The Chant of Savant

Thursday 12 February 2015

Zuma Aonja Joto ya EFF azomewa

MAIN-PHOTO(4).jpg
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini alijikuta kwenye maji mazito akizomewa na kushinikizwa alipe fedha za ujenzi wa makazi yake kijijini Nkandla. Kadhia hii ilimkuta wakati akitoka hotuba yake ya mwaka (The State of Nation) ambapo chama cha Economic Freedom Fighters  (EFF) cha Julius Malema kilimnyima fursa ya kuhutubia taifa hadi spika wa Bunge Beleka Mbete akaingilia kumuokoa kwa kuamuru EFF watolewa nje ya ukumbi wa bunge. Kuona hivyo,cha cha upinzani cha  Democratic Alliance (DA) kiliamua kupinga kitendo hicho. Baada ya Spika kushikilia msimamo wake DA waliamua kususia hotuba ya Zuma ambalo ni pigo kubwa kwake kama rais wa nchi. Kwa ufisadi ulivyo nchini mwetu, natamani wapinzani wamtolee uvivu Kikwete hivi.


2 comments:

Anonymous said...

Africa hiyo Watu kulindana kisa kupewa madaraka

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Anon umesomeka. Afrika ndivyo ilivyo. Kwanini tusiibadili sasa?