Free Thinking

I Fear Nothing But Fear Itself

The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Saturday, 27 May 2017

Eti Dom ni the big city of Bongo? Wow!


            Baada ya kufichuliwa madudu kwenye vitabu vya kiada kayani, walevi wengi walipigwa na butwaa kiasi cha kuamua kuhoji hata kama ni kilevi. Wengi walisikika wakitukana matusi ya nguoni ambayo pamoja na ulevi wangu siwezi kuyarudia.
            Kisa chenyewe kilianza pale ilipogundulika kuwa moja ya vitabu hivi hatarishi kimeandika eti Dodoma is the big city of Bongo; kikimaanisha mji mkuu. Huu ni ushahidi kuwa waliotunga hivyo vitabu ni vilaza, vibashite na vihiyo waliopaswa kuwa wanauza nyanya badala ya kupunyua mabilioni ya walevi ili kuwajaza sumu na ujinga vitegemezi vyetu. Na hapa lazima kuwa na mkono wa mtu mkubwa tena fisadi wa kunuka. Maana, bila hivyo, haiwezekani upuuzi kama huu ukafanyika tena kwenye sehemu nyeti ya ilm. Hapa lazima kuwa na majipu tena makubwa na yanayonuka yaliyoiva yakingoja kuguswa ili yatumbuke. Mnawanyima kazi watunzi wenye uwezo kwa kuendekeza njaa wakati hata sifa ya kuandika vitabu vilivyokwenda skuli hamna? Shame on you and kumbaff sana manyang’au nyie wana hizaya wajalaana na walaaniwa wakubwa. Hamna aibu wala maana. Heri yetu walevi kuliko nyinyi mnaojitiatia wasomi wakati ni vibashite vitupu.
            Baada ya kuinyaka Mlevi mmoja msomi akatoa mpya kuwa tujiandae kusikia vituko vingine. Hivyo usishangae kusikia mkiti wa CCM akiandikwa kwa kitasha kama the owner of the chair of CCM or the party of coup d’etat is John Alcohol Magufuli and the first wife is Mama Janet Magufuli.  Pia usishangae kusoma kuwa dini kubwa nchini ni Jesusism and Islamism. Sitashangaa kusikia watoto wakifundishwa kuwa the biggest mountain of Africa is Kilimanjaro na the largest Lake is Nyanza au the big sheik of Tanzania is so and so.
            Kesho utasoma the big minister of Tanzania is Katelephone Endowment Katelephone kama siyo big judge is professor Juma na mengine mengi. Hivi hawa walioandika utumbo huu walisomea wapi na lini? Je nani huyu mwenzao au wenzao waliowapa hii tenda ya mamilioni kujaza sumu na urongo kwenye vichwa vya vitegemezi vyetu? Je wanene wetu walikuwa wapi; au ni kwa vile wanapeleka vyao ughaibuni kupata elimu mufti huku vitegemezi vya walevi vikijazwa ujinga wa kudumu na kununua kwa kodi zao zinazotumika kuwalipa vilaza walioandika vitabu husika?
            Heri wangesema the biggest city of Bongo is Dar Si Salama but not Dom. Kwa sababu hata kama tutachukua mantiki ya lugha iliyotumika, bado Dodoma si kubwa kuliko Mwanza wala Arusha. Sitashangaa kusikia wakisema enchilada ni sambusa badala ya samosa kwa kitasha sahihi na mufti. Sishangai kusikia kuwa vitabu vingi ni mabomu. Kumbe ndiyo maana vyangu wetu wanaojifanya wapiga buku pale Chuo kikubwa cha Manzese wanabukanya! Utamsikia akisema “my milk are still standing and I’m a handsome lady that’s looking for a beautiful man to marriage me.” Juzi nilimsikia dingi mmmoja tena dingi kwelikweli akisema the deal had a lot of controversials badala ya controversies. Kama haitoshi aliongeza tell your children to come Bongo badala ya to come to Bongo! Jamani, kuna haja ya kujifunza lugha za watu kwa ufasaha japo kidogo kuliko kutuletea aibu na broken na mibomu yenu. Kumbe kuna akina Bashite kila sehemu hata kwenye elimu yenyewe! Hawa waliondika upuuzi huu wapelekwe kwa pilato na kufungwa maisha huku wakiamriwa warejeshe njuluku ya walevi na wawaombe msamaha kwa kuwajaza sumu vichwani vitegemezi vyao.
Hawa wafichuliwe hadharani na kuchukuliwa hatua. Maana ukiona hivyo wameishapunyua njuluku za umma.
            Ukikutana nao mitaani wanavyojidai wamepiga buku kumbe bashit mtupu.  Kama nilivyosema, hawa wafikishwe kwa pilato lau wakanonihino kwenye mtondoo au debe kule lupango.
Kwanini mnawalisha vitegemezi vyetu ujinga wakati wenu mkipeleka majuu ili visome vilivyo na kuja kuwala na kuwatawala vitegemezi vyetu? Kwani hatuwajui vitegemezi vya vigogo ambavyo sasa vimerithi ulaji wa wazazi wake kwenye ofisi za umma huku vikila kuku kwa umma watokanao na mali ya umma isiyouma? Kawaulize akina Jan Makambale, Hussy Muinyi, Emmy Nchimvi, Riz Kitwitwi, Sal Kitwitwi na wengine wengi wanaoendelea kutanua tokana na kuwa na majina makubwa.
            Kwa tamaa na upogo na ulafi wenu, mmeua watunzi na wachapishaji mahiri wa vitabu kwa kutaka kujipa tenda wakati hamnazo wala uwezo wa kutoa vitu vilivyokwenda shule? Hapa Dokta Kanywaji asipomtumbua mtu najinyotoa roho au kuhama kaya. Je mazabe haya yalianza lini na yameishaiingizia kaya hasara kiasi gani? ukisikia collective imbecilization si nyingine bali hii. Nina hasira sitatafsiri neno hilo lenye kufurahisha. Kwanini,kama kaya hamuoni hata aibu? Mnadhani mtaishi milele wakati mu makaburi yanayotembea? Shame on you! Mnatuimbia wimbo wa kuingia karne ya 21 ya sayansi na teknolojia wakati mnaendelea kufanya mambo ambayo hata Adam na Eva wasingefanya kwa kuogopa kuchekwa. Senzi kabisa na mkome na mkomae na broken zenu zitokanazo na kukwepa kupiga buku huku mkitumia masaburi na utumbo kufikiri badala ya vichwa.
Chanzo: Nipashe Jumamosi leo.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 06:48

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

Cordially and unlimitedly welcome to this blog.


Writing and reading are two different processes but which share the same goal-to educate, communicate and entertain.
It is my pleasure to have you as the guest of this tablet.
I, thus, warmly and always, welcome you to share ideas.
Importantly and eminently, shall there be anything amiss or you think can advance this blog, please donate it.
Allow me to humbly and kindly welcome you once again.
Nkwazi N Mhango- A Man And a Half

When wisdom brings no profit, to be wise is to suffer. Not all thoughts are good and constructive. Others are even worse than bullets. The good thinkers are the ones that think constructively for the manumission of all bin-Adams regardless their diversity. Mwl. Nkwazi N Mhango,
Canada.


Hail Mama SWAPO Nandi-Ndaitwah

Hail Mama SWAPO Nandi-Ndaitwah

I Love My Country Tanzania

I Love My Country Tanzania

The Curse of Salvation

The Curse of Salvation

Gen Z and Internet Revolution

Gen Z and Internet Revolution

I Cry for Ambazonia and Darfur

I Cry for Ambazonia and Darfur

How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do.

How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do.

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Yoo-hoo, Africa Is Yowling

Yoo-hoo, Africa Is Yowling

The Story of Stories

The Story of Stories

The Chant of Savant

The Chant of Savant

AFRICA’S CONTEMPORARY FOOD INSECURITY Self-inflicted Wounds through Modern Veni Vidi Vici and Land G

AFRICA’S CONTEMPORARY FOOD INSECURITY Self-inflicted Wounds through Modern Veni Vidi Vici and Land G

AFRICA MUST DEAL WITH BLATS FOR ITS TRUE DECOLONISATION

AFRICA MUST DEAL WITH BLATS FOR ITS TRUE DECOLONISATION

Epistle to Afrophobic South Africa

Epistle to Afrophobic South Africa

Magufulification

Magufulification

BORN NUDE

BORN NUDE

Total Pageviews

Heko Rais Magufuli

Heko Rais Magufuli

DECOLONISING EDUCATION

DECOLONISING EDUCATION

Kudos President Magufuli

Kudos President Magufuli

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

The Family Friend of Animals

The Family Friend of Animals
Children's Book

Matembezi Mbuga ya Wanyama

Matembezi Mbuga ya Wanyama
Kitabu cha Watoto

Our Heritage

Our Heritage
Children's Book

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

Perpetual Search

Perpetual Search

Africa's Best and Worst Presidents

Africa's Best and Worst Presidents

Psalm of the Oppressed

Psalm of the Oppressed
Psalm of the Oppressed

AFRICA REUNITE or PERISH

AFRICA REUNITE or PERISH
A new approach towards empowering Africa

BORN WITH VOICE

BORN WITH VOICE

Soul on Sale

Soul on Sale

Soul on Sale

Nyuma ya Pazia

Nyuma ya Pazia

We are one

We are one

SAA YA UKOMBOZI

SAA YA UKOMBOZI

Feel at home

You are always welcome to this epistle again and again time after time, ad infinitum.


Most read Posts

  • Sarkozy’s Take on African Fat Cats a Welcome Move
    At last the chicken are coming home to roost! French authorities made a groundbreaking decision by culling three most corrupt African presid...
  • Napanga kuanza kuuza mitumba na si maneno
    Ingawa mimi si mtumba, napanga kuuza mitumba. Nimechoshwa na jamii ya mitumba. Kila kitu mitumba. Mitumba, mitumba mitupu. Siasa za mitumba...
  • Better or Bitter Life for all?
    When I deeply muse on how an arrogant and brutal cabal of hoity toity (Coverted Con Men (CCM)) is tirelessly hoodwinking and dividing the ho...
  • Africa's Becoming more Despotic and Nepotistic
    "King of Kings" Gaddaffi The seven-day 40th anniversary of Libya strongman’s autocratic rule and charade elections in Gabon where...
  • Kuna siku tutataifisha haya mahekalu haki ya nani
    Taarifa kuwa waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alinunua nyumba kwa zaidi ya shilingi bilioni moja licha ya kuwastua wananchi na...
  • Nyangumi mdogo akutwa amekufa ufukweni BC
    Hii ni picha iliyotolewa ya Nyangumi aina ya Humpback ambaye alikumbwa na maji na kutupwa kwenye ufukwe wa bahari ya Pasifiki kwenye eneo l...
  • Kikwete, Charity Begins at Home!
    President Jakaya Kikwete Pea...
  • Kweli binadamu si chochote wala lolote, wamkumbuka huyu?
    Walioko madarakani mkiabudiwa kama miungu au sanamu kumbukeni vijana hawa hata baba zao  ambao maiti zao zinaoza jangwani. Ungewaambia...
  • Pinda kulia hakutoshi, awajibike
    INGAWA kilio cha Waziri Mkuu, Mizengo Peter Kayanza Pinda, kinaonekana kuyeyusha hasira za Watanzania kwa muda, kuna haja ya kudodosa zaidi....
  • Hawa si wachungaji bali ni fisi na mbwa mwitu
    KUMEZUKA mtindo mchafu na wa rejareja wa baadhi ya wachumia tumbo na matapeli kumtania hata kumtumia Mwenyezi Mungu kufanya utapeli na ujamb...

Followers

Blog Archive

  • ►  2025 (84)
    • ►  December (1)
    • ►  November (11)
    • ►  October (9)
    • ►  September (7)
    • ►  August (12)
    • ►  July (8)
    • ►  June (7)
    • ►  May (5)
    • ►  April (4)
    • ►  March (6)
    • ►  February (8)
    • ►  January (6)
  • ►  2024 (92)
    • ►  December (7)
    • ►  November (4)
    • ►  October (11)
    • ►  September (9)
    • ►  August (7)
    • ►  July (9)
    • ►  June (9)
    • ►  May (8)
    • ►  April (7)
    • ►  March (6)
    • ►  February (7)
    • ►  January (8)
  • ►  2023 (118)
    • ►  December (10)
    • ►  November (10)
    • ►  October (9)
    • ►  September (2)
    • ►  August (4)
    • ►  July (6)
    • ►  June (9)
    • ►  May (8)
    • ►  April (18)
    • ►  March (13)
    • ►  February (9)
    • ►  January (20)
  • ►  2022 (208)
    • ►  December (14)
    • ►  November (14)
    • ►  October (20)
    • ►  September (20)
    • ►  August (12)
    • ►  July (25)
    • ►  June (22)
    • ►  May (18)
    • ►  April (13)
    • ►  March (18)
    • ►  February (18)
    • ►  January (14)
  • ►  2021 (323)
    • ►  December (23)
    • ►  November (34)
    • ►  October (26)
    • ►  September (13)
    • ►  August (19)
    • ►  July (21)
    • ►  June (29)
    • ►  May (25)
    • ►  April (23)
    • ►  March (43)
    • ►  February (29)
    • ►  January (38)
  • ►  2020 (290)
    • ►  December (33)
    • ►  November (37)
    • ►  October (28)
    • ►  September (35)
    • ►  August (31)
    • ►  July (26)
    • ►  June (17)
    • ►  May (21)
    • ►  April (18)
    • ►  March (15)
    • ►  February (17)
    • ►  January (12)
  • ►  2019 (160)
    • ►  December (8)
    • ►  November (7)
    • ►  October (12)
    • ►  September (9)
    • ►  August (27)
    • ►  July (18)
    • ►  June (18)
    • ►  May (11)
    • ►  April (11)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (14)
  • ►  2018 (162)
    • ►  December (12)
    • ►  November (6)
    • ►  October (13)
    • ►  September (10)
    • ►  August (20)
    • ►  July (9)
    • ►  June (14)
    • ►  May (9)
    • ►  April (16)
    • ►  March (21)
    • ►  February (17)
    • ►  January (15)
  • ▼  2017 (306)
    • ►  December (20)
    • ►  November (23)
    • ►  October (20)
    • ►  September (26)
    • ►  August (31)
    • ►  July (31)
    • ►  June (34)
    • ▼  May (26)
      • Forgery is boil but not goosebumps
      • Magufuli: Mwalimu wa maendeleo Afrika?
      • Kijiwe kwenda ikulu kumpongeza rais
      • Magufuli Amtumbua Kamishina Mkuu wa Polisi
      • Graves, Magufuli, mineral sands and Muhongo
      • Makaburi, makinikia, Magufuli na Muhongo
      • Eti Dom ni the big city of Bongo? Wow!
      • Wiki hii nimekumbuka Botswana baada ya Tanzania ku...
      • Leave Tanzania out of Kenya’s upcoming election
      • Nani anakumbuka mauji ya kipumbavu kama ya Mvumi?
      • Kijiwe kukamata mali za mafisadi
      • Handcuffed President: Fall from Grace
      • Kuuawa Lowassa na Magufuli Gwajima achunguzwe
      • Fisi anapochunga kondoo wa Bwana
      • Is Trump’s move an accidental suicide?
      • Magufuli asipuuzie shutuma za Kenya dhidi yake
      • Kijiwe: Wachunaji Wachague Dini au Siasa
      • TPSF mnamuonea Magufuli bure
      • Njaa Inapopanda Kichwani PhD Hugeuka Bullshit
      • Mwakyembe Kukalia Ripoti ya Clouds Ni Kujidhalilisha
      • Kijiwe Chataka Vyeti Vya Wanasiasa Vihakikiwe Pia
      • Vyuo vya kitapeli vifutwe haraka
      • Baada ya kutemwa kwa kughushi: Mlevi kuvamia siasa
      • This Clip Will Offend Anybody That Knew and Loved ...
      • Kughushi: Viongozi wa umma wachunguzwe
      • Kijiwe chastukia zoezi la kuhakiki vyeti vya kibas...
    • ►  April (24)
    • ►  March (20)
    • ►  February (28)
    • ►  January (23)
  • ►  2016 (269)
    • ►  December (22)
    • ►  November (21)
    • ►  October (22)
    • ►  September (15)
    • ►  August (12)
    • ►  July (27)
    • ►  June (24)
    • ►  May (23)
    • ►  April (29)
    • ►  March (26)
    • ►  February (27)
    • ►  January (21)
  • ►  2015 (399)
    • ►  December (34)
    • ►  November (24)
    • ►  October (22)
    • ►  September (34)
    • ►  August (29)
    • ►  July (37)
    • ►  June (22)
    • ►  May (32)
    • ►  April (35)
    • ►  March (46)
    • ►  February (47)
    • ►  January (37)
  • ►  2014 (502)
    • ►  December (47)
    • ►  November (49)
    • ►  October (47)
    • ►  September (37)
    • ►  August (40)
    • ►  July (42)
    • ►  June (30)
    • ►  May (35)
    • ►  April (47)
    • ►  March (44)
    • ►  February (39)
    • ►  January (45)
  • ►  2013 (399)
    • ►  December (37)
    • ►  November (27)
    • ►  October (31)
    • ►  September (26)
    • ►  August (33)
    • ►  July (39)
    • ►  June (28)
    • ►  May (40)
    • ►  April (44)
    • ►  March (39)
    • ►  February (26)
    • ►  January (29)
  • ►  2012 (597)
    • ►  December (27)
    • ►  November (26)
    • ►  October (27)
    • ►  September (30)
    • ►  August (47)
    • ►  July (94)
    • ►  June (86)
    • ►  May (119)
    • ►  April (83)
    • ►  March (23)
    • ►  February (17)
    • ►  January (18)
  • ►  2011 (261)
    • ►  December (20)
    • ►  November (19)
    • ►  October (20)
    • ►  September (21)
    • ►  August (27)
    • ►  July (12)
    • ►  June (15)
    • ►  May (20)
    • ►  April (27)
    • ►  March (32)
    • ►  February (24)
    • ►  January (24)
  • ►  2010 (205)
    • ►  December (25)
    • ►  November (23)
    • ►  October (23)
    • ►  September (23)
    • ►  August (17)
    • ►  July (13)
    • ►  June (12)
    • ►  May (10)
    • ►  April (18)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (16)
  • ►  2009 (163)
    • ►  December (19)
    • ►  November (14)
    • ►  October (11)
    • ►  September (6)
    • ►  August (12)
    • ►  July (9)
    • ►  June (11)
    • ►  May (20)
    • ►  April (22)
    • ►  March (14)
    • ►  February (12)
    • ►  January (13)
  • ►  2008 (191)
    • ►  December (12)
    • ►  November (11)
    • ►  October (14)
    • ►  September (15)
    • ►  August (16)
    • ►  July (23)
    • ►  June (10)
    • ►  May (19)
    • ►  April (16)
    • ►  March (19)
    • ►  February (17)
    • ►  January (19)
  • ►  2007 (33)
    • ►  December (13)
    • ►  November (20)

About Me

My photo
View my complete profile

Travel theme. Powered by Blogger.