The Chant of Savant

Monday 30 April 2012

Kipi kitatumika kuunda baraza la mawaziri?


Kibonzo hiki licha ya kuchekesha kinaonyesha mawazo ya watanzania walio wengi hasa wakubwa. Hivi kama wakubwa tena wasomi wako hivi,  hao akina Mimi ni Maimuna hali ikoje? Je Baraza la mawaziri linalongojewa kwa udi na uvumba litaundwa kutegemea ushirikina, ushirika, udugu, kujikomba, sifa, kulindana, usanii au business as usual? Time will surely tell.
Muhimu usishangae kuwakuta ambao hukutegemea na kutegemea kuwakuta ambao uliwategemea. Hii ni CCM ambayo mara nyingi mambo yake ni yale yale. Akitoka kibaka  huyu atakuja jambazi yule. Kwa ufupi ni kwamba hakuna msafi anaweza kutokea CCM kwa sasa na kwa mfumo huu wa ufalme tunaoendelea nao. Laiti Bunge lingekuwa na mamlaka ya kumpa rais  majina ya watanzania na si wanachama wa kuteua kuwa mawaziri baada ya kuyapitisha kwa kura na kupata ushauri toka kwa wananchi! Hata  hivyo vumilieni. Danganyika ni nchi ya mazingaombwe na abracadabra nyingi. Mtafungwa kamba na mtakubali bila shaka.

No comments: