The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Wednesday, 11 March 2026

Kwanini watoi wanaonewa bure?

Japo sijui umri wala sura zenu, kwa walengwao mjijuao, nitakuiteni waheshimiwa msiojulikana mnaofanya mambo yanayojulikana tena ya kuudhi. Nawapa shikamoo kama ishara ya heshima ila siyo kuwazeesha bali kuwasifia na kuwafurahisheni msiniteke, kunipoteza, hata kunidedisha kama wale wenzangu. Juzi, nilisikitika sana na kushangaa. Nilihuzunika na kuchukia namna wengine wanavyokasirika na kufyatuka kiasi cha kupayuka na kufyatua waliokuwa wakifyatua kwa vile walidai nanyi mliwafyatua. Cha mno, nilisikitika na kuogopa sana. Ni pale nilipoona mliowazunguka na kuwatumikia wakizuga na kuzugana badala ya kuwashauri wakaamua kujishauri.
        Wapendwa na waogopwa tena mlioko juu, kwanza, nikiri. Najua kayani tuna watoi watundu waliokosa adabu, wavuta bangi wanaodaiwa kupenda njuluku kiasi cha kuhongwa na kutaka kubomoa hata kuchoma moto kaya yetu pekee waliyotuachia baba na babu.
        Nimehuzunishwa na kushangazwa na wazushao kuwa hawa watoto watundu walihongwa tena na mbuzi dume wachome kaya moto. Wapi ushahidi? Ilinishangaza sana kuona mafyatu wazima wakifanya mambo ya kikumbaff kiaisi. Yawezekana wamefanya hivyo kutokana kuwa mafyatu wanaoweza kufyatuka na kufyatua lolote ima kugoma au kugopa kuwafyatua tukafyatuana kikaeleweka. Sijui ni kwa sababu ya uzushi au kutaka kukwepa lawama.
        Kuna niliowasikia runingani na kuwaona redioni baada ya watoi watundu kufyatuka, kufyatua na kukukera, hawataki fyatu yoyote alalamike wala kuulizia hatma yao. Wapo waliolalama na kulaani sana wapanzi walioshindwa kuwafunza watoi wao adabu hadi wakaikosa na kutishia kutuumiza wote kayani. Katu, sikubaliani na hii dhana, dhuluma, na rongorongo uchwara. 
Nadhani kama wangesoma na kucheza na watoi wa maza wa kuwazaa mwenyewe tena munene wenye tabia nzuri na mafanikio, hakika, nao wangekuwa nayo. Kama wangeshirikishwa na maza wa kambo kwenye kamati ya uendeshaji wa kaya yao kama wake hadi hata warume wao, yote yasingetokea. Hayo leo tuyaache.
        Kingine nijuacho, hawa watoi watundu wengi wanatoka shule za Kayumba. Kama wangesoma intaneshno na Kimombo media, wasingekuwa watundu hivi bali kama kuku wa kitasha. Wangekuwa wamezaliwa kwenye hos za bei mbaya, wasingekuwa na utundu wala utukutu bali utanuaji tena wa dezo. Hivyo, nadhani sababu ya watoi kuwa watundu hadi wakataka kuchoma kaya ni ukapuku wa madingi zao. Mtoi anayelala kwenye ngwarangwara akielekea shulee hawezi kuwa na adabu wala tabia. Hawezi kuwa sawa na wale wanaoendeshwa kwenye midude ya bei mbaya ambayo ni full viyoyozi kama wa wanene. Hawezi huyu maskini. Ni kama tunawaonea au hatuwaelewi. Kama tunawaelewa, basi hatuelewi, hawatuelewi na hatuelewani.
Wapendwa, nilishangaa kusikia eti watoi watundu walitaka kuharibu kaya yetu ilhali ilishaharibiwa baada ya kupigwa mnada na ndugu zetu wenye uchu wa njuluku tena wahongwao peremende, udohoudoho, na upuuzi mwingine. Nani zwazwa awahonge njuluku watoi wachome kaya ambayo si yao tena? Au ni wale wenye tabia za mbuzi dume? Nadhani hata mbuzi wanajua kuwa kaya yetu ya urithi ilishapigwa mnada. Hata hivyo, tukiwa wakweli, nani ahongwi nyumbani kwetu? Muonyesheni ili watoi waende kwake wajifunze. Mnakumbuka yule baba aliyetuacha alivyowahi kusema. Kuna kuwa lile shamba la Bwagamoyo lisiuzwe vinginevyo watakavyofanya hivyo wawe machizi na mataahira wasiojua ukubwa na manufaa yake. Je, halikuuzwa?
Yule baba japo alikuwa na yake kama ukali kupita kiasi hata ukatili kiasi cha kuwachapa wenzetu hadi wakatekwa, wakapotea, na kufa, pia, alikuwa na uzuri wake. Nakumbuka. Hakuwahi kupendelea watoi wake na kuwaumiza watoi wa kufikia kama ilivyo. Sikumbuki kuona mtoi wake hata mkwewe au mkamwana kwenye kamati yake ya kuongoza kaya. Kwa hili, sitaacha kumkumbuka mbali na kupambana na wale vidokozi waliokuwa wakiiba na kuramba sukari na kufanya wengine tunywe uji wenye chumvi.
Juzi, kuna watoi wakorofi walivunja vikombe na kupiga mateke sufuria na mambo mengine. Bahati mbaya, wale walinzi wetu si waliwaunguza mikono eti wakiwaadhibu! 
Mpaka nifyatukapo, wapo waliokimbia kiasi cha kutojulikana walipo. Wapo wanaodai kuwa waliuawa na miili yao kutupwa mbali pasipojulikana kama wale wasiojulikana japo wanatenda jinai na ukatili vinavyojulikana. Wazushi walizua na kuzusha kuwa wale walinzi waliwaua na kuwatupa baharini ilhali maza yao akiangalia na kuwalaumu.
        Juzi, nilipita kijiweni. Niliyosikia yanatisha. Kumbe watoi watundu wenzao wanasema lazima walinzi washikwe na kushikishwa adabu hadi wawaonyeshe wenzao au miili yao badala ya kujitoa ufahamu na kukaa kimya kana kwamba waliopotea ni wadudu. Wanataka kujua nani alimuamuru kuua watoi wachanga tena kwa kuonyesha utoto wao. Mashambenga na wabaya wanazoza wazi kuwa kuwa kuna ubaguzi hasa kuwaacha walinzi wawaue kwa vile ni wana wa kufikia.
        Nani kawalipa nani na wangapi, nini, kiasi, na lini ili apate nini na kwanini? Je, ‘vyombo’ vilikuwa wapi? Tumuamini na kutomwamini nani?
Chanzo: Mwananchi Jtano leo.

Sunday, 8 March 2026

talaka yenu inawafundisha nini watoto wenu?


Si mara ya kwanza wala ya mwisho kujadili talaka. Leo, tutadurusu talaka na madhara kwa watoto wa watalaka. Japo talaka ni jambo la kuhuzunisha, kwa watoto wa watalaka wenye busara na wanaojua na kuchukia madhara ya talaka, linaweza kuwa funzo kubwa katika maisha yao. Hata hivyo, inategemea na wahusika. Wapo wanaoweza kuchukia talaka na kuhakikisha watakapokuwa na kufunga ndoa, hawatapenda kupitia waliyopitia. Pia, wapo, hatujui tuwaiteje wanaoweza kuona talaka kama jambo la kawaida.
Tutatoa mfano wa rafiki yetu toka Jimboni Darfur, Sudan. Huyu bwana ana mke mmoja. Kanada, ndoa za mitala  haziruhusiwi. Ajabu, huwa halali kitanda chumba wala kitanda kimoja na mkewe. Siku moja walitutembelea kama familia ya kulala kwetu. Ilipofika wakati wa kulala, tuliwaandalia chumba mke na mume Pia, kuwaandalia watoto wao vyumba viwili tofauti. Bila hili wala lile, wanandoa walituita kona. Walisema vyumba vitatu tulivyowatengea vilikua vingi. Walihitaji viwili tu. Tulishangaa. 
Tuliuliza kwanini wakati walikuwa wana watoto jinsia tofauti ambao tusingewalaza chumba kimoja. Walijibu kuwa watoto wa kike wangelala na mama yao, na wa kiume wangelala chumba kimoja na baba yao. Hatukuwapinga. Ila tuliwashangaa.
Zamu yetu ilipofika kuwatembelea, walitupangia vyumba viwili badala ya vitatu. Walitushangaa tulipouliza ni kwanini? Marafiki hawa walisema kuwa, kawaida, hawalali mke na mume pamoja. Tulishangaa hakuna mfano.
Hata hivyo, katika kuwadurusu kujua ni kwanini hawalali chumba wala kitanda kimoja, mume alijibu kuwa walikuta wazazi wao wakiwa na utaratibu huo. Katika kuzidi kuwadurusu, tulishangaa kugundua kuwa wazazi tajwa walikuwa na wake wengi. Hivyo, kwa kuzingatia kuwa waliishi kwenye vijumba vidogo vilivyojengwa sehemu moja ndani ya boma moja. Baba alikuwa na kijumba chake ambapo kila aliyemhitaji huenda kwa zamu kupata chakula cha usiku.
Tulizidi kushangaa ni kwanini wawili hawa waliamua kulala mbalimbali wakati ndoa yao ilikuwa ya mke mmoja. Jibu tulilopewa ni “tulikuta hali hii.”
Je, tukirejea kwenye talaka, hii inafundisha nini? 
Funzo la kwanza ni kwamba watoto, mara nyingi, huathiriwa na matendo na tabia za wazazi.
Pili, tuligundua kuwa kuna mambo watoto hufuata bila kuyapinga wala kuyadurusu na kujua maana na sababu zake.
Hivyo, basi, linapokuja suala la talaka, yawezekana kabisa watoto wa wataliki wakaona ni jambo la kawaida kiasi cha kutoona madhara yake kwao.
Kama tulivyogusia hapo juu, pia wapo wanaoweza kuichukia talaka wakaitahadhari katika maisha yao ya utu uzima. Maana, hata katika kisa cha marafiki zetu hapo juu, tuliambiwa kuwa wapo Wadarfur wanaolala kitanda kimoja na wake zao hasa wawapo kwenye nchi kama Kanada zisizoruhusu mitala. Tuliwabana na kuwauliza ni kwanini hawa hawafuati mila. Majibu yalikuwa tofauti. Walisema hii ni kutokana na usomi au kuiigiza ukristo na uzungu.
Je, ukiachia mafunzo tuliyotaja hapo juu, wewe unajifunza nini? Unawahukumuje hawa wanaofuata mila bila kuhoji? Je, wewe unayo mila gani uliyorithi kwa wazazi wako ambayo yaweza kuwa hasi na bado ukaifuata au ukaikataa?
Tukiachia mbali madhara ya kimahusiano, talaka yaweza kuwa chanzo cha ukosefu wa amani na raha kwa watoto. Kwani, huishi kwenye mvutano wa nani wawe naye baina ya wazazi wawili walioachana. Tunaye rafiki yetu ambaye ni tajiri wa kupigiwa mfano. Huyu baba alitalikiwa na mkewe. Wanao watoto wanne wa kike wawili na wa kiume wawili watu wazima. Kati yao, ni mmoja tu ameolewa. Katika maongezi naye mara nyingi, huwa anasema kuwa Watoto wake watatu ambao hawajaoa wala kuolewa huwa hawapendi kujadili suala la ndoa na yeye.
Pia, Watoto wake huwa wanaepuka kutaja majina ya baba au mama yao wala mambo yao kulingana wako nan ani. Jambo hili, haliwaathiri Watoto tu bali hata baba yao. Kwani, siku zote ana wasiwasi kuwa talaka yao imewaathiri vibaya watoto wao. Hayo ni machache tunayoambiwa. Kwa mujibu wa wataalamu wa mahusiano, ndoa, na saikolojia, yapo mengi hata ya kiakili na kiafya kwa ujumla kama msongo wa mawazo, chuki zisizo na sababu, hasira, upweke, na mengine mengi.
Ni vizuri kujua. Talaka ni hatari.
Chanzo: Mwananchi Jpilil leo.

Tuesday, 3 March 2026

Nitapiga marufuku kuzaa fyatuland


 Siku hizi, mambo kuwa si mambo. Maisha yamekuwa magumu. Napanga kutangaza sera ya kuzuia mafyatu kufyatua watoi japo kwa muda. Naona yule anatikisa kichwa akidhani mibangi imenifyatua hadi nikafyatua kitu hiki kifyatufyatu. Hapana. Nina sababu nuzuhu za kufanya hivyo. Twende kwenye hoja. Napanga kupiga marufuku kufyatua watoi hadi mambo yatakaporekebika na kufaa. Hivyo, zifuatazo ni sababu za kufanya hivyo.

Mosi, hakuna uhuru wa kufikiri kwa sasa. Hivyo, sitaki mafyatu wafyatue watoi mazezeta au wakaokataa uzezeta na kuishia kupatilizwa kama siyo kutekwa, kupotezwa, na kunyotolewa roho. Nani anataka mtoi wake atekwe au kupotezwa kwa kujiingiza kwenye dhambi ya kufikiri hadi anaishia kupinga?
        Pili, katika utafiti wangu binafsi wa kifyatu, nimegundua kuwa watoi wanazaliwa na msongo wa mawazo ambao huwazeesha hata kabla ya kuacha ziwa tokana na misongamano ya karibu kila kitu. Wanaamka usiku wa manane na kwenda skuli na kurejea home. Pia, wanabanwa kwenye ngwarangwara, madarasani, na kila mahali. Hapa, sijagusia wanavyobanwa kwenye mbavu za mbwa za kupanga. Funga kazi ni pale wengi wanapobanana hata vitandani au kwenye makochi walalamo. Kwani, hayapo? 
Hii huwasababishia woga wanapoona ngwarangwara na tukutuku vikivunja sheria mchana kweupe. Wanapata msongo wa mawazo zaidi wanapovuka barabara kwa kuogopa kugongwa na hawa wavunja sheria wasioshikishwa adabu. Hii inawaathiri kiakili na kimwili. Hivyo, kuendelea kuwafyatua ni kufyatua kaya yenye changamoto kubwa kiakili na kimwili. Nani analitaka hili? 
    Mfano, katika pitapita yangu kwenye miji mingi ya Fyatuland, niligundua kuwa kuna makelele ya kuua fyatu. Bahati mbaya yameruhusiwa chini ya visingizio kama vile biashara, kuburudisha, kuhubiri, kupayuka tu, ving’ora, na uhuru wa kila fyatu kuwa navyo.
        Tatu, sitaki mafyatu wafyatue vitoi vitakavyobanwa kama wao. Zamani tukifyatuka na kupayuka tulivyotaka. Siku hizi, fanya hivyo, ufyatuliwe kama siyo na maisha, basi watoi wenyewe hasa usawa huu ambapo adabu na maadili vimetoweka kama siyo kutekwa, kupotezwa, na kufishwa.
        Mbali na mibanano ya kimiwili, ipo ya kiakili. Usipojikomba, kusifu, na kuabudia, unakuwa hatarini. Dawa ni kukaa kimya. Nayo ni ugonjwa. Maana, mawazo hujaa na kuvia kichwani kiasi cha kuchizika taratibu. Maisha gani haya? Sijui kwanini hawa wanaotubana hawajui kuwa tusipoongea tunaishia kuchanganyikiwa baada ya kuchanganywa na wachanganyaji tokana na kuchanganya mambo!
        Nne, kwanini kufyatua watoi watakaofyatuliwa na umaskini usababishwao na upigaji njuluku za mafyatu ambao husababisha msongo wa chuki, hasira, na kichaa hata kutaka kujinyotoa roho? Wakati tukiminywa tusiongee, wapo wanaotupigia makelele wakitutisha au kuwasifia watubanao! Siku hizi, hata mimba zinabanwa ima tokana na ukosefu wa madawa, vifaa, na rushua. Hakiji kitegemezi hadi njuluku ikutoke!
        Tano, utafiti umegundua kuwa sababu na shida zote vimeungana. Baada ya hizo sababu hapo juu, kuna hili suala la msuguano wa kimawazo ambapo kutofautiana kumegeuka kosa la jinai. Huu nao huchangia sana matatizo tajwa hapo juu. Cha mno, hili husababisha matatizo mengi kiasi cha waathirika kuishi kwa kutegemea visungura kama njia ya kujiliwaza, kujipoza, na kusahau matatizo. 
Hili nalo limeongeza matatizo mengine kama utegemezi wa urahibu, udokozi, wizi, jinai, ukosefu wa maadili, adabu, aibu na mengine kama hayo. Hii imefanya nifyatuke ahead of time. Katika kufanya hivyo, nimegundua kuwa baada ya hayo matatizo na mazabe hapo juu, waathirika wataanza kutegemea vipanya hadi paka wawachukie kwa kusababisha ushindani pale bei ya visungura itakapopaa. 
Hii pia ina madhara yake. Watoi na waathirika wengine wataanza kubet ili watengeneze njuluku wasijue wajinga ndiyo waliwao! Nani aliwahi kuukwaa kwa kubet kama siyo kuishiwa akili na ubunifu? Baya zaidi, jinai hii imehalalishwa na kuonekana kama uwekaji wakati ni uchukuaji utokanao na uoza na uzwazwa wa kimfumo?
        Sita, nimeamua kuchukua uamuzi huu ili kuwaepusha mafyatu kufyatua vitoi vilivyojaa chuki, hasira, kukata tamaa, na mengine mengi tena yasiyo na sababu za msingi zaidi ya ubinafsi, uchoyo, upofu, na uzwazwa? Nani anapenda ajenge jamii ya woga kiasi cha mafyatu kufikia hata kuogopa vivuli vyao kama kule kwa wadanganyika? Nani anapenda kuwa na jamii hata inayoogopa wasiojulikana wala visivyojulikana? Nani anapenda kujenga jamii ambayo haina utaratibu unaoeleweka hadi fyatu akiona ndata wanaopaswa kumlinda anazimia kwa mashaka na woga?
        Saba, nimegundua kuwa hali tajwa hapo juu hufanya mafyatu ima wageuke au wafikiri kama wadudu. Hujasikia wanaojiita chawa, funza, kunguni, hadi luba? Kesho, sitashangaa wakijiita au kuitwa minyoo kama siyo virusi.
        Nane, wale wasioweza kugeuzwa wadudu, waweza kuwa majambawazi. Tokana na kukosa matumaini, mipango bora, na ubunifu, watoi ima hujiingiza kwenye uchangu hata ushoga kama siyo jinai za kila aina. Nani anataka ajenge kaya ya jinai usawa huu ambapo mapilato nao wamesongwa kiasi cha kutoa adhabu kama hawana akili nzuri? Hapa, sijaongelea ndata ambao nao siku hizi wamegeuka miungu tokana na kuwalinda miungu wanene kwenye jinai yao.
        Du! Nimesemaje! Kama ninabanwa na kusongwa na jinamizi!
Chanzo: Mwananchi Jtano leo.

Sunday, 1 March 2026

Msifanye ndoa yenu kuwa maabala

Tunaamini wengi wa wasomaji wetu wanaijua maabala. Maabala ni mahali ambapo hufanyika majaribio ili kupata nyenzo na ujuzi wa kufaa katika maisha. Japo si maabala zote, mara nyingi, maabala zimalizapo kazi zake au hata kutoleta matunda au kufikia malengo yaliyotarajiwa hufungwa. Ni maabala za taasisi za kielimu za kisayansi ambazo daima huendelea kuwepo.
Kama ada yetu, leo, tutadurusu na kuongelea ndoa na wanandoa. Tutakita kwenye namna wanaofanya kosa kubwa na kukubali kujigeuza au kugeuzwa maabala. Kwa watu wa Pwani wanajua neno chuo au vyuo. Kuna baadhi ya makabila ambayo ndoa zao ni kama maabala. Mama au baba anaingia kwenye ndoa na kuivunja na kudandia nyingine. Hapa, ndipo dhana ya chuo inapoanzia. Utamsikia mama akiulizwa “chuo changapi hiki? bimaana ni ndoa ya ngapi.
Pamoja na kuwa mila iliyokubalika kuoa na kuolewa na kuachika, si jambo jema kwa binadamu. Lina madhara mengi kibinafsi, kijamii, kimwili, kiakili, kiuchumi hata kimaisha Je, hii husababishwa na nini? Hatuna jibu moja wala jibu rahisi. Yapo mengi yanayosababisha umaabala huu. Moja, yaweza kuwa kuingia kwenye ndoa bila kufanya utafiti na kuielewa mila na shurti zake.
Pili, ni tabia ya wahusika. Wapo wanaokwapukia na kupwakia ndoa bila kujiandaa au kuandaliwa. Zamani, kulikuwa na taasisi za Kiafrika za kuwaandaa watarajiwa kuingia kwenye ndoa. Ziliitwa jando kwa wanaume na unyago kwa wanawake. Taasisi hizi zilitofautiana baina ya makabila. Tofauti hii ilitokana na utofauti wa mazingira na mila za jamii husika. Hata hivyo, zilifanana kwa kitu kimoja kikuu. Vijana wa kike na kiume walipelekwa sehemu maalumu na kufunzwa na kufundwa na makungwi namna ya kuishi katika ndoa.
Katika jando na unyago, yapo makabila ambayo yalitahiri vijana wa kiume na mengine hata wa kike. Kutahiri wanawake, kuna madhara makubwa kimwili na kiakili. Hivyo, zama hizi, mila hii imepitwa na wakati.
Kwa ufupi, katika jando na unyago, wahusika walifunzwa na kufundwa juu ya namna ya kuwa watu wazima wake na waume. Walifundishwa miiko ya ndoa na mambo mengine muhimu ili kuwasaidia kuishi maisha ya ndoa kwa furaha na ufanisi. Hata hivyo, siku hizi vijana wanafundwa na mitandao ambapo mambo mengi ya hovyo na uongo hufundishwa na wale wanaotaka kupata wafuasi ili wapate fedha.
Hata hivyo, baada ya ujio wa dini za kigeni, taasisi hii adhimu na muhimu iliuawa na kudharaulika kiasi cha kusababisha madhara makubwa kwa taasisi ya ndoa. Ni bahati mbaya. Si wengi wanashuku wala kuhoji uvamizi huu wa kimila ambao kimsingi, si chochote bali ukoloni kama ukoloni mwingine wenye lengo la kuwabadilisha wahusika ili kuwatawala na kuwanyonya.
Tatu, ni msukumo wa jamii iliyoacha maadili yake na kupwakia maadili ya kigeni bila kuyajua vizuri na athari zake hasi kwa walengwa. Mfano, siku hizi mabinti wengi hawajifunzi kunga za nyumba kama vile heshima, mapishi, usafi, uvumilivu, usiri, na mengine mengi ambayo zamani, yalithaminiwa sana. 
Nne, kukua kwa teknolojia. Tangu kuibuka kwa matumizi ya mtandao, mabinti wengi hawana nafasi ya kujifunza stadi za maisha. Mfano, wapo wasiojua kupika kabisa. Wanachofanya ni kwenda kwenye mitandao na kutafuta recipes za mapishi au mapishi, hatuna Kiswahili chake.
    Kama tujuavyo, japo binadamu ana uwezo mkubwa wa kujifunza, si mara zote huelewa anachofundishwa. Huweza kuelewa anachofundishwa kupitia kurudiarudia ndiposa huelewa na kukubuhu. Mapishi yatokanayo na kujifunza pindipo mhusika atakapo kupika hayamuweki kwenye nafasi nzuri ya kuyamudu. Kuna usemi kuwa njia ya kuingia kwenye moyo wa mwanaume hupitia tumboni. Hivyo, chakula kina nafasi kubwa katika kuimarisha au kudhoofisha ndoa.
Hata hivyo, tokana na usasa, stadi za mapishi zinaonekana kama jambo la zamani. Hapa, ndipo umaabala unapoanzia na kutamalaki. Pia, tunashauri jamii ianze kurejea mila na utamaduni vya zamani vinavyofaa na kuacha visivyofaa. Hii itasaidia kuepusha ndoa na wanandoa kuishia kuwa maabala na kujenga jamii ya kimaabala ambayo haidumu.
Chanzo: Mewananchi Jpili leo.

Thursday, 26 February 2026

Nimewasamehe ‘mamluki’ waliokinukisha wote tukanuka

     


 
Juzi, Fyatu mmoja aliyefyatuka bila aibu wala woga akanifyatua na kuzusha kuwa nina uroho wa madaraka kana kwamba yeye hanao! Nani asiyependa madaraka? Kwanza, sikuamini ningehusishwa na dhambi hii ambayo chanzo chake ni shetani kutaka kumfyatua Sir God aliyemfinyanga asijue. Huwa nashangaa. Kwanini Sir God ‘mjua yote’ hakujua kuwa sheitwan angejaribu kumfyatua? Siishii hapo. Kifyatufyatu, hujiuliza. Kama kweli sheitwan ‘alipanga’ kumfyatua Sir God, ilikuwaje tukatupiwa sisi na si aliyemfyatua? Tuache ngano za imani kama zile za imani ya amani. Yawezekana sheitwan ni Gen Ziro kama siyo zero brain. Sheitwan ashindwe na kulegea au atokomezwe akatokomee mbali watoi wapone. Ashindwe sawa na wale wanaoteka, kupoteza, na kuua ili wote wenye ufyatu tupone. Ashindwe pamoja na watesi wetu wanaojifanya kuwa wapenzi wetu.
        Nilijishangaa na kuwashangaa mafyatu fyatuliwa na fyatuzi waliofyatuliwa na wale wasioamini wasingeweza kufyatuka tukafyatuana. Si ni pale ‘mamluki’ wachochezi waliohongwa na mabeberu na mafahari walipofyatuka wakafyatua na ‘kuwachochea Gen Ziro wetu na kukikunisha hadi wote kunuka tusijue tulikuwa tunawapinga na kuwasweka ndani waliotabiri kuwa kingenuka kikanuka! Je, nani astahiki kushikwa na kuswekwa lupango kati ya waliosema kingenuka na waliokinukisha?
        Anayebisha, kupata jibu sahihi na ukweli, akamuulize Toto Tunda Lishe na wale waliomfyatua kwa kuzuia asiwafyatue wakaishia kufyatuliwa na kuaibika wasijue namna ya kujisafisha. Hapa, mwenye makosa ni waliofyatuka wakafyatua au wale walio fyatuka wakawafyatua waliokataa kufyatuliwa wakitaka kuzuia wasifyatuliwe? Lazima tufyatuke na kutaka kujua mwenye makosa ili tumfyatue kutoa somo kwa yeyote atakayepanga au kudhamiria kutufyatua siku zijazo. Hatufyatuliwi tena, fyatu anasema tena bila woga kuwa naweza kumfyatua kwa kumteka na kumpoteza! Kweli mambo yamebadilika!    
        Hakuna ufyatu ulionitisha na kunichukiza kama kusikia mafyatu tena wanene wakifyatuka bila aibu kuwa hakuna waliouawa wakati ushahidi unafyatua vinginevyo? Je, hapa nani anamfyatua nani ili iweje kama siyo kujifyatua ufahamu na kuongeza mafuta motoni? Unajifunza nini hapa?
        Hakuna kitu kilinifyatua nikafyatuka na kutamani kufyatua kama kusikia eti waliofyatuka wakakinukisha walikuwa mamluki! Hivi, kweli waliofyatuka hadi damu zikajaa kila mahali kayani kweli walikuwa mamluki? Kama ni kweli, waliowaua walikuwa nani? Fyatu ningependa kujua hao ‘mamluki’ wazandiki waliingiaje kayani bila vyombo vya uhasama, sorry, usalama kujua hadi wasiwafyatue kabla ya kuingia na kutufyatua kama ‘walivyotufyatua?’Hayo tuyaache. Mgoshi Machungi umeipata au unjifanya chura usisikie japo wasikia?
        Hakika, nilisikia watuhumiwa wa unyotoaji roho na ukatilii wakitoa ‘nsamaha’! Eti wanataka marudiano sijui maridhishano! Kilichotoka hakiwezi kurudi. Hamkani si shwari tena. Maji yeshamwaika. Hii ni kweli, inawezekana, au ni gea? Je, tunaanzaje ‘kusameheana’ hata kusemezana mbali na kuridhiana na kuridhishana bila kujua nani alifanya nini na kwanini na iwe nini? Nani mwenye mamlaka au kawapa mamlaka au ni kujipa mamlaka bila kuweka wazi nani anamsamehe nani na kwa mamlaka na uhalali vipi?
        Ukisia uchokozi wa kiwango cha SGR, ndo huu. Hivi, huwa unajisikiaje pale aliyekukosea na kukufyatua anapojifyatua ufahamu na kukataa au kushindwa kukuomba msamaha huku akijibaraguza kwa kukubagaza kuwa ‘anakusamehe’ kana kwamba hakukukosea? Nani wa kusamehe na kusamehewa hapa? Unasamehewa kwa makosa gani wakati mkosewa ni wewe? Je, nani apaswa kumhukumu, kumsamehe, hata kumuadhibu nani?
        Hebu tufyatuke kiakili na kuuliza. Je, ni nini chanzo cha haya manukishano? Kwani, hatujui chanzo na sababu au tunajifyatua ufahamu tukidhani na wahanga nao watatufuata wajifyatue badala ya kutufyatua kwa kuwafyatua?
        ‘Wasio’ waroho wa madaraka wanatuhimiza tuchukie wanaowapinga kwa sababu wana uroho wa madaraka! Ni uroho upi wa madaraka kati ya walioyapata kwa mlango wa nyuma na wanaoyatafuta kwa kufuata haki zao kikatiba? Nini uroho na usio uroho? Nani asiyependa madaraka huyu tumuone atufunze jambo au mawili tuache uroho wa madaraka? Je, kupenda au kutafuta madaraka ni uroho wa madaraka au ndiyo maana na roho ya madaraka? Nani asiye mroho wa madaraka aliye tayari kuyaachia bila kuyang’ang’ania ukiachia mbali kuyapoka hata kwa kuua wenzake?
        Hakuna kilichonishangaza kama kusikia walioamuru mauaji ya halaiki ya mamluki ‘wakihuzunika’ midomoni wakati rohoni wanafurahi! Ajabu ya maajabu ni pale mtuhumiwa anaposamehe na kuunda (timu siyo tume) eti kujichunguza kama njia ya kuwafyatua mafyatu! Je, mafyatu wataigia mkenge wafyatuliwe kirahisi hivi? Nani apaswa kuunda timu au hata tume kati ya aliyenyotoa roho na aliyenyotolewa roho? Hivi, yupo awezaye kuridhiana na marehemu? Ukifanya hivyo na ndugu zake, ujue wao siyo yeye wala hawajui angefanya au kusema nini kuhusiana na kunyotolewa roho bila hatia zaidi ya wahuni na waroho fulani kutaka au kung’ang’ania madaraka kinyume cha sharia, kikatili, na kizwazwa? Nimewasamehe ‘mamluki wote’ walionifyatua. Hivi, niko wapi, nafanya nini, na nimesema nini?
Chanzo: Mwananchi Jtano jana,

Monday, 23 February 2026

Ndoa ndoana inapomnasa aliyeitega


Aja Mali (28) (si jinale halisi) alibuni na kuingia ndoa iliyogeuka ndoana iliyomnasa vilivyo. Kijana huyu wa kihindi aliingia Marekani kwa mkataba wa kazi wa muda mfupi. Alifanya kazi vizuri. Hata hivyo, alijua fika. Muda aliokuwa amekubaliwa ungeisha, visa yake ya muda pia ingeisha. Hivyo, aliamua kufanya kitu ambacho kingemuwezesha kuendelea kuishi majuu asijue mwisho wake.
Kwa kutumia ujana na uzoefu wake, Aji, aliamua kumpenda mama mzee Linnie (60) (si jinale halisi) ikilinganishwa na umri wake. Fanya hesabu ujue tofauti ya kiumri. Kweli, shida haina adabu. Kwa vile Aja alidhamiria kufanikisha mpango wake wa kuendelea kuishi majuu, hakukata tamaa wala kufikiri mara mbili. Baada ya mapenzi kunoga japo kinafiki, Aja alifunga ndoa na Linnie mama tajiri mwenye nyumba na akiba si haba. Linnie aliongeza jina la Aja kwenye akaunti yake ya benki na kuifanya iwe ya pamoja.
        Kama haitoshi,Aja alimuomba mkewe mama aka mshangazi amdhamini kuendelea kuishi majuu. Mke hakukataa. Wanguwangu, alianza utaratibu wa kumdhamini apate kibali cha kudumu cha kuishi majuu. Mwanzoni, mapenzi yalikuwa motomoto. Wawili walipenda. Hata hivyo, binti mtu, ndugu, na marafiki hata majirani walishuku ndoa hii ambayo kwao ilionekana ya ajabu. Wapo waliosema kuwa Aja alifuata utajiri wa Linnie. Pia, wapo waliosema wazi kuwa Linnie naye alitaka kutumia shida na uhitaji wa Aja kumnyonya kingono. Kimsingi, ndoa hii ilikuwa kama mchezo wa karata tatu. Kila mmoja, alikuwa na lake akitaka kumtumia mwenzake kiasi cha kutumiana. Na kweli, walitumiana kabla ya ukweli kufichuka na ndoa kuingia doa. 
Hakupita muda, Aja alianza kuhamisha fedha Kwenda kwenye akaunti yake binafsi. Alianza kuongea kwenye simu kwa muda mrefu kwa kikwao tena akiwa nje ya chumba cha kulala. Hii ni baada ya Aja kujiridhisha kuwa mpango wa kumdhamini ulikuwa karibu kukamilika. Bila hili wala hili, hali hii ilimhuzunisha Linnie. Lakini alijipa moyo. Taratibu, ufa katika ndoa doa ulianza kupanuka. Aja alianza kukosa mawasiliano na ukaribu na Linnie. Linnie alianza kushuku kitu. Ila alijipa moyo kuwa mambo yangetengamaa asijue yasinge.
Bila simile wala woga, Aja alimkabili Linnie na kumueleza kuwa baada ya kukamilika udhamini wa kuishi majuu, angehama nyumbani kwa Linnie. Hili, kwa Linnie lilikuwa pigo lililomliza kiasi cha kusema lolote na liwe. Badala ya kumuomba asitekeleze azima yake, Linnie naye aliamua kujibu mapigo kivyake once and for all.
Bila kumstua Aja, Linnie alipanga mpango wa kumkomesha Aja. Baada ya kujiridhisha kuwa mpango wake usingefanikiwa kama alivyoupanga, Linnie aliamua kufanya vitu vyake. Wakati Linnie aliyekuwa ameishakata mawasiliano na binti yake kipenzi na wengine waliomzunguka kujua maji ndo yalikuwa yakimwagika mikononi mwake, aliamua liwalo na liwe na kweli lilikuwa. Hakumstua Aja wala kumuonyesha mabadiliko yoyote. Aliendelea kuwa mke hata kama ni wa kuigiza hasa ikizingatiwa wawili hawa hawakuwa na lolote waliofanana wala kufaana zaidi ya kutumiana.
Aja aliendelea kwenda kazini asubuhi na mapema na kurudi jioni kama kawaida. Huko nyuma, Linnie alirejesha mawasiliano na binti yake bila kumueleza sababu wala masahibu yake na kimwana wake. Alipiga konde moyo na kuamua kufanya kitu. Kwa vile mabadiliko ya Aja yalikuwa yamemletea ugonjwa wa kukosa usingizi hadi kwenda kwa daktari wake aliyemuandikia vidonge vya usingizi, aliamua kuvitumia zaidi ya alivyopaswa.
Aja aliporudi siku ya siku, alimuuliza Linnie juu ya udhamini. Linnie ambaye alishaukatiza wala hakumpasha kilichokuwa kikijiri. Kama kawaida ya watasha. Atakukumbatia kwa furaha halafu akudunge kisu mgongoni. Alimuandalia kila kitu mumewe. Kumbe kwenye chakula cha Aja Linnie ashajaza vidonge vya usingizi. Aja, bila ajizi, alikula msosi asijue ulikuwa ushadukuliwa.
Muda haukupita. Aja alijihisi usingizi. Alidhani ni uchovu wa kawaida. Taratibu alipanda kitandani mwao lau ajilaze kwa muda. 
Linnie aliyekuwa akisubiri ndege anase mtegoni, alichukua mto na kumziba hewa Aja hadi akakata roho usingizini. Chapchap alimpigia simu bintiye na kumpa inshu nzima. Binti alikuja na kumsaidia mamaye kuingiza mwili kwenye gari na kwenda kuutupa kwenye sehemu ya kutupia mabaki kiwanda jirani. Hivyo, ndivyo ndoa ilivyogeuka ndoana na kumnasa aliyeitega. Yapo mengi. Nafasi haitoshi.
Chanzo: Mwananchi Jpili jana.


Tuesday, 17 February 2026

Tufyatue Dhana ya familikrasia katika kisiasa

Leo, nazamia rubaa za kimataifa na kitafiti. Baada mtoi wa marehemu rafiki yangu kutemeshwa bungo tokana na kupata ukwasi kwa kutumia surname, leo, nazamia dhana mpya iitwayo Familikrasia, yaani unene wa kifamilia kama sehemu ya demokrasia mamboleo. 
            Nitarejea utafiti wangu wa shahada ya uzamizi, PhD kama wengi waijuavyo. Tasnifu hii ni ya kumi tena ya kubukua siyo kudukua, kununua, au kuzawadia kimagumashi kwa kukimbia umande. Ila nashauri mniite Fyatu na si daktari maana, udaktari siku hizi, umechafuka baada ya kuvamiwa na kuishiwa maana sababu mazwazwa wameunajisi na kuutumia vibaya.
            Lengo kuu ni kutaka kubaini kama familikrasia ina manufaa kikaya au kifamilia au vyote hasa baada ya kutema bungo au kufika ukomoni. Katika utafiti huu kuna matabaka makuu mawili ya ufyatuzi na ujembuzi. 
    Utafiti huu wa kidoktari na kifyatu uligundua mambo makuu yafuatayo:
        Kwanza, wahanga wanachukia familikrasia kimyakimya wakiogopa kupotezwa na kupatilizwa. Hili, limebainishwa na dhana ya Unapokula Kula Usijali Kesho Utajiju (UKUKU) ambapo wahusika hugeuka waroho, wakabila, mafisadi, na ving’ang’anizi kwenye ulaji kiasi cha demokrasia kuwa kichekesho, kikaragosi, na ghasia. Katika kufanya hivyo, hutenda makosa ambayo huwagharimu baadaye. Pia, nimegundua UKUKU ndiyo ulisababisha maanguko na vifo vya akina Kashafi na Sir Damu.
        Pili, familikrasia inachukiwa kwa sababu huhalalisha ufyatuaji mkubwa wa njuluku za mafyatu kutokana na uroho uliojificha nyuma ya UKUKU.
        Tatu, utafiti umegundua kuwa wengi, kama si wote, wa walaji hukosa vigezo vya kisomi isipokuwa ukaribu uwe wa kiukoo au kirafiki na mteuaji. Hivyo, wengi huwa mazwazwa na wasanii wa kawaida wasio na sifa yoyote hata ya kuongoza kundi la nyumbu.
        Nne, familikrasia hujihadaa na kujenga mfumo wa utukufu uchwara ambao msingi wake mkuu ni kutumia vitisho na kuzawadiana ili kuhimili vishindo vya uchakavu, ufisadi, na ulazimishi wake. Hii inapotokea, hujengeka upofu au myopia kwa kisambaa ambao nao hujenga kujisahau na kutojiamini kiasi cha kila asiyekuwamo kuonekana adui na tishio. Hivyo, huleta ukandamizi, usanii, ubabaishi, n.k. Muhimili wa familikrasia ambao ni kichwa chake hujijengea uungufyatu kiasi cha kutengeneza viini vya kujiteketeza wenyewe.
        Tano, familikrasia hulindwa kwa woga na kushuku. Hili, husababishwa na kupwaya na kutokubalika vizaavyo kutojiamini, kuaminika, na woga.
        Sita, familikrasia hubebwa na ukosefu wa aibu, udhu, ufyatu, na ukatili vya kutisha. Mfumo huu, unaweza kuua yeyote anayetaka kuuzuia, kuupinga, kuukosoa, hata kuuondosha. Hivyo, kusababisha maumivu kwa mafyatu mbali na kuwanyonya.
        Saba, familikrasia hutegemea sana matumizi mabaya ya njuluku na raslimali za mafyatu  hongo ya, ulaji, maguvu, majungu, vishawishi, ghilba, na vitisho. Kwa mtoi wa rafiki yangu, rahis wa zamani tena jobless, kilikutwa na mimamli kibao iliyotaifishwa. Je,viko vingapi duniani hii gunia?
        Nane, familikrasia hutegemea kulindana, kung'ang'ania unene ukichelea kung’olewa ambapo jinai yake hufichuka na kuishia ghaibu au lupango hata kuuawa kama ilivyotokea kwa watajwa hapo juu.
        Tisa, utafiti umeonyesha kuwa UKUKU, kwa mfano, kuna uwezekano wa wahalifu wa kiunene kunyatuliwa roho na mafyatu wenye hasira wanapouchoka na kuamua kuuangamiza usiwaangamize.
Matokeo ya utafiti
        Katika kutafiti dhana hii tata nilianzia mtaani kwangu Idodomya––––we koma!!––––na kuelekea Equatorial Guinea, kwa Tarampu. Nilimalizia kwa M7 ambako familikrasia imeota mizizi na kutamalaki kitambo sasa. Katika variables nilizotumia, kuna makundi makuu mawili yaani, kupeana ulaji kifamilia/kirafiki kwa kutegemea uhusiano wa damu au wa kindoa. Vigezo nilivyobaini ni utoi au ukweee. Mfano, kwa M7, vitegemezi na Bi Mkubwa ni sehemu ya sirkal ya Bwana Mkubwa kama sambamba na kwa Trampia ambako wakwe wanatesa katika ulaji. Kule Guinea ya Ikweta, vitegemezi vya munene vinatesa pia.
            Walaji wengi katika familikrasia wamethibitisha kuwa mifyatu mifala, milafi, yenye tamaa, na katili. Pia, mingi ya mifyatu hii ni mitoi, mikwezi, hata washirika wa bedroom hupenda ujiko kutanua ilhali upstairs ni kweupe. Haina aibu na ni michafu usipime. Ingekuwa nazo sawasawa, ingeonea aibu udandizi, wizi, na ulaji wa njuluku za mafyatu bila stahiki isipokuwa unene wa mabuda, maza, au wakweee zao.
Dokezo
Pamoja na kushauri utafiti zaidi, tunapendekeza waathirika si kuuchukia tu ufamilikrasia bali waukabili na kuuondolea mbali ili kupata HAKI na maendeleo kwa ujumla. Katika penye ufamilikrasia kunakuwapo na amani mawenge ambapo haki na usawa hutoweka kiasi cha kaya kuwa kama pango la majembuzi. Hivyo, dawa ya kuondokana na ufamilikrasia ni kuwapo na kutamalaki kwa haki, maadili, na mageuzi ya kweli kimfumo.
        Mwisho, ufamilikrasia ni jinai inayoanza kuzoeleka na kuota mizizi katika kaya nyingi za uswekeni hasa zinazojifanya kuendelea. Ushauri ni kwamba uchukiwe na kupigwa vita kulhali na na kuogopwa kama ukoma. Hii bangi, hivi niko wapi na nafanya nini yarabi!
Chanzo: Mwananchi Jtano leo.

Sunday, 15 February 2026

Letter from Canada where internet is a human right


 The heading is clear. There recently were some internet blackouts in some countries. This sacrilege can't happen in in Canada. Internet access is considered as one of the human rights everybody must enjoy. Therefore, unless otherwise stated, there’s no power whatsoever that can discretionary or out of desperation disconnect or turn internet off for whatever purposes or reasons except under certain circumstances provided for. Under Bill.C-8, the minister of Communication is strictly allowed to make an order to shutdown internet shall there be “reasonable grounds to believe that it is necessary to do so to secure the Canadian telecommunications system against any threat, including that of interference, manipulation, disruption or degradation.”

          As per the Government of Canada website, “the rights and freedoms that individuals have offline must also be protected online. Canada is committed to working with international partners to protect Internet freedom, including the rights to online freedom of expression, association and peaceful assembly, as well as to protect privacy online.” Thus, Canadians enjoy the rights of access and protection of internet.

            In Canada, it isn’t the choice or the discretion of the government or any institution to censure, disconnect, or discretionary provide internet. It’s like water and other essential amenities for Canadians. If anybody–––be it a person or a government––– denies Canadians such a right will not only be denying Canadians their rights but also committing an offence.

            Why has internet become a human right in Canada?

The answer is simple. Internet isn’t a choice or a favour. It’s an essential part and tool of life. You can measure the health of any nation by assessing its freedom of information. People use internet to do business, communicate, study, and many more. Therefore, whoever impinges on the right to access internet adversely affects the lives and the rights of millions. So, too, internet clampdown doesn’t only show how primitive and unfeeling a society that does so is but also can lead to criminal and tort liabilities.

            That said, Canadian leaders avoid such liabilities. If they don’t, they’ll foolishly lose their positions since whatever tort liabilities emanating from such a primitive act legally force the government to redress the victims. That’s because nobody is in power on her or his behalf but that of the citizens and the money paid for covering such wanton expenses comes from Canadian taxpayers. So, by committing such a crime, whoever does so, he automatically loses one of the qualities of leadership. Therefore, such a person or government can be shown the door for abuses of public funds, callousness, criminality, negligence, and others. No sane person does so or needs that. This is what is known as competent and good governance.

            That said, in my country, Tanzania, internet was shut down during chimeric elections wherein the incumbent President won by 98%! If anything, currently, this save for being one of the wonders of the world, can stand as a world record of Presidential ‘victory’ if indeed it’s won fairly and squarely, which even a little bird told me that it doubts this charade. That’s because even during the one-party dictatorship, no Tanzanian President won such a hugely convoluted and tantalising ‘victory.’

That said, such a ‘win’, in bootlicking science, is known as ‘the miracle of the miracle maker.’ Again, to connect this to internet, such a win was achieved during internet blackout. Guess what. If there wasn’t internet clampdown, it’d have interfered with the win and thereby adversely affect and endanger national security, which revolves around one demigod known as President.

            Howbeit, it’s key to know. Sometimes, in some primitive places, internet isn’t only a danger but also a deadly weapon for whoever controls it. For, hackers can use it to frustrate even destroy the win of the infallible mtukufu rais. You know what I mean. That’s the only person in a particular country who runs everything discretionary and effectively regardless of whatever flaws.

            In toto, internet is a human right that needs to be feared. For, it can make people ask for more rights or prevent young voters from voting, which can impinge on the rights of the high and the mighty. So, you know. When’ll cyberspace become a human right in Africa?
Source: Daily Nation today Sunday.

Ishini pamoja na siyo kwa pamoja


Kuna ndoa nyingi ambapo wanandoa wanaishi nyumba moja na kulala kitanda kimoja lakini hawaishi pamoja. Kimwili wako pamoja japo kiroho wako dunia tofauti.  Wanaishi kwa pamoja ila si pamoja. Tuliwahi kugusia madhara ya mitandao na rununu. Mfano, unakuta mke au mume hana haki wala mamlaka ya kujua nywila ya simu ya mwenzake achia mbali kuweza kuishika au kuitumia. Kwanini? Kwa sababu kwenye simu husika kuna mambo ambayo mwenzi hapaswi kuyaona wala kuyajua.
            Kama wanandoa, huwa tunashangaa inakuwaje? Binadamu yoyote timamu kiakili na kiumri ana siri moja inayokubalika kijamii. Nayo, ni kuficha uchi wake. Ni vichaa na watoto pekee wasioweza kufichi sehemu uhci wao. Waliobaki, hakuna kitu kigumu kufanya kama kutoka nje bila kujisitiri. Tena, husema uchi wa mnyama kwa vile ni wanyama tu wanaishi bila kuhitaji kujihifadhi. Hata nao ukiwaangalia kwa makini, hawako uchi.
            Katika ndoa, hakupaswi kuwapo siri baina ya wanandoa. Kama wanaweza kuvuliana nguo, inakuwaje kwanini wasivuliane mioyo? Kama uko kwenye ndoa kama hii, ujue. Mnaishi nyumba moja, kulala kitanda kimoja, kumilki mali na watoto pamoja lakini hamko pamoja. Dhana ya kuishi pamoja inahusisha kuwa pamoja katika kila jambo liwe kubwa au dogo. Huwezi kumficha mwenzio au kuwa na siri zako ambazo hutaki mwenzio azijue mkawa pamoja. Hapana. Kwenye baadhi ya dini, wakati wa kula kiapo cha ndoa, wanandoa huambiwa kuwa wanaacha kuwa miili tofauti na kuungana na kuwa mwili mmoja. Ni mwili gani ambao kiungo chake kimoja kikiumia, sehemu nyingine hazihisi au kushiriki yale maumivu?
            Ndoa siyo kama mashine ambayo inaweza kuwa na sehemu nyingi tofauti ambazo hazijuani wala kuwa na athari sawa.  Magari ya siku hizi yana sensor kiasi cha kuwa mwili hai. Ndoa ni sawa na mwili uwe wa mtu, mnyama hata mti. Ukichuma jani kwenye mti, mwili mzima wa mti unahisi kitendo ulichofanya. Utafiti umeonyesha kuwa miti ina hisia. Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC, 2023) ulioripotiwa na Bethany Nichols uitwao Plants Have Feelings Too miti ina hisia. Ikiguswa inajua. Utafiti huu ulionyesha kuwa miti inapata hata msongo tokana na mazingira iliyomo. Mfano, miti aina ya Arabidopsis thaliana, ikiguswa inajua. Mfano, mwaka 2014, Heidi Appel na Reginald Cocroft wa Chuo Kikuu cha Missouri walichapisha ripoti ya kushangaza. Katika utafiti wao, kwa kutumia vifaa maalumu, walichezesha sauti ya viwavi wakila majani, upepo ukivuma, wadudu chavushi wakija kuchavu na mengine. Miti ilionyesha miitikio tofauti kulingana na sauti iliyochezwa.
            Sasa tujiulize. Kama miti inaweza kuhisi, inakuwaje kwenye ndoa kuwa na siri binafsi kwenye mwili mmoja na sehemu mojawapo ya mwili isihisi au kujua?
            Hivyo, tunapoongelea dhana ya kuishi pamoja na kuishi kwenye nyumba au kitanda kimoja, tuzingatie kuwa kuna uwezekano watu wawili wakalala kitanda kimoja lakini wakaishi kwenye dunia tofauti. Jambo hili hi hatari sana kwa wanandoa. Lina gharama kubwa. Maana, hakuna gharama na usumbufu kama kulinda na kutunza siri. Hii inapotekea, licha ya kumomonyoa upendo na kuzalisha mafarakano, huwaumiza wahusika kisaikolojia kiasi cha kukumbwa na hatari na magonjwa vitokanavyo na msongo wa mawazo ambao kwa sasa ni tishio la afya ya akili duniani.
            Sasa,  nini kifanyike? Mosi, wanandoa waanze kujichunguza kama wanaishi pamoja au wanaishi kwenye nyumba pamoja. Pili, wanandoa waanze kujifunza kuishi pamoja na si kuchangia nyumba na vitanda.
            Tatu, wanaweza kuanza kwa majaribio. Matokeo watakayopata, yanaweza kuwapa la kuchagua ima kuendelea kuchangia nyumba na vitanda au kuanza kuishi pamoja.
            Nne, kwa wale wanaochangia nyumba na vitanda wafahamu kuwa hizo siri wanazoficha na kulinda kwa gharama yoyote zitakuja kufichuka siku moja na wagundue kuwa walikuwa wakihadaa wakiamini wanawahadaa wengine. Hakuna kitu hatarishi na kigumu kama kuwa na kutunza siri. Mshaambwa. Duniani hakuna siri. Kama ipo, ipo kwa muda tu ila si milele. Kama chaji ya simu imeisha, mwaweza kuaziman? Kama hamuwezi, mnaishi tofauti.
Hilo ndilo somo la leo. Kwa wenye maoni mnaweza kutufikia kwa barua pepe nesaa1977@yahoo au nkwazigatsha@yahoo.com.
Chanzo: Mwananchi Leo Jpili.

Tuesday, 10 February 2026

Fyatu kwenda Romu kuuombea Popu aombee Mafyatu

Mwenzenu napanga kwenda Vatikano kukutana na popu kumuomba na kumuombea aombee amani. Nitaadamana na baadhi ya mashehena sorry mashehu wenzangu. Tutahakikisha anaombea amani tu bila haki. Naona yule anashaangaa akadhani mibangi imenifyatua nikafyatuka na kutaka kuifyatua amani! Nina sababu nzuri tu za amani tena kwa amani. Baada ya mafyatu kuzidisha ufyatu hadi kutaka haki kwa gharama ya amani, kama mhimili mkuu wa amani Fyatuland, naanza kushindwa kuwafyatua walipofyatuka wanifyatue, na mwisho wa siku, amani itoweke.
        Sipendi niwafanyie kitu mbaya wakose amani na kunilazimisha kukimbilia kutafuta moto kwenya maji kama suluhu kama yule sulubu. Mpango mzima ni kuikomboa Fyatuland isijiangamize kwa ufyatu. Nikifika, nitamsihi sana aombe mafyatu wawe na amani katika kila jambo. Mfano, wakifyatuliwa, wawe na amani.Wakiburuzwa, wawe na amani.
            Nitamuomba na kumuombea popu aombe amani ili mafyatu, hata wakipigwa au kupigana, wafanye hivyo kwa amani, watulize boli wawe na amani. Maana, bila amani, itakuwa vigumu kuishi na kufyatuana. Amani ni uhai na uhai ni amani; haki ni vurugu iletayo machafuko itokanayo na mafyatu kutaka wapewe hata wasivyostahili kama kujua namna ninavyowafyatua.
 Najua popu atanielewa na kukubali ombi langu la kumuomba, kumuombea, aombee amani kwa amani. Nitafanya hivi kwa amani ili iwepo amani baina yetu. Nitamuomba na kumuombea aombe amani ili tuishi kwa amani bila kukwaruzana na kudaiana haki tena bila amani. Haki inaweza kuua Fyatuland kwa ukosefu amani. Uwepo wa amani utawezesha hata mvua kunyesha. Kutamalaki kwa amani kutawezesha ulaji wangu uwe na amani kiasi cha kufyatua kwa amani.
             Nitamsisitizia Bwana Mkubwa kuwa amani ni tunu ambayo niko tayari kuteka, kupoteza, hata kuua kwa ajili yake. Nataka niwe na amani ya kufyatua mafyatu ila wasiwe na haki ya kunihoji, kunituhumu, kunishitaki wala kunidai au kuwa na haki ya kuvuruga amani. Mafyatu wakiwa na amani, kila kitu kitakwenda vizuri. Hapatakuwapo madai ya kipuuzi kama vile kukinukisha, kuandamana, au kulalamika. Amani haitaki mambo haya. Nataka mafyatu wawe na amani kama kondoo. Kondoo ukimchinja kwa amani, anakufa kwa amani nawe unamla kwa amani.
             Kwa wasiojua haki na madhara yake, wanapenda sana kuomba na kuitaka. Haki ya nini wakati kuna amani hata kama ni ya imani? Haki inaweza kuleta machafuko. Nani anataka haki wakati haki haileti amani bali shari? Ukitaka kuepuka machafuko, basi omba amani tena kwa sana huku ukiikataa haki. Kama utaomba haki, basi omba haki isiwepo bila amani. Maana, bila amani, hata iwepo haki, tutavurugana na kufyatuana. Nitamuombea na kumuomba popu aombe tuwe na amani ya kuwafyatua wanaotaka haki tena kwa amani. Pia, nitamuomba aombe watakaofyatuliwa watulie kwa amani ili wasivuruge amani. Nitamsisitizia aombee Fyatuland iwe na amani na kuchukia na kuepuka haki.
Nitamshauri asiombe haki. Kwani, haki huvuruga amani. Haki huwapa haki mafyatu kuvuruga amani kwa kisingizio cha kuomba na kutaka haki. Amani ni muhimu kuliko haki. Kukitamalaki amani, kila fyatu anafanya na kufyatua kila atakacho kwa amani.
            Nitamuomba na kumuombea popu aombe amani kwa mafyatu waishi na kukubali kila jambo kwa amani. Wakifyatuana hata kuuana, wafanye hivyo kwa amani. Wakitekana au kupotezana, wafanye hivyo kwa amani. Watakaouawa au kufa, wafanye hivyo kwa amani. Wakizikana au kutopata maiti za waliofyatuliwa kwa sababu ya kiherehere cha kutafuta na kutaka haki, wafanye hivyo kwa amani.
            Mbona kuku wana amani japo hawana haki? Kama haki ni mali basi amani ni pepo. Hivyo, nawasihi mafyatu watafute amani. Haki wataikuta mbinguni. Waombe amani ili kila kitu kifanyike kwa amani. Tokana na kutokea mafyatu kama wale wa TEKI tena wanaojifanya wanamfuata popu kutaka kuvuruga amani kwa kudai haki, nitamuomba popu awaombee na kuwakataza kufanya hivyo kwa amani. Nitamshauri awaamuru wote wahubiri amani wakati wakijitenga na haki.
        Juzi, nilikwenda baa na kufanya vurugu kwa amani. Si waliitwa ndata wanidake kwa amani. Nawashukuru sana. Hawakunikamata kwa haki bali kwa amani. Walinipa kipigo cha amani hadi nikalalamika kwa amani. Baada ya hapo, walinifungulia kesi kwa amani. Sasa nangoja kuadhibiwa kwa amani.
            Najua pilato atanipiga mvua si kidogo kwa amani. Kabla ya kufanya hivyo, nitamuomba nijitetee kwa amani ili hata nikifungwa, nifungwe kwa amani. Nitamuomba pilato atoe amri kwa majamaa wa lupango wanifunge kwa amani. Hata pale pilato atakapotamka mvua nitakazokwenda kutumika lupango, nitamuomba atoe hukumu kwa amani. Nitajitetea kuwa nilipofanya vurugu, kimsingi, nilikata kalaji kwa amani nako kakanifyatua kwa amani kiasi cha kufanya vurugu kwa amani hadi nikakamatwa, kuhukumiwa, na kufungwa kwa amani. Kuanzia leo, Fyatuland itaitwa amani na itakuwa mwiko kwa fyatu yeyote kutuletea makelele haki. Du! Majinamizi mengine, acha tu! Inaonekana mgoshi Machungi keshanipiga zongo.
Chanzo: Mwananchi jtano leo.

Sunday, 8 February 2026

Letter to Muhoozi Keinerugaba, Tweet Even More Please


Muhoozi, before saying something, I must remind Ugandans of the best day the country has ever had. On 24th April 1974, Uganda and the world were blessed with and received one of the most powerful sons of presidents in the world, you. This is the time you (who avenges or revenges) came to this earth to save some of earthlings from the ennui of a long-time ruler who happens to be one of your makers. 
        It is the time your great mother gave birth to you, the great son of president who wields as much power as his father, the son who needs more power. Indeed, your arrival wasn’t a common occasion. It wasn’t like the birth of small men and women who come from poor and weak families. Yours was the birth of a saviour of some sort, especially for those who don’t believe that the more things change the more they remain the same. You know what I mean. Still, you’re a saviour for the status quo so to speak vis-a-vis Ugandan politics.
            Dear Muhoozi, a few weeks ago, you, as the most power son of the most powerful man you unveiled what Ugandans need to make do with. Yep, you started to bite at the power that your dad’s been eating on for long. Because of your significance, you openly want everybody to know and make do with you fired a tweet at the US asking it to not put its nose into Ugandan affairs. No joke. You’re not joking. 
            Did you mean business or you’re just looking the way take a bite on power and come out of the political closet. This, to me, shows your significance as the son of the most powerful man in Uganda who also is the most powerful son of the president. The twosome of–––without forgetting your mother––––are the most powerful people Uganda’s ever had. 
        Let Ugandans know that your trinity’s unshakably intact and unique since you’ve made Uganda what it’s today, although your detractors stupidly assert that Uganda was made rich for your family and poor for the rest. Let them know that you still have a lot to offer, and Ugandans must wait for more surprises from this trinity.
            Dear good General, underscoring your greatness and significance, I propose that next time you tweet, all Uganda’s media must support you by subscribing to your tweeter account. I also propose that your tweets must be made breaking news in all Ugandan media. I know those who don’t like you, dear good general, will wag tongues thinking I’m trying to get a mileage out of this assertion, or I might have been paid to say this. Nope, what I’m saying is as simple as the tweets themselves. I know those who don’t know the importance of the first family, namely you,  the mother general, and the father general, wrongly think that their lives are adversely impinged on with uncertainties your tweets cause. Go figure. Guys, who are you in Uganda? Who bewitched or cheated you not to get it?
            Dear General, when the story of your tweets warning the US surfaced in the media before you deleted them later, a friend sent me an email complaining about the uncertainties they’d cause. Also, he’s some concern about the EAC, which’s never delivered anything. I scolded him to stop being selfish, evil, and naïve since things have changed. Christians believe Jesus died for their sins though they’re told everybody to carry one’s cross. On the contrary, politicians believe that citizens must die for them and their sins. Methinks this is the genesis for many African rulers to live larger than life while their taxpayers live and lurch in penury. I told the guy to consider other related things such as the disturbances democracy’s been causing in many African countries that tried it and ended up abusing it through vote rigging and tampering with constitutions to extend their time in office.
            Dear General, methinks Ugandans––––whether they like it or not­­­­–––should brace themselves to see you becoming their leader shall anything happen to your father. This is simple to decipher. When I consider your gruff rise in the army, you can easily know what I mean. Also, if you interrogate the reason[s] behind your father’s clinging unto power, you’ll be on the same page with me. Moreover, if you consider the powers your mom has behind the curtains, you’ll agree with my hypothesis. 
            To give those who pretend to deny the truth, I want them to ask themselves as to why your tweets are leaving everybody shocked. Is the system testing the waters? Is it preparing Ugandans psychologically for what’s on the card in the upper echelons of power wherein manipulations are one of bread and butter of its mainstay? Why have you become such important this time around? Let’s get as serious as a seal instead of trying to screw over this rear up of your display. Those who don’t know your good intentions for Uganda stupidly argue that aim to achieve more power! What power is it while you already have it? Shame on them!
            Dear General, in sum, let me wish you a very spiffy tweeting mission. The Swahili sage’s it that clouds are the signs of rains. Therefore, what you’re seeing regarding your centrality is but the beginning if not the tip of the iceberg. Tweeting warning Uganda’s enemies is one leg in the waters. The sage’s it that if you can’t beat them, join them. Whether they like you or not, they need to understand Uganda’s power dynamics, especially after your dad came to power and altered everything to his advantage.  
        Look at foolish detractors. They foolishly allege that your father propped you up so quickly that way in the military. Nonsense. You’re born a soldier more of a commander. What’s wrong with you to be a presidential material? Once again, Dear General, you seem to brace yourself for big things. Big things come to big people. That’s my titbits of sagacity. Ring-a-ding-ding, nothing but.
Source: Daily Monitor today.