Kwa vile nilikuwa na inshu nyingi kwenda zangu ughaibuni kutanua na kujinadi, nilimlia pini. Si kwamba nilimgwaya. Never. Muache. Ngoja nipoe. Lazima nnitamfyatua ashike adabu na adabu imshike akome na kukomaa. Senzi kabisaka. Akizidisha kiherehere na kiranga chake, namfyatua kwa kumtumia wasiojulikana wamshughulikie kwa vile anajulikana. Hapa lazima nimpopoea kabla ya kunipopoa. Akishupaza shingo, namslowslow polepole na anapotea milele. Anacheza nami! Inaonekana hanijui vizuri.Anadhani upole wangu ni woga asijue mie ni katili hakuna mfano.
The Curse for Salvation
Friday, 19 June 2026
Onyo Mafyatu wanaohoji ulaji na uhalali wangu
Kwa vile nilikuwa na inshu nyingi kwenda zangu ughaibuni kutanua na kujinadi, nilimlia pini. Si kwamba nilimgwaya. Never. Muache. Ngoja nipoe. Lazima nnitamfyatua ashike adabu na adabu imshike akome na kukomaa. Senzi kabisaka. Akizidisha kiherehere na kiranga chake, namfyatua kwa kumtumia wasiojulikana wamshughulikie kwa vile anajulikana. Hapa lazima nimpopoea kabla ya kunipopoa. Akishupaza shingo, namslowslow polepole na anapotea milele. Anacheza nami! Inaonekana hanijui vizuri.Anadhani upole wangu ni woga asijue mie ni katili hakuna mfano.
Wednesday, 10 June 2026
Fyatu aanzisha vita ya ‘lapdogs’ na Tarampu
Kwa vile mie ni Fyatu zaidi ya Tarampu, nilimuonya. Kama ataendelea na ufyatu wake uchwara, nitazuia wake kuingia Fyatuland. Akiendelea nampiga marufuku hata yeye kuingia Fyatuland. Mambo ya Fyatuland yanamhusu nini au anadhani mie ni kama Maduro aje animaduro? Athubutu aone kilichofanya ngamia kuwa na nundu. Shauri yake.
Nimegundua kuwa Tarampu ni mwoga wa kaiwada na bingwa wa mikwara uchwara. Huenda anatingisha kibiriti kwa kutumia vita ya lapdogs ili anifyatue au anaogopa kunifyatua. Vinginevyo anataka kunitia kashkash ili apata namna ya kuifyatua Fyatuland kama alivyoifanyia Venezuela. Maana, haiinigi akilini ang’ang’anie kufyatua lapdogs ilhali mwenyewe nipo. Najiuliza bila majibu. Inakuwaje?
Huwezi kung’atwa na chawa ukawalaumu zaidi ya yule aliyewafuga au kuacha kuwateketeza. Mnaninyaka hapa? Imenishangaza sana. Eti dogii kuwararua wanakondoo anaadhibiwa bila kujali nani alimwamuru awararue! Kwani kazi ya dogii ni nini kama siyo kuwafyatua wengine kwa amri ya mwenye kumfuga? Nadhani amewaonea wivu lapdogs wangu niliowalisha wakanenepeana wakati wake wanakondeana. Kama siyo hivyo, basi uzee unamuijia vibaya. Haiingii akilini. Unamuadhibuje mbwa na siyo mwenye mbwa? Kweli, hii ni haki? Wahenga waliasa kuwa ukimuona dogii, jua kuna mwenyewe. Na dogii hafanyi kitu bila amri ya mwenye kumfuga. Inakuwaje unamwadhibu mbwa na kumuacha amfugaye? Kwanini kumfyatua mjumbe wakati aliyetuma humfyatui?
Sasa natangaza vita. Natangaza vita ya wanene na siyo guard dogs wao. Kama ataendelea kubwekabweka, nitamfanyia kitu ambacho hajawahi kufanyiwa Fyatu yoyote. Huwezi kuwaandama lapdogs wangu nami nikakuacha. Hapa, Tarampu ajue. Tutafyatuana hadi kieleweke.
Inaonekana wadukuzi wake ni wavivu wa kufikiri na kudukua. Kama hajui ni kwanini wanakondoo walifyatuliwa na attack dogs wangu si aniulize nimpe inshu nzima badala ya kutishiana kufyatuana na asifyatuke na kufyatua. Kwanini Tarampu hataki kukubali kuwa wanakondoo walivyatuliwa kwa sababu walitaka kujigeuza mbwa mwitu halafu wanifyatue?
Kwanza, namjuza Tarampu na wengine wanaojifyatua ufahamu. Wajue na wakome na kukomaa. Lapdogs wangu si washari. Ukiona wamewafyatua wanakondoo, ujue kuna kitu wanakondoo walitaka kufyanya. Maana, haiingii akilini kuwaacha wanakondoo waliozoea kuishi kwa amani kujigeuza mbwa mwitu. Ili iweje kama siyo kunifyatua mie mwenye kuwatunza?
Pili, namuonya Tarampu na wenzake wanaodhani wanaweza kunifyatua. Najua. Wameanza na lapdogs wangu ili baadaye nifuate. Sitakubali. Tarampu, who are you? Kama wana kondoo wangekuwa wake, lau angekuwa na hoja. Mambo ya Fyatu amuachia Fyatu mwenyewe. Hayamhusu hata kidogo.
Tatu, hakuna kondoo walioraruriwa toka Fyatuland. Waliofyatuliwa ni wa kaya ya jirani waliofyatuka na kutaka kuwafundisha umbwa mwitu kondoo wangu waaminifu na wasio na hatia wala washari.
Nne, namuonya kwa mara ya mwisho Tarampu. Asitake kutuletea ubeberu na kujitia ufahari asijue nasi tunauweza huo ubeberu wake. Tarampu ajue. Mie simshobokei wala kumnyenyekea eti kwa vile ana njuluku. Si alikata misaada kwa Fyatuland baada ya kukataa ubeberu uchwara wake. Kuna Fyatu amekufa kwa kukatiwa hiyo misaada yake?
Tano, Tarampu ajue hanitishi. Na kama ni ufyatu mie ndo mfalme wa Mafyatu akiwamo yeye. Lazima tuheshimiane. Aniheshimu. Aheshimu dog wangu. Akiendelea kujifyatuafyatua, nitamuwekea vikwazo vya kiuchumi. Angejua kuwa kupeleka lapdogs wangu kwenye kaya yake kulikuwa kunamuingizia njuluku kibao, asingejifyatua na kutaka eti kuwafyatua dog wangu wapendwa.
Sita, kama Tarampu ataendelea na ubeberu wake, nitaanza kufanya mipango ya kutengeneza bomu la nyukilia ili kiumane. Anadhani siwezi? Akamuulize Kiduku ambaye amekuwa akimtoa jasho. Hapa, sijagusia kwenda kwa swahiba yangu Xii Jin Pingu ampige pingu. Nlishaonya. Fyatuland inawenyewe na wenyewe ni sisi. Hatutishwi wala kuyumbishwa. Tunatesa kwa raha zetu. Hata kama nitaamuru attack dogs wawafyatue wanakondoo tena, yeye inamhusu nini. Si akafyatue wake waligeuka mbwa mwitu zamani kiasi cha kufyatuana wao kwa wao kwa vile dog wake hawana uwezo wa kuwafyatua.
Mwisho, ni vizuri Tarampu akajuzwa na kujua. Sisi huku tuna haki za kila kitu kuanzia dog hata chawa. Tunaheshimu haki za viumbe wote kwa sharti kuwa wasijifyatue kutaka kutufyatua. Hapa, tutawafyatua kama tulivyoamuru dog wawafyatue wanakondoo.
Du! Kwani, nimesemaje? Naongelea lapdog au madogii? Kumbe naota nikipata kichapo cha dirisha la Horumuziiii Uajemiii!
Chanzo: Mwananchi J'tano leo.
Wednesday, 3 June 2026
Fyatu Fwala na siasa za maji taka
Sina ugomvi na wanasiasa wala watu wanaojitafutia riziki––––ila kwa kuwafanya wengine hamnazo–––hasa kwa kutumia kile ambacho marehemu Sam Sixx, microphone wa zamani wa njengo–––alichoita siasa za maji taka.
Wote tunayajua maji taka. Ni machafu. Yananuka. Pia, yanakera kiasi cha kutushughulisha kuyaondoa katika makazi yetu. Kama maji ni hivyo, siasa za maji taka, hali inakuwaje? Tunaweza kuzomea waitwao machawa lakini tukawashabikia maji taka ya kisiasa wanaohamahama kwa kutoa sababu zisizoingia kichwani.
Tujikumbushe. Fyatu tajwa alisepa miaka miwili iliyopoita. Kati ya mengi aliyosema ni kwamba Fyatuland hakukuwa na chata kama cha maulaji akikionya kutoshirikiana na wapingaji. Ajabu ya maajabu, ndani ya miaka miwili, ndoa imemshinda akaamua–––ila hata chembe ya aibu–––kuramba matapishi yake! Je, huy Fyatu anakumbuka aliyosema hapo juu na alichomaanisha au kulikuwa na namna?
Wapo wanaodai Fyatu tajwa alitumwa kufanya ‘kazi maalumu’–––ipi ambayo sasa ‘ameikamilisha’ na kurejea nyumbani! Ajabu. Hii ni kumpa mhusika sifa asizostahili. Kwa wanaojua namna baadhi ya wasanii walivyo nyemelezi hata matapeli, hakubaliani na hili. Kwani, linawanyima kuaminika hata kuheshimika sawa na mwingine kama yule aliyewahi kusema kuwa kazi yake ya uchunaji na utapeli ni bora kuliko urahis. Ajabu, alipopitishwa kwa rafu kugombea unene jimbo fulani, alisahau sijui alichosema na kupwakia matapishi yake huku akiimba kila sifa hata zisizokuwepo.
Kumjua Fyatu tajwa na wengine wa aina yake, turejee maneno yake hapo juu ukiyalinganisha na aliyosema ndoa ilipomshinda. Alinukuliwa akisema kuwa ameamua kuachana na chamaulaji kutokana na unyotoaji uliofanyika juzi! Lahaula! Je, kuanzia wakati huo–––kama kweli analiyachukia na kuyapinga–––alikuwa wapi? Alingoja nini au alikuwa akivuta kamba lau apate mradi? Je, ameamua kutumia unyotoaji tajwa kupata ujiko kama mwenzake ambaye–––alipopigwa chini–––kuushupalia? Je, kufyatuka na kusepa vinaleta suluhisho? Je, mauaji unyotoaji roho chanzo chake hakiwezi kuwa siasa za maji taka zilizojitenga na ukweli na kukumbatia uongo na uzushi? Ni jemedari gani hukimbia mapigano akidhani analeta suluhisho au ushindi? Natamani chata cha maulaji wafyatuke na kufichua walivyompokea, kumjua, kumchukulia, na kumtenza hadi ndoa ikamshinda akarejea alikokandia vibaya.
Hapa, kuna maswali muhimu. Je, Fyatu tajwa na wengine kama yeye wanafuata sera au vyeo na ulaji? Je, kwanini ameamua kuramba matapishi yake na kujigeuza maji taka baada ya
Kwa mtu wa kada ya Fyatu tajwa ya uchungaji kama siyo ‘uchunaji’, wengi walitegemea awe mkweli, mwenye maadili na si wa kusema hili leo na kesho, anajipiga mtama. Angeona lau hata aibu kuwa ni vibaya kwa Fyatu mzima tena ‘ wa God’ kuonekana kigeugeu, kizabazabina, na mtata kiasi cha kufanya siasa kuwa maji taka ambayo yakishachafuka, huwezi kuyarejesha kwenye usafi na usalama. Je, Fyatu tajwa, wenzake, waliompokea, na wamaomshabikia wanayajua haya au la? Je, anaweza kuaminika na kuheshimika tena ilhali akisema hili na kesho akasema kinyume chake kiasi cha kufanya wanaomsikiliza wasijue kati ya ukweli, uongo, na uzushi ni upi mbali na uchumia tumbo na usasi wa ngawira?
Japo si kosa kwa Chandimu kumpokea na kumrejesha kundini Fyatu tajwa, je, hii haionyeshi kuwa baadhi ya vyata ni kama maabara ambayo kazi yake ni kufanyiwa majaribio? Je wanajua maana ya kuwa hivyo? Japo, Fyatu huyu si wa kwanza wala mwisho kufanya siasa hizi zinaoanza kuzoeleka, kuna haja ya wapiga kura na wananchi kwa ujumla kuweka nukta na kukumbuka matendo na matamshi ya wote wanaotuaminisha kuwa wanatufaa wakati hawafai wala kujifaa.
Mwisho, kwa alichofyatua Fyatu, nashindwa kumuelewa wala kumpongeza zaidi ya kumpa pole. Maana, ana ndimi mbili. Isitoshe, kama ni upotezaji na unyotoaji roho, kwani, vilianza awamu jana? Je, ni unyotoaji roho gani ni muhimu kuliko mwingine tena chini ya chata lile lile? Je, Fyatu alikwenda kuwafyatua wenzake wakaishia kumfyatua? Maswali ni mengi kuliko majibu. Niwezacho kusema ni kutahadhari siasa za maji taka na wanasiasa maji taka.
Wednesday, 27 May 2026
Twachukia mabeberu, kupenda, na kufanya ubeberu!
Kwanza, kwanini mabeberu yaliitwa mabeberu na siyo madume?
Japo tunawaponda mabeberu, ni kama tunajisahau kuwa huwa, wao, tofauti na mabeberu ya mbuzi, huwa tunajipeleka kwao wenyewe. Hivyo, sioni kama ni ufyatu badala ya uzwazwa kulalamika pale wanapoacha kutubembeleza. Hata hivyo, kila fyatu hata wadudu wanajua. Badala ya wao watubembeleze kama mabeberu wafanyavyo kwa majike, siye huwa tunawabembeleza pale unapotaka kuwatoa njuluku. Hapa, jina beberu hubadilika na kuwa mfadhili.
Mafyatu wana mambo. Ukiwa mfadhili ukawanyima njuluku wanakunanga hasa unapostukia rongorongo zao juu ya namna walivyotumia njuluku ulizowafadhii au kuwakopesha. Ukiwastukia, jiandae. Ghafla watageuka na kujifanya hamnazo kama siyo kujitoa ufahamu waanze kukuponda pale walipokuingiza chaka kuwa wanakupenda.
Utakuta mifyatu haichapi kazi. Badala yake inachapa majungu na starehe.Mingine inakwapua njuluku za mafyatu kwa mikono miguu na midomo utadhani itaishi milele. Mingine kazi yake ni kujikombokomba kama chawa na inzi. Halafu inataka eti nayo iheshimike au kufanikiwa kama kaya zilizoukata wakati kaya yao ikiendelea kuwa ombaomba na kopakopa!
Tukiwa wakweli, nani si beberu tena hata wengine majike? Nazoza hivi kwa sababu mabeberu, licha ya kuwa mafahari, hupenda ufahari. Huwa ni shapu yanapotaka vitu. Yanaweza kupata kwa kudandia au kubembeleza beebeeebeeebebe. Kinachofanya nipende mabeberu, kwanza, huwa hayana chawa.
Ukiachia mbali ubeberu kuonekana jambo baya hasa wale wanaoitwa mabeberu wanapostuka, hata wale wanaoukandia, ima wanao, kwa kujua au kutojua, au wanautamani na kuuonea gere. Nani asiyependa ubeberu ili awabeberu wenzake? Nenda kawaulize wahanga wa kweli wa ubeberu kama wale Gen Ziro wa kaya ya kufikirika jirani na Fyatuland. Du! Kumbe hii bangi kali!
Chanzo: Mwananchi Jtano iliyopita.
Mafyatu kuandamana kupinga kuhalalishwa upigaji
Kiherehere wangu alisema mambo mengi. Maskini, hakujua kuwa Mafyatu weshafyatuka. Ukiwafyatua, wanafyatuka na kukufyatua. Hata usipowafyatua, wanajifyatua na kukufyatua. Baada ya kiherehere kufanya kiherehere na kujifanya hamnazo, si nimezinyaka kuwa Mafyatu wanataka kufyatuka na kunifyatua na walaji wenzangu. Wanasema, mara hii, kitaeleweka hata kama hakieleweki. Wanataka kuzuia jinai ambayo niliyotaka kutenda na kuhalalisha.
Kwa tishio hili, nimeamuru wasiojulikana, lazima kijulikane. Natangaza rasmi. Yeyote asiyejipenda aingie mtaani ajue kilichowanyima ndege meno. Sikubali ufyatu huu kutaka kunifyatua nisifyatue? Sijui kwanini mafyatu wana akil ndogo kama kuku. Mnapewa fursa kupiga njuluku ndefu mnajifyatua ufahamu kama amfahamu dili zima!
Mifyatu kwa umbea na urongo, sina mfano. Si yapo Mafyatu yenye ntima nyongo na wivu yaliyodai eti sie wanene tumefyatua sana mali na njuluku za Mafyatu. Hivyo, tunajiwekea kinga iwapo siku moja tutafyatuliwa na kujikuta nje ya ulaji tupate pa kuangukia. Nani kawaambia? Yapo mafyatu yaliyokufuru yakidai eti katiba tukufu ya Fyatuland irekebishwe kuondoa kipengele kinachozuia Mafyatu kunifyatua mimi kama kiongozi wao. Hivi, kweli hawa wana akili? Sasa yakiondoa kipengee hiki hayajui kuwa Fyatuland itaingia kwenye machafuko tokana na wapenzi wangu kuchukizwa na kutishiwa na hila hii ya kifyatu? Mnataka wanene tule wapi? Mnataka mali zetu nasi na vitegemezi, na vigegemezi vya vitegemezi na maswahiba zetu vilindwe na nini dhidi ya kufyatuliwa na mafyatu wanaougua ugonjwa wa kufyatufyatuka hovyo?
Nilishawaonya Mafyatu kuwa Fyatuland ina wenyewe na wenyewe ni sisi. Sijui kwanini hawa Mafyatu hawaelewi inshu nzima! Kweli viumbe hawa wamelaanika sina mfano. Mliona wapi kiongozi wa kaya kama Fyatuland kushitakiwa kikatiba? Pamoja na Mafyatu kujifanya hamnazo, nina mpango mzuri wa kuwalinda Mafyatu wote. Mfano, kama kuna Fyatu atakayejiingiza kwenye ujambazi, uuzaji mihadarati, utakatishaji wa njuluku, na mengine kama haya, lazima mali na njuluku anazoita zake tuzitwae ili akome na kukomaa na kuacha uzwazwa na apigaji wa njuluku za Mafyatu.
Napanga kutoa elimu ya uraia ambayo itawapa ujuzi Mafyatu wa kutofautisha upigaji wa kalamu na ule wa silaha. Pia, lazima wajue kuwa kuna tofauti kati ya upigaji wa kisiasa na visasi. Hivyo, nikiri kuwa kiherehere wangu alikosea. Niliposema tufute sharia ya kutwaa njuluku zilizopigwa au kupatikana kiharamu, naamaanisha wale wasio wanasiasa. Kwanini Mafyatu hawajui kuwa siasa bila ‘kazi na dawa’, Fyatuland itakosa Mafyatu mahiri wa kuiongoza.
Inabidi Mafyatu waelimishwe na kuelimika. Wajue kuwa si kila ujambazi ni ujambazi. Upo uliohalalishwa na ule ulioharamishwa. Mbona wachunaji, sorry, wachungaji wanakunywa maziwa na kula nyama toka kwenye kundi la kondoo wao hamzozi? Kuongoza Fyatuland ni kazi kubwa inayompasa mwenye kuibeba kuwa na ukwasi ili asiaibishe kaya pale anapokutana na wanene wenye ukwasi wa kaya nyingine. Mfano, kiongozi wa Fyatuland, hapaswi kuonekana au kuwa kapuku. Akiwa hivyo, wachukuaji, sorry, wawekezaji, hawataweza kumwamini na kuwekeza. Hapa ndipo inapokuja diplomasia ya uchumi. Ili kuwashawishi wawekaji wawekao na kuchukua waa, lazima wanene wawe wananuka na kuonyesha ukwasi wa kufa Fyatu.
Hii inatokana na ukweli kuwa, ili kuwanasa wawekaji, lazima ufanane nao. Wao, wanakuja na njuluku, wengine mikoba mitupu na kuondoka na njuluku zaidi toka kwenye shamba la bibi, sorry, Fyatuland. Nimesemaje? Namaanisha kaya makini yenye kiongozi makini Fyatu Mfyatuzi mwana wa Mfyatuko mjukuu wa Mfyatuliko.
Huwezi kuvutia watega uchumi na wawekaji kama unanuka ukapuku. Lazima uwe na kila alama na sura za ukwasi. Njuluku huleta njuluku. Ukwasi huleta ukwasi. Uongo, sorry, uongofu huleta uongozi. Nani anaweza kumwamini kapuku akawekeza kwake? Si atajiuliza. Kama hawa uchumi wanao lakini wanaukalia, nitajuaje kama hawatakalia njuluku zangu. Lazima kuongoza kwa mfano. Ukitaka kaya yako itajirike, lazima ujitajirishe mwenyewe kwanza ili wengine waone na kuiga. Hii ndiyo sababu ya kutaka kuondoa sharia ya utwaaji njuluku za wanene.
Du! Hii gongo na mibangi, we acha tu. Badala ya kumwaga pwenti, tazama nimwaga pumba. Dharau kila kilichoandikwa hapa. Nilikuwa naota tu.
Chanzo: Mwananchi Leo Jumatano.
Wanawake wa Kitanga, hakuna libwata
Mfano, utasikia watu wakisema kuwa kuingia Tanga ni rahisi na kutoka ni vigumu. Je, ni kwanini? Hatuwezi kutoa jibu moja kwa moja au moja tu. Hatujui chanzo cha imani au msemo huu. Hivyo, ngoja tudurusu na kudadavua kidogo kuhusiana na wanawake hawa wa ambao wanasemekana kuwa wanaweza kumuandalia maji ya kuoga mwanamme na kuyachanganya na malashi ili akishaoga anukie vizuri. Je, hili si jambo zuri? Ni wapi tena hufanyika katika nchi yetu? Nani hawezi kuvutiwa na hili? Hebu jifikirie. Mume ni mvuvi. Anarejea zake nyumbani na shombo. Wewe kama mke utamfanyiani ili awezenukia uzuri? Au mme ni mkulima tena Msukuma au Muha. Anarejea nyumbani baada ya kupiga jembe kwa masaa saba na jasho. Utamsaidiaje?
Wengine wanakwenda mbali na kudai, japo hatuna ushahidi kuwa wanawake wa Kitanga wanaweza hata kumbeba mume mgongoni kama mtoto! Lahaula lakuata! Nani hawezi kuvutiwa na ukarimu huu?
Nani anaweza kuchukia kitu hii? Je, hili nalo ni limbwata au usafi? Hamjawahi kusikia kuwa mwanamke ni usafi? Kama ni limbwata, basi kwenye ndoa, linaswihi sana tu. Japo usafi unapaswa kuwa ni suala binafis la wanandoa wote, bado wapo wanandoa wanaosumbuka katika ndoa zao hasa akina mama tokana na kutozingatia suala la usafi wa miili na ndimi zao. Japo usafi ni suala binafsi, kwa wanaotaka kuepuka madhara yake, si chaguo bali wajibu.
Huwezi, kwa mfano, ukaingia kitandani ukiwa mchafu na unatoa harufu mbaya mambo yakaenda. Japo laweza kuonekana jambo geni, kwani, haya hayapo? Je, ni wangapi wanawaambia wenzao kuwa ni wachafu na hivyo wajisafishe? Msioneane aibu. Ambianeni ukweli. Wapo wasiopenda kukosoana kwa maneno bali mwa matendo. Ni heri kulaumiana kwa kuambiana ukweli iwe kwa maneno au matendo kuliko kukwazana, kuogopana, au kutofautiana hata kufarakana kwa kitu kidogo japo muhimu kama usafi. Hapa, mchague kunyamaziana na kuumizana au kukerana mkilinganisha na kuambiana na mkatatua tatizo pamoja.
Kuna baadhi ya jamii ambazo huwa hawapigi mswaki wakati wa kwenda kulala. Mtu anashinda anakula. Halafu anaingia kitandani bila kupiga mswaki. Wengine hata hawaogi wala kujitawaza. Jamani, binadamu si mnyama alale na kuamka mchafu. Hata kuku akikaribia kwenda kulala huoga kwa michanga lau alale msafi.
Tukizingatia hayo juu na kuyahusisha na sifa za wanawake wa Kitanga, huenda tunaweza kupata maana hata bila kuwahoji. Mbali na usafi. Kuna methali moja kuwa njia ya kuingia kwenye moyo wa mwanaume ni kupitia tumboni. Mwake. Hapa, ndipo umuhimu na ustadi wa mapishi unapoingia. Jieulize ni wanawake wangapi wanajua mapishi ya kumfanya hata mtu achukie hoteli.
Anayebishia au kupinga hili ajiulize. Kwanini biashara ya mahoteli ni moja ya biashara kubwa ulimwenguni. Ni kwa sababu binadamu wote hupenda chakula kizuri. Huwezi kupiga michemsho kila siku ukashindana na bingwa wa kuaangiza. Wapo watu matajiri wasiokula vyakula vizuri si kwa sababu hawana uwezo bali wahusika hawana ujuzi wa mapishi. Pia, wapo maskini wanaokula vizuri tu kwa sababu ya ufundi wa jikoni. Kimsingi, hakuna chakula kibaya wala kizuri. Kinachoweza kukifanya kiwe hivyo ua kisiwe ni mapishi tu.
Mambo ya chumba cha kulala hatugusi. Hata hivyo, kama ilivyo kwenye mambo mengine hapo juu, nako huko kwahitaji juhudi, maandalizi, na ufundi si haba. Leo, tunaishia hapa.
Chanzo: Mwananchi J'pili juzi.
Monday, 18 May 2026
Ndoa ni mwili mmoja wenye vichwa viwili na si kimoja
Kimsingi, dini nyingi hasa za kimamboleo zinamchukulia mwanamke kama chombo cha mwanaume kutumia atakavyo. Ndiyo maana, ukienda mbali, utakuta dhana nyingine yenye ukakasi inayodai kuwa mke aliumbwa toka kwenye ubavu wa mumewe. Kiakili, hii si kweli. Mke si ubavu wa mmewe vinginevyo na mume ni ubavu wa mkewe.
Je, chanzo cha hii dhana ni nini? Kama ilivyodhana ya mume kuwa kichwa cha mkewe iliyozalishwa na Paulo ambaye hakuwahi kuoa, hivyo, kutojua maana ya ndoa, inatokana na imani kuwa Eva aliumbwa atoka kwenye ubavu wa Adamu. Wapo wanaohoji busara na mantiki yake. Je, Mungu aliishiwa udongo kiasi cha kulazimika kutumia ubavu wa kiumbe mwingine? Je, haya ni maneno ya waandishi ambao wengi walikuwa wanaume yaliyolenga kujenga mazingira na mfumo vya kuwanyonya na kuwadhalilisha wanawake kama ilivyotokea baadaye? Hata maandishi yenyewe hayamuiti Eva mke wa Adam bali msaidizi wake sawa na housegirl.
Tutadurusu kwa ufupi kwanini mke na mume wote ni vichwa vya familia. Katika kufanya hivi, tutajitenga na imani na tamaduni ambazo kwa Waswahili ni za kigeni zikiwemo dini. Tunasema hivi tokana na ndoa kuakisi tamaduni za jamii zinamofungiwa. Tunajua. Imani za kimapokeo karibu zote zimesheheni ngano, uzushi, mila, tamaduni za waliozileta ili kuwatawala na kuwanyonya waliozipokea bila hata kujua walichokuwa wakipokea ikiwamo taasisi ya ndoa.
Kwanza, tumejitenga na kisa cha Adamu na Eva kwa vile hawakufunga ndoa na hawakuwa mke na mume zaidi ya kuwa mtu na msaidizi wake. Kwa vile safu hii siyo ya uchambuzi wa dini, hili tunaliacha.
Pili, tunaangazia ubaguzi, unyanyasaji na unyonyaji vya kijinisia ambavyo vimegeuka janga si kwa ndoa tu bali jamii, tuseme dunia nzima kiasi cha mke kugeuzwa kifaa kisichopaswa kuwa na hata utambuliko.
Tatu, tunaangalia umuhimu wa kichwa katika viumbe vyote hasa binadamu. Kichwa ndicho kinabeba hazina kuu au injini ya kiumbe, yaani ubongo. Kisayansi, ini, mapafu, moyo, na ubongo ndivyo viungo muhimu sana ambavyo visipokuwapo kiumbe hakiwezi kuishi, mara nyingi kiungo kinachotumika sana, kisichopumzika, na ni cha mwisho kufa na hivyo, kiumbe hutangazwa kufa baada ya ubongo kuacha kufanya kazi. Kuna watu au viumbe wanaoishi na kufana katika maisha na shughuli zao wasio na baadhi ya viungo kama vile miguu, mikono, ila bila kichwa, hakuna kiwezacho kuishi.
Nne, kichwa ndicho pia hujenga utambuliko wa kiumbe. Kwa binadamu ni zaidi kwa vile sura zetu zinabebwa na kichwa mbali na kuwa nyumba ya chombo cha maamuzi na ung’amuzi, yaani ubongo. Ukitaka kujua umuhimu wa kichwa, angalia kitambulisho chako cha utaifa aka NIDA au pasi ya kusafiria, au kadi ya benki. Pale, kuna kichwa chako ambacho ni wewe. Katika utambuliko ambao humtambulisha na kumtofautisha binadamu na wenzake, chenye kutambulika siyo viungo vingine kama kifua, tumbo, kiuno, mikono wala miguu bali kichwa.
Tano, mbali na hilo la utambuliko, hata kwenye lugha ya kawaida, mtu akikuita kichwa unajisikiaje? Je, akikuita kiuno, pia utajisikiaje? Kati ya viwili, utachagua kipi?
Tumalizie. Kwa uzoefu wetu, mume na mke wote ni vichwa. Hili linapofanyika, wawili huaminiana na kushirikiana bila wasi wasi wa kudhalilishwa au kunyonywa mbali na kunyanyaswa.
Chanzo: Mwananchi Jpili jana.
Thursday, 14 May 2026
Judge Chande Commission: Congrats President Samia on eye opener
Let’s start off from here. President Samia recently said “hii ni ripoti ya Rais. Aliyeunda tume ni Rais, kwa hiyo wasitokee watu wengine wakadai umiliki wa ripoti hii, ni ripoti ya Rais. Tume za huko nyuma zilikuwa zinabanwa kimya kimya, mimi nimeamua tuambizane, lakini ripoti ni mali ya Rais.” I don’t want to misconstrue or spoil what the president said.
We all know. There are chronic root causes that led to the October 29 mass slaughter as they revolve around injustices mainly the absence of freedom, corruption, inconducive environment for doing business, mismanagement of public funds and resources, poverty, unemployment, and above all, ineptitude. Historically, these problems didn’t commence yesterday under Samia. They’ve been seething for long, precisely since independence and others just recently.
I don’t seek to blame, convict, or exonerate anybody but put the records straight. The creation of the commission emanated from our quest to heal the injuries we as a nation. It all revolves around how the conflict was handled, or should I say, mishandled. For, soon after the bloodbath, the authorities made many bloopers and convoluted and confusing statements alleging without substantiating that protesters were hired and sponsored by the ‘enemies’ of our country.
Firstly, the authorities didn’t name names. Nor did it print a picture of how this plot escaped the scrutiny of our intelligence.
Secondly, the participants were ‘drugged mercenaries.’ For, Tanzanians known for their peaceability, wouldn’t commit such a sacrilege. Where were they from, who, and why? The authorities didn’t even bother to answer these key questions, which would have acted as a hunch of unearthing and thwarting the entire dud that resulted in the miscarriage of justice.
Thirdly, in law, he/she who alleges must prove or qui dicit, non qui negat. Thus, the authorities bear the burden of proof. That’s so to avoid offering a carte blanche for malicious people to maliciously make allegations to punish or tarnish their enemies.
Fourthly, if we honestly and seriously underscore the triggers of the conflict and the quest to address it, do truly the Judge Chande Commission report belong to the president really? I humbly beg to honestly agree to disagree with the take of the president. For me, and perhaps for all Tanzanians, though the commission is known as the presidential commission and Judge Chande Commission respectively, belong neither to Chande personally nor the president. They belong to the people as the funders and stakeholders besides being the victims of the bloodbath in question who own everything in their country.
Seriously, we must separate between the president as a person and as an institution whose legality and powers come from the constitution, which belongs to the people but not to the president. I honestly beg the president to abandon the position she’s quoted taking. For whoever pays the piper calls the tune.
Wednesday, 13 May 2026
Turidhiane, kuridhika bila kulidhishana?
Wednesday, 6 May 2026
Fyatu aunda timu kujichunguza na kuwachuuza mafyatu
Baada ya mafyatu kufyatuka na kunichosha kwa kunisingizia baadhi ya mambo, nina mpango wa kuunda na kutumia timu–––siyo tume–––ya kujichunguza na kuniweka huru. Hii ni kutokana na kuwafyatua mafyatu waliojitia kufyatukakufyatuka wakitaka kunifyatua wasijue ningewafyatulia mbali. Si niliwafyatua tena bila huruma. Baada ya kuwafyatua, si wakatokea mafyatu wakilalamika mie sina huruma wakati mie nasifika kwa kuhurumia wadudu hata wanyama. Hivyo, basi, kuondoa mzizi wa fitina, nimeunda timu ya ‘kutumika’ kunichunguza.
Kwa vile hii ni timu yangu na inanichunguza, lazima itoe ripoti kwangu. Hii ni ripoti ni mali yangu siyo ya mafyatu. Naweza kuizima au kufanya nitakalo. Ataye fanya fyoko, namfyatua. Ole wa owaje na mauzauza na rongorongo kuwa niliwafyatua mafyatu. Watakoma. Hata kama kweli niliwafyatua mafyatu waliotaka kunifyatua, walitaka nimfyatue nani? Je, walitaka nifyatuliwe kirahisi hivi bila kufyatuka na kujitetea?
Katika kuunda timu hii, nimezingatia yafuatayo:
Mosi, nitaiunda mwenyewe bila hata kumshirikisha mshirika wangu wa bedroom. Sitafanya kosa niwahusishe wengine. Nani ajua wanaweza kufyatuka wakanifyatua kama wale waliotaka kunifyatua nikawafyatua kabla hawajanifyatua?
Pili, nitawalipa wanaounda timu kwa njuluku zangu na si za mafyatu. Maana, nikifanya kosa nikatumia njuluku za mafyatu, mafyatua nao wenye njuluku zao watataka washiriki katika kuunda timu hii ya kunichunguza ili wanifyatue. Nani afanye kosa hili la wazi usawa huu wa kufyatuana kifyatufyatu? Hivyo, mkiona washirika wangu kwenye timu msishangae wala kupoteza muda wenu kufyatuka.
Tatu, ripoti ya tume, sorry, timu hii itabidi niipitie kwanza kabla haijawekwa wazi. Hapa, nalenga kuondoa makandokando yoyote yanayoweza kusababisha au kuwapa mafyatu fursa au ushahidi wa kunifyatua.
Nne, nitahakikisha timu hii inanyonga ushahidi wowote unaoweza kusababisha nifyatuliwe. Hapa, lazima wana timu wapewe darasa kabla ya kutoa ripoti ya ujichunguzaji. Nawajua fika mafyatu. Ukizubaa wanakufyatua tena kwa kujifyatulisha. Bila kuwabana, wapo tena maswahiba zako, wanaweza kukugeuzia kibao ukaishia kujikuta umeunda tume ya kujifyatua badala ya kujichunguza na kuwachuuza mafyatu watakao ufyatuliwe.
Tano, tokana na kuwa na uhuru wa kuunda timu na kutengua, nitahakikisha watakaoleta jambo lolote la kunihusisha na ufyatuaji nilioufanya, nawafyatulia mbali bila huruma. Kama hii italeta shobo, nitapokea ripoti ya timu ya kujichuguza na kuiweka kapuni hadi mafyatu wangoje, wachoke na kusahau. Kwani, nitakuwa wa kwanza kufanya huu ufyatuzi ambao kitaalamu huitwa ufyatuzi wa kuepuka kufyatuliwa. Inshu inakuwa hivi. Unaita kadamnasi ya mafyatu tena kwa mbwembwe. Unakabidhiwa makabrasha na kuyaweka kapuni. Wakizidi kukubana, unawafyatua kwa kuwafunga kamba kuwa una mambo mengine muhimu ya kikaya. Hivyo, unawazuia wasiwe na mbambamba. Wangoje tu. Maana, haraka haraka haina baraka na mvumilivu hula mbivu hata kama wakati mwingine ni mbovu.
Sita, nitapiga marufuku vyombo vya umbea kupewa nakala ya ripoti ya timu ili visianze kusambaza umbea unaoweza kusababisha nifyatuliwe tena kwa kazi niliyoanzisha mwenyewe. Lisrikal langu litafanya ripoti ya timu kuwa siri. Hivyo, atakayejitia kiherehere na kujifyatua kuijadili, ataozea lupango au nitamtumia wasiojulikane wamjue na kumteka na kumpoteza ili kupoteza kila kitu mbali na kuwatisha na kuwanyamazisha mafyatu ili wagwaye. Unacheza na mimi siyo?
Saba, nitahakikisha wataalamu wangu wanaandika ripoti na kuipa timu inikabidhi harafu niikalie kifyatu na kinomi ili kufunika kombe wanaharamu wapite.
Nane, sitatoa hadidu za rejea. Najua. Kufanya hivyo ni sawa na kuwapa vichaa rungu wanifyatulie mbali. Kwa mfano, nitatoa idadi ya mafyatu walionyotolewa roho. Kwa vile sitaki nionekane mie ni nduli kweli, napanga kuiambia timu itoea idadi ya mafyatu watano tu walionyotolewa roho. Tena, timu iseme kuwa walinyotolewa roho wakiwa wanakwapua mali kwenye maduka. Hii ni kutokana na asili na ukweli kuwa ndata wa Fyatuland karibia wote, walitaka kuwa makasisi lakini kale kamjezo kanakofanywa na wenzao wenye majoho ya uroho wa roho mtakakitu, kaliwashinda.
Hivyo, hawawezi kuua hata chawa. Abishaye ajikumbushe. Nani haoni chawa wanavyonenepeana Fyatuland? Hii ni kwa sababu ya upendo na kujali viumbe wote. Hivyo, ripoti ya timu itasema kuwa imegundua kuwa hakuna fyatu hata mmoja aliyenyotolewa roho isipokuwa watano waliojitakia kwa kutaka kupora mali za wenyewe ambao waliamua kuwakomesha kwa kuwafyatua.
Tisa, nitaiamuru timu iseme kuwa waliofanya uzwazwa wa kutaka kuvuruga amani na mshirikiano wa Fyatuland ni mamluki waliokuwa wamelipwa bangi na gongo ili wavuruge tunu hizi kwa sababu ya wivu wa kike tu.
Kumi, sitataja kiasi cha njuluku ilizopiga timu. Maana, nikifanya hivyo, nitakuwa nawachokoza mafyatu na kuwakumbusha ile kitu. Kutaja kiasi cha njuluku, licha ya kufanya wajue ni kiasi gani nimepiga, itawapa sababu mafyatu kufyatuka tena na kunifyatua. Nani afanye ufyatu huu? Thubutu yako! Timu imekula kiasi gani? Hii, huitwa chiri chirini njomba.
Kwa vile leo nimeupiga mma vilivyo, sisemi mengi. Hivi, nimesemaje? Fanya kila kitu usomacho hapa siri.
Chanzo: Mwananchi leo Jtano.
Wednesday, 29 April 2026
Fyatu kufyatua mafyatu wanaofyatukafyatuka kumkosoa
Saturday, 25 April 2026
My New Baby on Coups Resurgence in Africa
Publisher: Mwanaka Media and Publishing, Zimbabwe
Pages: 285
Year: 2026
Category: African Studies
Dimensions: 210×148 mm
This volume delves into coups d’état in Africa by exploring coloniality, historicity, reproducibility, and preventability. It bitingly ties coups to colonialism and coloniality that postcolonial Africa maintained, replicated, and kept in place at its perils. Markedly, the book foretells the chronicity, existentiality, and perversity of coups d’état if some measures to address and arrest them are not seriously and timely taken. Moreover, the book touches on how dictatorship creates its own fragility, susceptibility, and possibility for coups d’état. A main argument is that coloniality, corruption, dictatorship, and greed are among the anchors
and root causes of the prolongation of coups d’état in Africa where it is easy for les majeurs incapables, especially, politicians, soldiers, and warlords to grab power and abused it thereof. The book takes o with the history of coups and winds up with solutions to the problem warning Africa that is still a long way away from true democracy and peaceful transition sine coups d’état if it does not embark on, inter alia, accountability, democratic changes, good governance, and pragmatic fight against corruption, dictatorship, injustices, and poverty.
£30.00
