The Chant of Savant

Monday 28 May 2012

'Misaada' toka kwa wahindi hadi lini?

Spika wa Bunge Anna Makinda akipokea msaada toka kwa mkrugenzi wa GF Truck & Equipment Ltd, Imrani Karmali huku huku mwenyekiti wa kampuni hiyo Mehboob Karmali akifaidi kupigwa picha na spika.
Ni aibu kwa nchi yetu kuendelea kuwa tegemezi. Yaani tumefikia pabaya kiasi cha hata watu tuliowakaribisha wakiwa maskini kututumia kwa kisingizio cha misaada! Hawa ndugu wa Karmali wanalipa kodi vilivyo au ndiyo hivyo wanajikaribisha kwa wakubwa ili kupitisha mambo yao? Inashangaza kuona nchi yenye raslimali lukuki kuendelea kuwa Matonya. Ingawa kinachoonekana hapa ni msaada kwa ajili ya ujenzi wa barabara za Njombe, ukweli ni kwamba ni zaidi ya hicho. Kesho utasikia akina Karmali hawaguswi na yeyote hata wafanya madudu gani.  Huku ni kuuz anchi na kuwekwa mfukoni. Kwanini nchi iwasamehe hao hao kodi za mabilioni ya fedha lakini iendelee kuwaomba eti waisaidie? Akili mbovu bila shaka na za kifisadi. Shame on you viongozi wetu!

No comments: