The Chant of Savant

Monday 30 April 2012

Marais wa kwanza wanawake wa Afrika


Kushoto ni rais Sirleaf (Liberia) akiwa na mgeni wake rais Banda (Malawi) pichani kulia.
Rais mpya wa Malawi Bi. Joyce Banda amerejea nchini mwake akitokea Afrika Kusini na Liberia. Anasema alikwenda Afrika Kusini kushukuru kwa kutunza mwili wa mtangulizi wake huku akienda Liberia kujifunza. Je ni changomoto gani inawakabili akina mama hawa kama marais? Rais wa Liberia Ellen Johson Sirleaf anasifika kwa harakati zake za kuleta amani nchini mwake. Banda anasifika kwa kuwainua akina mama hadi akaitwa mama Mandasi au mandazi kwa kiswahili. Kuna imani kuwa wanawake si wabadhirifu kama wanaume. Je tutegemee kuliona hili hivi karibuni katika nchi mbili? Tuwape shime wadhihirishe hili ili angalau wawe kichocheo cha kupata marais wengine wanawake barani Afrika.

No comments: