The Chant of Savant

Wednesday 21 January 2015

Kijiwe chajadili uzabazabina wa escrew


 
          Baada ya kuanza kushuhudia mazingaombwe juu ya kuwafikisha wa pilato majembuzi ya esrew, Kijiwe kimekaa kama kamati kujaribu kupitia nini kifanyike na nini kimepungua. Kijiwe kinatamka wazi kuwa waishiwa walikosea kukilinda kigenge chao na lisirikali lake. Maana kwa mchoro ulivyo, hata huyu dingi mwenyewe, kama ukweli utawekwa wazi hanusuriki.
          Kapende anaingia akiwa ameshika gazeti la Tell It Today. Anaonyesha kichwa cha habari kisemacho kuwa mafisadi wa escrow wamefikishwa kwa pilato.
           Anasema, “Mnaichukuliaje hii ya kuwapeleka wapokeaji tena vidagaa kwa pilato wakati mapapa yakiendelea kukata maji?”
          “Wallahi mie naona huu ka usanii ntupu. Yawezekanaje walopokea njuluku waonekane wakosefu kuliko walioiba na kuwakati huo nshiko yarabi? Hakuna waliponchosha kama kusema eti na Mizengwe iliyopinda hajatenda kosa wakati alitaka hata kuwasafisha hawa wenzake.” Mpemba anajibu kwa hasira na mstuko.
          Kabla ya Mpemba kuendelea Mijjinga anapoka mic na kuzoza, “Kuna jamaa yangu anayefanya kazi benki amenitonya kuwa alimuona Rugamalayer akiweka njuluku nyingine kwa ajili ya mkuu fulani ili atumie kwenye uchakachuaji.”
          “Si useme tu kuwa huyu mdingi ni wa Mizengwe aliyeonekana kufumbia macho ujambazi huu wa mchana kwa vile anafaidika nao kibinafsi na kichama,” anazoza mzee Maneno huku akibwia kahawa yake.
          Anaangalia huku na kule na kuendelea, “Jamaa yangu amesema kuwa watu wa karibu na habithi huyu walintonya kuwa huwa anawasiliana kwa email na Njaa Kaya kiasi cha kumuamuru la kufanya na la kuacha.” Mpemba anazidi kumwaga tama.
          Tunaangalia tukishuku kidogo, maana kijiweni wakati mwingine hata kamba hupita ilmradi kunogesha maongezi.
          Mipawa anakula mic, “Mie hili la kuwa na email ya Njaa Kaya au la halinishughulishi. Kinachonishangaza ni kuona wanashitakiwa vidagaa tu.”
          Sofia Lion Kanungaembe leo anaingia mapema. Anakula mic, “Hivi nyie watu mfanyiwe nini mridhike? Mbona mtukufu keshaamuru Takokuu wawafikishe hawa watuhumiwa kwa pilato? Ushahidi unao kwenye gazeti lako.” Anaongea huku akimtazama Kapende anayeamua kumuingilia Sofia na kusema, “Urongo mtupu.  Mbona hakumuokoa nshomile mwenzake porofweza Anne Tiba?”
          Kabla ya Kapende kuendelea, Profesa Msomi Mkatatamaa anakwanyua mic, “Umenikumbusha haya mambo ya ukabila uchwara. Umeona kuwa wengi wa waliosuka na kupokea njuluku hizi ni nshomile watupu? Yupo KyaBK, Bakwekwea, Tiba, Ki-Soft, Luang-isha, Mujuliiizi and others.” Anapiga chafya kuonyesha kuwa hii si halali na kuendelea, “Bado tunangoja kujua magabacholi waliokatiwa na Harbinder. Maana inavyoonekana wizi huu unawanufaisha watu wa chama kimoja, kabila moja na dugu moja kama sikosei.”
          Kanji anamkata jicho Kapende na kunong’ona kitu na Sofi na kusema, “Dugu yangu veve chukia hindi sana hadi nahusisha kila baya natendeka hapa. Kama Harbinger Napata juluku basi ni yake na mke na toto yake lakini si ya hindi yote. Yeye siyo kama haya nagawa juluku hovyo hovyo.”
          “Kanji usemayo kweli. Hindi hapana gawa pesa hovyo hovyo kwa Swahili bali yeye chukua pesa yake weka Bombei kusaidia dugu yake na siyo Swahili.” Anachangia Mchunguliaji.
          “Mie nadhani gabacholi aihitaji kutembeza njuluku hasa ikizingatiwa kuwa anaombwa na wakubwa asimamie jinai yao. Mara hii mmesahau skandali ya Chavda! Hawa jamaa wanaletwa na wakubwa wasiotaka kujulikana. Maana wanajua wakiwashikirika waswahili wanaweza kuwachoma au kuwataja mambo yakizidi wakati gabacholi anachukua pasi yake na kurejea zake kwao au kwa Mama na mambo kwisha.” Anasema Msomi huku akibonyeza kisimu chake.
          Mgosi Machungi na mheshimiwa Bwege leo wamechelewa. Ndiyo wametia timu kitambo na hivyo hawajaronga. Wana unywaunywa wa kuronga.
          Mgosi Machungi anakamata mic na kumwaga uchungu, “Kwei usemayo Msomi. Hizi dii hapa kayani inaonekana zinachongwa na dugu moja yaani nshomie. Usitikumbushe wezi wengine akina Kyomuhendoo, lukazakaza, Mwesigwa, Maegesi na wengine wengi toka kanda hiyo hiyo.”
          Mheshimiwa Bwege anampoka Mgosi mic na kuongeza orodha ya majembuzi wetu wa escrew.
          “Nakubaliana nawe Mgosi. Hii mijizi inaonekana kutoka sehemu moja. Inafaa ichomwe moto kama siyo kutundikwa shamba mchana kweupe ili liwe somo kwa wengine. Hata hivyo nani amhukumu nani wakati hawa tunaowalilia nao ni washirika na washikaji wa mibaka hii? Unadhani ni kwanini munene anajifanya kutomhusu hadi anatuwekea viporo vya ufisadi. Anajua akiwawasha nao wanamuwasha na ngoma inakuwa droo au vipi?”
          Mijjinga anakatua mic na kuongeza orodha, “Umesahau nshomiee mwingine Porofedheha Sossi Muongo, Maswiswi na wengine nawahifadhi.”
          Kapende anamkosoa Mijjinga kwa kusema, “Hao siyo nshomile bali mura kaka japo wote wanatoka kumoja tena ni watani.”
          “Kwangu wote ni wale wale. Kwani kuna tofauti gani kati ya mura na murangila? Yote toto ya baba na mama moja bwana.” Anajibu Mijjinga.
          Msomi haridhishwi na mchango wa Mijjinga. Hivyo anaamua kurejea kwa upya. Anakamua mic, “Japo majina na sura zinaonyesha ni watu wa kanda moja, hakuna haja ya kuwaweka kwenye kapu moja. Hata hivyo, nakubaliana nawe kuwa kuna patern ya ukabila hapa. Maana ukiona Were-ma na hata Nkwingwa Ngereja na Chengee wote wanatoka kanda hiyo hiyo. Sijui kuna tatizo gani hapa.”

Kijiwe kikiwa kinango si ukapita msafara wa mdingi. Acha tuurushie mawe na matusi kabla ya kutawanyika kuepuka kuwaumiza ndata ambao wangejipendekeza kuja kututia adabu!
Chanzo: Tanzania Daima Januari 21, 2015.

No comments: