The Chant of Savant

Tuesday 11 December 2012

Bush akamatwa visiwa vya Cayman

Waziri mkuu wa visiwa vya Cayman McKeeva Bush amekamatwa kutokana na tuhuma za ufisadi. Pamoja na visiwa hivi kuwa pepo ya wakwepa kodi bado havikubali ufisadi! Bush aliingia madarakani mwaka 2009. Je tunajifunza nini watanzania? Kwa blogu hii ni kwamba hata kama unaweza kuruhusu wenzio waibe pesa zao kwao wawekeze kwako kwa sababu ya upumbavu wao, hutaruhusu kujiibia wewe mwenyewe. Kwa habari zaidi GONGA hapa.

No comments: