The Chant of Savant

Tuesday 25 August 2015

Migrants: Europe Needs to Go Back to History


Many desperate people from Africa, Asia and Middle East are now making perilous journeys in thousands in their attempts to reach Europe seeking green pastures. They are risking everything to cross the Mediterranean.  Italy’s ports have become modern-time Kilwa, Mafia, Dakar or Lamu for Africans to enter Europe as it was for Europeans to enter Africa landing in the above mentioned city states. Europe is grappling with the heavy load of invaders just as Africa did when Europeans invaded and colonized her in the seventeenth century. Those poor but energetic and ambitious Africans, Arabs and Indians are called a calamity there due to the danger they pose to the economies and cultures of European countries.
          Nevertheless, it is sad that Indians and Arabs are not seen with the same lenses as Africans are. Is it because of racism or ignorance? Why don’t they feel pity for them after considering how dangerous and adventurous their voyages are?  Is the history repeating itself or is the law of reciprocity based on times displaying its nature? It is time to tell Europe to stop worrying for no reasons.These folks are heroes who want to help poor relatives made poor by black colonialists that are always in bed with Western ones. Africa’s economies can’t support their population thanks to playing a service role to Western economies. If the situation remains the same, Europe must brace itself for even more. Maybe, this is the new way of deconstructing the archaic system of exploitation enacted by the same European countries under colonialism, slavery and imperialism. This is why I fully endorse it. For I know. It will help all of us to see the problem as ours not Africa's or/and third world's as those who created such a dichotomous schema have always wrongly maintained for many years. Importantly, Europe needs to open doors, borders and hearts the same Africa did when first Europeans inundated Africa seeking spheres of influence that later became colonies.
          Again, Europeans seem to have forgotten a simple fact that they once gone to Africa  thereby colonizing her and destroying her economy and her ways of life. What did they expect out of an unequal and inequitable trade relationship the world evidences today? When they invaded to Africa, they did not have passports the same way our people are doing now. They’re called floods that’ll wipe out European good life standards. So be it; if they wiped out our own life standards before introducing slavery and colonialism. Swahili sages have a saying kula na kulipa. You eat and pay for what you’ve eaten. Or when you eat expect to be eaten. Aren’t we eaten by bacteria after our dead bodies undergo rigor mortis, chemical changes, when we die? The Europeans came to Africa and robbed her everything. Fortunately for them, Africans are not going there to rob or colonize them. But they’re going there to work because they’re good and hard workers. They are honesty and innocent victims of manmade exploitation in their continent.  Again, the Europeans are the same humans who created the exploitation that is forcing Africans to flee their countries. That’s why they are not aiming at colonizing anybody. If Europeans flooded Africa in the seventeenth and  the eighteenth centuries, what’s wrong for Africans to flood Europe in the twenty first century as the sign of reciprocity?

           I think European countries honestly need to learn about globalization they introduced to the world. They must do so by using the waves of economic immigrants. They need to learn that when you leave a thorn back in the farm, the same will hurt you one day. Time for colonial monsters to pay what they ate is now. European countries need to understand that what’s going on is, essentially, the real product of their plundering policies championed by capitalism. Africans have a saying that the capital of a poor person is his or her energy. This is why Africans are looking for good life and jobs in Europe after colonial monsters conspired with black ones to deny them works at home. These folks are looking for the means to live dignified and meaningful lives. Invest in Africa and create jobs. You won’t see the assemblages of Africans coming to your doors to destroy and infringe on your cultures and standards the way you destroyed theirs.
Source: African executive Aug. 26, 2015.

10 comments:

Anonymous said...

Salaam Mwalimu Mhango,
Nimeisoma maakala yako hii nikielewa kabisa nini unachoongelea katika historia na kuwataka watu wa ulaya warudie historia hiyo ili walielewe somo hili la ya wahamiaji wa kiuchumi katika bara lao.Kuna ukweli wa kihistoria ambao umeungolea ambao sitotafautiana na wewe kabisa kwa kuja kwa walala hoi wa ulaya(wazungu)katika bara letu,wakatukoloni,wakatuibia,wakatudhalilisha na kutuharibia jinsi ya utaratibu wetu wa maisha na hata kutuletea dini zao za kigeni ambazo zimechanganyia kutunyanganya kila kitu chetu na zimebaki kama ni bomu la kutegewa katika jamii zetu za kiafrika.Na baya zaidi kutuachia kama ulivyowaita" wakoloni weusi" ambao wanashirikiana nao hadi hii leo katika kuendelea kutukoloni,kutuibia,kutudhalilisha na kuendelea kutuharibia mila na utamaduni wetu.

Naam,Mwalimu Mhango,ninachotofautiana na wewe katika makala hii ni ule muono wako wa kufanya uwiano wa historia ya wakazi wa ulaya (wazungu)walipokuja kwetu na sisi kuaanza kuteremka kwao,Kwanza kabisa nadhani hatutofautiana kwamba Afrika hakukuwa na nation states ambazo zingeweza kukabiliana na wimbi hilo la walala hoi hao wa ulaya na wala hakukuwa na serikali kuu (central goverments) ambazo zingeweza kuwadhibiti walala hoi hao wa ulaya na hatimae kuwawekea vikwazo na hata kuwafamisha kwamba hawakaribishwi ktika bara letu kwa wanavyotaka wao.Na kwa kukosa utaratibu huo wa kujitawala wenyewe hatimae tumetokea kuonekana mbele ya macho ya walala hoi hao wa ulaya kwamba ni ardhi ambayo haina mwenyewe (no man's lands),muono ambao umepelekea kwa walala hoi hao wa ulaya kukwapua ardhi yetu kwa tamaa na kwa pupa ya ajabu na hata kutuchorea mipika ambayo tunajivunia hii leo kama ndio mataifa yetu(Nation states)na tupo tayari kuingia vitani na kuuana wenyewe kwa wenyewe kwa mipaka hiyo tuliyochorewa na walala hoi hao wa ulaya.
Tofauti nyingine ya kimsingi ni kwamba wao walikuja kwa vyombo vyao vya usafiri ambavyo havikuambatana na hatari ukiachilia mbali msukosuko wa bahari na wala hawakupoteza watu wao kwa idadi ambayo sisi tumepoteza kwa uhamihaji wetu katka bara lao na hatimae katika mwanzoni mwa karne ya 20 wakawa na usafiri wa anga ambao umewawezesha kuwarahishia kila mbinu ya ukoloni na wizi.
Swala lingine Mwalimu Mhango la kulizingatia ni matokeo ya uhamiaji wetu kwa bara lao na athari zake kwetu sisi wenyewe waafrika,japo umelizingatia sana swala la utafutaji wa maisha bora na kuboresha maisha ya familia zao wapi walipotoka.Najua wazi kwamba kuja kwa walala hoi hawa wa ulaya katika bara letu kumetuachia na athari mbaya kwa upande mmoja katika jamii yetu kwa kutubomolea mila na utamaduni wetu na hata kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kutufutia utambulisho wetu,kwa maana tumepoteza dini zetu,majina yatu na hata mavazi ya kujidaia leo hii tunajidaia mavazi yao hata kama mavazi hayo hayaendani na hali ya hewa tuliyokuwa nayo.Lakini kwa upande mwingine-sisemi kwamba tuwashukuru-kuja kwao kumegeuza historia ya dunia yote kwa upande wa elimu,sayansi na teknolojia ambao wao ndio mabingwa wa uwanja huo hadi hii leo.Hofu yangu mimi Mwalimu Mhango,ni huu uhamiaji wetu sisi katka bara lao pamoja na manufaa ya kiuchumi kama ulivyoashiria lakini umekataa kuona athari kubwa na mbaya ambayo itakayotokea kwa kizazi cha kwanza cha wahamiaji hawa ambao wataishi katika hali ya kubaguliwa daima na kuongezeka kwa kasi ya wimbi la neo-fascism kwa wakazi wa asili la bara hilo,ambayo ilishaanza kujitokeza kabla ya wimbi hili la uhamiaji kuwa kubwa,na baya zaidi angalia matokeo ya kuanzia kizazi cha pili hadi cha tatu cha kiafrika ambacho kitamezwa moja kwa moja na utamaduni,mila na desturi za watu wa bara hilo la ulaya (assimilation) na hatimaye kubaki ni historia tu kwamba asili yao ni bara la afrika na vizazi hivyo havitokuwa na mchango wowote ule wa mana kwa bara lao la asili walipotoka.Na kizazi hiki si kama kile ambacho kiling'olewa kutolewa Afrika kwa sababu za biashara ya utumwa bali ni kizazi huru na mababu zao walikuwa huru na walijikuta wapo katika bara la ulaya kwa sababu za kiuchumi tu.
Inaendelea......

Anonymous said...

Mwalimu Mhango,
Namalizia kwa kusema kwa wale wakoloni wetu weusi wanapoisoma makala yako hii utawafanya wapate usingizi mzuri kwa kuwaona wachambuzi kama nyinyi mnawatupia lawama kubwa wakoloni wao wakati wakoloni hawa weusi ndio wanastahiki lawama kubwa na lana kubwa kwa sababu wao ndio chanzo kikubwa cha kuwafanya watu wao waishi katika umasikini,ujinga na maradhi leo hii kusababisha kudhalilika,kupoteza maisha yao kwa kupigania kupata mkate wa kila siku katika bara la ulaya.Na kuendelea kwa wakoloni hawa weusi kutowajali watu wao na nchi zao kwa kupigania kwa nguvu zao zote masilahi yao,ya familia zao na ya wakoloni wao.

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Anon,
Shukrani kwa mchango wako. Nakubaliana nawe kuwa makala yangu inaonekana kulalia upande mmoja. Ni bahati mbaya nilisahau kueleza kuwa nimeidokoa toka kwenye kitabu changu cha AFRICA REUNITE OR PERISH kinachotegemewa kutoka hivi karibuni. Maswali yote uliyoulizia yamejibiwa vilivyo kwenye kitabu husika. Nimesema wazi kuwa ingawa kulaumu ni haki yetu tunapaswa kujilaumu na kuwalaumu wakoloni weusi waliozuia Afrika kuungana. Kwa upande wazungu nimewapa changamoto mbili. Mosi, waache kuzilinda tawala zandiki barani ili waafrika wazipindue na kuweka serikali zinazowajibika kama zao huku Ulaya. Pili, waache mfumo wao wa kinyonyaji. Kwani waswahili na wahindi wataijaza Ulaya hadi nayo pole pole ianze kuwa maskini kama Afrika. Mfano mdogo wa sasa ni kwamba wazungu wengi wanakimbia ulaya kuja Kanada au kwenda Australia kutokana na kuanza kufilisika. Kwa ufupi kitabu hiki cha kurasa 340 kimegusia mengi kuanzia ukoloni, ubaguzi, ukoloni mambo leo, uchumi, utamaduni na mengine mengi. Kwa sasa kwa kushirikiana na profesa Munyaradzi Mawere wa Zimbabwe tuko tunaandika kingine cha The Manifesto of Africa. Nami binafsi nimeanza kuandika kingine cha THE BEST AND WORST AFRICAN MANAGERS. Pia nikupinge kuhusiana na vizazi vya watakaokuja ulaya kuwa na jina tu na si mila, hii ni hofu tu. Mie watoto wangu hata waliozaliwa huku wanajua kuwa kwao ni Afrika. Kwanza, wanapobaguliwa wanajitambua na kutafuta kutaka kujua kwao ni wapi. Hivyo, litakuwa ni kosa la wazazi ima kwa kukosa uwezo au kutojua kutowapeleka watoto Afrika ili walinganishe. Kwa mfano, huna haja kumpeleka mtoto mchanga ambaye hawezi kupambanua akaambua kitu. Umri mzuri ni kuanzia miaka nane hadi 12 kabla hajaharibikiwa. Ningependa niandike mengi, fursa ni ndogo kwa vile nina miraba minne au mitano ya kulisha kila wiki kwenye safu zangu ukiachia kuandika na kusoma mambo mengine. Nikushukuru tena kwa michango yako yenye faida kwangu na wasomaji wengine.

Anonymous said...

Salaamu Mwalimu Muhango,
Kwanza kabisa ningependa kuendelea kukupongeza kwa majuhudi yako endelevu ya kuandika vitabu vya kutufungua macho sisi waafrika kwa pande nyingi ambazo zinamgusa Mwafrika huyu barani afrika na ugenini,japo sisi waafrika hususa barani Afrika sio watu wa kupenda kujisomea isipokuwa nina imani kubwa kwamba maandishi yako haya yataleta na kuzaa matunda kwa kizazi kijacho hususa kwa kizazi cha kiafrika cha ugenini popote pale kilipo,lakini kizazi ambacho nilipenda nizidi niendelee kukiongelea hususa baada ya wimbi hili la uhamiaji wa wazazi na watoto wao kulivamia bara la ulaya.Tuanze kwanza na kizazi cha mwafrika kilichochukuliwa kutoka bara la ulaya kwa sababu za biashara ya utumwa, tunajua ni nini kilichotokea kwao kwa kuptoeza kila kitu chao kinachohusu uafrika na afrika yao kwa kusafishwa ubongo kwa hali ya juu sana kiasi ambacho walijikuta hawana cha kujidai au kukimbilia na hatimae kufikia kujikataa wao wenyewe kama waaafrika ambao waliotoka katika bara la Afrika.Kizazi hiki cha watumwa waliopita (x-slaves) ilifika wakati kwa kutokana na ukandamizwaji mkubwa na wa makusudi wa utambulisho wao kama waafrika waligundua nia na madhumuni ya mabwana wao waliopita(x-masters) ya kwamba hawakuwatakia kheri ya aina yoyote kama waafrika,naam,Mwalimu Mhango kizazi hicho kiliinuka na kuleta mapinduzi ya hali ya juu ya kupigania utambulisho wao kama waafrika na kuikubali asili yao na hata kuanza kutafuta ,kujijengea na kuwa na marejeo katika bara lao la Afrika,japo sio kwa kiwiliwili bali kwa kiakili na hata kiroho na kwa kiasi kikubwa wamefanikiwa katika mapinduzi yao hayo ya kupigania utambulisho wao na hata kufikia kuwa wenye kujivunia kwa kujiita au kuitwa WAMARIKANI WENYE ASILI YA KIAFRIKA( African Americans)
Mwalimu Mhango sina sababu ya kuendelea kuielezea historia ya mapambano hayo ya kizazi kipya cha watumwa waliopita (x-slaves ambayo wote tunaijua.kwa kusema hayao basi ningependa kukirejea kizazi cha waafrika katika bara la ulaya ambao walioamua kwenda kuishi katika bara hilo na wanaokwenda hivi sasa ambao wengi wao sababu yao kuu ya kimsingi ni ya kiuchumi kwa kukimbia UMASIKINI katika bara lao la Afrika,kizazi hiki sio kama kile kizazi cha waafrika waamerika,wao ni kizazi huru wao na mababa zao kama nilivyotangulia kuandika hapo awali.Kizazi hiki hakikupambana na changamoto ya utumwa kama kizazi cha waafrika wa Amerika bali kizazi hiki kimepambana na changamoto ya UKOLONI na UBAGUZI sababu ambazo zimewasababishia kuwabomolea uawafrika wao na hadi hii leo tuna wakoloni mambo leo katika kizazi kilichobaki afrika na kizazi cha ulaya kuamini kwamba mila,utamaduni na lugha ya mkoloni wao wa kizungu ni bora kuliko zao wao.
Inaendelea.....

Anonymous said...

Naam Mwalimu Mhango, tulipigania kujikomboa kutoka katika ukoloni wa kisiasa lakini hatukupigania hadi hii leo-japo kuna majuhudi ya watu kama nyinyi-ya kujikomboa na ukoloni wa kiakili na ukoloni mambo leo ambavyo vimetusababishia na kutuachia athari mbaya kwa waafrika wenyewe waliobaki nyumbani na kizazi kinachoishi hadi hii leo.Japo Mwalimu Mhango umeongelea kesi yako binafsi na ya watoto wako na kutoa aina ya ushauri,lakini umefumbia macho kwa kiasi kikubwa tatizo hili la kizazi cha kiafrika hususa barani ulaya na umejaribu kutoa ushauri na nasaha kwa wazazi nini cha kufanya kuhusu watoto wao.
Mwalimu Mhango,wache tuangalie ukweli wa ardhini kuhusu kizazi hiki cha kiafrika kinachoishi Barani ulaya,wazungu pamoja na ubaguzi wao lakini wanawapenda sana waafrika!!Je unajua ni kwa nini?Sababu ni nyepesi mno,nayo ni kwamba wazungu wanasema waafriaka wanazama,kujichanganya na kujiyayusha katika jamii ya kizungu(ASSIMILATION) kirahisi mno!! Je ni nini maana hiyo ya kuzama,kujichanganya na kujiyayusha kwa wazungu?maan yake ni kupoteza utambulisho wako kama mwafrika na kupigania utambulisho wa kizungu,na kizazi hiki cha kiafrika kinachoishi bara la ulaya ni kweli kimefanikiwa katika ASSIMILATION hiyo!!Kwa upande wa pili wazungu pamoja na ubaguzi wao pia lakini hawawapendi waarabu,waturuki na waasia wa aina yote wanayoishi katika bara la ulaya,sababu nini Mwalimu Mhango?Sababu ni nyepesi mno,kwamba wana jamii hao hawapo tayari kabisa kuzama,kujichanganya na kuyayuka(ASSIMILATION) katika jamii hiyo ya kizungu. Jamii hizo hupigania kwa nguvu zao zote kulinda lugha,mila,desturi na utamaduni wao katika jamii hiyo ya kizungu,kamwe hutokuta katika jamii hizo watoto wao wakapoteza lugha zao mama,kamwe hutokuta watoto wa jamii hizo kujivunia lugha za wakazi wa asili wa bara hilo,na jamii hizo zina utaratibu ambao ulioungelea wa kuwarejesha watoto wao kama ulivyogusia pindi tu wanapofika umri wa miaka 12 hadi 15 katika nchi zao mama ili wakajifunze na kuchukuwa kila kinachostahiki kuhusu utambulisho wao au kufanya ziara za mara kwa mara katika nchi zao hizo mama.Lakini kwa kizazi cha wafrika huyakuti hayo isipokuwa kwa wachache mno wenye mwamko wa kujidaia na kujivunia utambulisho wao kama waafrika.Kizasi hiki cha waafrika wa bara la ulaya kinahitaji kuangalia upya vinginevyo watabaki tu kama wafrika wa rangi na hawana chochote kile cha kujidaia au marejeo.Nataka tu nidokezo tatizo lingine la kijamii kwa kizazi hiki cha kiafrika cha ulaya au Amerika zote mbili nacho ni kupunguza machungu ya kubaguliwa,machungu ambayo uwapelekea baadhi yao kuchukua nafasi yoyote ile iliyopo mbele yao ya kuoa au kuolewa na wazungu na hatimae kupata kizazi mchanganyiko ambacho kwa kile kilichojificha ndani ya mioyo na akili zao kwamba watoto wao hao watakuwa na nafasi bora katika jamii ya kupungukiwa na kulengwa kiubaguzi kama wanavyolengwa wazazi wao katika jamii hiz,unaweza tu kuona mfano hai katika kiwanda cha burudani cha filamu za Hollywoodi,katika kiwanda cha burudani la music na kwingineko, kwamba kizazi hiki kilichochanganya huwa na nafasi kubwa ya kufaulu katika nyanja hizo; na kibaya zaidi hata katika famiila kizazi hiki kilichochanganya huwa kinapendelewa na kupewa hisani mbalimbali zaidi kuliko wengine.Mwalimu Mhango,huu ni ukweli wa ardhini kwa kizazi cha mwafrika kwa bara la ulaya amerika aidha ilikua ya kaskazini au ya kusini.
Inaendelea........

Anonymous said...

Mwalimu Mhango,umegusia kuhusu kuhama kwa wazungu wa bara la ulaya kuelekea aidha Canada au Australia kwa hoja ya za kiuchumi na kuashiria kwamba bara la ulaya litafilisika kiuchumi kwa kujazana kwa waafrika na waasia,wache nitofautiane nawe katika hoja yako hiyo,mimi naamini kwamba wazungu wanaoama kulekea nchi hizo ulizozitaja wanahama sio kwa sbabu za kiuchumi bali wanahama kwa sababu wao wana maradhi ya ubaguzi wa rangi wa hali ya juu sana ambao hawapo tayari kuishi kwa ukaribu au ujirani na waafrika au waasia kwa hiyo kwa kuamia katika nchi mbili hizo ulizozitaja wanajikuta tu wanaishi bila ya mchanganyiko wa aina yoyote ile wa waafrika na asia na tunazikuta hali kama hizo Amerika zote mbili,ulaya,Canada na hata South Afrika kwa neighborhood za WHITE ONLY!
Nitamalizia kwa kusema kwamba safari yako(yenu) bado ni ndefu na ina changamoto kubwa sana kwa kuwaamsha waafrika wa nyumbani na waafrika wa ughaibuni kwa kuwakomboa kutoka katika utumwa wa kiakili na hata naweza kusema wa kisaikolojia pia tutaendelea kukusoma na kutoa mchango wetu kila itakapolazimika kufanya hivy.Mola akupe muwafaka kwa majuhudi yako hayo.

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Asante Anon kwa mchango wako mwingine.
Naomba usome na hii huenda tunaweza kuanza kuelewana.
Western powers need to embark on a new way of looking at, and doing, things as far as the exodus of migrants is concerned. Africans who were treated like half beings for many years by enslaving and colonizing them are no longer the same today. Young people know too well what and where decent and meaningful life is. They know how to use internet to gain information that’s been the power that propelled Europe to success on the expenses of others. Time for Europe to stop the lie that Africa will remain the same is now. No more lies about Africa. The Dark Continent is now opening up brightly taking on those who brought her down. The light it emanates is now shining bright to those who caused and referred to Africa as the Dark Continent. Colonialism forgot one thing in that history has one permanent predisposition. It repeats itself. This is why today crowds of African modern-time missionaries, explorers, merchants and whatnot are taking on Europe to pay her back.
Look at how history is accurately and truly repeating itself. Europeans who paved way for colonialism came with boats the same way Africans are going to Europe. Colonial agents were all related to and supported by their home governments. The difference here however is that while Europeans were supported by their home governments, Africans are betrayed by theirs by making their lives miserably harder so as to risk their lives to travel to Europe. Even securing a passport, visa or a way to Europe is not that easy so to speak.
Another factor making this recurrence of history a reality is the law of proximity. It is much easier for Africans to go to Europe than going to other continents which, just like Africa, export their paupers. For instance, it is easier for a Tanzanian to go to Europe than going to India. Even travelling in Africa for an African is harder than travelling Europe thanks to systemic colonialism that the western enacted in Africa by exploiting her without developing her. After all, what would one go for in India where disadvantaged and poor Indians stowaway just like Africans and others end up in Africa? Some come and poach our animals. They fell our trees and transport them to their countries. Some steal our minerals in conjunction with our powerful homemade thieves. We see everything and know everything. Keeping mum does not mean that Africans don’t know where the problem lies. I think the problem for Africans is their designs of running away from home. By so doing, they give foreigners the opportunities to rob them even more. And arguably this is what their venal rulers want to happen. Africans know and understand everything however going to Europe for green pastures will never solve the problem without deconstructing it. If it does it will do so for a few and it will do so for a short time. As long as Africa remains divided, the problem will always haunt them after returning back home. So, they need to confront the right problem in the right way.
Africans know their weakness as well as their strength. They know where they went wrong.They know this no doubt about it. Again, when they think of taking actions, they think about our sisters and brothers who want to copy everything foreign. These copycats of ours are all over the place in Africa now. You see them behaving as if they’re westerners hopelessly. They swallow and devour whatever western comes to their ways in the name of fashions hook, line, and sinker. You can see them everywhere.

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Franz Fanon called them black masks white souls. We see them everywhere and in everything. They despise themselves due to their myopia and hard hearts. You see them in offices robbing our countries. The big ones steal and yet go to their masters to beg as if they’ve no hands, brains or resources. The flip side of all this is that all those living in the state of deny are not ready to help or cooperate with those that are conscious of who they are to take on the status quo. I think time to tell them is now. Please stop bringing us shame by begging and aping nonsensical things while we’ve everything. Stop borrowing so that you can get some money to stash in European banks while your people are starving. This is sacrilegious to have ruthless and heartless rulers in our offices. They hear me and pretend they don’t. They know what I am saying however they pretend not to get it. My wisdom to them is mere noise making. Again, for me such noise making is noble and it is better than silence that condones their illegality and criminality. Stealing from your coffers is as bad as stealing from your own house. True, for an African to be obliged to carry a passport when Africans travel in Africa is as bad as asking for a permission to enter some of the rooms in your own house which in this case is Africa. Forcing him or her to carry a bloody passport is to rob him or her. Doing so is robbing our identity and right to wonder in our continent as pleased. This should not go on shall we aspire to stand proudly before the international community. For, our enemies know how divided and weak we are. So they use our weakness to make us even weaker and weaker.

Anonymous said...

Salaamu Mwalimu Mhango,
Maandishi yangu ya kuhitimisha mada hii niiiandika "......Nitamalizia kwa kusema kwamba safari yako(yenu) bado ni ndefu na ina changamoto kubwa sana kwa kuwaamsha waafrika wa nyumbani na waafrika wa ughaibuni kwa kuwakomboa kutoka katika utumwa wa kiakili na hata naweza kusema wa kisaikolojia"Na kwa kusema hivyo basi ni matumaini yangu makelele yako yatasikika tu kwa kila pande zinazohusika hata kwa wale ambao hawataki au wanajifanya hawataki kuusikia na kuuona ukweli.Na kwa mada hii nadhani hakukuwa na tofauti ya kimsingi zaidi ya kutofautiana jinsi gani ya kuufikisha ujumbe kwa walengwa.Nami nasema ahsante kwa kuchukua wakati wako ghali kuweza kubadilishana fikra na wasomaji wako.

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Anon kwanza na kushukuru kwa welewa wako hasa kuhusiana na suala la muda na majukumu lukuki yanayonikabili. Ningependa lau niandike kwa kirefu kama ambavyo siku zote umefanya. Pia nashukuru kwa michango yako adhimu ambayo hunisaidi kuangalia mambo kwa jicho jingine. Nazidi kukukaribisha katika uga hii kila upatapo la kuchangia. Laiti wote wanaopita hapa wangekuwa na moyo kama wako, si haba ningeneemeka sana kiakili na kimkakati. Hili la kuandika vitabu sitaacha hadi pumzi ya mwisho. Maana ni kipawa nilichojaliwa lazima nikitumie.
Nakutakia kila la heri na karibu tena.