The Chant of Savant

Sunday 27 March 2011

Madege VS ubakaji Libya



Picha kwa hisani ya BBC


Taarifa za hivi karibuni zimeripoti kuwa imla wa Libya Muamar Gadaffi ameanza kutumia mbinu haramu kupambana na wapinzani. Ubakaji ni silaha ambayo ameigundua na kuanza kuitumia dhidi ya watu wake. Hii ni baada ya kudhoofishwa na mashambulizi ya washirika ambayo yamesababisha Gadaffi kupoteza miji yote aliyokuwa ameiteka hivi karibuni.
Madai ya ubakaji kutumika kama silaha yamethibitishwa na madaktari Suleiman Refadi na Abdul Rahim Aquila Najib waliowatibu wahanga wa jinai hii.

Jinai hii ilifichuka baada ya Iman al-Obaidi aliyebakwa na watu zaidi ya watano kujitokeza na kumwaga mtama.
Ingawa Gadaffi alikuwa akiwalaumu al-Qaeda kuwa nyuma ya upinzani, ameanza kutumia mbinu za al-Qaeda. Amekuwa akiwahimiza walibya kujitoa mhanga kwa kuwa taifa la kiislamu limevamiwa.
Baadhi ya maiti za wanajeshi wa Gadaffi zilizopatikana kwenye mji wa Ajdabiya zilikutwa zikiwa na kondomu pamoja na viagra.
Je mwanzo wa mwisho wa Gadaffi umewadia?

3 comments:

Unknown said...

ULIDHANI Gadaffi ni mzima Waarabu na waislamu ni wabakaji kwa asili. Hata mtume wao alikuwa bakaji.

Jaribu said...

Marekani kwa Wakristo kuna wabakaji wengi tu. Hebu acheni haya mambo ya kijinga. Mimi sio mtu wa imani, hasa kwa hizi dini za Abraham/Ibrahim, lakini sio busara kutukana dini za wenzako. Hiyo inaleta malumbano yasiyo na msingi.

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Jaribu uko sahihi. Watu wengine wanachanganya mambo. Hakuna sababu ya kuhukumu watu wote kwa kutumia udhaifu wa mtu mmoja au kundi la watu. Bayybayyz-Mamma umekosea sana na hasa umewakosea waislamu. Next time ukirudia nitafuta comment yako.