The Chant of Savant

Tuesday 18 October 2016

Soma wasfu wa Massaburi ugundue alivyoghushi udaktari

Ufuatao ni wasfu wa marehemu Didas Massaburi ambaye wengi tulimjua kama mission town lakini si Daktari pamoja na rafiki na mshirika wake Makongoro Mahanga. Wanaomjua, hakuwahi kuwa na hata shahada moja ya chuo. Ajabu alipokwenda Uingereza kufanya  Diplama ya ugavi akarejea akijiita Daktari na watanzania wakaendelea kuamini alikuwa daktari wakati ni kilaza. Wanasema wahenga, mficha maradhi, kilio kitamfichua. Hapa chini ni wasfu wa Masaburi kama ulivyosoma na mdogo wake. Je Tanzania inao akina Masaburi wangapi wanaongojea kifo kifichue ukilaza na ukihiyo wao?


WASIFU WA MAREHEMU
Dk. Masaburi alizaliwa Machi 24 mwaka 1960 na alisoma Shule ya Msingi Nseke iliyopo Serengeti na mwaka 1978 alijiunga na Sekondari ya Wavulana ya Tabora na kuhitimu mwaka 1981.
Mwaka 1982 Dk. Masaburi alijiunga na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) na kuhitimu mwaka 1985 na kupata cheti cha ufundi wa magari.
Mwaka 1985-1990 alichukua mafunzo ya ugavi na kupata Shahada ya Ununuzi na Ugavi kutoka  Bodi ya Ugavi wakati huohuo akichukua mafunzo ya ununuzi na ugavi nchini Uingereza Chuo cha Chartered Institute of Purchasing and Supply ambapo alitunikiwa cheti cha Diploma ya juu ya Ununuzi na Ughavi mwaka 1988.

No comments: