The Chant of Savant

Sunday 31 July 2016

Happy Birthday Nkwazi Mhango Jr.



Jana ilikuwa siku ya kuzaliwa kwa kitindamimba wetu Nkwazi Mhango Jr katikati. Alitimiza miaka minne jana akiwa anajiandaa kuanza Kindergarten mwakani inshallah. Junior alijumuika na dada zake na kaka yake pamoja nasi. Zawadi yake kwa siku hiyo ilikuwa kumrusha kwa ndege kwa saa moja jambo ambalo huwa analipenda sana.

Je uraia wa nchi mbili ni kwa wageni tu Tanzania?


Japo watanzania wamekuwa na mawazo na misimamo tofauti kuhusiana na uraia wa nchi mbili, kitu kimoja kiko Dhahiri; sheria ya Tanzania hairuhusu raia yoyote wa Tanzania kuwa na uraia wa nchi mbili. Rais Magufuli–sawa na watanzania wengine analijua au anapaswa kulijua hili–hivyo alichosema si kuteleza kwa ulimi wala utani. Hata hivyo–hivi karibuni katazo hili la kisheria lilionekana kuwa la kibaguzi–tokana na ukweli uliofichuliwa na rais John Pombe Magufuli. Akimkaribisha mgeni wake waziri mkuu wa India Narendra Modi aliyetembelea Tanzania hivi karibuni, rais Magufuli alikaririwa na vyombo vya habari akisema, “Amejisikia [Modi] raha sana; alivyoona anakaribishwa na wananchi wengi wa Tanzania ambao naamini katika wale waliomkaribisha wengine ni miongoni mwao waliompigia kura kwenye jimbo lake.” Maneno haya yanajifafanua hasa ikizingatiwa kuwa kwanza, Modi si mtanzania–ni mhindi tena kiongozi wa nchi–hivyo, kwa sheria ya Tanzania, hawezi kuwa na wapiga kura. Pili, kwa mujibu wa rais, Modi–pamoja na sheria za Tanzania kukataza–anajua kuwa ana wapiga kura nchini hata kama ni kinyume cha sheria. Tokana na ithibati ya rais wetu ambaye mara nyingi amekaririwa akieleza wazi anavyochukia unafiki na uongo, aliyosema ni ya kweli tupu na si unafiki wala kufurahisha genge. Pia, tokana na ukweli huu na uzoefu wa watanzania walio wengi hasa wa mijini, unaweza kujenga mahitimisho na kugundua ni kwanini:
Kwanza, wengi wa mafisadi wakubwa wanaoshirikiana na mafisadi wakubwa wazawa serikalini ni wahindi.
Pili, wahindi wamekuwa wakiwabagua waafrika kwa miaka yote waliyokaa Tanzania bila kushughulikiwa kwa vile wana haki zaidi ya wazawa.  Hatutaki kutoa madai bila kutoa ushahidi. Kwa miaka zaidi ya mia waliyokaa Tanzania, nionyeshe ndoa hata tatu baina ya waswahili na wahindi nitaondoa hoja hii na kuomba msamaha. Najua ukweli huu ni mchungu. Lazima usemwe ili tuweze kusonga mbele kama taifa baada ya kujisuta na kusutana kama watanzania bila kujali rangi ya ngozi zetu. Isitoshe mie si wa kwanza kuliona hili. Marehemu Christopher Mtikila aliliona na kuliongelea sana na kwa undani bila woga wala unafiki. Nanachofanya hapa ni kukumbusha tu ili kuondoa kuendelea jinai ya ubaguzi.
Tatu, waziri mmoja wa uchumi wa zamani aliwahi kusema kuwa uchumi wa Tanzania ulikuwa–kipindi fulani–unashikiliwa na wahindi kumi tu. Hili ni kweli. Kwanza, wahusika hawakukanusha na ukweli unaonyesha hivyo.
Nne, matajiri wengi nchini ni wahindi hasa ukiangalia uwiano wa idadi ya watu. Kama hii haitoshi, wengi wa matajiri hawa wanaishi kwenye nyumba za msajili wa majumba kwa bei nafuu wakati wana mahekalu yao wakiyapangisha kwa dola au wana uwezo wa kujenga majumba yao wenyewe.
Tano, Tanzania imeruhusu jamii hii kuwa na shule, dini, na shughuli nyingine za kibaguzi za jamii moja ukiachia mbali kubariki mfumo wao wa kikaburu wa kitabaka (caste system) ambao licha ya kuwa wa kibaguzi ni kinyume cha sheria na haki za binadamu.
Sita, rais alisema kuwa Bunge la Tanzania lina wabunge kumi wenye asili ya kihindi, jamii ambayo hivi karibuni imesifika kwenye vyombo vya kimataifa kwa kuwabagua waafrika ikiwaita nyani au absii, bander au kalu. Rejea kupigwa na kudhalilishwa vibaya kwa mwanafunzi wa kitanzania nchini aliyekuwa akisoma kwenye Chuo Kikuu cha Acharya, Bangalore, India hivi karibuni baada ya msudani mmoja kusababisha ajali ya barabarani bila kutaja mwanafunzi toka DRC Masunda Kitada Oliver aliyeuawa May kwa kugombea Bajaj.
Kweli usilojua ni usiku wa kiza. Sijui kama waswahili wangekuwa huko ugabacholini wangepewa hata ujumbe wa nyumba kumi chini ya mfumo wa kikaburu wa caste system. Ni bahati mbaya kuwa waswahili walifundishwa kujikana na kuwapapatikia wageni kiasi cha kuwa na methali isemayo mgeni karibu mwenyeji apone kuonyesha utegemezi na kutojiamini kwao. Walevi wana shaka na huu ushuhuba wa ajabu ajabu ambao haulengi kutatua matatizo kama vile utoroshaji raslimali zao, ubaguzi wa moja kwa moja tena wa muda mrefu na madudu mengine mengi ambayo tawala karibia zote zimekuwa zijifanya haziyaoni. Wenzetu husema charity begins at home, au hisani huanzia nyumbani.
Tumalizie hapa kwa kumtaka rais Magufuli na serikali yake ima kuruhusu uraia pacha au kuupiga marufuku kwa watanzania wote badala ya kubagua hata kusifia ubaguzi huu. Sheria ni msumemo kama ambavyo rais Magufuli hupenda kusema; haipaswi kubagua wala kupendelea, kutumika kibaguzi au kuwa utashi wa mtu, kikundi cha watu wala taasisi bali utashi wa sheria. Ni aibu kugundua kuwa taifa huru linaweza kuwanyima raia wake wazalendo na kuwaruhusu raia wa kigeni wautumie kuliibia. Je yote haya yanafanyika hivi kwa faida ya nani? Sijui kama India inaweza kuruhusu ujinga kama huu tena kwa waafrika ambao wanasifika kwa wanavyobaguliwa nchini India hata kwenye bara lao wenyewe kutokana na kuwa na uongozi wa kifisadi na usiojithamin kukosa uzalendo na kujiamini.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili.

Mlevi atamani kufanya biashara na NSSF


            Kwanza, nimpongeze rafiki, kaka yangu na msomaji wangu rahis Joni Kanywaji Makufuli kwa kuwatumbua walaji wa Shirika la Utafunaji wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii au Nominal Social Syndicate of Fraudsters (NSSF) baada ya jamaa kula kwa mikono na miguu tena bila kunawa. Nampongeza kwa kupewa rungu na nambari wani kuwatumbua majipu yote hata kama ni yale yaliyomkabidhi rungu lenyewe. Nasema bila kumung’unya “Tumbua Kaka.” Nashauri hata kauli mbiu yako ibadilishwe na kuwa “Hapa Kazi na Kutumbua Tu” au siyo? Ila katika kutumbuatumbua angalia usinitumbue mimi. Ukifanya hivyo utakosa ushauri na inshu. Hivyo, nakupa greenlight utumbue kila jipu isipokuwa mimi ambaye ujipu wangu ni wa kupiga mma na kuchoma jani. Pia naomba unikumbuke kama Lyatongolwa  najikomba kwako ding.
Baada ya kumpongeze mnene kupewa rungu ambalo–sina shaka–atalitumia bila huba, upendeleo wala uonevu kuwashughulikia walogeuza kaya shamba la chizi chini ya Jk, sorry, Njaa Kaya.
Hivi karibuni aliwatumbua vigogo wa NSSF tokana na ujinga na uroho ambao hata fisi–pamoja na uroho wa kupindukia–kusema ukweli, hana.  Mnakula hata nyayo wanahizaya nyie msie na aibu wala adabu! Shame on you! Sasa mtakoma na kukomaa. Hapa lazima Dokta Kanywaji afe na gendaeka. Hivi kweli unaweza kuamini; kiwanja kilichopaswa kununuliwa kwa madafu bilioni moja na nusu kilinunuliwa kwa madafu bilioni 15? Ukisikia kiwanja chenyewe unatamani ukamate gendaeka uwafanyie kitu mbaya. Hebu fikiria. Kiwanja Bongo, tena madongo kuinama, kinapunyua madafu bilioni zaidi ya 15 za walevi wanaonuka umaskini wa kutengenezewa na watawala washenzi na wapuuzi kama tulivyowashuhudia hivi karibuni Dk Kanywaji akiwananga kuwa waliachia kaya ikaliwa kama haina mwenyewe. Wakati mwingine unashindwa kuielewa miswahili.  Mijitu inakula hadi mapembe na kwato? Mbona hata Tokyo–kule Ujep na New York kwa Joji Kichaka na Obamiza–ambako viwanja ni aghali kuliko vyote duniani bei haijafika huko? Unashangaa kusikia eti hawa nao eti ni wasomi kweli? Tokana na sakata hili, Mlevi apanga kuonana na rahis Dk Kanywaji–si kujikomba kama Lyatongolwa–kumtaka abatilishe uteuzi wa aliyekuwa bosi wa wizi huu wa mchana aliyemteua balozi. Huyu alipaswa kuwa Keko lakini si zaidi. Anapewa ubalozi wa nini wakati mchezo wake mchafu ndiyo umefumka? Au Dk Kanywaji alipompa ubalozi alikuwa hajapata hili jipu alilotumbua hivi karibuni? Nalo hili nikipata appointment naye nitalipenyeza ili jamaa aende zake lupango akajiunge na wenzake.
Pia, nitamuomba Makufuli ima aniteue kuwa mnunuzi wa mali za NSSF; au niwe muuzaji kwake ili nichanganye njuluku hasa kutokana na kugundua kuwa kumbe kuna fursa za kutengeneza ukwasi kama sina akili nzuri.  Hapa uhitaji kutumia akili. Kinachotakiwa ni kutembeza hongo.  Kwa vile mimi ni msomi wa kweli na mzalendo tena muaminifu, nitakula kidogo na kubakiza kikubwa tofauti na hawa waliokuwa wakiiba kikubwa na kidogo ukiachia mbali kupokea chochote kile katika ujambazi huu wa mchana.
Kwa vile wizi wa mabilioni na matrilioni umezidi kayani, nitamshauri Dk Kanywaji afanye utaratibu wa kupeleka mswaada bungeni wa kuhakikisha wanaokwapua mabilioni na matrilioni wananyongwa sawa na majambazi wa kawaida.  Pia, nitashauri wahakikishe wahusika wakimatwa wasihukumiwe kifo chapchap. Waachwe; kwanza wasote lupango ili ndugu zao wawaletee habari chafu na chungu za washirika zao wa bedroom kuwa na washikaji wapya wa kuwadoadoa. Kwanini wasipate habari chafu wakati wao wameumiza walevi wengi kwa kuhomola njuluku zao?  Lazima hapa wafanyiwe kama akina Hasi Kitiliya, Sirori na Sinari. Unadhani washirika zao huko nje wako salama?  Bahati yao, niko mbali nao, nami ningetia timu kuwabugulia mali zao kama walivyobungua mali zetu. Tena, nilivyokuwa mnoma, usishangae wengine nengewaachia mbegu za walevi kwenye uzao wao ili wanikumbuke milele. Japo si vizuri kumuombea mja maafa, wahanga wa ushenzi huu wanaomba hawa jamaa wanyotoke roho haraka kama lile jambazi la Banki Kuu lililozikwa hivi karibuni kule Moro. Siku hiyo walevi tulikunywa na kuvuta kama hatuna akili nzuri.
Katika kuhakikisha njuluku za walevi hazipotei, napanga kumshauri Makufuli akamate mali za wahusika haraka kabla hazijatobolewa tobolewa na washirika wao. Pia, ahakikishe yule aliyeuza kiwanja kwa mabilioni haya naye anaunganishwa haraka kabla hajatorokea ughaibuni kama ilivyo fasheni ya baadhi ya washirika wa jinai hii hasa wenye uraia wa kaya nyingi.
Pia nitamshauri Dk Kanywaji kuchunguza gharama za ujenzi wa Daraja la Mzee Mchonga pale Kigamboni. Maana, kama wezi hawa wameweza kupaisha bei ya kiwanja, hilo daraja itakuwaje? Kwanza, mwenzenu nilishaapa kuwa sitakaa nipite kwenye daraja hilo kuelekea Mji Mwema. Kwa vile hii ni kaya ya kitu kikubwa na kidogo, nina wasi wasi limejengwa chini ya kiwango kama mighorofa mingi ya Bongo inayongoja kunyotoa walevi roho kama ule wa Uhindini.
Ama kweli Njaa Kaya alijua kututenda! Ajabu eti bado anakingiwa kifua. Achia rungu la ukiti utumbuliwe na wenzako. We ngojeni. Hawa wa NSSF walie tu. Lazima walipe;maana kula na kulipa ndiyo mwendo wa usawa huu.
Chanzo: Nipashe Jumamosi

Thursday 28 July 2016

Kijiwe champongeza Dk Kanwyaji


          Baada ya Dokta Joni Kanywaji Makomeo kupewa rungu la pili ili atumie kutumbua majipu, Kijiwe kinampongeza na kumtega. Kwani, sasa wachovu wanategemea kuona akifanya vitu vyake bila ya woga wowote hasa ikizingatiwa kuwa ana marungu yote.
Mpemba anaingia akiwa amevalia kofia yake nzuri ya tarabushi na kuamkua na kusema, “Yakhe mlokuwa mkisema sana kuhusiana na rahis Dokta Joni Kanywaji Makomeo sasa jiandaeni kusuka au kunyolewa tena bila maji.”
Mheshimiwa Bwege anamchomekea, “Yakhe wamaanisha nini? Unadhani kuna mabadiliko hapa au yale yale ya CcM?”
Mpemba anajibu, “Unakuwa kama wewe si mtu wa pwani? Kwani mie namaanisha nini? Basi ngoja nrudie. Nasema, mlokuwa mkisema sana sasa ntihani kwenu. Ombeni Subhanna huyu jamaa afanye kweli. Lakini asipofanya kweli mtaumbuka kweli kweli kiasi cha kuonekana kama mwalimwa mwajiona.”
Mgosi Makamba anakula mic, “Sisi tinampongeza dokta Kanywaji; pia tinamuombea afanye  kwei ii asijeonekana kanyabwoya kama siyo sanaa na kamba. Maana, sisi tiiofuatiia nchakato nzima tinaona kama kuna namna hasa tikikumbuka  waiovyosifiana.”
Mipawa anakula mic, “Kumbe nawe umeiona namna alivyowasifia wale anaowatuhumu kuwauza wachovu tokana na uzembe wao? Hata mie hapa nashangaa kiasi cha kuanza kuona kama usanii mwingine.”
Kapende, “Ulitegemea nini? Kwani hujui kuwa kambare wote wana sharubu au unadhani watabadilika usawa huu? Nasema wazi wazi tena kwa kinywa kipana; wanaotegemea mabadiliko basi walie tu. Kama yapo ni yale ya kutumbua vidagaa na kulala kitanda kimoja na nyangumi. Jiulize ni kwanini kushitaki mafisadi imekuwa kama aina fulani ya picha.  Mie kusema ukweli sitegemei lolote jipya zaidi ya kuwekana sawa na kufungana kamba kama kawa. Dk Kanywaji akitaka kunishawishi awakamate waliogeuza kaya yetu shamba la chizi.”
“Kaka hapo umetoboa. Hata mie atanitosheleza kama atakamata mafisadi bila kubagua. Nashangaa madudu kama Escrow, EPA, kuficha njuluku ughaibuni hayaguswi. Huoni hata mafisadi wa sukari wamemalizana naye; na sasa wanapeta? Unacheza na Danganyika nini?” anasema da Sofia Lion aka Kanungaembe.
Mbwamwitu ansema, “Da Sofi acha nikuchomekee. Unasema atakutosheleza kama atafanya nini?”
Sofia anajibu, “Wewe unaonaje kama swali hili angeulizwa mama yako? Wenzako wako seriously wewe unaleta utani hapa!  Acheni kucheza makidamakida kama Lyatongolwa Mlemavu aliyekwenda Idodomya kujikomba na kujivua nguo kwa sababu ya tonge la ugali.”
Mijjinga anatia guu, “Usinikumbushe huyu meku ambaye anaonekana hakuumbwa na aibu hata chembe hasa anapobanwa na njaa. Yote tisa, sikujua kuwa kumbe kile kizee cha kigosi bado kipo. Kijamaa kwa kamba. Eti kiliingia na gea ya uhubiri wakati nacho ni yale yale kutafuta ulaji wa dezo. Hakuna kiliponiudhi kama kuwasifia Njaa Kaya na Denjaman wakati waliuza kaya yetu.”
Mzee Maneno anakwanyua mic, “Unashangaa hiki kizee cha mikamba siyo! Ulitegemea kiseme nini wakati huu ambapo mtandao wao wa wizi uko hatarini chini ya Dokta Kanywaji? Pamoja na uhovyo wake, kilinifurahisha kilipomtolea uvivu mchunaji Jose Gwaijumaa aliyejitiatia kumkana Eddy Ewassa akidhani atawaingiza mkenge magamba asijue nao ni kama yeye ni wapigaji na wasanii wazoefu.”
Msomi aliyekuwa akibukua jarida moja la kimataifa akionyesha wazi kutokuwa na hamu na mjadala anaamua kuchomekea, “Hivi kamandoo wa Zenj yuko wapi;maana sikumtia machoni.”
Mpemba anajibu, “Unaulizia shuka matangani. Alikuwa kamandoo zama zile akiua wapemba. Baada ya Nyazi Mungu kuntia laana untegemeani?”
Kanji naye anachomekea, “Veve Somi iko fanya juri sana dugu yangu. Hata mimi iko wazi iko wapi ile kamandoo natingisa sana zama ile.”
Msomi anaamua kuigia jumla, “Nimesikiliza pwenti zenu nyote. Wapo wanaotegemea kuwa Dokta Kanywaji atatumia marungu yake kuwaponga kila nyani wanao na waliohujumu kaya. Mwenzenu nachelea kuamini hivyo hasa nikizingatia kuwa jamaa ni mwanasiasa. Pili, kwa alivyowamwagia ujiko wahujumu viongozi wa kaya hii, sitegemei lolote wala muujiza. Nashangaa amekuwa akilalamika kuwa kaya yetu ililiwa jambo ambalo ni kweli. Je ililiwa chini ya nani kama si hao anaowasifia kwa kumuumba na kumfundisha mengi? Nadhani–kwanza sitaki nionekana nawanga–tutarajie kipindi cha kushangaza ambapo mambo yatakuwa yakienda kutegemea anayeshughulikiwa ni nani. Sitaki kujipa matumaini yasiyokuwepo hasa nikijua namna wanasiasa wetu walivyo. Nadhani lao laweza kuwa moja hasa usawa huu ambapo siasa ni sehemu ya kutengenezea utajiri wa haraka hata kama ni mchafu.”
Anapiga chafya na kuendelea, “Japo namuaminia Dokta Kanywaji, napata shaka japo bado nakuwa na matumaini kuwa mara nyingine siasa za majukwaani huwa ni za kupakana mafuta kwa mgogo wa chupa; hivyo, lolote lawezekana.”
Mgosi Machungi anadandia, “Hapa timekueewa. Nikikumbua aivyomifukuza Ombeeni Sifuwi, naweza kusema loote laweza kutokea kwa Dokta Kanywaji. Hivyo, timpe moyo asiangalie nyani au tumbii usoni atakapoanza kutumia maungu haya aiyopewa juzi.”
Mchunguliaji naye anaamua kuzoza. “Hapo kaka nimekupata tena vizuri sana.”
Kabla ya kuendelea Mgosi anaamua kutaka kumkwida.
Kijiwe kikiwa kinanoga si akapita manzi chuma kweli kiasi cha kutufanya wote tumkatie shingo!
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano.

Sunday 24 July 2016

Makonda upangaji Nyumba za Msajili ni jipu lako


Baada ya kuondoa ombaomba, kutangaza kiama cha mashoga, mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda anakabiliwa na kibarua kingine ambacho kitapima sincerity na ithibati yake kama kiongozi wa umma. Sina shaka na uongozi wa Makonda japo mwanzoni nilikuwa na shaka naye hasa kutokana na siasa za ndani ya chama chake–hasa pale alipodaiwa kutaka kumdhalilisha waziri mkuu wa zamani Joseph Wairoba–jambo ambalo alilikanusha kwa umahiri zaidi ukiachia mbali Warioba kutolalamika binafsi.
Leo tunampa changamoto nyingine kubwa ambay–japo wengi hawapendi kuigusia –ipo na imekuwapo kwa muda mrefu. Sijui kama Makonda alishawahi kujiuliza sababu na mantiki ya jamii moja ya kiasia tena si kiasia tu bali ya kihindi kukalia karibu majengo yote ya Msajili wa Majumba ya katikati ya jiji?
Licha ya kuwa ubaguzi wa wazi wazi, kuna kila harufu ya rushwa kuhusu upatikanaji wa upangaji wa nyumba hizi ambazo–licha kuwa za bei nafuu–hazionyeshi sura ya Tanzania.
Ukiachia hayo hapo juu, kuna uwezekano wa kuwapo kwa jinai zinazoendelea ambazo zinatokana na makazi ya kibaguzi kama vile, kuficha wahamiaji haramu ambao ni wakimbizi wa kiuchumi waliojazana nchini wakiishi kinyume cha sheria ukiachia mbali kuchukua ajira na kufanya shughuli ambazo watanzania wanaweza kuzifanya.
Rejea kuwahi kufichuliwa magenge ya wasafirishaji binadamu ambapo wasichana wa kihindi walikuwa wakiletwa nchini kufanya umalaya kwa kisingizio cha kutoa burdani. Rejea tukio la mwaka jana ambapo wanaodhaniwa kuwa ni vyangudoa 22 toka nchini Nepal waliokuwa wameiingizwa nchini na kampuni ya Dhamaka Entertainment Center Limited walivyokamatwa.
Kama tutakuwa makini na wakweli, wakimbizi wa kiuchumi ni hatari kwa taifa letu kuliko ombaomba na mashoga ambao mara nyingi mambo yao ni suala la mtu binafsi na si mtandao mkubwa unaohusisha mataifa yenye watu wengi maskini na wasio na kazi wanaotumia ngozi yao kuhujumu taifa letu. Pia Makonda anapaswa kupambana na mitandao ya wazawa inayoshirikiana na wageni hawa kuhujumu taifa. Kukaa mahali popote nchini ni haki ya kila mtanzania. Inapokuja kufaidi matunda ya nyumba za umma kama vile za Msajili wa Majumba, lazima lisiwe suala la kuchagua bali kufuata sheria inayoakisi usawa wa watanzania. Bila rushwa wala ubaguzi, haiwezekani watu wa tabaka moja waishi sehemu yao maalumu halafu wawadanganye wanaowabagua kuwa wako sawa. Usawa gani huu wa bata na kuku?
Naamini Makonda amesoma historia ya ujio wa wahindi ambao waliletwa na wakoloni ili kujenga reli na baadaye wakawatumia kama watu kati wa kununua mazao ya waafrika ili kuwanyonya na kuwafanya wawe maskini ili iwe rahisi kuwatawala kwa lengo na kuwanyonya milele. Ni bahati mbaya, baada ya kupata uhuru–tokana na huruma ya baba wa taifa, mwl, Julius Nyerere aliyechukia ubaguzi–aliwaruhusu jamaa hawa waliokuwa wakihujumu uhuru wetu wazi wazi kuwa raia wa taifa jipya la Tanganyika.
Wakati wa viongozi wetu kuangalia mambo kama yalivyo ni sasa ambapo wenye uwezo waamriwe kujenga nyumba zao binafsi ili kuwapisha wasio na uwezo kutumia nyumba husika. nyumba hizi, kwanza, ni za umma; na ni alama ya uhuru wetu. Je watu wetu maskini –hasa wafanyakazi wa serikali –wataendeleaje kunyanyasika kwenye nyumba binafsi za kupanga wakati nyumba zao zinakaliwa na matajiri wenye mahekalu wanayopangisha kwa fedha za kigeni? Kama haitoshi, mfumo wetu, umeruhusu tabaka moja la wachache kutajirika wakati umma ukiendelea kuteseka kwenye umaskini. Makonda anapaswa kuanzia hapa. Na hili haliwezi kuonekana kama ubaguzi. Kwanini wao kukalia nyumba za umma tena kama tabaka moja halionekani kuwa ubaguzi wa wazi wa kiuchumi na kijamii?
Kwa wanaokumbuka huu ubaguzi wa wazi ulivyokuwa umehalalishwa, watakambuka namna marehemu Christopher Mtikila alivyoushughulikia hadi kuupunguza kidogo tena kwa muda. Kwa watu wa kizazi cha kuanzia miaka 50 kwenda juu waliokulia kwenye jiji la Dar Es Salaam, watakumbuka ambavyo wahindi–ambao Mtikila aliwaita magabacholi tokana na neno chori au mwizi ambalo walilitumia kuwaeleza waswahili kama wezi–walikuwa hata hawapandi dala dala wala kuchanganyikana na waswahili ukiachia mbali kuwatumia kama watumishi wa madukani na majumbani na walinzi wao.
Japo tunajua kuwa jamaa hawa wanatokana na mfumo mbovu wa kikaburu wa caste system, waliruhusiwa kuendelea na ubaguzi wa wazi wazi. Kama tulivyosema hapo juu, wakati wa kubomoa mfumo huu kimfumo ni sasa ambapo serikali yetu inapaswa kutangaza wazi wazi isivyoridhishwa wala kukubali jinai hii ya wazi.
Tumalizie kwa kumtaka mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam –ambaye ameonyesha kuwa na nia ya kuwakomboa wanyonge–aanze kubomoa mfumo huu wa kibaguzi mkoani mwake–kwa kuanza na nyumba za Msajili wa Majumba. Lazima nyumba hizi zionyeshe sura ya Tanzania na si ya India wala utajiri. Miaka zaidi ya 50 tabaka moja limefaidi nyumba za Msajili itoshe. Tutunge utaratibu wa kuzuia ubangishanaji wa kifisadi ambao umefanikisha na kuhimiri mfumo huu wa kibaguzi.
Tanzania Daima Jumapili.

Saturday 23 July 2016

Makufuli tumbua wachunaji

Image result for photo of gwajima na helkopta
            Juzi nilisika saka saka ya mchunaji mmoja anayejiita mchungaji akiihangaisha sirikali. Wabongo kwa kukuza mambo, hakuna mfano. Kwani, mchunaji mwenyewe punde si punde si alijitokeza. Wacha ndata wamzukie waishie kumgwaya. Kwani, tumepashwa kuwa alikwenda pale kituoni kama mtu anayekwenda mgahawani kupata chai na kuishia zake kwenye hekalu lake ambalo nalo hatujui alivyolijenga. Kwa kazi gani au ni kwa kutumia sadaka?
Huyu jamaa ambaye alijizolea umaarufu baada ya kumpa tafu Eddie Luwasha kwenye uchakachuaji uliopita ameniacha hoi baada ya kumkana na kujifanya anamzimii dokta Joni Kanywaji Makufuli. Ya kweli haya au ni janja ya kusaka ulaji ukiachia mbali kuogopa asitumbuliwe usawa huu anapomilki chopa bila kueleza wala kuonyesha alivyochanganya njuluku hadi akawa bonge la mkwasi ghafla bi vu? Kwa jeuri aliyoonyesha si haba. Who knows. Huyenda naye ana sirikali yake yenye siri kali kubwa kiasi cha ndata kumgwaya. Au ni kwa vile amejitoa kwenye upingani; hivyo, matamshi na tabia zake havihatarishi amani ya walaji wakubwa kayani? Bahati yake, angekuwa bado kitanda kimoja na Ewassa huenda hata hiyo chopa na hekalu vingekuwa vimeishanyakwa baada ya kutumbuliwa.
Ngoja niulize kibangibangi na kigongongo. Je huyu jamaa huwa anafanya kazi gani zaidi ya uchunaji? Hata hivyo sishangai. Baada ya neno la Bwana kugeuka bidhaa adimu ambayo kila tapeli anaweza kutumia kuukata, who knows hata kama uchunaji ni joho tu la kufichia biashara nyingine kubwa? Huoni wanavyoibuka wachunaji kila uchao hadi wengine kumuingiza nkenge Dokta Kanywaji hadi akawazukia kwenye maduka yao? Juzi nilinusurika kuzimia baada ya kusikia wachunaji wengine eti wakiandaa mkutano mkubwa wa kuombea kaya kana kwamba kaya inahitaji kuombewa badala ya kuambiwa ukweli kuwa ni shamba la bibi na kichwa cha mwendawazimu cha mzee Ruxa tulichokiona wakati wa Njaa Kaya na genge lake la ulaji na uzururaji. Tumekuwa na wanene wabovu kiasi cha kufuga mijizi ambapo kaya ilikuwa kwenye outpilot kila mchovu akijifanyia atakavyo. Hata hivyo, chini ya rahis Kanywaji, nina imani mambo yatabadilika kama hawatambadilisha kabla hajawabadilikia na kuwabadilisha.
Siku hizi si ajabu kuona wachunaji wakipanda mingoma mizito na kuishi kwenye mahekalu wakati yule bwana mkubwa wanayemhubiri alikuwa apeche alolo akiombaomba. Rejea Kaisari alipomtakisha kodi. Si alikuwa amewaka kiasi cha kuikopa njuluku kwa samaki? Sasa hawa wachunaji wanapata wapi hii ya kuwa matajiri wakati Yesu mwenyewe alisema kuwa ni heri ngamia kupita tundu la sindano kuliko wakwasi kuingia kwenye ufalme wa God? Msiseme nazusha. Hamuwaoni walivyo na mimali lukuki isiyo na maelezo?
 Linapokuja suala la watu kuwafisidi na kuwaibia wachovu, kaya yetu inaweza kuwa kinara. Hata hivyo, bwana mkubwa aliwahi kusema, “Macho wanayo. Lakini hawaoni. Masikio wanayo. Lakini hawasikii.Wengi wa wachunaji hata ukiona sura zao ni wababaishaji wa kawaida tu waliojificha nyuma ya majoho na madhabahu wakinajisi na kuibia wachovu wa God. Kwanini wachovu wanashindwa kuelewa kitu simpo kuwa; huwezi kutumikia mabwana wawili yaani bwana God na ukwasi ukauona ufalme wake. Kinachowapa ulaji ni ile hali ya wachovu na walevi kumsahau baba yao Kibwetere aliyewabwetere kondoo kwa kuwatia nari na kuondoka na mali zao. Japo nisemayo ni ya kilevi na bangi, sitashangaa kusikia Kibwetere mwingine akiibukia Bongo muda si mrefu. Chukulieni hili kwa makini. Kwani ni utabiri swaafi wa nabii wa walevi.
Wengi wamefikia hata kujiita mitume na manabii wakati ni mitumba na majangili. Hivi anaweza kupatikana mtume au nabii usawa huu kwenye dunia ya walafi na mafisi na mafisadi ambapo mali imechukua nafasi ya God siyo? Mara hii mmesahau aliyenaswa na nyara za umma akijifanya mchungaji wakati ni jangili. Ni manaigeria mangapi walishanaswa na bwibwi huku wakiwa wamevalia kama wachungaji wakati ni wachunaji na wasafirisha bwibwi? Wengine wanajiita watu wa Mungu wakati ni watu wa unga. Ukiangalia biashara fichi ya wachunaji, mbali na wengine kutumia misamaha ya kodi kuingiza bidhaa za wafanyabiashara wezi, kuna kila sababu ya kuamini wana biashara nyingi haramu nyuma ya pazia. Hapa hujagusia michango wanayowatwisha mbumbumbu wengi wenye matatizo na wizi wa sadaka.
Hata hivyo, hawa wachovu wajinga na wapumbavu wana bahati. Kama si mlevi kuwa mcha God, angeweza kuanzisha dhehebu lake la Ufufuko na Utajirisho ili awaibie mchana kweupe kama wanavyofanyiwa na matapeli tena wengi ambao hawakupiga buku kama mimi. Kwa elimu yangu ya saikolojia–kama ningeamua kuwaibia ningekuwa tajiri–kutokana na kuwachezea kisaikoloji. Jitu linatoa mimba linaishia kushindwa kupata mtoto eti linakwenda kuombewa baada ya kutapeliwa na waganga wa kienyeji wanaoishia kulibaka. Kama haitoshi, jingine linaolewa na kushindwa kutunza ndoa yake. Mambo yakiharibika linakimbilia kwa wachunaji. Kimsingi, kinachoendelea kayan–licha ya kuwa ushirikina na wizi wa mchana–ni zao la kukosa kujiamini na kukabili matatizo kama yalivyo. Kimsingi, wachunaji na waganga wa kienyeji tofauti yao ni majina. Sitashangaa siku moja–baada ya kuzoea kuona wachunaji wakibambwa na bwibwi–kusikia kuna wachunaji wamenaswa na viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi. Anyways guys, msinichukulie seriously kwa vile nimeutwika leo. Muhimu, Makufuli anapaswa kuwatumbua hata wachunaji.
Chanzo: Nipashe Jumamosi.

Tuesday 19 July 2016

Kijiwe chastukia uraia pacha wa Kanji

Image result for photos of narendra modi and magufuli
            Baada ya rais Joni Kanywaji Makufuli kufichua siri kuwa Bongo ina wapiga kura wa India, kijiwe kimembana Kanji aeleze kama naye yumo na yuko wapi kati ya Bongo na India.
Mheshimiwa Bwege ndiye anaanzisha mada. Baada ya kumuamkua Kanji na kumpa ofa ya kahawa anasema, “Kanji dugu yangu, iko sikia kuwa veve iko piga kura ya kula kule Indiani. Je hii iko kweli au ongo na veve iko sema nini dugu yangu?”
Msomi Mkatatamaa anadakia, “Hata mimi hili la mkuu kutoboa ukweli huu–ambao hata hivyo, si mpya–lilinistua na kunishangaza; hasa kugundua alivyoridhika nalo badala ya kutamka wazi kuwa ni kinyume cha sheria. Nadhani mkuu anapaswa kuambiwa kuwa anachofanya si kusifia ujinga na ubaguzi kama huu bali kupambana nao kwa vile nalo ni jipu tena la muda mrefu. Inakuwaje waswahili wazuiwe uraia wa nchi mbili nyinyi akina Kanji mruhusiwe? Hivi Mkuu hajui kuwa hiki ndicho chanzo cha kutorosha njuluku na mali za kaya? Nadhani Kanji anaweza kutupa jibu sahihi wakati tukingoja la mkuu mwenyewe.”
Kanji anajitetea, “Veve onea mimi bure dugu yangu. Veve wahi ona gabacholi nakuja kunywa gahawa hapa na veve? Mimi haiko gabacholi; iko hindi sikini nishi na Swahili sikini. Ile gabacholi tajir nabagua hata mimi hata kama haibagui kama nafanya veve Swahili. Kwanini veve lau hindi. Kwani hindi diyo naunda serikalini yenu?”
Mgosi Machungi anakamua mic, “Hata sisi imetishangaza kusikia kuwa kumbe kuna Wadanganyika wanaopiga kua huko ugabachoini. Sijui kwanini wanatinyima sisi hii haki na kuwapa wageni wasio na uchungu na kaya yetu? Hapa azima mkuu atieeze hadi ti-understand na ku-compuihend.” Anamegeukia Kanji na kusema, “Hata veve Kanji iko gabachoi. Huoni unavyosema seikai yenu na siyo seikai yetu? Hii maana yake ni kwamba veve haiko raia ya kaya hii. Hii nayo baguzi kuba ndugu yangu Kanji.”
Mipawa anampoka Mgosi mic, “Mwenzenu sikushangaa; hasa nikizingatia namna jamaa hawa ambavyo wamekuwa wakishirikiana na mafisadi wazawa kusikinisha kaya. Mara hii mmesahau namna majambazi kama Chavda, Saileth Vithlani na magacholi wengine walivyoibia kaya wakaishia kuondoka kayani kwenda kutanua ulaya?”
Kabla ya kuendelea, Mchunguliaji anamchomekea Mipawa na kusema, “Mbona Chavda alisharudi na anapiga mbonji mitaa ya Upanga au hujui. Hii Bongolalaland aka Danganyika bana. Waliwadanganya kuwa Chavda alikimbia kaya wakati yuko Upanga akihomola na kula kuku kama hana akili nzuri. Jiulize, yale mashamba ya mkonge waliyosema alitumia kuibia mbona hayajawahi twaliwa kama kweli aliondoka kayani?”
Mipawa anaendelea, “Hilo nililisikia na lisirikali halikuwa tayari kukanusha au kutoa maelezo. Hata hivyo, silaumu; kwani, wakati wa utawala wa Njaa Kaya, nani angepoteza muda kutoa maelezo? Nadhani lao moja na wao ni dugu moja kwenye kuibia kaya shamba la bibi au siyo?”
Leo ni kuchomekeana mtindo mmoja mmoja. Mpemba anakwanyua mic, “Yakhe hata mie sikushangaa. Nyie mwaongelea akina Chavda, Kagoda na wale wenginewe wa zamani. Mbona yupo huyu Kamran Ahmed aliyetoroshwa wanyama hai zaidi ya mia jana tu naye alitolewa rumande na kupewa pasipoti na pipa akaondoka zake na kaya ikaishia kula hasara? Hawa ndiyo magabacholi alioonya marehemu Chris Mtikisa. Na sasa ameondolewa, sijui nani atawatia kashkash wabaguzi hawa wa kunuka?”
Mijjinga naye anaamua kukamua mic, “Mkuu hakukosea. Huenda ulimi uliteleza au alitaka kuanzisha mjadala kama huu ili asionekane kalianzisha yeye.  Mimi sikushangaa hili la uraia wa kaya nyingi. Nadhani mnapaswa kuelewa kuwa kaya hii ina sheria moja inayotumika tofauti kwa kuangalia rangi na ukwasi wa mhusika. Ukiwa kigogo kama Jimmy Rugemalayer, Singasinga, Andi Chenga au Ni Zero Kadamage unaengwa wakati wezi wa kuku wakisulubiwa kwa uvivu wao wa kufikiri wakaiba kuku badala ya maburungutu.”
Sofia Lion aka Kanungaembe anakula mic, “Usemayo kaka Mijjinga ni kweli tupu. Huoni wanavyofaidi nyumba za Msajili wa Majumba wakiitana kila uchao wakati waswahili wakiendelea kunyanyaswa kwenye mbavu za mbwa za kupanga au kuangamia mabondeni wakati nyumba zinazoitwa zao zikikaliwa na wapiga kura wa India? Nani anashupalia hili jambo ambalo ni ubaguzi wa wazi?”
Kapende anakula mic, “Nadhani tunapaswa kupigania uhuru upya ili tujenge kaya isiyo ya kibaguzi na kigabacholi.sijui kama waswahili wangekuwa ndiyo wanaishi ugabacholini kama wangepewa upendeleo kama huu. Kama kaya, tunapaswa kuwatoza kodi kubwa–kwa vile ni matajiri–ili kuweza kujenga nyumba nyingine kwa ajili ya walalahoi wetu walionyonywa tangu ukoloni hadi sasa. Hapa hakuna cha nini wala nini bali kutendeana haki na kuuangalia ukweli kama ulivyo hata kama ukweli wenyewe ni mchungu. Mnasemaje wazee?”
Kijiwe kikiwa kinango si akapita manzi wa kigabacholi! Wacha Mbwamwitu ajisemee, “Kusingekuwa na ubaguzi huu wa ki-caste, huenda huyu manzi angekuwa bi mkubwa wangu.”
Kanji anajibu, “Dini yetu haikoruhusu Swahili oa hindi.”
Wanakijiwa tunageuka na kuangaliana kugundua kuwa jasiri haachi asili. Kwa pamoja, tulipanga kwenda kukuu kuamuru lisirikali lianze kushughulikia ubaguzi huu wa kizamani na kijima.
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano.

Monday 18 July 2016

Our Lives in History, Today 18 Years Ago





Today 18 years ago I quit bachelor club. It is the time my sweetheart Nesaa came into my life. Since then, we've been happily married. So, too, we're blessed with six children, four girls and two boys. We've cherished and enjoyed  more  our marriage more than anything we've ever had in our lives. Though years have lapsed, it still feels like yesterday. We're still wholeheartedly and sincerely committed to each other. Since the day we made our vows our love has never dwindled.  Our union has always been spiffy despite being mortals.
Today is a day
Our loves got a seal
It from this day
We're declared wife and husband
and, indeed,
It is from this very day
Two became one
We've since soldiered on
Joyful has always been our union

We stood whatever challenge
Love became our refuge
Just like any  human being
Cooperation has always been our forte
Ever since we've never staggered
We've stood together
We indeed are stronger

Our house became a home
for whoever that comes 
We make her or him feel at home
We are always calm
Whenever we face a storm
Love has been our weapon
Indeed, love has made us soldier on

We always thank God
To bring us together
 Going from strength to strength
Our marriage is always healthy
Patience and love are our hush-hush
Today is our anniversary





Sunday 17 July 2016

Twarana na nii (Nenda nami) -Jane Muthoni



Huwa napenda nyimbo za Kikuyu kwa vile nakifahamu japo si sana. Wimbo huu wa Jane Muthoni (Mkwe) huburudisha na kufundisha. Hapa nakudonolea kidogo tu.

Umeniita nikufuate
Kuna shida safarini
Nakuomba usiniache

Nenda nami
Twende nyumbani x2

Moyo wangu unataka kukutumia
Ninashindwa na shida za dunia hii
Hauna kifani upendo wako
Nenda nami mungu wangu
Twende nyumbani

Mambo mengi niyaonayo safarini

Marafiki zangu si sawa nawe

Saturday 16 July 2016

Tulia Ackson anapaswa kutulia

            Pamoja na kwamba uhuni Bungeni haukuanza jana–hasa kiti cha Spika kinapotumika vibaya kwa sababu binafsi au za kisiasa–Bunge la 11 linaweza kuvunja rekodi katika baadhi ya mambo tena yasiyopendeza wala kukuza demokrasia nchini. Zamani uspika ilikuwa ni taasisi yenye kuheshimika sana nchini; hasa ikizingatiwa kuwa ni moja na mihimili mitatu ya dola. Bunge linapaswa kuwa huru bila kuingiliwa au kuingilia mihimili mingine ya dola. Hata hivyo, baada kuingia ushindani wa vyama vingi, Uspika ulianza kugeuzwa sehemu ya utawala jambo ambalo ni kuupunguzia heshima na kuuingilia mhimili huu kati ya tatu ziundazo dola yaani Bunge, Mahakama na Utawala.  Hili si jambo jema kwa taifa hasa Bunge linapofikia mahali ukawa ni uwanja wa kulipiziana visasi kisiasa na kiutendaji.
            Dhana nzima ya kuwepo Bunge ni kutaka kutoa fursa ya mihimili ya tatu kutekeleza wajibu wake ambao kwa Bunge ni kupokea miswaada ya sharia, kuipitisha, kutunga, kurekebisha na kufuta sheria kunakofanywa na wabunge wanaowawakilisha wananchi moja kwa moja.  Baada ya hivi karibuni baadhi ya Wabunge wa kuteuliwa–tena na wakuu wa dola–ambao Spika wa zamani Samuel Sitta aliwahi kuwaelezea kama mizigo kuweza hata kuruhusiwa kugombea uspika au unaibu Spika japo hawamwakilishi yeyote zaidi ya matumbo yao na aliyewateua, ithibati ya Bunge imeanza kushuka au kupotea kabisa. Hali ya Bunge inakuwa mbaya pale inaposimamiwa na mtu au watu wasiotokana na kura za wananchi na badala yake wakateuliwa kirahisi tu. Kwani–mbali na kutowakilisha umma–wahusika hawajui machungu na mikiki mikiki ya kuupata Ubunge. Hivyo, wanaweza kutumia nyadhifa zao watakavyo ima kujiridhisha au kuwaridhisha waliowateua kama ilivyo sasa ambapo ukada na unazi vinaanza kuzoeleka Bungeni tangu kuchaguliwa kwa naibu Spika, Dk Tulia Ackson.
            Hata hivyo, Uspika si sehemu ya kuonyesha ukomavu, uongozi na uzalendo na si mabavu, ubabe wala upendeleo; bali kutenda haki hasa nafasi hii inaposhikiliwa na mtu anayejinakidi kuwa na shahada ya uzamivu katika masuala ya sheria. Inashangaza mtu mwenye kuitwa daktari wa sheria kushindwa kumaizi jambo rahisi kama hili. Je tatizo hapa ni busara, elimu za kuungaunga au uzoefu?
            Kwa wanaoujua thamani na umuhimu wa elimu, wengi walidhani daktari huyu wa sheria angejua umuhimu wa elimu; hivyo, kuonyesha umahiri wake katika kusimamia na kukuza demokrasia badala ya vurugu na kuiminya demokrasia. Hata hivyo–tokana na kadhia tulizoshuhudia ambapo naibu Spika wa Bunge Dk Ackson akionyesha wazi kulalia upande mmoja wa Utawala na kushindwa kujitofautisha na Spika aliyepita Anna Makinda aliyesifika kwa uburuzaji tokana na alivyopatina na kiwango chake cha elimu, wakati mwingine tunashindwa kuwatofautisha wawili hawa japo wana viwango tofauti vya elimu.
            Wengi waliofuatilia vikao vya Bunge na wingi wa Wabunge wa upinzani walioadhibia kwa kuzuia kuhudhuria vikao wanajiuliza: Je tatizo ni Wabunge au naibu Spika? Pamoja na udhaifu wake, mbona wakati wa kipindi cha Makinda, Wabunge hawakuadhibiwa kwa wingi na mfululizo kama ilivyotokea hivi karibuni? Ukiangalia utendaji wa Bunge kwa vipindi mbali mbali vya karibuni kuanzia uongozi wa mzee wa Viwango Samuel Sitta ambaye alikuwa pia mwamanasheria, watakubaliana nasi kuwa Wabunge wengi hasa wa upinzani wameadhibiwa kipindi Dk Tulia alipoendesha Bunge baada ya Spika kuwa nje kwa matibabu tena ndani ya muda mfupi.
            Makinda aliwasimamisha  Wabunge Tundu Lissu (Singida Magharibi), Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), Peter Msigwa (Iringa Mjini), Highness Kiwia (Ilemela), Godbless Lema (Arusha Mjini) na Ezekiah Wenje (Nyamagana) mnamo  tarehe 18, April 2013.
            Ackosn amewasimamisha wabunge Zitto Kabwe (Kigoma Mjini), John Heche (Tarime Vijijini), Halima Mdee (Kawe, Tundu Lissu (Singida Magharibi, Godbless Lema (Arusha Mjini), Pauline Gekul (Babati Mjini) na Esther Bulaya (Bunda Mjini). Mei 2016.
 Suzan Lymo (Viti Maalum) na Anatrophia Theonest (Viti Maalum) Juni 2016
Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), Saed Kubenea (Ubungo) na James Milya (Simajiro) Julai 2016.
            Ukiangalia mfuatano, ni kwamba, karibuni kila mwezi Ackson alikuwa akifukuza wabungu kwa wastani wa wabunge wanne au mbunge moja kila wiki. Je hapa tatizo ni Wabunge au naibu Spika mwenyewe? Mbona huko nyuma hakuwahi kutokea? Kimsingi, Ackson ataingia kwenye historia ya vitabu vya bunge kama mtu aliyekalia kiti cha Spika na kuvunja rekodi–si ya kufanikisha bunge–bali kuwatimua Wabunge wa upinzani. Je huu si ukada wa wazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho wakubwa zake nao wana rekodi ya kumteua kwa vyeo tofauti ndani ya muda mfupi? Kama Ackson ana mapenzi na ukereketwa wa chama chake hivi, si aende akafanye kazi za ndani ya chama badala ya kuaminiwa wadhifa wa kitaifa ambao ameonyesha kuutia aibu ukiachia mbali kutumia vibaya kiti cha spika?
Tumalizie kwa kumtaka Dk Tulia kutulia na kuonyesha ubobezi wake  katika sheria na si kufanya vinginevyo jambo ambalo linalishushia heshima Bunge naye binafsi kama msomi na kiongozi wa umma. Unapofukuza wabunge–licha ya kuwanyima wananachi uwakilishi–ni kuwafukuza wananchi kwenye chombo chao.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili.

Hotuba ya Mlevi kwa waziri mkubwa wa Hindi

Image result for narendra modi and magufuli
            




Baada ya kushuhudia ugeni wa mashaka toka Ugabacholini ulioongozwa na Nyabenda Moody waziri mkubwa ukija Bongo na kuondoka bila kujihangaisha kukutana na uongozi wa walevi, nimeshauriwa kutuma hotuba hii kwenye ubalozi wao ili kuwawasilishia yale ambayo rahis hakuyagusia kwenye kuwakaribisha hawa wageni wake tokana na sababu anazojua mwenyewe. Kwa wasiomjua huyu Moody, ni mnyasa wa Mbamba Bay aliyepotelea ugabacholini pamoja na jamaa waitwao Jarawa wanaobaguliwa kama wanyama kule.
Kuna mambo mengi tulitegemea rahis ayataje tena bila kumung’unya badala ya kumwaga ujiko kwa jamaa hawa wanaosifika kwa kubagua waswahili wakiwaita absii, bander, kalu au manyani na majina mengine mabaya tu wakati sisi tukiwaendekeza hapa kaya kiasi cha kuendelea kutubagua bila hata aibu na adabu.
Japo rahis aliipa ujiko sana Ugabacholini kwa kuwekeza kayani, tunachojua ni kwamba imekuwa ikichukua na si kuwekeza hasa ikizingatiwa kuwa kwa sasa ugabacholini inaongoza kwa kuuza tanzanite na si hindinite jambo ambalo rahis alikiri. Hii maana yake ni kwamba wanatuibia madini yetu jambo ambalo ni jinai ambayo rahis alipaswa ailalamikie badala ya kuisifu. Sijui yeye ananufaika vipi na jinai hii?
Ugabacholini imefanikiwa kutujazia wachovu wake wasio na ajira kuja kuajiriwa hapa kibaguzi kwa kujali rangi na asili badala ya maslahi ya pande zote mbili. Anayebisha aende kwenye viwanda vingi vya magabacholi na mahoteli aone waganga njaa waliojazana kule kutoka ugabacholini wakifanya kazi ambayo wachovu wanaweza kufanya. Aende kwenye makazi yao aone wanavyoishi kwa kujitenga.
 Wachovu tunaojazia hawaishii kuchukua kazi tu bali wajihusisha na kuvusha mali zetu kama tanzanite japo rahis alisema eti kuna maslahi ya pamoja wakati ni ya upande mmoja.
Hakuna sehemu rahis aliwaacha hoi walevi kama kuridhia ubaguzi katika kutoa uraia wa kaya mbili au zaidi kwa mlango wa nyuma. Rahis alisikika akisema kuwa baadhi ya magabacholi waliokwenda pale kumpokea mgeni wake ni wabongo waliompigia kura Moody huko ugabacholini. Hii maana yake ni kwamba wana uraia wa kaya mbili jambo ambalo ni jinai kwa sheria za kaya. Watakuwaje na uraia wa ugabacholini wakati wao ni Wadaganyika wanaopaswa kuwa na uraia wa kaya moja au uraia wa kaya nyingi unawafaa wageni kuliko wazawa?
Rahis alisema kuwa Hindi inasaidia kaya za Kiswahili wakati inazijazia bidhaa feki na wasasi ngawira na kazi bila kusahau kuzijazia bidhaa feki na vya chini ya kiwango (substandard goods).
 Rahis alishindwa kugusia namna magabacholi walivyogeuza wanyama ndugu zetu waitwao Jarawa kwenye visiwa vya Andaman tokana na Hindi kujengwa kwenye apartheid iitwayo caste system ambayo inafanyika hata kwenye kaya zetu ikitendwa na wale walioletwa na wakoloni kutuibia na kutunyonya ukiachia mbali kuendelea kutumiwa na wezi wazawa wenye mamlaka.
Inashangaza kusikia kuwa tuna magabacholi kumi mjengoni wakati mamia ya waswahili waishio kwenye visiwa tajwa waligeuzwa vivutio vya utalii bila huduma yoyote ya afya kiasi cha tofauti yao na wanyama kuwa sura zao tu. Kwa wanaotaka kujua zaidi ubaguzi huu http://www.aljazeera.com/indepth/features/2014/01/time-ticking-india-jarawa-tribes-20141314281424904.html.  Inasikitisha sana kuona wale walioletwa na wakoloni wakila kuzaliana, kunenepeana wakatajirika na kuita wengine wakati ndugu zetu wakiteseka kwa sababu ya rangi ya ngozi yao.
Hapa tunaongelea ubaguzi ambao rahis aliogopa kuugusia. Hatujagusia jinsi magabacholi wanavyoingiza wenzao kayani kufanya kazi ambazo wachovu wanaweza kuzifanya. Ajira zao nyingi ni za kibaguzi. Rejea kukamatwa kwa magabacholi wengi waliokuwa wakiishi kwenye kaya bila vibali. Hapa hatujagusia ubaguzi wa wazi wazi hata kwenye makazi ambapo magabacholi wengi wenye mahekalu, hata viwanda kuendelea kuishi kwenye kaya za bei mchekea za Asajile Mwaijumba katikati ya jiji huku wazawa wakitimkia Pugu Kajiungeni na Kimanzichana. Ukiingia downtown Bongo usiku unaweza kudhani uko Bombay. Sijui huyu Bwana Mdogo Po Makondakonda anashindwa nini kupitisha amri kuwa kila wenye uwezo wa kujenga mahekalu shurti waishi kwenye mahekalu yao badala ya kuwabana walevi kwenye nyumba za Asijile za bei poa.
Mlevi amewahi kuishi ugabacholini kwa miezi michache akifanya utafiti juu ya ubaguzi ambao umekuwa ukitokea ugabacholini ukiachia ule wa kwenye kaya ambao tawala zote zilijifanya kutouona. Hebu nionyesha lau binti mmoja wa kigabacholi aliyeolewa na mswahili nitajinyotoa roho kwa aibu ya kusema uzushi.
Kipindi fulani waziri mmoja aitwaye Idd Lion aliwahi kudai kuwa magabacholi kumi tu walikukwa wakimilki uchumi wote wa kaya ya Danganyika. Hata sasa, ukimuondoa mzee Bhakresa, matajiri wakubwa ni magabacholi; kwanini wakati hakuna waswahili matajiri ugabacholini ambako hata kwenda kusoma ni ubaguzi wa kuua mtu hadi waswahili kuitwa absii, bander na kalu yaani manyani.
Walevi wameshangazwa sana kitendo cha rahis kushindwa kumtaka waziri mkubwa wa ugabacholi kuomba msamaha kwa binti wa kitanzania (jina kapuni) akiwa na mwenzake  aliyedhalilishwa na kupigwa hadharani baada ya msudani ambao hupenda kujiita wamanga wakati wamanga wanawaona kama watumwa kumgonga maza mmoja wa kigabacholi.
Tumalizie kwa kusema kuwa walevi hatukuridhishwa na namna masuala yenye siha yalivyotalekezwa zikamwagwa sifa kwa jamaa ambalo halikufaa kumwaiwa ujiko wote huku wakati linaongoza kaya inayosifika kwa ubaguzi na unyonyaji wa waswahili. Lazima usuhuba huu mpya baina ya Bongo na ugabacholini upigwe darubini tusiendelee kulizwa.
Chanzo: Nipashe Jumamosi.

Friday 15 July 2016

Wiki hii niliwarusha makamanda wangu

Picha ya familia ya pamoja wakati makamanda na baba yao wakijiandaa kupasua anga 
Baba anaposhika usukani huku makamanda wakiwa nyuma yake wakijifunza namna ya kuendesha ndege
Picha na Makamanda baaada ya kushuka chomboni



Tulitumia ndege aina ya 1966 Piper Cherokee. Ni ndege nzuri japo ya kizamani. Hali ya hewa ilikuwa nzuri sana kiasi cha kutokumbwa na misukosuko kama ilivyo kawaida ya ndege ndogo.  Kama baba yao, makamanda wanapenda sana ndege kiasi cha kuwa usumbufu. Hivyo, kila nikipata fursa, nitakuwa nikiwapa ride  japo nao waanze kufuata nyayo mapema.

Wednesday 13 July 2016

Tusinunue ndege kwa 'madesa'

 Image result for photos of bombardier c 400
           
            Neno desa au kuchota ujuzi, taarifa au majibu bila kuyafanyia kazi na kuyatumia kwenye kazi yako au kunakiri bila kufuata sheria au kukwepa sheria–kabla ya kuchaguliwa kwa rais John Pombe Magufuli–lilikuwa limefungiwa kwenye kuta za madarasa na vyumba vya mihadhara ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM). Hata hivyo, baada ya kuchaguliwa Magufuli ambaye ni mhitimu wa shahada tatu zote toka UDSM, neno desa limeingia kwenye msamiati tawala (mainstream).
Hivi karibuni vyombo vya habari vilimkariri Magufuli si zaidi ya mara moja akitumia neno desa kuanzia alipohutubia jumuia ya wana UDSM hadi alipomkaribisha rais wa Rwanda Paul Kagame aliyesema amempa desa au mbinu ya kununua ndege mbili kwa mpigo. Magufuli alisema, “Mwezi wa tisa tutakuwa tumepata ndege mbili mpya, nimepewa namna nzuri ya kupata ndege hizo na Rais Kagame baada ya kuwatuma maofisa wake ambao ni wataalam wa ndege waje na kunipa desa.”
Si vibaya kwa viongozi kupeana mbinu za kufanya mambo ingawa hili linatia shaka kwa namna moja au nyingine. Pia linaacha maswali mengi kuliko majibu. Je Tanzania–pamoja na kupata uhuru zaidi ya miaka hamsini iliyopita–haina wataalamu wake wenye ujuzi na wa kuaminika kufanya kazi hiyo hadi tukope wataalamu toka Rwanda? Kwa mujibu wa matamshi ya Magufuli ni kwamba Tanzania haina wataalamu wa kutafuta na kununua ndege jambo ambalo ni aibu kwake na taifa.  Vyema, kuwa Magufuli amepewa desa; je amepewa na wataalamu wa kuendesha ndege husika? Je wataalamu wetu wanaolipwa kumshauri Magufuli wanalipwa kwa kazi gani kama rais analazimika kukopa washauri na wataalamu toka nje?           Je hilo shirika litaendeswa na hao wataalamu wa Kagame?
             Kisa cha Magufuli kupewa “desa” kinanikumbusha kisa cha jamaa mmoja aliyeomba ng’ombe kwa rafiki yake ili naye akafuge na kupata maziwa, mbolea na nyama. Hata hivyo, jamaa huyu alikuwa na kasoro nyingi; hakuwa na uwezo wala ujuzi wa kumtunza ng’ombe aliyezawadiwa. Hivyo, alipoletewa ng’ombe alisema, “Asante sana rafiki yangu. Hata hivyo, naomba mtu wa kumswaga huyu mnyama.” Mwenyeji wake alimjibu, “Umepata. Je una jingine?” mgeni alijibu, “Je nitapata wapi mtu wa kumkamua, kumlisha na kumtunza?” mwenyeji alisita kidogo na kusema, “Ngoja kidogo” alimwambia yule mtumishi aliyekuwa ameleta ng’ombe, “mrudishe huyo ng’ombe kwa wenzake hadi jamaa atapopata ujuzi na uwezo wa kumtunza atajua jinsi ya kuja kumchukua na kummilki.” Jamaa alibaki kujishangaa na kushangaa namna alivyojiaibisha.  Kwa ufupi ni kwamba; sitashangaa ndege husika zikaishia kuuzwa kwa hao hao manoadesa kwao. Hili liko wazi na wenzetu wanalijua. Kwani wengi wamezaliwa na kukulia na kusomea Tanzania. Mbali na hili, hata ukiangalia tulivyoinga kwenye Jumuia ya Afrika Mashariki kijinga, kuna uwezekano Tanzania ikaishia kuwa kimbilio la watu wasio na ardhi au kuja kuchuma na kurejea kwao. Mimi huwa siamini katika mashirikisho na jumuia za kimajimbo bali muungano wa haraka na moja kwa moja wa Afrika. Je muungano wa Afrika unawezekana wakati kila rais anang’ang’ania ulaji wake? Hili humu si mwake leo.
Japo Magufuli anasherehekea na kujisifia kupewa desa, anapaswa kufikiri na kuangalia mbali zaidi hasa usawa huu ambapo kila nchi inatafuta kila fursa kuwanufaisha watu wake baada ya nchi za kiafrika–kwa ujinga, uroho, upogo na kongwa za kikoloni zilikataa kuungana na kuwa nchi moja kama Marekani au China.  Watanzania kukiri kuwa hamna ujuzi na kuwaamini hawa watoa madesa, mmewapa kishawishi cha kuanga kujiandalia kurejesha ng’ombe zizini hadi mtakapopata uwezo na kuwa tayari kummlilki na kumtunza ng’ombe husika. kama shida ni wataalamu, kwanini Magufuli hakuwatuma wataalamu wake kwenda Rwanda kujifunza badala ya kuwaamini kazi wanyarwanda ambao hawako chini ya kiapo chochote wala uwajibikaji kisheria wa kuitumikia Tanzania? Kwanini hatutaki kujifunza tokana na wale tuliwatengeneza tukidhani ni watanzania wakaishia kutuacha Solemba?  Kwanini watanzania tunakuwa wepesi kufanya mambo muhimu kuwa ya mzaa kama kuamini uchumi wetu kuwa mikononi mwa wageni kama inavyozidi kubainika ambapo matapeli wa kigeni huja nchini wakijifanya wawekezaji wakiwa mikono mitupu na kuondoka na utajiri wa kutisha wakati watu wetu wakiwa maskini?
Kama tutakuwa wakweli, nchi iliyopata uhuru zaidi ya nusu karne ahitaji msaada hata wa namna ya kununua ndege. Hii maana yake–kama inashindwa kuwa na wataalamu wa kununa ndege–maana yake haina hata wataalam wala mipango madhubuti ya kuendesha shirika la ndege linalokusudiwa kuanzisha? Je tatizo ni wataalamu au uzalendo na mfumo bora? Mbona baadhi ya wataalamu wa Rwanda wamesoma tena bure hapa Tanzania wakijionyesha kama watanzania wakati ni wanyarwanda? Ajabu hatukuwachukulia hatua ikizingatiwa kuwa nchi yetu hairuhusu uraia wa nchi mbili. Je hawa waliotukimbia wataweza kutusaidia kweli? Mjinga ni yule anayeng’atwa na nyoka mara mbili kwenye shimo moja.
Tumalizie kwa kumshauri rais Magufuli kufikiria upya kuhusiana na mpango wake wa kuazima wataalamu toka Rwanda au kwingineko. Kununua ndege hakuna haraka. Anapaswa kutuma wataalamu kujifunza si Rwanda tu bali Kanada zinakotengenezwa ndege husika. Kama tunashindwa na jambo dogo ambalo makampuni ya watu binafsi kama lile la bilionea Richard Bronson yamefanya, nini maana ya kuwa huru akiri bila kufuata sheria au kukwepa sheria–kabla ya kuchaguliwa kwa rais John Pombe Magufuli–lilikuwa limefungiwa kwenye kuta za madarasa na vyumba vya mihadhara ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM). Hata hivyo, baada ya kuchaguliwa Magufuli ambaye ni mhitimu wa shahada tatu zote toka UDSM, neno desa limeingia kwenye msamiati tawala (mainstream).
Hivi karibuni vyombo vya habari vilimkariri Magufuli si zaidi ya mara moja akitumia neno desa kuanzia alipohutubia jumuia ya wana UDSM hadi alipomkaribisha rais wa Rwanda Paul Kagame aliyesema amempa desa au mbinu ya kununua ndege mbili kwa mpigo. Magufuli alisema, “Mwezi wa tisa tutakuwa tumepata ndege mbili mpya, nimepewa namna nzuri ya kupata ndege hizo na Rais Kagame baada ya kuwatuma maofisa wake ambao ni wataalam wa ndege waje na kunipa desa.”
Si vibaya kwa viongozi kupeana mbinu za kufanya mambo ingawa hili linatia shaka kwa namna moja au nyingine. Pia linaacha maswali mengi kuliko majibu. Je Tanzania–pamoja na kupata uhuru zaidi ya miaka hamsini iliyopita–haina wataalamu wake wenye ujuzi na wa kuaminika kufanya kazi hiyo hadi tukope wataalamu toka Rwanda? Kwa mujibu wa matamshi ya Magufuli ni kwamba Tanzania haina wataalamu wa kutafuta na kununua ndege jambo ambalo ni aibu kwake na taifa.  Vyema, kuwa Magufuli amepewa desa; je amepewa na wataalamu wa kuendesha ndege husika? Je wataalamu wetu wanaolipwa kumshauri Magufuli wanalipwa kwa kazi gani kama rais analazimika kukopa washauri na wataalamu toka nje?           Je hilo shirika litaendeswa na hao wataalamu wa Kagame?
             Kisa cha Magufuli kupewa “desa” kinanikumbusha kisa cha jamaa mmoja aliyeomba ng’ombe kwa rafiki yake ili naye akafuge na kupata maziwa, mbolea na nyama. Hata hivyo, jamaa huyu alikuwa na kasoro nyingi; hakuwa na uwezo wala ujuzi wa kumtunza ng’ombe aliyezawadiwa. Hivyo, alipoletewa ng’ombe alisema, “Asante sana rafiki yangu. Hata hivyo, naomba mtu wa kumswaga huyu mnyama.” Mwenyeji wake alimjibu, “Umepata. Je una jingine?” mgeni alijibu, “Je nitapata wapi mtu wa kumkamua, kumlisha na kumtunza?” mwenyeji alisita kidogo na kusema, “Ngoja kidogo” alimwambia yule mtumishi aliyekuwa ameleta ng’ombe, “mrudishe huyo ng’ombe kwa wenzake hadi jamaa atapopata ujuzi na uwezo wa kumtunza atajua jinsi ya kuja kumchukua na kummilki.” Jamaa alibaki kujishangaa na kushangaa namna alivyojiaibisha.  Kwa ufupi ni kwamba; sitashangaa ndege husika zikaishia kuuzwa kwa hao hao manoadesa kwao. Hili liko wazi na wenzetu wanalijua. Kwani wengi wamezaliwa na kukulia na kusomea Tanzania. Mbali na hili, hata ukiangalia tulivyoinga kwenye Jumuia ya Afrika Mashariki kijinga, kuna uwezekano Tanzania ikaishia kuwa kimbilio la watu wasio na ardhi au kuja kuchuma na kurejea kwao. Mimi huwa siamini katika mashirikisho na jumuia za kimajimbo bali muungano wa haraka na moja kwa moja wa Afrika. Je muungano wa Afrika unawezekana wakati kila rais anang’ang’ania ulaji wake? Hili humu si mwake leo.
Japo Magufuli anasherehekea na kujisifia kupewa desa, anapaswa kufikiri na kuangalia mbali zaidi hasa usawa huu ambapo kila nchi inatafuta kila fursa kuwanufaisha watu wake baada ya nchi za kiafrika–kwa ujinga, uroho, upogo na kongwa za kikoloni zilikataa kuungana na kuwa nchi moja kama Marekani au China.  Watanzania kukiri kuwa hamna ujuzi na kuwaamini hawa watoa madesa, mmewapa kishawishi cha kuanga kujiandalia kurejesha ng’ombe zizini hadi mtakapopata uwezo na kuwa tayari kummlilki na kumtunza ng’ombe husika. kama shida ni wataalamu, kwanini Magufuli hakuwatuma wataalamu wake kwenda Rwanda kujifunza badala ya kuwaamini kazi wanyarwanda ambao hawako chini ya kiapo chochote wala uwajibikaji kisheria wa kuitumikia Tanzania? Kwanini hatutaki kujifunza tokana na wale tuliwatengeneza tukidhani ni watanzania wakaishia kutuacha Solemba?  Kwanini watanzania tunakuwa wepesi kufanya mambo muhimu kuwa ya mzaa kama kuamini uchumi wetu kuwa mikononi mwa wageni kama inavyozidi kubainika ambapo matapeli wa kigeni huja nchini wakijifanya wawekezaji wakiwa mikono mitupu na kuondoka na utajiri wa kutisha wakati watu wetu wakiwa maskini?
Kama tutakuwa wakweli, nchi iliyopata uhuru zaidi ya nusu karne ahitaji msaada hata wa namna ya kununua ndege. Hii maana yake–kama inashindwa kuwa na wataalamu wa kununa ndege–maana yake haina hata wataalam wala mipango madhubuti ya kuendesha shirika la ndege linalokusudiwa kuanzisha? Je tatizo ni wataalamu au uzalendo na mfumo bora? Mbona baadhi ya wataalamu wa Rwanda wamesoma tena bure hapa Tanzania wakijionyesha kama watanzania wakati ni wanyarwanda? Ajabu hatukuwachukulia hatua ikizingatiwa kuwa nchi yetu hairuhusu uraia wa nchi mbili. Je hawa waliotukimbia wataweza kutusaidia kweli? Mjinga ni yule anayeng’atwa na nyoka mara mbili kwenye shimo moja.
Tumalizie kwa kumshauri rais Magufuli kufikiria upya kuhusiana na mpango wake wa kuazima wataalamu toka Rwanda au kwingineko. Kununua ndege hakuna haraka. Anapaswa kutuma wataalamu kujifunza si Rwanda tu bali Kanada zinakotengenezwa ndege husika. Kama tunashindwa na jambo dogo ambalo makampuni ya watu binafsi kama lile la bilionea Richard Bronson yamefanya, nini maana ya kuwa huru na kupoteza fedha kusomesha wataalamu ambao hawawezi hata kununua ndege?