The Curse for Salvation
Thursday, 26 March 2026
Rest in Peace My Dear Friend Assumpta Ocam Oturu
Thursday, 19 March 2026
The US must urgently learn from Africa
Before Trump’s re-election, the Federal Bureau of Investigation (FBI), at old hours, stormed Donnie’s Mar-a-Lago beautiful mansion. I was frozen. How do you send FBI sleuths to comb, swoop, and vandalise the home of the former and future President? Yes. According to Donnie then, the sleuths took some boxes from his mansion. When some of Donnie’s diehards spitefully thought his successor and predecessor, Joe Biden’s behind his predicaments, guess what? The then US Attorney General Merrick Garland whom Donnie appointed got the guts and heroically came forth and said he’s the one who decided to dispatch FBI to commit that sacrilege! Can any African director of whatever security outfit replicate this and survive?
Donnie must blame himself on not conscripting his sons in the army and for not them high ranks to see to it that they protect their family rule. Erickie and Donnie Jr would make very beautiful soldiers God’s ever created. They’d be in the class of Keineruxxba and others whose fathers drafted in their private so-called national armies to protect their family rules. If there’s anything that Donnie perfected is nothing but appoint his Daughter’s husband, Jerry Kushnei his advisor who pulls more strings than his siblings-in-law.
To perfect their ‘sacrilegious’ complot against Donnie and his empire and illegally and needlessly shame him, the FBI went in the middle of the night and disturbed the peace of the man and the first woman, who lives her American dream! Who, in Africa, can shamelessly go to the first house to search the residence of the biggest man or woman in the land under whatever pretexts and get away with murder? No officer worth his or her salt can search even big man’s or woman’s barns. Hajitaki huyu?
Hear what Garland said. “I personally approved the decision to seek a search warrant in this matter” (USA Today,11 August, 2022). When asked about the kind offence Donnie might had committed, Garland said that there “probable cause”, yada, yada, yada that Donnie might have committed a crime. How can a god commit a crime like possessing hush-hush materials while he or she knows everything about the country since it’s under her/his control? Donnie called the assault on Mar-a-Lago a pure witch hunt. Wow! How do you turn a President into a witch then hunt him or her? In Africa, it’s unthinkable and doesn’t add up for the President to break any law while s/he’s above the law, the law, and the constitution. Americans need to go to Africa to learn jurisprudence and its interpretations. Their sanity has petered out.
If Donnie were an African President, he’d have abolished the FBI. I’ve never understood why the US kept the President who controls the country like his private estate and can appoint his kids, wife, courtiers, and friends as he deems fit to help him milk, sorry, run his estate known as country aka banana republic to be precise. Is the US becoming a banana republic in its own light for the lack of respect to its leader let alone familicracy and nepotism?
How on earth can a sane person or organisation suspect the President, his family, or networks of any criminality? Why do Americans disrespect their leaders by denying them the infallibility and right to be above the law like their sacrosanct African colleagues? Who bewitched Americans in the first place?
Source: The Citizen, Thursday today.
Wednesday, 18 March 2026
Fyatu anapomkumbuka Fyatu Joni Kanywaji Makufuli
Najua unanisikia hata kama hutanijibu. Katika kumbukizi hili, mafyatu wenzako tunakukumbuka kinamna. Wapo wanaokulilia na wanaoshangilia kutegemea na hali. Leo, sitachonga sana bali kufyatuka.
Kwanza, wasalimiwa na mafyatu wako wote na wananzengo. Tunakumiss kifyatu.
Pili, pole kwa sababu, kama ulivyokuwa ukisema, kuna mafyatu utawashangaa. Ungerudi, ungejinyotoa roho namna mambo yalivyovurugika. Mfano, mafyatu na majipu uliyokuwa ukiyatumbua yalisharejeshwa na yanazidi kutanuka na kutanua. Juzi, wapigaji wa mwendofasta waliachiwa.
Tatu, unaweza kufyatua vibao mafyatu, tena uliowaamini na kutengeza. Si ulisema kuwa watakaofyatua Bwagamoyo ni mataahira na mazwazwa. Kumbe uliwajua! Ungekuwepo, nadhani eheee, kingeleweka. Hata hivyo, ujue. Simba akifariki, panya hutafuna ngozi yake. Ndviyo ilivyotokea. Yale ambayo hukuwahi kudhani yangetokea, yeshatokea zamani. Mafyatu waliogoma kufyatuka wakafyatua sasa wanafyatuliwa kama hawana akili nzuri.
Nne, ungerejea, kabla ya kujinyotoa na kufyatua watu mbanta, ugepata kichaa. Maana, wengi uliodhania wafuasi wako sasa wanaimba ngonjera na nyimbo za kukukandia na kukukana. Juzi, nilisikia mmoja uliyemtoa mikoani na kumpa kipaza sauti akisema eti wewe hukukusanya gold! Si alirambishwa asali, wengi siyo walikusaliti tu, bali wanapmbana kulihalli usahaurike kana kwamba hukuwahi kuwapo na kutisha.
Tano, mwaka jana kuna mafyatu waitwao ‘mamluki’ walikinukisha wote tukanuka hadi kufyatuana shaba. Wengine walifanyiwa kale ka mchezo ulikoacha. Wasiojulikana bado wapo. Waliwafyatua, kuwapoteza na wengine kuwanyotoa roho. Shaba zilitembea mitaani usipime.
Sita, walitokea mabeberu wakatuma mamluki wakatuonea wivu na kuja kuvuruga amani yetu. Walitutaimu siku ya uchaguzi wa amani na mshikamano. Walitaka kuuvuruga tukawavuruga ile mbaya tena kifyatufyatu. Siku hiyo, amani ilivugika hadi shaba zikageuka lugha pekee. Mwaka jana mwezi wa kumi tarehe 29 haitasahaulika kwa mafyatu siku walipokinukisha hawa mamluki hadi kisiwa cha amani kikageuka kisiwa cha vita na umwagaji damu ambavyo havikuwahi kutokea.
Saba, pamoja hila na wivu wao, tunamshukuru Mungu, rahis wetu alishinda kwa asilimia 98. Mbili zilizobaki ziliibiwa na wapingaji wachoyo wa madaraka. Baada ya kukinukisha na kufyatuana, sorry, kuwafyatua mamluki, tuliunda tume ya kujichunguza lau tujue nani alizembea hadi kikanuka. Wapo mabeberu waliotucheka na kutuzodoa kuwa tunawezaje kujichunguza. Hebo! Bila kujichunguza, utawezaje kujisuta. Hawa walitaka tuite wengine watuchunguze halafu watusute wakati tunaweza kufyatua vyote viwili, yaani kujichunguza na kujisuta na kuwatuliza mafyatu waliofyatuliwa tokana na uzwazwa wao wa kukataa kufyatuka wakafyatua hadi wakafyatuliwa.
Nane, nadhani unakumbuka wale mafyatu wa akina yero kule Ngolongolo. Walishafyatuliwa zamani gani. siku hizi wako ugosini wakijifunza kukata vikalio na kuacha na ngoma zao za kurukaruka. Ilibidi tuwafyatue ili kupisha uwekaji ili kujiongezea kipato.
Tisa, kabla sijasahau, ule uwanja wako wa home ulishadoda. Sikujua kuwa wewe ndo ulikuwa bidhaa kuu iliiyokuwa ikiupa shavu! Baada ya kuondoka si kila kitu kiliondoka. Naomba unisamehe. Usidhani nilikufyatua ua kukusaliti. Hapana. Hata ile biashara yangu ya hoteli niliyokuwa nimefungua Chato niliishafunga baada ya kukosa wateja. Napanga kuihamishia kule Kizinkazi ambako siku hizi ndiko kunatesa. You know what I mean.
Kumi, japo ulizuia watoi wako kushiriki siasa, siku hizi Jessie ni mheshi wa viti maalum. Tangu ulipoondoka aligeuka maalum kiasi cha kupewa kiti maalum tokana umaalum wake utokanao na wako.
Kumi na moja, unakumbuka ile kauli mbiu yako ya kutetea wanyonge? Tangu uondoke na unyonge ulikufuata hadi unatendewa kinyonge. Siku hizi, hakuna mnyonge hata mmoja. Ila wanyongaji bado wapo hasa wale maadui wa amani na mshimano wetu kama wale tuliowafyatua walipotaka kuvuruga uchaguzi wetu kwa vurugu badala ya kufanya hivyo kwa amani na mshikamano. Tuliwashika kwa mshikamano na kuwatia adabu kwa amani.
Baada ya kuondoa unyonge, wapo waliopagawa hadi wakageuka machawa. Zamani chawa walikuwa wadudu. Siku hizi uchawa au kuwa chawa ni sawa na kuwa superstaa. Tuna machawa kila aina. Wako wa maza, wa faza, hata chawa wa machawa. Kuna machawa wadogo, wakubwa, wanene, walikonda na wengine kama hao. Pia, wapo wanaojipendekeza, kujikomba, kujituma, kutumwa na wa kila aina.
Kabla sijasahau, nadhani swahiba yako Rao aka Jaduong Maduong yule wa kaya ya jirani wakimuita baba mshaonana au hajafika. Si naye aliwageuka Gen Ziro w akule walipokinukisha akajiunga na Kasongeyeye mobali nangai. Acha afyatuliwe kuwa alijigeuza msaliti. Alisononeka hadi akaresha namba akiwa amechafuka. Kuna mafyatu wanaodai kuwa alifyatuka kwa sababu ya usaliti uliosababisha umwagaji damu.
Kabla ya kusahau, wajua? Si kwa Joji kichaka walimchagua chizi aitwaye Donnie Tarampu. We, acha ainyooshe dunia. Ninavyochonga, yupo anazipiga na waajemi kiasi cha kupandisha wese. Ila anazidi kuzidiwa pumzi hadi anaomba nimpe tafu.
Mwisho, kuna busara ambayo sikuielewa ila leo naielewe. Kumbe asikuwepo na lake halipo! Kumbe hata kupe anaweza kuwa mkubwa na mwenye maguvu kuliko tembo aliyemnenepesha hadi akawa hivyo huku tembo akigeuzwa mdogo kuliko inzi. Du! Kumbe naota mchana!
Chanzo: Mwananchi Jtano leo.
Sunday, 15 March 2026
Yawezekana kufanikisha ndoa na mengine
Je, huwaje kunakuwapo watu waliofanikiwa kitaaluma, kiuchumi, na mengine lakini wakashindwa katika ndoa? Pia, kwanini kuna watu waliofeli katika mambo mengine lakini wakafanikiwa katika ndoa? Siri hapa ni nini? Mfano, unakuta mtu ni tajiri lakini maskini wa ndoa. Mwingine ni msomi wa kupigiwa mfano lakini asiye na ndoa au kama anayo, inayumbayumba au kukosa ladha na raha.
Wapo matajiri wa kuitwa utajiri lakini hawamo katika ndoa au ndoa zao zimevunjika. Jikumbushe watu waliofanikiwa kama vile Mfalme Charles wa Uingereza, Bill Gates, Donald Trump, Jeff Bizos na wengine ambao ni watu waliofanikiwa katika nyanja mbali mbali lakini ndoa ziliwashinda hadi zikavunjika au kuwa na maskandali kila uchao. Walinganishe hawa waliofanikiwa na watu wa daraja lao kama vile Tadashi Yanai tajiri mkubwa Japan, Warren Buffet, Zhong Shanshan tajiri mkubwa wa China, na wengine ambao ni matajiri wenye ndoa za kupigiwa mfano. Je, kuna siri gani katika kushinda na au kumudu taasisi tata lakini nyeti ya ndoa?
Jiulize. Ni wamama tena matajiri au wasomi aka mishangazi japo hatupendi kushabikia neno hili wangapi wanaishi bila ndoa tena wengine wakitamani au kutangaza kutaka kuolewa wasiolewe? Wakati huo huo, unaweza kumkuta muuza baa akiwa kaolewa na anafaidi ndoa!
Je, hapa, tatizo ni wahusika au jamii? Nini suluhu ya kadhia hii? Maswali haya chokonozi na tekenyeshi kifikra yanajibiwa na the American Boys and Men (2025) ambalo linabainisha kuwa ni asilimia 50 tu ya wanawake wasomi wanaoolewa tena na wasomi wenzao. Nusu ya idadi iliyobaki, huolewa na watu wasio wasomi. Waliobaki wanabakia bila ndoa.
Tumalizie. Ni wangapi unaowajua wanaojikuta katika hali hii tuliyodurusu? Je baadhi ya mafanikio ni chanzo cha maanguko katika ndoa na baadhi ya maanguko ni chanzo cha mafanikio katika ndoa? Ama kweli wahenga walinena kuwa Mungu hawezi kukupa au kukunyima vyote. Anakupa hiki au hivi na kukunyima vingine. Je, wewe kati ya mafanikio ya vitu na ndoa, unaridhika au kuchagua kipi? Kila la heri wanandoa na watalajiwa wote.
Wednesday, 11 March 2026
Kwanini watoi wanaonewa bure?
Wapendwa na waogopwa tena mlioko juu, kwanza, nikiri. Najua kayani tuna watoi watundu waliokosa adabu, wavuta bangi wanaodaiwa kupenda njuluku kiasi cha kuhongwa na kutaka kubomoa hata kuchoma moto kaya yetu pekee waliyotuachia baba na babu.
Nimehuzunishwa na kushangazwa na wazushao kuwa hawa watoto watundu walihongwa tena na mbuzi dume wachome kaya moto. Wapi ushahidi? Ilinishangaza sana kuona mafyatu wazima wakifanya mambo ya kikumbaff kiaisi. Yawezekana wamefanya hivyo kutokana kuwa mafyatu wanaoweza kufyatuka na kufyatua lolote ima kugoma au kugopa kuwafyatua tukafyatuana kikaeleweka. Sijui ni kwa sababu ya uzushi au kutaka kukwepa lawama.
Kuna niliowasikia runingani na kuwaona redioni baada ya watoi watundu kufyatuka, kufyatua na kukukera, hawataki fyatu yoyote alalamike wala kuulizia hatma yao. Wapo waliolalama na kulaani sana wapanzi walioshindwa kuwafunza watoi wao adabu hadi wakaikosa na kutishia kutuumiza wote kayani. Katu, sikubaliani na hii dhana, dhuluma, na rongorongo uchwara.
Kingine nijuacho, hawa watoi watundu wengi wanatoka shule za Kayumba. Kama wangesoma intaneshno na Kimombo media, wasingekuwa watundu hivi bali kama kuku wa kitasha. Wangekuwa wamezaliwa kwenye hos za bei mbaya, wasingekuwa na utundu wala utukutu bali utanuaji tena wa dezo. Hivyo, nadhani sababu ya watoi kuwa watundu hadi wakataka kuchoma kaya ni ukapuku wa madingi zao. Mtoi anayelala kwenye ngwarangwara akielekea shulee hawezi kuwa na adabu wala tabia. Hawezi kuwa sawa na wale wanaoendeshwa kwenye midude ya bei mbaya ambayo ni full viyoyozi kama wa wanene. Hawezi huyu maskini. Ni kama tunawaonea au hatuwaelewi. Kama tunawaelewa, basi hatuelewi, hawatuelewi na hatuelewani.
Juzi, kuna watoi wakorofi walivunja vikombe na kupiga mateke sufuria na mambo mengine. Bahati mbaya, wale walinzi wetu si waliwaunguza mikono eti wakiwaadhibu!
Juzi, nilipita kijiweni. Niliyosikia yanatisha. Kumbe watoi watundu wenzao wanasema lazima walinzi washikwe na kushikishwa adabu hadi wawaonyeshe wenzao au miili yao badala ya kujitoa ufahamu na kukaa kimya kana kwamba waliopotea ni wadudu. Wanataka kujua nani alimuamuru kuua watoi wachanga tena kwa kuonyesha utoto wao. Mashambenga na wabaya wanazoza wazi kuwa kuwa kuna ubaguzi hasa kuwaacha walinzi wawaue kwa vile ni wana wa kufikia.
Nani kawalipa nani na wangapi, nini, kiasi, na lini ili apate nini na kwanini? Je, ‘vyombo’ vilikuwa wapi? Tumuamini na kutomwamini nani?
Sunday, 8 March 2026
talaka yenu inawafundisha nini watoto wenu?
Tutatoa mfano wa rafiki yetu toka Jimboni Darfur, Sudan. Huyu bwana ana mke mmoja. Kanada, ndoa za mitala haziruhusiwi. Ajabu, huwa halali kitanda chumba wala kitanda kimoja na mkewe. Siku moja walitutembelea kama familia ya kulala kwetu. Ilipofika wakati wa kulala, tuliwaandalia chumba mke na mume Pia, kuwaandalia watoto wao vyumba viwili tofauti. Bila hili wala lile, wanandoa walituita kona. Walisema vyumba vitatu tulivyowatengea vilikua vingi. Walihitaji viwili tu. Tulishangaa.
Tuliuliza kwanini wakati walikuwa wana watoto jinsia tofauti ambao tusingewalaza chumba kimoja. Walijibu kuwa watoto wa kike wangelala na mama yao, na wa kiume wangelala chumba kimoja na baba yao. Hatukuwapinga. Ila tuliwashangaa.
Zamu yetu ilipofika kuwatembelea, walitupangia vyumba viwili badala ya vitatu. Walitushangaa tulipouliza ni kwanini? Marafiki hawa walisema kuwa, kawaida, hawalali mke na mume pamoja. Tulishangaa hakuna mfano.
Hata hivyo, katika kuwadurusu kujua ni kwanini hawalali chumba wala kitanda kimoja, mume alijibu kuwa walikuta wazazi wao wakiwa na utaratibu huo. Katika kuzidi kuwadurusu, tulishangaa kugundua kuwa wazazi tajwa walikuwa na wake wengi. Hivyo, kwa kuzingatia kuwa waliishi kwenye vijumba vidogo vilivyojengwa sehemu moja ndani ya boma moja. Baba alikuwa na kijumba chake ambapo kila aliyemhitaji huenda kwa zamu kupata chakula cha usiku.
Tulizidi kushangaa ni kwanini wawili hawa waliamua kulala mbalimbali wakati ndoa yao ilikuwa ya mke mmoja. Jibu tulilopewa ni “tulikuta hali hii.”
Je, tukirejea kwenye talaka, hii inafundisha nini?
Funzo la kwanza ni kwamba watoto, mara nyingi, huathiriwa na matendo na tabia za wazazi.
Pili, tuligundua kuwa kuna mambo watoto hufuata bila kuyapinga wala kuyadurusu na kujua maana na sababu zake.
Hivyo, basi, linapokuja suala la talaka, yawezekana kabisa watoto wa wataliki wakaona ni jambo la kawaida kiasi cha kutoona madhara yake kwao.
Kama tulivyogusia hapo juu, pia wapo wanaoweza kuichukia talaka wakaitahadhari katika maisha yao ya utu uzima. Maana, hata katika kisa cha marafiki zetu hapo juu, tuliambiwa kuwa wapo Wadarfur wanaolala kitanda kimoja na wake zao hasa wawapo kwenye nchi kama Kanada zisizoruhusu mitala. Tuliwabana na kuwauliza ni kwanini hawa hawafuati mila. Majibu yalikuwa tofauti. Walisema hii ni kutokana na usomi au kuiigiza ukristo na uzungu.
Je, ukiachia mafunzo tuliyotaja hapo juu, wewe unajifunza nini? Unawahukumuje hawa wanaofuata mila bila kuhoji? Je, wewe unayo mila gani uliyorithi kwa wazazi wako ambayo yaweza kuwa hasi na bado ukaifuata au ukaikataa?
Tukiachia mbali madhara ya kimahusiano, talaka yaweza kuwa chanzo cha ukosefu wa amani na raha kwa watoto. Kwani, huishi kwenye mvutano wa nani wawe naye baina ya wazazi wawili walioachana. Tunaye rafiki yetu ambaye ni tajiri wa kupigiwa mfano. Huyu baba alitalikiwa na mkewe. Wanao watoto wanne wa kike wawili na wa kiume wawili watu wazima. Kati yao, ni mmoja tu ameolewa. Katika maongezi naye mara nyingi, huwa anasema kuwa Watoto wake watatu ambao hawajaoa wala kuolewa huwa hawapendi kujadili suala la ndoa na yeye.
Pia, Watoto wake huwa wanaepuka kutaja majina ya baba au mama yao wala mambo yao kulingana wako nan ani. Jambo hili, haliwaathiri Watoto tu bali hata baba yao. Kwani, siku zote ana wasiwasi kuwa talaka yao imewaathiri vibaya watoto wao. Hayo ni machache tunayoambiwa. Kwa mujibu wa wataalamu wa mahusiano, ndoa, na saikolojia, yapo mengi hata ya kiakili na kiafya kwa ujumla kama msongo wa mawazo, chuki zisizo na sababu, hasira, upweke, na mengine mengi.
Ni vizuri kujua. Talaka ni hatari.
Tuesday, 3 March 2026
Nitapiga marufuku kuzaa fyatuland
Siku hizi, mambo kuwa si mambo. Maisha yamekuwa magumu. Napanga kutangaza sera ya kuzuia mafyatu kufyatua watoi japo kwa muda. Naona yule anatikisa kichwa akidhani mibangi imenifyatua hadi nikafyatua kitu hiki kifyatufyatu. Hapana. Nina sababu nuzuhu za kufanya hivyo. Twende kwenye hoja. Napanga kupiga marufuku kufyatua watoi hadi mambo yatakaporekebika na kufaa. Hivyo, zifuatazo ni sababu za kufanya hivyo.
Pili, katika utafiti wangu binafsi wa kifyatu, nimegundua kuwa watoi wanazaliwa na msongo wa mawazo ambao huwazeesha hata kabla ya kuacha ziwa tokana na misongamano ya karibu kila kitu. Wanaamka usiku wa manane na kwenda skuli na kurejea home. Pia, wanabanwa kwenye ngwarangwara, madarasani, na kila mahali. Hapa, sijagusia wanavyobanwa kwenye mbavu za mbwa za kupanga. Funga kazi ni pale wengi wanapobanana hata vitandani au kwenye makochi walalamo. Kwani, hayapo?
Tatu, sitaki mafyatu wafyatue vitoi vitakavyobanwa kama wao. Zamani tukifyatuka na kupayuka tulivyotaka. Siku hizi, fanya hivyo, ufyatuliwe kama siyo na maisha, basi watoi wenyewe hasa usawa huu ambapo adabu na maadili vimetoweka kama siyo kutekwa, kupotezwa, na kufishwa.
Mbali na mibanano ya kimiwili, ipo ya kiakili. Usipojikomba, kusifu, na kuabudia, unakuwa hatarini. Dawa ni kukaa kimya. Nayo ni ugonjwa. Maana, mawazo hujaa na kuvia kichwani kiasi cha kuchizika taratibu. Maisha gani haya? Sijui kwanini hawa wanaotubana hawajui kuwa tusipoongea tunaishia kuchanganyikiwa baada ya kuchanganywa na wachanganyaji tokana na kuchanganya mambo!
Nne, kwanini kufyatua watoi watakaofyatuliwa na umaskini usababishwao na upigaji njuluku za mafyatu ambao husababisha msongo wa chuki, hasira, na kichaa hata kutaka kujinyotoa roho? Wakati tukiminywa tusiongee, wapo wanaotupigia makelele wakitutisha au kuwasifia watubanao! Siku hizi, hata mimba zinabanwa ima tokana na ukosefu wa madawa, vifaa, na rushua. Hakiji kitegemezi hadi njuluku ikutoke!
Tano, utafiti umegundua kuwa sababu na shida zote vimeungana. Baada ya hizo sababu hapo juu, kuna hili suala la msuguano wa kimawazo ambapo kutofautiana kumegeuka kosa la jinai. Huu nao huchangia sana matatizo tajwa hapo juu. Cha mno, hili husababisha matatizo mengi kiasi cha waathirika kuishi kwa kutegemea visungura kama njia ya kujiliwaza, kujipoza, na kusahau matatizo.
Sita, nimeamua kuchukua uamuzi huu ili kuwaepusha mafyatu kufyatua vitoi vilivyojaa chuki, hasira, kukata tamaa, na mengine mengi tena yasiyo na sababu za msingi zaidi ya ubinafsi, uchoyo, upofu, na uzwazwa? Nani anapenda ajenge jamii ya woga kiasi cha mafyatu kufikia hata kuogopa vivuli vyao kama kule kwa wadanganyika? Nani anapenda kuwa na jamii hata inayoogopa wasiojulikana wala visivyojulikana? Nani anapenda kujenga jamii ambayo haina utaratibu unaoeleweka hadi fyatu akiona ndata wanaopaswa kumlinda anazimia kwa mashaka na woga?
Saba, nimegundua kuwa hali tajwa hapo juu hufanya mafyatu ima wageuke au wafikiri kama wadudu. Hujasikia wanaojiita chawa, funza, kunguni, hadi luba? Kesho, sitashangaa wakijiita au kuitwa minyoo kama siyo virusi.
Nane, wale wasioweza kugeuzwa wadudu, waweza kuwa majambawazi. Tokana na kukosa matumaini, mipango bora, na ubunifu, watoi ima hujiingiza kwenye uchangu hata ushoga kama siyo jinai za kila aina. Nani anataka ajenge kaya ya jinai usawa huu ambapo mapilato nao wamesongwa kiasi cha kutoa adhabu kama hawana akili nzuri? Hapa, sijaongelea ndata ambao nao siku hizi wamegeuka miungu tokana na kuwalinda miungu wanene kwenye jinai yao.
Du! Nimesemaje! Kama ninabanwa na kusongwa na jinamizi!
Sunday, 1 March 2026
Msifanye ndoa yenu kuwa maabala
Kama ada yetu, leo, tutadurusu na kuongelea ndoa na wanandoa. Tutakita kwenye namna wanaofanya kosa kubwa na kukubali kujigeuza au kugeuzwa maabala. Kwa watu wa Pwani wanajua neno chuo au vyuo. Kuna baadhi ya makabila ambayo ndoa zao ni kama maabala. Mama au baba anaingia kwenye ndoa na kuivunja na kudandia nyingine. Hapa, ndipo dhana ya chuo inapoanzia. Utamsikia mama akiulizwa “chuo changapi hiki? bimaana ni ndoa ya ngapi.
Pamoja na kuwa mila iliyokubalika kuoa na kuolewa na kuachika, si jambo jema kwa binadamu. Lina madhara mengi kibinafsi, kijamii, kimwili, kiakili, kiuchumi hata kimaisha Je, hii husababishwa na nini? Hatuna jibu moja wala jibu rahisi. Yapo mengi yanayosababisha umaabala huu. Moja, yaweza kuwa kuingia kwenye ndoa bila kufanya utafiti na kuielewa mila na shurti zake.
Pili, ni tabia ya wahusika. Wapo wanaokwapukia na kupwakia ndoa bila kujiandaa au kuandaliwa. Zamani, kulikuwa na taasisi za Kiafrika za kuwaandaa watarajiwa kuingia kwenye ndoa. Ziliitwa jando kwa wanaume na unyago kwa wanawake. Taasisi hizi zilitofautiana baina ya makabila. Tofauti hii ilitokana na utofauti wa mazingira na mila za jamii husika. Hata hivyo, zilifanana kwa kitu kimoja kikuu. Vijana wa kike na kiume walipelekwa sehemu maalumu na kufunzwa na kufundwa na makungwi namna ya kuishi katika ndoa.
Katika jando na unyago, yapo makabila ambayo yalitahiri vijana wa kiume na mengine hata wa kike. Kutahiri wanawake, kuna madhara makubwa kimwili na kiakili. Hivyo, zama hizi, mila hii imepitwa na wakati.
Kwa ufupi, katika jando na unyago, wahusika walifunzwa na kufundwa juu ya namna ya kuwa watu wazima wake na waume. Walifundishwa miiko ya ndoa na mambo mengine muhimu ili kuwasaidia kuishi maisha ya ndoa kwa furaha na ufanisi. Hata hivyo, siku hizi vijana wanafundwa na mitandao ambapo mambo mengi ya hovyo na uongo hufundishwa na wale wanaotaka kupata wafuasi ili wapate fedha.
Hata hivyo, baada ya ujio wa dini za kigeni, taasisi hii adhimu na muhimu iliuawa na kudharaulika kiasi cha kusababisha madhara makubwa kwa taasisi ya ndoa. Ni bahati mbaya. Si wengi wanashuku wala kuhoji uvamizi huu wa kimila ambao kimsingi, si chochote bali ukoloni kama ukoloni mwingine wenye lengo la kuwabadilisha wahusika ili kuwatawala na kuwanyonya.
Tatu, ni msukumo wa jamii iliyoacha maadili yake na kupwakia maadili ya kigeni bila kuyajua vizuri na athari zake hasi kwa walengwa. Mfano, siku hizi mabinti wengi hawajifunzi kunga za nyumba kama vile heshima, mapishi, usafi, uvumilivu, usiri, na mengine mengi ambayo zamani, yalithaminiwa sana.
Nne, kukua kwa teknolojia. Tangu kuibuka kwa matumizi ya mtandao, mabinti wengi hawana nafasi ya kujifunza stadi za maisha. Mfano, wapo wasiojua kupika kabisa. Wanachofanya ni kwenda kwenye mitandao na kutafuta recipes za mapishi au mapishi, hatuna Kiswahili chake.
Kama tujuavyo, japo binadamu ana uwezo mkubwa wa kujifunza, si mara zote huelewa anachofundishwa. Huweza kuelewa anachofundishwa kupitia kurudiarudia ndiposa huelewa na kukubuhu. Mapishi yatokanayo na kujifunza pindipo mhusika atakapo kupika hayamuweki kwenye nafasi nzuri ya kuyamudu. Kuna usemi kuwa njia ya kuingia kwenye moyo wa mwanaume hupitia tumboni. Hivyo, chakula kina nafasi kubwa katika kuimarisha au kudhoofisha ndoa.
Hata hivyo, tokana na usasa, stadi za mapishi zinaonekana kama jambo la zamani. Hapa, ndipo umaabala unapoanzia na kutamalaki. Pia, tunashauri jamii ianze kurejea mila na utamaduni vya zamani vinavyofaa na kuacha visivyofaa. Hii itasaidia kuepusha ndoa na wanandoa kuishia kuwa maabala na kujenga jamii ya kimaabala ambayo haidumu.
Thursday, 26 February 2026
Nimewasamehe ‘mamluki’ waliokinukisha wote tukanuka
Juzi, Fyatu mmoja aliyefyatuka bila aibu wala woga akanifyatua na kuzusha kuwa nina uroho wa madaraka kana kwamba yeye hanao! Nani asiyependa madaraka? Kwanza, sikuamini ningehusishwa na dhambi hii ambayo chanzo chake ni shetani kutaka kumfyatua Sir God aliyemfinyanga asijue. Huwa nashangaa. Kwanini Sir God ‘mjua yote’ hakujua kuwa sheitwan angejaribu kumfyatua? Siishii hapo. Kifyatufyatu, hujiuliza. Kama kweli sheitwan ‘alipanga’ kumfyatua Sir God, ilikuwaje tukatupiwa sisi na si aliyemfyatua? Tuache ngano za imani kama zile za imani ya amani. Yawezekana sheitwan ni Gen Ziro kama siyo zero brain. Sheitwan ashindwe na kulegea au atokomezwe akatokomee mbali watoi wapone. Ashindwe sawa na wale wanaoteka, kupoteza, na kuua ili wote wenye ufyatu tupone. Ashindwe pamoja na watesi wetu wanaojifanya kuwa wapenzi wetu.
Monday, 23 February 2026
Ndoa ndoana inapomnasa aliyeitega
Kwa kutumia ujana na uzoefu wake, Aji, aliamua kumpenda mama mzee Linnie (60) (si jinale halisi) ikilinganishwa na umri wake. Fanya hesabu ujue tofauti ya kiumri. Kweli, shida haina adabu. Kwa vile Aja alidhamiria kufanikisha mpango wake wa kuendelea kuishi majuu, hakukata tamaa wala kufikiri mara mbili. Baada ya mapenzi kunoga japo kinafiki, Aja alifunga ndoa na Linnie mama tajiri mwenye nyumba na akiba si haba. Linnie aliongeza jina la Aja kwenye akaunti yake ya benki na kuifanya iwe ya pamoja.
Kama haitoshi,Aja alimuomba mkewe mama aka mshangazi amdhamini kuendelea kuishi majuu. Mke hakukataa. Wanguwangu, alianza utaratibu wa kumdhamini apate kibali cha kudumu cha kuishi majuu. Mwanzoni, mapenzi yalikuwa motomoto. Wawili walipenda. Hata hivyo, binti mtu, ndugu, na marafiki hata majirani walishuku ndoa hii ambayo kwao ilionekana ya ajabu. Wapo waliosema kuwa Aja alifuata utajiri wa Linnie. Pia, wapo waliosema wazi kuwa Linnie naye alitaka kutumia shida na uhitaji wa Aja kumnyonya kingono. Kimsingi, ndoa hii ilikuwa kama mchezo wa karata tatu. Kila mmoja, alikuwa na lake akitaka kumtumia mwenzake kiasi cha kutumiana. Na kweli, walitumiana kabla ya ukweli kufichuka na ndoa kuingia doa.
Hakupita muda, Aja alianza kuhamisha fedha Kwenda kwenye akaunti yake binafsi. Alianza kuongea kwenye simu kwa muda mrefu kwa kikwao tena akiwa nje ya chumba cha kulala. Hii ni baada ya Aja kujiridhisha kuwa mpango wa kumdhamini ulikuwa karibu kukamilika. Bila hili wala hili, hali hii ilimhuzunisha Linnie. Lakini alijipa moyo. Taratibu, ufa katika ndoa doa ulianza kupanuka. Aja alianza kukosa mawasiliano na ukaribu na Linnie. Linnie alianza kushuku kitu. Ila alijipa moyo kuwa mambo yangetengamaa asijue yasinge.
Bila simile wala woga, Aja alimkabili Linnie na kumueleza kuwa baada ya kukamilika udhamini wa kuishi majuu, angehama nyumbani kwa Linnie. Hili, kwa Linnie lilikuwa pigo lililomliza kiasi cha kusema lolote na liwe. Badala ya kumuomba asitekeleze azima yake, Linnie naye aliamua kujibu mapigo kivyake once and for all.
Bila kumstua Aja, Linnie alipanga mpango wa kumkomesha Aja. Baada ya kujiridhisha kuwa mpango wake usingefanikiwa kama alivyoupanga, Linnie aliamua kufanya vitu vyake. Wakati Linnie aliyekuwa ameishakata mawasiliano na binti yake kipenzi na wengine waliomzunguka kujua maji ndo yalikuwa yakimwagika mikononi mwake, aliamua liwalo na liwe na kweli lilikuwa. Hakumstua Aja wala kumuonyesha mabadiliko yoyote. Aliendelea kuwa mke hata kama ni wa kuigiza hasa ikizingatiwa wawili hawa hawakuwa na lolote waliofanana wala kufaana zaidi ya kutumiana.
Aja aliendelea kwenda kazini asubuhi na mapema na kurudi jioni kama kawaida. Huko nyuma, Linnie alirejesha mawasiliano na binti yake bila kumueleza sababu wala masahibu yake na kimwana wake. Alipiga konde moyo na kuamua kufanya kitu. Kwa vile mabadiliko ya Aja yalikuwa yamemletea ugonjwa wa kukosa usingizi hadi kwenda kwa daktari wake aliyemuandikia vidonge vya usingizi, aliamua kuvitumia zaidi ya alivyopaswa.
Aja aliporudi siku ya siku, alimuuliza Linnie juu ya udhamini. Linnie ambaye alishaukatiza wala hakumpasha kilichokuwa kikijiri. Kama kawaida ya watasha. Atakukumbatia kwa furaha halafu akudunge kisu mgongoni. Alimuandalia kila kitu mumewe. Kumbe kwenye chakula cha Aja Linnie ashajaza vidonge vya usingizi. Aja, bila ajizi, alikula msosi asijue ulikuwa ushadukuliwa.
Muda haukupita. Aja alijihisi usingizi. Alidhani ni uchovu wa kawaida. Taratibu alipanda kitandani mwao lau ajilaze kwa muda.
Linnie aliyekuwa akisubiri ndege anase mtegoni, alichukua mto na kumziba hewa Aja hadi akakata roho usingizini. Chapchap alimpigia simu bintiye na kumpa inshu nzima. Binti alikuja na kumsaidia mamaye kuingiza mwili kwenye gari na kwenda kuutupa kwenye sehemu ya kutupia mabaki kiwanda jirani. Hivyo, ndivyo ndoa ilivyogeuka ndoana na kumnasa aliyeitega. Yapo mengi. Nafasi haitoshi.
Saturday, 21 February 2026
Tuesday, 17 February 2026
Tufyatue Dhana ya familikrasia katika kisiasa
Utafiti huu wa kidoktari na kifyatu uligundua mambo makuu yafuatayo:
Pili, familikrasia inachukiwa kwa sababu huhalalisha ufyatuaji mkubwa wa njuluku za mafyatu kutokana na uroho uliojificha nyuma ya UKUKU.
Tatu, utafiti umegundua kuwa wengi, kama si wote, wa walaji hukosa vigezo vya kisomi isipokuwa ukaribu uwe wa kiukoo au kirafiki na mteuaji. Hivyo, wengi huwa mazwazwa na wasanii wa kawaida wasio na sifa yoyote hata ya kuongoza kundi la nyumbu.
Nne, familikrasia hujihadaa na kujenga mfumo wa utukufu uchwara ambao msingi wake mkuu ni kutumia vitisho na kuzawadiana ili kuhimili vishindo vya uchakavu, ufisadi, na ulazimishi wake. Hii inapotokea, hujengeka upofu au myopia kwa kisambaa ambao nao hujenga kujisahau na kutojiamini kiasi cha kila asiyekuwamo kuonekana adui na tishio. Hivyo, huleta ukandamizi, usanii, ubabaishi, n.k. Muhimili wa familikrasia ambao ni kichwa chake hujijengea uungufyatu kiasi cha kutengeneza viini vya kujiteketeza wenyewe.
Tano, familikrasia hulindwa kwa woga na kushuku. Hili, husababishwa na kupwaya na kutokubalika vizaavyo kutojiamini, kuaminika, na woga.
Sita, familikrasia hubebwa na ukosefu wa aibu, udhu, ufyatu, na ukatili vya kutisha. Mfumo huu, unaweza kuua yeyote anayetaka kuuzuia, kuupinga, kuukosoa, hata kuuondosha. Hivyo, kusababisha maumivu kwa mafyatu mbali na kuwanyonya.
Saba, familikrasia hutegemea sana matumizi mabaya ya njuluku na raslimali za mafyatu hongo ya, ulaji, maguvu, majungu, vishawishi, ghilba, na vitisho. Kwa mtoi wa rafiki yangu, rahis wa zamani tena jobless, kilikutwa na mimamli kibao iliyotaifishwa. Je,viko vingapi duniani hii gunia?
Nane, familikrasia hutegemea kulindana, kung'ang'ania unene ukichelea kung’olewa ambapo jinai yake hufichuka na kuishia ghaibu au lupango hata kuuawa kama ilivyotokea kwa watajwa hapo juu.
Tisa, utafiti umeonyesha kuwa UKUKU, kwa mfano, kuna uwezekano wa wahalifu wa kiunene kunyatuliwa roho na mafyatu wenye hasira wanapouchoka na kuamua kuuangamiza usiwaangamize.
Matokeo ya utafiti
Dokezo
Pamoja na kushauri utafiti zaidi, tunapendekeza waathirika si kuuchukia tu ufamilikrasia bali waukabili na kuuondolea mbali ili kupata HAKI na maendeleo kwa ujumla. Katika penye ufamilikrasia kunakuwapo na amani mawenge ambapo haki na usawa hutoweka kiasi cha kaya kuwa kama pango la majembuzi. Hivyo, dawa ya kuondokana na ufamilikrasia ni kuwapo na kutamalaki kwa haki, maadili, na mageuzi ya kweli kimfumo.
Mwisho, ufamilikrasia ni jinai inayoanza kuzoeleka na kuota mizizi katika kaya nyingi za uswekeni hasa zinazojifanya kuendelea. Ushauri ni kwamba uchukiwe na kupigwa vita kulhali na na kuogopwa kama ukoma. Hii bangi, hivi niko wapi na nafanya nini yarabi!
Sunday, 15 February 2026
Letter from Canada where internet is a human right
The heading is clear. There recently were some internet blackouts in some countries. This sacrilege can't happen in in Canada. Internet access is considered as one of the human rights everybody must enjoy. Therefore, unless otherwise stated, there’s no power whatsoever that can discretionary or out of desperation disconnect or turn internet off for whatever purposes or reasons except under certain circumstances provided for. Under Bill.C-8, the minister of Communication is strictly allowed to make an order to shutdown internet shall there be “reasonable grounds to believe that it is necessary to do so to secure the Canadian telecommunications system against any threat, including that of interference, manipulation, disruption or degradation.”
As per the Government of Canada website, “the rights and freedoms that individuals have offline must also be protected online. Canada is committed to working with international partners to protect Internet freedom, including the rights to online freedom of expression, association and peaceful assembly, as well as to protect privacy online.” Thus, Canadians enjoy the rights of access and protection of internet.
In Canada, it isn’t the choice or the discretion of the government or any institution to censure, disconnect, or discretionary provide internet. It’s like water and other essential amenities for Canadians. If anybody–––be it a person or a government––– denies Canadians such a right will not only be denying Canadians their rights but also committing an offence.
Why has internet become a human right in Canada?
The answer is simple. Internet isn’t a choice or a favour. It’s an essential part and tool of life. You can measure the health of any nation by assessing its freedom of information. People use internet to do business, communicate, study, and many more. Therefore, whoever impinges on the right to access internet adversely affects the lives and the rights of millions. So, too, internet clampdown doesn’t only show how primitive and unfeeling a society that does so is but also can lead to criminal and tort liabilities.
That said, Canadian leaders avoid such liabilities. If they don’t, they’ll foolishly lose their positions since whatever tort liabilities emanating from such a primitive act legally force the government to redress the victims. That’s because nobody is in power on her or his behalf but that of the citizens and the money paid for covering such wanton expenses comes from Canadian taxpayers. So, by committing such a crime, whoever does so, he automatically loses one of the qualities of leadership. Therefore, such a person or government can be shown the door for abuses of public funds, callousness, criminality, negligence, and others. No sane person does so or needs that. This is what is known as competent and good governance.
That said, in my country, Tanzania, internet was shut down during chimeric elections wherein the incumbent President won by 98%! If anything, currently, this save for being one of the wonders of the world, can stand as a world record of Presidential ‘victory’ if indeed it’s won fairly and squarely, which even a little bird told me that it doubts this charade. That’s because even during the one-party dictatorship, no Tanzanian President won such a hugely convoluted and tantalising ‘victory.’
That said, such a ‘win’, in bootlicking science, is known as ‘the miracle of the miracle maker.’ Again, to connect this to internet, such a win was achieved during internet blackout. Guess what. If there wasn’t internet clampdown, it’d have interfered with the win and thereby adversely affect and endanger national security, which revolves around one demigod known as President.
Howbeit, it’s key to know. Sometimes, in some primitive places, internet isn’t only a danger but also a deadly weapon for whoever controls it. For, hackers can use it to frustrate even destroy the win of the infallible mtukufu rais. You know what I mean. That’s the only person in a particular country who runs everything discretionary and effectively regardless of whatever flaws.
Ishini pamoja na siyo kwa pamoja
Kama wanandoa, huwa tunashangaa inakuwaje? Binadamu yoyote timamu kiakili na kiumri ana siri moja inayokubalika kijamii. Nayo, ni kuficha uchi wake. Ni vichaa na watoto pekee wasioweza kufichi sehemu uhci wao. Waliobaki, hakuna kitu kigumu kufanya kama kutoka nje bila kujisitiri. Tena, husema uchi wa mnyama kwa vile ni wanyama tu wanaishi bila kuhitaji kujihifadhi. Hata nao ukiwaangalia kwa makini, hawako uchi.
Katika ndoa, hakupaswi kuwapo siri baina ya wanandoa. Kama wanaweza kuvuliana nguo, inakuwaje kwanini wasivuliane mioyo? Kama uko kwenye ndoa kama hii, ujue. Mnaishi nyumba moja, kulala kitanda kimoja, kumilki mali na watoto pamoja lakini hamko pamoja. Dhana ya kuishi pamoja inahusisha kuwa pamoja katika kila jambo liwe kubwa au dogo. Huwezi kumficha mwenzio au kuwa na siri zako ambazo hutaki mwenzio azijue mkawa pamoja. Hapana. Kwenye baadhi ya dini, wakati wa kula kiapo cha ndoa, wanandoa huambiwa kuwa wanaacha kuwa miili tofauti na kuungana na kuwa mwili mmoja. Ni mwili gani ambao kiungo chake kimoja kikiumia, sehemu nyingine hazihisi au kushiriki yale maumivu?
Ndoa siyo kama mashine ambayo inaweza kuwa na sehemu nyingi tofauti ambazo hazijuani wala kuwa na athari sawa. Magari ya siku hizi yana sensor kiasi cha kuwa mwili hai. Ndoa ni sawa na mwili uwe wa mtu, mnyama hata mti. Ukichuma jani kwenye mti, mwili mzima wa mti unahisi kitendo ulichofanya. Utafiti umeonyesha kuwa miti ina hisia. Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC, 2023) ulioripotiwa na Bethany Nichols uitwao Plants Have Feelings Too miti ina hisia. Ikiguswa inajua. Utafiti huu ulionyesha kuwa miti inapata hata msongo tokana na mazingira iliyomo. Mfano, miti aina ya Arabidopsis thaliana, ikiguswa inajua. Mfano, mwaka 2014, Heidi Appel na Reginald Cocroft wa Chuo Kikuu cha Missouri walichapisha ripoti ya kushangaza. Katika utafiti wao, kwa kutumia vifaa maalumu, walichezesha sauti ya viwavi wakila majani, upepo ukivuma, wadudu chavushi wakija kuchavu na mengine. Miti ilionyesha miitikio tofauti kulingana na sauti iliyochezwa.
Sasa tujiulize. Kama miti inaweza kuhisi, inakuwaje kwenye ndoa kuwa na siri binafsi kwenye mwili mmoja na sehemu mojawapo ya mwili isihisi au kujua?
Hivyo, tunapoongelea dhana ya kuishi pamoja na kuishi kwenye nyumba au kitanda kimoja, tuzingatie kuwa kuna uwezekano watu wawili wakalala kitanda kimoja lakini wakaishi kwenye dunia tofauti. Jambo hili hi hatari sana kwa wanandoa. Lina gharama kubwa. Maana, hakuna gharama na usumbufu kama kulinda na kutunza siri. Hii inapotekea, licha ya kumomonyoa upendo na kuzalisha mafarakano, huwaumiza wahusika kisaikolojia kiasi cha kukumbwa na hatari na magonjwa vitokanavyo na msongo wa mawazo ambao kwa sasa ni tishio la afya ya akili duniani.
Sasa, nini kifanyike? Mosi, wanandoa waanze kujichunguza kama wanaishi pamoja au wanaishi kwenye nyumba pamoja. Pili, wanandoa waanze kujifunza kuishi pamoja na si kuchangia nyumba na vitanda.
Tatu, wanaweza kuanza kwa majaribio. Matokeo watakayopata, yanaweza kuwapa la kuchagua ima kuendelea kuchangia nyumba na vitanda au kuanza kuishi pamoja.
Nne, kwa wale wanaochangia nyumba na vitanda wafahamu kuwa hizo siri wanazoficha na kulinda kwa gharama yoyote zitakuja kufichuka siku moja na wagundue kuwa walikuwa wakihadaa wakiamini wanawahadaa wengine. Hakuna kitu hatarishi na kigumu kama kuwa na kutunza siri. Mshaambwa. Duniani hakuna siri. Kama ipo, ipo kwa muda tu ila si milele. Kama chaji ya simu imeisha, mwaweza kuaziman? Kama hamuwezi, mnaishi tofauti.
Hilo ndilo somo la leo. Kwa wenye maoni mnaweza kutufikia kwa barua pepe nesaa1977@yahoo au nkwazigatsha@yahoo.com.
Chanzo: Mwananchi Leo Jpili.
Saturday, 14 February 2026
Tuesday, 10 February 2026
Fyatu kwenda Romu kuuombea Popu aombee Mafyatu
Sipendi niwafanyie kitu mbaya wakose amani na kunilazimisha kukimbilia kutafuta moto kwenya maji kama suluhu kama yule sulubu. Mpango mzima ni kuikomboa Fyatuland isijiangamize kwa ufyatu. Nikifika, nitamsihi sana aombe mafyatu wawe na amani katika kila jambo. Mfano, wakifyatuliwa, wawe na amani.Wakiburuzwa, wawe na amani.
Nitamuomba na kumuombea popu aombe amani ili mafyatu, hata wakipigwa au kupigana, wafanye hivyo kwa amani, watulize boli wawe na amani. Maana, bila amani, itakuwa vigumu kuishi na kufyatuana. Amani ni uhai na uhai ni amani; haki ni vurugu iletayo machafuko itokanayo na mafyatu kutaka wapewe hata wasivyostahili kama kujua namna ninavyowafyatua.
Najua popu atanielewa na kukubali ombi langu la kumuomba, kumuombea, aombee amani kwa amani. Nitafanya hivi kwa amani ili iwepo amani baina yetu. Nitamuomba na kumuombea aombe amani ili tuishi kwa amani bila kukwaruzana na kudaiana haki tena bila amani. Haki inaweza kuua Fyatuland kwa ukosefu amani. Uwepo wa amani utawezesha hata mvua kunyesha. Kutamalaki kwa amani kutawezesha ulaji wangu uwe na amani kiasi cha kufyatua kwa amani.
Nitamsisitizia Bwana Mkubwa kuwa amani ni tunu ambayo niko tayari kuteka, kupoteza, hata kuua kwa ajili yake. Nataka niwe na amani ya kufyatua mafyatu ila wasiwe na haki ya kunihoji, kunituhumu, kunishitaki wala kunidai au kuwa na haki ya kuvuruga amani. Mafyatu wakiwa na amani, kila kitu kitakwenda vizuri. Hapatakuwapo madai ya kipuuzi kama vile kukinukisha, kuandamana, au kulalamika. Amani haitaki mambo haya. Nataka mafyatu wawe na amani kama kondoo. Kondoo ukimchinja kwa amani, anakufa kwa amani nawe unamla kwa amani.
Kwa wasiojua haki na madhara yake, wanapenda sana kuomba na kuitaka. Haki ya nini wakati kuna amani hata kama ni ya imani? Haki inaweza kuleta machafuko. Nani anataka haki wakati haki haileti amani bali shari? Ukitaka kuepuka machafuko, basi omba amani tena kwa sana huku ukiikataa haki. Kama utaomba haki, basi omba haki isiwepo bila amani. Maana, bila amani, hata iwepo haki, tutavurugana na kufyatuana. Nitamuombea na kumuomba popu aombe tuwe na amani ya kuwafyatua wanaotaka haki tena kwa amani. Pia, nitamuomba aombe watakaofyatuliwa watulie kwa amani ili wasivuruge amani. Nitamsisitizia aombee Fyatuland iwe na amani na kuchukia na kuepuka haki.
Nitamshauri asiombe haki. Kwani, haki huvuruga amani. Haki huwapa haki mafyatu kuvuruga amani kwa kisingizio cha kuomba na kutaka haki. Amani ni muhimu kuliko haki. Kukitamalaki amani, kila fyatu anafanya na kufyatua kila atakacho kwa amani.
Nitamuomba na kumuombea popu aombe amani kwa mafyatu waishi na kukubali kila jambo kwa amani. Wakifyatuana hata kuuana, wafanye hivyo kwa amani. Wakitekana au kupotezana, wafanye hivyo kwa amani. Watakaouawa au kufa, wafanye hivyo kwa amani. Wakizikana au kutopata maiti za waliofyatuliwa kwa sababu ya kiherehere cha kutafuta na kutaka haki, wafanye hivyo kwa amani.
Mbona kuku wana amani japo hawana haki? Kama haki ni mali basi amani ni pepo. Hivyo, nawasihi mafyatu watafute amani. Haki wataikuta mbinguni. Waombe amani ili kila kitu kifanyike kwa amani. Tokana na kutokea mafyatu kama wale wa TEKI tena wanaojifanya wanamfuata popu kutaka kuvuruga amani kwa kudai haki, nitamuomba popu awaombee na kuwakataza kufanya hivyo kwa amani. Nitamshauri awaamuru wote wahubiri amani wakati wakijitenga na haki.
Juzi, nilikwenda baa na kufanya vurugu kwa amani. Si waliitwa ndata wanidake kwa amani. Nawashukuru sana. Hawakunikamata kwa haki bali kwa amani. Walinipa kipigo cha amani hadi nikalalamika kwa amani. Baada ya hapo, walinifungulia kesi kwa amani. Sasa nangoja kuadhibiwa kwa amani.
Najua pilato atanipiga mvua si kidogo kwa amani. Kabla ya kufanya hivyo, nitamuomba nijitetee kwa amani ili hata nikifungwa, nifungwe kwa amani. Nitamuomba pilato atoe amri kwa majamaa wa lupango wanifunge kwa amani. Hata pale pilato atakapotamka mvua nitakazokwenda kutumika lupango, nitamuomba atoe hukumu kwa amani. Nitajitetea kuwa nilipofanya vurugu, kimsingi, nilikata kalaji kwa amani nako kakanifyatua kwa amani kiasi cha kufanya vurugu kwa amani hadi nikakamatwa, kuhukumiwa, na kufungwa kwa amani. Kuanzia leo, Fyatuland itaitwa amani na itakuwa mwiko kwa fyatu yeyote kutuletea makelele haki. Du! Majinamizi mengine, acha tu! Inaonekana mgoshi Machungi keshanipiga zongo.