The Chant of Savant

Tuesday 29 May 2012

Muungano ukivunjika Visiwani patatosha?


Kumekuwapo na ushabiki hasa kutoka Visiwani kuvunja Muungano wakidai wanataka wawe huru kana kwamba hawako huru. Je kinachotakiwa ni uhuru au kikundi cha watu fulani kuwatumia watu wa kawaida wasiojua agenda zake za siri kufanikisha kuvuruga nchi na kutwaa madaraka? Je tatizo la Zanzibar ni Muungano au kuangalia mambo vibaya? Wengi tunajiliza: Ni kwanini harakati za kudai kuvunja Muungano zimekuja sambamba na madai ya kujitenga na Kenya kwa kundi la kigaidi liitwalo MRC au Mombasa Republic Council? Wakati tukitafakari maswali haya tujaribu kujiuliza swali moja kuu. Je Muugano ukivunjika visiwa vya Zanzibar na Pemba vitatosha kubeba idadi ya watu wa Visiwani waliozaliwa na kujazana bara? Je tutegemee Comoro nyingine ambayo itahitaji pesa na majeshi yetu kwenda kulinda amani? Think Twice.

No comments: