The Chant of Savant

Tuesday 28 February 2017

Kijiwe chataka rahis aunde tume ya Escrew na Lingumi

Image result for lugumi enterprises photos

Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi Said Mwema
                Baada ya kushuhudia sekeseke, hata kama ni kisiasa, la kupambana na bwimbwi, kuna somo tumejifunza. Tumejifunza kuwa tukiamua tunaweza. Tunaweza lolote lile ilmradi tuwe na utashi kisiasa na kijamii. Hivyo, leo Kijiwe kinatumia somo hili kupanua wigo lau tuweze kuwa na kaya safi, salama na yenye mafanikio ambapo kila mchovu anapata riziki yake na utajiri kihalali badala ya mazoea ya kuibiana na kuumizana. Katika kuondokana na mkwamo uliokuwa umeanza kuzoeleka na kuhalalishwa, tunashauri baadhi ya hatua mujarabu ili kukabiliana na matatizo na kadhia nyingine tena ambazo ni sugu na hatari kuliko hata bwimbwi.
            Mgoshi Machungi analianzisha “jamani hivi kashfa za Ungumi na Eskoo zimeishia wapi; mbona sisikii daktai wa kutumbua majibu akizitumbua au tumeingizwa mkenge tena? Mimi sieewi kusema ukwei.”
            Kapende anachomekea “unashangaa kitu ambacho ni cha kawaida! Haya ndiyo matokeo ya uvivu wa kufikiri ambapo yule aliyetutukana kuwa tu wavivu wa kufikiri alituuza na akajiuza mwenyewe huku akiendelea kukingiwa kifua na wavivu wenzie. Nani anaongelea Escrew na Lungumi wakati sinema imehamia kwenye bwimbwi?”
            “Yakhe hapa umepiga kwenyewe wallahi. Mie sidhani kama tutaamua kukumbushia hizi kadhia kama zinaweza kuzikwa tukiamua. Kama waathirika wa wizi huu wa kutisha, lazima tupaaze sauti zetu lau haki itendeke. Au vipi?” Kapende anajibu.
            Mipawa anakula mic “Ni kweli. Hakuna haja ya kushangaa. Nani asiyejua kuwa nyuma ya kashfa hizi wapo wazito wanaotumia madaraka yao kuendelea kutuzingua kwa kuanzisha hili na lile ilhali matatizo makubwa kama haya yakisukumwa chini ya busati? Tunapaswa kulikumbusha lisirikali kuwa lilituaminisha kuwa litapambana na uovu na uoza zikiwamo kashfa za Esrew, Lungumi, IptL, uDA na nyingine nyingi. Kama wameweza kuanzisha sekeseke la bwimbwi, wanashindwa nini kushughulikia mazimwi haya kama hawana namna wanavyonufaika nayo?”
            Mheshimiwa Bwege leo anaamua kutia guu wakati mada ikiwa mbichi. Anakula mic “mie napendekeza Kijiwe hiki kitukufu kiunde tume maalum kupambana na balaa la escrew ambapo matapeli wa ndani na nje hushirikiana kuwaibia wadanganyika tena kwa kushirikiana na wanene uchwara na mafisi katika kaya. Rejea kilichotokea ambapo jikampuni la IpTL lilivyopunyua mabilioni toka kwenye fuko la Escrow kwa njia ya esrew ambayo hadi sasa inaonekana kumtisha Dokta Kalaji ambaye ameonyesha umwamba kwenye kushughulika ugonjwa wa majipu huku akishihdwa ugonjwa hatari wa escrew ambao dalili zake na waathirika wake viko wazi..”
            Anapiga chafya nakuendelea “huwezi kupambana na gonjwa la escrew bila kuondoa viini vyake yaani IpTL yaani Immoral putrefaction Transmitted legacy.  Hivyo, tunashauri rahis aunde tume maalumu ya kushughulikia gonjwa hili.”
            Msomi Mkatatamaa anakwanyua mic “kaka kuna tatizo jingine liitwalo Lingumi. Baada ya kusikika kwenye vyombo vya habari kipindi fulani, inaonekana sasa hivi kashfa hii imefishwa kama siyo kufichwa au tuseme kusukumwa chini ya busati na wakubwa walioshiriki kuliasisi na kulianzisha. Kwa wasiojua Lingumi ni nini, ni kashfa ambapo mdudu mmoja aitwaye Lingumese intestiopsis norbitalis gluttonic and uncaring man especially and seemingly endangered. Yuko wapi mtuhumiwa mkuu wa ujambazi huu? Kuna source yangu iliyonitonya kuwa jamaa huyu kaishavushwa na yuko majuu akifaidi kuku huku sisi tukipigika. Tunapaswa kuondoa woga na kumtaka rahis ashughulikie Lungumi na Escrew kwa uzito aliouweka kwenye bwimbwi kama kweli anaanisha kuisafisha kaya.”
            Sofia Lion aka Kanungaembe anakula mic “kaka usinikumbushe kashfa hii. Yuko wapi yule gabacholi toka kaya jirani aliyeletwa akidai yeye ndiyo mmilki halali wa IpTL wakati ni tapeli na kinyago kilichotumiwa na wakubwa kutufunga kamba? Yuko wapi Jimmy Rugemalayer mbwahe mwingine aliyetumiwa katika ujambazi huu uliofanyika chini ya Bingwa wa uvivi wa kufikiri aka Denjaman Makapi? Ina maana dokta Kanywaji hajui yote haya au ni yale yale ya mtu aliye hai kuogopa makaburi tena yaliyojaa uoza?”
            Kanji naye anaamua kukwanyua mic “mimi ikosangaa sana dugu zangu. Mizi nakuja naiba naondoka na juluku yote. Nini kazi ya sirikali jamani? Mimi unga kono na guu vote nasema sirikali ikamatate vote naiba juluku yetu kama nakamata ile vote nauza bimbi.”
            Mchunguliaji anamkosoa Kanji “Kanji sema bwimbwi siyo bibi au bimbi.”
            Mijjinga aliyekuwa bize akisoma gazeti moja la kimataifa lichapishwalo Lushoto anakula mic “naona tunapoteza kuwalaumu akina Lingumi, esrew na IptL wakati wenyewe tunawaacha. Kwani hatuwajui waliosuka dili hili? Ukitaka kuwajua, jiulize madili yote haya yote yalifanyika lini na chini ya uongozi wa nani. Nashauri tuandamane kwenda kwenye ofisi zao na kuzitia nari ili wanaojifanya hawasikii wala kuona wapate salamu kuwa nasi tunaweza kuchukua hatua katika kupambana na maovu kwenye kaya yetu. Huu si wakati wa kugeuzana mabwege, kuburuzana na kuibiana huku tukiendelea kuteseka. Tumeshindwa hata uDA ambayo ni saizi yetu jamani! Tunadanganywa na nkwingwa Kisenena ambaye namjua tangu nyumbani kuwa hana chochote wala lolote bali ni con artist tu wa kawaida.”
            Wakati kijiwe kikinoga si likapita shumbwengu la IptL. Wacha tumkamate na kumfanyia kitu mbaya na kutawanyika!
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano leo

No comments: