The Chant of Savant

Saturday 25 February 2017

Hapa sijui nani anachanganya dini na siasa

Hakuna ubishi kuwa ndoa ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam na baadhi ya madhehebu ya dini inogile kiasi cha kutoonekana bughudha ya kuchanganya dini na siasa. Sijui nani anamtumia nani hapa na nani anamdanganya nani. Haya anayefanyiwa huyu dogo wangefanyiwa upinzani ungesikia kuwa ni mwiko kuchanganya dini na siasa Tanzania. Je huu ni usanii, woga au unafiki? Je nani atatoa nini na nani atapata nini? Je hapa kuna uwezekano wa kuambiana ukweli au kufurahishana ilmradi kila mtu apate chake? Ama kweli bembeleza kafiri upate mradi na isitoshe baniani mbaya kiatu chake dawa. Kama zilivyo ndoa za namna hii zenye kutia kila aina ya shaka, siku itakapobuma mtasema alisema. Sisi yetu macho na masikio.

No comments: