The Chant of Savant

Tuesday 30 November 2021

Mheshimwa Rais, nakusalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama kiongozi wake tena mwanzilishi wa salamu hii. Leo barua yangu inaweza kuonekana kama yenye kungung’unika hata kukata tamaa. Naweza kukiri kuwa sina raha kuhusiana na ninalokuandikia. Naandika kuhusiana na sintofahamu ya mradi tata wa uwekezaji wa Bandari ya Bagamoyo ambao Hayati Dkt John PombeMagufuli alisema wazi wazi tena mchana kweupe kuwa ni wa hovyo; na hata kichaa hawezi kuukubali. Tarehe 7 Juni, 2019, akihutubia Baraza la Taifa la Biashara (TNBC), Hayati Magufuli alisema kuwe “kwenye mkataba wa ujenzi wa bandari hiyo kulikuwa na vipengele vya hovyo” ambavyo hata kichaa asingeweza kuvipitisha na kuutekeleza mradi tajwa. Alisema kuwa “wawekezaji hawa wanakuja na masharti ya ajabu na ni kichaa tu anaweza kuyakubali.”
Magufuli aliendelea kumwaga mtama ambao kuku sasa wanatema kuwa “huruhusiwi kukusanya revenue…. unatakiwa uwape guarantee (dhamana) ya kwanza bila hata kuulizwa kwa miaka 33. Unatakiwa uwape lease (mkataba wa kumiliki wa ardhi) tofauti na sheria za nchi ‘for 99 years’ (kwa miaka 99) na huruhusiwi hata kwenda kumuuliza atakayekwenda kuwekeza pale na wao wawe na mandate (mamlaka)ya kuchukua hilo eneo kama ardhi yao.” 
        Kuzidi kutoa maarifa zaidi Magufuli alisema “ni nchi gani hiyo ambayo unajenga Bandari ya Da res Salaam, tunachimba sasa hivi bath (gati) 0 hadi 10 kwa gharama ya Sh1.2 trilioni, tumekopa fedha… na contractor (mkandarasi) yupo na inawezekana at the end of this year (mwishoni mwa mwaka) watamaliza…tutakuwa tunapata mizigo karibu ya mara tatu inayoingia…leo hii unakwenda kudump (kutupa) hela pale Bagamoyo maana yake siutakuwa unaua bandari hii iliyoachwa na Nyerere?”
Japo Magufuli alikuwa binadamu, linapokuja suala la uzalendo, sijui kama kuna mwenye shaka juu yake hasa tukiangalia mambo aliyoweza kufanikisha ndani ya muda mfupi wa uongozi wake mfupi lakini wenye kutukuka. Hivyo, tunapomlinganisha na wanaotuambia mambo tofauti na yale aliyosema, ukweli, tunaingia kwenye kishawishi cha kuanza kujenga mashaka hata kabla ya kupata maelezo japo Magufuli hakuwa malaika bali binadamu na mwanasiasa.
        Mheshimiwa Rais, hata kabla mwili wa Hayati Magufuli haujaoza wala kauli zake kufanyiwa kazi, aliibuka Waziri wa Viwanda na Biashara Godfrey Mwambe––naye akisema hadharani japo bila kutoa maelezo ya kina kuwa––––hakuna mkataba wakati Rais alisema upo na ni wa hovyo. Kusema ukweli, Mwambe alituchanganya na kutushangaza wengi kwa kusema na kurudia kuwa hapakuwa na mkataba. Alituacha hoi zaid pale aliposema kuwa mengi yaliyosemwa hata hajui yalitoka wapi wakati si ya kweli. Mapaka sasa, tunaomfahamu Hayati Magufuli nawe Mheshimiwa Rais hatujaamini masikio yetu achilia mbali ukweli wa suala zima. Tunashindwa kuelewa ukweli na uongo ni upi na kwanini na kunani. 
    Mheshimiwa Rais, katika kukumbuka na kutafakari kauli za Magufuli, je hapa ukweli ni upi? Je hapa tumwamini nani kati ya Hayati Magufuli, mzalendo wa kweli kwa maneno na vitendo na mteule wake Mwambe ambaye anasema anakuwakilisha wewe ambaye ulikuwa msaidizi wa Magufuli ambaye bila shaka ulijua kila kitu tokana na nafasi yako? Je maneno na msimamo wa mwambe ndiyo vyako? Je wakati Magufuli akisema aliyosema si ulikuwepo? Kama hukujua tueleze na kama ulijua tueleze na kwanini sasa U-turn kama wasemavyo watasha.
        Mheshimiwa Rias, kwa vile Hayati Magufuli na Mwambe ni binadamu tena wanasiasa, tungeomba uingilie kati tujue ukweli na uongo na sababu za kugeuka ghafla bin vu kwa jambo ambalo liliwekwa wazi na kiongozi ambaye wengi walimwamini.
        Mheshimiwa Rais, kwa kumbukumbu zilizopo ni kwamba wewe na Waziri Mkuu mlihudhuria mkutano huu ambapo Hayati Magufuli aliamua kuweka mambo wazi. Sina uhakika kama Mwambe alihudhuria japo nina uhakika anajua kila kitu alichosema Magufuli. Kwa vile maelezo ya Mwambe yanakanganya na yanakosa kujitosheleza, ima wewe uingilie kati au umuamuru aeleze ukweli zaidi hasa akitueleza kati ya yeye na Magufuli nani anasema ukweli au la na kwanini na ili iweje. 
        Mheshimiwa Rais, naomba, kwa heshima, taadhima na unyenyekevu nikushauri kuwa uwe makini mradi huu ambao ni wa fedha nyingi na wenye ushawishi mkubwa. Nadhani ni haki ya umma wa watanzania si kujua ukweli tu bali hata maslahi ambayo mradi unayo kwao. Kwani, haya matrilioni yatakayokopwa na kutumiwa na mradi watalipa wao au watoto au wajuu zao. Kimsingi, watalipa watanzania. Hivyo, wanaoingia mikataba ya hovyo wajue wasijue ni kwamba mwisho wa siku watakaolipa ni watanzania hata kama siyo wa sasa. Niseme wazi kuwa una bahati kuwa uhusiki na kuanzishwa kwake. Hivyo, unaweza kukaa pembeni na kufanya uchambuzi wa kina upya kujua pumba na mbegu baina ya mtangulizi wako na hawa aliosema kuwa walikuwa wakifanya lobbying kupitisha mradi wa hovyo ili kuwaibia watanzania.
       Mheshimiwa Rais, naomba–––chonde chonde–––ututuoe kizani kwa kutafuta na kuupata ukweli ili ukuweke na kutuweka huru kama taifa badala ya kutuacha na shaka huku wasio na subira wakiona kama mtangulizi wako anasalitiwa na watu wake jambo ambalo halifai hata kulifikiria. Naomba leo nisiseme mengi nikingoja kuona uamuzi na hatua utakazochukua.
Chanzo: Raia Mwema kesho

 


Saturday 27 November 2021

Muungano wa Afrika na Ubinafsi wa Watawala

Taarifa kuwa baraza la Mawaziri la Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) inayoleta pamoja nchi za Burundi, Kenya, Rwanda, Sudan Kusini, Tanzania na Uganda limeridhia uanachama wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ni habari njema si kwa DRC bali hata kwa wenyeji wake na eneo la Maziwa Makuu kwa ujumla hasa ikizingatiwa kuwa DRC si nchi ndogo wala maskini kulhali. Kwa kujiunga na EAC, DRC inapunguza uwezekano wa kuvamiwa na vinchi na vikundi vya kihalifu vilivyokuwa vimezoea kuivamia na kuiibia raslimali zake za thamani na lukuki ilizojaliwa. Pili, DRC inapata wenzake wanaoweza kuisadia hata kwenye vita inayoendelea kwa sasa kama nchi husika zitaacha ubinafsi na upogo na zikawa kitu kimoja kweli. Kwani, hali tete nchini DRC inasababisha ukosefu wa usalama si kwa nchi hizo tu bali hata eneo zima la Maziwa Makuu (GLR).
         Baada ya kujiunga kwa DRC–––kama wakuu wa jumuia hii wangekuwa wanaona mbali na si wabinafsi–––wangeungana haraka na kutengeneza ji nchi moja kubwa na lenye nguvu kisiasa na kiuchumi hasa ikizingatiwa kuwa DRC ina ardhi kubwa na raslimali zinazoweza kuifanya nchi hii iwe nae neo kubwa kuliko nchi yoyote ya Afrika bila kuzungumzia vyanzo vikubwa vya raslimali za thamani. Mbali na DRC, Tanzania nayo ina ardhi na raslimali nyingi ambavyo  vikiongezewa na ujio wa DRC vinaweza kufidia kwa nchi nne yaani Burundi, Kenya, Rwanda na Uganda ambazo hazina ardhi wala raslimali zaidi ya watu wake ambao nao mchango wao si haba.
        Akiwa nchini Afrika Kusini Rais Uhuru Kenyatta aligusia suala mipaka akisema wazi kuwa iliwekwa ili kutunyonya na kuwahudumia wakoloni lakini siyo kutuhudumia wala kutuendeleza kama wakazi wa nchi zetu. Hili ni jambo zuri. Ila viongozi wengi wanaongelea kuondoa mipaka na kuungana mbele za watu lakini nyuma ya pazia wanakwamisha juhudi za kuunganisha nchi zao kwa kuhofia kupoteza madaraka na ulaji wake. Huu ni ukweli mchungu na unaoudhi ambao wengi hawataki kusikia. Kwanini Kenyatta hajawaambia wenzake wa Afrika Mashariki ambao tayari wana Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) kama wao si kikwazo kikubwa kinachozuia muungano wa EAC na Afrika kwa ujumla? Kenyatta aliongelea kugawanywa kwa wamasai na waluhuya kati ya Tanzania na Kenya na Kenya na Uganda mtawalia. Alitolea mfano wa ndugu wawili wa baba na mama mmoja, Moody Awori aliyekuwa Makamu wa Rais wa Kenya na mdogo wake Aggrey Awori ambaye alikuwa alikuwa Waziri kwenye serikali ya Uganda akiwa mganda  tokana na kurithi shamba lililokuwa Uganda baada ya kugawanywa kabila lao kati ya nchi mbili zilizoundwa na wakoloni. Mifano tunayo mingi. Hata hizi nchi tulizoundiwa na kujivunia kwa sasa si chochote wala lolote bali kongwa za kikoloni. shingoni mwetu kama mataifa na jamii.  Wakati wa kuunganisha Afrika ni sasa. 
        Mwaka 2015 nilitoa kitabu kiitwacho Africa Reunite or Perish nikiongelea umuhimu wa kurejesha muungano wa Afrika na faida zake. Niligusia mambo kama vile umaskini ambao unaweza kuondolewa na muungano wa Afrika pale itakapokuwa imeondokana mambo yanayoifanya iwe maskini kama vile utitiri wa marais, majeshi, benki kuu, visa, kutokuwa na uhuru kwa waafrika kwenda watakapo wakati watakapo kwenye bara lao na mengine mengi kama vile. nchi nyingi kufanya biashara na mataifa ya mbali huku yakikwepa majirani zake wa kubambikiwa wakati wao ni kitu kimoja. Mfano mdogo ni pale unapokuta nchi haina dawa za malaria wakati haikosi mabomu ya machozi.Mfano mkubwa niliotoa ni kuangalia matumizi ya majeshi yetu kwa kila nchi ikilinganishwa na huduma za jamii.
        Ukisikiliza maneno matamu na mazuri ya Kenyatta, yanatia moyo. Hata baba wa taifa, Hayati Mwl Julius Nyerere alizoea kuongelea na kupigania muungano wa Afrika. Lakini hakuna kilichofanyika tokana na marais kunogewa na urais na kulitekeleza bara letu kiasi cha kuonekana wakoloni zaidi ya wale wa kizungu. Kadhalika, Baba wa taifa la Ghana, Hayati Kwame Nkrumah alitaka Afrika iunganishwe mara moja kama ilivyogawanywa. Lakini Nyerere alitaka iunganishe taratibu kiasi cha kushindikana. Tujiulize; kama siyo ubinafsi na uchu wa urais, nini kimewazuia kuuganisha Afrika kama siyo kuendekeza ubinafsi na ukoloni wakati wakijua fika kuwa hivi vichi tulivyo navyo vimegwa na wakoloni ili kutudhoofisha, kututawala, na kutunyonya waafrika? Hata hivyo, baada ya kupata uhuru wa bendera, wakubwa wetu walishindwa kuviunganisha tena kwa kuogopa kupoteza urais wao.
        Tumalize kwa kuuliza maswali yafuatayo hata kama yanaudhi:
    Je tutaendelea hivi hadi lini wakati tunajua chanzo cha udhalili na umaskini wetu kuwa ni kuendelea na mipaka ya bandia ya kinyonyaji na kikoloni iliyowekwa na wakoloni?
    Je kuungana kunahitaji wafadhili toka Ulaya kiasi cha kuendelea kusuasua wakati tatizo siyo nia ya wananchi bali uchu wa urais wa watawala wetu japo si wote? Je wananchi wetu wanasemaje ikizingatiwa kuwa ndiyo wahanga wakubwa wa ukoloni huu wa kujitakia?
        Mwisho, kwanini tusianze sasa kama Jumuia ya Afrika Mashariki tukatoa mfano kwa wengine ambao wanaweza kuvutiwa na mafanikio yetu? Badala ya kuendelea kuwadanganya na kuwahadaa watu wetu na dunia kuwa tuna nia ya kuunganisha Afrika kama kitendo cha kujivua ukoloni wa kujitakia, watawala wetu wafikie mahali waamue kuwa wakweli. Waseme wazi wanavyopenda, kunufaika na kuridhika na mgawanyiko wa Afrika kwa vile unawapa madaraka binafsi au waachane na tamaa binafsi tuunganishe nchi zetu haraka sana kwa faida kubwa ya wote. Wananchi wako tayari.  Hivi kweli ukiwauliza wamasai wa Namanga, wajaluo na wakurya wa Musoma au wahangaza wa Ngara kuunganisha nchi zetu, kweli watakuwa na sababu yoyote ya msingi kupinga wakati mipaka imegeuka kama kongwa kwenye shingo zetu? Kuna haja ya kuacha uvivu wa kufikiri––––nikikopa maneno ya Hayati Benjamin Mkapa––––na kuanza kuunganisha nchi zetu haraka k ama zilivyogawanywa mwaka 1884 kwenye mkutano wa kijambazi wa Berlin. EAC lazima iwe mwanzilishi wa muungano wa Afrika.
Chanzo: Raia Mwema leo.

Thursday 25 November 2021

60 YEARS OF INDEPENDENCE : REFLECTIONS ON BUNGE ’s POST-INDEPENDENCE PERFORMANCE.

On  Monday  last  week,  by  prior  arrangement  and  agreement;  a  delegation  of  information  officers  from  the  Speaker’s  Office  in  Dodoma,   visited  me  at  my  cozy  retirement  home  in  Ukerewe;  on  a  dedicated  mission  to  make  a  video  recording  of   the   memorabilia  of  a  retired,  long- serving   Speaker  of  the  National  Assembly,   regarding  BUNGE’s   “growth  and  development”  during  the whole  of  this  period  of  six  decades. I  was,  of  course,  very  delighted  to  receive  them,  and  made  a  spirited  oral  presentation  of  all  that  I  could  remember  lasting  for  approximately  one  and  a  half  hours;   essentially  adopting  the  old  Ukerewe  culture  and  tradition  of  the grandfather telling  stories    to  his  grandsons in  the evenings at the family ‘s   ekikome  (fireplace).                            
        They  said  they   will  subsequently  publish   that  information  in  their   BUNGE  journal,  and  in  the  other  dedicated  BUNGE  media  channels.  But  since  this   narrative  fits  very  well  into    my  series  of  articles  on  “Sixty   years  of  independence”;  today’s  article  will  largely  be  a  repeat   of  this  ‘mind-refreshing’,   political  history   information   relating  to  BUNGE’s   post-independence performance. And  it  will  focus  primarily  on   the  following   specific  areas:-   
(i) Bunge’s  structural  development,  i.e.   the  progressive  changes in  the  composition  of  its  membership;                                                
 (ii)  the  consolidation  of  its  powers  and  privileges;  and                                             
(iii)   my  own  personal  involvement  in   this  institution’s  affairs.
BUNGE’s  STRUCTURAL  DEVELOPMENT.
The   story  of  the  Tanzania  Parliament,  or  “ BUNGE  LA  TANZANIA” in  Kiswahili, actually  starts  way  back   in  1926,  when  the  British  colonial  Administration  in  Tanganyika (which  was  administered as a “British   Mandated  Territory” under the mandate dully  granted  to  it  by  the  United  Nations Organization),  advised  the  British Government in London, to enact legislation establishing  a  Legislative  Body  for  Tanganyika.   That  advice  was  accepted,  and  resulted  in the  enactment by the  British  Parliament,  on  19th  March,  1926,  of  a  statute  titled:  “The  Tanganyika  (Legislative  Council)  Order-  in- Council,  1926”.   
        After   its  establishment,  the  new   Legislative  Council,  consisting  of  20  members  nominated  by  the  Governor,   held  its  first  session   in  Dar es  Salaam   on  7th  December,  1926.    However,  for  a  period  of  20  long  years,  the  Tanganyika  Legislative  Council  had  no  Tanganyika  Africans  among  its  members.     The  entry  of  such  members   first  occurred  on   24th  September  1945;  when  Governor  Sir  William  Battershill    appointed   Chief  Abdiel  Shangali  and  Chief   Kidaha  Makwaia.  The third  African  member  Chief  Adam   Sapi  Mkwawa,   was  appointed  two  years  late  on   3rd  June,  1947,  closely  followed  by  the  fourth  African  member  Mr.  Juma  Mwindadi,  who  was  appointed  on  1st  April,  1948.  
        Another  structural  development  occurred  in  1953;  when the  Governor  ceased  to  be  Chairman  of  that  Institution,  upon  the  introduction  of  the  post  of Speaker  of  the  Legislative  Council.   The  first  such   Speaker  was    Brigadier  William Scupham,  who  took  the  oath  of  office  in  that  capacity,   on  1st  November,  1953.
          Mwalimu  Nyerere’s  nomination,  and  resignation :  a  lesson  in  ethical  leadership.
Of  much  greater  political  significance  during  this  period,  was  the resignation  of  Mwalimu  Julius  Nyerere,  only  six  months  after  he  had  been  nominated  to  the  membership  of  the  colonial  Legislative  Council;  purely    for ethical  reasons.   It  has  been  said  that  “ethics  is  the  heart  of  leadership”    This  big  heart  was  amply   demonstrated  by   Nyerere  trough  that  heroic  action.
        Mwalimu  Julius  Nyerere  was  nominated  by  the  Governor to  the  membership  of  the  Legislative  Council  in  July,  1957.  But  only  six  months  later  in  December  of  the  same  year,  he  announced  his  resignation  there  from, and  publicly  explained his   sole  reason  for  doing  so,  which  was that  the  colonial  Government  was  paying  no  attention  to  any  of  his  reasonable  proposals  which  he  submitted  to the  House  relating  to  the  pace  of  constitutional  development  to  the  country’s    independence. 
        The  next  major  change  in  the  Legislative  Council’s  structure  was  introduced   in  1959;  when  the   Council’s   first  elected  members  entered  the  House;    as  a  result  of  the  country’s   first-ever    Parliamentary  general  election  of  1958/59.                               
        Further   structural  changes    which  were   subsequently  introduced,  include   that  of  1st  May,  1961,  when  the  name  of  the  Tanganyika’s Legislature was changed  from  “Legislative  Council” to “National  Assembly”,  through  another  statute  enacted  by  the  British  Parliament, which  was  titled: “The  Tanganyika  (Constitution)  Order-in-Council, 1961”.  
THE  ENTRY  OF THE  FIRST   WOMEN  MEMBERS  THEREIN.  
“ A  woman  with  a  voice  is,  by  definition,  a  strong  woman”   (from   “Women  Quotes”  by  Belinda  Gates).   Parliament  is,  indeed,  the  most  appropriate forum  for  giving  women  an  effective  “voice”  in  the  affairs  of  the  country’s   governance.     women’s  participation  in  the Legislature of  Tanganyika,  started  during  the  colonial  Administration  period,  precisely   1955;    when  the  first  three  women  were  appointed  by  the  Governor  as  Members  of  that                          Legislative  Council,  and  they took  the  oath  of  office  on  19th  April,  1955. They   were,  respectively,   Elifuraha  Mkamangi  Marealle; K.F. Walker;  and  S.  Keeka.  Further  nominations  of  women  Members  were  made  by  the  Governor  in  1956  (Mary  Kashindi);  and  in   1958  (Bertha  Akim;  and  J,  Davies.   
        It  is  the   independence  Parliament  (1960 – 1965), which  brought  on  board  the  first  elected    Members.  They  were: Marion  Lady  Chesham  (Iringa);   Babro  Johansen (Mwanza);  E. Markwada (Tanga  Urban);  Bibi  Titi  Mohamed  (Rufiji);  Sophia  Mustafa  (Arusha);  and  Mwami Theresa  Ntare (Kasulu);  plus  two  nominated  Members:   Lucy  S.  Lameck  and  Cecilia  Paes.
The  subsequent  post-independence  Parliaments  have  progressively  increased  their  numbers,  especially  after  the  introduction  of  the  new category  of   “women’s  special  seats”.
        The  independence  Parliament (1960: its  conversion  to  the  designation  “Parliament”. 
In  recent  times,  there has  developed  a  convenient  practice  of  referring  to  the  successive  phases  of  BUNGE  LA  TANZANIA  in terms  of  numbers.  For  example,  the  current  phase  BUNGE  is  generally  referred  to  as  the  “Twelfth  Parliament”.  It  may  be  helpful  to  explain  that  this  counting  actually  starts  with  the  1st  post-Independence  Parliament  of  1965 – 1970.    It  is   precisely  for   that  reason,  that  the  Parliament  which   existed  at  the  time  when  UHURU  was  achieved,  is  referred  to  as  the  ‘Independence  Parliament’. 
        The  Legislative  Council’s  conversion  to  the  designation  ‘Parliament”. In the  British  parliamentary  usage  and  practice;  the  term  “Parliament”  is   normally  used  to  describe  one  of  the  three  ‘pillars’ of an independent  State,  as  its   Legislative   Branch. The  other  two  pillars  of  State  are   the  “Executive”  and  the  “Judiciary”  Branches.   And  that   is  precisely   the reason   why,   before  Tanganyika’s  independence,   the  country’s  legislative  Branch  was  designated  not  as  the ‘Parliament’;   but  as  the  ‘Legislative  Council’,  or  subsequently   as   the  ‘National  Assembly’. However,  article  62(1)  of  the  Constitution  of  the  United  Republic  of  Tanzania   provides  that  ‘Parliament’   shall  consist  of  two  distinct  parts:  one  of  which  is   the  President  of  the  United Republic;  and  the  other  is  the  National  Assembly;    But,  the  Kiswahili   designation   of    “Bunge  la  Tanzania”,  is  inclusive  of  both  these  parts,  and  is  freely   used interchangeably,  to  mean  either  the  National  Assembly  alone,  or  the  entire  Parliament.  
        The “teething”  challenges  of    the  ‘Independence  Bunge’  (1960 -1965). “We  must  run,  while  others  walk”;   is  one  of  President  Nyerere’s  famous,  immortal, tit-bits.             The  Independence  Bunge  of  1960 -1965)  was  characterized   notably  by  the  exceptionally  high  speed  at  which  it  enacted  legislation;  under  the  “Certificate  of  Urgency”   National  Assembly  procedures;  which  enable  the  Government  to  present  a  Bill   at  a  much  shorter  notice,  which  is  anything   less    than  the  stipulated   21  days  notice. The  first   post-independence  government  understandably  made   very  extensive  use  of  this  provision;  but   it  was  indeed  necessary,  in  the  prevailing  circumstances  at   the  material  time.   
        Among  the  most urgent  tasks  facing  President  Nyerere  upon  his  assumption  of  the  Presidency,  was,  inevitably,  that  of the  need  to  de-colonization   the  government  structures,  processes,  practice  and  procedures;  in  respect  of  all  the  areas  of  government activities ,  by   urgently  dismantling  all  the  colonial  structures  and  processes  that  had  been left  behind  by  the   previous   colonial  Administration;  and  almost  all  of  this  work  had  to  be  carried  out  through  the  urgent  introduction  of  appropriate   legislation,  in  order  to  reform  the  entire  governance   system.  This  is  what  justified  the  government’s  resort  to  the  special  procedure  of  presenting a  large  number  of   Bills  in  the  National  Assembly   under  ‘certificates  of  urgency’.
        But  this  was,  in  a  way,  a  serious  challenge  to  the  inherent  right  of  National   Assembly  members  to  be  given  ample  time  to  consider  government  proposals;  especially  legislative  proposals,  in  order  to  avoid  the  danger  of  enacting  legislation  without  having  given  sufficient  consideration  to   their contents.
        However,  this  implied  challenge  was  amicably  resolved  by the  MPs  themselves  who,  presumably  in their  patriotic  enthusiasm  and  commitment to  support  the  decolonization  process,  they  always    willingly  and   readily  cooperated;   as  evidence  by  the  fact  that  almost  all    of  such  Bills  easily  sailed  through  all  the  prescribed  stages  in  a  matter  of  only   a  few  hours,  and  always  without  even  a  single dissenting  voice  being  heard.  
THE  CONSOLIDATION  OF  BUNGE’s  POWERS  AND  PRIVILEGES :
 protecting   BUNGE  from  undue  interferences  by   the  EXECUTIVE  Branch. It  should  also  be  noted  that concerted  efforts  have  been  made,  through  appropriate  constitutional  provisions,  to  protect    BUNGE  from  undue  interference  by  the  Executive  Branch  of  Government;  in  two  specific  areas:-  
 (i) there   can  be  no  “prorogation”  of  the  National  Assembly ;  and 
 (ii)  the  President  cannot  just  dissolve  the  House  at  his  discretion. 
No  prorogation  of  the  National  Assembly.
One  established   way  of  exercising  such  interference,  is  through  a  process  known  as  the   “prorogation  of  Parliament”;  whereby  the  country’s Head  of State is constitutionally   empowered  to  send  the  House “on compulsory  holiday”.  These efforts to  protect the  House   were  first  manifested  during  the  making  of  the  Tanganyika  Republican  Constitution  of  1962 ;  when  a  provision  was included  which   denied   that  power  to  the  Head  of  State.  This  power  had  been  provided  for in  the   previous   Independence  Constitution.  As  was  explained  by  Prime  Minister  Rashid  Kawawa,   in  his  speech  introducing  the  motion  for  the  Second  Reading  of  the  Bill  for  the  new  Constitution,  in  which  he  said  the  following:-    “Mr.  Speaker,  the  abolition  of  the  power   to  prorogue  the  National  Assembly  is  a  departure  from  previous  practice.  We  have  accepted  it  after  full  consideration,  in  order  to  emphasize  the  sovereignty  of  Parliament.   
No  discretional  dissolution  of  Parliament.
And,   in  addition  to  that,  there  is  another  provision  in  the  current  (1977)  Constitution  of  the  United  Republic,  (article  90 (2);  which  denies  the  Head  of  State  the  discretion  to   dissolve  Parliament  at   any  time  he  may  wish  to  do  so.  This,   again,  was  designed  in  order   to  emphasize  the  sovereignty  of  Parliament.    
My  own  close  association  with  BUNGE  LA  TANZANIA.
        My   personal,   close,  and   direct   involvement  in the  affairs  of  BUNGE  commenced in  1960,   during   the  Independence  Parliament;  when  I  was  appointed  Clerk-Assistant  of  the  National  Assembly  (Training  Grade),  apparently  in  preparation  for  my  possible  subsequent  taking  over  the  Clerkship  of  the  House  from  the  British  officer  Geoffrey  Hucks  after  the  country’s  independence,  if  I  successfully  made  it.    Fortunately  I  made  it,   and was  appointed  to  that  position  effective  from  9th  December,  1962,  the  first  anniversary  of  the  country’s  independence.                                                But  I  had  to  deal  with  the  inevitable   ‘teething’  challenges  which arose as  a  result  of  this  fundamental  transition    from  colonialism;  and  particularly  the  need  to  transform  the  Parliament  itself  from  its  entrenched  colonial  model,  to  an  entirely  new  and  different  model  that  would  be   is  in  line  with  the  country’s  new  independence  status;  a  task  which  turned  out  to  be  pretty  challenging.  
piomsekwa@gmail.com /0754767576.
Source: Daily News today.              

Almost Three Months Without Nobesuthu Mbadu


It is almost three month since we lost Nobesuthu Mbadu, of the Mahotella Queens group who untimely left us. Those who use to love the group–––I hope–––still badly and lovely miss this music icon who was among the creators of Mbaqanga. We, thus, today, take deep breath to remember our lost heroine Nobesuthu Mbadu (RIP).
I sincerely take this rare opportunity to pay tributes to my lost dear friends, namely John Njema Ndamu (1st June, 1957––––27th June, 2021) of Githakwa, Tetu, Nyeri Kenya; and 
Attilio Tagalile  (1950–––2021) of Mbezi Tangi Bovu, Dar es Salaam, Tanzania, who untimely passed on this year.  Those who call me Dr and Prof Nkwazi don't know the giants on who knew me and on whose shoulders I stood to become who I am. May Their humble and loving Souls Be Accepted and Rest in Eternal Peace. Aaaamin.
Late Chairman John Ndamu Njema



Late Attilio Tagalile 







 

Wednesday 24 November 2021

Know Magdalena Andersson Swedish PM Who Served for Hours

 

Being the first Swedish female Prime Minister, Magdalena Andersson shocked many when she resigned soon after being confirmed. Why did she do so? CLICK THE LINK to know more about this unique leader.


Tuesday 23 November 2021

Wengi Wasichojua Kuhusu Ng'ambo

Hivi juzi, nchi ya jirani ya Marekani, kijana wa kizungu Kyle Rittenhouse aliishangaza dunia alipoachiwa huru baada ya kukutwa hana hatia kwa mashitaka matano ya uuaji. Kilichofanya ashangaze dunia ni ile imani kuwa angekuwa siyo mzungu, angefungwa kwa makosa yote si kwa sababu aliyatenda au la bali kwa vile ni mweusi. Hivyo, leo, nitaongelea ubaguzi wa kimfumo japo kwa usiku. Kabla ya kuanza kuishi hapa Kanada, sikujua ubaguzi katika uhalisi wake. Ubaguzi haukuwa moja ya suala ambalo lingenihangaisha kama ilivyo sasa hasa baada ya kuingia kwenye taaluma ya kusuluhisha migogoro, diplomasia na vita hasa ugaidi. Nikiwa nyumbani, nilizoea kumsikia Hayati Christopher Mtikila akilaani ubaguzi japo kwa ubaguzi jambo ambalo sikuliunga mkono. Hata hivyo, Mtikila atakumbukwa kama mtanzania aliyesimamia haki na usawa wa watanzania ambao–––hata hivyo, bahati mbaya–––si wengi walimuelewa.
Nilipoanza kuishi hapa nilianza kumkumbuka na kumuelewa Mtikila kuliko wakati nilipokuwa nyumbani hasa baada ya kuona hapa tunavyoitwa watu wa rangi au peoples of colour. Niligundua ubaguzi ndani ya ubaguzi. Nani alidhani, kwa mfano, mhindi hapa angewekwa daraja moja na mswahili wakati mzungu huyu huyu alipokuwa akitutawala alimpa daraja lake na kumtofautisha nasi ukiachia mbali kuwa, kihistoria, wahindi wana mfumo wa kibaguzi uitwao caste? 
        Nilishangaa kuona wazungu wakiwaweka waafrika, waarabu, wahindi, wafilipino na wengine kundi moja huku wachina na wajapan wakiwekwa kwenye kundi lao. Nilikumbuka nilipokuwa kwenye mji wa Winnipeg nilipoingia kwenye duka la mhindi mmoja nikasikia anaongea Kiswahili nikamsalimia naye akajibu kwa kusema “karibu brother’ kitu ambacho si rahisi kulisikia tukiwa Dar. Hapa ndipo kilipo kigeugeu, kizungumkuti na mizungu ya mzungu kwa wale wasiomjua.
Katika kuishi hapa, niligundua kuwa hataw wazungu wanabaguana wao kwa wao kama wahindi. Hivyo, japo siungi mkono ubaguzi wa aina yoyote, naweza kusema kuwa bila ubaguzi, wazungu hawana maendeleo ya kivitu wanayojivunia. Ndiyo, bila ubaguzi, wazungu na hata waarabu wasingemkamata binadamu mwenzao na kumfanya mtumwa au punda mnyama na wakaendelea kumbagua na kumnyonya hata akiwa barani mwake. Hii ndiyo siri ya nchi za kiafrika kuendelea kuwa maskini. Zinatumikia mfumo wa kibaguzi wa dunia ambapo mtu hunufaika kutokana na rangi yake bali siyo stahiki wala ujanja wake. Hii ndiyo maana mzungu akija Afrika ananyenyekewa na kuonekana mjuzi hata kama hana ujuzi wakati mswahili akionekana hajui lolote hata kama hana ujuzi. 
Tokana na kujenga na kunufaika na mfumo wa kibaguzi na kinyonyaji, si ajabu kukuta mswahili mwenye elimu ya juu na nzuri akiwa na bosi ambaye hata hafai kuwa mwanafunzi wake. Si ajabu kukuta waswahili wanaonekana tishio Ulaya sasa wanapovuka bahari kwenda kule wakati wazungu walipovamia na kuitawala Afrika halikuwa tatizo la kumtoa mtu jasho kama ilivyo sasa. Ndiyo maana hata wenzetu walioko China na India na Mashariki ya Kati wanabaguliwa sisi tukiwanyenyekea na kuwashobokea wao. 
        Kwa wenye kutaka kufuatilia, hebu tafitini jamii moja ya kiafrika iliyoko India iitwayo Jarawa waishio kwenye kisiwa cha Andaman ambapo wahindi huenda kuwaangalia kama waangaliavyo wanyama kwenye mbuga za wanyama na hakuna nchi ya kiafrika inayotaka angalau maelezo. Hapa ndipo ulipo mzizi wa fitina. Je nini somo hapa?                     Msipoanza kujithamini na kuacha kushobokea wageni hasa kwa kuwaona wao ni wa maana kuliko nyinyi mtaumia. Je nani anasoma haya na kuchukua hatua? Kwanini hafanyi hivyo zaidi ya kuponzwa na imani kuwa mtu mweupe ni bora kuliko mtu mweupe na mkombozi wake wakati kihistoria ni mtesaji na mnyonyaji wa kawaida kama tutarejea biashara ya utumwa, ukoloni, unyemelezi na ulowezi kama haya mabaki ya watu walioletwa na wakoloni na kuendelea kutukuzwa wakati hawana pa kwenda na kama kuko hakuna lolote sawa hapa.
Nadhani wengi mnakumbuka mauaji ya waswahili kule hapa nchi ya jirani ya Marekani yanayofanywa na polisi. Mswahili anauawa kama mnyama na hakuna kinachofanyika. Tatizo ni mfumo huu wa kibaguzi.  
        Mzungu mmoja akitekwa kwenye nchi ya kiafrika, au ya Asia, wenzake wanavunja hata sheria kwa kutoa fedha aachiwe. Je mswahili akifanyiwa hivyo?  Nani anajali iwapo hata waswahili wenzake–––kama wanyama pori wanaomwacha simba amrarue mwenzake–––hawajali. Tujifunze kujaliana, kujithamini na kuheshimiana. 
        Kipindi fulani nilitaka kuwapiga picha ombaomba wa kizungu nilipokuwa nimefika hapa–––nikiwa bado mshamba. Nilionywa nisifanye hivyo. Kwani, madhara yake yangekuwa makubwa kuliko nilivyotegemea wala kudhania.  Niliufyata. Kwani, nilikuwa kwenye nchi ya watu njapo nilidhani mambo ni kama kwetu ambapo kila kitu ruksa hata udhalilishaji utokanao na ujinga wetu wa pamoja, collective ignorance. Je ni waswahili wangapi wanapigwa picha na mashirika ya kizungu na kuja huku na kutengeneza mabilioni ya dola kwa kisingizio cha kusaidia waswahili maskini wakati ukweli ni kwamba wanapewa kiduchu, na kuaminishwa kuwa wao ni maskini wasioweza kuishi hadi wafadhiliwe? Hapa ndipo lugha ya wafadhili ilipoanzia na kuota mizizi.
Tumalizie kwa kusema wazi. Hisani huanzia nyumbani. Upendo, heshima na thamani vinaanzia nyumbani. Kama hujipendi, usitegemei wengine wakupende. Kama hujiheshimu au kujithamini, usitegemee wengine wakupende au kukuthamini. Kama watu tuliojaliwa na Mola wetu rangi yetu, tuionee na kujionea fahari huku tukijifunza na kupambana na mifumo inayotubagua na kutukandamiza ili iendelee kutunyonya. Kwa wasiojua hali ilivyo majuu, lau wamepata mlango wa kuanza kujifanyia utafiti na kugundua na kuibua mengi. Nangoja maoni ya wasomaji wangu.
Chanzo: Raia Mwema leo.

Tutumie Malimwengu Kujitafakari na Kuitafuta Busara

Hapa duniani kuna vitu vingi vipo na si wengi wanavidurusu hata kukukumbuka kuwa vina mengi ya kuwafundisha ili lau wapate busara. Kama ilivyo ada ya safu hii, huwa tunadurusu mambo ya kijamii ya kila siku bila kusahau kufundisha busara. Leo tungalia busara yetu inachimbuka wapi na kwanini na ili iwe nini. Tuanze na kitu ambacho kila mmoja anakifahamu. Kaburi hung’ara kwa juu lakini ndani hujaa uoza wa mifupa na harufu mbaya. Ndani ya kaburi umejaa uharibifu usio wa kawaida. Nani haogopi kaburi? Je hawa wanaozini kwenye makaburi siyo mashetani hata kama wana sura na viwili wili vya binadamu? Hawa siyo makasha matupu yasiyo na mioyo wala akili timamu ukiachia mbavu ubinafsi na upogo wa kunuka? Kipi bora; kufanya kazi ya kusafisha kikombe ndani na nje? Je nani mpumbavu anaweza kupamba mzoga?         Dunia ya sasa imeharibika. Imelaaniwa si haba. Haina tofauti na mzoga. Je waja hawapendi uchafu kuliko usafi, giza kuliko mwanga, uongo kuliko ukweli,  haramu kuliko halali ukiacha mbali kupenda kujidanganya na kudanganya? Anayebisha aniambie kwanini tunahangaika kama tunavyohangaika. Mwenye mali anamuogopa asiye nayo na maskini anamchukia tajiri kwa sababu ya utajiri wa na si vinginevyo. Je sisi si makaburi?             Hatung’ari juu na kunuka ndani? Dunia imejaa silaha za maangamizi kila aina. Zipo za sumu na moto. Zipo hata za kelektroniki. Zipo hata za kibaolojia na nyingine nyingi zitagunduliwa katika mashindano haya ya ukichaa wa kuiangamiza dunia. Dunia imejaa chuki kuliko upendo, tamaa kuliko kuridhika na upofu kuliko kuona.
        Kazi ya silaha ni kuua siyo kuponya. Leo binadamu wanaogopana kuliko hata simba! Lugha ya sasa ni ya vita vita vita tupu. Mhalifu anamhukumu mhalifu saa nyingine mwenye nafuu kuliko yeye! Hapana. Mwenye hatia anamhukumu mwenye haki huku mchafu akimfundisha usafi msafi. Je hakimu na polisi waombao na kuchukua rushwa siyo wahalifu? Waulize mshahara wao na thamani ya mali zao utajua kinachoongelewa. Mtu anaamka maskini analala tajiri ni watu wanaona. Hata kama hawamwambii wanajua kinachoendelea. Je haya ni maisha ya heshima au ni nifaki na kujilisha pepo?        
         Kujilisha pepo ni tabia ya wapumbavu sawa na wavuta bangi. Maana mvuta bangi akiishavuta bangi yake hujuhisi yeye ni yeye wakati si chochote wala lolote bali mhalifu wa kawaida apaswaye kuishi korokoroni. Je ni wahalifu wangapi wanatanua mitaani ilhali wasio na kosa wanaoza magerezani? Fikiri na upige picha uone hali ikoje.
Binadamu wameukumbatia uharibifu kiasi cha kuigeuza dunia kuwa kaburi na wao wakiwamo! Je viumbe wa aina hii wanaweza kumcheka hayawani pweza ambaye kwa mapezi yake mwenyewe na upumbavu wake hujiteketeza?
        Machukizo makufuru na baya zaidi ni kichekesho kuwa wanadai waliumbwa kwa mfano wa Mungu! Mungu gani anajiteketeza mwenyewe? Watamjuaje Mungu wakati hawajijui? Kwanini kumsingizia Mungu au ni kwa vile hawezi kuonekana? Leo dini kwa dini zinachukiana hata kuwagawana watu! Dini bora ni ile itumikiao utu na kuijenga jamii siyo kuinyonya na kuibomoa. Si njia  zote huelekea kuliko hata kwema. Njia nyingine huelekeza machinjioni na bado ni njia. Kwa hiyo siyo kila njia ni njia ya kufuata.
        Kuna vilio kila kona. Kila kona kuna vilio. Uchafuzi wa mazingira, uwindaji haramu, utoroshaji wa magogo na madini. Yote hii ni ukaburi.  Uchafuzi wa maadili na haukubaki nyuma. Dunia imechafuka kweli kweli. Nani ataisafisha kama siyo wewe na mimi? Watu wanatumikia leo wakiisahau na kuiharibu kesho utadhani wataishi milele!
Wanadamu wameharibikiwa. Wanatumia pesa nyingi kwenye misiba wakati marehemu kabla ya kufa alilazwa hospitali kwa muda mrefu wasiende kumuona wala kumlipia gharama za matibabu. Wengine walimfilisi kwa kumfanyia matibabu ya uongo huku bila aibu wakimhadaa kuwa wamemsaidia kutibu ndwele yake wasijue wamemsaidia kubeba dhambi zake kwa sababu ya kutu yao ya kuchuma na kuvuna wasipopanda. Kwao hawa matatizo ni mtaji. Lakini wanasahau kuwa na wao wana matatizo saa nyingine makubwa na mengi na magumu kuliko ya huyu wanayemuongezea matatizo wakijidai wanayapunguza!
        Watu wapumbavu wanachangishana pesa za kusafirisha maiti lakini siyo za kuuguza! Je waliwahi kufikiria wangelikuwa ni wao? Ukitaka kujua ukubwa wa mguu wa tembo vaa viatu vyake. Utamchongeaje mtu jeneza la mamilioni wakati kuna umma unataka maelfu bado ubaki mzima? Wewe huna tofauti na mdudu bungua aozeshaye ubao maana unazika vitu ukijua vitaoza. Mbona hamuwaziki na vyakula na vinywaji walivyovipenda hata watu waliowapenda ambao ni nyinyi?
        Tumalizie kwa angalizo. Mara zote, busara huwa inaumiza kuwa nayo hata kuitafuta. Hivyo, sitashangaa kusikia kuwa kuna wasomaji wanaona hili katika haya niyasemayo hapa. Ndiyo busara ilivyo. Busara ni sawa na kwenda jandoni kutahiriwa. Siyo sawa na kwenda harusini au. Kwenye party. Ni sawa na kwenda kwenye matanga. Hivyo, msichoke kuitafuta busara kwani, kama ukweli, itawaweka huru.
Chanzo: Raia Mwema leo.

Sunday 21 November 2021

Barua kwa Rais Samia Kuhusu Mgao wa Umeme

Mheshimiwa Rais, kama ada, nakusalimia kwa jina tamu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni kitambo sasa tangu tuwasiliane hata kama, mara nyingi, hujibu kwa maneno bali vitendo. Kwa heshima na unyenyekevu mkubwa, naomba leo nigusie suala kero na nyeti si kwa taifa tu bali hata kwako binafsi kama kiongozi wa nchi ambaye mambo, yanapoharibika mambo, hata kwa hujuma na uzembe wa wengine, ndiye unayelaumiwa. Kwanza, nikupe pole na hongera kwa ziara yako nchini Misri, japo nina maswali mengi kuhusiana na nchi hii ambayo imekuwa ikitaka kuziburuza na kuzidharau nchi za kiafrika hasa zile za kwenye bonde la mto Nile kwa kulinda maslahi yake kitaifa kwa kuyahujumu ya wananchi wa nchi husika. Niende moja kwa moja kwenye hoja. Kwa sasa, watanzania wanakabiliwa na jinamizi na zahama ambazo walishazisahau hasa baada ya awamu ya tano uliyokuwa mmojawapo wa wakuu wake ilikomesha. Hili si jingine bali ni mgao wa umeme na ukatikaji wa mara wa umeme mambo ambayo athari zake ni kubwa kwa maisha na uchumi wa taifa letu.
        Mheshimiwa Rais, unajua kuwa kwa sasa siishi Tanzania. Nipo masomoni Kanada japo moyo na roho yangu viko nyumbani. Hata hivyo, ndugu zangu na watanzania wenzangu wanaishi hapo. Hivyo, kama mtanzania halisi na mzalendo, kila linalowagusa, kwa namna moja au nyingine linanigusa. Hivi karibuni, ulikaririwa na vyombo vya habari ukisema “kuna watu wanalima karibu na vyanzo vya maji haya yote mawili yanapelekea vyanzo vya maji kupungua. Yanapungua na hayaendi kule yanapotakiwa yaende.” Je tatizo ni kilimo tu au/ima hujuma kwako binafsi, mazoea na ufisadi? 
        Mtangulizi na bosi wako aliyekuamini kuwa makamu wake na ambaye, kwa kiasi kikubwa, imani yake kwako na uamuzi wake, vimechangia pakubwa wewe kuwa Rais, Hayati Dkt John Pombe Magufuli (RIP) aliwahi kufichua kuwa mgao wa umeme nchi siyo sababu ya mapenzi ya Mungu bali binadamu wabinafsi, wachoyo na waovu ambao alisema kuwa walikuwa wakishirikiana na wauzaji wa majenereta kwa kufungulia maji usiku na kusema hakuna maji ya kutosha ili kuwawezesha wahalifu hawa kufanya biashara ya kuwanyonya watu wako. Je hapa tatizo ni mazingira au hujuma ukiachia mbali ufisadi na mazoea? Tafadhali chunguza.  Hili bila shaka, halina shaka hasa ikizingatiwa kuwa aliyeliibua alikuwa mkuu wa nchi aliyesifika kwa ufuatiliaji na uzalendo wake. Je         Mheshimiwa Rais, utakubaliana nami kuwa tatizo hili halikupatiwa suluhu? Je mchezo mzima bado unaendelea ili kuwanufunufaisha wenzetu ambao ni wachukuaji wanaojiita wawekezaji wakati hawawekezi chochote zaidi ya hujuma? Chonde chonde. Nakuomba uliangazie na kulitafakari hili.         Mheshimiwa Rais, kiti ulichokalia ni kikubwa na kina utamu hakuna mfano. Naamini umeliona na utaamini nisemayo. Ili kukipata, kwa wale ambao wanakinyemelea, lolote linawezekana ukiachia mbali ubinafsi, tamaa, upogo na uovu.
            Hivyo, nakuomba uangalie mbali zaidi ya matatizo ya kimazingira ambayo sina ubishi wala ugomvi nayo kuwa yapo na ni sababu tosha, kati ya nyingi, zinazosababisha uwepo wa mgao usio wa lazima wa umeme kwa nchi iliyojaliwa vyanzo vingi vya umeme isipokuwa ujuzi na utashi wa kufanya hivyo.
            Hivi karibuni, ndugu yangu mjasiliamali maarufu na mkubwa aishie Dar es Salaam aliniandikia ujumbe ufuatao akilalamika kwa kusema “huyu mama naona kama anachemka yaani juzi nimepata ahibu kubwa kwa mtu anatakuwekeza kwenye soko kubwa la frozen products ghafla umeme ukatika siku nzima na biashara yangu ikazimikia hapo tena mtu nimemtoa mbali.” Alipoandika ‘huyu mama’ alimaanisha wewe. Sijui alifikiaje hitimisho na uamuzi huu vipi na kwa vigezo gani. Binafsi, sina cha kuficha au kuchelea wala sababu ya kufanya hivyo hasa nikizingatia kuwa nimekuwa nikikushauri kizalendo si kwa kuchaguliwa, kuteuliwa au kutaka bali kusukumwa na mapenzi na uzalendo kwa nchi yangu. Baada ya kupata ujumbe huu–––ambao haupendezi hata kwangu––––nilijiuliza maswali mengi mojawapo myakiwa: je ni wangapi wameathirika? Je ni wangapi wana hasira, mawazo na maoni kama haya? Je hakuna haja hapa ya kuwafahamisha wadau ukweli ili kuepuka lawama kama hizi ambazo si nzuri kwa kiongozi na mkuu wa nchi ambaye hana shaka katika mapenzi na utumishi wake kwa umma?
            Kama wasaidizi na washauri wako, ima wanakuogopa au kuogopa kukwambia ukweli, haya ndiyio yanayozungumzwa. Hizi ndizo hasira na hisia za watu wako ambao hawana uwezo wa kuwasiliana nawe kama mimi.  Je nini kifanyike? Kuna mengi ya kufanya hapa ili kutatua tatizo. Hivyo nashauri yafuatayo:
            Mosi, napendekeza vyanzo vyote vya matatizo vikabiliwe vilivyo bila huruma wala simile. Mfano, watu binafsi wanaochepusha maji washughulikiwe mara moja si kwa hasira bali kuangalia namna umma na wao wanavyoweza kunufaika na raslimali hii muhimu.
            Pili, tashhisi za hujuma kama alivyowahi kuzifichua Hayati Magufuli zimulikwe kuangalia kama kweli kuna uhusiano kati ya ukosefu wa maji na biashara ya majenereta ambayo ni mambo ya mwaka 47 katika karne hii.
            Leo sitaandika mengi ili kukupa muda wa kutafakari, kuchunguza na kuamua. Je, kweli, Tanzania nchi yenye vyanzo vingi vya umeme visivyotumika, inastahiki kuwa na mgao au ukatikaji wa umeme katika karne ya 21? Maswali muhimu na stahiki ya kujiuliza ni: kwanini sasa na nini kifanyike kuyapatia majibu sahihi na haraka ili kuepuka ngoa na sintofahamu zinazoendelea? Je hii inajenga mazingira gani na matokeo yake ni nini kwako na kwa taifa? Sipendi kutoa fursa ya wananchi kuanza kulinganisha na kuanza kuishi kwa kutamani Hayati angerejea japo ni haki yao lakini si kwa kulazimika. Je kweli tuna uhaba stahiki wa umeme au wa kujitakia wakati tumejaliwa vyanzo lukuki? Je nini kinakosekana kama siyo uadilifu na utashi? Je hizi sababu ndizo vyanzo pekee vya matatizo yetu au ni zaidi? Je matatizo haya–––ambayo, kimsingi, ni ya kujitakia–––yataisha lini na madhara yake ni yake yawe ya muda mfupi au mrefu kwa taifa? Je tumekubali kuwa mateka wa kujitekea kwa wahujumu na wahalifu wachache? Leo, sisemi mengi zaidi ya kushauri kwa dhati na uwazi kuwa umeme ni haki ya kila mtanzania kwa maendeleo na maisha ya taifa na watu wake.
         Mheshimiwa Rais, tafakari hata kama matokeo ya kufanya hivyo ni kuwatumbua baadhi ya wasaidizi na watendaji wako husika kwenye maeneo haya ambao wanaonyesha kuwa mzigo kwako. Kuna haja ya kuwaelimisha hawa kuwa hapa muhimu siyo sura zao bali utekelezaji wa dhamana walizoaminiwa na umma unaohangaika kwa sasa tokana na ukosefu wa ubunifu na utekelezaji wa majukumu yanayofanya walipwe. Kila la heri dada yangu.
Chanzo: Raia Mwema kesho.

Jiulize kwanini mambo huwa hivi

Tokana na kutamalaki kwa Upungufu wa Busara Duniani, safu hii itakuwa ikiwaletea wapenzi wake makala juu ya busara ili lau tufundishane na kupeana busara. Tungetamani kusikia maoni ya wasomaji wetu. Baruapepe ipo. Kuna sababu nyingi kwanini wema na wenye busara hawadumu. Yawezekana hutokea hivi ili kuepuka kukua na kujichanganya. Hivyo uhai wa mwenye busara sawa na mwenye mali huwa mfupi lakini wenye maisha marefu baada ya yeye kuondoka. Maana huaacha mali na maarifa. Ni wangapi wanaishi maisha ya kijungujiko lakini marefu kuliko waishio kwa vinono na sifa wakakatiziwa uhai wao? Je lipi bora–––maisha marefu ya ufukara au maisha mafupi ya ushufaa? Mungu hawezi kukupa wala kukunyima vyote. Kama waliopewa vyote ni wachache. Ukipata hiki unakosa kile ili uweze kusaidiana na kutegemeana kuwa sawa na wenzako. Hii ndiyo maana ya tembo mwenye maguvu ya kuangusha miti kukosa nyumba lakini mchwa na ndege wasio na maguvu wala vikumbo wakawa na viota vyao. Wakati wanyama wenye maguvu hawana pa kuita kwao au kuweka mbavu zao, viumbe wadogo kama wadudu na ndege wana viota na mashimo yenye joto la kuwafanya walale kama wafalme kwa viwango vyao. Je fisi na simba wangejua kutumia visu wanyama wengine wangekuwapo? Je Nyati na tembo wangekula nyama fisi na simba wangekuwapo? Je pamoja na maguvu, meno na makucha yao fisi, simba na tembo huwa hawalali hata wakati mwingine kufa njaa? 
         Usicheze wala kufanyia njaa masihara. Hata malaika hulala njaa wakati mwingine. Mtoto mchanga anapofiwa na mama hula nini? Je wenye nguvu wote wangepewa utajiri nani angebeba mizigo? Je matajiri wangepewa kujiamini maskini wangekula nini? Je matajiri si maskini wa sifa ambao hutaka wasifiwe na maskini? Je matajiri wana vyote? Kama wanavyo, mbona wanatumia utajiri wao kuwaridhisha maskini? Je utajiri wa wenye nao waliupata wapi kama siyo kwa maskini ambao nao utajiri wao waliukosa kwa vile uko kwa wenye utajiri? Je wakubwa hawawaogopi wadogo tena wanaowatawala? Kama hawawaogopi, walinzi na mituringa vilivyowazunguka vya nini?
Je kati ya mwanamme na mwanamke kuna aliye bora kuliko mwenzake wakati wote wanategemeana? Bila mwanamke, mwanaume angezaliwa na nani na bila mwanaume mwanamke angezalishwa na nani? Wengi wangejua ushujana uvumilivu ukiachia kukjitoa mhanga vinaohitajika kuhimili uchungu, wasingehata fikiria kuwadharau wauhimilio. Je ni wanaume wangapi waliweza kushuhudia wake zao wakijifungua lau wapate elimu na kujua busara hii maana yake ni nini?                 Kabla ya kumdhalilisha mwanamke, mkumbuke mama yako. Na kabla ya kumdharau mwanaume, mkumbuke baba yako. Bila wawili hawa ungekuwa wapi kiumbe wewe? Epuka na ogopa mtu anayejua namna ulivyotengenezwa hata kama ni kwa bahati mbaya au makosa. Shukuru umetengenezwa. Je ungekuwa mdugu ungekuwa wapi sasa? Kwa kujua ukweli na umuhimu huu, epuka kumtukania mwenzako wazazi wake kwani nawe unao. Je hapa kuna mjanja wa kumdharau au kumnyonya mwenzake au ujinga na upogo mtupu? Je mtoto wa jana siyo mkubwa wa kesho na mkubwa wa kesho siyo mtoto wa jana?
        Kila zama ina yake; ndiyo maana wakaja wanafalsafa katika maumbo mbali mbali. Wapo waliokuja na falsafa za kisayansi wengine kidini kadhalika na kadhalika. Lakini wote lengo lao lilikuwa moja; kujaribu kuyadurusu malimwengu kwa kadri walivyoona kuelewa na kuweza. Walifanya yote haya pamoja na hatari na ugumu wake ili kuwapa jibu wanadamu waishi maisha mazuri. Wapo waliofanya hivyo ili kujinufaisha tokana na wengi kutopenda kutafuta maarifa. Wapo waliosukumwa na upendo wao na thamani yao kwa utu vilivyowasukuma kutoa zawadi hii ambayo wengi hawajui kuipokea wala kuitumia. Kadhalika wapo waliokuja kujilisha pepo kwa kuwatumia badala ya kuwatumikia wengine. Wapo waliosukumwa na tamaa zao kutafuta kuwatumia na kuwafaidi wenzao.
         Wengi mnakijua kisa cha mwanafalsafa wa kiyunani aliyesifika kwa  kudurusu. Aliwahi kutembea mchana kweupe akiwa na chemli. Alipoulizwa kwanini alikuwa akiwasha taa mchana kweupe, alijibu kuwa alikuwa anawatafuta watu wenye maadili asiwaone. Kadhalika nami nikikwambia kuwa kuna watu wanakufa kwa kiu wakiwa mtoni au ziwani utadhani uzushi. Kama unadhani hivyo, angalia ulipo. Jiulize ni kwanini wageni hukimbilia nchini kwako wakati wewe ukiikimbia. Kama tutajiruhusu na kukubali kufikiri kwa pamoja tutagundua vitu vingi ajabu.                         Usishangae ukakuta mahakamani hakuna haki na madhabahuni wamejaa wenye dhambi wakiwapoteza watu wema lakini waliokosa maarifa na busara. Wala usishangae kukuta vyuo vimejaa wajinga huku wenye elimu wakiwa mitaani bila ajira wala kuthaminiwa. Je kuelimika ni kupoteza miaka mingi vyuoni na kuwa na utitiri wa vyeti au kutatua matatizo yetu na ya wenzetu kama binadamu? Je msomi anayepotezwa na mjinga na mjinga nani msomi nan ani mjinga wa kweli? Je wasomi wanaodai rushwa hata ya ngono na majambazi wanaoua watu wana tofauti? Msomi anayedai rushwa anaua kesho ya mhanga wake sawa na jambazi anayemfanya mhanga wake asiione kesho.  Je tajiri mwenye magonjwa yanayomzuia kula kila atakacho hazidiwi na mbwa aliyemfuga anayeweza kula kitu?
        Ujambazi huu wa kuchezea hata kufikia kuiuza na kuinunua haki umewafanya watu wenye haki kuwa wanyonge. Hakuna suluhu baina ya mnyonyaji na mnyonywaji isipokuwa moja. Mnyonyaji kuacha kumnyonya mnyonywaji na mnyonywaji kuacha kukubali kunyonywa kwa kila hali hata kama kwa shari. Mkandamizaji aache kumkandamiza mkandamizwaji. Je kuna mkandamizaji mwenye akili timamu atakubali kuacha kukandamiza wakati kwake maisha ni ukandamizaji? Ni kupe gani yuko tayari kutoka mgongoni mwa ng’ombe? Hapa lazima mwenye kupambana na viumbe hawa laanifu aamue liwalo na liwe kwani hana cha kukosa bali kujikomboa. Nani hajui kuwa simbiko halisimbuliki ila kwa mikukuriko?
        Hapa hakuna mjadala wala namna isipokuwa kutenda haki tena haki tupu. Anayepaswa kutenda haki asipoitenda wanaofanya kutendewa lazima wamuasi kwa gharama yeyote. Je haki tupu ni ipi? Kila mmoja kuishi kwa jasho lake huku utu ukiongoza na kupanga kila kitu kwa ajili ya utu na watu wote kwa usawa. Zaidi ya hapa hakuna maelewano wala maisha hayana maana tena. Kiongozi hata mtawala mpumbavu ni yule asahauye waliompandisha kwenye ukuu. Maana hana tofauti na apandiaye ngazi akaipiga teke asijue wakati wa kuteremka ukifika ataporomoka badala ya kushuka. Hana tofauti na mtu apangusaye mashonde kwenye busati analotumia siku zote. Huu ni upumbavu hata ufanywe na wateule.
Chanzo: Raia Mwema kesho.


East Africa needs to join Uganda to fight terrorism


Author: Nkwazi Mhango

What you need to know:

  • Terrorism is as old as humanity. However, its prominence surged recently. The global war on terror that the United States declared was a very ambiguous thing that can be used to serve different purposes; good and bad. 
  • Terrorism is a very complex phenomenon that can be construed and interpreted into many things, depending on the purpose(s) of whoever defines or uses it.

Terrorism is as old as humanity. However, its prominence surged recently. The global war on terror that the United States declared was a very ambiguous thing that can be used to serve different purposes; good and bad. 

This informs us about the daunting task we have as countries to address and arrest terrorism. Therefore, it begs cooperation, audacity and lucidity of purpose[s].


But due to its ambiguity and controversies, terrorism can easily be used by some countries to further their hidden interests and exploit others. We, therefore, need to reassess and restudy the phenomenon. There is room for agreeing or disagreeing, if our takes of the phenomenon are aimed at doing justice equally and fairly.

This piece seeks to debunk the myth revolving around national interests as opposed to international interests, and the manner in which the global war is fought. Also, criminal groups use terrorism as their weapon for seeking attention.

Further, terrorism becomes even more sophisticated due to the fact that it is connected with some faiths though in pseudo ways. Underscoring the complexity, intricacies and sensitivity of terrorism resulting from the plethora of definitions and the way it is approached, it is important for the phenomenon to be addressed and studied. 

Hübschle (2006) cited in Mhango (2017) observes that “defining terrorism has been a particularly difficult task on the African continent” (p. 16). This shows how different governments, organisations and people have different definitions of terrorism. 

This mix-up and difficulty can be seen on how the global war on terror is fought mainly in the age of drones that have oft been reported to kill unintended civilians. There is need to interrogate the security of the countries where these technologically advanced machines are sent for surveillance, not to mention military bases that are now established in various African countries. 

Can’t they be used to spy on such countries; and thereby compromise the security of these countries? Why are drones and military bases welcome to poor countries of the South but not otherwise?

 Where is reciprocity in this war? Do poor countries contribute inputs on how to fight the very global war on terror? Such questions cannot be gainsaid or be treated like trivial matters.

What transpired in Kampala this week speaks volumes. It is horrendous, unforgivable and diabolic. While Uganda needs to stand its ground and thwart the phenomenon, it must underscore the fact that it needs other countries to fight it. 

Nonetheless, as a sovereign entity, Uganda needs to be chary about the encumbrances that come with the cooperation in fighting terrorism. I condemn the attacks on Uganda carried out by spineless criminals that claimed innocent lives in the strongest terms.

As I urge Ugandans to stay put to see to it that they’re not lowering their guard since these criminals could be plotting more attacks. East African countries need to join Uganda to fight this scourge instead of waiting until they are attacked.

Mhango is a lifetime member of the Writers’ Alliance of Newfoundland and Labrador  nkwazigatsha@yahoo.com.

Source: Daily Monitor today.

Moses Wetang’ula, a boxer above his weight

Ford Kenya party leader Moses Wetang'ula.

Dennis Onsongo | Nation Media Group

Professor at SUNY Buffalo Law School and Chair of the KHRC




Bungoma Senator Moses Masika Wetang’ula has a knack for finding the sweet spot in the inner sanctum of power. The man from Sirisia has always been an insider – it doesn’t matter whether he was in government, or the opposition. And yet it’s flummoxing why Mr Wetang’ula has risen so high in Kenya’s political society. On the face of it, there’s nothing remarkable about the man. He’s a socially awkward politician who wears a permanent scowl on his face.

        I don’t believe I’ve seen a picture of him cracking a smile. Who’s Mr Wetang’ula? Why does he seemingly punch above his weight? He’s like a boxer who’s always boxing above his weight class. What’s the secret to his political success?I raise these questions not because I find Mr Wetang’ula’s biography arresting. No – I want us to assess his value to the One Kenya Alliance (OKA), and other likely outfits from which he might seek to benefit.         That’s because he’s a political leech who always seems to find the most opportune moment to feather his nest. One might call him an opportunist, a strategic genius, or a cunning tactician. The fact I am writing about him means that he’s “somebody”. I think he’s living proof that in life you can go far without being abundantly gifted if you believe in yourself. Some might even say he’s Exhibit A that all dreams are valid. Let’s peel the onion and expose it.
        First, a confession. Mr Wetang’ula was one class ahead of me in law school at the University of Nairobi. In those days, the Moi-Kanu regime held untrammelled power. The University of Nairobi had the only law school in the country. Getting a law degree was akin to a licence to print money, or have your pick of any plum job.
        Penury – unlike today – wasn’t the lot of lawyers. The Kanu regime was very interested in the law school because that’s where it recruited its lackeys from. Usually, future Kanu state leaders were groomed while at the University of Nairobi. Whether it’s true, or not, the student leaders – of which I was one – believed Mr Wetang’ula was close to Kanu.
        Second, what followed after law school did nothing to quiet those rumours. In 1992, Mr Wetang’ula was nominated by Kanu as an MP. He had served as a magistrate and chair of the Electricity Regulatory Board, the latter being a boondoggle for Kanu insiders. He was clearly what we would call a “teacher’s pet” in President Daniel arap Moi’s orbit. Since those early state favours, Mr Wetang’ula hasn’t looked back.
Embassy scandal
He was elected MP in 2002 and in 2008 was appointed Minister for Foreign Affairs, a position he left because of the so-called Tokyo embassy scandal involving a shady property sale. He was cleared of the corruption allegations. He soon left as minister and was elected Bungoma County Senator.
        Third, he’s had a rocky, if checkered, career in the Senate. In 2013, his election as senator was nullified on grounds of electoral shenanigans. But he handily beat his opponent in the ensuing by-election and was named by Cord as Senate Minority Leader. However, in 2018, he was controversially removed as Minority Leader and replaced by Siaya Senator James Orengo.
        It appears that his fidelity to Nasa, the opposition coalition, was under a cloud. Mr Wetang’ula’s political muscle appears to come from his tenuous leadership of Ford-Kenya, the party whose support base is among the Bukusu. Since the Bukusu are the most numerous and powerful of the Luhya “Mulembe Nation”, Mr Wetang’ula has used that identity to bargain with other groups for a seat at the national table.
        This explains Mr Wetang’ula’s political chops in OKA. But in that seemingly moribund outfit, Mr Wetang’ula is the third wheel in the pecking order.
ANC’s Musalia Mudavadi is clearly ahead of him among the Luhya, but both are second fiddle to Wiper’s Stephen Kalonzo Musyoka, the presumptive OKA chief. Kanu’s Gideon Moi barely registers on the Richter scale in OKA.
        In fact, I would go as far as to say that Mr Wetang’ula has been Mr Musyoka’s political pupil since their Kanu days. I don’t think he makes any significant moves without Mr Musyoka’s approval, or counsel. In the end, he’s likely to go where Mr Musyoka goes. In other words, Mr Musyoka is Mr Wetang’ula’s Svengali, or godfather.
        Kenya’s political landscape is very shaky today, but that will start to change in December, or latest February 2022, when political bigwigs, including Mr Wetang’ula, find a political home. Assuming UDA’s William Ruto faces off with ODM’s Raila Odinga in the race for State House, Mr Wetang’ula will roll the dice with Mr Musyoka.
Mr Wetang’ula, like Mr Musyoka and Mr Ruto, are Mr Moi’s political scions. So it could be an option for them to band together. But I don’t see Mr Musyoka subordinating himself to Mr Ruto, whom he considers his junior. Mr Musyoka and Mr Wetang’ula could go with Mr Odinga.
 Makau Mutua is SUNY Distinguished Professor and Margaret W. Wong Professor at Buffalo Law School. He’s Chair of KHRC.  @makaumutua.
Source: Sunday Nation today.