Free Thinking

I Fear Nothing But Fear Itself

Epistle to Afrophobic South Africa

Epistle to Afrophobic South Africa

Saturday, 31 October 2015

Wadanganyika wote tumeshinda na tusherehekee basi

  • ... to be a close race between John Magufuli (left) and Edward Lowassa
Baada ya wadanganyika wote kushinda kwenye uchakachuaji uliopita –kama ilivyokuwa wakati wa kampeni –ni wakati wa kushangilia kwa pamoja. Naona yule anatikisa kichwa akidhani naongea kwa nguvu ya mupipi na bangi na si bongo. Ngoja basi niprove pwenti kwanini nayasema haya nisemayo.
            Nina sababu ya kushangilia sawa na wewe. Ngoja basi. Mbona hivyo lakini? Si ungoje nikukufikishe badili ya kuhemkwa hata kabla sijafanya vitu vyangu?
            Basi okey. Poa, ngoja ngoja huumiza matumbo. Ngoja nikupe dozi ya kwanini unapaswa kuja kushangilia nami.
            Mosi, kwanini tushisherehekee kwa kuonyesha ulimwengu mzima tulivyo kaya ya amani hata kama tunaumia? Nani alitegemea Chama Cha Mafwisadi kama watani wao wanavyokiita kupeta? Ngoja niulize kidogo. Je hapa mnailauma CCM au wapingaji wenye pupa mliofanya kosa kuamini longo longo zao wakati nao walikuwa wakitafuta ulaji? Ngoja nifafanue. Hivi mlitegemea kada wa CCM aishinde CCM akiwa kwenye upinzani? Nani aliwaroga nyie ambao hamkujua kuwa jamaa hakuondoka kule kwa hasira bali kuwakomesha viherehere waliokuwa wakimpakazia kaya nzima kuwa yeye ni fisadi? Wako wapi sasa baada ya kupwakia matapishi yao na kuweka heshima, imani na vyama vyao rehani wakichezea kwenye nyavu za jamaa na chata lake? Ngoja niulize kilevi. Kwanini wadanganyika ni wagumu wa kuisoma na kuilewa historia? Yaani mara hii mmesahau jinsi Lyatongolwa alivyoizamisha Eni Si Si ara Mageuko? Ajabu ya maajabu sijui kwa sababu ya umaimuna au uroho na upogo mmeruhusu Eddie Luwasha azamishe vyama vinne kwa mpigo! What a titanic blow dudes! Hayo ya wachovu na waroho wa maulaji tuwaachie wenyewe.
            Pwenti ya pili, kwanini tusisherehekee iwapo tumerejesha ngoma ile ile ili itufanyie mambo yale yale nasi tusifanye lolote kama ambavyo tumefanya kwa miaka zaidi ya thelathini? Juzi juzi walikuwa wakiuza wanyama hai, sasa ngoja muuzwe nyinyi wadanganyika kwa ujuha wenu wa kutegemea wasanii wa kisiasa wawakomboe. Mie simo. Hauzwi mlevi hapa.
            Pwenti ya tatu kwanini wote mnapaswa kusherehekea ni kwamba kuisha kwa kampeni na uchakachuaji ni jambo la kufurahia. Angalau sasa walevi wanaweza kwenda kupiga kazi kama zamani badala ya kutegemea kula dezo na kujazwa ahadi za akina Abunwas na makando kando yake. Nenda mkachape kazi wenzenu waanze kula. Kama mlishindwa kuuliza ni kwanini deni la kaya limeumka kwa haraka unadhani hawa mliowapa watashindwa kuhomola kwenye shamba hili la bibi?
            Pwenti ya nne ni kwamba japo wote tumeshinda, washinda wa zaidi ni wawili yaani Dokta Kanywaji Makufuli anayekwenda kuenjoy pale Magogoni na Eddie ambaye ushindi wake ni kwenye maeneo mawili yaani kushinda hata kabla ya kuingia kwenye debe kwa kuwachanganya UKAUA hadi wakaingia kwenye anga zake akawaua tena kwa mpigo. Kama nilivyoeleza ushindi wa pili ni kuwalazimisha mahasidi wake waliomvurugia ulaji hapo mwaka 2008 kwa kufichua ulaji wake na kuleta mswaada uliomfanya ateme uwaziri mnene. Ni ajabu kuwa wanasiasa wetu huwa hawana kumbukumbu. Kwanini hawakujiuliza swali lipi la:Jamaa atupende kwa lipi wakati sisi ndiyo tuliasisi maanguko yake?  Pamoja na mibangi na ulevi wangu, kama ningekuwa UKAUA jamaa wala asingenipata wala nisingejiingiza kichwa kichwa kudhani nimepata wakati nimepatikana. Ushindi wa jamaa huyu hauna kifani. Kwani jamaa walidhani watamtumia akaisha kuwatumia na kuwazika huku akiondoka akichekelea. Nashauri CCM wampe nishani ya mikakati. If anything, the dude is a guru in strategies so to speak. Sitatafsiri kwa leo kwa wale wasioumanya ung’eng’e tusameheane. Ningekuwa nimeishauweka ningeweza kutafsiri. We aliyekuwa ukizungusha kichwa sasa umeona mantiki ya kusema wote tumeshinda? Tuonane wiki ijayo.
Chanzo: Nipashe Okt., 31, 2015.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 06:52 No comments:

Friday, 30 October 2015

Zama Zile Muziki Ulikuwa Shule


Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 19:22 No comments:

Thursday, 29 October 2015

UKAWA walaumu pupa, upogo, ubinafsi kushindwa vibaya

  • Tunapompmgeza Dk John Magufuli... wa urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Pombe Joseph Magufuli
Kushindwa vibaya kwa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kunaweza kufupishwa kirahisi kwa kuangalia yafuatayo:
Realpolitik za Tanzania na historia ya UKAWA
Wananachi kuichoka CCM lakini wakanyimwa chaguo na UKAWA
Kumleta Edward Lowassa na kumpitisha kuwa mgombea wa UKAWA
Kutokuwa na hoja kwa UKAWA
Kujipiga mtama na kuondoka kwenye misingi iliyosimamia UKAWA
Lowassa kuwa bubu na kushindwa kuinadi na kuitetea UKAWA
Uchapakazi wa Magufuli nao ulikuwa kikwazo kwa UKAWA

Nguvu ya CCM kifedha na kimkakati ikililinganishwa na UKAWA
Hivi UKAWA wangemsimamisha Dk Slaa tungekuwa tunaongeaje sasa?
Kinachoshangaza ni ile hali ya wakuu wa UKAWA kushindwa mambo rahisi kama haya. Wengine tena ni maprofesa. Ni bahati mbaya kuwa wote walikuwa kama vipofu walioamua kumchagua kipofu mwenzao awaongoze.
Sina shaka kama UKAWA ingemsimamisha Dr Slaa kazi ingekuwa kubwa kutokana na sifa walizokuwa wameishajizolea. Ni wakati muafaka kwa CCM kujipima na kujirekebisha. Maana inavyoonekana imepigiwa siyo kubeepiwa. Kwa mchapakazi kama huyu na asilimia walizopata, hivi kama Magufuli angegombea na mtu mwenye udhu na uwezo hali ingekuwaje? Je CCM miaka kumi ijayo itakuwa na Magufuli mwingine kweli?
Hongera Magufuli. Sasa kazi kwako kutimiza ahadi zako na kukidhi matumaini makubwa ya watanzania kwako.

Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 18:03 No comments:

Wednesday, 28 October 2015

Wanaosaka Madaraka Waimbe wimbo Huu Wamalizie na Tanzania


Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 17:06 No comments:

Tuesday, 27 October 2015

Kijiwe chatabiri ushindi kwa wadanganyika wote


            Baada ya wadanganyika kutumbukiza kura zao za kula kwa walaji wao, Kijiwe leo kinakaa kutafakari na kutathmini mambo yatakavyokuwa huku kikija na utabiri wa aina yake ambao utawashangaza wengi.
            Kapende ndiye anafungua dimba kwa kusema, “Wazee kwanza nawapongezeni wote kwa kufanya uchakachuaji wenye amani na utulivu.”
            Mipawa anamchomekea, “Mbona kuna sehemu hiyo amani hawakuiona achilia mbali kuiona? Mara hii umesahau kuwa poti kule Mwanza watu wametembezewa mikong’oto na kulipuliwa mibomu ya michozi?”
            “Hayo huwa hayakosekani kwenye kaya za kipuuzi. Mara hii umesahau kuwa ndata huwa wanawashwawashwa kuwamwagia watu maji ya washawasha na mibomu ya michozi ili kuonyesha kuwa nao wamo?” anajibu Mchunguliaji huku akiendelea kubukua gazeti la Danganyika Daima.
            Mpemba anakula mic, “Yakhe hata mie hiyo amani mnosifia sijaiona hasa ikizingatiwa kuwa kule Pemba watu walipigwa kwa kutaka kulinda kura zao.”
Mgosi Machungi anakula mic, “Taifa niizopata ni kwamba kue Ushoto mambo yaikwenda shwai sana na hakuna aiyepigwa waa kumwagiwa mimaji ya kuwasha waa mibomu ya michozi. Ndata wanaijua Ushoto. Wamwage upupu wapigwe zongo.”
            Msomi Mkatatamaa anakula mic, “Kwa ujumla zoezi limekwenda vizuri sana. Sema  hatujatoka nyikani. Ngoja tungoje matokeo ingawa yanaonyesha kuwa wote watashinda kwa kishindo kuanzia wapiga kura hata wagombea wote.”
            “Una maanisha nini Msomi mbona umeniacha kizani? Watashindaje wote wakati lazima wawepo wa kushinda na kushindwa? Itakuwaje wakati wengine wameishaanza kukiri kudondoshwa kwa kusema kuwa watakwenda kuchunga ng’ombe kule kwa aina Laibon?” Mzee Maneno anauliza huku akibwia kahawa yake.
            “Umeuliza  swali zuri sana mzee wangu. Nitatoa ufafanuzi ili kila mtu anielewe wakiwamo wahusika wakuu. Kwanza, nianze na Eddie Luwasha. Huyu bwana alishinda hata kabla ya kuanza kampeni. Unadhani ni ushindi kidogo kukimbia chata lake na kupewa kijiti aviue vyama vinne vilivyokuwa tishio kwa nambari wahedi? Kwangu, huu ni ushindi wa kwanza. Pili, ushindi wa pili ni ile hali ya Eddie kuwalazimisha mahasidi wake waliomwita fisadi kwenda kumsafisha kaya nzima huku wakijivua nguo na kujidhalilisha ingawa si wote.”
            Mbwamwitu anachomekea, “Una maanisha nini kuwa si wote wakati wote waliandamana naye kumsafafisha ingawa kwa wapiga kura kama sisi hakusafishika?
            “Swali zuri hili. Namaanisha akina Dk Silaha na Profwesa Pumba ambao walikataa kuramba matapishi yao.”
“Hapo nimekupata vizuri sana,” anajibu Mbwamwitu huku akitabasamu.
            “Msomi naye anajibu. Nami nimekupata ten asana. Tuendelee,” anakohoa kidogo na kuendelea, “Mshindi wa pili na Dk Kanywaji Makufuli ambaye –kwa taarifa nilizo nazo –ni kwamba anaongoza kwa mbali sana. Hivyo, tegemea lisirikali la Makufuli. Je atawafunga mafwisadi kama alivyoahadi? Je ataanza na akina Escrow, EPA au Richmond?”
            Mheshimiwa Bwege anakula mic, “Kwa njia moja au nyingine nakubaliana na uchambuzi wako wa kisomi hasa kuhusiana na Eddie ambaye kwa sasa yuko anachekelea akingoja kwenda kuchunga ng’ombe baada ya kuwazika wapingaji. Mie nadhani alitumwa na Nambari wahedi kwenda kuwarahisishia kazi ya ushindi.”
            Msomi anarejea, “Washindi wa mwisho hapa ni wapiga kura ambao walifanya kweli kukwepa kuingiza kaya kwenye matatizo zaidi ingawa hawajaleta ukombozi kwa kuondoa balaa lenyewe. Kimsingi, naweza kusema hapa waliopoteza ni UKAUA ambao –baada ya matokeo kutoka na kugundua changa la macho walilopigwa na Nambari wahedi watajilaumu maisha yao yote. Wengine waliopoteza ni akina Sumuye, Kimdunge Ngumbaru Mwehu na wale viranja wa nambari wani waliomfuata Eddie kula njuluku zake.”
            Sofia Lion aka Kanungaembe anaamua kukamua mic, “Yako wapi na kiko wapi? Wengi hapa niliwaambia kuwa wapingaji hawakuwa na sera mkaniona hamnazo. Wengine mlinishutumu kuwa na mapenzi ya kibubusa msijue nayamanya haya mambo. Sasa kiko wapi? Uko wapi ukombozi mliokuwa mkihanikizia na kushangililia msijue tutachukua ngoma?”
            Kanji naye hataki kuachwa nyuma, “Mimi ikosangaa sana vatu ya kaya hii. Iko nazugwa na Eddie kuwa iko pinzani na pinzani kwa jinga na pofu yao naingia kenge. Sasa tajua kama suka au nyoa iko rahisi dugu zangu.”
            Mijjinga aliyekuwa akisoma gazeti anaamua kutia timu, “Kanji nakubaliana nawe. Siasa za kaya hii ni miradi ya wajanja wachache waliogeuza vyama kuwa kama NGO zao. Mimi ni mwanachama hai wa CHAKUDAME. Nilipinga sana movie hii lakini hawakunielewa. Sasa ngoja matokeo yatoke uone watakavyotoka nduki kuelekea kusikojulikana. Inasikitisha kuwa vyama vilikuwa vimejijengea umaarufu mkubwa na imani kubwa kwa wachovu lakini wakaharibu mwishoni kwa tamaa na ubinafsi na upogo wao. Lazima hapa watazomewa sana.”
            Kapende anarejea, “Mie wazomewe wasizomewe au kupigwa wasipigwe hanisikitishi. Kinachonisikitisha ni ile hali ya kuwa kila baada ya miaka mitano, tumaini linafutika kutokana na kutokuwa na vyama huru na vyenye lengo la kukomboa kaya. Hawa, kimsingi wameonyesha walivyoweka mbele maslahi binafsi wakatutelekeza. Sijui watatwambia nini baada ya Nambari wani kuchukua na kuweke waa ikachukua tena?”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si ukaja msafara wa wakota wa Nambari wani wakishangilia ushindi hata kabla ya matokeo rasmi kutoka! Kwa hasira kila mmoja alijikata kivyake kupinga kushuhudia shamra shamra hizi ambazo ni maudhi kwa Kijiwe.
Chanzo: Tanzania Daima Okt., 28, 2015.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 20:11 No comments:

I predicted UKAWA's defeat on August 23

I now predict once again. Dr. Silaha’ll follow suit after finding that he made odd bedfellows for long without reckoning with it. Now that message sent, I comfortably predict that the good Doc’ll soon divorce his former bad bedfellows to take on other partners preferably CcM. Shall this occur–and of course–it’ll occur, the so-called UKAUA will die naturally so to speak.
Shall the good doc decide to soldier on so as to lick his vomits; the dent will become more humongous. Either way, whether he stays or leaves this unscrupulous marriage, UKAUA will go under. Believe ye me. The stars don’t favour them, especially, when they became myopic so as to look at only positive side of their new bride by ignoring the ugly one. What’ll they tell boozers regarding all criminality they hurled at Luwasa in the first place? I heard one of them saying that the shotgun marriage with Luwasa is God’s plan. Wow! Which God is this? How does one bless sins in the name of God? Methinks a man should not act like a dog that is known for licking its own vomits.
I predict once again that after the coming elections coming to an end and resulting coming out favouring CcM, many fracas will erupt so as people to end up indicted before the International Criminal Court. If Luwasa assured himself that he is the anointed one, what do you expect will happen if the verdict comes favouring his opponents? Given that there won’t be any loophole for him to try his hand once again on presidency, I’m sure he’ll end up trying to create unrest that’ll guarantee the powers that be to quash it and thus create an issue. So, those thinking that things will be spiffy need to think twice.
I’m not making this up. Looking at Luwasa’s inexorable ardour for presidency, I can tell you this: The man’ll never go under without a fight come next elections. So, CcM needs to be prepared for such an eventuality.
Sometimes back, I predicted that CcM will face a lot of hurdles among which is the desire for every bigwig to aspire to become president which resulted into Luwasa’s kerfuffle.
When I look at CHAKUDEMA and KAF, I see a very tough tussle. Now that the prof is out, who comes next? Many former MPs from Simiyu, Rukwa, Dar, and other provinces will rock the boat just soon. As for KAF, things will be so tough in Zenj where a long-time suitor who’s now getting older will cause a lot of hubbub for the fear of losing his last chance of becoming the president of Zenj. This plus Luwasa’s manoeuvres, will give CcM a heck of time technically. I predict that many power seekers will suffer a lot of heart attacks due to losing millions of dosh.
Given that I’ve not gotten some Bangi and kanywaji–for today–I’ll doff hither asking you to keep an eye on what I’ve boldly predicted.
Source:Guardian Aug., 23, 2015.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 19:10 No comments:

Wakati nikingoja matokeo nilisikiliza muziki huu

I Met Girl ni muziki ambao unanikumbusha mambo ya miaka 20 iliyopita. Uniulize mambo yapi. Huyo Girl niliyekutana naye pia usiniulize ingawa yupo hapa karibu akisikiliza nami.

 I met a girl
 She made me smile, she made me wait
 She crossed the street, she crossed my heart
 She fixed her dress, she bit her lip, she lit me up
 I met a girl with crazy shoes and baby blues
 The way she moves is changing my whole world
 I met a girl

The sunshine waits for her to wake up
 She’s a pony tail no makeup Saturday
 She don’t need umbrellas in the summer rain
 She could catch the eye of a hurricane in blue jeans and pearls

Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 18:33 No comments:

Monday, 26 October 2015

Bootlicking is part of obedience in Kenya

Looking at how this geezer is self-dressing down you wonder if what he is doing is part of rule of law or true democracy or cronyism and "whiz kidding". Deputy President William Ruto and Kigumo MP Jamleck Kamau chat during a fund-raising.Deputy President William Ruto and Kigumo MP Jamleck Kamau chat during a fund-raiser for Muirini Mixed Day Secondary School in Kandara, Murang’a County, on Friday. At left is Governor Mwangi wa Iria, who earlier confronted Mr Kamau, accusing him of defamation. PHOTO | JOSEPH KANYI | NATION MEDIA GROUP
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 19:33 No comments:

Sunday, 25 October 2015

Oct., 25th is the moment of truth

           













October 25th marks the end of celebrations and temporal generosity that boozers used to enjoy. It officially marks the end of  politicking and entering fake and shotgun marriage. The time for relaxed and lax law enforcement that allowed boozers to swallow kanywaji and smoke marijuana is sadly over now.  Those who used to depend on campaign economy must go back to their troubles of chasing a Schilling without catching it. So, too, the language of pleading and courting is officially over today. However, boozers will miss this season of eating, drinking and enjoying performance for free. For, they dined and wined and rubbed shoulders with, and hugged the unhugable. They touched untouchable high and mighty that’ll soon become an expensive items soon after getting what they wanted.
            Those who used to get closer to the high and the mighty should prepare themselves to be pushed back by the bodyguards soon reminding them that the convenience marriage is now over. Boozers heard and saw the movers and shakers of whom; some will soon be shaken after losing it big. We evidenced all sorts of things from nice and long speeches to short ones by those who seemed either to be afraid of talking much or having nothing substantial to say or sick. I remember one boozer complaining that one of the presidential contenders became a dumb for fear of touching on his denting past history that's always haunted him up till this day.  Others speculate that the guy is dead in the water and sick. Boozers, too, were dumb to some extents. They failed to question contenders who were offering mshiko how they got it and who was sponsoring them and how he or she'd get the money back without compromising their rights and lives. Sometimes, you can argue that boozers are the victims of their own sheepishness and silence if not compliance in eating up dirty dosh that ends up buying, and torturing them for five years. I wonder sometimes. Somebody is bribed with offal and cheap things and offer her or his  precious vote to end up complaining for five years. Don’t they know that the law gives eaters power to do as pleased for five years? Had the new constitution been rewritten, such eaters would have been shivering? For, it strictly provided that those eaters who are letdowns should be recalled.
            Boozers wish campaigns should take forever so that they can enjoy the beauties and goodies that come therefrom especially sideshows and entertainments they used to enjoy for free however there are hidden costs in the just near future.
            We enjoyed their offers of offal compared to what they targeted. For, this fete won’t avail itself up till after five years. Instead what will surely happen is hardship and desperation after boozers misused their votes after being induced with offers and artificial generosity.
            Boozers are now pregnant with nice promises waiting for those promising them to deliver still babies in the name of politics. Again, it is ironic that boozers seem to be so forgetful that they don’t look at the outgoing kit and caboodle that promised the same and never lived up to its promises. To win boozers, you keep on feeding them with the same meme coupled with the mantra of development and change. Unfortunately for boozers, they don’t question the “change” you promise. Change is neuter. It can be positive as well as negative however –in politics –the later is the norm.  This is what booze scientists call politricks whereby smart chaps take boozers for a ride by pretending to stand for their interests.  If there is anything out of such milieu of promises is nothing but the memories of kanywaji and some cheap T-shirts, khangas, banquets and whatnot we were offered to soften us and give our votes for the coming eaters.
The hunk was awash with cash clean and dirty dosh. However, now you can see that the ball is in politicians’court up till results come out. Some will carry the day going home smiling while others will claim foul play simply because they didn’t make it. We’ve already heard some complaining even where they were not supposed to.Let's say it loudly and boldly. The ending campaigns brought some outright winners such as those who coaxed their nemeses to cleanse them as they committed suttee due to their myopia and greed. My friend Eddy even if he loses will go home smiling after punishing his foes from both sides of the divide. Bad new is that –shall UKAUA be knocked out, four dependable political outfits will, so, too, go under with him just like NssR Ma-change did with Gus Lyato in 1995. More bad news, the campaigning era evidenced the loss of ace politicos like Chris Mtikisa, Mood Mtoy, Deo Phil-ku-Njombe and many more. What a grueling battle that it was!
Source: Guardian Oct., 25, 2015.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 18:12 No comments:

Saturday, 24 October 2015

Ushauri kwa wapiga kura


  • ... , Dr John Magufuli for CCM and Mr Edward Lowassa for Chadema
            Leo ni moja ya siku inayowasumbua wengi. Kwani ni siku ambayo kura za watanzania zitaamua nani awe rais wao kwa miaka mitano ijayo. Hata hivyo, ukipita mitaani unaweza kutabiri kirahisi nani ataibuka mshindi. Katika siku hii ambayo ni muhimu sana –si kwa wapiga kura tu –bali watanzania wote, nitoe ushauri wa mwisho. Katika kipindi chote cha kampeni –katika makala zangu –nimejitahidi kumfagilia yeyote kati ya wagombea.
Naweza kusema kuwa rais mtarajiwa anajulikana kutokana na maongezi vijiweni, maofisini, kwenye vyombo vya usafiri hata majumbani. Pamoja na rais kujulikana, ngoja nami niongeze sauti yangu leo kupitia nafasi hii. Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia katika kupiga kura.
Mosi, mpiga kura lazima aangalie mgombea anayekidhi matarajio yake na si kwa maneno bali hata matendo yake binafsi. Hapa lazima kuangalia historia ya mgombea. Nasema hili kutokana na psychology iliyojitokeza ambapo watu wanasema wako tayari hata kuchagua shetani hata jiwe ilmradi wakiondoe chama tawala. Sidhani kama mawazo ya namna hii ni sahihi na yanajenga.
Pili , wapiga kura watafakari kwa makini kauli mbinu iliyotawala yaani, mabadiliko. Wajue kuwa mabadiliko yanaweza kuwa hasi hata chanya na bado yakaitwa mabadiliko. Hivyo, tunapoongelea mabadiliko tujikite kwenye mabadiliko chanya na si mabadiliko hatari ya kubadili vya na kuweka watu wasiofaa. Mfano, wapo wanaoona kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) hakifai kwa vile ndicho kimesimamia uoza uliopo. Ni kweli, je mgombea binafsi ameshirikje? Hili ni swali muhimu kutokana na ukweli kuwa wagombea wanaoonekana kuwa tishio ambao mmojawao atakuwa rais yaani Dk John Pombe Magufuli na Edward Lowassa, wamezaliwa, kulelewa na kukulia CCM hata kama mmojawapo ameijiunga na upinzani kwenye dakika za mwisho tokana na kuamini kuwa hakutendewa haki. Hivyo, Magufuli na Lowassa hawawezi kukwepa lawama au pongezi tokana na matendo na rekodi za CCM kiutendaji.
Tatu, wapo wanaojinasibisha na marehemu baba wa taifa , Mwl Julius Nyerere aliyewahi kusema kuwa watanzania wanataka mabadiliko. Na wakiyakosa ndani ya chama watayatafuta nje yake. Hata hivyo, wanashindwa au wanakwepa kuendelea na wosia huu adhimu wa mwalimu. Kwani katika wosia huu alimalizia kwa kusema kuwa bado CCM ndicho chama ambacho kilikuwa kinafaa. Nadhani, alichosema mwalimu ni kwamba watanzania wanachukia na wamechoshwa na ufisadi. Hivyo, tunapotaka kutumia wosia wa mwalimu, tuwapime wagombea kwa kuangalia wanauchukia au kuushiriki vipi  ufisadi. Sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu anaweza kubisha kuwa wawili wanaoongoza katika kinyang’anyiro hiki ni watu wawili tofauti japo wote wanaungana kwenye historia zao na CCM. Sidhani kama watanzania watatumia mihemko na kukata tama wakachagua mtu wanayejua fika hana mpango na maslahi yao zaidi ya maslahi yake binafsi.
Nne, wapiga kura wanapaswa kutafakari na kudurusu mambo kama vile afya za wagombea, ahadi zao, historia zao  na  hata sera zao. Waepuke kufanya jambo la maana kama kumpata kiongozi kwa miaka mitano kuwa suala sawa na kwenda kununua nyanya. Kura zao zitaamua mustakabali wao na wa taifa kwa ujumla. Mfano, vyombo vya habari vyenye uthubutu vimelalamikia afya za baadhi ya wagombea. Nao kwa –ma kuogopa kumwaga mtama kwenye kuku wengi au kutokuwa na majibu –wameshindwa  kutoa utetezi. Hii maana yake ni kwamba lisemwalo lipo na kama halipo basi laja.
Tano, kwa vile mabadiliko yanayotakiwa ni yale yatakayowahakikishia watanzania kuwa kuna mwenye nia na uwezo wa kupambana na ufisadi, basi warejee kutafakari kauli za wagombea  hawa wawili juu ya kupambana na ufisadi. Watafakari usayansi na uwezekano wa ahadi za wahusika. Mfano, Dk Magufuli alisema ataunda tume au tuseme mahakama maalumu ya kushughulikia watuhumiwa wa ufisadi ambao rais anayeondoka aliwagwaya au kujifanya hasikii kutokana na sababu ajuazo. Lowassa amejitahidi kutogusia suala la ufisadi kabisa. Wapo wanaoona kuwa ameepuka kuingia malumbano juu ya tuhuma za uongo na za kweli vinavyomkabili. Pia, wapo wanaomkosoa kama mtu ambaye hawezi kupambana na ufisadi. Kimsingi,ni kwamba watanzania watakuwa wamepoteza fursa adimu –kama watazugwa na wakakubali ima kutokana na hongo au lugha tamu –wakamchagua mtu fisadi au hata mgonjwa.
Sita, wapiga kura waepuke ushabiki wa vyama. Kwani rais atakayechaguliwa atakuwa rais wa watanzania wote wakiwamo vya vyama pinzani na wale ambao walimnyima kura au kutopiga kura kabisa. Hivyo, tunapaswa kuweka utaifa wetu mbele kuliko vyama vyetu au mapenzi a kibubusa. Kinachopaswa kuzingatiwa ni ukweli kuwa rais akishachaguliwa,  hakuna mechanisms za kumuondoa hata aboronge namna gani hadi amalize miaka mitano. Hivyo, kuchagua rais si jambo la kubabaisha wala la kufanya maamuzi mepesi zaidi ya kujikita kwenye mambo ya msingi kama baadhi yalivyoainishwa hapo juu.
Tumalizie kwa kuwataka watanzania wawe makini wasije wakachagua mtu atakayewaingiza kwenye matatizo zaidi ya haya wanayotaka kuondoa. Tusisitize kuwa wasichague mtu wanayeshuku afya yake ina ugogoro au ambaye hata ithibati na ujasiri wa kuongelea, kukemea hata kupambana na ufisadi.
Wekeni kwenye makini .Tukutane wiki ijayo. Nawatakia uchaguzi wenye busara na wa amani. Amina.
Chanzo: Tanzania Daima Okt., 25, 2015.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 18:34 No comments:

Thursday, 22 October 2015

Wimbo wa wiki


Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 21:30 2 comments:

Tuesday, 20 October 2015

Kijiwe chahoji wanene kudedia ugabacholini

Baada ya kuwazidi kuzoeleka taarifa za kuhuzunisha ambacho wanene wetu wanadedia kwenye hospitali ya Apollo huko Ugabacholini, Kijiwe kimeamua kujitoa kimasomaso na kuhoji deal hili ambapo wanene sana wanawateua wanene kiasi wagonjwa ili kutibiwa kwa njuluku za kijiwe huku wanakijiwe wakiteketea kwa magonjwa yanayoweza kuzuilika na kutibiwa.
            Leo Kapende analianzisha, “Jamani waheshimiwa mwaonaje hili dili la wanene wetu kudedia ugabacholini wakati huduma za afya hapa kayani zikizidi kuhujumiwa na kudumaa?”
            Mipawa anakula mic, “Hata mie nashangaa uroho na roho mbaya hii ambapo wanene wanaijihudumia kwenye hospitali zenye kila kitu huku wakituachia hospitali zisizo na kitu chochote zaidi ya mateso na mauti. Sijui inakuwakuwaje hadi wanene wagonjwa wanabakizwa kwenye ulaji ili wafie humo na matibabu yao tubebeshwe sisi.”
            Mijjinga ananyakua mic, “Unashangaa hili! Kwa taarifa yako hii ni kaya ya wagonjwa na walafi ambapo –kwa makusudi mazima –wajamaa wanaojijua kuwa wako hoi bin taabani wanawania ulaji na kupita bila kupimwa afya zao jambo ambalo linaongeza mzigo kwa wachovu wa kaya hii. Nani anajali iwapo kila mnene anaona ni zamu yake kula?”
            Mpemba anakatua mic, “Yakhe mie nshashangaa sana. Kwanini tusibadilishe sharia kiasi cha kutaka kila anayegombea nafasi ya umma apimwe afya yake ili kuepuka kaya yetu kugeuzwa mfadhili wa wagonjwa tena wenye njuluku nyingi?”
            Msomi Mkatatamaa anatia guu kwa zali na kusepa, “Hakuna haja ya kushangaa hasa ikizingatiwa kuwa kikundi kidogo cha walaji, mafisadi, wezi, wasanii na wababaishaji wamepoka kaya yetu kiasi cha kufadhiliana hata kwa gharama ya afya na maisha ya wachovu wetu. Ukiangalia takwimu unaweza kuzimia. Sell Kombania, Abdi Kikalio, na yule mama mwingine sijui anaitwa nani wamedidia kule wakitibiwa kwa njuluku za umma. Ukiangalia waliodedia kule Apollo tangu fasheni ya kuhujumu na kuua huduma za afya ianze unaweza kuzimia. Inashangaza mnene mkuu anayeondoka kuwa bingwa wa kuteua wagonjwa ilhali wachovu wazima na wasomi tupo.”
            Mheshimiwa Bwege anakula mic, “Msomi usinichekeshe japo si kwa furaha. Nani akuteua wewe uende kuwaumbua kwenye wizi, ufisadi na ulaji wao? Thubutu!  Kayani sifa za kitaaluma hazina maana tena zaidi ya kujuana na mitandao mingine ya kishenzi inayohujumu kaya yetu. Laiti kama rahis au mkewe wangekuwa ndugu zako unadhani ungekuwa hapa kijiweni ukilalamika wakati una elimu ya kutosha na ya juu kuliko hata rahis mwenyewe? Mie nadhani wanene watueleze waziwazi kuwa tumegeuka kaya ya wagonjwa. Vinginevyo tusipoamka na kushupalia wizi huu wa kulindana na kufadhiliana, tutaendelea kunyotoka roho huku wenzetu wakienda majuu kupima hata kutibiwa mafua.”
            Sofia Lion aka Kanungaembe anakwanyua mic kwa usongo, “Hivi jamani nani aliwaroga wachovu wa kaya hii?  Mnataka wanene nao wakasongamane na kutolewa njuluku kwenye hospitali zetu uchwara kana kwamba wao si wanene siyo? Kwanza mmempata wapi huu uongo kuwa wanatibiwa kule kwa njuluku zenu kama siyo umbea na roho mbaya? Nani amewazuia nyinyi kwenda kutibiwa Apollo kama siyo roho mbaya tu?”
            Kanji anakatua mic, “Mimi iko unga kono veve dada yangu Sofi. Kama India natoa huduma bora zito yote takwenda kupata huduma bwana. Kama nasindwa jenga hospitali zuri yako tegemea nini jamani? Nasahau kuu nakwenda kwa Joji Chaka tibiwa ile gonjwa nafisha ogopa stua nyinyi penzi yake?”
            Mgosi Machungi anakatua mic kwa usongo, “Da Sofia na Kanji tiheshimiane na tisitiane madole eheee! Titachenjiana hapa.  Kwani inataka kusomea inteijensia kujua kuwa wanakwapua njuuku yetu? Nadhani kama wewe hujui waivyo waroho na wenye roho mbaya basi hupaswi kuja hapa na kama utakuja hapa basi ujinyamazie.”
            “Mimi mwenzenu hakuna kilichoniumiza kama kifo cha huyu Phil-ku-Njombe aliyekufa kwenye ajali ya chopa hivi karibuni. Utadhani mwaka huu ni wa wanasiasa!” analalamika Mchunguliaji ambaye mara nyingi huwa hachangii sana.
            “Ni kweli inahuzunisha. Nadhani kuna haja ya kuoni vyombo na miundo mbinu yetu. Maana nijuavyo, kwenye ufisadi uliotamalaki, kila kitu huwa hatari hasa vyombo kama ndege. Nadhani haya makampuni yanayoendesha hii biashara ya chopa yanapaswa kumlikwa kuona kama yanafuata taratibu zote za kiusalama. Hata hivyo sina shaka watashughulikia kutokana na kuwa nyenzo hii mara nyingi inatumiwa na wanene ambao mara nyingi huwa hawataki shida,” anajibu Msomi.
            Anakohoa na kuendelea, “Kuhusiana na hili la kama wanatumia njuluku zetu au zao mfukoni, nadhani kila kitu kiko wazi ingawa da Sofi anajitahidi kuupaka rangi upepe. Mgosi umemjibu vizuri. Kwa walivyo waroho, wabinafsi na wenye roho mbaya bila shaka wanalipiwa na njuluku yetu ya kodi ambayo licha ya kulipiana matibabu wamekuwa wakiiba na kuwapa washihrika zao misamaha ya mabilioni ya njuluku.”
            Kijiwe kikiwa ndiyo kinanoga si ukapita msafara wa geneza la kamanda Deo Phil-ku-Njombe likielekea kwenye hekalu lake alilolioacha bichi kule Kijichi. Wote tuliamua kumsindikiza kamanda huyu aliyechukia ufisadi na aliyonyotoka roho akiwa bado mbichi.
 Chanzo:Tanzania Daima Okt.,21, 2015.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 21:26 No comments:

Huu mtambo kweli kweli


Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 18:39 No comments:

Je Amani ni pale Lowassa anapokuwa na tonge akinyang'anywa si amani tena


Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 18:17 2 comments:

Sunday, 18 October 2015

Wasanii ni wakereketwa au njaa na upogo?

Kampeni za uchaguzi mkuu zinazoendelea zimefichua uoza mkubwa sana hasa kuhusiana na tasnia ya sanaa hasa za maigizo. Japo ni haki ya wanasanaa kuchagua ni wapi pa kuuza huduma yao, kufanya hivyo lazima kuenende na maslahi ya taifa. Maana bila taifa hakuna wasanii wala wanasiasa au aina yoyote ya tasnia na nyanja. Katika kampeni zinazoelekea ukingoni, kumejitokeza “mapenzi” ya ajabu kwa chama tawala yaani Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kwanini tunasema hivi? Msanii akikodiwa sawa na mwenye bodaboda au taxi kazi yake ni kumfikisha abiria wake aendako. Hiyo ndiyo kazi halali inayofanya apewe ujira.  Zaidi ya hapo ni kukiuka miiko na maadili ya kazi husika. Hetu tutoe mfano zaidi. Si kazi ya dereva wad ala dala au taxi au bodaboda kujenga uhusiano wa ndani na wateja wao zaidi ya ule wa kikazi. Hili ni takwa la aina yoyote ya kazi iwe ndogo au kubwa. Inashangaza kuona wasanii waliokodiwa kutumbuiza wakaishia kuhutubia mikutano ya siasa wakionyesha wazi kushambulia upande fulani huku wakiuhami upande mwingine. Hii si kufanya sanaa bali siasa kwa mgongo wa sanaa. Wasanii wa namna hii wanapaswa kuonywa na ikiwezekana kuchuliwa hatua. Kwanini iwe haramu, kwa mfano, viongozi wa kidini kuonyesha ushabiki wa siasa lakini iwe halali kwa wanasinii?
Juzi juzi tumewasikia baadhi ya wasanii wakilaani upinzani kana kwamba ni wapinzani wao. Hii siyo sawa. Msanii kama dereva wa daladala, bodaboda na taxi hapaswi kubagua wateja wake. Msanii ni sawa na barabara. Hapaswi kubagua magari. Hata rubani wa ndege –pamoja na hadhi ya nafasi yake –hawezi kuwabagua abiria wake. Je wasanii wanatenda jinai hii kwa jamii kutokana na uhaba wa elimu au makusudi mazima ili kujiweka karibu na chama chenye ulaji ili wapate ulaji? Tumewaona wengine wakigombea ubungu wa dezo na kubwagwa chini wakiishia kutoa nadhiri kuwa wao ni wanachama wa CCM hadi kufa.  Nadhani tatizo jingine hapa ni ile hali ya siasa kuwa biashara inayoingiza utajiri wa haraka bila kutoa jasho. Ndiyo maana wasanii, wanataaluma, wafanyabiashara hata wahalifu wanawania nafasi za kisiasa.  Kwa vile wanasanii sawa na wanajamii wowote wana haki ya kushiriki siasa, basi wavae kofia moja ya usanii au ya siasa lakini siyo kuchanganya. Kufanya hivyo si kutenda haki hata kidogo. 
Kinachogomba ni ile hali ya wasanii kufunga ndoa na chama tawala kwa sasa wakati ni chama kile kile kilichotelekeza maslahi yao hadi watu binafsi kama Msama Promotion walipoingilia kuwaokoa na wizi mkubwa wanaoendelea kufanyiwa na wafanyabiashara wa kihindi. Kwani hii ni siri? Ni ajabu kuwa wasanii hawa hawa wanaotumiwa nao wakajiachia kutumiwa kesho utawasikia wakilia serikali hawajali wakati wao hao hao ndiyo wametumiwa kuiingiza madarakani. Wapo wanaodhani kuwa kinachowasumbua baadhi ya wasanii ni njaa na uwezo mdogo wa kupembua mambo.  Msanii anapaswa kuwa kioo cha jamii. Anapogeuka kuwa dodoki la jamii kidogo inatia shaka na –kama sikosei –mhusika anaanza kuuzika usanii wake. Maana unapokubali kutumiwa kama msanii, basi ujue unaondoka kwenye mstari na kufanya vitu ambavyo vitawapendelea watu fulani na kuwaumiza wengine. Sambamba na wasanii wanaojirahisi na kujiruhusu kutumiwa ni waandishi wa habari nyemelezi almaaruf kanjanja. Nadhani kadhia ya waandishi wa habari sawa na wasanii kutumiwa kufanya kazi chafu za wanasiasa na vyama vya siasa zilianza hapo 2005 ambapo waandishi waliokuwa wakionekana nguli walitiwa mifukoni mwa wanasiasa fisadi waliokuwa wakiwania madaraka. Wapo waliofanikisha kazi hii chafu na hovyo na kulipwa fadhili. Kadhalika wapo wengi walioshia kutumiwa kama vyangudoa wasiambulie ujira wowote. Baada ya kumaliza kuwachafua na kuwadhalilisha waandishi wa habari, sasa wanasiasa wamewadandia wasanii ambao nao kwa upogo na ufinyu wa uoni wamejiachia na kujitoa kufanya kazi chafu ya wahusika kwa malipo uchwara yatakayowafanya wajione wamepata kwa sasa wasijue wanachouza ni cha thamani na cha muda mrefu kuliko hizo peremende na bakhshsh wanazopewa. Hawa kwa kiarabu huitwa muafinati kama ni wanawake au maufinini kama ni wanaume. Maana ya neno hili ni kwamba mhusika anayekuwa muafin au muafina hana tofauti na kinyesi kwa kero anayowasababishia wengine. Kwanini nasema ni kero wanayopata wenzake?  Taifa letu liko msambweni kwa sasa. Wasanii wanapotumia vipaji vyao kuwahadaa na kuwapotosha wananchi wanakuwa sawa na kinyesi. Kwani uoza na harufu na madhara ya nafasi yao itasimama kwa miaka mitano kuanzia sasa.
Hivyo, bila kusema mengi, tunashauri wasanii wanaotaka kuwa wanasiasa basi waachane na sanaa na kuwa wanasiasa kuliko kuwa wasanii-wanasiasa.  Pia wasanii wengi wafahamu kuwa si rahisi kupata ulaji wa dezo wa kisiasa kama vile ubunge iwe wa kuchaguliwa au kuteuliwa. Nafasi ni chache na zinataka watu walioiva kielimu na siyo umaarufu tu. Hivyo, badala ya kukubali na kujirahisi kutumiwa, wasanii wanapaswa wajikite kuwapima wagombea kubaini ni wapi wanaweza kuwaondolea kadhia zao hasa kudhalilishwa na kunyonywa.
Chanzo: Tanzania Daima Okt., 2015.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 06:22 7 comments:

Tuesday, 13 October 2015

South African withdraw from ICC misguided

  • The Hague; Exterior of International Criminal Court or ICC in the ...

When the South African ruling party, the National African Congress (ANC) came up the drive to see South Africa withdrawing from the International Criminal Court (ICC) many were dismayed, saddened and shocked. How could the icon of liberation in Africa act this way? The Daily Telegram October 11th, 2015 quoted Obed Bapela, head of ANC’s international relations commission as saying “They would rather put their own interests first than the world's interests, and as a result of that the commission and the NGC has just confirmed that the national interest policy must be fast-tracked in Parliament so that the nation can comment on it.” Whose interests are these if not those of a kit and caboodle of government officials? Methinks the interests of South Africans should come first.

Due to her weight, South Africa, since she acquired her independence, has been a key player in Africa’s and world’s issues. She is the second biggest economy after Nigeria. So, too, her history of struggle against inhumane regime is an asset that would have guided the ANC in reaching such detrimental decision not for South Africa only but also for Africa. Many would think that the South Africa that recently evidenced the upsurge of xenophobia attacks would encourage other African countries to stay in the ICC as her efforts to create a good rapport in the realpolitik of the world. However, there are those who think that the ANC took such a misguided decision aiming at shifting the attention of South Africans vis-à-vis corruption and incompetent rule in the country presided over by the same ANC. Although it is the countries right to remain or withdraw from any organisation, it is irrational and counterproductive for South Africa to withdraw from the ICC. I wonder, if –let say –we reverse the clock and see some apartheid top brass before the ICC charged for crimes against humanity for the many years they mismanaged south Africa, would the ANC take the same stance? Isn’t this holier than though apart from being hypocritical and selfishness. I don’t know how people in Darfur Sudan that have suffered for long from genocide committed by Omar Bashir’s regime will take such news. Again, if there is a big beneficiary of ANC’s move is none other than Bashir whom South African authorities failed to apprehend and submit to the ICC when he was in the country to attend an African conference in June 2015. Many thought this was enough. Now the ANC has purposely and willingly decided to do Bashir’s dirty laundry. Why?

South Africa is supposed to be a leader in the quest for justice and human rights in the continent and in the world. I am wondering. I don’t think if Nelson Mandela or Thabo Mbeki were in power still would buy into such a decision aimed at humiliating South Africa by portraying her as the state that sponsors criminals such as those who committed genocide in Sudan. Where does the ANC get such chutzpah? Did the ANC underscore negative impacts such misguided step will cause South Africa? It is time to tell South Africa to rethink her stance on the ICC. Her take would be misconstrued as laying a foundation for inhumane treatments against those opposing corruption in the country. Is South Africa taking preemptive measures to avoid her high-ranking officials to be brought before the ICC after committing Marikana massacres?

It doesn’t cross any mind for South Africa to embark on such dressing down aimed at protecting individual at the expense of the entire nation. South Africans should stand up and oppose machinations that aimed at portraying a country in the bad light. The ICC is still a valid entity as far as combating crimes against humanity is concerned. So, too, South African authority, especially the ANC must be told to their face that they were not coerced to join the ICC. It pains beyond imagination when the oppressed of yesterday becomes the oppressor of today. The ANC must restrain itself from going on being a letdown as far as South Africa is concerned.
Source: African Executive Oct., 14, 2015.

Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 20:12 No comments:

Kijiwe chamuomboleza Mtikila

            Baada ya kutokea kifo cha ghafla cha Chris Mtikila, Kijiwe kilikaa kama kamati kumkumbuka gwiji huyu wa ukombozi pamoja na utata wake. Kijiwe kilihuzunishwa na kifo cha Mtikila hata kama hakiungi mkono misimamo yake yote.
            Msomi Mkatatamaa ndiye analianzisha. Anaingia akiwa na huzuni wazi wazi jambo ambalo si kawaida kwake. Anasema, “Mwenzenu nina huzuni sina mfano. Kaka Mtikila hatunaye tena. Ameaga dunia kwenye ajali itokanayo na ubovu wa sheria za barabarani na barabara pia. Kaya imepata pigo jingine baada ya lile la Mchonga.” Anainamisha kichwa kama ishara ya kuiombea roho ya marehemu.
            Sofia Lion aka Kaunungaembe anakula mic, “Inasikitisha ila kifo ni jambo la kawaida kwa kila mja. Nadhani wakati wake ulifika hivyo hatuna la kufanya. Sikubaliani na kumlinganisha Marehemu na baba wa taifa. Walikuwa vitu viwili tofauti. Hata hivyo ametuachia somo kubwa kuhusiana na mahusiano yetu kama wanajamii.”
            Mgosi Machungi anapoka mic, “Da Sofi acha utani. Unaongea kama vie hujaguswa na kifo cha gwiji huyu wa Saa ya Ukombozi na magabachoi. Unaonyesha wazi kuwa hukumpenda huyu gwiji sijui ni kwanini,” anamaliza sentensi huku akimtazama Kanji kwa chati.
            Sofia anajibu, “Niguswe nisiguswe hili si muhimu. Nimepende nisimpende hiyo si kazi ya mtu.  Kwani alikuwa ndugu yangu? Kwa taarifa yako, mimi sikupenda hotuba zake za chuki na uchochezi zilizolenga kutochonganisha na kutugawanya. Hata hivyo, nasikitika amepotea.” Anamalizia huku akitabasamu jambo ambalo linawashangaza wengi.
            Mipawa anakamua mic, “Dua la kuku halimpati mwewe da Sofi. Heri yeye amefunga chake kuliko hawa wanaoshangilia kifo chake kana kwamba wao hawatakufa. Nadhani tunapaswa kumuangalia marehemu kwa yale aliyosimamia. Pia tutazame mema yake tukipuuzia mabaya. Nani ni malaika? Heri yake alisema na kuweka msimamo wake wazi kuliko wanafiki na mafisadi wanatudanganya kwa kubadili vyama kama nepi.”
            Kapende anadandia mic, “Mie huyu bwana nilikuwa namkubali na ni mtu pekee aliyenitoa na kuingia mitaani  na kushiriki maandamano kwa mara ya kwanza na ya mwisho miaka ile ya magabacholi aliosema wamemiliki uchumi wa kaya yetu huku sisi tukiteseka. Haya ndiyo masuala ya kuongelea au vipi?”
            Msomi anarejea, “Kwanza niwapongeze kwa michango yenu ya kisomi na tekenyeshi. Ni kweli, kama alivyosema Dk Mipawa ni kwamba tusiwe na mawazo mafupi ya kujadili watu badili ya masuala. Hebu tusiwe wezi wa fadhila. Nionyeshe mwanasiasa yeyote aliyehai anayeweza kuvaa viatu vya marehemu. Tumpate wapi jasiri kama yeye? Tumpate wapi mtu aliyeweza kueleza hoja zake kwa lugha na staili vinavyoeleweka? Tuwe wakweli. Marehemu alikuwa jasiri na mwenye kuchukia upuuzi ambao umetufikisha hapa,” anakohoa na kuendelea, “Tunapomlinganisha marehemu na baba wa taifa, hatuna maana ya kumkosea yeyote heshima au kumpalilia. Tunachomaanisha ni kwamba, hata kama walitofautiana na baba wa taifa, wote walikuwa na misimamo inayoeleweka hata kama hatukukubaliana nao, walikuwa wakweli, jasiri na wajuvi wa mambo na wenye ufasaha kwa kueleza mawazo na hoja zao huku wakijua kujenga na kubomoa hoja za wapinzani wao.”
            Mpemba anakamua mic, “Yakhe msemayo kweli. Hata kama twawachukia watu, wakishakufa twapaswa kuwasamehe. Mie huyu bwana aliniudhi sana pale aliposema eti nasi ni magabacholi wakati ni wanakaya. Hata hivo, namsamehe sana na kumuombea maghufira aamin. Hakuna haja ya kushangilia mauti ya mwenzio. Kullu nafsin zaikatul maut, kila mtu yatamfika mauti.”
            Kanji anachangamkia mic, “Mimi iko penda sana yeye Tikila. Hapana chukua ile yote nasema. Yeye nasema moja kwa moja. Iko nyingi nachukia sisi lakini hapana sema wazi wazi. Mie iko penda adui naambia mimi kuliko ile nacheka na mimi.”
            Mheshimiwa Bwege anakula mic, “Kama alivyosema Profesa Msomi, hebu tuwe wakweli. Kweli dhambi ya marehemu unaweza kuilinganisha na majambazi kama Rugemalayer au hawa wanaotuhadaa tuwachague wakati walishatutesa kwa kutuibia sana? Nadhani marehemu alikuwa msemakweli hata kama ana utata wake. Angalau yeye alisema wazi wazi kuliko wanaoficha na kututapeli. Saa ya Ukombozi ni sasa.”
            Mzee Maneno anakamua mic, “Nyinyi hamjui. Marehemu alikuwa mshirika na mshauri wangu wa karibu ingawa sijawahi kuwaambia hili. Tulishauliana mambo mengi kuhusiana na ukombozi. Hivyo kifo chake kimenitia simanzi ajuaye Mungu mwenyewe. Ni muhimu tumsamehe na kusimamia yale aliyosimamia tunayoona yana maana katika maisha yetu.” Baada ya kumaliza kuongea tunaangaliana kama kuonyesha kuwa hili la marehemu kuwa mshauri wa mzee Maneno ni kama changa la macho.
            Wakati tukiwa tumebung’aa na kuangaliana, Msomi anakula mic tena, “Mie nadhani huyu bwana alikuwa mtu wa watu kwa kiasi kikubwa. Kuna kipindi alikuwa na msimamo si kawaida ingawa baadaye alilainika. Hata hivyo, sijui kilichomlainisha ingawa kipindi hiki alikuwa amerejea upya kuonyesha msimamo wake dhidi ya harakati za mafisadi kutaka kututawala.”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si tukaona msafara wa magari yaliyosindikiza mwili wa marehemu ukifika. Wote tulifunga kijiwe na kuelekea Diamond Jubelee kumuaga shujaa huyu wa walalahoi na kiboko ya magabacholi na mafisadi.
Chanzo: Tanzania Daima Okt., 14, 2015.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 20:08 No comments:

Monday, 12 October 2015

Rais ajaye aepuke yafuatayo

         Si kawaida kwa mgombea wa chama kulaumu chama chake au serikali yake hasa pale kinapokuwa chama tawala. Mgombea wa Chama Cha Mapinduzi, Dk John Magufuli na katibu mkuu wa CCM Abdulrahaman Kinana wamesikika mara nyingi wakikosea serikali ya rais anayeondoka Jakaya Kikwete. Lawama zinapotolewa na watu hawa zinakuwa na ukweli na zinapaswa kuwa na athari kuliko zikitolewa na wapinzani ambao mara nyingi hulaumiwa kwa kulaumu hata kama wanachosema ni kweli.
            Hakuna ubishi kuwa serikali ya awamu ya nne ni moja ya serikali mbovu Tanzania ilizowahi kuwa nazo. Tutatoa sababu.          
            Kwanza, hakuna ubishi kuwa serikali ya Kikwete haikutimiza ahadi zake jambo ambalo wakosoaji wake huliita usanii au utapeli.
            Pili, imesababisha uchumi na sarafu yetu kudorora. Nakumbuka wakati Benjamin Mkapa akiondoka madarakani shilingi yetu ilikuwa ikibadilishwa kwa takribani 1,200 kwa dola. Sasa imeporomoka zaidi ya nusu.
            Tatu, ilisababisha deni la taifa kuumka bila maelezo tokana na matumizi mabaya kama vile kusafiri kwa rais nje mara kwa mara akiandamana na walaji wengi ukiachia mbali kutokusanya kodi vilivyo na kupanua serikali bila sababu. Rejea kuongeza idadi ya mikoa na wilaya kwa sababu za kisiasa zaidi ya za kiuchumi.
            Nne, serikali ya awamu ya nne ilifuga na wakati mwingine kushiriki ufisadi. Rejea kuingia kwake kuhusishwa na kashfa ya EPA na sasa Escrow ambayo walioisuka wako nje wakiendelea kuheshimiwa hata kupewa tuzo za uongo na ukweli.
            Tano, ilipoteza fedha nyingi za umma kwenye mambo ya hovyo kama vile kutumia mabilioni kugharimia ukusanyaji wa maoni ya katiba mpya iliyoishia kuuawa huku maoni aghali kama haya yakidharauliwa. Wengi wanajiuliza: Kama Kikwete hakutaka kuwa na katiba mpya ni kwanini aliharibu muda na fedha vya umma?
            Sita, iliua elimu kiasi cha wasomi wetu wanaozalishwa kwa sasa kushindwa kuajirika hata kujiajiri.
            Saba, iliahidi kurekebisha mikataba ya uwekezaji ikaishia kuingia mikataba mingine michafu na ya hovyo kuliko hata ile iliyopaswa kuirekebisha. Rejea uuzaji wa Richmond kinyemela kwa Dowans ambayo nayo iliingia kinyemela kiasi cha kuendelea kupoteza fedha za umma. Rejea utata wa ubinafsishaji wa lililokuwa Shirika la Usafiri Dar Es Salaam kwa kampuni yenye kutia shaka ukiachia mbali kuhusishwa na vigogo ya Simon Group.
            Nane, kutumia fedha nyingi kujenga barabara zisizofikia viwango wala kulingana na gharama ya fedha zilizotumika. Rejea madai yaliyotolewa na vyombo vya habari kuwa barabara nyingi–licha ya kujengwa chini ya viwango–zimepunjwa ukubwa wake kiasi cha kugeuka makaburi ya abiria wasio na hatia. Hata tuhuma zilizotolewa, serikali haikujihangaisha kukanusha wala kutoa maelezo.
            Kimsingi, makosa ya serikali ya awamu ya nne hayawezi kujadiliwa kwenye makala moja au hata kumi. Hivyo, kwa kuangalia hayo machache juu, tunashauri rais ajaye afanye yafuatayo.
            Kwanza, asijiingize kwenye jinai ya kuzurura ughaibuni bila sababu. Akifanya hivyo, atakuwa hajifunzi kutokana na makosa.
            Pili , afufue uchumi kwa kukusanya kodi , kuziba mianya ya kukwepa kodi na kuzuia misamaha ya kodi ambayo mara nyingi ni dili kati ya wafanyabiashara na wakuu wa idara za mapato.
            Tatu, afumue mikataba ya uwekezaji ya kijambazi ili lau taifa liweze kunufaika na raslimali zake.
            Nne, awashughulikie watuhumiwa wote wa ufisadi wanaojulikana ambao serikali inayoondoka –iliwaogopa au kuwaacha kwa sababu ijuazo –kiasi cha kusababisha tuhuma kuwa nayo ilikuwa ikila nao.
            Tano, ahakikishe elimu yetu inafufuliwa kwa kurejesha mfumo wa zamani uliwapa changamoto wanafunzi kusoma vitabu mbali mbali badala ya vichache wanavyosoma kwa sasa na kumaliza shule bila kupikwa na kuiva vya kutosha.
Sita yote katika yote, ahakikishe katiba ya wananchi iliyouawa kwa hofu za kifisadi inapatikana. Hili –licha ya kuwa muhimu–ni rahisi kulitimiza tokana na kuwepo maoni yaliyokusanywa na Tume ya Jaji Warioba.
            Saba, asiendelee na tabia ya kuunda mikoa na wilaya kwa sababu za kuzawadiana na kufadhiliana kisiasa kama ambavyo imekuwa.
            Nane, atimize ahadi alizotoa kwenye kampeni kiasi cha kuwashawishi wananchi kumchagua. Nadhani aibu anayoipata Kikwete inatosha kutorudiwa vinginevyo ajaye awe ni photocopy ya utawala unaoondoka kiasi cha kuwafanya wapiga kura wajutiea kuwa wanawaamini wanasiasa bila kuwa na mfumo wa kuwawajibisha ambao kimsingi ulikuwa kwenye katiba mpya iliyouawa.
            Mwisho, rais ajaye asiruhusu mkewe kujiingiza kwenye biashara ya kuanzisha NGO kwa ajili ya kufanya biashara ikulu. Pia atangaze mali zake na za mkewe ili ujue ameingia na kiasi gani na akiondoka ataje ujue ataondoka na kiasi gani. Tusisitize kuwa rais ajaye asiwe kama Mkapa aliyeingia akiwa maskini akaondoka akiwa tajiri kiasi cha kushindwa kutaja utajiri wake.
Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 11,2015.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 07:26 No comments:
Newer Posts Older Posts Home
Subscribe to: Posts (Atom)

Cordially and unlimitedly welcome to this blog.


Writing and reading are two different processes but which share the same goal-to educate, communicate and entertain.
It is my pleasure to have you as the guest of this tablet.
I, thus, warmly and always, welcome you to share ideas.
Importantly and eminently, shall there be anything amiss or you think can advance this blog, please donate it.
Allow me to humbly and kindly welcome you once again.
Nkwazi N Mhango- A Man And a Half

When wisdom brings no profit, to be wise is to suffer. Not all thoughts are good and constructive. Others are even worse than bullets. The good thinkers are the ones that think constructively for the manumission of all bin-Adams regardless their diversity. Mwl. Nkwazi N Mhango,
Canada.


Epistle to Afrophobic South Africa

Epistle to Afrophobic South Africa

Magufulification

Magufulification

BORN NUDE

BORN NUDE

Total Pageviews

Heko Rais Magufuli

Heko Rais Magufuli

DECOLONISING EDUCATION

DECOLONISING EDUCATION

Kudos President Magufuli

Kudos President Magufuli

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

The Family Friend of Animals

The Family Friend of Animals
Children's Book

Matembezi Mbuga ya Wanyama

Matembezi Mbuga ya Wanyama
Kitabu cha Watoto

Our Heritage

Our Heritage
Children's Book

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

Perpetual Search

Perpetual Search

Africa's Best and Worst Presidents

Africa's Best and Worst Presidents

Psalm of the Oppressed

Psalm of the Oppressed
Psalm of the Oppressed

AFRICA REUNITE or PERISH

AFRICA REUNITE or PERISH
A new approach towards empowering Africa

BORN WITH VOICE

BORN WITH VOICE

Soul on Sale

Soul on Sale

Soul on Sale

Nyuma ya Pazia

Nyuma ya Pazia

We are one

We are one

SAA YA UKOMBOZI

SAA YA UKOMBOZI

Feel at home

You are always welcome to this epistle again and again time after time, ad infinitum.


Most read Posts

  • Sarkozy’s Take on African Fat Cats a Welcome Move
    At last the chicken are coming home to roost! French authorities made a groundbreaking decision by culling three most corrupt African presi...
  • Napanga kuanza kuuza mitumba na si maneno
    Ingawa mimi si mtumba, napanga kuuza mitumba. Nimechoshwa na jamii ya mitumba. Kila kitu mitumba. Mitumba, mitumba mitupu. Siasa za mitumba...
  • Better or Bitter Life for all?
    When I deeply muse on how an arrogant and brutal cabal of hoity toity (Coverted Con Men (CCM)) is tirelessly hoodwinking and dividing th...
  • Africa's Becoming more Despotic and Nepotistic
    "King of Kings" Gaddaffi The seven-day 40th anniversary of Libya strongman’s autocratic rule and charade elections in Gabon whe...
  • Kuna siku tutataifisha haya mahekalu haki ya nani
    Taarifa kuwa waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alinunua nyumba kwa zaidi ya shilingi bilioni moja licha ya kuwastua wananchi na...
  • Nyangumi mdogo akutwa amekufa ufukweni BC
    Hii ni picha iliyotolewa ya Nyangumi aina ya Humpback ambaye alikumbwa na maji na kutupwa kwenye ufukwe wa bahari ya Pasifiki kwenye eneo l...
  • Kikwete, Charity Begins at Home!
    President Jakaya Kikwete ...
  • Kweli binadamu si chochote wala lolote, wamkumbuka huyu?
    Walioko madarakani mkiabudiwa kama miungu au sanamu kumbukeni vijana hawa hata baba zao  ambao maiti zao zinaoza jangwani. Ungewaambia...
  • Pinda kulia hakutoshi, awajibike
    INGAWA kilio cha Waziri Mkuu, Mizengo Peter Kayanza Pinda, kinaonekana kuyeyusha hasira za Watanzania kwa muda, kuna haja ya kudodosa zaid...
  • Hawa si wachungaji bali ni fisi na mbwa mwitu
    KUMEZUKA mtindo mchafu na wa rejareja wa baadhi ya wachumia tumbo na matapeli kumtania hata kumtumia Mwenyezi Mungu kufanya utapeli na ujamb...

Followers

Blog Archive

  • ►  2023 (20)
    • ►  January (20)
  • ►  2022 (208)
    • ►  December (14)
    • ►  November (14)
    • ►  October (20)
    • ►  September (20)
    • ►  August (12)
    • ►  July (25)
    • ►  June (22)
    • ►  May (18)
    • ►  April (13)
    • ►  March (18)
    • ►  February (18)
    • ►  January (14)
  • ►  2021 (323)
    • ►  December (23)
    • ►  November (34)
    • ►  October (26)
    • ►  September (13)
    • ►  August (19)
    • ►  July (21)
    • ►  June (29)
    • ►  May (25)
    • ►  April (23)
    • ►  March (43)
    • ►  February (29)
    • ►  January (38)
  • ►  2020 (290)
    • ►  December (33)
    • ►  November (37)
    • ►  October (28)
    • ►  September (35)
    • ►  August (31)
    • ►  July (26)
    • ►  June (17)
    • ►  May (21)
    • ►  April (18)
    • ►  March (15)
    • ►  February (17)
    • ►  January (12)
  • ►  2019 (160)
    • ►  December (8)
    • ►  November (7)
    • ►  October (12)
    • ►  September (9)
    • ►  August (27)
    • ►  July (18)
    • ►  June (18)
    • ►  May (11)
    • ►  April (11)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (14)
  • ►  2018 (162)
    • ►  December (12)
    • ►  November (6)
    • ►  October (13)
    • ►  September (10)
    • ►  August (20)
    • ►  July (9)
    • ►  June (14)
    • ►  May (9)
    • ►  April (16)
    • ►  March (21)
    • ►  February (17)
    • ►  January (15)
  • ►  2017 (306)
    • ►  December (20)
    • ►  November (23)
    • ►  October (20)
    • ►  September (26)
    • ►  August (31)
    • ►  July (31)
    • ►  June (34)
    • ►  May (26)
    • ►  April (24)
    • ►  March (20)
    • ►  February (28)
    • ►  January (23)
  • ►  2016 (269)
    • ►  December (22)
    • ►  November (21)
    • ►  October (22)
    • ►  September (15)
    • ►  August (12)
    • ►  July (27)
    • ►  June (24)
    • ►  May (23)
    • ►  April (29)
    • ►  March (26)
    • ►  February (27)
    • ►  January (21)
  • ▼  2015 (399)
    • ►  December (34)
    • ►  November (24)
    • ▼  October (22)
      • Wadanganyika wote tumeshinda na tusherehekee basi
      • Zama Zile Muziki Ulikuwa Shule
      • UKAWA walaumu pupa, upogo, ubinafsi kushindwa vibaya
      • Wanaosaka Madaraka Waimbe wimbo Huu Wamalizie na T...
      • Kijiwe chatabiri ushindi kwa wadanganyika wote
      • I predicted UKAWA's defeat on August 23
      • Wakati nikingoja matokeo nilisikiliza muziki huu
      • Bootlicking is part of obedience in Kenya
      • Oct., 25th is the moment of truth
      • Ushauri kwa wapiga kura
      • Wimbo wa wiki
      • Kijiwe chahoji wanene kudedia ugabacholini
      • Huu mtambo kweli kweli
      • Je Amani ni pale Lowassa anapokuwa na tonge akinya...
      • Wasanii ni wakereketwa au njaa na upogo?
      • South African withdraw from ICC misguided
      • Kijiwe chamuomboleza Mtikila
      • Rais ajaye aepuke yafuatayo
      • As we celebrate Mtikila
      • Kijiwe chatuma wajumbe Bondeni kupinga ufisadi
      • Nitakavyomkumbuka Kikwete
      • Mlevi ampiga shule Fest Leidi
    • ►  September (34)
    • ►  August (29)
    • ►  July (37)
    • ►  June (22)
    • ►  May (32)
    • ►  April (35)
    • ►  March (46)
    • ►  February (47)
    • ►  January (37)
  • ►  2014 (502)
    • ►  December (47)
    • ►  November (49)
    • ►  October (47)
    • ►  September (37)
    • ►  August (40)
    • ►  July (42)
    • ►  June (30)
    • ►  May (35)
    • ►  April (47)
    • ►  March (44)
    • ►  February (39)
    • ►  January (45)
  • ►  2013 (400)
    • ►  December (37)
    • ►  November (27)
    • ►  October (31)
    • ►  September (26)
    • ►  August (34)
    • ►  July (39)
    • ►  June (28)
    • ►  May (40)
    • ►  April (44)
    • ►  March (39)
    • ►  February (26)
    • ►  January (29)
  • ►  2012 (598)
    • ►  December (27)
    • ►  November (26)
    • ►  October (27)
    • ►  September (30)
    • ►  August (47)
    • ►  July (95)
    • ►  June (86)
    • ►  May (119)
    • ►  April (83)
    • ►  March (23)
    • ►  February (17)
    • ►  January (18)
  • ►  2011 (261)
    • ►  December (20)
    • ►  November (19)
    • ►  October (20)
    • ►  September (21)
    • ►  August (27)
    • ►  July (12)
    • ►  June (15)
    • ►  May (20)
    • ►  April (27)
    • ►  March (32)
    • ►  February (24)
    • ►  January (24)
  • ►  2010 (205)
    • ►  December (25)
    • ►  November (23)
    • ►  October (23)
    • ►  September (23)
    • ►  August (17)
    • ►  July (13)
    • ►  June (12)
    • ►  May (10)
    • ►  April (18)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (16)
  • ►  2009 (163)
    • ►  December (19)
    • ►  November (14)
    • ►  October (11)
    • ►  September (6)
    • ►  August (12)
    • ►  July (9)
    • ►  June (11)
    • ►  May (20)
    • ►  April (22)
    • ►  March (14)
    • ►  February (12)
    • ►  January (13)
  • ►  2008 (191)
    • ►  December (12)
    • ►  November (11)
    • ►  October (14)
    • ►  September (15)
    • ►  August (16)
    • ►  July (23)
    • ►  June (10)
    • ►  May (19)
    • ►  April (16)
    • ►  March (19)
    • ►  February (17)
    • ►  January (19)
  • ►  2007 (33)
    • ►  December (13)
    • ►  November (20)

About Me

My photo
View my complete profile

Travel theme. Powered by Blogger.