The Chant of Savant

Tuesday 10 March 2015

Kijiwe Chahoji Prof Muongo Kutofikishwa Kamati ya Madili

          Baada ya Nshomile Annae Kajua Mlo kuchemsha kwa kupayuka, Kijiwe kimeamua leo kumshukia na wale wote waliolewa ulaji kama yeye. Tunawataka waache upuuzi wa kuturingishia njuluku walizotuibia. Wanakijiwe wamehuzunishwa na kushangazwa na kauli kuwa milioni kumi hata kama ni za madafu kutumika kununulia mboga utadhani Nshomile Annae ni tembo!
          Mbwa Mwitu leo analianzisha. Anakamua mic, “Wakuwa mmesikia mpya ya Porofwedha Annae Kajua Mlo Tiba na mboga ya madafu milioni kumi?”
Mgosi Machungi anajibu kwa dharau ya wazi akisema, “Huyo nshomie kalewa njuuku kiasi cha kusahau kuwa kuna wachovu wanaishi kwa roho mtakatifu wakati wao wakiishi kwa roho mtakakitu.
          Mpemba anampoka mic na kuchonga, “Yakhe nadhani huyu bibi si nzima. Apaswa apelekwe Milembe kuchunguzwa akili zake maana haziko sawa ati. Au kishaingiliwa na popobawa huyu wa kuibia umma na kutembeza njuluku?”
          Kapende anakamua mic, “Hivi huyu sister amesomea wapi hiyo PhD au ni zile za gagulo? Nadhani kama usemavyo, huyu popo bawa wa escrew kesha-m-screw maana kumpa mtu bilioni na ushei bila kutoa huduma ya nguvu si rahisi.”
          Sofia anamkata jicho Kapende na kula mic, “Kapende hiyo kashfa. Kwani una ushahidi wa usemayo?”
          Kabla ya Kapende kujibu Mheshimwa Bwege anamchomekea Sofia.anasema, “Da Sofi siku hizi umegeuke pilato au mwanasheria. Maana akiongea mtu wewe unataka ushahidi wewe unao wa huo ushahidi unaotaka?”
          Kabla ya Sofia kujibu Mbwamwitu anachomekea, “Huyu nadhani ni mshakaji wa Rugemalayer hasa ikizingatiwa kuwa ni open cheque hata kama ameisharamba chumvi kibao. Kwani ni kosa gani wakikatiana?”
          “Veve siku zote sema Tibajuka katia Rugemalayer. Hii katia ndiyo nini? Kama nakata yeye si yote nakatika na umia sana?”
          Kijiwe hakina mbavu jinsi Kanji anavyobukanaya uswa na kujifanya haujui wakati anaumanya kuliko hata wajalaana wengine toka mikoani kama Stivi Wahasira.
          Mijjinga aliyekuwa kauramba huku akiwa bize akisoma tabu lake kubwa anaamua kula mic, “Mie huyu hanihangaishi kwa vile ameishajivua nguo. Nashangaa kwanini profedha Sauce Pie Muongo naye hafikishwi au kuna watu na viatu?”
          Msomi Mkatatama alieyekuwa akim-email mshikaji wake wa Washington anakula mic “Muongo haguswi. Akiguswa na muungu wao utaguswa. Hivyo, ukimburuza Muongo kwa pilato na mkulu Njaa Kaya ataburuzwa hata kama hatahudhuria kwa sasa ambapo ameshikila ulaji. Ila siku moja yeye, Tunituni Ben wa Kiwila na baba Ruksa wataburuzwa kwa pilato kama akina Freddie Chilubha. Nani anapenda Muongo apelekwe mbele ya Tume ya Madili? Je akibwabwaje kama Anna unategemea kutakuwa na usalama kwa bosi hasa ikizingatiwa kuwa mshiko wao ulikuwa mkubwa kiasi cha kupakia kwenye mabehewa? "
          Ankunywa kahawa yake na kuangalia huku na kule. Anamgeukia Mipawa na kusema, “Kanda ya Maziwa ina matatizo gani? Maana ukiangalia wajivuni wote wanatoka kule. Mzee wa Vijisenti, kule, Rugemalayer wa vijisenti vya ugolo, kule, Profedha Muongo na Tiba-Ijuka kule na hata Shimon Kisena wa UdA kule kule kunani?”
          Kabla ya kujibu Mzee Maneno anachomekea, “Umesahau kuwa na Ngeleza na Kadamage wa Buzwagi nao wanatoka kule?”
          Mijjinga hangoji. Akamua mic, “Hata habithi Mabinha aliyeuawa na wachovu wenye hasira baada ya kuiba ardhi yao naye alikuwa akitokea kule bila kusahau waziri Mashere bingwa wa kutukana mabalozi.  Kanda yetu tukufu imeingiliwa bila shaka. Lazima kutakuwa na tatizo kule si bure.”
          Mgosi anaamua kumpa mwenzie ushauri. Anakula mic, “Nadhani mnahitaji kutambikiwa ili kuondoa hivyo vitu vinayowaingia watu hawa vinginevyo mtaingiiwa wengi.”
          Kabla ya kuendelea Mijjinga akula mic na kumpinga akisema, “Mgosi angalia hiyo lugha. Huna haja ya kututukana kuwa tumeingiliwa kana kwamba una ushahidi kama da Sofi. Kwani nyie Lushoto hamjaingiliwa na kirusi cha vitoto kutaka ukuu?”
          Msomi baada ya kuona kuwa utani unaanza kuchukua nafasi tena, anaamua kula mic, “Japo tumekuwa tukiwaandamana hawa maprofesa uchwara waliopata elimu wakaisaliti na kujivua nguo, nadhani tunapaswa kumuuliza mkulu mantiki ya kuhangaika na dagaa huku akilala kitanda kimoja na mapapa yenyewe yaani Rugemalayer na Harbinger Seti Sing. Sijui ni kwanini anatumia sheria kwa ubaguzi na upendeleo au anaogopa wasitaje wazi wazi kiasi alichokatiwa yeye na watu wake?”
          “Msomi hapa wankuna kweli kweli. Hata mie ndhani kama huyu bwana ataka aonekane nsafi au hajashiriki huu utwahuti basi awafikishe kwa pilato hawa wenzake wawili haswa.” Mpemba anajibu kwa usongo huku akitupa kipisi cha sigara kali aliyoipoka kwa Mgosi.
          Msomi anacheka kidogo na kuendelea, “Hakuna kitu kimeniacha hoi kama profesa mzima kupayuka hata bila kufikiri. Hivi unawezaje kuwaambia wachovu kuwa unatumia milioni kumi kununua mboga utadhani mboga hiyo ni ya bangi au almas kama siyo lulu na rubi? Wakati mwingine kusoma hakuondoi upumbavu na ujinga wa mtu. Maana hili halikutaka hata washauri kujua madhara yake. Hata hivyo, utamcheka nani umwache nani wakati mkulu mwenyewe ndiyo kiongozi wa maprofesa wenzake kwa kupayuka?”
          Kijiwe kikiwa kinanoga si likapita shangingi limembea porofwedheha Nshomile na Rugemalayer wasijue tulikuwa tunawangoja kuwatia adabu! Kama siyo ndata kutupiga mibomu ya michozi mbona tungewafanya kitu mbaya!
Chanzo: Tanzania Daima Machi 11, 2015.

No comments: