The Chant of Savant

Tuesday 21 February 2017

Kijiwe chataka wasiojua lugha ya taifa wasipewe uongozi

            Baada ya Kijiwe kujikita kwenye kadhia ya biashara hatari na haramu ya bwimbwi, leo kinakuja na inshu moja kali na nyeti kwa kaya. Msomi ambaye hana kawaida ya kuanzisha mada, leo anavunja mwiko wake. Anaamukua na kuanza, “mwenzenu juzi nilinusurika kuvunja TV yangu tena Hi Def.” kabla ya kuendelea Mbwamwitu anamchomekea, “kwani ilikutukana hadi uivuje au ni kutokana na usanii wa kupambana na bwimbwi kijinga?”
Msomi anajibu “hakuna kitu kilitibua siku yangu kama kuona clip mmoja ambapo muishiwa mmoja gabacholi akimtukana rahis tena kimzahamzaha huku waishiwa wenzake wakimshangilia utadhani alichokua akitenda si jina na machukizo kwa kaya yetu. Bila aibu wala woga gabacholi huyu baniani aliamua kumtukana rahisi kwa kujifanya kakosea majina yote ya rahis. Alimwita Mapombe Makufuli. Kituko zaidi ni kwamba matusi na kejeli hizi vilifanyika mjengoni huku vyombo vya habari na kamera zake vikirekodi.” Anatulia kidogo na kuendelea “Gabacholi huyu alishangiliwa sana kiasi cha kupata mori wa kuendelea kubomoa lugha ya taifa letu na viongozi wetu. Ajabu ya maajabu waishiwa waliangua vicheko badala ya kuomba mwongozo ili mhusika afute upotoshaji na kusanifu huku kwa majina ya mkuu wa kaya kiasi cha kuwafanya wote wawe washiriki katika jinai hii.”
Kabla ya kuendelea Kapende anakula mic na kusema “hata nami niliona jamaa akiongea Kiswahili kibovu kiasi cha kunifanya nijiulize: Inakuwaje watu wasiojua au wanaojifanya kutojua Kiswahili ambacho ni lugha ya kaya wanapewa dhamana wakati kwenye kaya zote duniani, huwezi kupewa dhamana kama hujui lugha ya taifa. Kwa mfano, huwezi kuwa mbunge wa India kama hujui mojawapo ya lugha za india.”
            Mijjinga naye anapoka mic na kuronga “ukiachia baadhi ya jamii kujifanya kutojua lugha ya kaya au kudharau kujifunza, zinasifika kwa ubaguzi dhidi ya watu weusi. Je hapa lawama ni kwa nani?
Tunahitaji kubadili mfumo huu wa kikokolo ambapo kila ajaye anapewa fursa ya kupewa dhamana ya umma bila kuangalia yeye ni nani na ana mchango gani.”
            Mipawa anachomekea “wapo waliokataa kutangamana nasi kama vile kuoleana, na kuwa karibu. Hawa hawafai kupewa dhamana za uongozi kwenye kaya yetu ili kuwakilisha wabaguzi wenzao kwa mgongo wa wajinga wetu wanaowapa kura ya kutula. Je wanapataje dhamana hii? Je hapa tatizo ni rushwa, ujinga au kupinda sheria kama siyo kujibagua binafsi kama watu weusi tunaobaguliwa karibu na kila jamii hata nyingine za kiafrika ima kwa rangi au nywele?”
Mpemba anakatua mic “mie wallahi sishangai hata kidogo. Kwani hawa wamejitenga wengine kiasi cha kuwa na shule, dini na kila kitu chao. Nasi kwa ujinga na kujibagua, tumeruhusu ubaguzi huu kuwa sehemu ya mfumo wetu. Kuna haja ya kuwa wakweli kwa nafsi zetu na kuambiana ukweli. Kwani kuna baadhi ya jamii miongoni mwetu kama vile magabacholi, wamanga na hata baadhi ya waswahili wenzetu wa kialshabaab ambao wanajiona bora kuliko sisi kiasi cha ima kuchanganyikana nasi kwa kutuolewa au kutoruhusu ndoa kabisa ukiachia mbali kujiweka mbali na sisi. Nenda mikoa ya pwani kwa mfano. Wamanga na mazalia yao huwa na fursa ya kuoa waswahili lakini si waswahili kuwaolea wao. Inapokuja kwa magabacholi na maalshabaab, hakuna cha kuchanganyikana. Je hii itaendelea hadi lini?”
Kanji kwa aibu ya wazi anakula mic “dugu zanguni, hapa hukumu vatu vote kama moja nafanya kosa. Mimi kama napata bibi Swahili naona kesho.”
Kabla ya kuendelea Mgoshi Machungi anampoka mic na kusema “hei Kanji ungejinyamazia. Tinajua janja yenu yote. Tangu mkooni mwingeeza awabwage hapa hamjawahi kutaka kuchanganyikana nasi. Tinabaguiwa wazi wazi na mamuaka zinanyamaza. Sasa titaona kama wakubwa watamiadhibu hii baniani uchwaa. Ajabu kama huyu mwishiwa angekuwa wa upingaji, tingesikia makeee ya kuomba mwongozo na kumtaka afute kaui zake za kishenzi. Lakini kwa vie huyu ni gabachoi, hakuna kiichofanyika kiasi cha kutionyesha kama majuha yanayojitukana yenyewe.”
Bi Sofia Lion aka Kunungaembe anaamua kukatua mic “kusema ukweli hata mimi kashfa hii imenikera. Ajabu waandishi wa utani wakibadilisha majina ya rahis wanaambiwa wanamtukana kiasi cha kuonywa mara kwa mara. Hapa kinachojitokeza wazi ni kwamba hawa jamaa, licha ya kutubagua, wanatudharaua na kutuona kama hamnazo. Naungana na Mgoshi kusema wazi kuwa kama wahusika hawatafanya lolote, watakuwa wamethibitisha madai yetu kuwa wanawagwaya magabacholi. Leo wanamwita Mapombe Makufuli. Kesho watamwita bwimbwi, gongo na matusi mengine ya ajabu ajabu. Kama mtu hana la kuchangia basi anyamaze. Mie hakuna kilichonichefua kama naibu kipaza sauti bi Asiye Tulia kuchekelea na kusifu matusi haya pamoja na PhD yake tena ya sharia.”
Kijjiwe kikiwa kinanoga si likapita shangingi la baniani! Acha tulitoe mkuku tukitaka fanyia yeye kitu bay asana. Matusi yalisikika kila aina huku wazomeaji wengine wakisema “ponjoro nenda kwenu katukane hao magabacholi wenzako lakini si viongozi wetu. Mapombe baba yako na makufuli maza wako, unabwia bwimbwi nini, mbona huna adabu wala aibu?”
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano kesho.

No comments: