The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Wednesday, 15 July 2026

Fyatu kuleta haki kwanza amani baadae


Juzi, nilipiga kanywaji hadi nikazimika na kuzimia kabla ya kuzimuliwa na Fyatuwe aka Bi Mkubwa. Si pale niliposikia mafyatu wakijifyatua, kujidanganya, na kudanganya wengine eti tuombe amani kwa kaya yetu bila kuwajua na kuwakomesha wavunja amani! Ili iweje?  Je, hapa, nani anajidanganya na kutaka kumfyatua nani? Hivi, kweli inawezekana kuwapo amani bila haki? Hawa wanaodai amani, kuivunja, kuiua, na kuipuuzia, wana akili kweli? Hivi, hawajui kuwa amani ni mtoto wa haki? Wapi kuliwahi kuwapo amani bila haki? Haki ni haki. Daima huvunja milima. Haki haitegemei amani kama ambavyo amani hutegemea haki.
            Haki ya kweli haiwezi kuwepo bila amani. Haki siyo siasa wala sanaa bali haki. Yeyote anayetaa kuwapo amani bila haki anahitaji msaada tena wa bure. Huwezi kutetea haki kwa kudharau, kusahau, au kukandamiza haki.
            Kama haki ni kiumbe, basi amani ni kizalia chake japo wote ni viumbe. Kama amani ni muhimu, haki ni lazima na muhimu. Yeyote anayekufyatua akidai uombee au kutetea amani bila haki anakugeuza bunga kama siyo zwazwa. Mkatae. Mkemee. Na ikibidi mfyatue. Kwani, analenga kukufyatua. Hivi, kweli inawezekana jiwe kutoa maziwa achilia mbali maji? Sasa, inawezekanaje kuwa na amani bila haki? Haki ahitaji amani bali ukweli na uwajibikaji. Amani inahitaji haki kwanza, na mengine yanafuatia hata yasipofuatia. Haki inaweza kushamiri bila kuhitaji msaada wa haki ila amani, bila haki, inakufa hata bila kupigwa kisu wala risas!i.
            Nasikia wengine, hasa mabambataa na mazwazwa wakiwahadaa mafyatu eti waombe amani! Wanakwenda mbali na kusema eti Fyatuland iombewe. Hapana. Fyatuland inahitaji kuambiwa tena ukweli kuwa mambo si mambo. Mtaomba hata utupu lakini amani haitakuwapo bila kuwapo haki. Fyatuland inahitaji kuambiwa kuwa bila haki hakuna amani. Na amani tunayoongelea hapa si ya wachache bali wote. Nani anataka amani ya wachache kula kwa amani wakati wengi wakinyimwa haki? Huu ni utani mbaya. Hayo, tuyaache kwanza.
            Juzi, nilipita kwenye hekalu la tapeli mmoja aliitalo la Mungu. Msimuingize Mungu kwenye utapeli na usanii wenu. Mafyatu mazwazwa wengi walikuwa wakipiga mikelele wakiomba amani utadhani Sir God ni kiziwi! Walipayuka kama machizi wakijihadaa wangemfyatua Sir God achanganywe na makelele ambayo matapeli wa kiroho waliojaa uroho hutumia kuwahadaa na kuwafyatua. Wako wapi akina Gwjimy na matapeli wengine tena mazwaza? Hawa, waweza kuomba na kuleta amani kweli wakati maombi yao hayana amani achilia mbali imani?
            Kama amani ni dunia, haki ni maji ambayo ndiyo chanzo cha kila kitu. Kama amani ni jengo au nyumba, basi haki ni msingi na sementi viianzishayo na kuihimili maisha yake yote. Kama ni gari, basi haki ni injini iendeshayo hili gari. Kama amani ni dhahabu, basi haki ni rhodium, osmium, na painite ambayo ni aghali kuliko yote duniani. Ngoja niache kuleta madude yetu maprofesa ili nisiwachanganye mafyatu na wasomaji wangu. Hayo tuyaache.
            Tuanze kufyatuka na kutafakari pamoja. Hebu tujiulize na kujibu maswali haya pamoja tena kwa ukweli na uwazi.
            Kwanza, amani ni nini? Iko wapi na inapatikanaje na kwanini? Nini uzuri wa amani? Nani analinda, kujenga,au kuivunja amani? Bila kudurusu na kujibu maswali haya adhimu, tunajidanganya na kutaka kuwadanganya na kuwafyatua mafyatu waliogoma kufyatuka wakafyatua wawafyatuao.
            Pili, tujiulize. Tunajua tunachotaka au kutaka tusichojua?Je, tutakipataje na lini na kwa njia gani? Tunapaswa kuwa wakweli katika kuiendea na kuipata amani. Amani haitaki ubabaishaji, urongo na usanii. Japo tunaiita tunu, ni tunu gani ambayo hatuilindi na kuitunza kwa kufuata ukweli na usayansi wake?
            Tatu, ni amani gani inaweza kuwepo na kushamiri katikati ya ubabaishaji, ukatili na uovu? Tunawezaje kuwa na amani ilhali wapo wenye haki ya kuwa nao hata kuivunja kuliko wengine?
            Nne, ni amani ya nani na kwanini? Je, tumeweka misingi ya amani au ya imani ya amani kwa kuitelekeza hata kuichukia kama siyo kuiepa haki? Je, sheria na taratibu zetu zinajenga au kubomoa amani? Je, wanaowaibia wenzao na wanaoibiwa wanaweza kuwa na amani sawa?
          Tano, kwanini hakuna amani? Na je, tumewahi kuwa nayo? Kama ilikuwapo, imekuwaje ikatoweka? Nini kimesababisha itoweke na tangia lini? Je, kama tulikuwa nayo, ilikuwa amani ya kweli au amani ya imani ya amani?
            Sita, je, nini kifanyike kuirejesha hii amani inayotuhangaisha?
            Bila kujibu maswali haya na mengine, tunapoteza muda na kupigiana nakeleke kwa kisingizio cha kusaka amani. Tutafute na kutenda haki kwanza. Tukifanya hivi, amani itakuwapo na kutamalaki. Pia, tuhakikishe amani husika inakuwa ya wote na si ya baadhi.
            Kumbe kumekucha! Amani, we acha tu. Haki ziii! Amani hoyee!
Chanzo: Mwananchi Jtano leo.

Wanandoa kutendeana haki na wema si hisani


Japo halifurahishi, ni kawaida kuona au kusikia wanandoa wakitendana. Hutofautiana, huchukiana, husuluhishana, baya kuliko yote, huumizana kwa kutenzana ndivyo siyo. Ni jambo jema wanandoa wanapotendeana hasa katika mambo baadhi au yote ya haki kiasi cha kuridhiana, kuridhishana, na kuendelea kufaidi ndoa zao wapaswavyo na watakavyo. Hapa, hakuna miujiza wala mazingaombwe. Ni suala la kuelewa na kuchagua kusuka au kunyoa ili usukwe au kunyolewe.
    Leo, tutaongelea kutendeana kwa maana ya kutenzana. Kuna tofauti kati ya mawili haya. Kutendeana ni kufanyiana mambo yawe mabaya au mazuri. Kutenzana, kimsingi, ni kuumizana. Ukimtenda mwenzio, utamchukia na kumchukuza, utamhujumu, utamhukumu, na hata kumdhulumu. Huku, ndiko kutenzana. Kuhusiana na kutendeana na si kutendana, tushaeleza hapo juu.
            Tukirejea na kutia nukta kwenye, yaani kutendeana haki, tuseme wazi. Hili, ni dhamira na hitajio kuu la ndoa ingawa halifanyiki bila kuwepo kupendana. Kwa vile mzizi wa ndoa ni kupendana, hatutaongelea hili kwa vile lazima liwepo kabla ya mengine, ingawa kadri muda unavyokwenda mambo hubadilika.
            Kwanini kutendeana haki si hisani bali wajibu? Kwanza, hakuna aliyewalazimisha kupendana na kuoana. Hivyo, mkiwa wakweli kwa malengo, nia, na viapo vyenu, bila kutenda na kutendeana haki, ni kama hakuna ndoa. Kama ipo, basi ni ndoa jina ila si ndoa kwa maana yake. Kwanza, mlitafutana, mkapendana, na kuamua, kuapishana, na kuoana ili kuishi kwa pamoja. Je, kwanini mlifanya yote hayo? Jibu ni rahisi. Kila mmoja alikuwa akitafutaakitakacho lakini asichonacho kwa mwenzake. Hivyo, kutendeana haki si chaguo wala hisani bali hitajio muhimu la uwepo wa ushirika wenu.
            Sisi waandishi ni wanandoa waliodumu kwenye ndoa kwa takribani miaka 30. Tunaijua ndoa ndani na nje. Tunaijua kwa mapana na marefu yake. Tunajua raha na karaha zake. Hivyo, tunapoandika haya, hatusomi sehemu zaidi ya kujisoma na kukumbuka mapito yetu m bali na kufanya utatifi juu ya suala zima.
            Kuna usemi maarufu wa kifaransa kuwa l’essence du droit est l’essence du devoir, yaani, bila wajibu hakuna haki. Kwa lugha nyepesi tena kwetu waswahili ni kwamba linapokuja suala la haki ni sawa na mikono miwili kunawishana. Au tuseme ni nikune nikukune. Ndoa ni kukunana na kupata haki kwa kuwajibika na si vinginevyo.
            Tuna usemi wetu binafsi. Kwetu, ndoa ni biashara ya watu wawili wenye malengo na vichaa vinavyofanana na kukubaliana. Kama kweli mnapendana, mtatendeana haki. Hapa, haki si hisani wala ombi bali wajibu. Katika ndoa, haki huja sambamba na upendo na heshima.
            Kama, mfano, mume anataka mke amtii kama haki yake na wajibu wa mke. Je inawezekana akatiiwa bila yeye kumtii huyu atakaye amtii? Kumbuka. Mwenzio siyo roboti lisilo na hiari wala kuweza kuhoji.  Kwanini utake mtu, tena mwenye akili kama wewe au hata zaidi akutii bila wewe kuwa tayari kumtii? Je, inawezekana kutiiwa bila kumtii anayekutii kwenye maisha ya kawaida? Hili, linawezekana kwenye ukoloni, utumwa, na utwahuti lakini si kwenye jamii ya watu wastaarabu. Kama wanadoa waitikiavyo kila jambo, lazima na kwenye kutenda haki wafanye hivyo.
            Katika hili, sisi tunayo kanuni moja mujarabu na rahisi. Huwa tunaulizana. Je, wewe ungekuwa mimi ungefanyaje hasa unapohitajika kunifanyia nini? Nini ungenifanyia sawa na kile ambacho ungekuwa mimi ungependa na kutaka nikufanyie? Tumaanishacho ni kwamba kila umfanyiacho mwenzio, unajifanyia wewe kwa kumtumia.
            Bila kuficha wala kufumba, wawili mpeanavyo ‘chakula cha usiku’, nani humtegea mwenzake? Nani hutoa bila kutegemea kupokea au kupokea bila kutegemea kutoa? Ukitaka kujibu swali hili vizuri, jiulize. Kama mwenzio asingekuwapo kwa sababu yoyote iwayo, hali ingekuwaje? Kama hujui jua. Utoacho ndiyo upatacho toka kwa mwenzako. Ujue pia kuwa yote hutegemea nawe mwenyewe kwa vile kila ufanyacho kwa mwenzio, unajifanyia mwenyewe.
            Waingereza wana msemo kuwa ukitenda wema, utakurudia na ukitenda ubaya, utazunguka na kukuridia pia. Hivyo, elewa. Ukimpenda mwenzio, unajipenda. Pia, ukimchukia, unajichukia. Kadhalika, ukimnya haki au kumdhulumu, unajinyima haki na kujidhulumu mwenyewe. Nini faida ya kufanya hivyo ilihali unajua utapata matokeo yale yale hasa kwa upande wa kudhulumiana au kuumizana?
 Tumalizie kwa kurejea kwenye kuishi pamoja na kupeana ‘chakula cha usiku.’ Lazima mjue. Kupata au kutoa ni nini zaidi ya vile tutoavyo? Lazima kukubali kuwa utapata kadri utoavyo na kukosa kwa kadri usivyotoa. Kila chakula uhitaji maandalizi. Na kula  kadhalika. Mfano, kama hujamlainisha, hutaingia, na kama hatakulainisha, waweza kuingia kwa maumivu mwishowe chakula kikakosa radha. Tunadhani tunaeleweka. Kwanini msilainishane ili wote mpate mkitakacho?
Kila mnachofanyiana kinachokubalika ni haki kwenu sawia. Kadhalika, kila mnachonyimana ni dhuluma sawia.
Chanzo: Mwananchi Jpli juzi.

Saturday, 11 July 2026

Letter to Muhoozi on media blackouts

 

 

Muhoozi, before saying something, I must remind that you’re now the most powerful person in Uganda. This, Ugandans need to know and accept due to the frailty of your father who ‘gave’ you power to act at will. Ugandans need to know that your father is Uganda and Uganda is your father and you’re the most powerful son of the most powerful man in Uganda. Ugandans must know and accept that you are one of the most powerful sons of presidents in the world who use their fathers’ power to rule. Like father like son. The sage has it. This is the time you (he who avenges or revenges) decided to shut down the media to avoid contaminating the minds of good Ugandans. This aims to save some of earthlings from the ennui of a long-time ruler who happens to be one of your makers.
I warn the media to stop doing things the way the like or deem fit as if it does not know who is above the law in the nation. You know what I mean. Another thing I congratulate you on is the fact that you’re now preparing Ugandans psychologically for transitions shall anything undesirable however natural–––God forbid–––happen to your great dad who gave you all of his power to rule on his behalf without necessarily abdicating the throne.
            Dear Muhoozi, congrats on putting your opponents on notice. Yep, you started to bite at the power that your dad’s been eating on for long. Because of your significance and that what you want everybody to know and made do with you wanted to show the world who is boss. No joke. You’re not joking. Did you mean business or you’re just looking the way take a bite on power and come out of the political closet. This, for me, shows your significance as the son of the most powerful man in Uganda as the most powerful son of the president over the insignificance of the rest that can be taken for a ride. The twosome of–––without forgetting your mother––––are the most powerful people Uganda’s ever had. Let Ugandans know that your trinity’s unshakably intact and unique since you’ve made Uganda what it’s today, rich for them and poor for the rest.  Let them know that you still have a lot to offer, and Ugandans must wait for more surprises from this trinity.
            Dear good General, underscoring your greatness and significance, I propose that next time you blackout the media, all Uganda’s pro-regime media must report and all Ugandans must support you by subscribing to your tweeter account I propose that your tweets must be made breaking news in all Ugandan media. I know those who don’t like you, dear good general, will wag tongues thinking I’m trying to get a mileage out of this assertion, or I might have been paid to say this. Nope, what I’m saying is as simple as that. I know. Those who don’t know the importance of the first family (you, the mother general, and the father general and brothers-in-law), wrongly think that their lives are adversely impinged on with uncertainties regarding the good actions you take. Go figure. Guys, who are you in Uganda? Who bewitched or cheated you not to get it?
            Dear General, when the story of your rebuke to the media, a friend sent me an email complaining about the uncertainties they’d cause. Also, he’s concern about who’s who in matters good governance! Good governance for whom? I scolded him to stop being selfish, evil, and naïve since things have changed. Christians believe Jesus died for their sins though they’re told everybody to carry one’s cross. On the contrary, politicians believe that citizens must die for them and their sins. Methinks this is the genesis for many African rulers to live larger than life while their taxpayers live in penury. I told this gullible bloke to consider other related things such as the disturbances democracy’s been causing in many African countries that tried it and ended up abusing it through vote rigging and tampering with constitutions to extend their time in office.
            Dear General, methinks Ugandans––––whether they like it or not­­­­–––should brace themselves to see you becoming their leader shall anything happen to your father. This is simple to decipher. When I consider your gruff rise in the army, you can easily know what I mean. Also, if you interrogate the reason[s] and the nuances behind your father’s clinging unto power, you’ll be on the same page with me. More so, if you consider the powers your mom has behind the curtains, you’ll agree with my hypothesis. To give those who pretend to deny the truth, I want them to ask themselves as to why your tweets leave everybody shocked. Is the system testing the waters? Is it preparing Ugandans psychologically for what’s in the cards in the upper echelons of power wherein manipulations are one of bread and butter of its mainstay? Why have you become such important this time around? Let’s get as serious as a seal instead of trying to screw over this rear up of your display. What do you aim to achieve if not more power?
            Dear General, in sum, let me wish you a very spiffy mission of getting Uganda rid of sinners like the media. The Swahili sage’s it that clouds are the signs of rains. Hence, what you’re seeing with regards to your centrality is but the beginning if not the tip of the iceberg. Punishing the media is one leg in the waters. The sage’s it that if you can’t beat them, join them. Whether they like you or not, they need to understand Uganda’s power dynamics, especially after your dad came to power and altered everything to his advantage. If he were able to prop up you so quickly that way in the military, how can he fail to do so in the office of the president? Once again, Dear General, you seem to brace yourself for big things. Big things come to big people. That’s my titbits of sagacity. Ring-a-ding-ding, nothing but.

Wednesday, 8 July 2026

Fyatu kuwafyatua wateule wajigongao na kujikomba


 Wanatumia vitegemezi, washirika wa bedroom kunivisha kiremba cha ukoka. wanaboronga halafu wanajigonga na kujikomba kwangu ili waendelee kunigeuza bunga. Huwa sipendi sifa. Mie ni Fyatu. Siyo Mungu wala muungu. Wafuatao wajiandae kufyatuliwa wote:

Mosi,Wapo matapeli na mazwazwa wanaowatumia ndugu zao hata vitegemezi vyao ambvyo bado vimevaa dipers kisiasa kujigonga na kujipendekeza kwangu wasijue sipendi kamchezo haka ka kitapeli na kifwala. Sitaki kukwezwa wala kupewa sifa nisizo kuwa nazo. Unakuta jitu zembe hata kufikiri eti nalo linataka kuniingiza cha kike kwa kunipa sifa za kipuuzi. Mtanisifu nikiachia ngazi a uni kugeuza bunga na zwazwa kama nyinyi? Mkome na kukomaa kabla hamjakomolewa. Juzi, niliona kitetemezi cha zwazwa moja nene mtandaoni eti likinisifu kwa kumpa ulaji dingi wake! Acheni vitegemezi visome na kujitegemea na siyo kutegemea majina ya ukoo. Eti linanisifia na kunipongeza kwa ajili ya dingi wake. Komeni huu mchezo ambao ni balaa kwa kaya kesho msipoangalia. Msiendekeze njaa na uzwazwa kana kwamba hakuna kesho.
        Pili, mafisadi, mafisi, na majambazi ya kisiasa wenye makandokando yanayonuka na kuwaumiza mafyatu tena kwa kupiga njuluku yao ndefu. Utakuta Fyatu linanuka uchafu wa kila aina yajapo maadili halafu eti linanisifia ili nifumbie macho uchafu na ukatili wao kwa Mafyatu wangu walio wengi. Mmenoa na mtaishia kuula wa chuya.  Hii mjizi na mijambazi inayonisifusifu inadhani sijui mazabe yake. Nayaona mengi kwenye mitandao ya kijamii yakijikomba kwangu ili niyape uteuzi. Mengi utakuta ni mifyatu iliyokwisha retire na kuexpire ukiachia ile mivivu ya kufikiri iliyokosa ubunifu ikashikilia umdudu,ushamba, na uzwazwa. Japo nimekuwa najifanya siyanyaki haya machezo, nayanyaka na kuyanyamazia kwa muda. Acbeni ujambazi na wizi na siyo kujificha kwenye kunisifiasifia. Sisifiki wala sipendi sifa kama wale wapenda sifa uchwara. Hamjui kuwa kupenda sifa ni aina fulani ya ugonjwa wa akili na utumwa licha ya kuwa uzwazwa?
        Tatu, wenye shahada, vyeti feki na za kununua au kuzawadiwa kimchongomchongo. Hawa nina maya nao hakuna mfano. Unakuta jitu liliogopa umande halafu linanunua PhD na kuanza kujiita daktari. Mnaujua ugumu wa kuupata huo udaktari au ni uzwazwa unawasumbua? PhD siyo ya kila mmoja bali wachache kama mie Fyatu Mfyatuzi ambaye ninazo magunia tena za kusotea siyo kununua au kupewa.
        Nne, wanaopenda eti kuniombea. Mnaiombia kwani mie maiti hadi niombewe au mnajiombea kwa kujifanya mnaniombea? Hapa haombewi Fyatu. Kama kuomba, najiombea mwenyewe. Siko tayari kuombewa na mifyatu yenye midhambi inayonuka hakuna mfano. Kama kuomba dili, basi jiombeeni kwanza niache kuwapiga na kuwahangaisha nyambaff wakubwa nyie. Utakuta haya yenye magunia ya madhambi yanayojitia kuniombea yanatenda dhambi kila uchao. Yapo mauza mihadarati, mazinzi, maongo, mafitini na kila balaa halafu eti yananiombea. Mnadhani Sir God ni zwazwa kama nyinyi? Mkome kabla sijawaombea muungue mkiwa hai.
        Tano, wapendao kunipogeza hata kwa upuuzi. Mbali na kusifiwa, napongezwa hata nikipiga chafya. Haya mazwazwa yanifanya niwe na uwezo wa ajabu. Yananifanya tajiri kuliko hata Ilon Musk yule mbaguzi wa kwa mzee Madiba aliyeukata kule kwa Joji Kichaka. Lisrikal langu likitimiza wajibu wake kama vile kutoa huduma za kijamii, nasifiwa mimi kana kwamba njuluku inayotumika ni yangu. Utayasikia yakisema “Mheshimiwa Mpendwa na Msikivu sana Fyatu amefanya hili au lile.” Komeni. Natumia njuluku za Mafyatu ambazo nyingine nazipiga, sorry, nazitunza.
        Sita, wanaonizeesha kwa kuniita dingi yao. Fyatu ni dingi wa vitegemezi vyetu na bibi Mkubwa siyo dingi wa wote. Kama hamuwajui madingi zenu, nendeni kaulize waliowazaa wawambie kuliko kunipakazia uzinzi wa kuzalisha kila jikombaji, tapeli, na zwazwa.  Kama ilivyo kwenye sifa za kipuuzi, nikachia ulaji mtaendelea kuniita dingi wenu? Unafiki na utapeli mtupu. Kwani, mnanifanya mie hamnazo au kipofu ambaye siwezi kujua wala kuona wengi wa wanaoniita dingi wao ni wazee kuliko mimi? Niliwazaaje wakati walizaliwa kabla sijazaliwa? Kama kuwa dingi wa kila Fyatu ni dili basi, kawatafute wapenda sifa majuha na mazwazwa muwaite dingi zenu. Nimechoka na sifa hizi za kikumbaff.
        Sasa nimalizie. Nawashauri wote wanaofanya hayo hapo juu wajue:
Mosi, siyapendi wala kuyahitaji hayo machukizo na usanii wanavyofanya kwa namna yoyote.
Pili, hayatawasaidia kwa vile hawatafanikiwa kuniingiza mkenge kizwazwa hivi. Hivyo, wakome kabisa.
            Tatu, najua kila machezo yote. Hivyo, wasiendelee kufanya hayo. Kwangu, hayatawasaidia zaidi ya kuwaumiza. Kama wana ugonjwa wa kuyafanya hayo, nawashauri wakawatafute wasiowajua na wanaoyapenda tokana na kukosa sifa na kutojiamini. Mie ni bonge la msomi tena profesa wa kweli.
Nne, mimi siyo Mungu wala muungu bali Fyatu wa kawaida mwenye udhu hakuna duniani. Hivi wakijua ukweli kuwa huwa nafaidi sifa
watanifanya nini? Kumbe bangi!!
Chanzo: Mwananchi Jtano jana.

Vitu muhimu kufikiria kabla ya ndoa


Japo tumewahi kugusia kwa mbali na, kwa ufupi kudurusu, kujadili masuala yafuatayo kuhusiana na ndoa hasa mambo muhimu kudurusu na kujua kabla ya kuamua kufunga ndoahatukuyajadili kwa undani. Sasa tunarejerea, Tunafanya hivyo kwa kujua wazi kuwa hatukuzama sana. Isitoshe, binadamu ni kiumbe anayesahau kirahisi. Hivyo, leo tutadurusu baadhi ya mambo ambayo hatujawahi kuyagusia kwa undani na upekee kuhisiana na ndoa hasa kwa wanandoa ambao wanatarajiwa au hawajingia kuingia kwenye ndoa. Haya mambo ni ya kawaida  ila muhimu sana. Hivyo, ni bahati mbaya na kawaida kutoyazingatia tokana na sababu mbali mbali ziwe za bahati mbaya au makusudi.
            Tuanze na dini. Japo hatupendi kuingilia mambo ya dini japo nayo yanaingilia mambo ya wengine, tukiri. Katika maisha hasa ya ndoa, huwa hapakosi migawanyiko, ubaguzi wa kidini au udini, na mengine kama hayo. Dini ni suala mtu binafsi tena nyeti na tata kwa jamii zilizopokea dini za kimapokeo ambazo zimetugawanya sana japo tunajitahidi kuficha kana kwamba kila kitu ni shwari.
Mosi, dini zote za kimapokeo zinachukiana na kushindana kutafuta wafuasi ili kujipatia kipato na uhalali. Hivyo, kwa waliozipokea, hujikuta wakiwa wahanga hata kwa mambo ambayo si hawajui tu bali hata hayawafai. Ndoa pia haiepuki mambo haya.
            Pili, dini husika, licha ya kuzuia au kuweka mazingira magumu kwa wafuasi wake kuoa au kuolewa na wafuasi wa dini pinzani, ni changamoto kubwa tu. Mfano, mkristo au muislam haruhusiwi kumuona kuoa asiye wa dini yake hadi ambadili dini! Kwa wanaojua jinsi dini zilivyojikita kwa wahusika, kwa watu wa kawaida wasio wabishi, hili jambo ni gumu japo linawezekana. Tokana na ugumu na unyeti hata utata wake, tunawashauri watarajiwa waliomo kwenye dini tofauti kulizingatia hili kwa makini kabla ya kufunga ndoa.
            Tatu, japo binadamu ana uwezo wa kuishi popote akiamua, jiografia ina mchango mkubwa katika kufaniksiah au kutofanikisha hili. Hii maana yake ni kwamba tumejikuta tukizaliwa tulipo bila kupanga wala kuchagua. Hivyo, kabla ya kuamua kuoa au kuolewa, ni vizuri kujua jiografia ya unapokwenda kuishi kwa wale wanaoungana na wenzao au mwenzio anakotoka. Hii ni kwa sababu jiografia na mazingara yetu huathiri kwa kiwango kikubwa mila na tabia zetu tunapokuwa kwenye maeneo tofauti.
Katika utafiti waliofanya Chuang na Capellan (2025) wanasisitiza kuwa tusidharau au kuisahau jigorafia kwenye ndoa kama sehemu mojawapo ya maisha isiyoepukika. Kwani, ina athari, japo fichi, kwenye ndoa. Hebu fikiria. Mgogo, Mnyanturu, Mrangi,  au Msukuma anajikuta Arusha, Karatu, Lushoto, Manyara au Mbeya kwenye baridi tofauti na kwao kwenye joto.  Mbali na hiyo, mhusika kazaliwa na kukulia kwenye tambarare na ukame. Ghafla bin vuu, anajikuta kwenye miinuko na milima yenye kijani na vito kila mahali. Vaa viatu vyake, ungekuwa wewe, ungejisikiaje?
            Nne, tujue. Hakuna jambo ambalo linafanyika bila malengo. Ndoa, kadhalika, ina malengo na matarajio ya muda au ya kudumu. Ndoa si jambo wala tarajio la muda bali la kudumu. Unapoamua kuoa au kuolewa, lazima uwe na malengo, matarajio, na ndoto unavyolenga kukamilisha na kutimiza.
            Tano, tunaweza kujidanganya na kujisahaulisha ili tufanikishe mambo yetu. Baada ya kujieweka malengo unayolenga kukamilisha, lazima ujiulize swali moja kuu. Je, haya malengo yangu yanafanana au kwendana na malengo ya mwenzangu? Hapa, lazima ujue malengo ya mwenzako ambaye pia anapaswa kujua yako. Ndoa ni safari ya maisha. Lazima wawili wasafiri pamoja kwa ukaribu. Pia, lazima waelekee upande mmoja na kushuka kwenye kituo kimoja.
Sita, kuna suala hili la mila. Hapa, tunamaanisha imani na mambo ambayo yote  madogo na makubwa tuuafanyayo kwa sababu ima tumeyarithi au tumeyaamini kama vile mila za asili na dini za kimapokeo. Mara nyingi, huwa tunafanya mambo haya bila hata kufikiri wala kujua Japo tunaweza kuvidharau au kuvipuuza vitu hivi, vina mchango mkubwa katika maisha ya ndoa.
            Tumalizie. Yaliyojadiliwa hapa ni muhimu katika maisha ya binadamu kwa sababu ni sehemu yake iwe utambulisho au hisia zake za ndani au psyche kwa kimombo. Hivyo, ukiyapuuza, hayatakupuuza.
Chanzo:Mwananchi Jpili juzi.


Thursday, 2 July 2026

Tuchangamkie misaada dunia imebadilika kkkk!

 

 Kabla ya kutongoa, nakusihi. Jikumbushe kisa cha ‘sizitaki mbichi hizi. na rumba la Madilu System’ Hii, ni kwa wale waliosoma enzi za Mchonga kabla ya UPE na uholela baada ya hapo. Sungura zwazwa, japo aliyejihisi mjanja. bila kuzingatia ufupi wake na uwezo wake mdogo wa kuruka, alitaka kula ndizi. Akiwa kwenye mishemishe zake si aliona ndizi mbivu! Alijaribu kukwea mgomba azinyakue na kuzifaidi asifue dafu. Hivyo, japo ndizi zilikuwa mbivu, alisema ‘sizitaki mbichi hizi.’ Juzi, nilimsikia fyatu–––si sungura aliyenikumbusha kisa hiki na mafunzo lukuki.
        Kwanza, sikuamini kuwa mja aweza kuwa kama mnyama achilia mbali mdudu. Hayo, tuyaache. Ni kujiuliza na kujijibu. Je, unawezaje kuwa juha kama sungura zwazwa katika kisa hiki?
        Pili, niulize kifyatufyatu, tena kwa unyenyekevu. Je, amelijua hili leo au ni baada ya kupigwa pini kutokana na mazabe na ufyatu vya kufuja hiyo misaada?
        Tatu, je, haya yalitoka moyoni au ni rongorongo mdomoni kuwazingua na kuwazuga mafyatu wabebao zigo la misaada au ni ‘sizitaki hizi mbichi’ baada ya kutofikika na kushikika? Mwenzenu nahitaji misaada. Maana, bila misaada, sitaweza kuwatawala mafyatu.
        Nne, je, kama yalosemwa ni kweli, nini mikakati ya kujitegemea ili kuachana na utegemezi kama si aina fulani ya utegemezi kiakili au kujifyatua ufahamu kwa vitu vilivyo wazi? Kuongopa ni vibaya; vibaya zaidi ni uongo wenyewe unapokosa mashiko na ushawishi na kukinzana na uhalisia. Bila misaada, mafyatu wanaozaliana kama hawana akili nzuri nitawalisha nini? Naomba maelezo fikirishi na tunduizi yasiyo na utundu na rongorongo uchwara.
        Tano, je, mafyatu waliogoma kufyatuka kuwafyatua wanaowafyatua kama huyu wana jeuri, uwezo, na utamaduni wa kujitegemea? Je, kati ya hawa tegemezi wapewa misaada wakaifuja na waitoawao, nani kapitwa na wakati na nani abadilike?
         Sita, tuwe wakweli. Je, kwa sanaa na mazingaombwe haya, mhusika atanya kweli au ni kufuruhisha kijiwe au ataramba matapishi yake kama yule aliyewahi kubweka akahoji wasiohojiwa eti ‘nyinyi ni nani’ asijue ni mafyatu?
        Saba, je, mafyatu, japo hawafyatuki na kufyatua wapaswao kufyatuliwa kama  huyu ni mataahira hadi kuamini upupu utokanao na ulevi wa maulaji na ukosefu wa busara? Nani anaweza kuishi bila misaada wakati misaada ni sera?Je, kati ya walaji na waliwaji nani aishiye kwa misaada?
           Nane, wakati tukiwakamia na kuwandia watoa misaada, tujiulizwe swali rahisi tu. Je, nani anamwendea nani kati ya mtoa na mpokea misaada? Ama kweli, wahenga walisema, shibe ni mwana malevya na njaa mwana malegeza!
        Tisa, inakuwajekuwaje fyatu mzima anafyatua vitu visivyoingia hata kwenye ubongo wa kuku? Nani anamfyatua nani kwa urongo huu mchana kweupe? Kweli kupe anaweza kusimama na kusema ‘sasa kutegemea damu mwisho kwa vile ng’ombe wamegoma kunyonywa? Tunaambwa dunia imebadilika? Imebadilika vipi na tangu lini na kwanini wakati huu?
            Kumi, Fyatu ni muumini wa ukweli hata uwe mchungu kiasi gani. Tuache masihara. Tunaacha utegemezi kwa mipango ipi ya maana na inayoingia akilini? Tunaachaje utegemezi bila kuacha upigaji njuluku za mafyatu na matumizi ya hovyo? Juzi, fyatu Tarampu kakinukisha pale Ghuba hadi wese likapanda na kuadimika. Je, mafyatu tumeacha kupenda misafara mirefu ya ndinga hata kwenda kwenye jando na unyago? Je, tumeacha kulindana hasa pale misaada inapopigwa na wapigaji? Je, tunachapa kazi au kuchapa soga kama kudai eti dunia imebadilika, hivyo, nasi tubadilike bila kubadilika zaidi ya kutoa matamko yasiyoingia hata kwenye ubongo wa chawa na funza?
            Kumi na moja, tembo japo ana maguvu mengi ya kuweza kuangusha miti na magogo, hana hata kibanda cha kuweka ubavu wake. Anazidiwa na ndege. Pamoja na kuwa na ubongo mdogo usiojaa hata kwenye kijiko, nyuni hujenga kiota chake na akautononoa usingizi na vifaranga vyake. Mamba, pamoja na maguvu yake, humeza kila kiingiacho mdomoni. Kuku hula asichozalisha na kuzalisha asichokula. Nani huyu fyatu akumbatiaye ukuku na akijiona mjanja kama sungura katika kisa cha sizitaki mbichi hizi?  
            Kumi na mbili, wakati tukijihadaa na kujiridhisha kuwa tunawahadaa mafyatu kuwa tutaanza kujitegemea, twapaswa kujiuliza. Nini mbadala wa kuishi bila kutegemea misaada wakati tangia kale na kale, tumekuwa tukiishi kwa kutegemea misaada tusijue tutalipa vipi? Je, kwanini hatuwaelezi mafyatu ni kwanini tuliishi kwa ku misaada ilhali Mwenyezi God alitujalia raslimali lukuki au ni yale ya kuku kuzalisha mayai akaishi kwa nafaa kavu isiyo na virutubisho? Nani huyu tumuone aishie bila kutegemea misaada? Je, ukweli na uhalisia ni vipi katika hili?
            Wakati mwingine kunyamaa ni bora kuliko kufyatuka usijue uwafyatuao nao wana akili. Heri alaye kimyakimya kuliko alewaye maulaji hadi akapayuka na kufyatuka visivyofyatulia.
Mnaochukia misaada siwalazimishi kuipenda. Mie na misaada ni kama samaki na maji.
            Hizi bange! Hivi, naongelea nini? Kumbe najiandaa natunga kitabu cha ‘Hadithi za Fyatu na Fyatuzi!’  Plizi, usisome upuuzi huu.
Chanzo: Mwananchi J'tano jana.

Tuesday, 30 June 2026

Tusiwacheke na kuwahukumu watalaka



Kawaida, wawili wafungapo ndoa hutegemea kuishi pamoja hadi kifo kiwatenganishe. Haya ndiyo maneno wasemayo katika viapo vya ndoa kwa wakristo. Kwa imani nyingine, hatujui. Hata kama hawatamki au kutamkiana haya maneno, tunaamini wote wanaofunga ndoa hutegemea kuishi pamoja maisha yao yote. Hapa, swali ni je, ni kwanini ndoa huvunjika japo si zote? Hili swali, japo ni fupi na dogo ni gumu na halija jibu moja.
            Tujuacho ni kwamba kudumu au kuvunjika kwa ndoa ni matokeo ya mambo mengi hata majaliwa, hasa wawili wanafungapo ndoa bila kujua wanachofanya japo wanaweza kujihisi wanajua wasijue hawajui. Pia, yapo mambo mengine mengi ambayo ni matokeo ya matendo au tabia za wahusika. Hivyo, kudumu au kutodumu kwa ndoa ni mkusanyiko wa mambo mengi makubwa na madogo.
            Tokana na uzoefu, kitu tunachoweza kusema ni kwamba wanaojenga ndoa ndiyo hao waidumishao au kuibomoa. Mfano, wawili wanapofunga ndoa, hufikia uamuzi huu wao peke yao tena bila shuruti. Hivyo, kila matokeo ya ndoa huwategemea wao. Hata hivyo, pamoja na kuamua wenyewe peke yao, wapo baadhi ya ndoa ambao huigeuza ndoa kama klabu au ushirika. Hii maana yake ni nini? Bahati mbaya, wahusika huwaruhusu wasiohusika kujihusisha na ndoa yao. Kimsingi, wawili husahau kuwa ndoa ikidumu au kuvunjika, wanufaika au waathirika ni wao na si hao waliowahusisha.
            Katika suluhisha migogoro mingi ya ndoa au kushuhudia zikivunjika, tumejifunza mambo makuu manne.
Mosi, wote huumia hata kuumizana tokana na pigo au hasara wanayopata tofauti na walivyotegemea wala kupanga. Asikudanganye mtu kuwa anaweza kuacha au kuachika akasherehekea japo, siku hizi, kumezuka uongo wa walioachika au kuacha kujifanya wanasherehekea. Ndiyo, wanaweza kutuonyesha kuwa wanasherehekea usoni. Ila nyoyoni wanaumia. Hili, halina mjadala. Jiulize. Walipofunga ndoa walihuzunika au kufurahi? Jibu liko wazi. Sasa inakuwaje waathirika hawa washerehekee hasara na pigo kubwa kama hili?
            Pili, wote uhisi hasara na hata mapungufu. Kwanini wengine waweze sisi tushindwe? Binadamu, kiasili, anapenda mafanikio na kuchukia maanguko. Hivyo, ndoa inapodumu, wanandoa huona fahari na furaha. Ikivunjika, hata wajikaze vipi, maumivu tena makubwa yapo. Kwanza, kuna wasi wasi wa namna jamii inavyowaangalia. Pili, kuna malengo na matarajio yaliyouawa. Na tatu, kuna aibu ya kushindwa tofauti na ridhiko la kufanikiwa. Mara nyingi, wengi walioacha au kuachwa hasa wenye watoto, hushindwa kuwashauri watoto wao juu ya ndoa kwa vile wao walishindwa.
            Tatu, ipo jamii inayowazunguka. Hapa, ndipo kichwa cha makala hii kinapoingia na kugusa pabaya. Wengi hasa wasiojua uhalisia wa ndoa wanaweza kuwacheka na kuwaona wanandoa ambao ndoa yao imesambaratika na kuvunjika kama watu walioshindwa. Hapa ndipo tatizo la kuwacheka wahusika au kuchekwa linapoanza. Kama tulivosema, wanaovunja ndoa ni wanandoa wengine wakisaidiwa na wasio wanandoa kwa namna mbalimbali. Je, kuna haja ya kuwacheka au kuwaonea huruma?
            Nani anajua kesho yake au nani ni mkamilifu kiasi cha kuwacheka wengine badala ya kuwaonea huruma na kuwasaidia? Kabla ya kuwacheka, vaeni viatu vya wahusika. Jiulize swali moja kuu japo dogo lakini lenye mafunzo makubwa na mengi “je, ingekuwa mimi, ningetaka wenzangu wanifanyie nini au kunichukuliaje?” Tuwe na huruma na utu. Badala ya kuwacheka wanandoa, tushukuru Mungu kuwa hatupitii wanayopitia. Tujifunze kitu toka kwao badala ya kuwabaghaza, kuwacheka, na kuwasimanga. Kwani, hujafa hujaumbika na kutenda makosa ni asili ya binadamu.
            Wanandoa ambao ndoa yao imevunjika ni kama wagonjwa. Hakuna haja ya kuwalaumu wala kuwasimanga bali kuwaonea huruma au kuwasaidia. Hakuna anayependa ndoa yake ivunjike japo wahusika wanavunja ndoa yao tokana na ujinga juu ya mambo fulani fulani yawe ya kimalezi, kitabia, kimahusiano, kiuchumi, kitaaluma, ubinafsi, uchoyo, upumbavu, hata kutojali mambo fulani fulani kwa wakati fulani.
            Tumalizie kwa kusisitiza kuwa kuwacheka wanandoa walioachana si kuwatendea haki. Maana, kitanda usicholalia hujui kunguni wake. Ni rahisi kuhukumu, kulaumu, hata kutweza. Je, ushawahi kujiuliza? Ningekuwa mimi, ningependa nichukuliweje hasa kipindi hiki kigumu na pigo kubwa katika maisha?
Kwani, si wote wanaoacha au kuachika huoa au kuolewa tena. Tuwaoneeni huruma watu hawa.
Chanzo: Mwananchi Jpili juzi.

           

Wednesday, 24 June 2026

Fyatu afaidi IEFUDI kwa raha zake!

Juzi, nikiwa napata kalaji si nikajifunza kitu. Kwanza, nilikasirika nusu niue fyatu. Nilichanganyikiwa hadi nikachanganyikana! Nikiwa ndo nimerudi kupata, si akaja afisa wa mamlaka ya kuibiana. Kumbe kuna jirani yangu mnoko alinichoma. Si niliuza vikuku vitatu tena kwa bei ya kutupa. Loh! Jamaa kanijia nyumbani eti kutaka nimuonyeshe IEFUDI . Nilimuuliza IEFUDI  ni mnyama gani. Hakujibu zaidi ya kunitisha kuwa lisrikali litakamata kuku wangu waliobaki hadi nionyeshe IEFUDI . Bila ajizi, nilimuomba naye anipe hiyo IEFUDI yake kama siyo ukosefu wa ubunifu, ujambazi na wizi vya kichovu.
            Kwa uzwazwa wake alinijibu kuwa mie nilikuwa nani kumtakisha  IEFUDI  wakati yeye ndiye hiyo IEFUDI . Nilizidi kumchanganya. Niliuliza hilo lisrkali lake mbona halituonyeshi IEFUDI  linapopata misaada na kukopa likaihomola na kuondomola. Niizidi kumzonga anieleze nielewe kama wapigaji wa njuluku ndefu inayofichuliwa kila mwaka na KAG (Kagua, Aibisha, na Kuufyata), nao, wana hiyo IEFUDI . Jamaa zwazwa kweli. Si lilianza kupayuka utadhani kaya ya Fyatuland ni mali ya baba au mama yake. Baada ya kuona rongorongo zimezidi, nililipiga mkwara kwa kupiga simu ya mshirika wangu wa bedroom nikijidai ni mwanasharia wangu ili alishitaki na waliolituma.
            Huu ujambazi na wizi wa mchana umeniudhi sana. Mbona pale kwa Gabacho wanauza bidhaa zilizoisha muda wa matumizi. Je, hawa wa IEFUDI hawaoni haya au wanatuchukulia ufala na uzwazwa? Nani hajui kuwa Fyatuland ishauzwa zamani gani au wanataka kutuuza baada ya kutuchuuza? Mbona misongamano imezidi hadi makaburini? Je, kazi ya lisrikal ni nini au ni kutupiga Mafyatu wachovu? Kweli, wamejua kututenda na kututenza. Kuanzia leo, nataka kujua mwenye kaya kati ya wanakaya na walakaya ili kijulikane. Kama mbaya mbaya. Fyatu anaanzisha genge. Kila jizi, tena bila aibu wala adabu linakuja kudai sijui tozo la nini, sijui IEFUDI sijui utopolo na upuuzi gani. Je, namna hii twaweza kuendelea au kuendelea katika kutoendelea?
            Ngoja nizoze kiprofesoo. Hivi, tumeishiwa hivi kiasi cha kuhangaishwa na mafyatu wadogo na vitu vidogo wakati uchumi tunao tunaukalia na wachukuaji wanakuja na kujizolea? Je, Fyatuland siyo shamba la bibi tena bibi mwenye kipofu na taahira? Basi, tubadili jina iitwe Shambalabibiland kijulikane. Ajabu ya maajabu, hii mijizi inayokuja kutunyima raha haijui hata hiyo njuluku inatafutwaje. Kazi, kuja kutughasi na kutuibia. Nasi Mafyatu tuna dhambi. Kwanini tunakubali wizi huu wa nchana? Hii njuluku wanayozoa na kupiga wanaifanyia nini? Kazi yao ni nini au wanatugeuza kuku na mbuzi? Kwanini tujirahisi na kukubali kunyonywa hivi na chawa, kunguni, funza, luba, na wadudu wengine ambao siku hizi wamenenepeana wakati twakondeana? Hivi, nani alituroga  hadi tukajihisi wageni kwetu?
            Hapa, naongelea IEFUDI . Bado madude mengine ya kimchoromchoro yaliyotamalaki. Ajabu, haya machawa na ma IEFUDI yanayotunyonya na kutuuma yanajiita matumishi ya umma! Ni matumishi ya umma au ya kuuma Mafyatu? Kama unaona mimi kufuga vijikuku vitatu na kuuza nawe ukanijia na hizo IEFUDI  zako, jaribu ufuge uone cha moto. Huwa siachi kuudhika na kushangaa. Hii soma kimya kimya. Juzi, si kuna changu kaniuzia dhambi zake. Baada ya kumaliza kanchezo si alitaka nimpe ujira wake. Sikupinga wala kubisha. Nilimtaka anipe IEFUDI  yake ili nimlipe na kunipatia risiti. We! Hilo zegere, usipime. Dada wa watu alinifyatukia na kunitukana mitusi ya nguoni kama hakuwa na akili nzuri. Baada ya kumalizana aliponitishia angekwenda kudai kwa bi Mkubwa wangu, nilimlipa na kutoka nduki kama kibaka aliyekwapua cheni pale Migomigo.
Tuache utani. Kama ni hivyo, ili kutenda haki, na wala rushwa wakipokea mlungura lazima nao wawe na IEFUDI s na kutoa risiti. Badala ya kudai haki eti tunafundishwa kudai risiti wakati wanaosimamia hizo risiti nao haawatoi risiti. Uko wapi usawa na haki hapa au navyo vinaendelea kuwa machukizo mbele ya majizi wanene?
            Pamoja na kuichukia IEFUDI, siku hizi naanza kuipenda badala ya kuiponda. Kwani, nakata kanywaji bila kulipa. Nikiletewa vyupa,  navipiga kwa raha zangu. Baada ya hapo, akija muuzaji, namtakisha IEFUDI ili anipe risiti. Hivyo, hivyo, nimepiga kalaji dezo hadi wauza wakagutuka. Siku hizi, nikiingia tu na kuagiza, wanataka nilipe kwanza. Huwa nawatakisha IEFUDI. Maskini wengi hawajui hata hiyo IEFUDI ni nini! Hata niendapo kwenye vyoo za kulipia, huwa nadai wanipe IEFUDI . Huu ndiyo uzuri wa IEFUDI kwa wajanja kama mimi.
Hayo tuyaache. Kama ni lazima kuwa na IEFUDI s, basi, na wanene watoe risiti wanapokwapua njuluku za Mafyatu waliogoma kufyatuka wakawafyatua wanaowafyatua kila uchao. Bila kufyatuka na kufyatua, Mafyatu watafyatuliwa hadi waone kaburi. Hivi, hawa wanaotuuzia ulabu, nao wanazo IEFUDI? Haya si mmbo ya nchezo wala uchonganishi na uchocheaji bali jiani iliyohalalishwa na kuwa nyenzo ya wachache kutupiga na kutuumiza. Kesho, mtatwambia tutoe hata risiti za marehemu wetu waliozikwa miaka mingi iliyopita.
            Sina ugomvi na kukusanya njuluku na mapato. Je, Mafyatu wananufaika vipi na hayo mapato wakati kila mwaka KAG anaibua kashfa ya upigaji wa njuluku ndefu na majizi hayakamatwi wala kushitakiwa? Hapa, hatujaliwa tukijiona kweli? Tunahitaji sana kufanya mapinduzi ya kifikra. Hivi, naota au naweweseka!!! Kkkkkk!
Chanzo: Mwananchi leo Jtano.

Friday, 19 June 2026

Onyo Mafyatu wanaohoji ulaji na uhalali wangu


Kuna mafyatu katika kaya yangu ya Fyatuland waliofyatuka kwelikweli hadi wanataka kunifyatua kabla sijawafyatua. Siku hizi,  mafyatu wangu wana kamchezo ka kunifyatua bila aibu wala sababu. Si juzi, kajitokeza mmoja aliyetaka kunifyatua na kunivua nguo tena haradhani akiongelea mambo ya kale. Hakujua kuwa ya kale yananuka hata kama yaliwahi kunuka baada ya mafyatu kukinukisha. 
            Kwa vile nilikuwa na inshu nyingi kwenda zangu ughaibuni kutanua na kujinadi, nilimlia pini. Si kwamba nilimgwaya. Never. Muache. Ngoja nipoe. Lazima nnitamfyatua ashike adabu na adabu imshike akome na kukomaa. Senzi kabisaka. Akizidisha kiherehere na kiranga chake, namfyatua kwa kumtumia wasiojulikana wamshughulikie kwa vile anajulikana. Hapa lazima nimpopoea kabla ya kunipopoa. Akishupaza shingo, namslowslow polepole na anapotea milele. Anacheza nami! Inaonekana hanijui vizuri.Anadhani upole wangu ni woga asijue mie ni katili hakuna mfano.
Wakati akizoza, nilimuuliza tena kwa upole ‘manapata wapi jeuri kuhoji wasiohojiwa au kutaka kuwafyatua wasiofyatuliwa ila kuwafyatua nyinyi mafyatu ambao kumbe mkifyatua ni hatari eeh? Nadhani hawa wanatumwa na mabeberu waje kunibeberu wasijue mie siyo mbuzi jike bali  beberu lenyewe tena la kunuka na kukinukisha. Akawaulize wale wahuni waliojifyatua wakataka kunifyatua nikawafyatua wakasahaulika. Hawa mahuluku taabu wana taabu, we acha tu.
    Ngoja niwape inshu nzima. Tulikuwa na uchaguzi wa ndani siku zilizopita ambapo nilishinda baada ya wanoko fulani kutaka kuniengua nikaishia kuwaengua na kujisimika na kushinda kwa kishindo na vishindo na kuwaacha solemba. Baada ya kuona walitaka eti kugombea nami, nikaitisha kikao cha chata changu cha Chata cha Mafyatu (CcM) wakanipitsha bila kutaka pale walipotaka nitoke nje eti wanichinje nikagoma nao wakagwaya na kuniptisha bila kupingwa. 
    Tokana na kuwafyatua mafyatu waliotaka kunifyatua, si kuna mafyatu waliojitokeza kunipaka matope. Si walihoji kuwa nilishiriki uchaguzi sijui uchakachuaji sijui uchafuzi, wala sijui. Kwanza, walitaka eti yapelekwe majina kadhaa kwenye kamati kuu inikamate! Kuona hivyo, nilichenji gea angani na kufyatua taratibu zote za chata letu. Badala ya kufuata katiba, niliamua kuifyatua na kuwafyaulia mbali hadi nikashinda ulaji kihalali na kwa kishindo japo mafyatu adui wanadia kuwa nilishinda kwa fujo, ukatili, na mambo mengine ambayo sitaki kuyarudia. Unawezaje kushinda kwa asilimia 1000 kama kweli kuna kamchezo ulifanya? Mie napendwa na kukubalika bwana. Hata kama ndege na wadudu wangeruhusiwa kupiga kura, wangenichagua mimi chaguo na kipenzi cha Mungu Dk. Dk. Dk. Daktari, Profesa, Shehe, Askofu, Field Marshall, Jenerali, Al haj, Mtakatifu Fyatu Mfyatuzi Esq n.k.n.k.
    Ilibidi nijiapishe mwenyewe tena kwenye chumba chetu cha kulala na bi Mkubwa. Waweza kuamini? Wengi walizoza na kusema eti haya yalikuwa maajabu na matokeo ya uchakachuaji. Kwani, niliwazuia wasichakachue? Walitaka niapishwe kwenye uwanja wa mpira wanipopoea kwa mimawe nami niwaslowslow kama siyo kuwapoteza. Mie ni mtu wa Mungu na mcha Mungu hakuna duniani isipokuwa mimi. Kawaulize wale mashehena wanaonijua. Si waliwaasa kuwa baada ya kuumbwa mwana wa Maria na Ntume, hakuna kiumbe bora mwingine aliyeumbwa isipokuwa Fyatu Mfyatuzi mjukuu wa Mfyatuko? Walidhani hawa wanaweza kuongopa?
    Baada ya kuwazidi kete mafyatu uchwara nilisikia wakilalamika. Mara chata kililazimisha mgombea wake wa urahis hata kwa kuvunja na kuvuruga kanuni zake chenyewe. Eti chata letu lilipoteza njuluku na muda kutupigia makelele kwa kisingizio cha kampeni za uongo na vitisho. Wamezoza na kuzua mengi. Mara eti chata letu linadai linadumisha amani kwa kuivunja tena kwa miaka mingi tena kwa kuongoza kwa fujo. Ebo! Bila fujo waweza kuongoza au kuongozwa? Wanadai ninawaminisha kuwa nitatenda haki wakati ni bingwa wa kudhulumu, kuteka, kupoteza, na kuua. Wanadai najiridhisha kutaka kuwaridhisha kuwa nilivyofanya ni sawa.  
        Nalaumiwa kwa kusifiwa na kujisifu hata ninapostahili kulaumiwa na kulaaniwa! Ebo! Hamjaambwa raha jipe mwenyewe? Nisipojisifu, nani atanisifu? Nilizuliwa eti nawanyanyasa wapingaji wangu. Ebo! Mlitaka niwaache waninyanyase hata kupoka ulaji wangu wa dezo!  Nani yuko tayari kufua nguzo zake za ndani hadharani tena mbele ya maadui zake huyo? Japo mafyatu wanasema niko uchi nikijidanganya nimevaa, nasema sibadiliki.
Hakuna umbea na urongo vimeniudhi kama kudai niligombea na kivuli changu. Walitaka nigombee na nani wakati wao ndiyo vivuli vyangu? Si wapo waliosusa sie tukajitwalia na kujilia wakabaki kulalama na kulaani wakidhani kelele za chura zinamzuia nguruwe kunywa na kunya kwenye kisima. Lo! Imkula kwao.
Kwa vile naipenda sana Fyatuland kiasi cha kuwa tayari kuua, sorry, kuuawa kwa ajili yake, sitasikia kelele za vyura. Naendela kukandamiza na kutanua na kutesa wakati mafyatu wanajifyatua na kulalamika wakati mie nazidi kuziba masikio.
Kwa hiyo, natoa onyo la mwisho. Komeni kuniandama. Nendeni mkaandamane mkione cha moto. Kula na kutesa ni kwa zamu. Ngojeeni zamu yenu. Tumeelewana? Lo! kumbe nililewa chakari hadi nikalala mtaroni!
Chanzo: Mwananchi Jtano juzi.

Wednesday, 10 June 2026

Fyatu aanzisha vita ya ‘lapdogs’ na Tarampu


Baada ya mtanange wa ghuba ya Ua Jeni kukaza, si Tarampu akajifyatua ufahamu na kuanzisha vita ya lapdogs na Fyatuland! Japo Tarampu ni fyatu uchwara, si aliwafyatua lapdogs wangu eti wasiende majuu kujienjoi! Nilipata habari hii mbaya nikiwa pipani nikielekea majuu kwa Put in. Nsharejea wanoko msianze kutafuta mambo yangu na kunifyatua. Sikujua kuwa Tarampu anafyatuka vibaya. Si aliamua kuwafyatua lapdogs eti kwa vile walirarua wanakondoo! Alisema wasikanyage Umarekanini! Nilishangaa sana. Kwani, wanakondoo wangu wanamhusu nini yarabi? Kutaka sifa na kukimbia kipigo cha maajemi si Tarampu akajifyatua na kuwafyatua bila kujali kuwa wanafanya kazi zangu! Ukijifyatua na kunichokoza au kutaka kunifyatua, nawaamuru wakufyatue haraka sana.
Kwa vile mie ni Fyatu zaidi ya Tarampu, nilimuonya. Kama ataendelea na ufyatu wake uchwara, nitazuia wake kuingia Fyatuland. Akiendelea nampiga marufuku hata yeye kuingia Fyatuland. Mambo ya Fyatuland yanamhusu nini au anadhani mie ni kama Maduro aje animaduro? Athubutu aone kilichofanya ngamia kuwa na nundu. Shauri yake.
Nimegundua kuwa Tarampu ni mwoga wa kaiwada na bingwa wa mikwara uchwara. Huenda anatingisha kibiriti kwa kutumia vita ya lapdogs ili anifyatue au anaogopa kunifyatua. Vinginevyo anataka kunitia kashkash ili apata namna ya kuifyatua Fyatuland kama alivyoifanyia Venezuela. Maana, haiinigi akilini ang’ang’anie kufyatua lapdogs ilhali mwenyewe nipo. Najiuliza bila majibu. Inakuwaje?
Huwezi kung’atwa na chawa ukawalaumu zaidi ya yule aliyewafuga au kuacha kuwateketeza. Mnaninyaka hapa? Imenishangaza sana. Eti dogii kuwararua wanakondoo anaadhibiwa bila kujali nani alimwamuru awararue! Kwani kazi ya dogii ni nini kama siyo kuwafyatua wengine kwa amri ya mwenye kumfuga? Nadhani amewaonea wivu lapdogs wangu niliowalisha wakanenepeana wakati wake wanakondeana. Kama siyo hivyo, basi uzee unamuijia vibaya. Haiingii akilini. Unamuadhibuje mbwa na siyo mwenye mbwa? Kweli, hii ni haki? Wahenga waliasa kuwa ukimuona dogii, jua kuna mwenyewe. Na dogii hafanyi kitu bila amri ya mwenye kumfuga. Inakuwaje unamwadhibu mbwa na kumuacha amfugaye? Kwanini kumfyatua mjumbe wakati aliyetuma humfyatui?
Sasa natangaza vita. Natangaza vita ya wanene na siyo  guard dogs wao. Kama ataendelea kubwekabweka, nitamfanyia kitu ambacho hajawahi kufanyiwa Fyatu yoyote. Huwezi kuwaandama lapdogs wangu nami nikakuacha. Hapa, Tarampu ajue. Tutafyatuana hadi kieleweke.
Inaonekana wadukuzi wake ni wavivu wa kufikiri na kudukua. Kama hajui ni kwanini wanakondoo walifyatuliwa na attack dogs wangu si aniulize nimpe inshu nzima badala ya kutishiana kufyatuana na asifyatuke na kufyatua. Kwanini Tarampu hataki kukubali kuwa wanakondoo walivyatuliwa kwa sababu walitaka kujigeuza mbwa mwitu halafu wanifyatue?
            Kwanza, namjuza Tarampu na wengine wanaojifyatua ufahamu. Wajue na wakome na kukomaa. Lapdogs wangu si washari. Ukiona wamewafyatua wanakondoo, ujue kuna kitu wanakondoo walitaka kufyanya. Maana, haiingii akilini kuwaacha wanakondoo waliozoea kuishi kwa amani kujigeuza mbwa mwitu. Ili iweje kama siyo kunifyatua mie mwenye kuwatunza?
            Pili, namuonya Tarampu na wenzake wanaodhani wanaweza kunifyatua. Najua. Wameanza na lapdogs wangu ili baadaye nifuate. Sitakubali. Tarampu, who are  you? Kama wana kondoo wangekuwa wake, lau angekuwa na hoja. Mambo ya Fyatu amuachia Fyatu mwenyewe. Hayamhusu hata kidogo.       
            Tatu, hakuna kondoo walioraruriwa toka Fyatuland. Waliofyatuliwa ni wa kaya ya jirani waliofyatuka na kutaka kuwafundisha umbwa mwitu kondoo wangu waaminifu na wasio na hatia wala washari.
            Nne, namuonya kwa mara ya mwisho Tarampu. Asitake kutuletea ubeberu na kujitia ufahari asijue nasi tunauweza huo ubeberu wake. Tarampu ajue. Mie simshobokei wala kumnyenyekea eti kwa vile ana njuluku. Si alikata misaada kwa Fyatuland baada ya kukataa ubeberu uchwara wake. Kuna Fyatu amekufa kwa kukatiwa hiyo misaada yake?
            Tano, Tarampu ajue hanitishi. Na kama ni ufyatu mie ndo mfalme wa Mafyatu akiwamo yeye. Lazima tuheshimiane. Aniheshimu. Aheshimu dog wangu. Akiendelea kujifyatuafyatua, nitamuwekea vikwazo vya kiuchumi. Angejua kuwa kupeleka lapdogs wangu kwenye kaya yake kulikuwa kunamuingizia njuluku kibao, asingejifyatua na kutaka eti kuwafyatua dog wangu wapendwa.
            Sita, kama Tarampu ataendelea na ubeberu wake, nitaanza kufanya mipango ya kutengeneza bomu la nyukilia ili kiumane. Anadhani siwezi? Akamuulize Kiduku ambaye amekuwa akimtoa jasho. Hapa, sijagusia kwenda kwa swahiba yangu Xii Jin Pingu ampige pingu. Nlishaonya. Fyatuland inawenyewe na wenyewe ni sisi. Hatutishwi wala kuyumbishwa. Tunatesa kwa raha zetu. Hata kama nitaamuru attack dogs wawafyatue wanakondoo tena, yeye inamhusu nini. Si akafyatue wake waligeuka mbwa mwitu zamani kiasi cha kufyatuana wao kwa wao kwa vile dog wake hawana uwezo wa kuwafyatua.
            Mwisho, ni vizuri Tarampu akajuzwa na kujua. Sisi huku tuna haki za kila kitu kuanzia dog hata chawa. Tunaheshimu haki za viumbe wote kwa sharti kuwa wasijifyatue kutaka kutufyatua. Hapa, tutawafyatua kama tulivyoamuru dog wawafyatue wanakondoo.
            Du! Kwani, nimesemaje? Naongelea lapdog au madogii? Kumbe naota nikipata kichapo cha dirisha la Horumuziiii Uajemiii!
Chanzo: Mwananchi J'tano leo.

Wednesday, 3 June 2026

Fyatu Fwala na siasa za maji taka

Japo Fyatu Fala–––binafsi simjui –––ambaye wengi humuita mnene wa kiroho bila kumalizia, sawa na wengine wa aina yake, kuwa ni wa kujipa au kujipachika, amenifikirisha hata kunifyatua. Kwanza, nampongeza kwa ufyatu wake. Najaribu kumdurusu kwa sifa zake za utata alizoonyesha hivi karibuni. Huwa siandiki juu ya Mafyatu. Ila, leo, nimewiwa. Naufyatua mwiko niliojiwekea baada ya kusoma habari kuwa Fyatu tajwa amerejea Chandimu akitokea Chawalaji. Japo ni haki yake kuruka vyata, kwani katiba inaruhusu––– alinistua na kunitanza hadi nikafyatuka. Je, Fyatutajwa anakumbuka aliyosema aliposepa na sasa kujifyatua na kujirejesha baada ya kufyatuliwa na aliotoka kuwafyatua? Je, anajua kuwa na Mafyatu wana akili na kumbukumbu? Je, huu ni utoto au usanii kisiasa au? Nashindwa kujua. Hakuna kilichonigomba na kunifyatua kama sababu kinzani alizotoa na za kushangaza.
Sina ugomvi na wanasiasa wala watu wanaojitafutia riziki––––ila kwa kuwafanya wengine hamnazo–––hasa kwa kutumia kile ambacho marehemu Sam Sixx, microphone wa zamani wa njengo–––alichoita siasa za maji taka.
            Wote tunayajua maji taka. Ni machafu. Yananuka. Pia, yanakera kiasi cha kutushughulisha kuyaondoa katika makazi yetu. Kama maji ni hivyo, siasa za maji taka, hali inakuwaje? Tunaweza kuzomea waitwao machawa lakini tukawashabikia maji taka ya kisiasa wanaohamahama kwa kutoa sababu zisizoingia kichwani.
              Tujikumbushe. Fyatu tajwa alisepa miaka miwili iliyopoita. Kati ya mengi aliyosema ni kwamba Fyatuland hakukuwa na chata kama cha maulaji akikionya kutoshirikiana na wapingaji. Ajabu ya maajabu, ndani ya miaka miwili, ndoa imemshinda akaamua–––ila hata chembe ya aibu–––kuramba matapishi yake! Je, huy Fyatu anakumbuka aliyosema hapo juu na alichomaanisha au kulikuwa na namna?
                Wapo wanaodai Fyatu tajwa alitumwa kufanya ‘kazi maalumu’–––ipi ambayo sasa ‘ameikamilisha’ na kurejea nyumbani! Ajabu. Hii ni kumpa mhusika sifa asizostahili. Kwa wanaojua namna baadhi ya wasanii walivyo nyemelezi hata matapeli, hakubaliani na hili. Kwani, linawanyima kuaminika hata kuheshimika sawa na mwingine kama yule aliyewahi kusema kuwa kazi yake ya uchunaji na utapeli ni bora kuliko urahis. Ajabu, alipopitishwa kwa rafu kugombea unene jimbo fulani, alisahau sijui alichosema na kupwakia matapishi yake huku akiimba kila sifa hata zisizokuwepo.
             Kumjua Fyatu tajwa na wengine wa aina yake, turejee maneno yake hapo juu ukiyalinganisha na aliyosema ndoa ilipomshinda. Alinukuliwa akisema  kuwa ameamua kuachana na chamaulaji kutokana na unyotoaji uliofanyika juzi! Lahaula! Je, kuanzia wakati huo–––kama kweli analiyachukia na kuyapinga–––alikuwa wapi? Alingoja nini au alikuwa akivuta kamba lau apate mradi? Je, ameamua kutumia unyotoaji tajwa kupata ujiko kama mwenzake ambaye–––alipopigwa chini–––kuushupalia? Je, kufyatuka na kusepa vinaleta suluhisho?  Je, mauaji unyotoaji roho chanzo chake hakiwezi kuwa siasa za maji taka zilizojitenga na ukweli na kukumbatia uongo na uzushi? Ni jemedari gani hukimbia mapigano akidhani analeta suluhisho au ushindi? Natamani chata cha maulaji  wafyatuke  na kufichua walivyompokea, kumjua, kumchukulia, na kumtenza hadi ndoa ikamshinda akarejea alikokandia vibaya.
            Hapa, kuna maswali muhimu. Je, Fyatu tajwa na wengine kama yeye wanafuata sera au vyeo na ulaji? Je, kwanini ameamua kuramba matapishi yake na kujigeuza maji taka baada ya
            Kwa mtu wa kada ya Fyatu tajwa ya uchungaji kama siyo ‘uchunaji’, wengi walitegemea awe mkweli, mwenye maadili na si wa kusema hili leo na kesho, anajipiga mtama. Angeona lau hata aibu kuwa ni vibaya kwa Fyatu mzima tena ‘ wa God’ kuonekana kigeugeu, kizabazabina, na mtata kiasi cha kufanya siasa kuwa maji taka ambayo yakishachafuka, huwezi kuyarejesha kwenye usafi na usalama. Je, Fyatu tajwa, wenzake, waliompokea, na wamaomshabikia wanayajua haya au la? Je, anaweza kuaminika na kuheshimika tena ilhali akisema hili na kesho akasema kinyume chake kiasi cha kufanya wanaomsikiliza wasijue kati ya ukweli, uongo, na uzushi ni upi mbali na uchumia tumbo na usasi wa ngawira?
            Japo si kosa kwa Chandimu kumpokea na kumrejesha kundini Fyatu tajwa, je, hii haionyeshi kuwa baadhi ya vyata ni kama maabara ambayo kazi yake ni kufanyiwa majaribio? Je wanajua maana ya kuwa hivyo? Japo, Fyatu huyu si wa kwanza wala mwisho kufanya siasa hizi zinaoanza kuzoeleka, kuna haja ya wapiga kura na wananchi kwa ujumla kuweka nukta na kukumbuka matendo na matamshi ya wote wanaotuaminisha kuwa wanatufaa wakati hawafai wala kujifaa.
            Mwisho, kwa alichofyatua Fyatu, nashindwa kumuelewa wala kumpongeza zaidi ya kumpa pole. Maana, ana ndimi mbili. Isitoshe, kama ni upotezaji na unyotoaji roho, kwani, vilianza awamu jana? Je, ni unyotoaji roho gani ni muhimu kuliko mwingine tena chini ya chata lile lile? Je, Fyatu alikwenda kuwafyatua wenzake wakaishia kumfyatua? Maswali ni mengi kuliko majibu. Niwezacho kusema ni kutahadhari siasa za maji taka na wanasiasa maji taka.
Chanzo: Mwananchi, leo Jtano.
 

Wednesday, 27 May 2026

Twachukia mabeberu, kupenda, na kufanya ubeberu!

Tokana na ufyatu, leo naja kifalsafa kama mwanafalsafa nguli ambaye hajawahi kutokea isipokuwa mimi. Sipigi pembeni wala kuzungusha. Leo nipo na ‘mabeberu’ yanayowabeberu mabebera hadi wanalalamika kama vichanga mbali na kubumburuka tokana na kubumburushwa na mabeberu. Jamaa hawa wanatisha usipime. 
    Mabeberu, hayawani au mafyatu ni viumbe dhalili, hstari, na hovyo.Huchukiana, kushukiana, kuchukuliana, kuibiana, kuogopana, kuogopeshana, na kusingiziana. Huchukua vya wezao wakichukia vyao kuchukuliwa.Kwao, kila fyatu ni mbuzi jike.
Kwanza, kwanini mabeberu yaliitwa mabeberu na siyo madume? 
    Kwa waliowahi kufuga au kuchunga mbuzi, wanajua namna mabeberu yanavyowabumburusha majike lau kuijaza dunia na kutupatia nyama. Kiasili, mabeberu siyo viumbe wabaya. Maana, wasingekuwapo, hata nyama choma isingekuwapo.              Pamoja na nia na uzuri wao, mabeberu huwa yanafanya makeke na kusababisha mikikimikiki na mshike mshike hadi wapate wanachotafuta. Kila beberu akitaka mambo, utamsikia akibembeleza mbuzi jike bee bee beeebeee hadi mswahili anasema hili linabembeleza jike tu. Jamani, huu siyo ustaarabu uliokiuka hasa kwa dunia ya mafyatu wabakaji hadi wanabaka hata kaya? Kwa lugha rahisi, beberu hubembeleza jike tofauti na fahari ambalo hurukia tu na kupata mchezo.
            Tuachane na mabeberu mbuzi. Tuje kwa mafyatu. Kimsingi, kwa mafyatu, mabeberu si wamakonde bali watasha. Tena ni wakwasi usipime. Ukiwapendeza wanakupiga njuluku hadi unaona kuwa kubomu na kukopa ndiyo utaratibu wa maisha hasa kwa zile kaya uchwara zinazokalia mali na kuendekeza kubomu bomu na kukopa kopa. Mabeberu hupenda sana kaya hizi. Uzuri ni kwamba Fyatuland haimo kwenye kundi hili uchwara linalojivua nguo hadharani wakati mali linazo ila linazikalia.
            Japo tunawaponda mabeberu, ni kama tunajisahau kuwa huwa, wao, tofauti na mabeberu ya mbuzi, huwa tunajipeleka kwao wenyewe. Hivyo, sioni kama ni ufyatu badala ya uzwazwa kulalamika pale wanapoacha kutubembeleza. Hata hivyo, kila fyatu hata wadudu wanajua. Badala ya wao watubembeleze kama mabeberu wafanyavyo kwa majike, siye huwa tunawabembeleza pale unapotaka kuwatoa njuluku. Hapa, jina beberu hubadilika na kuwa mfadhili.                    
     Waswahili wana msemo kuwa mfadhili mbuzi, fyatu ana maudhi. Alichanacho fyatu, sawa na mabeberu, ni ukosefu na wizi wa fadhila. Ukimpa fyatu njuluku, unaitwa mfadhili, mdau, mshirika na majina mengine matamu. Hepu muulize kazitumiaje. We, utakoma. Utaitwa beberu kana kwamba una akili kidogo kama mbuzi. Huu nao upuuzi tena wa wazi ufanywao na mafyatu chizi wazijue twajua.
            Mafyatu wana mambo. Ukiwa mfadhili ukawanyima njuluku wanakunanga hasa unapostukia rongorongo zao juu ya namna walivyotumia njuluku ulizowafadhii au kuwakopesha. Ukiwastukia, jiandae. Ghafla watageuka na kujifanya hamnazo kama siyo kujitoa ufahamu waanze kukuponda pale walipokuingiza chaka kuwa wanakupenda. 
    Ama kweli, wasohaya wana mji wao. Si unajua sizitaki hizi mbichi? Japo wanajitia kulalamika lau waonewe huruma, mafyatu bumburushwa wana tabia kama ya mafahari aka madume ya ng’ombe. Tokana na ufahari wao, tena uchwara na kupenda ufahari wakati ni mafakiri wa kunuka, hujifaharisha hadi kujisahau na kuwadharau, kuwathumu, hata kuwatukana mabeberu wawapao fahari feki waipendayo na kuifuja.
                Utakuta mifyatu haichapi kazi. Badala yake inachapa majungu na starehe.Mingine inakwapua njuluku za mafyatu kwa mikono miguu na midomo utadhani itaishi milele. Mingine kazi yake ni kujikombokomba kama chawa na inzi. Halafu inataka eti nayo iheshimike au kufanikiwa kama kaya zilizoukata wakati kaya yao ikiendelea kuwa ombaomba na kopakopa! 
    Loo! Mingine inapiga njuluku tena ndefu ya mafyatu wenzao na kuishia ima kuifuja au kuificha ughaibuni. Mingine, inapoteza njuluku kuzurura kama yule habithi wa Kireno Vasco da Gama au yule Mbayuwayu wa zama zile aka Njaa Kaya. Halafu yakiambwe mfanyayo siyo yanagomba, kuzoza, kulalama, na kuwatukana wafadhili kuwa ni mabeberu. 
        Kama ubeberu ni rahisi, ujaribuni muone. Kama mabeberu ni wabaya, mbona mnajipeleka wenyewe? Kama mabeberu ni mabaya, mbona mnapenda nyama choma? Kwani waliofilisi kaya ni hao mabeberu au mabu na mafisi na mafisadi? Huwa nashangaa mafyatu wazima kuogopa mabeberu wakati mbuzi majike, pamoja na uhayawani wao, hawawaogopi. Wakipewa maji, wanatoa wana mbuzi na mafyatu tunakula nyama. Sasa hapa, ubaya wa mabeberu uko wapi?
            Tukiwa wakweli, nani si beberu tena hata wengine majike? Nazoza hivi kwa sababu mabeberu, licha ya kuwa mafahari, hupenda ufahari. Huwa ni shapu yanapotaka vitu. Yanaweza kupata kwa kudandia au kubembeleza beebeeebeeebebe. Kinachofanya nipende mabeberu, kwanza, huwa hayana chawa. 
        Pili, huwa si manafiki. Yakitaka kitu, kila kit uni mambo hadharani. Hamjayaona yanavyowakimbiza na kuwabeberu majike siyo?
Ukiachia mbali ubeberu kuonekana jambo baya hasa wale wanaoitwa mabeberu wanapostuka, hata wale wanaoukandia, ima wanao, kwa kujua au kutojua, au wanautamani na kuuonea gere. Nani asiyependa ubeberu ili awabeberu wenzake? Nenda kawaulize wahanga wa kweli wa ubeberu kama wale Gen Ziro wa kaya ya kufikirika jirani na Fyatuland. Du! Kumbe hii bangi kali!
Chanzo: Mwananchi Jtano iliyopita.