The Chant of Savant

Sunday 27 May 2012

Utumwa mwingine karne ya 212

Ingawa kila chombo cha habari kina uhuru wa kuwa na sera yake, vyombo vyote vya habari huunganishwa na kanuni moja kuu, kuandika ukweli kama ulivyo. Inashangaza gazeti linaloendeshwa kwa kodi ya watanzania kuanza kuandika upuuzi na uzushi ambao hata ndege pamoja na udogo wa ubongo wake, hawezi kuuuamini. Huku ni kuchezea akili za watu hasa wasomaji na waandishi pia. Wanafanya hivi ili wapate kitumbua chao na kuwaridhisha wakubwa wao wapumbavu kama wao. Namna hii taaluma ya uandishi wa habari inaanza kugeuka uchangudoa wa kiakili.

1 comment:

Anonymous said...

Mzalendo linaendeshwa kutokana na kodi za watanzania kivipi, au unamaanisha ruzuku ambayo vyama vya siasa hupewa kutokana na kuwa na Wabunge!!? Basi hata TANZANIA Daima nalo linaendeshwa kwa kodi zetu kama ni hivyo.