The Chant of Savant

Sunday 27 February 2011

Friday 25 February 2011

Angalia wenye utu na akili na si mafisi wetu

WASOMAJI WANGU WANANISIKITISHA KUTOACHA UJUMBE LAU NUSU MSTARI.

Marie na Ollier pichani

Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ufaransa Michelle Alliot Marie ameamua kujiuzulu baada ya kugunduliwa kuwa yeye na mchumba wake Patrick Ollier walikodishiwa ndege na mshirika wa rais wa zamani wa Tunisia, Zine al Abidine ben Ali.

Wawili hawa ambao wote ni mawaziri Ollier akiwa waziri wa masuala ya uhusiano wa bunge walitenda kosa chini ya sheria za Ufaransa.

Marie angekuwa waziri wa ulinzi wa Tanzania ambapo mabomu yameua makumi ya watu wasio na hatia huenda angejinyonga ili kutubu dhambi yake.

Marie alipotakiwa kujiuzulu hakutafuta visingizio wala kuzungusha bali kukiri na kujiuzulu huku akiomba msamaha. Hili ni suto kwa mawaziri wetu kama Dk. Hussein Mwinyi ambaye kung’ang’ania kwake madaraka kumemuondolea heshima aliyokuwa akipata kutokana na kazi nzuri ya baba yake.

Wapo waliowahi kusema kuwa alikuwa akiandaliwa kuwa rais wa Zanzibar. Lakini kwa doa alilopata hili haliwezekani tena.

Mwinyi angesoma habari za wenzake ili ajifunze lau kujisuta na kujiwajibisha badala ya kungoja kusukumwa kama akina Mubarak na Gadaffi.
Bahati yake, Jakaya Kikwete, bosi wake naye amechafuka kiasi cha kukosa busara na ithibati ya kumwajibisha kwa vile roho yake inamsuta.

Wednesday 23 February 2011

Congrats Museveni on “Tsunami-like win”



Dear Mr President of Uganda Yoweri Kaguta Tibuhaburwa Museveni,

Though Iam not your voter, I come from the same background like that of your humble voters. I come from the country where voters and all hoi polloi are but sheepish beasts of burden for hoity toitty like in your country. And they like this. For playing this role is a great honour for them.

So too, we share nexus in that when you were fighting for Uganda, you had your base and support in my country. We supported you so as to punish our arch enemy Idd Amin who toppled our best friend Milton Obote. I understand. By being of the same origin politically, there are a couple things we know about each other.

I am Tanzanian by blood and water. Like Uganda, our country has been ruled by one party since independence just like your NRM has been doing though not since independence. Our good ruling party is infallible and holy so as not to be questioned or opposed. So you can see. Those accusing you of overstaying are making a grave mistake. You are not alone in this clean game of enjoying power.

I heard your opponents complaining about vote rigging! I was shocked to death. Didn’t they know that without applying this golden rule no ruler would be in power in Africa? Who is clean in East African Community that did not do the same to cling unto power? Let he be the first to cast a stone. Kimya!

For reminder, as a precedent, we did just this two months ago in Tanzania. You know what happened? Our money was stolen in the name of charade known as elections. The good thing is: elections were true and fair simply because the ruling junta won thanks to this science of duplicating and multiplying votes.

Therefore, it must be underscored. Rigging is not a crime in Africa. It is but a claim. Just like nepotism, corruption, cronyism, nihilism, rigging will be glorified by seating-duck-like rulers whose actions are only seen in rigging and robbing our treasury. You are not among or one of them.

Mr President, you should not listen to opponents’ frog-like noises. They goofed and thought that voters can decide who should rule them. The role of voters is to humbly vote; but not to question the results even if they are cooked or their voters stolen. First of all, president cannot steal pieces of papers. Such president must be stupid and a dog.

Do you remember this quote of yours you made just short time before elections? You said thus: ““I like my cows better than this State House, but no one is right to take over. I cannot live the country to these time wasters. Change from what? From one weakness to another weakness? This is not a beauty contest. 2016 shall be decided according to the strength of Africa.” So those daydreaming that this is your last term in office should think twice.

If an individual, thanks to abusively using the power he stole from citizenry can tamper with the constitution to remain in power, what is there to boot him out of the very power, Pieces of papers otherwise known as votes? Dare you not to day dream that power-hungry wolves will let power go without going to Tahrir square. The good thing is. Mr President you are not among or one of them.

First of all, the so-called voters are ignorant and confused thanks to hell on earth they are put in.

This coupled with intimidation, manipulation, gagging the media or buying it help in elections. And when such impetuses are used you declare elections free and fair. Those who oppose or support opposition’s claims of rigging just brand them the enemies of national security. Don’t they know that national security is all about big men and their cronies to milk the country?

Another thing, use the army and police forces to see to it that people are voting for you not just because they love you-just because they fear chaos your cronies can cause if declared a loser. The role of police and armed force in Africa except those crooks in Egypt is to see to it that the big man wins.

So too, these military guys can be used to deliver stuffed ballot boxes that favours you. When anybody tries to question their acts or presence at voting stations they beat them severely. If those opponents persist you accuse them of provoking security organs which is the hugest crime in Africa. Why should people question infallible organ of the state?

I know Mr President. You are the smartest guy I have ever seen. Nobody except you has enough brain and constitutional right to rule Uganda. Why don’t Ugandans thanks Lord for sending them a messiah in you? My wish is that Ugandans should amend the constitution to make you king or president for life. For you have more experience than any bin-Adam in Uganda thanks to being in power for over two decades.


How could Ugandans become such stupid to think that you’d lose elections? Those doubting this should look at the constitution of electoral commission. To make sure that nobody is stealing your votes, you appoint your trusted friends and consigliore to see to it that you win with Tsunami-like win as it has always been.


Mr President,

I don’t want to waste your time. For you have a lot of thing to do to see to it that Uganda is overtaking the US so as to become the first super power from Africa. I know you. As you said, you won’t leave power till this becomes a reality. So too, I am sure. Once your dreams become reality, you will become the first president of East African Union so as to help it the way you did to Uganda.


Long live the king in making. We hope to see you crowned come 2016.

Dk. Mwinyi anangoja nini kung’atuka?





KUNA usemi kuwa mtoto wa nyoka ni nyoka. Wakati mwingine si kweli. Japo si kwa sura, kuna kipindi mtoto wa nyoka anaweza kuwa kijimjusi cha kawaida tu na si nyoka kama mzazi wake.

Kwa wanaokumbuka simanzi, hasara na majonzi vilivyotokana na milipuko ya mabomu huko Gongo la Mboto ndani ya muda mfupi baada ya ile ya Mbagala, tutaelewana.

Baada ya tukio hili la kizembe na kichwa ngumu vya watendaji wetu, macho na masikio yote yameelekezwa kwa Waziri wa Ulinzi, Dk. Hussein Mwinyi, ambaye silaha zake zimelipuka na kuua raia.

Wengi, kwa kujua uungwana wa baba yake, na ahadi aliyoitoa yalipolipuka mabomu ya Mbagala, walidhani siku ya pili ya milipuko Mwinyi angewajibika bila kungoja kuandikiwa tahariri na makala.

Maana aliahidi mwenyewe kuwa hili lisingetokea tena chini ya uangalizi wake. Sasa limetokea. Anangoja nini?

Kama Mwinyi ataendelea kung’ang’ania madaraka, licha ya kumwangusha baba yake anayeshimika sana, atakuwa amejiingiza kirahisi kwenye kundi la mafisadi na ving’ang’anizi.

Pili, ukiangalia idadi ya waathirika, tunaambiwa waliofariki dunia ni 39 na majeruhi 292, kama hatajiwajibisha, unagundua Mwinyi mwingine tofauti ya yule tuliyezoea kumuona.

Tatu, ikizingatiwa kuwa hii ni mara ya pili ndani ya muda mfupi, Mwinyi anajikuta hana utetezi wala sababu ya kuendelea kushikiliwa wizara inayoua wananchi.

Nne, ukirejea ahadi aliyoitoa mwenyewe bila kulazimishwa, kutoitekeleza anazidi kujiweka kwenye kundi la watu waongo na waroho wa madaraka hakuna mfano.

Tano, ukiangalia usafi, staha na faida ya kujiwajibisha kwa baba yake, Mwinyi anaonyesha dharau kwa mfano huu ambao hurudiwa kila zinapoibuka kashfa. Kwa lugha nyepesi ni kwamba anamdharau baba yake.

Kwa mwenye kujaliwa kujisuta na kuwa na huruma na utu, idadi ya waathirika bila kutaja mali ni kubwa sana. Hapa hujaongeza idadi ya waliokufa kwenye milipuko kama hii ya Mbagala.

Dk. Mwinyi anaweza kuja na wimbo ambao tumezoea kukisikia kuwa yeye si mtunzaji wa ghala la silaha. Akumbuke. Baba yake alipojiuzulu hakuwa mlinzi wala polisi waliowaua akina Nzegenuka kule Kanda ya Ziwa.

Mzee Mwinyi alijiuzulu kutokana na vifo vya watu wasiofikia hata kumi. Hii ni changamoto kwa mzee Mwinyi na mwanae.

Dk. Mwinyi atakuwa mtu wa ajabu na asiyefaa kama hataliona hili. Uko wapi na utekelezaji wa ripoti ya milipuko ya Mbagala.

Kuwajibika, mara nyingi huwakumba wenye kusimamia idara au wizara kutokana na kuguswa vibaya kwa wizara zao. Hata hivyo, tukumbuke. Kuwajibika ni hatua na njia ya wanyoofu na si wapotofu na mafisadi.

Dk. Mwinyi angepaswa kuelewa na kujiuliza baadhi ya maswali ili ajipime na kubaini anavyopwaya kwa kuchelewa kuwajibika. Kama anangoja rais amwajibishe anakosea sana. Rais wetu hana nia, silka wala udhu wa kuweza kumwajibisha yeyote kutokana na kuchafuka sana.

Hakuna kituko kilichoniacha hoi kama maneno ya Jakaya Kikwete kwenye eneo la tukio. Alikaririwa akililia vifaa badala ya watu.

Alikaririwa akisema: “Haya ni maafa ya kitaifa, kwa sababu kikosi hiki ndiyo makao makuu ya hifadhi ya kijeshi, ikiwemo silaha na mavazi yao, ambayo mpaka sasa hivi naongea vyote vimeteketea kwa moto.”

Aliendelea kusema: “Kwa taarifa nilizonazo ni askari mmoja aliyejeruhiwa, hivyo basi ninawaomba wananchi waondoe wasiwasi juu ya tukio hilo, serikali iko pamoja nao kuhakikisha kuwa hatari zilizopo zinadhibitiwa, na kwamba wananchi wanarudi katika hali yao ya kawaida.”

Huyu si mtu wa kuwajibika, wala kumwajibisha mtu kutokana na tunavyomjua. Mtu anayelilia askari mmoja na vifaa akipuuzia maelfu ya watu wasio na hatia utamuweka kundi gani?

Pia Mwinyi anapswa kujua kuwa wananchi hawajui ajali wala nini. Hata ingekuwa ajali bado haizuii sheria kuchukua mkondo wake. Madereva wengi waliofungwa magerezani wamefungwa kutokana na ajali kama hii ya Gongo la Mboto na Mbagala.

Ajali inaweza kusameheka kama hakuna uzembe nyuma yake. Swali ambalo litamsumbua sana Mwinyi ni kwanini hakujifunza kutoka Mbagala wala kutimiza ahadi yake?

Maswali mengine ambayo Daktari mwinyi anapaswa kujiuliza ni Kwanini silaha kuwekwa kwenye maeneo wanamoishi raia?

Kwanini wahusika hawakujifunza kutoka kwenye tukio la Mbagala ambalo ni la karibuni kabisa ukiacha yaliyowahi kutokea huko nyuma?

Je, huu si uzembe unaotufanya tumshauri na kumtaka Mwinyi aachie ngazi? Ingekuwa nchi za wenzetu hata rais na serikali yake wangefurushwa na kuweka watu wenye kujua kazi kwenye nafasi zao.

Tunatawaliwa na watu wasio na roho zaidi ya uroho. Kama ukijiuliza utitiri wa kashfa unaoendelea kukaliwa na serikali ya sasa, utakubaliana nami kuwa tunatawaliwa na viumbe wa ajabu wasio na utu wala nafsi zenye kufanya kazi sawa sawa.

Hebu tujikumbushe kashfa za EPA, Richmond, Dowans, kughushi vyeti vya kitaaluma, kuzagaa noti bandia, milipuko ya Mbagala, mauaji ya hivi karibuni huko Arusha, uchakachuaji na wizi wa kura na nyingine nyingi.

Watuhumiwa wamefanya nini zaidi ya genge husika kuendelea kulindana? Nani anawawajibisha? Nani anawajibika? Anyway, haya yanaandaa safari ya kwenda Tahrir kuwafurusha Mubarak wetu.

Tumalizie kwa kumpa mwana wa Mwinyi busara nyepesi. Baba yake yaani mzee Mwinyi angetaka kung’ang’ania kwa tamaa ya madaraka angeweza. Kwanza wakati huo haukuwepo ustaarabu wa kuwajibika zaidi ya kuhamishwa.

Lakini hakutaka kuendelea kupata vinono vyenye damu ya watu nyuma. Pia hakutaka kutolewa kama mfano mbovu wa uwajibikaji kama wale waliolazimishwa au waliokataa kuwajibika.

Kwake, mzee Mwinyi, cheo ilikuwa ni dhamana na si urathi wala mtaji wa kuukata kama ilivyo sasa.

Kama kuna alichoshindwa Dk Mwinyi kutoka kwa baba yake si kingine bali kusoma alama za nyakati na kujisuta ambako kulimletea heshima baba yake.
Chanzo: Tanzania Daima Februari 23, 2011.

Nilivyonusurika kulipukiwa na mibomu

MWENZENU nina bahati ya mtende. Nani alijua kuwa ndiyo nilikuwa nimehamia kwenye banda langu litokanalo na pesa niliyokwapua kwenye kijiwe?

Nani angejua kuwa nilikuwa na home pale Gongo la Mboto? Siri imefichuka. Kweli mficha maradhi kilio humfichua.

Msilaumu kwanini nilificha home kwangu. Unajua kupayuka ni kazi ya hatari sana. Unakuwa na maadui kila kona kama noti mpya zilizomwagwa na waliozitengeneza ili kuziba pengo la matumizi yao ya uchakachuaji.

Hivi kuwakalia kooni kina Njaa Kaya na mafisi wenzake unadhani mchezo?

Thubutu kama hujageuzwa past tense baada ya siku moja. Kama si kuwa janja la wanjanja, hawa mijitu wangekuwa wameishaninyotoa roho. Siri ya kwanza ni kutojua niishipo. Pili ni kutokujua sura yangu wala nichimbukacho.

Lo! Unajua ukiwa na gonjwa la kupayauka, utapayuka hata pasipohitajika kufanya hivyo kama Jamaa alivyoigiza kupayuka kwenye majonzi akaishia kuwa stori na makala ya Mpayukaji mwenyewe orijinale. Kama unadhani nchezo kamuulize mgosi Yusufu Makambale ambaye anaogopewa kwa kupayuka utadhani ushuzi!

Okey poa. Tuachane na wapayukaji uchwara waliolewa midaraka kutokana na kuweka rumenya na mafisi ahadi.

Nikiwa ndiyo nimeanza maisha mapya ya kutanua na kuitwa baba hausi au mwenye nyumba kama waswahili wa bongolalaland wapendavyo kuitwa hata kama hausi yenyewe ni ubavu wa dogi, si mibomu ikalipuka.

Kama siyo kuchelewa Kimanzichana kuuchapa ulabu na kula ndung’u na washikaji, sasa hivi mafisadi wangekuwa wanachekelea kuwa kiboko yao nimerejesha namba.

Najua akina, Ewassa, Rostitamu, shankupe la Kinsomile na gendaeka wengine wangeangusha bonge la party. Nawataarifuni kuwa wasifanye kosa mzee bado nipo nadunda baada ya kushuhudia kutimuliwa kwa mwenzao Hosni Mubarak.

Milipuko ya mibomu imenichanganya. Kwanza maelezo yanayotolewa hayakuniingia akilini. Yangeingiaje akilini wakati machozi ya majonzi ya Mbagala yalikuwa bado hayajakauka?

Baada ya kusikia milipuko na kushuhudia wapendwa majirani zangu wakiwa past tense nilikumbuka kisa cha majeshi ya Masri. Nilitamani tubinafsishe majesi yetu na kuwekeza yale ya Masri.

Wakati majesi ya Masri yanalinda uhuru na ukombozi wa kaya yao, yetu yananyotoa roho halafu yanakuja na lugha za kipuuzi!

Kabla ya kuendelea, nachukua fursa hii kuwafahamisha kuwa rafiki yangu mkubwa, Msomi Mkatatamaa, amepata msiba mkubwa. Kwani katika wale thelathini sijui mia tatu waliokufa na kujeruhiwa mmojawapo alikuwa shangazi yake.

Mie namshukuru Mungu kuwa siku ya tukio mama Kapayukaji alikuwa ngomani na Kapayukaji ndiyo alikuwa amekwenda wilayani kwetu kujiunga na shule ya kata ambazo tunapenda kuziita shule za kukata tamaa au shule za ukata wa kiakili.

Hivyo, unaweza kuona nilivyo na bahati ya mtende. Kutokana na siba hili kubwa, niliitisha kikao cha ghafla cha kijiwe kulaani uzembe huu.

Tulielekeza laana zetu kwa mkuu ambaye anaendesha kaya kihuni. Pili laana zetu zilielekezwa kwa waziri wa magesi, Hossen Muinyi na waziri wa mipango miji ambaye jina lake limenitoka.

Pia laana zetu zilielekezwa kwa wafanyakazi wa halmashauri ya wilaya ya Meteke ambao watatumia madai yetu kupachika nyumba hewa za kulipwa fidia kama walivyofanya hivi karibuni kwenye upanuzi wa uwanja wa njiwa.

Baada ya kumaliza kuomba dua, tulitoa azimio kuwa kaya yetu ibadilishwe jina toka Bongolalaland kwenda Milipuko. Maana kila siku lazima ilipuke mibomu. Kama siyo ya machozi ya kuwatwanga wanafunzi wa vyuo vikuu basi italipuka ile ya AR. Kama siyo hii basi italipuka mibomu ya kashfa kama hii ya Dowanis. Hapa hujaongea bomu la nyuklia liitwalo mgawo wa umeme. Bado hujazungumzia bomu la uhaba wa maji, ajira, maisha bora, usalama, heshima na thamani ya maisha.

Katika mibomu yote hii waathirika ni walevi na si wengine.

Kiasi fulani walevi wameanza kuota sugu ya kulipukiwa mibomu. Laiti wangekuwa wamasri mbona wangewatimua nyani kwenye shamba la bibi!

Turejee kwenye mibomu. Baada ya kushuhudia maangamizi ya Gongo la Mboto tungojee ya Kigamboni, Lugalo, Kunduchi na kwingineko ambako mibomu inatunzwa kwenye maeneo ya walevi.

Kweli walevi ni walevi. Hivi kama si ulevi unaofanana na utaahira, uliona wapi silaha zikitunzwa kwenye maeneo ya civilian?

Hapa tunaongelea milipuko. Bado ile mibomu iliyobaki bila kulipuka haijaanza kufanya vitu vyake kama tulivyoona kule Mbagala.

Bado watoto wetu hawajaiokota au kuikanyaga wakicheza chandimu na mipira yao ya kichovu.

Ingawa roho bado inauma, hakuna kitu kinaendelea kuniumiza roho nusura kujinyotoa kama maneno mbofu ya mkuu aliyekaririwa akiombolezea vifaa na si wapendwa wetu.

Sitaki nimkariri nisije nikajinyotoa roho au nikaanza kusaka mibomu ambayo haikulipuka nikamualkaida mtu mie nikaitwa gaidi bure.

Hivi gaidi ni nani zaidi ya genge linaloua watu wasio na hatia iwe ni kwa nia au uzembe? Hivi kuna ugaidi zaidi ya kunyotoa roho za watu tena wasio na hatia? Mie kusema ukweli matukio ya juzi nayaona kama September Eleven ya hapa kayani.

Hivi kama si ulevi, ugaidi na utaahira ni busara gani kwenda kwenye matanga ya watu wasio na hatia hata kama ni walevi kuanza kulilia sare na mibomu ilhali watu wamepoteza watafuta unga wao? Kuna siku nitawaleta jamaa zangu wa Masri tufanye kweli hebu nyie ngojeni na kuendelea na ukondoo na ulevi wenu.

Puuuuuu! Ngoja nitimke maana naona mibomu ishaanza. Lo! Kumbe pancha ya kweche la Gongo la Mboto Mwenge!
Chanzo: Tanzania Daima Februari 23, 2011.

Sunday 20 February 2011

The Gadaffi we did not know






No doubt that what is unfolding in Libya has left many shocked. Nobody would risk thinking that Libyan strong man Muamar Gadaffi would easily been cowered as it happened.

Two days after disgruntled Libyans took to the street, Gadaffi was nowhere to be seen or heard. Who would believe that Gadaffi who has been everywhere in Libya from seating room to bathroom would not come to defend his autocratic regime?

To save the face, his son Al- Saif Al- Islam Gadaffi (Uday Saddam Hussein of Libya) recorded confused message that was aired by Libya TV. Instead of helping his father, he poured yet more fuel to the already raging fire. He accused police and the army of being unprofessional. He played down the number of those that were felled by his father’s notorious regime. Who would believe that a sane person would argue that those that were killed in demonstrations were just 14 not 173?


Gadaffi’s son made some concessions after witnessing the fall of Benghazi the second biggest city in Libya. He offered to change things to suit the demand of the mass. Nobody would subscribe to this bulimia thanks to the fact that Al Islam has no locus standi to enter any concession with anybody. Being a tick on the back of his father, desperate Al Islam made up some allegations. He said that demonstrators were labouring under the influence of drugs and they wanted to divide Libya into Islamic caliphates. This is sick to hear. It is the first time Libyans and the world have ever heard of such a thing. Who is labouring under influence between demonstrators and Gadaffi's son who is labouring under power intoxication?

Gadaffi the son went a mile ahead claiming that Libya is going to be divided in tribe states. If this were the case it would make sense simply because his falling father is the fan of tribe chiefs in all Africa. Is this Iran-like hypocrisy whereby Iranian barbaric regime supported demonstrators in Egypt? But when Iranians took to the street to do what the regime was supporting Egyptians for, it dispatched killers to finish them.

No doubt. Like Saddam Hussein, Gadaffi has proved to be a coward that can be easily cowered and toppled altogether. For those conversant with the dynamics and theatrics of powers, Gadaffi will nary take long before being bundled out with his cronies.

Being a wino, Gadaffi threw vitriol onto Tunisians and Egyptians when they took on their dictators. Now his turn has come, he is nowhere to be seen.

Analysts agree on one thing. What is happening in Libya is but the beginning of the end. The fire that started in Tunisia will gut the whole continent. This means. Even dictators and thieves south of Sahara should brace themselves for the show.

Gadaffi has been in power for 42 years. Though he does not have constitutional title of king, he has ruled like other Arab kings. Libya became his private estate. Who doubts this should ask himself or herself, if this was not the case, where did his son get the power to address the nation?

Archaic and myopic as Gadaffi’s rule has always been, now it is on its deathbed waiting to be buried any soon from now. Let keep our fingers closed to see another dirty regime cascading down to historical dust bin.

To cut the story short, Libyans will give the world the worthy and unique gift by booting out their long time thief-cum-tormentor.


Good news, it is true, is the fact that Libyan army has boycotted more orders aiming at shooting to kill more protesters. Allah Akbar. Gadaffi is now showing his hate to Islam. If he could offer millions of dollars to build mosques all over Africa, what is wrong with having an Islamic regime in Libya? This means: Gadaffi was taking Muslims and Islam for a ride. What is the logic behind his son’s warning that Libyans should not allow Islamic regime to be formed? Hypocrisy and sheer lies. Ironically the meaning of Al Saif Al Islam is the "Sword of Islam." what hypocrisy!

Thank Lord that now the world knows Gadaffi who was hidden behind power and fanfares resulting from it-the coward and harsh Gadaffi who could order the army to shoot to kill.Is this the beginning of the the end of Gadaffi? Libya is bleeding to death. Air force is used to bomb peaceful civilians that are standing for their constitutional rights. Where are African Union and Arab League? Where is EU? where is UN? Where is everybody?

Source: Afro Spear Feb. 20, 2011.

Gadaffi anywea mwanae abwabwaja waandamanaji wazidi kupeta


Mtoto wa imla wa Libya, Al Islam Gadaffi kachafua hali ya hewa kwa kuongeza mafuta kwenye moto. Amelaumu jeshi kwa kutokuwa na viwango huku akikanusha mauaji ya wazi ya watu zaidi ya 172. Kijana ambaya hana mamlaka yoyote kisheria amebwabwaja hadi kuahidi kubadili bendera na wimbo wa taifa kama waandamanaji watapenda.

Kwa waliomtazama kwenye runinga wametoka na picha moja-Gadaffi kwisha kazi yake. Na inavyoonekana, haitachukua muda mrefu kama Misri au Tunisia. Wengi tumeshangaa mantiki ya kulaumu jeshi wakati bila jeshi hawa wezi hawana pa kushika. Mji wa Benghazi umeishakamatwa na waadamanaji na habari zaidi zinasema waandamanaji wanaelekea Tripoli kutoka miji ya jirani. Benghazi ni sherehe za kuanguka utawala dhalimu wa miaka 42 ya imla Gadaffi.

Mtoto wa Gadaffi akiwa amechanganyikiwa wazi, ametoa mpya kwa kusema eti waandamanaji wamefanya hivyo kutokana na kutumia mihadarati! Ni vituko vitupu. Tuzidi kuomba wimbi hili liendelee na kushuhudia kihiyo huyu akiondolewa kwa aibu zote. Wengi walizoea kumuona Gadaffi kama mtu jasiri. Kumbe, kama Saddam Hussein, ni hovyo tu! Kuna uvumi kuwa Gadaffi mwenyewe ameishakimbia nchi.

Je huu ni mwanzo wa mwisho wa Gadaffi?





Dikteta wa Libya Muamar Gadaffi amekuwa madarakani kwa zaidi ya miaka 40. Anaingia kwenye vitabu vya historia kuwa mtawala katili aliyeweza kung'ang'ania madaraka kwa muda mrefu.

Sasa mambo yamebadilika. Baada ya walibya kushuhudia madikteta na wezi wakitimuliwa katika nchi jirani za Misri na Tunisia, wameamua kuamka na kumkabili imla wao.

Taarifa zisizothibitishwa zinasema kuwa waadamanaji wameishauteka mji wa pili kwa ukubwa wa Benghazi. Al-Jazeera iliripoti kuwa vifaru vinne vimeishatwaliwa toka jeshi la Gadaffi huku makao makuu ya polisi mjini Benghazi yakiwa yanawaka moto.

Waandamanaji wameapa kutorudi nyuma pamoja na wenzao zaidi ya 200 kuuawa huku wengine wapatao 1,000 kujeruhiwa.

Habari njema ni kwamba mjini Benghazi jeshi limeamua kuwaunga mkono waandamanaji kama ilivyofanyika huko Misri. Tuzidi kuwaombea wenzetu wakati tukitafakari mustakabali wetu kutokana na kuwa katika hali mbaya kuliko wenzetu wa Maghreb.

Macho na masikio yetu yako Libya. Je mwanzo wa mwisho wa utawala zandiki wa Gadaffi ndiyo umeanza?

Friday 18 February 2011

Mauaji ya Gongo la Mboto Dk Mwinyi anangoja nini kujiuzulu?



Kwa wanaokumbuka mauaji ya kizembe yaliyotokea na milipuko ya mabomu kwenye maghala ya kijeshi kule Mbagala mtakumbuka viapo na ahadi vya serikali hasa waziri mhusika Dk Hussein Mwinyi.

Aliahidi kuwa maafa haya yasingetokea tena. Alitoa ahadi hii wakati akipinga shinikizo la kumtaka ajiuzulu ikiwa ni kama kuomba fursa kutokana na lile kuwa kosa la kwanza. Sasa kabla hata waliofariki Mbagala kuoza, Dk Mwinyi ameanikwa. Je anangoja nini kutekeleza ahadi aliyoitoa kwa hiari yake?

tunajua aliyepaswa kuwajibishwa ni serikali nzima. Ila kwa utawala mfu na mbovu tulio nao hili sahau.

Kwanini Dk Mwinyi haigi mfano mwema wa baba yake aliyejiuzulu kutokana na vifo vya watu wasiofikia hata kumi ikilinginshwa na halaiki iliyouliwa na mabomu kutokana na uzembe wa wizara yake naye binafsi akiwa mkuu wa wizara. Je maafa ya Mbagala na Gongo la Mboto si ushahidi kuwa utawala wetu ni wa kizembe na usiojali maisha ya watu wake?

Hebu soma nukuu ya rais Jakaya Kikwete alipokuwa akiongolea mkasa huu.
Alikaririwa akisema: "“Haya ni maafa ya kitaifa, kwa sababu kikosi hiki ndio makao makuu ya hifadhi ya kijeshi, ikiwemo silaha na mavazi yao ambayo mpaka sasa hivi naongea vyote vimetekelea kwa moto.”

Aliendelea kuonyesha ubovu wake kwa kusema, "Kwa taarifa nilizonazo ni askari mmoja aliyejeruhiwa, hivyo basi ninawaomba wananchi waondoe wasiwasi juu ya tukio hilo, Serikali iko pamoja nao kuhakikisha kuwa hatari zilizopo zinadhibitiwa, na kwamba wananchi wanarudi katika hali yao ya kawaida.”
Kwa ufupi ni kwamba tuna watawala wasio na roho bali uroho. Hawana huruma wala utu bali makatili na fisadi wa kupita kiasi.

Wednesday 16 February 2011

Is the South of Africa Reading Egypt’s Script?





The dramatic fall from grace of former Egyptian strong man, Hosni Mubarak was unprecedented, though what happened in Tunisia tells it all. Defiant and arrogant, as the nobody thought he would easily be toppled in 18 days.

If comparably affluent Egyptians can vent their pent-up anger by booting out their leader, what of the wretched of the earth south of Egypt? Egyptians are relatively better compared to their cousins in the south. For example, currently, Tanzanians are facing an acute shortage of power unnecessarily. Rationing is the norm next to reality. Corruption is the order of the day as accountability faces detumescence. So too, Ugandans have known but just a one man show for over two decades. What is their take of what happened in Egypt and Tunisia? Generally speaking, life is harsher in SSA than it is in Egypt even Maghreb in general.

While Ethiopia as well as Kenya, Tanzania and Uganda are suffering from chronic mega corruption, Arab countries are suffering from dictatorship and monarchism. Thanks to globalization, whatever happens in any country of the world is echoed and aped all over the world. That’s why what transpired in Tunisia gave birth to the revolution in Egypt which soon will escalate to Algeria, Yemen and elsewhere.

Many careless and myopic rulers would sooth their hearts thinking that Tunisia-cum-Egypt Jasmine Revolution has nothing to do with them. But again, this time, as US president indicated, is time for eradicating dictators and crooks. The timing of this new world order is accurate and people’s power is unstoppable. The US president Barack Obama was jeered at for supporting the voice of the people before Mubarak hit the road. The climax of this impasse has however vindicated him as a visionary and trustworthy leader, who reads the mood of the people.

Egyptians, for thirty years, were regarded as the most docile people on earth thanks to not taking on their tyrant. When Sudanese staged demonstration in the heart of Cairo, Egyptians were left baffled. They wondered. How could one get the guts of agitating against the government and fall short of being totally insane? But when hunger and misery are at work, anything can happen. Who would risk thinking that Mohammed Bouazizi would be the power behind the toppling of tyrants?

Another crucial aspect of the whole history making is the fact that the military is coming of age. The decent and reasonable way the Egyptian military acted (as opposed to their police counterparts) in this process must be emulated by other napkin-like armies in the continent. Bombs, tanks and military muscles will nary defeat people’s power. This is a nugget of knowledge to those that are still day dreaming thinking that they can use the army to intimidate and rob the hoi polloi. Mubarak had the mightiest army under his disposal compared to SSA. But by not sitting on their brain, they deserted him at the very time he needed them most. They understood the might of people’s power. They accepted the reality that presidents come and go but not the citizenry.

Now that Mubarak and his gang are out of the big picture, what should we expect? Will the military live up to their promises? Is it the beginning of the end of dictators? Selma, salmah means peace as the Egyptians put it. Is SSA ready for a peaceful transition or revolution? Mubarak is history. What of other tyrants and thieves in SSA?
Source: African Executive Magazine Feb. 16, 2011.

Somo kwa wake wa marais Afrika












LEILA Ben Ali au binti Trebelsi, mke wa Rais wa Tunisia aliyeangushwa na umma alijulikana kama ‘Imelda Marcos wa ulimwengu wa Kiarabu’ kutokana na israfu na wizi wa pesa ya umma.

Mhudumu huyu wa saluni wa zamani alifanikiwa kumuingiza majaribuni Ben Ali kiasi cha kutimuliwa kama mbwa kutoka madarakani hivi karibuni.

Leila mama tamaa hakuwa peke yake katika mchezo huu mchafu. Inasemekana tangu mumewe kuingia madarakani alikuwa mtu safi. Ben Ali alianza kuharibikiwa alipomuoa mama huyu mpenda raha.

Ndoa ya Leila na rais ilimwezesha Leila kutengeneza ukoo wa mabilionea yaani, kaka zake wapatao 10. Walimiliki kila biashara iliyoingiza pesa kuanzia internet café, uuzaji wa magari, hisa katika mabenki na shirika la ndege la Tunisia na kupata upendeleo katika mikopo hadi kaka yake kuanzisha benki iitwayo Zeitouna, ambayo ilichomwa moto na waandamanaji.

Uliza walikopata mtaji. Ni sehemu moja. Dada yao alikuwa anamiliki chumba cha kulala na rais. Mtaji wa ajabu sana kama tutaangalia hili kwa makini.

Je, ni wangapi Afrika wanatumia mapenzi yao kwa marais kujinufaisha wao na familia zao? Leila hakuwa na haja ya kuanzisha NGO ili kupata pesa ya kificho zaidi ya kuiingiza ukoo wake kwenye ujambazi dhidi ya umma.

Kuna uvumi genge hili la ndugu Watunisia walilozoea kuita mafia lilikuwa likijihusisha na utoroshaji wa pesa na biashara haramu ya mihadarati.

Kilichofanyika Tunisia ni picha ya kinachoendelea kwenye nchi nyingi za Kiafrika.

Huu ndiyo utukufu na ukuu katika nchi za Kiafrika ambapo mpaka kati ya rais, watoto zake, mkewe na waramba viatu wake haupo.

Rejea jinsi walioko nyuma ya kashfa ya Richmond-Dowans-Kagoda wanavyolihenyesha taifa.

Nchini Zimbabwe, Grace Gucchi Mugabe, mke wa imla Robert Mugabe, anaweza kufanya kufuru yoyote kifedha na asiulizwe kisa analala kitanda kimoja na rais. Ni mama mwenye ushawishi si kawaida. Hata uhusiano wake wa kimapenzi na Gavana wa Benki Kuu ya Zimbabwe (RBZ), Gideon Gono ulipofichuliwa, Mugabe hakuchukua hatua yoyote.

Nchini Ethiopia mke wa Waziri Mkuu, Meles Zenawi, aitwaye Azeb Mesfin huitwa Queen of Mega, kutokana na kushiriki ufisadi mkubwa (Mega Corruption).

Nchi ya jirani ya Kenya, mke wa rais, Lucy Kibaki, ana madaraka kiasi cha kuvamia vyombo vya habari na kuwazaba vibao waandishi kwa kuandika uoza wa familia yake.

Pale Uganda ndiyo usiseme. Mke wa imla wa nchi hiyo, Janet Museveni ni mbunge, First Lady na waziri, ukiachia mbali kuwajaza wanawe na ndugu zake kwenye ofisi ya rais na sehemu nyingine za ulaji. Hapa kwetu, sitaki kusema, utajua mwenyewe.

Wengi wanaona kama huu ni ufisadi wa aina yake. Wangetaka wake za marais wa Kiafrika waache kutumia madaraka ya waume zao kujineemesha wao na ndugu zao na mashoga zao.

Siku hizi wamebuni hata mtindo wa kuwa na vikao sambamba na waume wao kwenye mikutano ya Umoja wa Afrika kama mlivyoona hivi karibuni. Mbona hatuoni wake au waume wa viongozi wa Jumuia ya Ulaya wakifanya hivyo kama huu si ufisadi na ukupe wa kutupwa?

Turejee kwa Leila. Alimgeuza rais wa nchi bwege na kifaa cha kuchumia utajiri haramu na haraka kwake na ndugu, mashoga na waramba viatu wake. Si rais wala mkewe, hakuna aliyeona mbali. Je, wako wangapi kama hawa barani Afrika?

marehemu Baba wa Taifa, Mwl. Julius Nyerere alituhusia kuwaogopa watawala wanaotawaliwa na wake zao. Hakuruhusu mkewe na watoto wake watumie ofisi ya umma aliyokuwa ameaminiwa na umma kujineemesha wala kujidai.

Alijua mipaka ya madaraka yake kiasi cha kuacha historia inayong’ara ambayo imewashinda wengi waliofuatia.

Siku hizi si ajabu kuona mtoto wa rais akiwa kijirais kidogo chamani mwake au mke wake akiwa kijirais nyuma ya pazia, kwa sababu tu analala kitanda kimoja na rais.

Nyerere hakuwa mchovu wala wa hovyo hivi. Aliona mbali kiasi cha kujitenga na ufisadi huu unaooanza kuhalalishwa ambapo Ikulu nyingi zinaendeshwa kama magenge ya ujambazi dhidi ya umma. Kilichotokea Tunisia ni ushahidi wa kutimia kwa utabiri na wosia wa Mwalimu.

Hakika kilichojiri Tunisia ni changamoto kuwachunguza watawala wetu na familia zao. Ni suto kwa wale wote wasiosoma alama za nyakati kama Ben Ali na Leila wake ambao wanaishi kama vibaka uhamishoni huku wakisakwa nyumbani kwao waadhibiwe.
Chanzo: Tanzania Daima Februari 16, 2011.

Mkuu wa kijiwe alipoikana Dowans mara tatu

HIVI karibuni nilicheka hadi mshirika wangu wa bedroom akadhani nimepata kichaa cha ufisadi. Alidhani nimechanganyikiwa hadi kugeuza kituko na kichekesho kama wale wanaodanganya mchana kutwa kuwa ni wasafi wakati ni wachafu kuliko hata chawa.

Nilicheka sana baada ya kumuona Mkuu kupitia runinga yangu ya Hi Def bomba kali, akiwadanganya wabongolalalanders kuwa haijui Dowanis wakati yawezekana ndiye mshitiri na mnufaika wake.

Nilicheka kwa hasira kiasi cha kuanza kuweweseka kutokana kupandisha mwenembago kiasi cha kutaka kwenda kuwanasa vibao walevi, kumbaffu zao.

Kitu kilichonikera ni kusema, “siijui” Dowanis. Hata hivyo, hajajinasua, na hatajinasua kwenye mtego huu uliogeuka msalaba kwake.

Alisema haijui Dowanis. Ukweli ni kwamba anaijua nayo inamjua saana tu. Kama angekuwa haijui angesema sijawahi kuijua Dowanis. Hata hivyo ungekuwa upuuzi kusema haijui Dowanis wakati li-sirikali lake ndiyo liliingia mkataba wa ujambazi na Dowanis.

Sasa tumsaidie. Kama haijui Dowanis ingawa anaijua tu, aende kwa shoga yake Rostitamu mwenye funguo na mikoba yote ya jinai hii. This goon has all damn power of attorney. Naongea kimombo mjue mie ni msomi tena wa sheria.

Wenzangu huniita our learned brother hata kama wengi wao wanakula rushwa kiasi cha kutoa elimu ya jinsi ya kuingia mikataba mibovu na kupata mipesa mingi baadaye kama yule Maregereresi wa Kagodoka. Mie nilikataa upuuzi huu nikaamua kufanya kazi ya upayukaji badala ya kutetea mibaka.

Narejea maelekezo ya Mkuu wetu kijiweni, kuijua Dowanis kwa kusisitiza aende kwa Rostitamu. Kumbuka. Hawa ni marafiki wa kufa na kuzikana. Hamuoni alivyogoma kumshughulikia ukiachia mbali juhudi zake za nyuma ya pazia kutaka walipwe haraka?

Hili halina ubishi. Dowanis imekuwa lisirikali ndani ya lisirikali. Kwanini tusiwafanyie kama Tunisia jamani?

Kimsingi, kisanii, alichosema ni “Siijui, I mean, naijua Dowanis nami ni sehemu ya jinai hii.” Period. Ni tusi la nguoni kwa walevi wote wa Bongolalaland. Ni ubakaji wa haki.

Kama haijui na hataki kuonana na Rostitamu ammegee kila kitu basi angemuuliza Nshomile Silvia Rweyependekeza ambaye aliwahi kufanya kazi ya kuisafisha Richmonduli, mama mzazi wa Dowanis mke wa Kagodoka.

Kama Nshomile amekosa kumbukumbu angemuuliza Eddie O’ Shea aliyetaka kuizima Richmonduli bila mafanikio. Kama basi wote hawa hawapatikani angemuuliza Ewassa aliyesuka mipango yote.

Ikizidi ikipungua angemuuliza Mwana wa Idd Majaala ambaye na wanasheria wengine mbwa mwitu walitoa ushauri wa janga hili la kaya.

Mkuu hata akane vipi tunajua, tunaelewa, tunafahamu na kuamini yeye anaijua na hata kiboko yake Dk. Sihala alisema yeye ndiye Dowanis,
Au tuseme kama haijui Dowanis, basi Dowanis inamjua na kumhusu hadi siku kiama maana hata walevi wanajua hakuna Dowanis nyingine isipokuwa mkuu na wenzake.

Kwa tunaomjua hatukushangaa wala hatutajisumbua na kushangaa. Kama aliweza kukwepa HEPA iliyomwingiza kwenye ulaji, atashindwa Dowanis?

Huyu jamaa si mjinga kama wengi wanaovyomchukulia. Kicheko chake kimeficha mengi.

Anajua udhaifu wa walevi wa Bongolalaland. Anajua walivyo woga na wanafiki kwa nafsi zao. Ukipandisha bei ya mkate badala ya kuingia tahrir square kuandamana wanapanga jinsi ya kudokoa kwenye ofisi za umma.

Wapo wanaojiingiza hata kwenye rushwa na hongo za ngono kwa akina mama na dada hata usenge kwa kina baba. Huu ndiyo huwa naita ukeketwaji kiakili ambao ni mbaya kuliko wa kimwili. Inaudhi najua. Lakini nitumie lugha gani mtume Mpayukaji mie nieleweke? Niwakere vipi ili mchukie na kuchukua hatua?

Najua wapumbavu wananichukia mimi badala ya kuchukua almasi ya kiakili niwapayo.

Mie sipayuki kipumbavu kama kina mgosi Makambale na Nshomile. Natema busara tena kwa lugha na ujasiri vilivyowashinda wengi.

Mafisadi wanaweza kujiridhisha kuwa yao hayajulikani, yatajulikana siku wakitoka walipo.

Narejea tena, kama huijui mbona umeshindwa kuwafungulia mashtaka kina Kagodoka, na wengine wanaojulikana wazi? Ukiwashitaki watakuumbua. Hii ndiyo siri ya Kagodoka na Dowanis kupeta ukiachia mbali maslahi yako.

Ni kituko cha mwaka eti mkuu wa kaya hajui Dowanis! Kwanini asiseme kuwa anaijua jinsi ilivyochangia kuinua mtaji wa kuula? Ningekuwa mimi, ningewambia walevi kuwa tusameheane kwa vile nao walipata mgawo wao waliokuwa wakiufakamia wakati wa kampeni ya uchafuzi ulioishia kwa uchakachuaji.

Mlichakachua benki kwa Ma-EPA na mahepe. Hamkutosheka. Achovyaye kwenye buyu la asali hachovyi mara moja.

Mmechakachua kula. Sasa mnataka mchakachue hata akili zetu yarabi? Mbona hata mijusi wanajua kuwa Dowanis ni ya nanihino? Mbona hata kunguru wanajua kuwa huu ni uhuni na wizi wa mchana unaofanywa na wale wanaoitwa waheshimiwa wakati matendo yao yanawaonyesha wa hovyo kama chawa!

Nimalizie kwa kuwaibia siri. Jamaa aliwaona nyinyi makenge kusema haijui Dowanis wakati yeye ndiye…, malizieni. Siri ni kwamba mkiamua kuingia mitaani kwa amani, kinaweza kueleweka.

Msiogope mibunduki ya majambazi yenye sare maana Mureno Okampo yuko pale kwenye nchi ya nyao. Msidhani yale ya AR yanaweza kurudiwa na Okampo akachekelea. Kazi kwenu siri zote mmepewa mkiendelea kuzubaa mtaliwa mpaka mkome.

Haloo, haloo. Huyu naona anabeep. Wabongolalalander kwa kubeep! Ngoja nifiche kibroadband changu vibaka wasije kukinyofoa kama Rostatimu anavyotaka kunyofoa njuluku za walevi. Kwaheri.

Chanzo: Tanzania Daima Februari 16, 2011.

Monday 14 February 2011

Suto kwa wadini wa Tanzania ufisadi hauna dini









Picha zote toka Jamii Forums.

Hakuna ubishi kuwa mtu akijitambua na kujua haki zake za msingi huwa hana kikwazo. Yaliyotokea hivi karibuni nchini Misri ni ushahidi tosha.

Baada ya wamisri kuchoshwa na ufisadi, hawakukubali kugawanywa kwa misingi ya dini, jinsia, kabila au rangi. Wakristo na waislamu walisimama bega kwa bega kumfurusha Hosni Mubarak na waramba viatu wake.

Ajabu hawa ndiyo wenye kujua chanzo na mzizi wa dini iwe ukiristo au uislamu.
Ukiangalia watanzania wanavyogawanywa kwa misingi ya dini kiasi cha baadhi yao kuwa maajenti wa ufisadi, unashangaa.

Tatizo ni kupokea au kutojua? Maisha mabovu yatokanayo na ufisadi na utawala wa kijambazi hayajui dini ya mtu.

Ukitaka kujua nimaanishacho, jiulize: kwa sasa mgao wa umeme unawaumiza nani zaidi kati ya waislamu na wakristo kama si watanzania wote? Jiulize zaidi. Kupanda kwa mahitaji na gharama za maisha kunawaumiza nani kama si watanzania bila kujali dini zao? Jiulize tena. Wanaohangaishwa na mikopo ya elimu ya juu au kukamatwa wakiandamana hata kuuawa si watanzania wote?

Uzoefu unaonyesha kuwa waathirika wakubwa wa majanga ya kuletewa na watawala mafisadi ni vijana kuliko kundi lolote.

Wakati wenzetu wakijikomboa sisi tunajikomba na kujichelewesha kwa kujifungia kwenye udini na upuuzi mwingine. Ufisadi hauna dini. Rais akiwa fisadi hata awe wa dini yako hakusaidii zaidi ya kukuumiza. Huyu kimsingi dini yake ni ufisadi na tamaa si uislam wala ukristo. Mshenzi ni mshenzi na fisadi ni fisadi hana dini. Tutatafakari.

Sunday 13 February 2011

Lowassa na machozi ya mamba na yaliyojiri Misri











Wengi wameshangaa ushupavu na mapendo ya ghafla ya Edward Lowassa waziri mkuu aliyefukuzwa kutokana na ufisadi wa Richmond.

Lowassa amewaacha wengi hoi kujitokeza mbele ya runinga kuwapongeza wamisri huku akiwaonya watawala wasiosoma alama za nyakati! Ama kweli nyani haoni nonihino lake! Ni Lowassa huyu huyu tunayemjua au mwingine? Je ndiyo huku kuanza kujisafisha ili kugombea urais 2015? Nisaidieni jamani.

Kumbuka Richmond hii ya Lowassa ndiyo ilizaa Dowans inayolisumbua taifa linaloendelea kuteketea kwa kiza na wizi wa mabilioni ya kulipa Dowans.
Wapo waliojitokeza kumtetea, kumpongeza hata kuanza kumsafisha Lowassa. Amewafurahisha wanaompigia debe kwa kukemea kilichotokea Misri ambapo rais aliyetimuliwa Hosn Mubarak anasemekana kuwa na ukwasi wa takriban Dola za Kimarekani 40 hadi 70,000,000,000.

Hili "limemkera" sana Lowassa ambaye, kwa bahati mbaya naye anatuhumiwa kujirundikia utajiri utokanao na kuuibia umma ule ule anaodai kuutetea!
Rejea madongo ya kujilimbikizia utajiri aliyorushiwa na marehemu baba wa taifa mwalimu Julius Nyerere na asijibu. Rejea kuchunguzwa kwa mwanae nchini Uingereza anakodaiwa kuingiza mabilioni yasiyo na maelezo. Rejea kuhusishwa kwake moja kwa moja na Richmond hadi kutimka bila kutoa maelezo.

Lowassa anasema asichotenda na kutenda asichosema ili kumhadaa nani? Kama ni ushauri wa bure ampe swahiba yake Jakaya Kikwete na si kutafuta umaarufu wa reja reja akidhani watanzania hawajui yake.

Je Lowassa anataka kumhadaa nani ahadaike na kumwamini? Yaliyotekea Misri yako mlangoni Tanzania ambako hali ni mbaya zaidi ya Misri. Wizi unaotendeka Tanzania ni mkubwa kuliko wa Misri. Linganisha maisha ya wamisri na watanzania utajua ninachomaanisha.

Kama Lowassa anamaanisha anachosema na kusema anachomaanisha, arejeshe pesa yetu kwanza na kuomba msamaha kwa kutuingiza kwenye kiza mbali na kutuibia mabilioni nyuma ya Dowans.

Lowassa anawapongeza wamisri kwa lipi iwapo wamewatimua akina Lowassa wao?

Saturday 12 February 2011

Je hawa ndiyo vinara wa ufisadi Tanzania?

Je orodha imekamilika? Unaweza kuongeza wale unaodhani wameachwa nje. Tunaibandika kama tulivyoipokea toka Jamii Forums leo.









No Questions Taifa la Tanzania lina angamizwa na hawa Mubarak wetu hapo juu. Juhudi kubwa wanazofanya kulindana kuliharibu Taifa la Tanzania na kuhakikisha "Watanzania Wanawaogopa" Taarifa tunataka wana-CCM muwafikishie ni hivi:
Watanzania Tupo Hatua kumi Kufikia Tahrir Square na Tukifika Haturudi Nyuma

Chanzo: Jamii Forums

Friday 11 February 2011

Hebu angalia utabiri huu wa kukera kwa CCM,CUF, NCCR na nyumba ndogo nyingine


Source: Jamii Forums

Hatimaye umma waangusha gogo liitwalo Mubarak




Imetangazwa rasmi kuwa imla wa Misri Hosni Mohammed Mubarak amebwaga manyanga baada ya shinikizo la umma kushinda. Ni furaha si kwa wamisri tu bali dunia nzima hasa Afrika ambako kuna Mubarak wengi tu.

Japo inatia shaka busara iliyotumika kulikabidhi jeshi madaraka, kuna haja ya kutopoteza matumaini kutokana na jeshi lilivyochangia kumwangusha Mubarak baada ya kugoma kumuunga mkono.

Hili ni somo tosha kwa majeshi mengine ambayo yamegeuzwa nepi za watawala wezi.
Je kuanguka kwa Mubarak ni mwanzo wa mwisho wa uimla barani au kizazi kipya cha vuguvugu la ukombozi wa pili na wa kweli wa bara hili?
Je baada ya Mubarak nani atafuatia? Libya, Algeria, Sudan, Morocco, Mauritania, Saudia, Yemen, Jordan, Kuwait na Afrika Kusini mwa sahara kuondoa Afrika Kusini, Botswana na kidogo Kenya watawala wamo msambweni. Je nchi yangu ya Tanzania itanusurika? Je ushindi huu ni wa umma au wanajeshi? Nini kitafuatia? Ni swali gumu kujibu.