubwa akiipata naye si ataamua kunikomoa kama hana akili nzuri? Maana kwa mfumo dume huu tumekuwa kama vipofu bila kuangalia upande wa pili. hivi bi wakubwa zetu wakiamua kulipiza kisasi kuna mtu atapona kweli?

Baada ya kugutuka na kujikuta mimi na mashuka ya hoteli, nilipigwa na butwaa huku nikihisi kuchanganyikiwa jinsi nitakavyotengeneza stori ya kusadikika kwa ndata. Unadhani bila kutengeneza stori bi mkubwa angenielewa? Laiti angejua kilichosababisha nikwapuliwe wala asingehangaika kunionea huruma bali kunikomoa. Kwa vile wakubwa huwa hawaadhiriki, ilinibidi nicheze chess na ndata wambambikizie mzoba mmoja kesi ili kuninusuru. Unacheza na uzito nini?



 
Unaweza kuamini kuwa kama changu aliyeniliza angekuwa jambazi ningefungwa? Maana wakati akinisanya, nilikuwa kulikuwa na bastola niliyokuwa nimeazima kwa jamaa yangu ili kujilinda. Pia kulikuwa na SMG kali sana. Hamna haja ya kuanza kupiga ramli tena. Kinachoitwa SMG siyo bali jambia la kimasai. Hata hiyo bastola si ya kweli bali toy lake. Hayo tuyaache. Maana nisingeweza kuwa na bastola hata kama siku hizi ni ruksa kuzinunua na kuzitumia utakavyo kama brother Dittope. Kwa mtu kama mimi SMG la nini wakati mimi si jambazi? Hii imenikumbusha rafiki yangu mzee Headguard Makorora Majogoo aliyesafiri na gobole lake toka Bongo hadi ugabacholini bila kustukiwa. Walijisemea wahenga. Unaweza kumtoa mtu porini lakini huwezi kutoa pori kichwani mwake. sasa mzito mzima na misilaha ya kivita ya nini? tena hali inakuwa mbaya unapokuwa umebeba midude kama ile halafu ukajiingiza kwenye uchangudoa na uhuni kama ilivyotokea. Licha ya kunitokea mimi, imetokea wapi? Nachema chichemi njomba.
Pia mabingwa wa udaku nawashauri na kuwaonya wasihusishe kisa changu na cha yule kijogoo mwana wa Milima ya Kigoma aitwaye jina mumewe Eva. Yeye aliafanya uhuni watoto wa mjini wakamuingiza mjini kikweli kweli. Kwanza mzito na SMG wapi na wapi kama siyo ulimbukeni na ushanba? Wazito wanalindwa na bodigadi. Mi-SMG na mibastola ya nini kama siyo kuwa na kazi zaidi ya moja? Maana bila kuwa na shughuli za siri mtu wa aina yake asingeweza kujizungushia mizana mizito mizito kama Osama bin Laana.

 
 
Turejee kwenye kisa changu. Kwa vile huyu changu aliyeniibia amejifanya mjanja, basi ajue amejiharibia yeye na vyangu wote wa kaya hii. Maana mwakani nitakapogombea uzito na kuupata nitakuwa sichukui vyangu wanuka jasho wa kaya hii. Badala yake nitakuwa nachukua vikinda vya shule au chuo na kwenda kutanua navyo majuu ambako siwezi kugutukiwa wala kuibiwa. Ikizidi nitakuwa nachukua vyangu wa kizungu badala ya hivi vya Kiswahili ambavyo vina shughuli zaidi ya moja; yaani uchangu na ujambazi. Kuanzia leo natangaza rasmi. Changudoa yeyote atakayepita mbele yangu naramba shaba au njaramba. Sina mchezo tena. Machangudoa wote wawe wa kisiasa au kingono washindwe na kunyong’onyea. Na shetani aliyenishwawishi nikalala na changu akaniibia naye ashindwe pamoja na changudoa wake.
Hivi hii ni kweli? Nimeinyaka kuwa tangu jamaa alizwe kule kwenye mji karibu na bahari, vyangu sasa wanaipata fresh hasa pale ndata wanapowasanya kulipiza kisasi kwa kuingizwa mjini bwana wao. kuna mbea amenipa stori kuwa ndata nao wana lao. Maana wakiwakamata machangu huwatoa mchicha hata huduma ya chap chap. Jamani, miwaya itatumaliza hata tukijizungushia mipisto na miesmjii.
Chanzo: Tanzania Daima Machi 21, 2012.

5 comments:

Malkiory Matiya said...

Duh! hii kali. Je ni mji karibu na bahari au mji kasoro bahari kama wasemavyo wenye? kama ni mji kasoro bahari basi ujumbe umefika.....

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Bwana Malkiory umeanza nawe! Hapa ni mji ndani ya bahari ya milima. Upo hapo mshirika? Kazi kwao sisi tumemaliza.

Malkiory Matiya said...

Duh! nimeambulia surface meaning tu, lakini hidden meaning pengine inagusia moja kwa moja tukio la hivi karibuni la kule mji kasaro bahari.

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Yote bado ni maana hujakosea.

Anonymous said...

Kaaz kwer kwer!