The Chant of Savant

Monday 23 April 2012

Rais mwenye wake wengi na mwenye nyumba ndogo nyingi yupi hovyo?


Rais Jacob Zuma akisakata ngoma ya kienyeji baada ya kuopoa jiko jipya hivi karibuni akitimiza jumla ya wake wa nne.Rahma Kharoos Kasiga aliyesababisha uvumi mwingi nchini Tanzania kutokana na kuwa nyumba ndogo ya mkubwa ambaye siku hizi amefichwa baada ya tishio la upinzani kumtumia kulipua wenye chao.
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini huwa hafichi tamaa yake ya ngono. Licha ya kuwa na wake wengi, amewahih kufikishwa mahakamani kwa kosa la kumbaka binti wa rafiki yake. Mambo yalimalizwa kinamna na Zuma akanusurika. Wengi wamekuwa wakimuandama Zuma kwa kupenda kuoa sana. Kimsingi, Zuma ni tofauti na marais wengi wa Afrika ambao hujifanya hawataki kuoa lakini wakawa na nyumba ndogo kibao. Je kati ya Zuma mpenda kuona na marais wengine wapenda vimwana hadi kuwa na nyumba ndogo nani wa hovyo zaidi?

No comments: