Utafiti huu wa kidoktari na kifyatu uligundua mambo makuu yafuatayo:
Pili, familikrasia inachukiwa kwa sababu huhalalisha ufyatuaji mkubwa wa njuluku za mafyatu kutokana na uroho uliojificha nyuma ya UKUKU.
Tatu, utafiti umegundua kuwa wengi, kama si wote, wa walaji hukosa vigezo vya kisomi isipokuwa ukaribu uwe wa kiukoo au kirafiki na mteuaji. Hivyo, wengi huwa mazwazwa na wasanii wa kawaida wasio na sifa yoyote hata ya kuongoza kundi la nyumbu.
Nne, familikrasia hujihadaa na kujenga mfumo wa utukufu uchwara ambao msingi wake mkuu ni kutumia vitisho na kuzawadiana ili kuhimili vishindo vya uchakavu, ufisadi, na ulazimishi wake. Hii inapotokea, hujengeka upofu au myopia kwa kisambaa ambao nao hujenga kujisahau na kutojiamini kiasi cha kila asiyekuwamo kuonekana adui na tishio. Hivyo, huleta ukandamizi, usanii, ubabaishi, n.k. Muhimili wa familikrasia ambao ni kichwa chake hujijengea uungufyatu kiasi cha kutengeneza viini vya kujiteketeza wenyewe.
Tano, familikrasia hulindwa kwa woga na kushuku. Hili, husababishwa na kupwaya na kutokubalika vizaavyo kutojiamini, kuaminika, na woga.
Sita, familikrasia hubebwa na ukosefu wa aibu, udhu, ufyatu, na ukatili vya kutisha. Mfumo huu, unaweza kuua yeyote anayetaka kuuzuia, kuupinga, kuukosoa, hata kuuondosha. Hivyo, kusababisha maumivu kwa mafyatu mbali na kuwanyonya.
Saba, familikrasia hutegemea sana matumizi mabaya ya njuluku na raslimali za mafyatu hongo ya, ulaji, maguvu, majungu, vishawishi, ghilba, na vitisho. Kwa mtoi wa rafiki yangu, rahis wa zamani tena jobless, kilikutwa na mimamli kibao iliyotaifishwa. Je,viko vingapi duniani hii gunia?
Nane, familikrasia hutegemea kulindana, kung'ang'ania unene ukichelea kung’olewa ambapo jinai yake hufichuka na kuishia ghaibu au lupango hata kuuawa kama ilivyotokea kwa watajwa hapo juu.
Tisa, utafiti umeonyesha kuwa UKUKU, kwa mfano, kuna uwezekano wa wahalifu wa kiunene kunyatuliwa roho na mafyatu wenye hasira wanapouchoka na kuamua kuuangamiza usiwaangamize.
Matokeo ya utafiti
Dokezo
Pamoja na kushauri utafiti zaidi, tunapendekeza waathirika si kuuchukia tu ufamilikrasia bali waukabili na kuuondolea mbali ili kupata HAKI na maendeleo kwa ujumla. Katika penye ufamilikrasia kunakuwapo na amani mawenge ambapo haki na usawa hutoweka kiasi cha kaya kuwa kama pango la majembuzi. Hivyo, dawa ya kuondokana na ufamilikrasia ni kuwapo na kutamalaki kwa haki, maadili, na mageuzi ya kweli kimfumo.
Mwisho, ufamilikrasia ni jinai inayoanza kuzoeleka na kuota mizizi katika kaya nyingi za uswekeni hasa zinazojifanya kuendelea. Ushauri ni kwamba uchukiwe na kupigwa vita kulhali na na kuogopwa kama ukoma. Hii bangi, hivi niko wapi na nafanya nini yarabi!