The Chant of Savant

Friday 27 April 2012

Seriously, natafuta mwekezaji anunue ikulu

Image Detail
Kama mtanzania ninayeambiwa nina haki juu ya nchi yangu, nimeona heri nibinafsishe ikulu yetu kwa vile imegeuka yao na haiingizi faida. Nafanya hivyo baada ya kusikia maoni ya gwiji la uwekezaji Benjamin Mkapa aliyesema kuwa waliamua kubinafsisha mali za umma kwa vile zilikuwa haziingizi faida zaidi ya hasara. Hivyo nami naona tuanze na ikulu kwa vile, licha ya kuwa chaka la mafisadi, imekuwa ikiliingizia taifa hasara  hasa kutokana na wakazi wa mle kufanya watakavyo bila kuguswa. Wanapenda sana matumizi makubwa na kuzurura hata bila kujipa nafasi ya kufikiri na kufanya kazi yoyote zaidi ya uharibifu. Hivyo natangaza rasmi kuwa kama mtanzania nataka nipewe haki yangu ambayo ni  kubinafsisha ikulu ilil angalau tupate watu wenye akili ili tutie akili.

No comments: