The Chant of Savant

Thursday 30 May 2013

Maskini Profesa Anna Tibaijuka!


Ingawa kibonzo hiki kinaweza kutafsiriwa kama utani, kina ukweli zaidi ya utani. Kwa ufupi ni kwamba Msaoud Kipanya anajaribu kuonyesha jinsi waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi profesa Anna Tibaijuka yumo kitanzini baada ya Yuda Iskariot yaani bosi wake kumuacha asulubishwe. Pia ni suto kwa wana taaluma wanaoacha taaluma zao na kujiingiza kwenye siasa za kifisi na kibabaishaji. Na kama kuna vipande thelathini vitakavyomsulubisha profesa Tibaijuka si vingine bali vile vilivyotolewa na mwenye nyumba ya Indira Gandhi na ile ya  Getrude Rwakatare ambayo ilijengwa kwenye eneo lisiloruhusiwa kisheria. Je Tibaijuka ataufyata na kuendelea kuramba matapishi yake au ataamua kulinda heshima yake na kuachia ngazi? Time will accurately and punctually tell.

Tuesday 28 May 2013

Tufanye mpango Kikwete aende kutalii mwezini

Picha kwa hisani ya Michuzi blog


Wapo waliomheshimu na kumwita Vasco da Gama wakimaanisha yule jambazi wa kireno aliyezunguka dunia akitafuta pa kupora. Wasio na muda wa kufichaficha walimwita mzururaji huku wale wanaomheshimu walimwita mtalii. Wengine wanamwita msanii kutokana na tabia yake ya kufanya mambo kisanii. Yote amefanya hili la kuizunguka dunia limemkaa. Rais anazurura utadhani waziri wa mambo ya nchi za nje! Kwa vile Kikwete na mkewe walishaizunguka dunia nzima, napendekeza afanyiwe mpango aende kutalii anga za juu kupitia mradi wa sasa wa kupeleka watalii kule unaofanywa na vyombo vya anga binafsi.

Uombaomba wetu ni wa kujitakia


TAARIFA na ripoti za kufichuliwa wizi wa mabilioni ya shilingi unaotokea kila mwaka zinasikitisha sana.
Hivi karibuni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alifichua kuwa makampuni ya uchimbaji madini kwa mwaka wa fedha uliopita yalikwepa kulipa kodi kiasi cha dola za Marekani bilioni moja.
Hii ni pesa nyingi hasa kwa taifa maskini na ombaomba kama Tanzania. Hizi dola bilioni moja ni makampuni ya madini tu. Je, hayo makampuni ya simu, wahamiaji haramu wanaofanya kila aina ya biashara halali na haramu, mabenki, waagizaji na wauzaji bidhaa nje, makampuni ya utalii, maduka ya kubadili fedha za kigeni, wafanya magendo na wengine wanatuibia mabilioni mangapi?
Inatia kinyaa kuona mamlaka zinazembea kukusanya kodi na badala yake zinaendekeza kukopakopa na kuombaomba bila sababu ya msingi.
Ukiangalia mianya ya misamaha ya kodi na ukwepaji kodi nchini, unagundua kuwa taifa letu ni tajiri sana. Laiti ungepatikana uongozi unaoweza kukusanya kodi hata kwa kiwango cha robo, taifa letu linaweza kujitosheleza kwa bajeti yake na kuwa na kiasi cha kuweka benki.
Ni aibu na ajabu kuona kuwa pesa tunayodhalilishwa kwayo kwa njia ya kuombaomba na kukopa ni tone katika bahari ikilinganishwa na ile tunayozembea kukusanya na kufuja.
Hakuna nchi iliyowahi kuendelea kwa njia ya kuzembea kukusanya kodi na badala yake ikawekeza kwenye kuombaomba na kukopa hovyo tena mikopo yenyewe yenye riba kubwa.
Kama kuna jinsi ya kuelezea hivi, ni kwamba tuna umaskini na uombaomba wa kujitakia. Ni kwanini hatuoni hata aibu kuona rais wetu anavyodhalilika kila uchao kwenda nje kuomba wakati pesa inapotea hivi hivi kutokana na watu wachache mafisadi na waroho kuruhusu wengine waibe pesa yetu na kusamehe kodi ukiachia mbali kuachia mianya ya kukwepa kodi? Tunamkomoa nani?
Je, kwanini wakubwa wetu wanafanya hivi? Jibu ni rahisi kuwa wameridhika na mabaki ya ‘ten percent’ wanayopewa kiasi cha kushindwa kuelewa kuwa wangeamua kukusanya kodi na kusimamia rasilimali zetu vizuri wana uwezo wa kujilipa hata mara tatu ya mabaki wanayohongwa.
Kama siyo hivi ni nini? Kwanini wanafanya hivyo wakati wana elimu ya kutosha? Lazima kuna sababu tena zaidi ya hiyo tajwa hapo juu. Hata hivyo, tunaweza kufupisha matatizo yote kwenye neno moja tu- UFISADI.
Hivi karibuni Mbunge Zitto Kabwe Kigoma Mashariki (CHADEMA) alikaririwa akishangaa kuhusu hujuma hii tunayotendewa kama taifa.
Alisema kuwa Rwanda ambayo wateja wake wa simu ni wa kampuni moja ya Vodacom, iliweza kukusanya kodi ya dola milioni 14 wakati Tanzania yenye makampuni mengi ya simu ilikusanya kiasi cha dola milioni 1.4. Kabwe alisema: “Sasa serikali ikusanye kodi iache bla bla, TCRA ipewe mamlaka kama TMAA, sasa imetosha.”
Kinachoshangaza ni kwamba Kabwe alipofichua hujuma hii kwa taifa, mamkala husika zilikuja na vitisho kuwa ni kinyume cha sheria kufuatilia shughuli zake.
Je hawa jamaa wa TCRA wanadhani hayo maofisi wanayotumia kuhujumia taifa ni mali ya mama zao?
Inahitajika roho ya mwendawazimu kukubali kuwa taifa lenye kila aina ya rasilimali hasa madini linaweza kuzidiwa na viinchi jirani kama Kenya na Rwanda ambavyo havina rasilimali hata nusu yetu.
Sijui kwanini hatujisuti na kuona aibu tunavyoonekana mataahira waliokalia utajiri mkubwa huku tukiombaomba kuanzia misaada hadi rushwa?
Tumejigeuza majuha na hayawani kama samaki aliyekufa kwa kiu kutokana na kushindwa kutumia maji aishimo!
Tusiwe kama tembo ambaye huwa ana nguvu nyingi ya kuangusha miti lakini akaishi bila hata kibanda huku akishindwa na nyuni ajijengeaye kiota pamoja na udhalili na utepetevu wake.
Ajabu ya maajabu yetu ni pale tunaposhabikia kuwa na serikali kubwa bila sababu.
Kila awamu ukiachia mbili za mwanzo inasifika kwa kuanzisha wilaya na mikoa mipya ili kukidhi haja binafsi za baadhi ya wanasiasa wakubwa au marafiki zao. Pigo ni pale tunaposhabikia hata kununua migari ya bei mbaya karibu kwa kila mkubwa hata wa ngazi ya chini.
Kama wendawazimu unaoendelea hautakomeshwa, tutaendelea kuonekana kama jamii ya mazuzu na wehu.
Tutashindwaje kuonekana mataahira iwapo tunao ubingwa wa kurudia makosa na madudu mengi hivi?
Ni ajabu kuwa hata watawala wetu hawalioni hili. Kwanini, kwa mfano, kuendelea kushuhudia rais wetu akiombaomba kana kwamba nchi yetu haikujaliwa raslimali na akili?
Sijui kama rais anajisikia vizuri kwenda kuwapigia magoti marais wenzake kuomba hata pesa ya bajeti. Tumsaidie rais wetu aachane na udhalili huu.
Ni bahati mbaya kuwa mfumo wetu umekuwa wa kihasara hasara. Hebu angalia kwa mfano tulivyo na serikali kubwa bila hata sababu ya kufanya hivyo.
Ni bahati mbaya kuwa tangu kuondoka mzee Mwinyi karibu kila rais aliyeingia baadaye alianzisha au ameanzisha wilaya na mikoa bila sababu za msingi zaidi ya masilahi binafsi ya baadhi ya wanasiasa.
Mkapa alianzisha Mkoa wa Manyara nyumbani kwa waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye huku Kikwete akianzisha Katavi nyumbani kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Geita, Njombe na Simiu. Tunaongeza mikoa kwa utajiri gani?
Hebu kwa mfano angalia majirani zetu wa Kenya. Serikali mpya pamoja na kuruhusiwa kuunda baraza la mawaziri wasiozidi 22, kwa kuzingatia mzigo kwa uchumi, iliunda wizara 18. Sie tunao 50 na ushei! Hii ni akili au matope?
Kwa ufupi ni kwamba kinachoisumbua nchi yetu si ukosefu wa rasilimali kuanzia watu hadi madini na vitu vingine bali ombwe la utawala.
Utawala wa namna hii hauwezi kuivusha nchi yetu zaidi ya kuizamisha kama inavyoanza kujidhihirisha ambapo rasilimali zetu zimegeuka laana badala ya Baraka.
Kuna haja ya watawala wetu kujua kuwa kila jambo lina wakati wake. Wajifunze kutoka kwenye tawala zilizowahi kuamini kuwa haziwezi kuguswa na walalaho. Mfano wa karibu ni anguko la aibu na ajabu la Muamar Gaddafi kule Libya hivi karibuni.
Chanzo: Tanzania Daima Mei 28, 2013.

Monday 27 May 2013

When Waishiwa, sorry, wahishimiwa became MPigs!

 I was invited to Nairobi aka Nairobbery just recently to participate in the just concluded peaceful demos aimed at stopping greedy Member of Mjengo from increasing their yum-yum. Under what’s known as over-the-top-greed-reloaded, Kenyan patriots wanted to show the MPs how Mpigs they've become. The first bird gets the worm. I, thus, didn't waste any time. How could I take a back seat and wait to be told while such avarice needed patriotism- reloaded action? Needless to say, who knows? When my own hishimiwas become as greedy as pigs or next to it? Methinks shall this happen, my Kenyans allies will reciprocate by joining me to call ‘em Mpigs.
There are some realities one needs to ponder on. Why’d the so-called representatives of the people become the representatives of their tummies in the first place? Why’d they turn a hunk into shamba la bibi like Danganyika aka Bongolalaland?  Instead of letting the Mpigs make modifications on their ploy, we wanted to force the make mortification in their ulaji.
Thirdly, why’d Mpigs go to Mjengo and deliberate on issues that the voters didn’t send them to?
Four, why’d Mpigs feel neither pity nor shame just like pigs?
If anything, the answers to these questions are what we called Mpigs in lieu of MPs. Metaphorically, even organically; this is a strong message to all self-seekers in public services all over the globe.
The second contentious issue’s why Mpigs should use their power to make laws that favour them instead of their boss namely voters?
After musing on all those important questions, among others, I found myself traveling to Kenya to help other boozers to teach those Mpigs a lesson.  I was under what psychologists call impunity rage. This is the situation that causes rage to those affected by impunity just like Road rage to drivers.
Having a non-forgery PhD in Mass Mobilization and Human Behaviour Analysis, I was the most welcome force on the occasion. Again, those who think I went to blow somebody ass out of the water got it wrong. I went there to save humanity from the hands of greedy Mpigs. Mine’s to make an experiment to see how pigs behave when they become MPs even for a second as it happened in Nairobbery. True, pigs are cool and non-hypocritical when it comes to shamelessly display their greed. That day we dispatched our pigs and piglet at Kenya’s Mjengo, they started displaying their rapacity right away. The difference from MPigs is that Pigs know no sanaa or pretense and ballyhoos.
You know what.  I’m the one who coined the name Mpigs. Whether this is true or not, pretend that truth has many meanings and characteristics. Those who studied ethos, logos and pathos know what this is. Truth, just like any concept, is polysemic by nature. Your truth is not necessarily my truth. There are many truths and this is my truth.
Against all odds, after arriving in Nairobbery, I advised Bunge la Mwananchi to bring me some piglets, sows or gilts that we’d use symbolically to depict the MPs by showing them the logic of calling them Mpigs. As I said above, logos constituted with pathos were at work.
Why piglets and gilts? We wanted to show how guilty of greed Mpigs are just like pigs are. We agreed that if Mpigs’ cupidity goes on we’ll bring hyenas, fox, rats and caterpillars next time to symbolize greed a great deal more. Essentially, we wanted to show how dirty and shameless Mpigs are. Those who know pigs well will agree with me that they don’t have the word pity in their small brains. So too, pigs eat without stopping even if they’ve had their fill.   They eat and poop wherever they are just like insects. The difference from Pigs and Mpigs is that Mpigs use both hand and legs to eat without even washing them. Pigs have big heads but small brains. Also, pigs don’t care about other as far as eating’s concerned.
  Those fyatus in Kenya were saying that many fat Mpigs should be convicted and the evidence that they are greedy must be their tummies resulting from swindling public trust and property. In a nutshell, pigs and Mpigs are among nasty beasts one can have.
Aren’t the folks who sleep in mjengo Mpigs? What of those dudes who steal money and stash in offshore banks such as Jersey Island, Island of Man you name it? What of the Mpigs who go to mjengo just to solicit sitting aka makalio allowances? How about those who abuse others like Mr. F**k you aka Sheukamba, Lushinde, Khatibuu and others who turn mjengo into kijiwe as some form four failures once wrote in their final exam?
Guess what. We discovered that parliaments are full of wrong people. Right people are in the streets. Jails are full of wrong people and wrong people are free in our streets and offices robbing us. Who’d believe that we’d be beaten for telling the truth? Why shooting a messenger?  By beating us they’re beating the voters we represented. Like many African hunks, Kenya’s such a notorious police force that can be abusively used by politicos to humiliate innocent earthlings.
 Segway, soon I’ll invite my Kenyan sons and daughters of guns to help me take on Anna Makidamakida who’s wantonly turned our mjengo into a piggery.
Coming next week’s a special message to Sheikh Jake Kikwete on his take on religious chaos which he said are caused by foreigners while they actually are caused by our home-grown pampered terrorists and some members of his outfit lead by Mwiguu Nchemba.


So long,
Source: Thisday May 27, 2013