The Chant of Savant

Tuesday 28 February 2017

JE TANZANIA INAHITAJ MAOMBI AU KUUELEKEA UKWELI? JIBU ANALO ANONYMOUS HAPA CHINI

           Pongezi zangu nyingi sana kwako kwa kuligongomea sanduku la maiti MSUMARI WA MWISHO kuhusu hawa Matapeli wa kidini.Tukumbushe tu kihistoria kwamba tangu jamii za kiduni(Primitive society) waliposhindwa kuelewa jinsi gani tabia(nature) inavyofanya kazi kwa uchanga wao wa kiakili zao kufikiri kisayansi wakaja na fikira kwamba kila tabia(nuture)ambayo wameshindwa kuielewa jinsi inavyofanya kazi na ikawa inawaletea madhara na kushindwa kujitetea na madhara hayo kwa kufikiri kisayansi,wakaja na ufumbuzi wa kwamba kila tabia(nature)inayowadhuru au kuwanufaisha kuuimbia miungu mbali mbali na kuiabudu na hatimae kuifanyia madhabahu ya kuwafurahisha na kuwaridhisha miungu hiyo pale tu wanapogundua kwamba miungu hiyo imekasirika kwa madhara wanayoyapata kwa kuwatoa wanadamu kafara katika madhabahu yao au kuwafikishia mazao yao na wanyama wao kama ni sadaka pale tu wanapoona wamefanikiwa katika maisha yao.Na zilipokuja dini za mbinguni zikaondoa kafara ya wanadamu na kuwatoa wanyama kama ni sadaka au kafara katika madhabahu hayo.Na tunakuta tu kwamba MAKUHANI,WACHAWI NA WATAWALA WALIKUWA NI KITU KIMOJA KATIKA KUHAKIKISHA KWAMBA UTARATIBU HUO UNAENDELEA KWA KUUFANYA KAMA NI DINI NA KUNUFAIKA NA WANANCHI WAO KWA KUWANYONYA KWA KILA NJIA YA HADI HII LEO UTARATIBU HUO UNAENDELEA NA DINI KUWA NI TATIZO KATIKA JAMII BADALA YA KUWA UFUMBUZI NA UFUMBUZI WA DINI NI KWAMBA NCHI NI YA WOTE NA DINI NI YA MUUMINI NA ANACHOKIAMINI NA KUKIABUDU NA BILA YA KULAZIMISHANA,KUUANA,KUCHUKIANA NA KUIINGIZA KATIKA SIASAWA.
        Watu wa ulaya walipofanikiwa kuzitenganisha taasisi za kidini na kiserikali katika zama za kufikiri kisayansi na baada wanadamu kujua ni jinsi gani tabia(nuture)inavyofanya kazi kwa kupitia nyanja zote za kisayansi.Makuhani wamepoteza nafasi zao au haiba zao za kuombea jamii au kuliombea taifa na kufikisha kafara na sadaka mbele ya madhabahu.Na katika makala yako ya hivi karibuni uligusia kwa kusema kwamba jamii ambayo watu wake ni wajinga na washirikina matapeli wa kidini wataendelea na utapeli wao huu wa kidini.Kwa hiyo Muda wa kudumu jamii yetu bado ina mihimili yote ya jamii duni(primitive society) na hatuna utaratibu wa kufikiri kisayansi ndio upuuzi huu na ujinga huu utaendelea kubaki daima na milele.Swali ambalo linalojiuliza hapa je hivi watawala wetu nao hawashiriki katika kuundeleza ujinga,ushirikina na upuuzi huu?Je ni kweli tumefeli kiasi hiki kwa kushindwa kuwaandaa watu wetu wawe na uwezo wa kufikiri kisayansi tangu mashuleni na sio kuwapa elimu na shahada za kupatia riziki?


Nakumbuka vyema tu kwamba katika kinyang'anyiro cha mashindano ya kombe la dunia la mpira wa miguu ya mwaka 1982 yaliyofanyika Uhispania ambapo nchi ya Poland iliyashiriki,viongozi wa timu hiyo na wachezaji wake waliamua kwenda kumuona Pope John Paul 11,Mpoland mwenziwao ili awaombee kwa Mwenyezi Mungu ili waweze ushindi wa kulitwaa kombe hilo la dunia katika mashindano hayo.Lakini Pope John Paul 11 aliwajibu kwamba "Katika mpira wa miguu Mwenyezi Mungu apendelei timu yoyote".Kwa msemo huo wa Pope ni kuwaambia viongozi na wachezi wa timu hiyo kwamba ni maandalizi yenu na majuhudi yenu ndio yatakayo waletea ushindi.Kwa mfano huo hai kinyume chake ni kwamba timu za mpira wa miguu zilikuwa klabu binafsi au timu ya taifa utakuta makuhani wa kidini,waganga na wachawi wanaziombea,kuzirogea na kuzichawia timu hizo ili zitoke na ushindi.Sasa tunategemea nini katika jamii kama hizi?Kwa hiyo makuhani hawa wa kidini kusema kwamba wanaliombea taifa ili iweje na je ikiwa makuhani wa kila taifa watamuomba Mwenyezi Mungu kuhusu taifa lao je hapa hatuoni kwamba Mwenyezi Mungu atakuwa na aina moja au nyingine ya ubaguzi kwa kuwapa taifa moja na kulinyima taifa lingine ambayo hii sio sifa yake Mwenyezi Mungu?Katika kitabu cha Waisilamu kuna aya inayosema"Hakika Mwenyezi Mungu habadili yaliyoko kwa watu mpaka wabadili wao yaliyomo naf- sini mwao"
Hapa hata Mwenyezi Mungu anawakumbusha waumini wa dini kwamba hakuna mabadiliko yoyote yale katika jamii au nchi yatakayopatikana kwa MAOMBI TU mpaka waumini hao wabadilike wao wenyewe kwa kuyabadilisha yale yote ambayo yanayo wakwamisha kijamii au katika Taifa na hapo ndipo Mwenyezi Mungu atawapa sapoti yote kwa kubadilika kwao huko.
      Ninachoelewa mimi katika historia ni kwamba ni taifa moja tu kama linastahiki kuitwa taifa ni lile taifa la watoto wa Israel alipopewa Mtume wao Moses na Mwenyezi Mungu Jukumu la kuwatoa watu hao kutoka Misri na kuwafikisha katika Ardhi walio ahidiwa.Na ni Mwenyewe Mungu mwenyewe ndie aliekuwa mstari wa mbele kuwaongoza na kuingilia kati katika maisha yao, kuwaadhibu wanapomkosea na kuwapa faraja wanapomtii na hata kupigana vita kwa niaba yao dhidi ya mataifa mengine.Lakini mwisho wa siku watoto hao wa Israel au taifa hilo lilimkana Mwenyezi Mungu wao na wakaamua kujitawala wenyewe kama wanadamu na kumuweka Mwenyezi Mungu wao pembeni na kufuata sababu na visababisha vyote vya kujiendeleza kama wanadamu bila ya kuhitaji MSAADA WA MWENYEZI MUNGU.
Mwalimu Mhango.Msumari wa mwisha umesha ugongomelea kwa nguvu zako zote,je kuna sikio litakalo sikia?kuna akili itakayofahamu na kufanyia kazi maelezo yako haya?Au ndio matapeli wa kidini wataendelea kupeta tu na kutanua katika jamii ya wajinga na washirikina?

No comments: