The Chant of Savant

Wednesday 4 April 2012

Mbunge ‘Chichim’ alivyomwaga mitusi Arumeru

LEO tumeamua kukaa kikao cha wanakijiwe wote ili kumjibu chizi mmoja aitwaye mheshimiwa japo sisi si machizi. Kama mkituona machizi shauri yenu. Tunaweza kuonekana walevi kutokana na kunywa kahawa na shida nyingi lakini bado si machizi kama Leavingstorm Lushinde chizi nambari wani wa Chama Cha Machizi (CCM).

Mie kama mwenyekiti naanzisha mjadala.
Nilikohoa kidogo na kuanza, “Waheshimiwa wanywa kahawa, kwanza naona mmechukia kutokana na matusi yalivurumishwa na mbunge wa ndugu yetu na rafiki yetu Mbwamwitu ambaye ni mpiga kura wa jimbo la Mtela,”

Wote kwa pamoja wanatikisa vichwa wakiashiria kukubaliana na pwenti yangu. Naendelea, “Mie leo si msemaji bali mwezeshaji. Hivyo naomba rasmi nifungue kikao hiki kitukufu ambacho licha ya kumjadilli huyu bwana kitatoa maazimio.”

Mbwamwitu anaamsha mkono na ninamruhusu arambe mic. Anaanza, “Ndugu zangu nashukuru sana kwa kuliona hili na pole zenu nimezipokea ingawa bado roho inaniuma. Hata hivyo msishangae sana. huyu jamaa kama alivyosema kweli ni chizi na aliwahi kukamatwa mara nyingi kwa makosa ya kuvuta bangi, udokozi na mazambe mengine mengi. Hivyo nina wasi wasi alipokuwa akiwekwa ndani mara nyingi, huenda lolote limemtokea na ndiyo maana anawasingizia wenzake kufanyiwa mchezo mbaya kama alivyowahi kufanyiwa.”

Kabla ya kuendelea Mchunguliaji anakula mic, “Hakuna kitu kimenikera kama jamaa kuwaita wenzake mashoga kiasi cha kutufanya tuamini yeye ndiye. Halafu anawatukana watu eti wana mimba, kwani mama yake alimzaa bila kubeba hiyo mimba? Huyu jamaa inaonekana anawadhalilisha akina mama akiwamo mama yake wallahi,”

Wakati Mchunguliaji akimwaga usongo wake, Mzee Kidevu anadandia, “Huyu jamaa kweli chizi nimeamini. Kwanza, huyu chizi kihiyo hajui hata Kiswahili. Mnakumbuka aliposema eti dokta Silaha aliposema ana uchungu na nchi hii eti alimshagaa mwanaume anawezaje kuwa na uchungu? Kwani uchungu ni wa kuzaa tu?”

Mara Mipawa anachomekea, “Jamaa ana ugomvi na mimba huyu. Huenda kichaa chake kinachukia mimba.”

Watu hawana mbavu wanacheka ingawa habari yenyewe si ya kuchekesha zaidi ya kuhuzunisha. Mara Mbwamwitu anakatua mic tena, “Basi mwenzenu nina uchungu naye. Laiti nikikutana naye kwenye kiza ataipata hiyo mimba anayowapa wenzake. Huyu inaonakana anataka kupewa mimba.”

Msomi Mkatatamaa aliyekuwa kimya muda wote aliamua kutia guu, “Jamani msijipasue vichwa. Kimsingi, Lushinde alichofanya ni kuthibitisha madai ya siku nyingi kuwa chama chake kimeishiwa sera. Kilianza na usanii, kikachemsha. Kilidandia uongo, kimechemsha. sasa kimeona haitoshi kimedandia matusi.” anavuta kombe lake na kubwia kahawa na kuendelea, “Matusi ya Lushinde kimsingi si ya kuwahuzunisha wala kuwalenga wapinzani bali chama chake na viongozi wake waliokuwa wakichekelea alipokuwa akitumia mdomo wake kutoa haja kubwa. This annoyed me to death so to speak.”

Anakatua kashata na kuendelea. “Kila mtu kwake shoga. Inakuwa vigumu kujua huyu bwana kwanini anapenda sana ushoga na kuchukia mimba,” Msomi Mkatatamaa alizidi kuchanja mbuga kwa taaluma na busara zake baada ya wazee kumwambia apunguze hasira kuongea kikameruni hata kama alikuwa akiongelea habari za mkameruni mhishimiwa.

Aliendelea, “Hakika wazazi wake, mke wake, watoto wa Mkameruni Lushinde wamekula hasara. Anavyowatia aibu sina hamu. Hata yule mheshimiwa Sonko wa Nonihino huvuta bangi, kunywa gongo na kupayuka lakini hajawahi kuona mdomo choo kama wa Lushinde. Maana kama sera basi chama chake cha Matusi (CCM) kimepata mpiga debe. Ila itakuwa muujiza kama walengwa wa makombora ya Lushinde wasipomfikisha mhakamani. Sisi kijiweni ukimtukana mjumbe au mwenyekiti tunasema umetukana kijiwe kizima. Hivi Lushinde anapotukana wabunge si kama anatukana jimbo zima?”

Nami sikujivunga. Nilichomekea, “Namkaribisha Lusenge sorry Lushinde aende Kijiweni Mwenge akapige debe au akiweza aende zake gerezani akauze unga. Namshauri Lushinde aje nimuonyesha picha niliyopiga na mzee Matonya ili aone tofauti ya masikio yaliyotobolewa kimila na haya ya kishoga.” wanakijiwe hawana mbavu.

Mgosi Machungi naye hataki kikao kiishe bila kukifunga. Anakula mic, “Mie sikujua kuwa kumbe Ushinde na wenzake wamechanjwa makalioni tena na poofesa Maji Mafupi. Angejua aipotoka kwao N’koogwe akaja Ushoto kue Irente kutafuta wachawi kioo chake kiivunjika akarudi kwa haraka.”

Mpemba “Yaelekea huyu jamaa ashafungwa sana na kufanyia nchezo mbaya kiasi cha kudhani kila aendaye jela afanyiwa nchezo kama alofanyiwa,” kijiwe hakina mbavu.

Mchunguliaji. Msomi mkatatamaa anaamua kurejea ili kutoa usomi na busara zake. Tunamheshimu na kumtegemea sana maana huwa hana mdomo mchafu ingawa leo ameudhika kiasi cha kuvunja mwiko na kutoa lugha ya ukali. Anakatua mic, “Nilipokuwa masomoni ulaya nilizoea kusikia watu wenye midomo mibovu kama hivi wakiitwa Chiwawa yaani vijimbwa vidogo vinavyobweka sana vikimuona mtu lakini akivikaribia vinafyata mkia na kutoka mkuku,”

Anakunywa kahawa yake na kuendelea, “Kwa hiyo sitashangaa kama Chakudema hawatamchukulia hatua chiwawa huyu maana wanajua chiwawa ni chiwawa hata ukimpeleka mahakani bado hakimu atamuachia kwa vile ni chiwawa.”

Mzee Kidevu anatuacha hoi. Anasema, “Ingawa mie sijawahi kwenda Ulaya, anawajua hawa mbwa ambao Kiswahili huitwa kusiri. Hivyo, tuna bahati mbaya kuwa na mbu… samahani simalizii mwenye tabia kama za kusiri. Je, tuseme hiki ni chama cha Makusiri?

Wanakijiwe tunaangaliana kuonyesha jinsi mzee mwenzetu alivyochomekea kitu kingine kwani Kusiri na Chiwawa ingawa wote ni mbwa. Wanakutana kwenye sifa moja yaani uchizi wa kubweka bweka hovyo.

Mpemba ambaye alikuwa akibofyabofya simu yake kiasi cha kuachwa nyuma kimaongezi anastuka na kula mic, “ Yakhe mie naona kama huyu jamaa ashaingiliwa na popobawa. Maana popobawa siku zote aja wakati wa uchaguzi na apenda sana wao wa chama cha Machizi kwani naye chizi.”

Wajumbe hawana mbavu. Wakati tukijiandaa kuendelea na kikao si chizi Lushinde alipita na mshangingi wake. Tuliinuka na kumtoa nje tayari kumfanyizia ili tumpige picha na kuonyesha umma alivyo chakula. Usimwambie mtu, kuwa kweli jamaa si riziki.
Chanzo: Tanzania Daima Aprili 4, 2012.

No comments: