The Curse for Salvation
Wednesday, 13 May 2026
Turidhiane, kuridhika bila kulidhishana?
Wednesday, 6 May 2026
Fyatu aunda timu kujichunguza na kuwachuuza mafyatu
Baada ya mafyatu kufyatuka na kunichosha kwa kunisingizia baadhi ya mambo, nina mpango wa kuunda na kutumia timu–––siyo tume–––ya kujichunguza na kuniweka huru. Hii ni kutokana na kuwafyatua mafyatu waliojitia kufyatukakufyatuka wakitaka kunifyatua wasijue ningewafyatulia mbali. Si niliwafyatua tena bila huruma. Baada ya kuwafyatua, si wakatokea mafyatu wakilalamika mie sina huruma wakati mie nasifika kwa kuhurumia wadudu hata wanyama. Hivyo, basi, kuondoa mzizi wa fitina, nimeunda timu ya ‘kutumika’ kunichunguza.
Kwa vile hii ni timu yangu na inanichunguza, lazima itoe ripoti kwangu. Hii ni ripoti ni mali yangu siyo ya mafyatu. Naweza kuizima au kufanya nitakalo. Ataye fanya fyoko, namfyatua. Ole wa owaje na mauzauza na rongorongo kuwa niliwafyatua mafyatu. Watakoma. Hata kama kweli niliwafyatua mafyatu waliotaka kunifyatua, walitaka nimfyatue nani? Je, walitaka nifyatuliwe kirahisi hivi bila kufyatuka na kujitetea?
Katika kuunda timu hii, nimezingatia yafuatayo:
Mosi, nitaiunda mwenyewe bila hata kumshirikisha mshirika wangu wa bedroom. Sitafanya kosa niwahusishe wengine. Nani ajua wanaweza kufyatuka wakanifyatua kama wale waliotaka kunifyatua nikawafyatua kabla hawajanifyatua?
Pili, nitawalipa wanaounda timu kwa njuluku zangu na si za mafyatu. Maana, nikifanya kosa nikatumia njuluku za mafyatu, mafyatua nao wenye njuluku zao watataka washiriki katika kuunda timu hii ya kunichunguza ili wanifyatue. Nani afanye kosa hili la wazi usawa huu wa kufyatuana kifyatufyatu? Hivyo, mkiona washirika wangu kwenye timu msishangae wala kupoteza muda wenu kufyatuka.
Tatu, ripoti ya tume, sorry, timu hii itabidi niipitie kwanza kabla haijawekwa wazi. Hapa, nalenga kuondoa makandokando yoyote yanayoweza kusababisha au kuwapa mafyatu fursa au ushahidi wa kunifyatua.
Nne, nitahakikisha timu hii inanyonga ushahidi wowote unaoweza kusababisha nifyatuliwe. Hapa, lazima wana timu wapewe darasa kabla ya kutoa ripoti ya ujichunguzaji. Nawajua fika mafyatu. Ukizubaa wanakufyatua tena kwa kujifyatulisha. Bila kuwabana, wapo tena maswahiba zako, wanaweza kukugeuzia kibao ukaishia kujikuta umeunda tume ya kujifyatua badala ya kujichunguza na kuwachuuza mafyatu watakao ufyatuliwe.
Tano, tokana na kuwa na uhuru wa kuunda timu na kutengua, nitahakikisha watakaoleta jambo lolote la kunihusisha na ufyatuaji nilioufanya, nawafyatulia mbali bila huruma. Kama hii italeta shobo, nitapokea ripoti ya timu ya kujichuguza na kuiweka kapuni hadi mafyatu wangoje, wachoke na kusahau. Kwani, nitakuwa wa kwanza kufanya huu ufyatuzi ambao kitaalamu huitwa ufyatuzi wa kuepuka kufyatuliwa. Inshu inakuwa hivi. Unaita kadamnasi ya mafyatu tena kwa mbwembwe. Unakabidhiwa makabrasha na kuyaweka kapuni. Wakizidi kukubana, unawafyatua kwa kuwafunga kamba kuwa una mambo mengine muhimu ya kikaya. Hivyo, unawazuia wasiwe na mbambamba. Wangoje tu. Maana, haraka haraka haina baraka na mvumilivu hula mbivu hata kama wakati mwingine ni mbovu.
Sita, nitapiga marufuku vyombo vya umbea kupewa nakala ya ripoti ya timu ili visianze kusambaza umbea unaoweza kusababisha nifyatuliwe tena kwa kazi niliyoanzisha mwenyewe. Lisrikal langu litafanya ripoti ya timu kuwa siri. Hivyo, atakayejitia kiherehere na kujifyatua kuijadili, ataozea lupango au nitamtumia wasiojulikane wamjue na kumteka na kumpoteza ili kupoteza kila kitu mbali na kuwatisha na kuwanyamazisha mafyatu ili wagwaye. Unacheza na mimi siyo?
Saba, nitahakikisha wataalamu wangu wanaandika ripoti na kuipa timu inikabidhi harafu niikalie kifyatu na kinomi ili kufunika kombe wanaharamu wapite.
Nane, sitatoa hadidu za rejea. Najua. Kufanya hivyo ni sawa na kuwapa vichaa rungu wanifyatulie mbali. Kwa mfano, nitatoa idadi ya mafyatu walionyotolewa roho. Kwa vile sitaki nionekane mie ni nduli kweli, napanga kuiambia timu itoea idadi ya mafyatu watano tu walionyotolewa roho. Tena, timu iseme kuwa walinyotolewa roho wakiwa wanakwapua mali kwenye maduka. Hii ni kutokana na asili na ukweli kuwa ndata wa Fyatuland karibia wote, walitaka kuwa makasisi lakini kale kamjezo kanakofanywa na wenzao wenye majoho ya uroho wa roho mtakakitu, kaliwashinda.
Hivyo, hawawezi kuua hata chawa. Abishaye ajikumbushe. Nani haoni chawa wanavyonenepeana Fyatuland? Hii ni kwa sababu ya upendo na kujali viumbe wote. Hivyo, ripoti ya timu itasema kuwa imegundua kuwa hakuna fyatu hata mmoja aliyenyotolewa roho isipokuwa watano waliojitakia kwa kutaka kupora mali za wenyewe ambao waliamua kuwakomesha kwa kuwafyatua.
Tisa, nitaiamuru timu iseme kuwa waliofanya uzwazwa wa kutaka kuvuruga amani na mshirikiano wa Fyatuland ni mamluki waliokuwa wamelipwa bangi na gongo ili wavuruge tunu hizi kwa sababu ya wivu wa kike tu.
Kumi, sitataja kiasi cha njuluku ilizopiga timu. Maana, nikifanya hivyo, nitakuwa nawachokoza mafyatu na kuwakumbusha ile kitu. Kutaja kiasi cha njuluku, licha ya kufanya wajue ni kiasi gani nimepiga, itawapa sababu mafyatu kufyatuka tena na kunifyatua. Nani afanye ufyatu huu? Thubutu yako! Timu imekula kiasi gani? Hii, huitwa chiri chirini njomba.
Kwa vile leo nimeupiga mma vilivyo, sisemi mengi. Hivi, nimesemaje? Fanya kila kitu usomacho hapa siri.
Chanzo: Mwananchi leo Jtano.
Wednesday, 29 April 2026
Fyatu kufyatua mafyatu wanaofyatukafyatuka kumkosoa
Saturday, 25 April 2026
My New Baby on Coups Resurgence in Africa
Publisher: Mwanaka Media and Publishing, Zimbabwe
Pages: 285
Year: 2026
Category: African Studies
Dimensions: 210×148 mm
This volume delves into coups d’état in Africa by exploring coloniality, historicity, reproducibility, and preventability. It bitingly ties coups to colonialism and coloniality that postcolonial Africa maintained, replicated, and kept in place at its perils. Markedly, the book foretells the chronicity, existentiality, and perversity of coups d’état if some measures to address and arrest them are not seriously and timely taken. Moreover, the book touches on how dictatorship creates its own fragility, susceptibility, and possibility for coups d’état. A main argument is that coloniality, corruption, dictatorship, and greed are among the anchors
and root causes of the prolongation of coups d’état in Africa where it is easy for les majeurs incapables, especially, politicians, soldiers, and warlords to grab power and abused it thereof. The book takes o with the history of coups and winds up with solutions to the problem warning Africa that is still a long way away from true democracy and peaceful transition sine coups d’état if it does not embark on, inter alia, accountability, democratic changes, good governance, and pragmatic fight against corruption, dictatorship, injustices, and poverty.
£30.00
Sunday, 19 April 2026
Letter from Canada to Besigye, Kyagulanyi, and Museveni
May I humbly address you as real men on whom all Ugandans’ eyes are. I beseech you to face it and do the right thing for yourselves and your country. Thus, I address you as people with power though differently.
Firstly, I fully understand that you all have followers whose ambitions, expectations, and hopes you carry and fight for. May he perish whoever ignores this fact.
Secondly, you’re seasoned politicians/leaders who are supposed to be creative and dependable. If you lack what it takes to resolve your differences creatively and constructively, why should Ugandans keep on trusting you? May I say it point blank. Whoever is an impediment to what I’m to aver, must be viewed as a wrong person to carry even the hopes of animals let alone humans.
Thirdly, I understand. You’re all Ugandans. That’s nothing if one lacks patriotism and trust, which are the qualities that require everybody to do justice to himself and others as the citizens of one country.
Fourthly, just remember. Power is always evanescent. Nobody’ll have it forever despite what. Therefore, whoever abuses or tramples on the humanity and the rights of others must not be in any public office. For, he’s unfit even to herd a herd of wildebeest aka confusion.
Fifthly, you’re all Christians some of whom swear by lifting the Bible. If I go by and with what Christianity commands, your first commandment is love. Thus, you’re dutybound to love each other more than yourselves apart from your ‘enemies’ even in politics. Leaders are role models and teachers. What love do you teach through animosity, injustices, and tortures? I know. You’re not pretenders.
Mature men don’t fight over what doesn’t belong to them. Refer to the famous song by the Les Wanyika Sina Makosa. Like it’s in this song, power doesn’t belong to you. It only belongs to Ugandans but not to their leaders or ruler. Fighting for what doesn’t belong to you is like fighting over or killing for somebody’s lover or wife while you truly know she doesn’t belong to any of you. Who commits such folly? If you know that, then chuki ya nini ndugu zangu while the lady isn’t yours? Kindly, listen to that song for a reminder.
Seventhly, forgive each other so that you can be forgiven. Love each other so that you can be loved. Without loving each other and banking on hating and demolishing each other, nobody’ll succeed. No doubt. If you live by sword, you’ll die by sword. If you live by hatred, you’ll die by it. If you live by lies and manipulations, they’ll one day adversely affect you. Who sows thorns and walk barefoot? Remember that.
Eighthly, it’s utter madness to fight over something you can’t keep or permanently own. Power belongs to the people. Whoever seeks it must understand this and faithfully do and show that. As men of probity, you still have time to take a look in the mirror and do the right thing, especially for those who self-appointed to be the judge while they’re supposed to be judged in the court of public.
Lastly, I truly love you all. Similarly, love each other so that those you portend to seek to serve might love and trust you. That is my message from Canada.
Source: Daily Monitor Sunday today.
Waopanga au kutamani kuoa au kuolewa majuu wajue
Leo, tutaongelea visa vinne kama mfano ili kuonyesha changamoto wanazopata baadhi ya wale walioingia Marekani kwa kutumia njia ya ndoa. Kisa cha kwanza kinamhusisha mwanaume aitwaye Njamba (si jina lake halisi). Njamba alifanikiwa kumuoa mama mjane wa kimarekani aitwaye Mercy (si jinale halisi). Waliishi kwa furaha na amani kwa muda. Punde, mambo yakaanza kuharibika tokana na mke kutokubali kuishi maisha ya Kiafrika ambapo baba huwa na nguvu zisizopingika. Kwa Marekani, ni kinyume. Sheria za huku zinampa mama madaraka makubwa kuliko hata ya baba wa Kiafrika. Hivyo, mama anaweza kuamua kwenda likizo nchi yoyote peke yake na baba asiwe na uwezo wa kumzuia.
Piga picha. Hali inakuwaje kwa baba wa Kiafrika aliyezoea kummilki na kumpangia mkewe? Hii ndiyo hali iliyomkuta Njamba. Taratibu, alianza kujihoji kama ameoa au ameolewa. Katika kupambana na hali hii, Njamba aliamua kuonyesha uanaume wake. Alianza kutoa matishio kwanza. Baadaye, alianza kumtandika mkewe. Kwanza, mama hakuamini kama Mswahili angejiamini na kufanya haya. Wakati haya yakiendelea, wawili hawa walikuwa ndiyo wanamaliza kulipia deni la nyumba waliyoinunua kwa mkopo kama ilivyo kawaida huko Marekani.
Tokana na kuwa na deni la nyumba na kujua sheria na taratibu za Marekani vinavyompendelea mwanaume, mama alivumilia mateso kwa muda akisubiri wamalizie deni la nyumba naye afanye vitu vyake. Siku ya kwenda benki na kuagana nayo kwa kumaliza kulipia nyumba yao, mama aliruddi nyumbani na kuaza kujiamini na kujibu mapigo. Njamba hakuamini macho wala masikio yake kwa aliyoona na kusikia.
Kwa kujiamini kabisa, mama alimwambia kuwa alikuwa amechoka na mateso na hivyo, alitaka waachane. Kwanza, Njamba alidhani mkewe alikuwa akimtishia nyau asijue atafanya kweli. Mwezi ulipita halali ikiwa tete. Kumbe mama alishaenda kwa mwanasheria wake na kufungua kesi ya talaka bila hata mumewe kujua.
Siku ya siku, mama alirejea nyumbani na kumuamuru Njamba ahame toka nyumbani kwake. Njamba alishangaa, kuchukia, na kuhoji iweje wakati nyumba ni ya wawili? Mama alimjibu kuwa hayo hayajui wala hayamhusu. Isitoshe, alimwambia kuwa shauri la kuvunja ndoa lilikuwa tayari limeishafunguliwa mahakamani na Njamba angejulishwa wakati wowote.
Njamba aliapa kwa miungu yake yote kuwa asingehama kwenye nyumba yake. Naye, kadhalika alimtaka mkewe ahame kabla hajamfanyia kitu mbaya. Mama naye aliona kama alikuwa akitishia tu. Hivyo, aliinua simu na kupiga namba ambayo wengi huku wanaigopa kama ukoma yaani 911. Aliwajulisha polisi kuja haraka na kumhamisha mumewe toka nyumbani kwake kwa sababu alikuwa amemtishia angemfanyia kitu kibaya mbali na kumnyanyasa kindoa.
Kwanza, Njamba hakuamini masikio yake. Hivyo, alimuamuru mkewe kukata simu. Mama hakukubali. Aliendelea kupiga makelele kwenye simu akiomba polisi waje haraka. Bila hili wala lile, Njamba aliingia chumba cha kulala na kuchukua bunduki na kumpiga risasi saba na kumuua hapo hapo Mercy.
Baada ya hapo, alijigeuzia bunduki na kujimaliza. Hivyo, ndivyo ndoa ya majuu ya kuukata ilivyoishia kumkata Njamba baada ya kupitia mengi kiasi cha kukata tamaa na kuamua kuua na kujiua.
Kwa wale wanaopanga kuoa au kuolewa majuu bila kufanya utafiti na kujua tofauti za kimila na kijamii wajifunze kitu kuwa si kila king’aracho ni dhahabu.
Thursday, 16 April 2026
Is Iran war the beginning of the end of Hegemonia Americana?
Like any global superpower, the US enjoyed many feats but also created many enemies within and without in its own orbit before the then USSR came in as a challenger. However, in late 90s, the US outfoxed, demised the USSR, and remained as a sole superpower.
Although the Strait of Hormuz is in Iran and Oman, it’s a lot to do with US hegemony and economic muscles. It’s a door through which oil and gas pass to go to the world. Is it true that the US doesn’t have anything to do with the US, which doesn’t depend on energy from the Middle East?
Firstly, the gas and oil from the Middle East are priced and traded in the US dollar, hence petrodollar.
Secondly, the US makes billions of even trillions of dollars by selling weapons to the oil-rich gulf states.
Thirdly, it makes more money by protecting the monarchies in the region.
In the biggening, it was like a walk to the park. After Iran became a hard nut to crack, the US asked its allies to crack it for it. The duo flatly refused to be drawn into US’s war of choice. Thereof, Trump fired back saying that the US didn’t need them since they’re a tiger paper.
Typically, without gas flowing through the strait of Hormuz, American dollar will lose value just overnight. The world knows how the US benefits and depends on the Middle East oil after sabotaging and abandoning the gold standard wherein nations depended on the amount of gold they’d in treasurers.
Let the US know. Shall the war go on, the biggest victims won’t be Iran but the US. Why? That’s because the gas price will swell globally, which isn’t a problem only for the US. Again, since gas price is globally interconnected and depends on capitalistic conjectures, the US will become the first to suffer. Shall this happen, though it’s already started to happen, the Republicans will lose midterm elections, which is due soon.
In sum, is the war with Iran the beginning of the end of Hegemonia Americana?
Fyatu wafyatua vitegemezi vyake tegemezi japo virume
Inshu iko hivi. Mtoi wa mdosi wa kule wa zamani alikuwa anamilki mahekalu, madude ya bei mbaya usipime ambavyo hakuna maelezo ya miujiza iliyotumika kwa fyatu kula kulala alivyoipata. Je, aliupataje huu ukwasi ambao unawahangaisha na kuwashinda Mafyatu wachakalikaji? Simpo. Dingi wake alikuwa dingi wa kaya. Hivyo, kwa kutumia mamlaka na ubini aka surname wa dingi, jamaa alipiga njuluku ndefu pakubwa. Wakati wanakaya wakisota hadi kunyotolewa roho na ukapuku, mtoi alikuwa akijienjoi tu na kuwacheka na kuwashangaa. Je, wapo wangapi kama huyu chawa, au tuseme funza, barani kwetu? Kweli, usiposhangaa ya Abudili aka mtoi wa madili, utashangaa ya Dalie mwana wa rungu. Jamaa alikuwa na ndinga kama mia hivi na mihekalu kama hamsini. Hapa, hatujagusia njuluku alizosweka ughaibuni na zile anazotapanya akijichotea ujiko kumbe jizi tu. Anyways, hayo ndo maajabu ya bara letu linaloitwa kapuku wakati ni tajiri wa kunuka.
Juzi, tulifanya kikao cha ghafla na Bi Mkubwa na kudurusu kadhia hii nyemelezi ya mafyatu nyemelezi watumiao unene wa madingi au ndugu zao. Tulikuja na mkakati wa kuokoa mali za Mafyatu na kulinda hesima yetu. Baada ya hapo, tuliwaita vitegemezi wetu wote na kuwapasha inshu na uamuzi wetu kuntu.
Kwanza, hawakuamini. Walidhani tulikuwa tunawatania wakati huwa hatuna utani nao. Ilibidi waumie tu na kukubali haya mabadiliko adimu duniani japo kwa shingo upande.
Pili, walijaribu kupinga. Niliwapa wazi kuwa unene wangu si wao. Nao, wakatafute wao kama ni rahisi kama walivyokuwa wakifyatua njuluku za mafyatu kwa kunitumia. Mie ni faya na nomi kinomi. Siyo kama akina Mobutu na M7.
Nne, tumepiga marufuku kutumia ubini wetu kuwapiga Mafyatu. Tumewapa wazi kuwa tunachelea mafyatu wanaweza kufyatuka wakatufyatua kwa kuwafyatua kizwazwa. Wewe uliona wapi mtoto mchanga kunyonyesha? Uliona wapi?
Zamani, nilidhani wachunwao na vyaungudoa ni warume wakwere. Kumbe na wanene wanachunwa tena na vitegemezi vyao, jamaa, mashosti, na marafiki zao! Fyatu zima linaacha kuchapa kazi. Linanyonya na kuwafyatua mafyatu kwa vile ni rafiki, toi, au shosti la munene. Acheni uvivu. Tafuteni ngori mheshimike.
Kwa vile mie naona mbali, nimeamua rasmi kukomesha upigaji wa kutumia mamlaka yangu. Hata Bi Mkubwa tumekubaliana afute ile asasi yake ya ulaji Ulaji iitwayo BiMkubwa Opportunity and Maulaji ya Unene (BOMU). Hata ile bajeti iliyokuwa ikipangiwa ofisi yake nimeipiga panga. Lazima kieleweke. Kuanzia sasa, nakinukisha kwa wale wote wapenda dezo kwa kutumia migongo ya madingi wao wanene. Nimewaamuru vitegemezi vyetu kutafuta kazi halali. Kwa vile vimeishatimiza umri wa mafyatu wazima, havitaruhusiwa hata kupewa ndinga za mafyatu. Kwani, alivichagua nani na vinamtumikia nani zaidi ya matumbo na tamaa zao? Lazima tubadilike kabla hatujabadilishwa. Isitoshe, ulaji wa dezo na unene vina mwisho.
Katika kutenda haki, kuanzia sasa, nimetoa amri ya watoi wote wa wanene na wanene wenyewe kusoma alama za nyakati. Itawabidi wajiandae kusomea kwenye shule za Kayumba kama mafyatu wengine. Kwa wanene, hakuna kupeleka watoi ughaibuni au kwenye intaneshno skuli wakati shule na vyuo tunavyo hapa tena vya kumwaga. Hii, itasaidia kuwazuia wanene kupiga njuluku za mafyatu. Pia, natoa amri wanene wote kwenye Fyatuland kuacha kwenda ughaibuni kujichunguza afya zao wakati hapa tunayo mahospitali lukuki.
Kuongoza kwa mfano, nimeamuru vitegemezi vyetu viwili vilivyogoma kwenda chuo, vitafute vyuo na kuchukua nkopo kama mafyatu wengine. Hakuna cha kutegemea jina langu tena kuishi dezo kana kwamba havina mikono na vichwa. Nimechukua hatua hizi adimu duniani kwa kuogopa kuendelea kuwafyatua mafyatu hadi wafyatuke wanifyatue. Mwenye macho asikie uzuri tu. Mwenye masikio ajionee.
Lazima ningoze kifyatu tena kwa mfano. Kuanzia sasa, hakuna ndugu yangu awe wa kweli au wa kuokoteza atapewa upendeleo. Hata kule kijijini kwetu ambako tulikuwa tumeanza miradi ya upendeleo, nimepiga kalamu. Nimesemaje? Kwani, niko wapi?
Chanzo: Mwananchi, Aprili 9, 2026.
Ndoa ya majuu inapogeuka shubiri na maafa
Kijijini kwa Bibby kulikuwa na James mtoto wa maskini aliyebahatika kwenda majuu na kuukata.
Muda hakupita, Bibby alikwenda kwa wazazi wa James na kuomba namba yake ya simu. Wazazi walifurahi na kumpa namba ya simu. Bila ajizi, Bibby alimpigia simu James akiuliza ni kwanini alimsahau. Kwa vile James alikuwa amekamia kumuoa, aliona kama ndege kajiingiza mtegoni mwenyewe. Hivyo, aliomba wakutane sehemu ya faragha lau waongee mawili matatu. Bibby alifurahi na kukubali kwenda kukuta na James. Wahenga waliasa. Usitukana mkunga na uzazi ungalipo na isitoshe hakuna ajuaye ya kesho.
Siku ya siku ilipofika, wawili walikutana kwenye hoteli moja maarufu mbali na kijijini kwao. Mambo yalikwenda haraka. Waliongea, wakala, wakanywa, wakapanga, hadi wakalala kule. Haraka haraka, Bibby alimwambia James kuwa alikuwa akimpenda na wala hakumkataa bali kumpima uvumilivu wake ambao siku hii ulikuwa umelipa.
Mipango ya ndoa ilipangwa na ndoa ikafanyika tayari kuanza kuishi kama mke na mume. Moyoni mwa wawili hawa, kila mmoja alijifariji kuwa alikuwa amempata mwenzie wasijue wamepatikana wote. Kiukweli, Bibby hakumpenda James bali alitaka amtumia kama pasi ya kuingia majuu na mengine angejua huko huko.
Naye James hakumpenda Bibby bali alimtaka tokana na urembo wake. Na alijua fika kuwa Bibby alikubali amuoe kwa vile alikuwa keshaukata na anaishi majuu. Nani angekataa fursa hii tena iliyojileta yenyewe toka kwa mtu ambaye amewahi kumuudhi kwa kumkatalia ndoa?
Wawili hawa walifunga ndoa. Muda wa James kuondoka kurudi majuu ulifika. Aliondoka na kumuacha Bibby kwa wazazi wake akimuahidi kumtumia tiketi au kumjia ili waende kuishi wote majuu. Bibby na wazazi hata marafiki walifurahi sana. Muda haukupita, James akarudi kuja kuchukua mkewe ambaye alimuacha tayari mjamzito baada ya Bibby kumtegeshea mimba ili asibadili mawazo au kushawishiwa na mabinti wengine pale kijijini waliokuwa wakimmezea James mate.
Wawili waliondoka kwenda zao majuu. Baada ya Bibby kufika majuu mambo yalibadilika. James alianza kumnyanyasa na kumsimanga kuwa hakumpenda kwa dhati isipokuwa kwa sababu ya mafanikio yake jambo ambalo lilikuwa kweli. Naye Bibby alijibu mapigo kwa kumwambia James kuwa hakumpenda bali kumtaka kwa uzuri wake na kumkomoa kiasi cha kumsimanga kwa mambo ya zamani.
Bibby alikuwa akiishi majuu kwa kutegemea vibali vya kuishi vya mumewe. Hivyo, asingeweza kufurukuta bali kuvumilia hadi apate vyake. Muda ulizidi kwenda na Bibby akaongeza watoto wawili huku akipanga kulipiza kisasi siku ambayo angepata vibali vyake amuache James na kuanza maisha yake akiwa mtu huru.
Muda haukupita Bibby akapata vibali. Bila kungoja, alimwambia mumewe nia yake ya kutaka kuachana. Kabla ya kufanya hivyo, Bibby alipata ushauri kuwa kwa vile watoto wao walikuwa bado wachanga, kama wangeachana, angebaki na watoto na serikali ingemsaidia kuwatunza na pia kwa kumlazimisha James atoe pesa ya matunzo ya familia.
Kwa kuwa na haki ya kukaa na watoto, pia Bibby alipata haki ya kubaki na nyumba yao. Hili, halikuingia akilini mwa James aliyembembeleza warudi nyumbani Afrika walimalize. Bibby alikataa katakata.
James aliamua kumuua kwa kumpiga na kitu kizito na kunyonga watoto wao na kukimbia hadi alipokamatwa na kufungwa maisha na ndoa ya majuu ikaishia kuwa maanguko ya wote.
Msiuane kwa mali mtakamatwa au kuziacha
Kwa wale wa kizazi chetu, yaani wa kuanzia miaka 50 kwenda juu, wimbi la mauaji baina ya wanandoa wakigombea mali ni jambo ambalo halikuzoeleka japo lilikuwapo si kwa kiwango cha sasa. Hata hivyo, kwa wengi waliokua wakati wa mfumo wa ujamaa, tulifundishwa kutopenda vitu bali utu. Hata hivyo, hii haizuii zile jamii zinazojulikana kwa uovu huu ambazo ziliendelea na tamaa, unyama na uvivu wa kutafuta vya kutaka kuvuna wasipopanda. Kwanini kuaana kwa ajili ya mali kana kwamba mtaondoka nazo mtakapokufa?
Ni ukatili na unyama kiasi gani kuuana kwa ajili ya vitu vinavyoweza kutafutwa vikapatikana? Tokana na matukio mengi tuliyodurusu kwa muda kitambo, tuligundua kuwa hao wanaowaua wenzao ili wachukue mali peke yao, mara nyingi, hubainika na kuishia gerezani kama siyo damu za waliowaua kuwataabisha.
Kuna kisa kimoja cha kusikitisha kilichotokea nchini Marekani mwaka jana kwenye jimbo la Texas ambako mwanamke mmoja katili alimuua mumewe kwa kumpiga risasi tatu ili achukue mali zake za mamilioni. Pamoja na kujitahidi kuficha ushahidi ukiwamo mwili wa marehemu aliyetoweka, alikamatwa. Sasa anangojea haki ichukue mkondo wake akiwa korokoroni.
Mama huyu unayeweza kumuita shetani, aliuficha mwili wa marehemu chini ya sehemu ya kuhifadhia takataka na kudai kuwa mume wake alikuwa nchi jirani akijirusha na kimwana wakati alishamnyongelea mbali. Baada ya majirani kutomuona mume, walipiga simu polisi ambao walikuja na kumhoji akatoa taarifa za kujichanganya na kuwafanya watafute hati ya upekuzi na kugundua mwili wa marehemu ukiwa umeishaoza baada ya kufichwa kwa miezi minne.
Katika kufuatilia visa hivi vya kikatili na kinyama, tuligundua kuwa wengi wa wanaofanya unyama huu ni wavivu wa kutafuta, wakatili, wajinga, waroho na wapenda vya dezo. Kwanini kumuua mwenzio tena kwa mali alizotafuta mwenyewe kama kweli wahusika siyo kama chawa wapendao kunyonya wenzao? Hata chawa huwa hawawaui wale wanaowanyonya.
Pamoja na madhaifu tajwa hapo juu, kesi nyingi za aina hii zinaonyesha kuwa kuna uwezekano wa ugonjwa wa akili unaowasumbua wauaji hawa ambao hawana tofauti na wauaji wengine. Wapo wanaosema kuwa mauaji na ukatili huu ima husababishwa na chuki, hasira, visasi, woga, na mengine mengi kama hayo yatokanayo ya kuachika au kuchelea kuachika.
Katika baadhi ya jamii, yapo makabila yenye mchezo huu yatokanayo na mashindano na tamaa ya utajiri. Watu hawa huolewa kwa makusudi wakijua wanachopanga kufanya baadaye. Mara nyingi, huwalenga wenye nazo na siyo hohehahe. Katika jamii hizi mke au mume kumuua mwenzake kwa ajili ya tamaa ya utajiri wa haraka ni jambo la kawaida.
Kitu kingine kilichojitokeza kwenye jinai na kadhia hii ni wahusika kuishia kutofaidi hizo mali japokuwa wapo wachache wanaofanikiwa. Hata hivyo, bado wanaonusurika huishi kwa matatizo yawe ya kiafya au kiakili tokana na hisia za hatia waliyotenda. Japo hatujafanya utafiti wa kisayansi, kuna imani kuwa yeyote amwagaye damu ya mwenzake, damu hiyo itamuandama. Kuna ukweli katika hili. Wauaji wanaweza kuficha mateso wanayopata au kupitia, ukweli ni kwamba wanatesema kwa hatia hasa nyoyoni mwao.
Mwisho, badala ya jamii kuangalia na wengine kushabikia hata kushangilia hawa wale wenye uvivu wa kutafuta lakini wakawa na tamaa ya mali, inabidi ianze kuchukua hatua kama vile kupinga ujahili na unyama huu. Ukitaka kujua ukweli wa haya tunayoandika, kama kuna yeyote aliyewahi kufanya hivi unayemjua au kumsoma, jikumbushe mwisho wake. Wengine wanaishi kwa kutegemea madawa ya usingizi na ulevi kutokana na mateso ya dhambi na ukatili walivyowafanyia wenzao. Haiwezekani uue ambacho huwezi kukiumba uwe salama. Na kama utakuwa salama ni kwa muda.
Thursday, 9 April 2026
Fyatu afyatua vitegemezi vyake tegemezi na wapenda dezo mgongoni mwake
Sunday, 5 April 2026
Msiuane kwa mali mtakamatwa au kuziacha
Kwa wale wa kizazi chetu, yaani wa kuanzia miaka 50 kwenda juu, wimbi la mauaji baina ya wanandoa wakigombea mali ni jambo ambalo halikuzoeleka japo lilikuwapo si kwa kiwango cha sasa. Hata hivyo, kwa wengi waliokua wakati wa mfumo wa ujamaa, tulifundishwa kutopenda vitu bali utu. Hata hivyo, hii haizuii zile jamii zinazojulikana kwa uovu huu ambazo ziliendelea na tamaa, unyama na uvivu wa kutafuta vya kutaka kuvuna wasipopanda. Kwanini kuaana kwa ajili ya mali kana kwamba mtaondoka nazo mtakapokufa?
Ni ukatili na unyama kiasi gani kuuana kwa ajili ya vitu vinavyoweza kutafutwa vikapatikana? Tokana na matukio mengi tuliyodurusu kwa muda kitambo, tuligundua kuwa hao wanaowaua wenzao ili wachukue mali peke yao, mara nyingi, hubainika na kuishia gerezani kama siyo damu za waliowaua kuwataabisha.
Kuna kisa kimoja cha kusikitisha kilichotokea nchini Marekani mwaka jana kwenye jimbo la Texas ambako mwanamke mmoja katili alimuua mumewe kwa kumpiga risasi tatu ili achukue mali zake za mamilioni. Pamoja na kujitahidi kuficha ushahidi ukiwamo mwili wa marehemu aliyetoweka, alikamatwa. Sasa anangojea haki ichukue mkondo wake akiwa korokoroni.
Mama huyu unayeweza kumuita shetani, aliuficha mwili wa marehemu chini ya sehemu ya kuhifadhia takataka na kudai kuwa mume wake alikuwa nchi jirani akijirusha na kimwana wakati alishamnyongelea mbali. Baada ya majirani kutomuona mume, walipiga simu polisi ambao walikuja na kumhoji akatoa taarifa za kujichanganya na kuwafanya watafute hati ya upekuzi na kugundua mwili wa marehemu ukiwa umeishaoza baada ya kufichwa kwa miezi minne.
Katika kufuatilia visa hivi vya kikatili na kinyama, tuligundua kuwa wengi wa wanaofanya unyama huu ni wavivu wa kutafuta, wakatili, wajinga, waroho na wapenda vya dezo. Kwanini kumuua mwenzio tena kwa mali alizotafuta mwenyewe kama kweli wahusika siyo kama chawa wapendao kunyonya wenzao? Hata chawa huwa hawawaui wale wanaowanyonya.
Pamoja na madhaifu tajwa hapo juu, kesi nyingi za aina hii zinaonyesha kuwa kuna uwezekano wa ugonjwa wa akili unaowasumbua wauaji hawa ambao hawana tofauti na wauaji wengine. Wapo wanaosema kuwa mauaji na ukatili huu ima husababishwa na chuki, hasira, visasi, woga, na mengine mengi kama hayo yatokanayo ya kuachika au kuchelea kuachika.
Katika baadhi ya jamii, yapo makabila yenye mchezo huu yatokanayo na mashindano na tamaa ya utajiri. Watu hawa huolewa kwa makusudi wakijua wanachopanga kufanya baadaye. Mara nyingi, huwalenga wenye nazo na siyo hohehahe. Katika jamii hizi mke au mume kumuua mwenzake kwa ajili ya tamaa ya utajiri wa haraka ni jambo la kawaida.
Kitu kingine kilichojitokeza kwenye jinai na kadhia hii ni wahusika kuishia kutofaidi hizo mali japokuwa wapo wachache wanaofanikiwa. Hata hivyo, bado wanaonusurika huishi kwa matatizo yawe ya kiafya au kiakili tokana na hisia za hatia waliyotenda. Japo hatujafanya utafiti wa kisayansi, kuna imani kuwa yeyote amwagaye damu ya mwenzake, damu hiyo itamuandama. Kuna ukweli katika hili. Wauaji wanaweza kuficha mateso wanayopata au kupitia, ukweli ni kwamba wanatesema kwa hatia hasa nyoyoni mwao.
Mwisho, badala ya jamii kuangalia na wengine kushabikia hata kushangilia hawa wale wenye uvivu wa kutafuta lakini wakawa na tamaa ya mali, inabidi ianze kuchukua hatua kama vile kupinga ujahili na unyama huu. Ukitaka kujua ukweli wa haya tunayoandika, kama kuna yeyote aliyewahi kufanya hivi unayemjua au kumsoma, jikumbushe mwisho wake. Wengine wanaishi kwa kutegemea madawa ya usingizi na ulevi kutokana na mateso ya dhambi na ukatili walivyowafanyia wenzao. Haiwezekani uue ambacho huwezi kukiumba uwe salama. Na kama utakuwa salama ni kwa muda.
Chanzo: Mwananchi Jpili leo.
