The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Sunday, 19 April 2026

Letter from Canada to Besigye, Kyagulanyi, and Museveni


 Dear esteemed leaders,
May I humbly address you as real men on whom all Ugandans’ eyes are. I beseech you to face it and do the right thing for yourselves and your country. Thus, I address you as people with power though differently.
        Firstly, I fully understand that you all have followers whose ambitions, expectations, and hopes you carry and fight for. May he perish whoever ignores this fact.
        Secondly, you’re seasoned politicians/leaders who are supposed to be creative and dependable. If you lack what it takes to resolve your differences creatively and constructively, why should Ugandans keep on trusting you? May I say it point blank. Whoever is an impediment to what I’m to aver, must be viewed as a wrong person to carry even the hopes of animals let alone humans.
        Thirdly, I understand. You’re all Ugandans. That’s nothing if one lacks patriotism and trust, which are the qualities that require everybody to do justice to himself and others as the citizens of one country. 
        Fourthly, just remember. Power is always evanescent. Nobody’ll have it forever despite what. Therefore, whoever abuses or tramples on the humanity and the rights of others must not be in any public office. For, he’s unfit even to herd a herd of wildebeest aka confusion.
        Fifthly, you’re all Christians some of whom swear by lifting the Bible. If I go by and with what Christianity commands, your first commandment is love. Thus, you’re dutybound to love each other more than yourselves apart from your ‘enemies’ even in politics. Leaders are role models and teachers. What love do you teach through animosity, injustices, and tortures? I know. You’re not pretenders. 
        Thus, you must emulate the late Festo Kivengere who loved Idi Amin despite killing his people. He knew too well the dangers of hatred and how foolish and mentally unfit whoever does so for whatever reasons is. Who wants to be such a loser in the afterlife, especially for you Christians, if indeed you truly are? 
        Mature men don’t fight over what doesn’t belong to them. Refer to the famous song by the Les Wanyika Sina Makosa. Like it’s in this song, power doesn’t belong to you. It only belongs to Ugandans but not to their leaders or ruler. Fighting for what doesn’t belong to you is like fighting over or killing for somebody’s lover or wife while you truly know she doesn’t belong to any of you. Who commits such folly? If you know that, then chuki ya nini ndugu zangu while the lady isn’t yours? 
Kindly, listen to that song for a reminder.
            Sixthly, loving each other is the only means you need to see each other not only as equal but also as people. If indeed what you always say is what you mean and what you mean is what you say, you don’t have any choice but to love and show that you truly do. If indeed you’re the men who are fighting to diligently and selflessly serve the country but not to serve yourselves and your families like one of you once said, it’s only love you need. The rest will fall into place thereafter. If a few people like you can’t iron out your differences or look at each other as humans, how’ll you serve millions of Uganda? Charity always begins at home. 
        Seventhly, forgive each other so that you can be forgiven. Love each other so that you can be loved. Without loving each other and banking on hating and demolishing each other, nobody’ll succeed. No doubt. If you live by sword, you’ll die by sword. If you live by hatred, you’ll die by it. If you live by lies and manipulations, they’ll one day adversely affect you. Who sows thorns and walk barefoot? Remember that.
            Eighthly, it’s utter madness to fight over something you can’t keep or permanently own. Power belongs to the people. Whoever seeks it must understand this and faithfully do and show that. As men of probity, you still have time to take a look in the mirror and do the right thing, especially for those who self-appointed to be the judge while they’re supposed to be judged in the court of public.
            Lastly, I truly love you all. Similarly, love each other so that those you portend to seek to serve might love and trust you. That is my message from Canada.
Source: Daily Monitor Sunday today.


Waopanga au kutamani kuoa au kuolewa majuu wajue


Hivi karibuni, kumetokea visa vya kusikitisha tena vya kinyama. Jamaa waliohama Afrika wakitegemea kuukata ukaishia kuwakata. Wanaume hawa walipata mama wa kizungu toka nchini Marekani. Kwa matarajio na mapenzi makubwa, waliamua kuoa mama wa kizungu. Walihamia Marekani kwenye nchi inaayoitwa nchi yenye fursa ambako, ukiwa na dhamira na mipango madhubuti, unaukata.
Leo, tutaongelea visa vinne kama mfano ili kuonyesha changamoto wanazopata baadhi ya wale walioingia Marekani kwa kutumia njia ya ndoa. Kisa cha kwanza kinamhusisha mwanaume aitwaye Njamba (si jina lake halisi). Njamba alifanikiwa kumuoa mama mjane wa kimarekani aitwaye Mercy (si jinale halisi). Waliishi kwa furaha na amani kwa muda. Punde, mambo yakaanza kuharibika tokana na mke kutokubali kuishi maisha ya Kiafrika ambapo baba huwa na nguvu zisizopingika. Kwa Marekani, ni kinyume. Sheria za huku zinampa mama madaraka makubwa kuliko hata ya baba wa Kiafrika. Hivyo, mama anaweza kuamua kwenda likizo nchi yoyote peke yake na baba asiwe na uwezo wa kumzuia.
Piga picha. Hali inakuwaje kwa baba wa Kiafrika aliyezoea kummilki na kumpangia mkewe? Hii ndiyo hali iliyomkuta Njamba. Taratibu, alianza kujihoji kama ameoa au ameolewa. Katika kupambana na hali hii, Njamba aliamua kuonyesha uanaume wake. Alianza kutoa matishio kwanza. Baadaye, alianza kumtandika mkewe. Kwanza, mama hakuamini kama Mswahili angejiamini na kufanya haya. Wakati haya yakiendelea, wawili hawa walikuwa ndiyo wanamaliza kulipia deni la nyumba waliyoinunua kwa mkopo kama ilivyo kawaida huko Marekani.
Tokana na kuwa na deni la nyumba na kujua sheria na taratibu za Marekani vinavyompendelea mwanaume, mama alivumilia mateso kwa muda akisubiri wamalizie deni la nyumba naye afanye vitu vyake. Siku ya kwenda benki na kuagana nayo kwa kumaliza kulipia nyumba yao, mama aliruddi nyumbani na kuaza kujiamini na kujibu mapigo. Njamba hakuamini macho wala masikio yake kwa aliyoona na kusikia.
Kwa kujiamini kabisa, mama alimwambia kuwa alikuwa amechoka na mateso na hivyo, alitaka waachane. Kwanza, Njamba alidhani mkewe alikuwa akimtishia nyau asijue atafanya kweli. Mwezi ulipita halali ikiwa tete. Kumbe mama alishaenda kwa mwanasheria wake na kufungua kesi ya talaka bila hata mumewe kujua. 
        Siku ya siku, mama alirejea nyumbani na kumuamuru Njamba ahame toka nyumbani kwake. Njamba alishangaa, kuchukia, na kuhoji iweje wakati nyumba ni ya wawili? Mama alimjibu kuwa hayo hayajui wala hayamhusu. Isitoshe, alimwambia kuwa shauri la kuvunja ndoa lilikuwa tayari limeishafunguliwa mahakamani na Njamba angejulishwa wakati wowote. 
            Njamba aliapa kwa miungu yake yote kuwa asingehama kwenye nyumba yake. Naye, kadhalika alimtaka mkewe ahame kabla hajamfanyia kitu mbaya. Mama naye aliona kama alikuwa akitishia tu. Hivyo, aliinua simu na kupiga namba ambayo wengi huku wanaigopa kama ukoma yaani 911. Aliwajulisha polisi kuja haraka na kumhamisha mumewe toka nyumbani kwake kwa sababu alikuwa amemtishia angemfanyia kitu kibaya mbali na kumnyanyasa kindoa.
        Kwanza, Njamba hakuamini masikio yake. Hivyo, alimuamuru mkewe kukata simu. Mama hakukubali. Aliendelea kupiga makelele kwenye simu akiomba polisi waje haraka. Bila hili wala lile, Njamba aliingia chumba cha kulala na kuchukua bunduki na kumpiga risasi saba na kumuua hapo hapo Mercy.
        Baada ya hapo, alijigeuzia bunduki na kujimaliza. Hivyo, ndivyo ndoa ya majuu ya kuukata ilivyoishia kumkata Njamba baada ya kupitia mengi kiasi cha kukata tamaa na kuamua kuua na kujiua.
Kwa wale wanaopanga kuoa au kuolewa majuu bila kufanya utafiti na kujua tofauti za kimila na kijamii wajifunze kitu kuwa si kila king’aracho ni dhahabu.
Kuna kitu kinaitwa ndoto ya Marekani au American dream. Kitu hiki, kimewaponza wengi. Kuna njia nyingi za kufanikisha ndoto hii kubwa na ya kupigiwa mfano kwa wasiojua kilichoko nyuma ya pazia. Pamoja na kuwa sisi waandishi hatuishi Marekani, tunaishi jirani kwenye bara la Amerika. Kwa kiasi fulani, tunajua ukweli na undoto wa ndoto hii ambayo imegeuka jinamizi kwa wengi walioingia bila kufanya utafititi wa kutosha.
Chanzo: Mwananchi Jpili leo.


Thursday, 16 April 2026

Is Iran war the beginning of the end of Hegemonia Americana?

The United States has dominated the world soon after the world war after unseating the British empire. Ever since, the US has ruled the world unchallenged. It was once challenged by the then USSR, which it outfoxed, slayed, and became the sole world superpower. It created what we academically call Hegemonia Americana or American hegemony. Considering how the US is grappling with the war in the Middle East, I can comfortably say that, if things aren’t straightened up peacefully and end the war, it marks the beginning of the end of its hegemony.  That’s natural though we blame everything on the current President, Donald Tramp. Who voted him in?
        Empires rise, dominate for a certain time and fall like everything else. The US can’t escape this natural law. There were other powerful empires, which went under like the US will. Some of these empires were Qing dynasty, Inca, Aztec, Mayas, Songhai, Mongol, Greek, Roman, Ottoman, British and many more. Where are they? They died simply because everything has a certain non-negotiable lifespan.
            Like any global superpower, the US enjoyed many feats but also created many enemies within and without in its own orbit before the then USSR came in as a challenger. However, in late 90s, the US outfoxed, demised the USSR, and remained as a sole superpower. 
    Recently, the US attacked Iran, which historians know as an empire slayer. Weak as it might seem, Iran is one of continuous civilisations that slayed many of them. Using its geographic and strategic significance, Iran blocked the Strait of Hormuz, which transports close to 20% of world energy. After the US bombed and killed it leaders, Iran took out its trump card and blocked the Strait of Hormuz knowingly what the ramifications to the global economy are.
            Although the Strait of Hormuz is in Iran and Oman, it’s a lot to do with US hegemony and economic muscles. It’s a door through which oil and gas pass to go to the world. Is it true that the US doesn’t have anything to do with the US, which doesn’t depend on energy from the Middle East?
         Firstly, the gas and oil from the Middle East are priced and traded in the US dollar, hence petrodollar.       
     Secondly, the US makes billions of even trillions of dollars by selling weapons to the oil-rich gulf states.       
  Thirdly, it makes more money by protecting the monarchies in the region.
 Fourthly, the US, by uses the power of its dollar, which also draws its power from being the only currency in which oil is priced and traded. 
Fifthly, the US prints and mints dollars at will. We all know. The petrodollar agreement with Saudi Arabia, which was entered in the 1970s has expired without any renewal. This means the dominance of the dollar will soon come to an end. Shall this happen, the US dominance too will. 
Equally, the US has lost its important allies, the EU and NATO, which opposed and flatly have flatly refused to participate in this war of choice. This costs the US its economic clout as a world powerhouse, which currently spends billions of dollars on war while its people are suffering.
            Historically, when a great empire is involved in wars, it starts to crumble. This means that the US has to shoulder war expenses. Unfortunately, the US didn’t learn a lesson from Afghanistan and Iraq. When it started the war, its misguided plan was that Iranians would rise against their government. Sensing what transpired in Afghanistan, Iraq, and Libya, Iranians united and refused to do US’ dirty laundry and destroy themselves.
        In the biggening, it was like a walk to the park. After Iran became a hard nut to crack, the US asked its allies to crack it for it. The duo flatly refused to be drawn into US’s war of choice. Thereof, Trump fired back saying that the US didn’t need them since they’re a tiger paper. 
    Blockading the strait of Hormuz adversely affects global economy. Underscoring that, the US wanted the international community to address this mess pretending that the US has nothing to do with this danger to the world. Ironically, when Trump started this foolish war, he ignored those he’s now blaming and coercing to do his dirty laundry. They know who the first casualty is. Instead of facing it and abandoning the war, currently, Trump is hollering at the top of his lungs that Iran is a danger to the world. Again, who started this war of choice? Is it the victim or the perpetrator? Who truly is the very danger?
            Typically, without gas flowing through the strait of Hormuz, American dollar will lose value just overnight. The world knows how the US benefits and depends on the Middle East oil after sabotaging and abandoning the gold standard wherein nations depended on the amount of gold they’d in treasurers.
            Let the US know. Shall the war go on, the biggest victims won’t be Iran but the US. Why? That’s because the gas price will swell globally, which isn’t a problem only for the US. Again, since gas price is globally interconnected and depends on capitalistic conjectures, the US will become the first to suffer. Shall this happen, though it’s already started to happen, the Republicans will lose midterm elections, which is due soon. 
    We know Americans. They love their beloved cars, whenever gas prices upsurge, they’ll stop at nothing but to show Trump’s party the door. Neither Trump nor Republicans like this to happen. Why? First of all, Trump doesn’t want to soil his political standing. Secondly, losing election will destroy his daydream of either running for the third term or decide on who should run shall his megalomaniac dreams flop, which it surely will.
        In sum, is the war with Iran the beginning of the end of Hegemonia Americana?
Source: The Citizen Wednesday today.

Fyatu wafyatua vitegemezi vyake tegemezi japo virume

Baada ya kushuhudia kilichotokea kaya jirani kwa fyatu mwenzangu hayati Ken Aliyeunda kaya, nimestuka na kuogopa japo najiamini sana. Kwa wasionyaka inshu ni kwamba, kule Dhambia, kitegemezi cha munene wa zamani kilijikuta pakanga. Katika kufanya uchunguzi na unoko, lisrikal la kule kwa ‘roho’ mbaya yake si liliinyaka kuwa kitegemezi cha munene wa zamani aliyenyotoka roho kule kwa Fyatu Madiba kilikuwa na ukwasi wa kutisha. Kila mwanakaya alishangaa namna kitegemezi ambacho hakijawahi kupiga mzigo wowote  hata kufagia chumba chake zaidi ya kubukanya mali za mafyatu kilivyokuwa na ukwasi wa kunuka. Je, viko vingapi kama hivi kwenye bara hili lililopotea kwa uzwazwa wakati lina uchumi lakini linaukalia?
            Inshu iko hivi. Mtoi wa mdosi wa kule wa zamani alikuwa anamilki mahekalu, madude ya bei mbaya usipime ambavyo hakuna maelezo ya miujiza iliyotumika kwa fyatu kula kulala alivyoipata. Je, aliupataje huu ukwasi ambao unawahangaisha na kuwashinda Mafyatu wachakalikaji? Simpo. Dingi wake alikuwa dingi wa kaya.         Hivyo, kwa kutumia mamlaka na ubini aka surname wa dingi, jamaa alipiga njuluku ndefu pakubwa. Wakati wanakaya wakisota hadi kunyotolewa roho na ukapuku, mtoi alikuwa akijienjoi tu na kuwacheka na kuwashangaa. Je, wapo wangapi kama huyu chawa, au tuseme funza, barani kwetu? Kweli, usiposhangaa ya Abudili aka mtoi wa madili, utashangaa ya Dalie mwana wa rungu. Jamaa alikuwa na ndinga kama mia hivi na mihekalu kama hamsini. Hapa, hatujagusia njuluku alizosweka ughaibuni na zile anazotapanya akijichotea ujiko kumbe jizi tu. Anyways, hayo ndo maajabu ya bara letu linaloitwa kapuku wakati ni tajiri wa kunuka.
        Juzi, tulifanya kikao cha ghafla na Bi Mkubwa na kudurusu kadhia hii nyemelezi ya mafyatu nyemelezi watumiao unene wa madingi au ndugu zao. Tulikuja na mkakati wa kuokoa mali za Mafyatu na kulinda hesima yetu. Baada ya hapo, tuliwaita vitegemezi wetu wote na kuwapasha inshu na uamuzi wetu kuntu.
         Kwanza, hawakuamini. Walidhani tulikuwa tunawatania wakati huwa hatuna utani nao. Ilibidi waumie tu na kukubali haya mabadiliko adimu duniani japo kwa shingo upande.
        Pili, walijaribu kupinga. Niliwapa wazi kuwa unene wangu si wao. Nao, wakatafute wao kama ni rahisi kama walivyokuwa wakifyatua njuluku za mafyatu kwa kunitumia. Mie ni faya na nomi kinomi. Siyo kama akina Mobutu na M7.
        Tatu, walistuka na kuchukia. Baada ya kuwapasha inshu, tuliazimia kuwa, kuanzia sasa, maulaji yangu kama prezo wa Mafyatu utakuwa wangu na Bi Mkubwa tu. Hivyo, wajiju,
         Nne, tumepiga marufuku kutumia ubini wetu kuwapiga Mafyatu. Tumewapa wazi kuwa tunachelea mafyatu wanaweza kufyatuka wakatufyatua kwa kuwafyatua kizwazwa. Wewe uliona wapi mtoto mchanga kunyonyesha? Uliona wapi?
        Zamani, nilidhani wachunwao na vyaungudoa ni warume wakwere. Kumbe na wanene wanachunwa tena na vitegemezi vyao, jamaa, mashosti, na marafiki zao! Fyatu zima linaacha kuchapa kazi. Linanyonya na kuwafyatua mafyatu kwa vile ni rafiki, toi, au shosti la munene. Acheni uvivu. Tafuteni ngori mheshimike.
Kwa vile mie naona mbali, nimeamua rasmi kukomesha upigaji wa kutumia mamlaka yangu. Hata Bi Mkubwa tumekubaliana afute ile asasi yake ya ulaji Ulaji iitwayo  BiMkubwa Opportunity and                     Maulaji ya Unene (BOMU). Hata ile bajeti iliyokuwa ikipangiwa ofisi yake nimeipiga panga. Lazima kieleweke. Kuanzia sasa, nakinukisha kwa wale wote wapenda dezo kwa kutumia migongo ya madingi wao wanene. Nimewaamuru vitegemezi vyetu kutafuta kazi halali. Kwa vile vimeishatimiza umri wa mafyatu wazima, havitaruhusiwa hata kupewa ndinga za mafyatu. Kwani, alivichagua nani na vinamtumikia nani zaidi ya matumbo na tamaa zao? Lazima tubadilike kabla hatujabadilishwa. Isitoshe, ulaji wa dezo na unene vina mwisho.
        Katika kutenda haki, kuanzia sasa, nimetoa amri ya watoi wote wa wanene na wanene wenyewe kusoma alama za nyakati. Itawabidi wajiandae kusomea kwenye shule za Kayumba kama mafyatu wengine.  Kwa wanene, hakuna kupeleka watoi ughaibuni au kwenye intaneshno skuli wakati shule na vyuo tunavyo hapa tena vya kumwaga. Hii, itasaidia kuwazuia wanene kupiga njuluku za mafyatu. Pia, natoa amri wanene wote kwenye Fyatuland kuacha kwenda ughaibuni kujichunguza afya zao wakati hapa tunayo mahospitali lukuki.
        Kuongoza kwa mfano, nimeamuru vitegemezi vyetu viwili vilivyogoma kwenda chuo, vitafute vyuo na kuchukua nkopo  kama mafyatu wengine. Hakuna cha kutegemea jina langu tena kuishi dezo kana kwamba havina mikono na vichwa. Nimechukua hatua hizi adimu duniani kwa kuogopa kuendelea kuwafyatua mafyatu hadi wafyatuke wanifyatue. Mwenye macho asikie uzuri tu. Mwenye masikio ajionee.
        Lazima ningoze kifyatu tena kwa mfano. Kuanzia sasa, hakuna ndugu yangu awe wa kweli au wa kuokoteza atapewa upendeleo. Hata kule kijijini kwetu ambako tulikuwa tumeanza miradi ya upendeleo, nimepiga kalamu. Nimesemaje? Kwani, niko wapi?
Chanzo: Mwananchi, Aprili 9, 2026.

Ndoa ya majuu inapogeuka shubiri na maafa

Leo, tunaongelea kisa kingine cha Mswahili aliyeoa mama wa kizungu na kupata watoto na baadaye yakawakuta yaliyowakuta. Bibby (si jinale halisi) alikuwa mama aliyejaliwa urembo si haba. Wengi walikuja kumchumbia akawakataa. Alitaka aolewe na mume mwenye kujiweza na siyo wabangaizaji. Wanaume wengi kijini kwao walimuogopa kwa vile walijua alichokuwa akitafuta. Alizoea kueleza wazi wazi kuwa hawezi kutoa uzuri wake kwa mume asiye na uwezo.
Kijijini kwa Bibby kulikuwa na James mtoto wa maskini aliyebahatika kwenda majuu na kuukata.
     Akiwa amewahi kutaka kumposa Bibby akamkataa, baada ya kuukata majuu alirejea nyumbani. Aliwajengea wazazi wake bonge la jumba na kuwanunulia gari. Kila mmoja kijijini alitamani mwanae angekuwa kama James. Mmoja wa waliotamani mafanikio ya James ni Bibby. Licha ya yote aliyofanya kijijini mwake, James alikamia kuwa angemuoa Bibby aliyekuwa kamkataa miaka ya nyuma.
        Muda hakupita, Bibby alikwenda kwa wazazi wa James na kuomba namba yake ya simu. Wazazi walifurahi na kumpa namba ya simu. Bila ajizi, Bibby alimpigia simu James akiuliza ni kwanini alimsahau. Kwa vile James alikuwa amekamia kumuoa, aliona kama ndege kajiingiza mtegoni mwenyewe. Hivyo, aliomba wakutane sehemu ya faragha lau waongee mawili matatu. Bibby alifurahi na kukubali kwenda kukuta na James. Wahenga waliasa. Usitukana mkunga na uzazi ungalipo na isitoshe hakuna ajuaye ya kesho.
        Siku ya siku ilipofika, wawili walikutana kwenye hoteli moja maarufu mbali na kijijini kwao. Mambo yalikwenda haraka. Waliongea, wakala, wakanywa, wakapanga, hadi wakalala kule. Haraka haraka, Bibby alimwambia James kuwa alikuwa akimpenda na wala  hakumkataa bali kumpima uvumilivu wake ambao siku hii ulikuwa umelipa.
        Mipango ya ndoa ilipangwa na ndoa ikafanyika tayari kuanza kuishi kama mke na mume. Moyoni mwa wawili hawa, kila mmoja alijifariji kuwa alikuwa amempata mwenzie wasijue wamepatikana wote. Kiukweli, Bibby hakumpenda James bali alitaka amtumia kama pasi ya kuingia majuu na mengine angejua huko huko.
        Naye James hakumpenda Bibby bali alimtaka tokana na urembo wake. Na alijua fika kuwa Bibby alikubali amuoe kwa vile alikuwa keshaukata na anaishi majuu. Nani angekataa fursa hii tena iliyojileta yenyewe toka kwa mtu ambaye amewahi kumuudhi kwa kumkatalia ndoa?
        Wawili hawa walifunga ndoa. Muda wa James kuondoka kurudi majuu ulifika. Aliondoka na kumuacha Bibby kwa wazazi wake akimuahidi kumtumia tiketi au kumjia ili waende kuishi wote majuu. Bibby na wazazi hata marafiki walifurahi sana. Muda haukupita, James akarudi kuja kuchukua mkewe ambaye alimuacha tayari mjamzito baada ya Bibby kumtegeshea mimba ili asibadili mawazo au kushawishiwa na mabinti wengine pale kijijini waliokuwa wakimmezea James mate.
        Wawili waliondoka kwenda zao majuu. Baada ya Bibby kufika majuu mambo yalibadilika. James alianza kumnyanyasa na kumsimanga kuwa hakumpenda kwa dhati isipokuwa kwa sababu ya mafanikio yake jambo ambalo lilikuwa kweli. Naye Bibby alijibu mapigo kwa kumwambia James kuwa hakumpenda bali kumtaka kwa uzuri wake na kumkomoa kiasi cha kumsimanga kwa mambo ya zamani.
        Bibby alikuwa akiishi majuu kwa kutegemea vibali vya kuishi vya mumewe. Hivyo, asingeweza kufurukuta bali kuvumilia hadi apate vyake. Muda ulizidi kwenda na Bibby akaongeza watoto wawili huku akipanga kulipiza kisasi siku ambayo angepata vibali vyake amuache James na kuanza maisha yake akiwa mtu huru.
        Muda haukupita Bibby akapata vibali. Bila kungoja, alimwambia mumewe nia yake ya kutaka kuachana. Kabla ya kufanya hivyo, Bibby alipata ushauri kuwa kwa vile watoto wao walikuwa bado wachanga, kama wangeachana, angebaki na watoto na serikali ingemsaidia kuwatunza na pia kwa kumlazimisha James atoe pesa ya matunzo ya familia.
Kwa kuwa na haki ya kukaa na watoto, pia Bibby alipata haki ya kubaki na nyumba yao. Hili, halikuingia akilini mwa James aliyembembeleza warudi nyumbani Afrika walimalize. Bibby alikataa katakata.
        James aliamua kumuua kwa kumpiga na kitu kizito na kunyonga watoto wao na kukimbia hadi alipokamatwa na kufungwa maisha na ndoa ya majuu ikaishia kuwa maanguko ya wote.
Chanzo: Mwananchi, Aprili 12, 2026.

Msiuane kwa mali mtakamatwa au kuziacha

 Kuna visa vingi vinajulikana ambapo wanandoa hutoana roho kisa mali. Japo tutakachojadili hapa si kipya, kuna mafunzo mapya tunaweza kutoa tokana na ima uzoefu wetu au wenu. Hivi karibuni,visa vya wanadoa kutoana uhai juu ya mali vimezidi kushamiri. Si kwamba havikuwepo. Hasha. Vilikuwapo. Ila siku hizi vimezidi. Hii ni kutokana na utanda wazi na welewa wa binadamu juu ya dhana nzima ya mali au utajiri.
            Kwa wale wa kizazi chetu, yaani wa kuanzia miaka 50 kwenda juu, wimbi la mauaji baina ya wanandoa wakigombea mali ni jambo ambalo halikuzoeleka japo lilikuwapo si kwa kiwango cha sasa. Hata hivyo, kwa wengi waliokua wakati wa mfumo wa ujamaa, tulifundishwa kutopenda vitu bali utu. Hata hivyo, hii haizuii zile jamii zinazojulikana kwa uovu huu ambazo ziliendelea na tamaa, unyama na uvivu wa kutafuta vya kutaka kuvuna wasipopanda. Kwanini kuaana kwa ajili ya mali kana kwamba mtaondoka nazo mtakapokufa?
            Ni ukatili na unyama kiasi gani kuuana kwa ajili ya vitu vinavyoweza kutafutwa vikapatikana? Tokana na matukio mengi tuliyodurusu kwa muda kitambo, tuligundua kuwa hao wanaowaua wenzao ili wachukue mali peke yao, mara nyingi, hubainika na kuishia gerezani kama siyo damu za waliowaua kuwataabisha.
            Kuna kisa kimoja cha kusikitisha kilichotokea nchini Marekani mwaka jana kwenye jimbo la Texas ambako mwanamke mmoja katili alimuua mumewe kwa kumpiga risasi tatu ili achukue mali zake za mamilioni. Pamoja na kujitahidi kuficha ushahidi ukiwamo mwili wa marehemu aliyetoweka, alikamatwa. Sasa anangojea haki ichukue mkondo wake akiwa korokoroni.
            Mama huyu unayeweza kumuita shetani, aliuficha mwili wa marehemu chini ya sehemu ya kuhifadhia takataka na kudai kuwa mume wake alikuwa nchi jirani akijirusha na kimwana wakati alishamnyongelea mbali. Baada ya majirani kutomuona mume, walipiga simu polisi ambao walikuja na kumhoji akatoa taarifa za kujichanganya na kuwafanya watafute hati ya upekuzi na kugundua mwili wa marehemu ukiwa umeishaoza baada ya kufichwa kwa miezi minne.
            Katika kufuatilia visa hivi vya kikatili na kinyama, tuligundua kuwa wengi wa wanaofanya unyama huu ni wavivu wa kutafuta, wakatili, wajinga, waroho na wapenda vya dezo. Kwanini kumuua mwenzio tena kwa mali alizotafuta mwenyewe kama kweli wahusika siyo kama chawa wapendao kunyonya wenzao? Hata chawa huwa hawawaui wale wanaowanyonya.
            Pamoja na madhaifu tajwa hapo juu, kesi nyingi za aina hii zinaonyesha kuwa kuna uwezekano wa ugonjwa wa akili unaowasumbua wauaji hawa ambao hawana tofauti na wauaji wengine. Wapo wanaosema kuwa mauaji na ukatili huu ima husababishwa na chuki, hasira, visasi, woga, na mengine mengi kama hayo yatokanayo ya kuachika au kuchelea kuachika.
            Katika baadhi ya jamii, yapo makabila yenye mchezo huu yatokanayo na mashindano na tamaa ya utajiri. Watu hawa huolewa kwa makusudi wakijua wanachopanga kufanya baadaye. Mara nyingi, huwalenga wenye nazo na siyo hohehahe. Katika jamii hizi mke au mume kumuua mwenzake kwa ajili ya tamaa ya utajiri wa haraka ni jambo la kawaida.
            Kitu kingine kilichojitokeza kwenye jinai na kadhia hii ni wahusika kuishia kutofaidi hizo mali japokuwa wapo wachache wanaofanikiwa. Hata hivyo, bado wanaonusurika huishi kwa matatizo yawe ya kiafya au kiakili tokana na hisia za hatia waliyotenda.  Japo hatujafanya utafiti wa kisayansi, kuna imani kuwa yeyote amwagaye damu ya mwenzake, damu hiyo itamuandama. Kuna ukweli katika hili. Wauaji wanaweza kuficha mateso wanayopata au kupitia, ukweli ni kwamba wanatesema kwa hatia hasa nyoyoni mwao.
            Mwisho, badala ya jamii kuangalia na wengine kushabikia hata kushangilia hawa wale wenye uvivu wa kutafuta lakini wakawa na tamaa ya mali, inabidi ianze kuchukua hatua kama vile kupinga ujahili na unyama huu. Ukitaka kujua ukweli wa haya tunayoandika, kama kuna yeyote aliyewahi kufanya hivi unayemjua au kumsoma, jikumbushe mwisho wake. Wengine wanaishi kwa kutegemea madawa ya usingizi na ulevi kutokana na mateso ya dhambi na ukatili walivyowafanyia wenzao. Haiwezekani uue ambacho huwezi kukiumba uwe salama. Na kama utakuwa salama ni kwa muda.
Chanzo: Mwananchi,Jpili 5 Aprili, 2026.

Thursday, 9 April 2026

Fyatu afyatua vitegemezi vyake tegemezi na wapenda dezo mgongoni mwake

 


 Baada ya kushuhudia kilichotokea kaya jirani kwa fyatu mwenzangu hayati Ken Aliyeunda kaya, nimestuka na kuogopa japo najiamini sana. Kwa wasionyaka inshu ni kwamba, kule Dhambia, kitegemezi cha munene wa zamani kilijikuta pakanga. Katika kufanya uchunguzi na unoko, lisrikal la kule kwa ‘roho’ mbaya yake si liliinyaka kuwa kitegemezi cha munene wa zamani aliyenyotoka roho kule kwa Fyatu Madiba kilikuwa na ukwasi wa kutisha. Kila mwanakaya alishangaa namna kitegemezi ambacho hakijawahi kupiga mzigo wowote  hata kufagia chumba chake zaidi ya kubukanya mali za mafyatu kilivyokuwa na ukwasi wa kunuka. Je, viko vingapi kama hivi kwenye bara hili lililopotea kwa uzwazwa wakati lina uchumi lakini linaukalia?
            Inshu iko hivi. Mtoi wa mdosi wa kule wa zamani alikuwa anamilki mahekalu, madude ya bei mbaya usipime ambavyo hakuna maelezo ya miujiza iliyotumika kwa fyatu kula kulala alivyoipata. Je, aliupataje huu ukwasi ambao unawahangaisha na kuwashinda Mafyatu wachakalikaji? Simpo. Dingi wake alikuwa dingi wa kaya. Hivyo, kwa kutumia mamlaka na ubini aka surname wa dingi, jamaa alipiga njuluku ndefu pakubwa. Wakati wanakaya wakisota hadi kunyotolewa roho na ukapuku, mtoi alikuwa akijienjoi tu na kuwacheka na kuwashangaa. Je, wapo wangapi kama huyu chawa, au tuseme funza, barani kwetu? Kweli, usiposhangaa ya Abudili aka mtoi wa madili, utashangaa ya Dalie mwana wa rungu. Jamaa alikuwa na ndinga kama mia hivi na mihekalu kama hamsini. Hapa, hatujagusia njuluku alizosweka ughaibuni na zile anazotapanya akijichotea ujiko kumbe jizi tu. Anyways, hayo ndo maajabu ya bara letu linaloitwa kapuku wakati ni tajiri wa kunuka.
            Juzi, tulifanya kikao cha ghafla na Bi Mkubwa na kudurusu kadhia hii nyemelezi ya mafyatu nyemelezi watumiao unene wa madingi au ndugu zao. Tulikuja na mkakati wa kuokoa mali za Mafyatu na kulinda hesima yetu. Baada ya hapo, tuliwaita vitegemezi wetu wote na kuwapasha inshu na uamuzi wetu kuntu.
         Kwanza, hawakuamini. Walidhani tulikuwa tunawatania wakati huwa hatuna utani nao. Ilibidi waumie tu na kukubali haya mabadiliko adimu duniani japo kwa shingo upande.        
            Pili, walijaribu kupinga. Niliwapa wazi kuwa unene wangu si wao. Nao, wakatafute wao kama ni rahisi kama walivyokuwa wakifyatua njuluku za mafyatu kwa kunitumia. Mie ni faya na nomi kinomi. Siyo kama akina Mobutu na M7.
        Tatu, walistuka na kuchukia. Baada ya kuwapasha inshu, tuliazimia kuwa, kuanzia sasa, maulaji yangu kama prezo wa Mafyatu utakuwa wangu na Bi Mkubwa tu. Hivyo, wajiju,    
         Nne, tumepiga marufuku kutumia ubini wetu kuwapiga Mafyatu. Tumewapa wazi kuwa tunachelea mafyatu wanaweza kufyatuka wakatufyatua kwa kuwafyatua kizwazwa. Wewe uliona wapi mtoto mchanga kunyonyesha? Uliona wapi?
            Zamani, nilidhani wachunwao na vyaungudoa ni warume wakwere. Kumbe na wanene wanachunwa tena na vitegemezi vyao, jamaa, mashosti, na marafiki zao! Fyatu zima linaacha kuchapa kazi. Linanyonya na kuwafyatua mafyatu kwa vile ni rafiki, toi, au shosti la munene. Acheni uvivu. Tafuteni ngori mheshimike.
            Kwa vile mie naona mbali, nimeamua rasmi kukomesha upigaji wa kutumia mamlaka yangu. Hata Bi Mkubwa tumekubaliana afute ile asasi yake ya ulaji Ulaji iitwayo  BiMkubwa Opportunity and Maulaji ya Unene (BOMU). Hata ile bajeti iliyokuwa ikipangiwa ofisi yake nimeipiga panga. Lazima kieleweke. Kuanzia sasa, nakinukisha kwa wale wote wapenda dezo kwa kutumia migongo ya madingi wao wanene. Nimewaamuru vitegemezi vyetu kutafuta kazi halali. Kwa vile vimeishatimiza umri wa mafyatu wazima, havitaruhusiwa hata kupewa ndinga za mafyatu. Kwani, alivichagua nani na vinamtumikia nani zaidi ya matumbo na tamaa zao? Lazima tubadilike kabla hatujabadilishwa. Isitoshe, ulaji wa dezo na unene vina mwisho.
    Vitegemezi nilivyovipa uteuzi sasa naubatilisha vikahangaike nyenyewe nymbaff kabisa.
            Katika kutenda haki, kuanzia sasa, nimetoa amri ya watoi wote wa wanene na wanene wenyewe kusoma alama za nyakati. Itawabidi wajiandae kusomea kwenye shule za Kayumba kama mafyatu wengine.  Kwa wanene, hakuna kupeleka watoi ughaibuni au kwenye intaneshno skuli wakati shule na vyuo tunavyo hapa tena vya kumwaga. Hii, itasaidia kuwazuia wanene kupiga njuluku za mafyatu. Pia, natoa amri wanene wote kwenye Fyatuland kuacha kwenda ughaibuni kujichunguza afya zao wakati hapa tunayo mahospitali lukuki.
            Kuongoza kwa mfano, nimeamuru vitegemezi vyetu viwili vilivyogoma kwenda chuo, vitafute vyuo na kuchukua nkopo  kama mafyatu wengine. Hakuna cha kutegemea jina langu tena kuishi dezo kana kwamba havina mikono na vichwa. Nimechukua hatua hizi adimu duniani kwa kuogopa kuendelea kuwafyatua mafyatu hadi wafyatuke wanifyatue. Mwenye macho asikie uzuri. Mwenye masikio ajionee.
        Lazima ningoze kifyatu tena kwa mfano. Kuanzia sasa, hakuna ndugu yangu awe wa kweli au wa kuokoteza atapewa upendeleo. Hata kule kijijini kwetu ambako tulikuwa tumeanza miradi ya upendeleo, nimepiga kalamu. Nimesemaje? Kwani, niko wapi?
Chanzo: Mwananchi Jtano jana.

Sunday, 5 April 2026

Msiuane kwa mali mtakamatwa au kuziacha


Kuna visa vinavyozidi kuongezeka ambapo wanandoa hutoana roho kisa mali. Japo tutakachojadili hapa si kipya, kuna mafunzo mapya tunaweza kutoa tokana na ima uzoefu wetu au wenu. Hivi karibuni,visa vya wanadoa kutoana uhai juu ya mali vimezidi kushamiri. Si kwamba havikuwepo. Hasha. Vilikuwapo. Ila siku hizi vimezidi. Hii ni kutokana na utanda wazi na welewa wa binadamu juu ya dhana nzima ya mali au utajiri.
            Kwa wale wa kizazi chetu, yaani wa kuanzia miaka 50 kwenda juu, wimbi la mauaji baina ya wanandoa wakigombea mali ni jambo ambalo halikuzoeleka japo lilikuwapo si kwa kiwango cha sasa. Hata hivyo, kwa wengi waliokua wakati wa mfumo wa ujamaa, tulifundishwa kutopenda vitu bali utu. Hata hivyo, hii haizuii zile jamii zinazojulikana kwa uovu huu ambazo ziliendelea na tamaa, unyama na uvivu wa kutafuta vya kutaka kuvuna wasipopanda. Kwanini kuaana kwa ajili ya mali kana kwamba mtaondoka nazo mtakapokufa?
            Ni ukatili na unyama kiasi gani kuuana kwa ajili ya vitu vinavyoweza kutafutwa vikapatikana? Tokana na matukio mengi tuliyodurusu kwa muda kitambo, tuligundua kuwa hao wanaowaua wenzao ili wachukue mali peke yao, mara nyingi, hubainika na kuishia gerezani kama siyo damu za waliowaua kuwataabisha.
            Kuna kisa kimoja cha kusikitisha kilichotokea nchini Marekani mwaka jana kwenye jimbo la Texas ambako mwanamke mmoja katili alimuua mumewe kwa kumpiga risasi tatu ili achukue mali zake za mamilioni. Pamoja na kujitahidi kuficha ushahidi ukiwamo mwili wa marehemu aliyetoweka, alikamatwa. Sasa anangojea haki ichukue mkondo wake akiwa korokoroni.
            Mama huyu unayeweza kumuita shetani, aliuficha mwili wa marehemu chini ya sehemu ya kuhifadhia takataka na kudai kuwa mume wake alikuwa nchi jirani akijirusha na kimwana wakati alishamnyongelea mbali. Baada ya majirani kutomuona mume, walipiga simu polisi ambao walikuja na kumhoji akatoa taarifa za kujichanganya na kuwafanya watafute hati ya upekuzi na kugundua mwili wa marehemu ukiwa umeishaoza baada ya kufichwa kwa miezi minne.
            Katika kufuatilia visa hivi vya kikatili na kinyama, tuligundua kuwa wengi wa wanaofanya unyama huu ni wavivu wa kutafuta, wakatili, wajinga, waroho na wapenda vya dezo. Kwanini kumuua mwenzio tena kwa mali alizotafuta mwenyewe kama kweli wahusika siyo kama chawa wapendao kunyonya wenzao? Hata chawa huwa hawawaui wale wanaowanyonya.
            Pamoja na madhaifu tajwa hapo juu, kesi nyingi za aina hii zinaonyesha kuwa kuna uwezekano wa ugonjwa wa akili unaowasumbua wauaji hawa ambao hawana tofauti na wauaji wengine. Wapo wanaosema kuwa mauaji na ukatili huu ima husababishwa na chuki, hasira, visasi, woga, na mengine mengi kama hayo yatokanayo ya kuachika au kuchelea kuachika.
            Katika baadhi ya jamii, yapo makabila yenye mchezo huu yatokanayo na mashindano na tamaa ya utajiri. Watu hawa huolewa kwa makusudi wakijua wanachopanga kufanya baadaye. Mara nyingi, huwalenga wenye nazo na siyo hohehahe. Katika jamii hizi mke au mume kumuua mwenzake kwa ajili ya tamaa ya utajiri wa haraka ni jambo la kawaida.
            Kitu kingine kilichojitokeza kwenye jinai na kadhia hii ni wahusika kuishia kutofaidi hizo mali japokuwa wapo wachache wanaofanikiwa. Hata hivyo, bado wanaonusurika huishi kwa matatizo yawe ya kiafya au kiakili tokana na hisia za hatia waliyotenda.  Japo hatujafanya utafiti wa kisayansi, kuna imani kuwa yeyote amwagaye damu ya mwenzake, damu hiyo itamuandama. Kuna ukweli katika hili. Wauaji wanaweza kuficha mateso wanayopata au kupitia, ukweli ni kwamba wanatesema kwa hatia hasa nyoyoni mwao.
            Mwisho, badala ya jamii kuangalia na wengine kushabikia hata kushangilia hawa wale wenye uvivu wa kutafuta lakini wakawa na tamaa ya mali, inabidi ianze kuchukua hatua kama vile kupinga ujahili na unyama huu. Ukitaka kujua ukweli wa haya tunayoandika, kama kuna yeyote aliyewahi kufanya hivi unayemjua au kumsoma, jikumbushe mwisho wake. Wengine wanaishi kwa kutegemea madawa ya usingizi na ulevi kutokana na mateso ya dhambi na ukatili walivyowafanyia wenzao. Haiwezekani uue ambacho huwezi kukiumba uwe salama. Na kama utakuwa salama ni kwa muda.
Chanzo: Mwananchi Jpili leo.

Mila, ndoa, na sherehe vya ajabu

Leo, tutaongelea baadhi ya mila za ufungaji ndoa katika baadhi ya jamii za sasa na za zamani duniani. Huko Usikochi, marafiki huwapaka rangi nyeusi iliyochanganywa na masizi, manyoya, maziwa yaliyochacha, na unga, hasa bwana harusi na wakati mwingine bibi harusi. Hii huwaandaa kwa ugumu maishani na hii hufanyika hadharani.
        Huko Uchina, katika jamii ya Watujia, bi harusi hupaswa kulia kwa saa moja kwa mwezi mzima akiwa kwa wazazi wake. Baadae, bibi na dada zake humsaidia katika kulia kama namna ya shukrani. Nako Kongo, kwa kipindi kizima cha harusi, watarajiwa hawapaswi kucheka bali kununa! Nako nchini India, wanawake waliozaliwa kwenye hali fulani za kinyota waitwao Manglik dosha huolewa na mti, hasa mgomba, ambao baadae hukatwa ili kuondoa laana.
        Nako Korea ya Kusini, bwana harusi hufungwa kifundo cha mguu na kuchapwa na samaki makanyagioni kuthibitisha ushupavu wake kitabia. Nchini Ujerumani, kwenye mkesha wa ndoa, vifaa vyote vya udongo huvunjwa na watarajiwa husafisha kila kitu kumaanisha umoja katika kutatua matatizo. Katika tukio hili, ni mwiko kuvunja glasi kwa vile huleta mkosi.
Kwa wamasai, baba humtemea mate  bintiye mtarajiwa kwenye kichwa na kifua kama ishara ya baraka. Baada ya hapo, bi harusi huondoka bila kutazama nyuma ili asivuruge bahati yake. Nako Indonesia kwenye jimbo la Java, bi harusi huoshwa na nduguze wazee kwa maji yaliyotiwa maua kama ishara ya kutakaswa. Huko Uswidi, waalikwa hawafichi furaha yao. Bwana harusi akitoka kidogo, wageni wa kiume hupanga mstari kumbusu bi harusi sambamba na bi harusi akitoka wasichana na akina mama huenda kumbusu bwana harusi.
        Huko Romania, marafiki wa bi harusi hutekwa na marafiki zake hadi wajadiliane namna ya kumrejesha. Hii hulenga kupima utashi na utayari wa bwana harusi kumrejesha. Nako nchini Ugiriki, rafiki wa bwana harusi hunyoa ndevu siku ya harusi kuonyesha uaminifu baina ya marafiki hawa. Baadae, ndugu wa familia humlisha asali na matunda ya mti wa mlozi. Hii, huashiria ndoa itakayofana.
Turejee tena Kaskazini mwa India. Kuna kitu kiitwacho Joota Chupai, ambapo ndugu wa bi harusi huiba kiatu cha bwana harusi pindi aingiapo nyumbani kuashiria ushindani na inaweza kuisha kwa kutoa dau kubwa. 
            Kule nchini Mongolia, kabla ya ndoa, lazima achinjwe kuku mchanga na kutolewa ini ili kupata ini lenye afya. Lisipopatikana, utaratibu huu utaendelea hadi lipatikane linalofaa. 
Huko Chekoslovakia, ndugu na marafiki huweka kichanga kwenye kitanda cha watarajiwa kabla ya ndoa kuashiria ndoa itakuwa na watoto. Pia, mchele na nafaka husambazwa kitandani kuonyesha wingi wa neema. Kule Japan nako, kuna sherehe ya San-San-Kudo Sake au nilohunshu kinywaji kitokanacho na mchele uliochacha ambapo watarajiwa hawabadilishani pete. Badala yake, hunywa mara tisa, tatu tatu kila mara toka vikombe vitatu vya sake kuashiria kuwaunganisha watarajiwa na familia zao. Na hii huchukuliwa kama ishara iliyobarikiwa kuliko kula viapo.
        Huko Afrika Magharibi, baadhi ya jamii ambazo bi harusi huwekwa kwenye vibanda maalumu na kulishwa na kunenepa ili kupata unene unaoridhisha. Kuna imani kuwa bi harusi wanene wanapendeza na wana uwezo wa kuzaa watoto wenye afya! Funga kazi ni kule Spartan huko Ugiriki. Bwana harusi hupigwa kwa fimbo na mawe ili kuonyesha uvimilivu na ustahimilivu katika maisha. 
Kwenye mila za Waceltic kule Ulaya uhitaji kitanda cha maharusi kubarikiwa na makasisi wakati waliohudhuria sherehe wakiangalia. Sherehe uhusisha unyunyiziaji maji ya baraka kitandani. Unyunyiziaji maji huu ulidhaniwa kuwa ilikuwa ni alama ya ulinzi na uzazi kwa wanandoa. Warumi nao walikuwa na yao. Mabwana harusi waliwabeba bi harusi na kuwusha vizingiti maalumu kuepuka pepo wabaya kuwaingia kupitia miguuni. Warumi waliamini kuwa pepo wabaya ambao huishi ardhini na wanaweza kuingia kwa wanawake waingiapo kwenye nyumba mpya. Hivyo, kuwabeba kuliepusha wao kukutana na nguvu hiii ya ajabu.
Mwisho, wapo wayahudi. Hawa wangelinganisha watarajiwa na ndoa hufungwa kwa kutema mate ardhini kabla ya kupeana mikono. Wayahudi waliamini kwa mate yana nguvu ya kinga za kuweza kufukuza pepo wabaya.
Chanzo: Mwananchi Jpili 29 Machi, 2026.


Wednesday, 1 April 2026

Fyatu kutumia wese kufyatua mafyatu

Si kwamba najidai. Hasha. Kwa tunaomilki mikweche na mbavu za mbwa, imekula kwetu. Mwenzenu nimeweka kweche langu juu ya mawe. Naona yule anabeua midomo. Unadhani mchezo usawa huu wa kufyatuliwa na kufyatuana? Kama hujafyatuliwa, usinicheke wala kujihadaa. Utafyatuliwa tu. Tangu Tarampu na Niitenyau wakinukishe kule kulikoungua jembe ukabakia mpini, si mafyatu wachovu tutaipata. Tokana na vita hii ya kujitakia si wese limepaishwa. Leo, kila mwiz, sorry, fyatu anapanga kupandisha bei ya kila kitu. Ukiuliza kwai, waambwa vita. Unapata somo hapa? Hivi wese tutakalolanguliwa si liliingizwa miezi mingi iliyopita? Sasa itakuwaje kupandishia bei wakati wese tunalonunua ni kiporo kilicholetwa miezi mingi iliyopita?
            Juzi, niliwaita wapangaji wangu kuwaandaa kitakapoumana.Niliwaamsha usiku na kuwapa inshu! Walidhani kulikuwa na la maana la kuwapasha kumbe maumivu matupu! Si niliwafyatua kuwa kuanzia sasa kodi ya pango itapanda mara mbili! Walipouliza kwai, niliwajibu kuwa watazame runinga na siyo kushobokea shoo za kizwazwa. Niliwaliwashangaa wanaishi dunia gani wasijue wese limepanda. Si fyatu mmoja alidakia “kwani ubavu wa dogi, sorry, nyumba nayo inatumia wese kama gari?” Wee! Acha nifyatuke! Si alijifanya msomi tena wa sayansi ya wese. AlijibuNilimuuliza alichosomea na wapi kiasi cha kutojua bei ya wese ikipanda, kila kitu kinapaa.
            Nilibanja sana na kuwapa kavukavu kuwa atakayeona kupanda kwa kodi hakuwezi, atafute pa kwenda. Walipodadisi, niliwapa shule kuwa wese ndiyo roho ya biashara zote na wafanyabiashara wanaongeza cha juu watakavyo na hii ni fursa sawa kwa wote. Sijui nayo ilifia wapi? Kweli, kufa kufaana! Niliwapasha kuwa nilikuta bidhaa zote sokoni zimepaa. Hivyo, nimeamua kupaisha bei ya bidhaa yangu yaani pango. Tokana na mtanange huu, nimegundua kuwa hakuna fyatu salama vinginevyo awe sehemu ya lisirikali ambalo tukianza kupigwa na kufyatuliwa litaangalia na kutafuta namna ya kutufyatua zaidi. Usishangae hata ndata wakapandisha dau la kitu kidogo.
            Kuanzia sasa, nina mikakati ya kupambana na makali ya kufyatuliwa.
        Mosi, nitapunguza leshini home. Hakuna kula hovyo. Milo mitatu kwa siku mwisho. Huu ni uharibifu wa chakula na miili.
        Pili, ukiondoa vitegemezi vyetu vichanga, waliobaki kayani lazima waanze ‘mfungo wa wese.’
            Tatu, sitapokea wageni, vinginevyo wawe wemefunga. Sina bajeti ya wageni tena. Sifanyi hivi kwa roho mbaya, uchoyo, au ulafi. Wese limepanda jamani. Pia, wale waliozoea kuja kupiga soga wakati wa msosi, huu mwisho wao.
        Nne, nitaokoka. Sitakata kalaji kama nilivyozoea. Pia, nashauri ifuatavyo:
        a)     Wachunaji wanaotusumbua kwa fungu la kumi na sadaka wafunge hadi vita iishe.
        b)     Wanene wapunguze matumizi, safari, na vikao visivyo vya lazima. Najua watajifyatua ufahamu. Wakumbuke. Kama hawatapunguza kwa vile mali ya umma haiumi, Gen Ziro bado wapo. Watauma kama walivyofanya mwaka jana.
        c)     lisirikali lisijitoe ufahamu. Liingilie kati vinginevyo kinaweza kunuka. Si mnajua tena. Wakati tulio nacho kidogo tukilia, vipi hawa wasio na ajira wala kipato? Msitake kuongeza idadi ya majambazi na vibaka.
         Tano, kwa wenye viliba tumbo, huu ni wakati mzuri wa kupunguza uzito. Badala ya mafyatu wazima kukimbizana na barabara, punguza kubukanya na kupiga kanywaji mfurahie neema ya kupaa kwa wese.
        Sita, wauza vyakula na wenye vyombo vya usafiri, muogopeni Mungu. Siyo muanzishe vita yenu wenyewe kwa kupatupandishia bei mkisingizia wese.
        Saba, kwa vile nimeamua kuokoka na kuacha kupiga kanywaji, hata nyumba ndogo naachia. Nani atunze nyumba ndogo usawa huu wa kupaa wese? Na wale waliozoea kubomu, nao nawashauri wangoje vita iishe japo wese lishuke.
        Nane, kupunguza bili za umeme unaoliwa na miwaya, kuanzia sasa, kuangalia runinga ni saa moja tu. Baada ya hapo, wasiopenda lazima waanze kujifunza kulala mapema ili kupunguza matumizi ya umeme.
        Tisa, wale wote wanaonidai nawashauri wanifutie madeni au wangoje vita iishe pale bei na hadi pale bei ya wese itakaposhuka kama kweli itashuka. Maana, kwangu, hakuna kinachozalisha. Wajua kuwa hata bata na kuku wetu siku hizi hawatagi kutokana na kupanda kwa bei ya wese?
        Kumi, wale wa vikoba na kausha dau walie. Wasije kutusumbua na bi Mkubwa hadi vita iishe vingenevyo wanataka vita ya sisi kwa sisi.
        Kumi na moja, vitegemezi vyetu vilivyokuwa kwenye shule za upigaji na ufyatuaji za bei nawarejesha kwenye shule za Kayumba hadi wese lishuke. Kwa waliokuwa wanahudhuria tuisheni ndo mwisho hadi vita iishe. Maana, juzi kuna ticha kanipandishia bei ya tuisheni kwa sababu wese limepanda hadi kufikiri na kuandaa notice kunammalizia wese.
        Kumi na mbili, lisirikali lianze kumwaga njuluku. Yale ya maza anamwaga njuluku ambayo hajawahi kunimwagia, nayataka sasa kama ni ya kweli na si rongorongo za kisiasa za visasi. Wauza wese na lisirikali Mungu hata Sheitwani wanawaona.
Hivi leo nimekunywa chupa ngapi?
Chanzo: Mwananchi Jtano leo.

Thursday, 26 March 2026

Rest in Peace My Dear Friend Assumpta Ocam Oturu

 

Ugandan born and California based journalist Assumpta Oturu (1953 – July 2, 2025) was a great person, poet, storyteller, and a scholar. She used to host me on her program very often.  We last spoke before I left with my family for Africa. A month after, she was no more. She used to ask for my expertise when she was doing her PhD that she did not finish. RIP My dear Friend Assumpta.


Thursday, 19 March 2026

The US must urgently learn from Africa

Evidencing how the US and the world struggling under eccentric convict felon Donnie Trumpet aka Mr. Tarriffman, I feel something is amiss. Considering how Donnie’s ‘Making America and the World Great’ with his wars and tariffs, I suggest that the US must abolish term limits to enable Donnie to rule forever. When I see Donnie, I see a monarch like Kaguuuta and others. Nevertheless, Donnie must blame himself for wasting precious time accusing Africans and other ‘shitholes’ of all sorts of racist hooeys without seeking advice from constitution tampers that Africa’s in hundreds.
            Before Trump’s re-election, the Federal Bureau of Investigation (FBI), at old hours, stormed Donnie’s Mar-a-Lago beautiful mansion. I was frozen. How do you send FBI sleuths to comb, swoop, and vandalise the home of the former and future President? Yes.                     According to Donnie then, the sleuths took some boxes from his mansion. When some of Donnie’s diehards spitefully thought his successor and predecessor, Joe Biden’s behind his predicaments, guess what? The then US Attorney General Merrick Garland whom Donnie appointed got the guts and heroically came forth and said he’s the one who decided to dispatch FBI to commit that sacrilege! Can any African director of whatever security outfit replicate this and survive?
        Donnie must blame himself on not conscripting his sons in the army and for not them high ranks to see to it that they protect their family rule. Erickie and Donnie Jr would make very beautiful soldiers God’s ever created. They’d be in the class of Keineruxxba and others whose fathers drafted in their private so-called national armies to protect their family rules. If there’s anything that Donnie perfected is nothing but appoint his Daughter’s husband, Jerry Kushnei his advisor who pulls more strings than his siblings-in-law.
        To perfect their ‘sacrilegious’ complot against Donnie and his empire and illegally and needlessly shame him, the FBI went in the middle of the night and disturbed the peace of the man and the first woman, who lives her American dream! Who, in Africa, can shamelessly go to the first house to search the residence of the biggest man or woman in the land under whatever pretexts and get away with murder? No officer worth his or her salt can search even big man’s or woman’s barns. Hajitaki huyu?
        Hear what Garland said. “I personally approved the decision to seek a search warrant in this matter” (USA Today,11 August, 2022). When asked about the kind offence Donnie might had committed, Garland said that there “probable cause”, yada, yada, yada that Donnie might have committed a crime. How can a god commit a crime like possessing hush-hush materials while he or she knows everything about the country since it’s under her/his control?                 Donnie called the assault on Mar-a-Lago a pure witch hunt. Wow! How do you turn a President into a witch then hunt him  or her? In Africa, it’s unthinkable and doesn’t add up for the President to break any law while s/he’s above the law, the law, and the constitution. Americans need to go to Africa to learn jurisprudence and its interpretations. Their sanity has petered out.
        If Donnie were an African President, he’d have abolished the FBI. I’ve never understood why the US kept the President who controls the country like his private estate and can appoint his kids, wife, courtiers, and friends as he deems fit to help him milk, sorry, run his estate known as country aka banana republic to be precise. Is the US becoming a banana republic in its own light for the lack of respect to its leader let alone familicracy and nepotism?
        How on earth can a sane person or organisation suspect the President, his family, or networks of any criminality? Why do Americans disrespect their leaders by denying them the infallibility and right to be above the law like their sacrosanct African colleagues? Who bewitched Americans in the first place? 
        Garland said that’s looking for classified documents it believed Donnie took from the White Home when he lost an election that he’s never conceded up until now. As President, the country and everything belong to him or her. This is the biggest lesson Africa needs to teach the US. 
    To borrow a ‘nugget of wisdom’ from Doctor Professor Emeritus Idi Amin, Americans need to learn to love and respect their leaders but not to shame them. Poor Donnie! What’ll he do after his last term in office?
Source: The Citizen, Thursday today.

Wednesday, 18 March 2026

Fyatu anapomkumbuka Fyatu Joni Kanywaji Makufuli



Nkwingwa, ng’wadila Bhabha,
Najua unanisikia hata kama hutanijibu. Katika kumbukizi hili, mafyatu wenzako tunakukumbuka kinamna. Wapo wanaokulilia na wanaoshangilia kutegemea na hali. Leo, sitachonga sana bali kufyatuka.
            Kwanza, wasalimiwa na mafyatu wako wote na wananzengo. Tunakumiss kifyatu.
            Pili, pole kwa sababu, kama ulivyokuwa ukisema, kuna mafyatu utawashangaa. Ungerudi, ungejinyotoa roho namna mambo yalivyovurugika. Mfano, mafyatu na majipu uliyokuwa ukiyatumbua yalisharejeshwa na yanazidi kutanuka na kutanua. Juzi, wapigaji wa mwendofasta waliachiwa.
            Tatu, unaweza kufyatua vibao mafyatu, tena uliowaamini na kutengeza. Si ulisema kuwa watakaofyatua Bwagamoyo ni mataahira na mazwazwa. Kumbe uliwajua! Ungekuwepo, nadhani eheee,  kingeleweka. Hata hivyo, ujue. Simba akifariki, panya hutafuna ngozi yake. Ndviyo ilivyotokea. Yale ambayo hukuwahi kudhani yangetokea, yeshatokea zamani. Mafyatu waliogoma kufyatuka wakafyatua sasa wanafyatuliwa kama hawana akili nzuri.
            Nne, ungerejea, kabla ya kujinyotoa na kufyatua watu mbanta, ugepata kichaa. Maana, wengi uliodhania wafuasi wako sasa wanaimba ngonjera na nyimbo za kukukandia na kukukana. Juzi, nilisikia mmoja uliyemtoa mikoani na kumpa kipaza sauti akisema eti wewe hukukusanya gold! Si alirambishwa asali, wengi siyo walikusaliti tu, bali wanapmbana kulihalli usahaurike kana kwamba hukuwahi kuwapo na kutisha.
            Tano, mwaka jana kuna mafyatu waitwao ‘mamluki’ walikinukisha wote tukanuka hadi kufyatuana shaba. Wengine walifanyiwa kale ka mchezo ulikoacha. Wasiojulikana bado wapo. Waliwafyatua, kuwapoteza na wengine kuwanyotoa roho. Shaba zilitembea mitaani usipime.
Sita, walitokea mabeberu wakatuma mamluki wakatuonea wivu na kuja kuvuruga amani yetu. Walitutaimu siku ya uchaguzi wa amani na mshikamano. Walitaka kuuvuruga tukawavuruga ile mbaya tena kifyatufyatu. Siku hiyo, amani ilivugika hadi shaba zikageuka lugha pekee. Mwaka jana mwezi wa kumi tarehe 29 haitasahaulika kwa mafyatu siku walipokinukisha hawa mamluki hadi kisiwa cha amani kikageuka kisiwa cha vita na umwagaji damu ambavyo havikuwahi kutokea.
            Saba, pamoja hila na wivu wao, tunamshukuru Mungu, rahis wetu alishinda kwa asilimia 98. Mbili zilizobaki ziliibiwa na wapingaji wachoyo wa madaraka. Baada ya kukinukisha na kufyatuana, sorry, kuwafyatua mamluki, tuliunda tume ya kujichunguza lau tujue nani alizembea hadi kikanuka. Wapo mabeberu waliotucheka na kutuzodoa kuwa tunawezaje kujichunguza. Hebo! Bila kujichunguza, utawezaje kujisuta. Hawa walitaka tuite wengine watuchunguze halafu watusute wakati tunaweza kufyatua vyote viwili, yaani kujichunguza na kujisuta na kuwatuliza mafyatu waliofyatuliwa tokana na uzwazwa wao wa kukataa kufyatuka wakafyatua hadi wakafyatuliwa.
            Nane, nadhani unakumbuka wale mafyatu wa akina yero kule Ngolongolo. Walishafyatuliwa zamani gani. siku hizi wako ugosini wakijifunza kukata vikalio na kuacha na ngoma zao za kurukaruka. Ilibidi tuwafyatue ili kupisha uwekaji ili kujiongezea kipato.
            Tisa, kabla sijasahau, ule uwanja wako wa home ulishadoda. Sikujua kuwa wewe ndo ulikuwa bidhaa kuu iliiyokuwa ikiupa shavu! Baada ya kuondoka si kila kitu kiliondoka. Naomba unisamehe. Usidhani nilikufyatua ua kukusaliti. Hapana. Hata ile biashara yangu ya hoteli niliyokuwa nimefungua Chato niliishafunga baada ya kukosa wateja. Napanga kuihamishia kule Kizinkazi ambako siku hizi ndiko kunatesa. You know what I mean.
            Kumi, japo ulizuia watoi wako kushiriki siasa, siku hizi Jessie ni mheshi wa viti maalum. Tangu ulipoondoka aligeuka maalum kiasi cha kupewa kiti maalum tokana umaalum wake utokanao na wako.  
            Kumi na moja, unakumbuka ile kauli mbiu yako ya kutetea wanyonge? Tangu uondoke na unyonge ulikufuata hadi unatendewa kinyonge. Siku hizi, hakuna mnyonge hata mmoja. Ila wanyongaji bado wapo hasa wale maadui wa amani na mshimano wetu kama wale tuliowafyatua walipotaka kuvuruga uchaguzi wetu kwa vurugu badala ya kufanya hivyo kwa amani na mshikamano. Tuliwashika kwa mshikamano na kuwatia adabu kwa amani.
            Baada ya kuondoa unyonge, wapo waliopagawa hadi wakageuka machawa. Zamani chawa walikuwa wadudu. Siku hizi uchawa au kuwa chawa ni sawa na kuwa superstaa. Tuna machawa kila aina. Wako wa maza, wa faza, hata chawa wa machawa. Kuna machawa wadogo, wakubwa, wanene, walikonda na wengine kama hao. Pia, wapo wanaojipendekeza, kujikomba, kujituma, kutumwa na wa kila aina.
            Kabla sijasahau,  nadhani swahiba yako Rao aka Jaduong Maduong yule wa kaya ya jirani wakimuita baba mshaonana au hajafika. Si naye aliwageuka Gen Ziro w akule walipokinukisha akajiunga na Kasongeyeye mobali nangai. Acha afyatuliwe kuwa alijigeuza msaliti. Alisononeka hadi akaresha namba akiwa amechafuka. Kuna mafyatu wanaodai kuwa alifyatuka kwa sababu ya usaliti uliosababisha umwagaji damu.
Kabla ya kusahau, wajua? Si kwa Joji kichaka walimchagua chizi aitwaye Donnie Tarampu. We, acha ainyooshe dunia. Ninavyochonga, yupo anazipiga na waajemi kiasi cha kupandisha wese. Ila anazidi kuzidiwa pumzi hadi anaomba nimpe tafu.
            Mwisho, kuna busara ambayo sikuielewa ila leo naielewe. Kumbe asikuwepo na lake halipo! Kumbe hata kupe anaweza kuwa mkubwa na mwenye maguvu kuliko tembo aliyemnenepesha hadi akawa hivyo huku tembo akigeuzwa mdogo kuliko inzi. Du! Kumbe naota mchana!
Chanzo: Mwananchi Jtano leo.

Sunday, 15 March 2026

Yawezekana kufanikisha ndoa na mengine

Katika maisha ya binadamu, kuna mambo mengi ya kufanya na kutofanya. Kwa vile hii ni safu ya ndoa, leo, tutaangalia mafanikio na maanguko katika ndoa. Hapa, kuna swali huwa linatushughulisha sisi kama wanandoa tena wa muda si haba. Je, inakuwaje baadhi ya wanandoa huweza kufanikisha mambo yanayowashinda wengi katika ndoa wakati wengine wakishindwa kabisa japo wana mafanikio mengine nje ya ndoa?
            Inakuwaje mtu anakuwa kiongozi, msomi, au tajiri kubwa lakini anashindwa ndoa? Je, ni kupanga au majaliwa au ni kuonyesha namna ambavyo binadamu haawezi kupata vyote? Katika kudurusu hali hii, tutaanza mfano wa Malkia wa Uingereza marehemu Elizabeth (21 Aprili 1926 – 8 Septemba 2022). Huyu mama, tokana na usiri wake, hatuwezi kusema kuwa tunaijua ndoa yake vilivyo.
            Hata hivyo, kwa juu inajulikana. Pamoja na matatizo ya hapa na pale, Malkia alibainisha kuwa ndoa inaweza kuwa na mafanikio katika mambo ambayo wengi huwashinda hata kusababisha wawe na ndoa zenye changamoto na mazonge tokana na baadhi ya mafanikio yao.            
             Tunadhani Elizabth ni mmoja katika wachache waliokaa kwenye ndoa na mafanikio ya kiutawala kwa miaka mingi karibia kuliko wote. Kwani, aliishi kwenye ndoa kwa takriban miaka 74 na kwenye utawala kwa takriban miaka 64. Hii ni kutokana na baadhi ya matatizo ya wahusika kuwa kikwazo kwa ndoa zao kutokana na majukumu kiasi cha kutokuwa na muda wa kuimarisha ndoa yao.
        Je, huwaje kunakuwapo watu waliofanikiwa kitaaluma, kiuchumi, na mengine lakini wakashindwa katika ndoa? Pia, kwanini kuna watu waliofeli katika mambo mengine lakini wakafanikiwa katika ndoa?  Siri hapa ni nini? Mfano, unakuta mtu ni tajiri lakini maskini wa ndoa. Mwingine ni msomi wa kupigiwa mfano lakini asiye na ndoa au kama anayo, inayumbayumba au kukosa ladha na raha. 
               Wapo matajiri wa kuitwa utajiri lakini hawamo katika ndoa au ndoa zao zimevunjika. Jikumbushe watu waliofanikiwa kama vile Mfalme Charles wa Uingereza, Bill Gates, Donald Trump, Jeff Bizos na wengine ambao ni watu waliofanikiwa katika nyanja mbali mbali lakini ndoa ziliwashinda hadi zikavunjika au kuwa na maskandali kila uchao. Walinganishe hawa waliofanikiwa na watu wa daraja lao kama vile Tadashi Yanai tajiri mkubwa Japan, Warren Buffet, Zhong Shanshan tajiri mkubwa wa China, na wengine ambao ni matajiri wenye ndoa za kupigiwa mfano. Je, kuna siri gani katika kushinda na au kumudu taasisi tata lakini nyeti ya ndoa?
            Pia, lipo kundi la mabilionea ambao hawajawahi kuoa au kuolewa kama vile Andreas von Bechtolsheim, Diane Hendricks, Elon Musk, Oprah Winfrey, Michael Bloomberg, na wengine. Je, tatizo ni nini? Utakuta mtu maskini au asiye msomi ana ndoa imara kuliko ya tajiri ilhali wasomi na matajiri zinawashinda. Nenda mbele zaidi. Utakuta mama mrembo asiye na ndoa ilhali yule asiye mrembo anayo tena imara. Inakuwaje matajiri, wasomi, na warembo japo si wote wasiolewe lakini maskini, wasiosoma, na wasio warembo wakaolewa na kuishi kwenye ndoa imaara? Hapa kuna fumbo vile vile somo. 
        Jiulize. Ni wamama tena matajiri au wasomi aka mishangazi japo hatupendi kushabikia neno hili wangapi wanaishi bila ndoa tena wengine wakitamani au kutangaza kutaka kuolewa wasiolewe? Wakati huo huo, unaweza kumkuta muuza baa akiwa kaolewa na anafaidi ndoa!
        Je, hapa, tatizo ni wahusika au jamii? Nini suluhu ya kadhia hii? Maswali haya chokonozi na tekenyeshi kifikra yanajibiwa na the American Boys and Men (2025) ambalo linabainisha kuwa ni asilimia 50 tu ya wanawake wasomi wanaoolewa tena na wasomi wenzao. Nusu ya idadi iliyobaki, huolewa na watu wasio wasomi. Waliobaki wanabakia bila ndoa.
           Tumalizie. Ni wangapi unaowajua wanaojikuta katika hali hii tuliyodurusu? Je baadhi ya mafanikio ni chanzo cha maanguko katika ndoa na baadhi ya maanguko ni chanzo cha mafanikio katika ndoa? Ama kweli wahenga walinena kuwa Mungu hawezi kukupa au kukunyima vyote. Anakupa hiki au hivi na kukunyima vingine. Je, wewe kati ya mafanikio ya vitu na ndoa, unaridhika au kuchagua kipi? Kila la heri wanandoa na watalajiwa wote.              
Chanzo: Mwananchi Jpili leo.

Wednesday, 11 March 2026

Kwanini watoi wanaonewa bure?

Japo sijui umri wala sura zenu, kwa walengwao mjijuao, nitakuiteni waheshimiwa msiojulikana mnaofanya mambo yanayojulikana tena ya kuudhi. Nawapa shikamoo kama ishara ya heshima ila siyo kuwazeesha bali kuwasifia na kuwafurahisheni msiniteke, kunipoteza, hata kunidedisha kama wale wenzangu. Juzi, nilisikitika sana na kushangaa. Nilihuzunika na kuchukia namna wengine wanavyokasirika na kufyatuka kiasi cha kupayuka na kufyatua waliokuwa wakifyatua kwa vile walidai nanyi mliwafyatua. Cha mno, nilisikitika na kuogopa sana. Ni pale nilipoona mliowazunguka na kuwatumikia wakizuga na kuzugana badala ya kuwashauri wakaamua kujishauri.
        Wapendwa na waogopwa tena mlioko juu, kwanza, nikiri. Najua kayani tuna watoi watundu waliokosa adabu, wavuta bangi wanaodaiwa kupenda njuluku kiasi cha kuhongwa na kutaka kubomoa hata kuchoma moto kaya yetu pekee waliyotuachia baba na babu.
        Nimehuzunishwa na kushangazwa na wazushao kuwa hawa watoto watundu walihongwa tena na mbuzi dume wachome kaya moto. Wapi ushahidi? Ilinishangaza sana kuona mafyatu wazima wakifanya mambo ya kikumbaff kiaisi. Yawezekana wamefanya hivyo kutokana kuwa mafyatu wanaoweza kufyatuka na kufyatua lolote ima kugoma au kugopa kuwafyatua tukafyatuana kikaeleweka. Sijui ni kwa sababu ya uzushi au kutaka kukwepa lawama.
        Kuna niliowasikia runingani na kuwaona redioni baada ya watoi watundu kufyatuka, kufyatua na kukukera, hawataki fyatu yoyote alalamike wala kuulizia hatma yao. Wapo waliolalama na kulaani sana wapanzi walioshindwa kuwafunza watoi wao adabu hadi wakaikosa na kutishia kutuumiza wote kayani. Katu, sikubaliani na hii dhana, dhuluma, na rongorongo uchwara. 
Nadhani kama wangesoma na kucheza na watoi wa maza wa kuwazaa mwenyewe tena munene wenye tabia nzuri na mafanikio, hakika, nao wangekuwa nayo. Kama wangeshirikishwa na maza wa kambo kwenye kamati ya uendeshaji wa kaya yao kama wake hadi hata warume wao, yote yasingetokea. Hayo leo tuyaache.
        Kingine nijuacho, hawa watoi watundu wengi wanatoka shule za Kayumba. Kama wangesoma intaneshno na Kimombo media, wasingekuwa watundu hivi bali kama kuku wa kitasha. Wangekuwa wamezaliwa kwenye hos za bei mbaya, wasingekuwa na utundu wala utukutu bali utanuaji tena wa dezo. Hivyo, nadhani sababu ya watoi kuwa watundu hadi wakataka kuchoma kaya ni ukapuku wa madingi zao. Mtoi anayelala kwenye ngwarangwara akielekea shulee hawezi kuwa na adabu wala tabia. Hawezi kuwa sawa na wale wanaoendeshwa kwenye midude ya bei mbaya ambayo ni full viyoyozi kama wa wanene. Hawezi huyu maskini. Ni kama tunawaonea au hatuwaelewi. Kama tunawaelewa, basi hatuelewi, hawatuelewi na hatuelewani.
Wapendwa, nilishangaa kusikia eti watoi watundu walitaka kuharibu kaya yetu ilhali ilishaharibiwa baada ya kupigwa mnada na ndugu zetu wenye uchu wa njuluku tena wahongwao peremende, udohoudoho, na upuuzi mwingine. Nani zwazwa awahonge njuluku watoi wachome kaya ambayo si yao tena? Au ni wale wenye tabia za mbuzi dume? Nadhani hata mbuzi wanajua kuwa kaya yetu ya urithi ilishapigwa mnada. Hata hivyo, tukiwa wakweli, nani ahongwi nyumbani kwetu? Muonyesheni ili watoi waende kwake wajifunze. Mnakumbuka yule baba aliyetuacha alivyowahi kusema. Kuna kuwa lile shamba la Bwagamoyo lisiuzwe vinginevyo watakavyofanya hivyo wawe machizi na mataahira wasiojua ukubwa na manufaa yake. Je, halikuuzwa?
Yule baba japo alikuwa na yake kama ukali kupita kiasi hata ukatili kiasi cha kuwachapa wenzetu hadi wakatekwa, wakapotea, na kufa, pia, alikuwa na uzuri wake. Nakumbuka. Hakuwahi kupendelea watoi wake na kuwaumiza watoi wa kufikia kama ilivyo. Sikumbuki kuona mtoi wake hata mkwewe au mkamwana kwenye kamati yake ya kuongoza kaya. Kwa hili, sitaacha kumkumbuka mbali na kupambana na wale vidokozi waliokuwa wakiiba na kuramba sukari na kufanya wengine tunywe uji wenye chumvi.
Juzi, kuna watoi wakorofi walivunja vikombe na kupiga mateke sufuria na mambo mengine. Bahati mbaya, wale walinzi wetu si waliwaunguza mikono eti wakiwaadhibu! 
Mpaka nifyatukapo, wapo waliokimbia kiasi cha kutojulikana walipo. Wapo wanaodai kuwa waliuawa na miili yao kutupwa mbali pasipojulikana kama wale wasiojulikana japo wanatenda jinai na ukatili vinavyojulikana. Wazushi walizua na kuzusha kuwa wale walinzi waliwaua na kuwatupa baharini ilhali maza yao akiangalia na kuwalaumu.
        Juzi, nilipita kijiweni. Niliyosikia yanatisha. Kumbe watoi watundu wenzao wanasema lazima walinzi washikwe na kushikishwa adabu hadi wawaonyeshe wenzao au miili yao badala ya kujitoa ufahamu na kukaa kimya kana kwamba waliopotea ni wadudu. Wanataka kujua nani alimuamuru kuua watoi wachanga tena kwa kuonyesha utoto wao. Mashambenga na wabaya wanazoza wazi kuwa kuwa kuna ubaguzi hasa kuwaacha walinzi wawaue kwa vile ni wana wa kufikia.
        Nani kawalipa nani na wangapi, nini, kiasi, na lini ili apate nini na kwanini? Je, ‘vyombo’ vilikuwa wapi? Tumuamini na kutomwamini nani?
Chanzo: Mwananchi Jtano leo.