The Chant of Savant

Friday 1 April 2016

Bongo: Shamba la bibi au la bangi?


            Kasheshe iliyotokea hivi karibuni kule kwa akina Omushuma aramu mushaija iwe nogambaki omuzira nkende Rwabunonihino na Rweyependekeza kama anavyopenda kuwasanifu John Kanywaji Makufuli, ilimuacha mlevi hoi pamoja na mibangi na ulabu wake. Wakati akitafakari jinsi kaya ilivyogeuzwa shamba la bibi kama Dk Kanywajia alivyofichua hivi karibuni, sikujua! Kumbe nalanguliwa bangi hapa Bongo wakati naweza kutia timu KG na kuondoka na magunia! LOL! Acha nijiandae kutia timu kule nije na zana tena za kutgengenezea uchache wa chapchap hasa usawa huu ambapo lisirikali limewagwaya wauza bwimbwi.
            Sikujua kaya hii ni smart kiasi cha kuruhusu uwekezaji kwenye uzalishaji mihadarati baada ya kugundua kuwa akina IpTL bin Escrow wanapiga dili na kuondoka wakiiacha kaya apeche alolo! Sasa nimejua. Lile dili la kwenda Moro kwa Mkude kusaka mijusi au kwenda Selous kuua tembo naachana nalo. Lazima niende zangu kwa akina mulangila nizoe ganja na kuja kuwalangua wakuda hapa Bongo.
             Najua, mwanzoni akina Ben Nkapa walikunya nkojo ya uwekezaji hasa kwenye uchimbuaji madini wasijue wataachwa Solemba baada ya kuwa mbwi na kuachia ulaji wakibaki kutegemea huruma ya warithi wao wasifichue vi-Kiwira vyao. Waliigeuza Bongo No-Man’s land wakati Mwinyi akiigeuza kichwa cha chizi na Njaa Kaya chaka la mafisadi. Hivyo, akina Njaa Kaya waliona wawekeze kwenye uzalishaji wa mibangi ili kupata njuluku ya haraka! Ama kweli usilolijua ni sawa na usiku wa giza!  Nani angeamini: kaya inayojiita kisiwa cha amani iruhusu uzalishaji mibangi tena ukifanywa na wakimbizi na wahalifu wengi wakikimbia mauaji ya halaiki kule Ruanda? Nashauri watuhumiwa watumwe kwa Po Kagame kuhakiki kama hawana tuhuma za mauaji ya halaiki.
            Mwenzenu nilikuwa najua Bongo ni shamba la bibi kwa akina absiii na kalu na wachukuaji waitwao wawekezaji kuja kupiga dili na kuondoka na madini huku wachainizi wakiondoka na vipusa na nyara zetu huku tukiwekeza kwenye kubomu nje, kondomu, baa, short time guest houses, dini na upuuzi mwingine. Kumbe kuna wajanja zaidi kama Escobar wa Kolombia wanaokuza na kusepa na mibangi na miunga wakati sisi tukiendelea kushangaa shangaa kama hamnazo? Sijui Dk Kanywaji hili atalibebea mbeleko gani yarabi kwa aibu na hasira.
            Hata hivyo, kuna kipindi nilistuka hasa pale jamaa yangu Madabidabi alipotuhumiwa kujihusisha na biashara haramu ya mihadarati lakini Chama chake cha Mafisi na Mafisadi (CCMM) kikamkingia kifua huku akina Njaa Kaya wakijifanya hawakuwa wakiinyaka. Mie nilijua kuwa mchezo ungeishia kwenye kutoa matishio kuwa wanene wana orodha ya wauza mibwimbwi lakini hawakuona haja ya kuwapelekea kwa pilato wala kuwatupa lupango washikaji na washitiri wao wa kisiasa, kumbe wenzetu walishaanzisha mashamba ya bangi kando yam to Kagera huku wakimwagilia kama hawana akili nzuri!
            Kwa vile mimi ni mteja wa bange, lazima nifanye kila hali nihamie Kagera lau niwe napata kaya na lupisi na ile kitu roho inataka na kutononoka. Nikihamia kule lazima ninenepe. Maana nikishatua lazima nimtamfute Kokugonza anichambue kama karanga baada ya kuchambua mibangi na kanywaji kangu. Kama haitoshi, lazima nimtafute brother Jimmy Rugemalayer anikatie mshiko wa Escrow ili nikimaliza kutenda madhambi yangu niende kwa Faza Kisoft bin Laini anisamehe madhambi yangu kabla sijafunga safwari kwenda kwa Porofwedha Anae Tamaa Kajuamlo Tiba anipe tiba na kunifundisha jinsi ya kuji-defend ovu course befwore ze government thinking of akichuari teikingi mi to the pilato.
            Nikimaliza kufanya yote haya ikatokea ndata wakaninyaka, lazima niende kwa advocate Rutagatina ili anitetee kama ndata watanifungulia kesi au vipi?
            Nikihamia Kagera lazima nifwaidimo maisha bwana. Nikishapata tubangi na tunywaji lazima nipate nyama choma itokanayo na nyama ya ng’ombe aina ya ankole wanaovuka mpaka toka kwa jamaa yangu Kaguta na Kagame kuja kulishwa na kunenepeshwa kwenye shamba la bibi na la bangi au vipi? Lazima hapa niwaalike marafiki zangu akina Muchimbazo, Rwakatongo na Rwakanonihino waje tupate ile kitu roho inataka huku tukisindikizwa na akina Koku na Saida kama siyo Kayitesi na Nyininka toka UG na RD au vipi?
            Kabla ya kwenda KG lazima nipite Chato nikapate tafu toka kwa sista yangu Njile na Ndebile ndipo nipige zangu kwenda kupata ganja na rubisi na kimpumu. Nikitoka pale lazima nipite Mwibara kwa akina Nchagwa na Matiko lau wanipe tafu twende zetu kwa wanchari na warenchoka ili kuonja bangi lao kabla halijasepa kwenda kaya ya nyayo ambapo rahis wao UK alisema wana taaluma ya kukwapua.  Hapa ndugu zangu Waikoma, Wangoreme, Wanata na Waisenye hamtataka niwape tafu kuwabonda Watimbaru, Wanyabasi na Wakira. Nikiona noma lazima nivuke mpaka nizame zangu Nyariba Chake au Kitutu Masaba ili nikapate musima na musiri na omugusii Nyandusi na kufaidi musiki wa Ong’eng’o na Sungusia.  Lasima to toboe hapa na entururu kama siyo Ingochande beka ekapeti.
Lo! Kumbe ni mibangi! Wasubati wa Kuruya, Kentare, Kemambo na Kumasuka mpo!
Chanzo: Nipashe, Aprili 2, 2016.

No comments: