Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Liberal Peace Conflict, Gender, and Peacebuilding

Sunday 21 July 2024

Mwenye mapenzi anaona tena sana

Kuna imani au tuseme usemi kuwa mwenye mapenzi haoni. Je kweli mwenye mapenzi haoni hata kama macho anayo? Je ukweli ni upi haoni au anaona tena sana? Ingawa “mwenye mapenzi haoni” ina tafsiri nyingi kutegemea na hali yaliyomo mapenzi, ukweli ni kinyume. Tutatoa sababu zifuatazo:
        Kwetu mwenye mapenzi lazima aone na aone kwelikweli. Utawezaje kuujua uzuri na mvuto wa mwenzako kama kweli mwenye mapenzi haoni? Ingekuwa hivyo, watu wengi wenye changamoto za aina mbalimbali za ulemavu ambazo ni kazi ya Mungu wasingenyanyapaliwa, kukataliwa, na wengine kutoolewa kabisa au kuachika tokana na changamoto ambazo siyo matokeo ya kazi wala utashi wao. 
            Pia, ukitaka kujua mwenye mapenzi aone, jiulize ni visa vingapi wanandoa waliopeanda haswa walipoachana au kuuana baada ya mmojawapo kumtendea mwenzie mabaya? Kuna kisa cha wanandoa wawili ambapo mke alikuwa si mzuri wa kuvutia ikilinganishwa na mumewe ambaye alimpenda mkewe vilivyo. Hata hivyo, kwa kujua anapendwa, mke alipata msukosuko wa ndoa akatembea na mganga wa kienyeji. Pamoja na mapenzi makubwa yaliyovutia wengi, mume alimuacha mkewe bila hata kumpa nafasi ya kujitetea. Kwa ufupi ni kwamba mwenye mapenzi anaona tena mambo mengine ambayo katika hali ya kawaida huwezi kuyaona wala kudhania yanaweza kuonekana. 
        Kisa kingine ni cha jamaa tunayemfahamu mwenye ulemavu wa macho. Ndugu zake walimtafutia mke toka nchini kwao kuja Kanada bila kumwambia ukweli kwa vile aliwahakikishia kuwa anampenda yule Bwana. Kufanya mambo kuwa magumu zaidi, walimuonyesha picha ya mdogo mtu badala ya muoaji mwenyewe wakiamini akifika Kanada, atazubazwa na uzuri na hali nzuri ya maisha. 
            Pamoja na kuwaonya kuwa walipaswa kumueleza mchumba mtarajiwa kuwa ndugu yao alikuwa na changamoto ya kutoona, hawakufanya hivyo wakiamini mtarajiwa akifika asingeweza kumwacha mtu aliyemfadhiri kuja Kanada. Waliogopa kumwambia wakiogopa kuwa mtarajiwa angeweza kutumia fursa hii kujia Kanada kama ambavyo wengi wako tayari hata kuzama bahari au kudhalilishwa na wasafirishaji binadamu ilmradi wafike majuu. Na kweli, huyu bibie alipata fursa kuingia Kanada kama ilivyotokea. 
            Jamaa akiwa amefurahi kuwa amepata jiko na ndugu zake kadhalika wakifurahi wamemhifadhi ndugu yao, mama alipofika, alilala siku mbili. Kwa sababu mwenye mapenzi anaona, yule mama alishangaa na kuchukia baada ya kugundua kuwa kumbe yule aliyeonyeshwa hakuwa mtarajiwa wake. Alikaa kimya ili lau ajipe muda wa kupokea hali ile iliyomfadhaisha sana.
         Siku ya tatu alisema bila aibu wala kumuogopa Mungu kuwa hawezi kuolewa na kipofu! Je hapa tatizo ni nini? Kuna matatizo mawili. Kwanza, yule mama alikuwa akitarajia mumewe angekuwa mwenye kuwa timamu kwa sababu hakuambiwa kuwa alikuwa na changamoto au tuseme ulemavu wa macho. Pili, yule mama alikuwa na matarajio tofauti na hali aliyoikuta. Alifichwa ukweli ili kuamua kama alikuwa tayari kuishi naye au la pamoja na mapungufu yake.
Kufupisha hadithi ndefu, tunapoandika, hatujui huyu bibie aliishia wapi zaidi ya kujua kuwa alikataa kuishi na mumewe licha ya kumdhanimi kwa matarajio kuwa wangeungana kupiga maisha majuu. Alichoacha ni sononeko kwa yule mume na nduguze.
        Turejee kwa mwenye mapenzi haoni. Anaona. Hebu jiulize. Ulipokuwa ukimtafuta au kutafutwa na mwenzako ni vitu gani ulikuwa unaangalia kwa vile ndivyo vilikuwa vigezo vyako vilivyokuvutia? Mwenye mapenzi anaona tena sana. Wakati mwingine anaona visivyoonekana. Vinginevyo wafitini wasingevunja au kuyumbisha uchumba hadi Waswahili wakaja na busara kuwa ficha uchumba na kutangaza ndoa kwa kuhofia mambo yanayoweza kuzushwa na wafitini na yakapewa umuhimu hata kama ni fitina na uzushi. Ndiyo maana tuna sifa na vitu vya kupatikana kwenye yule unayetaka kuoana naye. Ingekuwa hivyo basi kusingekuwapo na kuwahusisha jamaa kumuangalia na kumpima mtarajiwa wako. Unawaonyesha ili iweje kama siyo kutaka kusikia wanamuonaje? 
        Jamaa mmoja nchini Saudia aliona picha ya msichana mrembo wa kimisri aliyekuwa anatafuta mchumba mtandaoni. Alimpenda na kuridhika na sura yake kiasi cha kutoa mahari dola za kimarekani laki tano. Kitu ambacho msaudia hakujua kuwa kumbe yule msichana aliyekuwa ameweka picha yake kwenye mtandao alikuwa na dada yake mwenye makengeza ambaye hakuwa amebahatika kuolewa kutokana na mwonekano wake. Jamaa baada ya kulipa mahari ilifika siku ya kwenda Misri kuchukua jiko. 
        Alipofika akiwa na hamu ya kumuona mkewe, alionyeshwa dada mtu. Jamaa alipomuona, aliruka futi mia na kusema yule aliyeonyeshwa hakuwa yule aliyemuona na kumpenda. Kufupisha hadithi ndefu, jamaa alitaka arudishiwe fedha yake haraka. Wake walitia ngumu. Jambo hili lilifikishwa serikalini baada ya Saudia kutishia kuvunja uhusiano na Misri kama raia wake asingerudishiwa fedha yake. Je kama mwenye mapenzi haoni, si huyu Msaudia angebeba alichopewa?
        Mwisho, je mpaka hapa, bado unaamini mwenye mapenzi haoni au anaona sana tu? Kwa ufupi, mwenye mapenzi anaona sana tu. Siyo kila usemi unapaswa kuchukuliwa bila kufikiri hata kuhojiwa kama ilivyo dhana hii potofu kuwa mwenye mapenzi haoni wakati anaona sana.
Chanzo: Mwananchi leo.


Watufilisio wamefilisi, tumefilisika wamefilisika!

“Kufilisika kubaya. Jamanini kufilisika kubaya. Heri ufilisike mali kuliko akili. Heri ung’atwe na dogi kuliko kung’ata dogi.” Hayo ni maneno ya wimbo nilioutunga zamani nikakosa vifaa ukaishia kwenye makabrasha. Tuachane na mistari ya dhahabu ya zama za dhahabu. Naami mafyatu wote mnajua maana ya kufilisika. Niwasaidia wasiojua. Ni kuishiwa kitu chochote iwe akili au njuluku hata sera. Leo nitaongelea namna mafyatu wanavyofilisiwa na wanaowafilisi wanaopaswa kuwafilisi ili sote tufilisike na watufilisio wakiwamo ngoma droo ili kutenda haki.
Kunyaka mantiki ya somo, nitafudisha kupitia maswali kama ifuatavyo:
Mosi, je unapoteua cahawa kuwa mlongaji wa chata lako huligeuzi chata kuwa Chata cha Machawa (CcM)? Niliwaonya tusifanye mchezo na waharifu mafyatu wakadharau. Yako wapi sasa? Si tuliweka kikaragosi kikafyatufyatuka kikitaka kutubomoa eti kwa kujijenga baadaye eti kichukue ulaji wangu kama rahis wa mafyatu. Yametukuta mafyatu. Juzi katika kijiwe chetu cha uongozi si tukapendekeza fyatu mmoja aliyewahi kupatikana jinai ya kuteka na kuua mafyatu wenzake. Jamaa huyu chawa na changu kisiasa alijipenyeza, akapenya, na tukapenyeka tukamteua kuwa mlongaji wa Chama Cha Mafyatu (CCM). Naomba msichanganye CCM letu na nambari one ya twawala. Huko sipo. 
        Kufilisika nifundishao hauwahusu hao, kwani, walifilisika zamani machawa yalipowanyonya hadi wakaonda hata upstairs hadi wakawa wanalindwa na mbwa aliyekonda utadhani makondakonda sorry makandokando ya mikweche ya akina Daodi, Alubati, na Buushit.
Pili, unapofungulia mbwa, tena mwenye kichaa cha dog akawang’ate mafyatu usijue anaweza kukung’ata hata wewe, unategemea nini? Je hapa hujafilisika kisiasa? Je ulishajiuliza itakuwaje dogii akiamua kufilisika kama mwenyewe na kukung’ata wewe umfugaye? Hii huitwa mbwa kula mbwa kwani mbwai mbwai. Je unajua kuwa hizi ni baadhi ya dalili za kufilisika pale mwenye mbwa unapotegemea mbwa akulinde na kukuhakikishia usalama hata kukubalika kwako kwa mabavu wakati mbwa ni mbwa atabwabwaja na kufanya uumbwa? 
        Je unaambua nini kwenye ushauri huu wa bure toka kwa gwiji Dk, Profesa, Alhaji, Mhashamu, His Excellency, His Eminence, HH etc. Fyatu Mfyatuzi bin Mfyatuaji bin Mfyatukage wa Mfyatulizi mwana wa Mfyatukizi mjukuu wa Fyatuafyatua mwana wa Mfyatuizi? Naona yule anashangaa na kutikisa kichwa. Hujui naweza kutaja majina elfu na ushei ya kizazi changu kama kilivyoandikwa kwenye vitabu vitakatifu ingawa lilibadilishwa likawekwa la ka jamaa toka Mashariki ya nonihino? 
        Tatu, wewe unayeendelea kufanya makosa kuendekeza mbwa ukidhani atakuletea amani na usalama hata kwa kuwang’ata wachapakazi wako? Huku ndiko kufilisika kunakoongelewa hapa. 
        Nne, unapompa bangi mbwa mwenye kichaa tayari kung’ata wabaya au wapingaji wako  kwa sababu ana uzoefu wa kung’ata, kwanini nao wasijitoe akili wakamng’ata ikawa habari halafu wakakufyatua nawe na jibwa lako fyatu? Huku ndiko kufilisika kunakotufilisi kwa kufilisiwa na hawa waliofilisika wakatufilisi nasi.
        Tano, ili kuonyesha hawajafilisika, kwanini mafyatu wasinyongelee mbali hili jibwa ili wasing’atwe na kuendekeza madogiii? Huu si wakati wa madogii kutuchezea na kutung’ata kama kipindi kile walipokuwa wakibweka na kung’ata huku aliyewafuga akizidi kuchekelea na kuwanenepesha tena kwa njuluku na mamlaka ya mafyatu wafyatuliwa na kufilisiwa.
        Sita, mafyatu walipoona wanene tumempitisha huyu dogi, walisema wazi kuwa kipindi hiki ang’atwi fyatu hata mmoja. Badala yake mafyatu watang’ata hata mbwa mng’ataji. Hivi unapowaletea mafyatu mbwa, ina maana mafyatu wamekwisha au ni ile hali ya kuzidiwa na kunyonywa na chawa au kufilisika?
Saba, hivi inawezekanaje mbwa kuwazidi akili mafyatu tena wakubwa kiumri na kimaulaji? Je hapa mbwa na fyatu ni yupi au mmebalishana baada ya kufyatuka na kufilisika hadi mkaruhusu mbwa awafyatue na kuwafilisi? Je mfupa uliomshinda fisi nyinyi mtauweza?
Nane, inakuwaje mbwa anaendekezwa ili ang’ate mafyatu waliokwishafyatuka wakati tunao wanyama kibao na mabaki kibao kwa wale wanene wanaokula nyama? Kwanini wasimtupie mabaki ya milo yao badala ya kutaka awang’ate mafyatu wasio na noma na yeyote?
Baada ya kumaliza kuuliza maswali ambayo sitegemei kuletewa majibu ili yachapishwe kwa vile fyatu anayenihariri na kuruhusu hii kitu itoke hewani mafyatu wasome hataruhusu. Naye kuna siku nitamfyatua. We acha tu. Ukisoma hii, soma kimya asisikie akanifyatua nikashindwa kuwafyatua mafyatu wanaotufyatulia mimba itufyatue wasijue usawa huu, tutaifyatua kama mbaya, mbaya. Kwani mbwai mbwai kwa kimombo.
        Je tuko tayari kuendelea kung’atishwa majibwa tena yaliyochoka baada ya kujaribu hata kuwang’ata waliowakota majalalani? Inakuwaje mbwa koko anaendekezwa kiasi cha kuwazidi mafyatu wakati ananenepa kwa njuluku zao? Je kinachoendelea ni mbwa kugeuka chawa au chawa kula akanenepa na kugeuka mbwa?
Nimalizie. Kweli wametulifisi mali nao wakafilisika mawazo! Du! Kwani niko wapi?
Chanzo: Mwananchi Jumatano iliyopita.

Friday 12 July 2024

Mwapambana na ‘Machangu’ Wapi?

Kama mwanasharia na msomi, najua madhara ya kujadili jambo ambalo ni sub judice yaani lililoko mahakamani. Hivyo, nitaongelea kasheshe la baadhi ya mafyatu wanene kunyaka, kudhalilisha, na kuwapeleka kwa pilato dada wachovu eti kwa vile ni machangu. Pamoja na kutokuwa na ushahidi wala mashiko, niseme wazi. Uchangu si kosa kisheria bali aibu. Kama madada wanauza maungo yao, matatizo au mateso gani mafyatu tunaupata ikilinganishwa na wale wanaotuibia au kutuuza jumlajumla? Nani ananunua hizo laana zao? Naona yule anatikisa kichwa. Sitetei uchangudoa. Kinachogomba nikafyatuka kwa hasira na usongo ni kubaguana, kudanganyana, kudhalilishana na kuoneana.
Kamusi ya mafyatu inafasiri. Changudoa wako aina mbili, changu na changudoa (changu mwenye madoa) wapatikanao kwa wingi baharini kuliko wengine. Ni wa kike na wa kiume kama ngurumbili walio machangu. Tofauti, samaki si malaya wala wakware, wanyonyaji, wajinga, na wachafu kama chawa. Kosa lao ni upatikanaji wao kirahisi kama changu mafyatu.
Kwangu, changu ni fyatu yoyote asiyeaminika na mchumiatumbo ahiariye kutweza hata kuuza utu wake ilmradi apate tonge. Uchangu hauna unene, unono au unyonge. Hauna usomi wala ujinga. Ni fyatu aliyeishiwa akili hata ubunifu kiasi cha kujidhalilisha ili kujaza tumbo. Changu anaweza kuwa murume au jike. Anaweza kuuza mwili wake hata watu wake. Anaweza kuwa wa kijamii au hata wa kisiasa hata kiuchumi. Kimsingi, vyangu wote ni mafyatu wa kujidhalilisha kwa kushindwa kuheshimu utu wao. Machangu na machawa hawana tofauti. Tofauti iliyopo ni kwamba machawa ni machangu wa kisiasa na vyangu ni wa kijamii. Pia,wa kisiasa huwaonea wa kijamii.
Kwanini nafyatuka kwa hasira leo? Kama nilivyofyatua hapo juu, nilishika kichwa hadi tama, nilipoona mafyatu wazima, wanene, tena machawa, sorry, machangu, sorry, wenye ulaji wakiwakamata na kuwadhalilisha machangu wenzao wachovu. Wote, kifyatu, ni machangu. Tofauti yao ni waliposimama. Huwezi kumtofautisha changu wa kisiasa kama yule aliyetimika juzi na kwenda kuramba matapishi yake na hawa wakamatwao na kudhalilishwa. Nimesemaje? Nimesema Pita yule aliyemkana Tunda Lishe, sorry, Yesu? Message sent. Pita Msigwer ni shabiki wangu. Siwezi kumuita changu japo kwenye siasa kuna uchangu unaonekana kuhalalishwa na kuheshimika wakati ni uchangu kama uchangu wowote. Wala siwezi kusema ameramba, kubwia, na kupwakia marapishi yake. Si ndiye alisifika kuiponda Fisiemu akiwa Chakudema? Yethu na Maria. Nini hii la hawla wa la quwwata illa Billah.
Turejee dhana ya uchangu. Changu awezafanya chochote asijali madhara wala utu ilmradi apate atakalo. Anaweza kutoa mwili wake ale. Anaweza kuwaibia  wamtumiao, wakware au wanasiasa kama ambavyo mtashuhudia msimu huu wa usanii na uchawa kuelekea kwenye uchakachuaji. Mtawaona mafyatu wanene msiowezawadhania wakifanya uchangu kisiasa kwa vile ni halali kisheria. Kama nilivyofyatuka hapo juu, uchangu ni uchangu uwe wa kisiasa, kisanii, au kingoni. Changu avaaye vimini na avaaye suti au Tshirt za vyama wote vyangu. Changu atembea pekupeku na yule apandaye mashangingi na mashankupe wote vyangu. Nakazia. Changu ni changu awe mnene au mnyonge. Uchangu ni kama magonjwa mengine. Hayabagui. Tofauti ni kwamba uchangu ni ugonjwa wa kujitakia sawa na ujinga au imani kibubusa.
Uchangu ni kujiuza wewe na utu wako. Uchangu una sura nyingi tena mbaya. Unaweza kuunganisha uchangu na ukosefu wa maadili au upigaji madili. Wasomi wenzangu wanaoingia mikataba hatarishi kweli si machangu kimaadili na kiuchumi? Je hawa wanaotuibia kila uchao si machangu walio tayari hata kuumiza wenzao kama changu anavyoweza kumtilia mteja madawa ya usingizi kwenye kinywaji amfyatue uchache na rununu na kuishia? Hata wanaoahidi wasiyotekeleza na kupata kura ya kula ni machangu kisiasa. Wale wanaoruka viama kama daladala ni machangu tu. Heri uwe fyatu kuliko kuwa changu. Heri uwe fyatu kuliko kuwa chawa.
Natoa ujumbe mahsusi kwa wanaopoteza njuluku na muda vya mafyatu kuwinda na kukamata machangu. Waache uchangu. Kama watakamata basi wakamate machangu wote wa kimaadili na kisiasa. Uchangu ni uchangu. Unapaswa kushughulikiwa kwa namna na nguvu sawa bila kubagua wapi wa kukamata na wapi wa kukaribisha hata kuandalia halfa na kutangaza kwenye runinga wasijue nao ni uchangu tu. Nashauri, kuanzia leo, kuwe na usawa katika uchangu na ushughulikiwavyo. Mfano, penye machangu wa kike wapo wa kiume kwani wanafanya pekee. Dhana ya ukahaba vivyo hivyo. Kahaba ni wanawake na wanaume. Huko leo siendi japo ukahaba na uchangu ni mapacha. Tofauti ni matumizi yake hasa usawa huu wa kushitakiana hata kunyamazishana. 
Tumalizie kwa kuuliza. Mwapambana na changu wapi kulingana na mchanganuo huu? Woooi! Kumbe sijaenda baa sorry, ofisini, sorry, sokoni, sorry, Sinzer kuona vyangu!
Chanzo: Mwananchi Alhamis


Ndoa Zote Zina changamoto


Ndoa zote, sawa na taasisi yeyote ihusishayo binadamu zina chagamoto. Kinachotofautisha mafanikio na maanguko ya ndoa ni namna ya kuzikabili na kupambana na changamoto. Zinapotokea changamoto, jambo ambalo haliepukiki katika ndoa na maisha kwa ujumla, lazima wanandoa, kwanza wazikubali. Pili, wasisome na kuzielewa ili kuzitafutia majibu na ufumbuzi sahihi na kwa wakati. Tatu, wasione kama ni kitu kipya au cha ajabu. Hawa wote mnaona kama wamefanikiwa ima kitaaluma, vyeo, hata mali, bado ndoa zao zina changamoto sawa na binadamu wowote.
         Hivyo, changamoto katika ndoa ni jambo la kawaida na la lazima. Malkia wa Uingereza Elizabeth alisifika kwa ukubwa na hadhi ya mamlaka yake licha ya kuwa na changamoto katika ndoa yake. Changamoto ya kwanza ilitokana na mumewe Philip kupenda vimwana. Pili, changamoto nyingine ilitokana na kuvunjika kwa ndoa za watoto wake wote wa kike na kiume mbali na kashfa zilizowahusu. Cheo, mali au mamlaka ya mtu havifanyi awe na ndoa iliyofanikiwa. Hivyo, hata rais, profesa, milionea, wote wana changamoto katika ndoa zao. 
        Mfano, jarida maarufu la Marekani la the Washington Post (Desemba 25, 2017) https://www.washingtonpost.com/news/retropolis/wp/2017/12/16/fact-checking-the-crown-is-prince-phillip-a-total-jerk/ lilifichua kuwa Mwana wa mfalme. Philipo ambaye “hakuwa mwaminifu katika ndoa wa kiwango chake. Kwa miaka mingi, alikuwa akihusishwa na wanawake mbalimbali.” Je changamoto za ndoa ya Malkia zilijificha vipi?       
        Kwanza, malkia hakuwahi kulalamika au kutangaza mgogoro kwa kujua madhara yake kwake binafsi na cheo chake. Alitunza siri. Pili, waingereza wanasifika kwa unafiki na usiri wao. Hivyo, hawakutaka kumuaibisha kiongozi wao.
Mbali na Malkia wa Uingereza taifa linalojidai kufuata taratibu za kimila kwa kiwango cha juu, Ghengis Khan (1162–1227) anasifika kama mfalme aliyejenga himaya kubwa na yenye nguvu kuliko zote zilizowahi kutokea duniani. 
        Hata hivyo, alikuwa na udhaifu kingono. Mpaka anakufa, kuna taarifa kuwa alikuwa na watoto 44 aliowazaa na wanawake mbalimbali tena kwa kuwabaka. Kwa kuwazaa watoto wengi tena kwa njia hii, mke wake Khan aliyeitwa Hö’elün, unadhani alikuwa na changamoto kiasi gani hasa ikizingatiwa kuwa aliyekuwa akimkosea wakati wa uhai wake alikuwa na mamlaka kuliko mtu yeyote? Je ni wangapi wenye fedha, taaluma, na mamlaka wenye udhaifu huu? Ajabu, viumbe dhaifu na wadogo ukilinganisha nao kama vile njiwa, wanawazidi ufanisi katika hili. 
        Una habari kuna wanyama ambao wakioana ndo wamemaliza hadi watenganishwe na kifo wakiwa na mapenzi na uaminifu wao? Mjusi wapatikanao huko Australia waitwao shingleback au bobtail or Australia sleepy Lizards wanasifika kwa kuwa waaminifu kiasi cha kuishi na kufa bila kuchepuka. Basi, tuwapeni maua yao. Mbali na mijusi hao, kuna samaki waitwao diploozoom paradixum ambao nao wanaishi pamoja hadi kufa kwa sababu wawili wanapoamua kuwa kitu kimoja hubaki hivyo hadi kifo kiwatenganishe. Wengine ni tumbusi weusi waitwao kwa kimombo coragypas atratus. Hawa jamaa ni po asana. Katika kuzaa na kulea husaidiana kwa usawa tofauti na wanadamu na viumbe wengine waliolewa mfumo nyonyaji dume.
        Kwa ufupi, uzinzi na ukosefu wa uaminifu katika ufalme wa Uingereza, sawa na wengine waliofanikiwa kifedha, kimamlaka, na hata kitaaluma ni kitu cha kawaida. Unaweza kukuta tajiri mkubwa akiyumba katika ndoa huku maskini hata walemavu wakitanua na kuifaidi ndoa. Ndoa haina daktari, rais, profesa wala mwanasayansi. Ni taasisi ambayo imewakwaza wengi na kuwaenzi wachache. Helen Sirleaf na Mary Banda marais wa zamani wa Liberia na Malawi mtawalia, pamoja na urais, mafanikio na ukubwa wa nyadhifa zao waliachika. Pamoja na kuwa kiongozi mwenye nguvu sana duniani na anayeogopewa, Rais wa Urusi, Vladmir Putin alishindwa na ndoa kiasi cha kuishi kiseja bila kuta. 
        Kadhalika Rais wa zamani wa Kenya Daniel arap Moi, aliishi bila mke kwa muda wote aliokuwa madarakani. Hapa hatujagusia watu maarufu na wenye ushawishi sana duniani waliooa na kuacha baada ya taasisi hii kuwapiga chenga tokana na sababu mbalimbali zilizo wazi na za siri. Ngugi wa Thiong’o (Kenya) na Wole Soyinka (Nigeria), pamoja na umahiri wao katika liwaya na uandishi walitaliki. waliachika. Wole Soyinka (Nigeria), watangazaji wa kimataifa kama vile Larry King (CNN), Dana Bash, Christiane Amanpour (CNN), matajiri kama vile Bill Gates, Elon Musk na wengine walivyoshindwa katika ndoa zao pamoja na kufanikiwa kifedha na kiuchumi. 
        Hili linatufundisha kuwa ndoa ni taasisi ya ubinadamu inayopaswa kuukubali na kuushughulikia ubinadamu na udhaifu wake. Hakuna wanandoa ambao ni malaika. Wapo hata walioogopa kuoa kama Plato, baba wa falsafa wa Kigiriki, Ludwig Beethoven, bingwa wa kupiga piano, Nicola Tesla mvumbiuzi wa kimarekani na William James Sadis aliyeaminika kuwa na kiwango kikubwa kiakili, pamoja na umahiri wao, waliishi na kufa wasera. Ndoa haina tajiri wala maskini, ukubwa wala udogo, uzuri au ubaya. Ndoa siku zote ni ndoa na lazima itakuwa na changamoto hata iwe imefanikiwa kiasi gani. Bill Gates, Elon Musk, Jeff Bizos, Reginald Mengi, pamoja na ukwasi wao, walishindwa hadi kutalakiana na wenzi wao.
          Tumalizie kusema kuwa kila ndoa ina changamoto yake iwe ya mkubwa au mdogo. Muhimu ni kupambana nazo kiakili na kwa usiri ili kulinda ndoa husika.
Chanzo: Mwananchi.

Wednesday 3 July 2024

Mkimbinafsisha Bi Mkubwa Wangu Naua Mjue


Mtukufu Dk. Rahis, msikivu, mwenye maono, ndoto, uthubutu, ukimya, nk., naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu, rahis, du! A’udhu billahi min ash-shaytaan-ir-rajeem. Nimemsahau Mtume! Naona yule anshangaa. Kwani nazusha? Wanagapi, sijui chawa, sijui kunguni, wakianza kuchonga wanafanyahivyo kwa maangamizi yao na mafyatu wao?
Nasikia kila mara rahis akisifiwa kuwa na ‘maono’ tena yasiyooneka. Kupitia maono, amegawa, sorry, binafsisha bahari, bandari, barabara, mbuga za waanimo, n.k. kama ni kweli. Hii inantisha kwelikweli. Naomba leo nifyatue kitu. Hivi huyu Bi Mkubwa ni Mungu, muungu, malaika, hata ntume? Hakosei? Je hizi sifa za kweli au kupakana mafuta kwa ngongo wa chupa au uchawa na ukunguni wa kutumia matumbo kufikiri badala ya vichwa ili kujaza matumbo?
Nasikia Bi Mkubwa ametenda ‘maajabu.’ Je ni maajabu kweli katenda au ni ajabu kusema katenda? Kamwaga njuluku. Mafyatu wanazipata? Kamwaga kiasi gani na kwa yupi?  Nasikia. Kamwaga pikipiki. Tunahoji ni za nini na hiyo njuluku ameitoa wapi au kuipataje na anategemea kupata nini na kwanini sasa tunapoelekea kwenye uchakachuaji wa uchaguzi? Ananunua nini? Ajabu, wakati rahis akitoa pikipiki kwa kila nkoa bwerere, akina maza wenzake wajawazito wanajifungulia nje ya zahanati! Mwe! Kwani hajui adha ya ujauzito na machungu ya kujifungua? Hayo tuyaache.
         Je rahis ni tajiri kiasi gani na nini chanzo cha ukwasi, ‘huruma na upendo’ hivi, ni vya nini, na anategemea kupata nini? Mafyatu tukienda hospitali tunaandikiwa dawa tukanunue! Maji ya mgao! Je hizi njuluku za pikipiki zingesaidia wajawazito, mafyatu, hata upatikanaji wa maji kiasi gani? Je hii njuluku ingeondosha michango ya hovyo na tozos kiasi gani? Je mikoa yetu inahitaji pikipiki wakati pesa inayopata tokana na bajeti ni kiduchu? Kwanini hatangazwi mmojawapo wa mabilionea wa kaya? Inakuwaje anakwenda ughaibuni kukopa na kubomu wakati ana ukwasi kiasi hichi? Kaya yake inashindwa hata kuendesha mangwalangwala ya mwendo kinyonga, sorry, kasi?
Tunapaswa kuwa wakweli. Pia, naye awe mkweli kwake na kwa mafyatu. Hizi pikipiki ni za nini kama hakuna namna ya kuhongana, sorry, kuchanganyana, kuelekea kwenye uchakachuaji mwakani? Kwanini sasa na si jana wala juzi? Je huyu bilionea wa sirini analipwa nshahara kiasi gani? Tukiuliza haya, mengine, na mengineyo tunakosea?
Turejee kwenye uwekezaji ambao wapingaji wanauita uchukuaji kama siyo uchakachuaji na uhujumu uchumi uliohalalishiwa na kufanywa na wanene tena kwa mlango wa nyuma. Bandari, tumewekeza. Juzi tuliona magawio la madafu 153.9 bilioni sawa na dolari za Kijoji Kichaka milioni 80! Kiduchu hichi kwa mwaka! Je waliingiza kiasi gani tujue kama kweli ni gawio au zenguo? Tunapaswa tujiulize na kuwauliza wamepata nini na wanatupa nini na nini tulipaswa kupata kisheria na kimakadirio. 
        Tusifanye magawio kuwa hisani bila kujiridhisha kuwa tunachopata ndiyo sitahili yetu badala ya kujiruhusu kupigwa na kufyatuliwa kijiiinga tu.  Fine. Je kwa namna bandari inavyotema njuluku kweli tulichopewa ni stahiki au chenga la mato? Mwaka 2016, bandari iliripoti mapato ya shilingi trilioni 13.37 (Mwananchi, Julai 6, 2016). Je kwa gawio hili walipata kiasi gani? Je walifikia, kutofikia, au kuvuka malengo? Je hiki ndicho tulichoahidiwa na kutegemea baada ya kugawiwa, sorry, kuuzwa, sorry, kubinafsishwa bandari kwa watasha wa Do Buy?
        Barabara tunawekeza baada ya kuunguza njuluku ndefu za mafyatu kuzitengeneza ili kuwanufaisha wachache? Nafyatua maswali yote haya na mengine kuepuka kuuziwa goat kwenye gunia tunajiona.
        Bahari, tumebinafsisha. Natamani na visiwa vibinafsishwe uone wazenj watakavyocharuka na kudai uhuru. Natamani hata makaburi yabinafsishwe. Bado milima na mito. Tukimaliza yote haya, tunabinafisha na machawa. Sijui nani atakuwa tayari kuwanunua wamkondeshe kama mafyatu. Tukimaliza vyote kweli kesho hamtabinafsisha hata hewa? Je Bi. Wakubwa zetu watanusurika? Wallahi, ikifikia kubinafisishana na mkamgusa Bi. Mkubwa wangu––––tate nane tate nane––––nakufa na fyatu. Hata hivo, kabla ya kumfyatua fyatu, nitamwambie Bwa. Hafith amwambie Bi Nkubwa wake ajibinafsishe kwa wamanga aone inavyouma na kuumiza. Nimesemeje? We koma!
Najua Ngolongolo akina Yero weshabinafsishwa na kuhongwa, sorry, kujengewa vibanda kule Msomea. Ukisikia maono ya maza na wamanga ndiyo haya. Si juzi niliowaona wakiwa wameishakubuhu kukata vikalio utadhani walizaliwa Tangamano. Huo nao uwekezaji au siyo. Soon, nitawaona wamanga wamepiga migolole ya kiyero wakipambana na lion. Nao ni uwekezaji au siyo.
Nimalizie. Hata kama mnatuaminisha hata kutufyatua kuwa uwekezaji ni muhimu kama kweli ni uwekezaji kama siyo uchukuaji, basi wekezeni kwa busara, tushirikishe, msituhamishe na kutuchuuza kama ilivyo sasa. Pia, wajibikeni na kueleza mnavyotumia njuluku zetu na zenu kama mnazo kama kwenye skandali ya pikipiki. Hivi Bi Nkubwa wangu bado yu salama kwa sera hizi? Hivi niko wapi? Kama naota!
Chanzo: Mwananchi leo.

Wednesday 26 June 2024

Maza Fyatua Bashee Baada Kumfyatua Nawander


Juzi mafyatu tulisuuzika roho baada ya kuvuja tuhuma za doktari Yah-yah Nawander kumbaki mwanachuo huko Shimiyu. I just wonder about Nawander. Sitafyatuka mengi. Uchunguzi haujakamilika. Sijui kama kesi iko kwa pilato au la. Tulisuuzika kufyatuliwa wanene wasiofyatuliwa lau kwa kutemeshwa ulaji bila kuwafunga. Doktari maza alimfyatua Nawander baada ya kutuhumiwa kufyatua Embedodo hadi maganda na kokwa tena kulikooza. Sijui Embedodo lilingiaje mchumani, kama hakukuwa na makubaliano? Je ni kweli jamaa alikula vyote hata mbegu iliyooza? Yaani mnofu wa Embedodo umeisha hadi fyatu mzima–––tena munene na doktari kama wa kweli siyo wa kugushi au honoris cause––––unahangaishwa na kokwa chafu? Huyu udoktari ni wa nini na aliupataje au ni ule wa akina Philo na Sofia? Je hii ni kweli au kuna namna? Je usingefanyika usodomu––––kama kweli ulifanyika––––Embedodo lililoanguka kwenye mchuma wa Nawander––––lingelalamika? Ajabu, nasikia mnaifungia twinter kwa kuhamasisha usodomu wakati wanene ndo wanaoufanya–––kama kweli Nawander aliufanya. Je hawa wanajuana na kukomoana nasi tunafyatuliwa changa la mato au ni siasa kama za kina Sir Baya? Mbona sielewi. Hayo tuyaache.
            Leo, kama kawaida ya mshauri wa maza asiyelipwa chochote isipokuwa kusukumwa na ufyatu na uzalendo, natoa ushauri kuntu tena bwerereee. Ushauri wenyewe ni huu. Fyatulia mbali Husaini Basheee aliyetuhumiwa na Mheshimiwa Luhager Mpiner tena kwa ushahidi kuntu unaoonyesha wazi jamaa alitengeza uhaba hadi sugar ikageuka shubiri! Mwe! Mmejua kutufyatua bila kujali tunaweza kufyatuka na kuwafyatua. Kabla ya Mpiner kumwaga mtama, nilikuwa nimehadaika nikatokea kumuona Bashee mzalendo kumbe wapi? Alivyokuwa akifyatuka na ‘kulaani’ uzembe utadhani alimaanisha! Kumbe sanaa. Sipendi kufyatua maneno mazito ila naweza kusema hii ni nifaki tosha. Sikutegemea fyatu aliyekuwa anafyatua mapofu 'kuwatetea' wafa kwa ngwamba angekuwa ndiye anayewaumiza mafyatu wa kaya yote.
            Doktari Mazeri, naomba nikushauri kumfyatua Basheee na akina Mwiguuu Nchember, Jan Makamber, na Riz One niliowataja siku zilizopita kwa sababu zifuatazo:
            Kwa ushahidi wa Mpiner, kuna kila dalili za upigaji njuluku ndefu kupitia kuongeza cha juu kwenye sugar, kutengeneza faida na rushwa kubwa kwa wanene na walanguzi wa sugar vilivyofanywa na Bashee ukiachia mbali Nchember. Alipojipiga kifua akitapika urongo mjengoni kuwa si waziri boya kumbe boyo! Je kuna mawaziri maboya? Kumbe na mtufuku rahis  anaweza kuteua maboya kweli? Kuna uboya kuliko ufisadi waziwazi tena wa kutumwa na akina Mood Doweji? Waziri anapogeuka broker, we acha tu apaswa kuwa mikononi mwa Takokuru kama siyo kunonihino kwenye debe lupango aungane na Nawander.
            Pili, kudanganya kaya na mjengo aliojifanya kuuita mtukufu wakati anaufanyia utukutu mbali na kutoa vibali vya kuagiza sugar nyingi kupita naksi iliyokuwapo kayani ni kosa la uhujumu wa uchumi. Ukimsikia jamaa anavyomtaja Sir God, utadhani anamwamini kumbe kamba! Kaya hii kweli ya sanii iko sema Kanjicholi. Haiwezekani umfyatue Nawander kwa masuala binafsi ushindwe Bashee ambaye skandali yake imeumiza umma wa mafyatu wote.
            Tatu, kutoa vibali kwa makampuni feki mengine yakiwa ni ya mamantilie ukiachia mbali la yule bilionea fisadi nauchwara wa kaya. Je haya makampuni siyo yake au mafyatu wake wapigaji njuluku ndefu ya makapuku wanaofyatuliwa na umaskini tena wa kutengezwa na akina Bashee, Nchember, na wenzake? Je huyu jamaa na wenzake wameishapiga njuluku kiasi gani? Je wako wangapi kayani? Je haya huyajui? Kama huyajui, ni kwanini? Kama unayajua, kwanini hufyatui? Je ni kweli unafaidika na akina Bwashee kama mafyatu wapingaji wanavyodai? Je kwenye bidhaa muhimu kama wese zinapigwa kiasi gani? Je Nchember na wenzake wameishapiga ngapi? Bandarini nako je? Vipi jamaa wa mbuga za waanimo na utalii? Madini nako vipi? Uhamiaji wajua?
            Nne, kusamehe kodi nusu trilioni tena kwa kaya kapuku. Ajabu, wewe maza unatembeza bakuli kukopa na kubomu hadi wengine wanakuita Vasco da Gama kama yule wa Musoga. Kuna haja gani kudhalilika hivi wakati uchumi tunao ila tunaukalia huku wengine wakiugawa kama huyu Bashee. Kwanza, kweli huyu ni mdanganyika na mzalendo kweli au ana uraia pacha? Je ni wale aliowahi kudai munene mmoja wa geshi kuwa kuna wageni wamepewa nyadhifa kuu kwenye ulaji wa juu? Pili, je huyu jamaa hawezi kuwa anauza hata siri za kaya na sirkal kwa maadui zetu wakiwamo magaidi kama vile al Shabubu?
            Tano, usipomfyatua, wapingaji wanaaamini kutakuwa na namna unavyofaidika. Wanataja zile pikipiki zilizoandikwa SSH, yaani Sasa Shida Hiyo au Seemingly Self-inflicted Hazard zilizosemekana kugawiwa bure nkoani. Wanadai hizi ndinga zimekula zaidi ya bilioni 50. Je hii njuluku ilipatikanaje? Zitolewe bure kwani duniani bado kuna cha bure? Kwanini sasa kuelekea kwenye uchakachuaji, sorry, uchafuzi, sorry, uchaguzi? Je nani mwenye hizi ndinga ambaye anaonekana kuwa mkwasi wa kutisha? Pamoja na Luhager kufyatuka kutuhabarisha na kutufumbua mato eti madame Spiker aka Spooker anamtunishia misuli kwa kumpeleka kwenye kamati ya madili wafanyie dili tuhuma zake! Kaya hii kwa maajabu, we acha tu.
            Kwa vile nawahi kanywaji, leo nakomea hapa. Hivi nimesema Bashee apandishwe cheo?
Chanzo: Mwananchi leo.

Wednesday 19 June 2024

Hii Kaya Sasa ya Chawa na Sanii

 

Siku hiji kaya yetu nageuka kaya ya sanii. Kila kitu ni sanii. Rahis nafanya sanii.  Wajiri nafanya sanii. Narudia neno nasema bungeni iliyopita. Natuma kampuni hewa. Nasamehe kodi. Kodi naingia fukoni yake. Sirkal nafanya sanii. Nakwenda bungeni. Nalialia na chovu naona yeye zalendo. Kama Pina nachambua yeye, naona fisadi kuba. Napoteza kodi. Nakwenda omba ghaibuni kama ile Tonya. Iko uliza wajiri ya kilimo na juluku na samaha ya kodi kampuni ya fukoni? Kama napigia yeye kelele, nageuka chura. Kama veve napiga kelele kama pinjani, chura nakaa kimya. Kama nazidi kelele. Yeye naonya hapana kanyaga guru vake nauza. Sasa iko ogopa sana.
         Kama rahis nageuka nyoka hapana umma umma sana? Kama nageuka chatu hapana kula vote na yote dugu yangu? Sasa mimi anza ogopa sana hii sanii. Bila fanya sanii mambo yako yote naharibika kabisa. Vatu nafanya sanii ili naishi. Nageuka chawa. Nyingine nageuka kunguni. Nyingine nakuwa fyatu nafyatua juluku ya chovu na sikini. Kila moja iko sanii. Kama hapana jua sanii, napotea na kuteseka vakati vote dugu yangu.
Juzi nakwenda Bombei kuona bibi na toto. Naacha yeye na toto moja nakuta toto tano na yote nakuwa sanii. Nakwenda sule nataka Ipad. Narudi Tanjania nakuta kila kitu sanii kila Swahili hata Hindi sanii. Sirkal nafanya sanii ya kupiga juluku. Naanzisha tozo na chango mpaka tumboni nauma. Kuku nakuwa sanii nataga yai ya rangi. Bila kuwa sanii, maisha iko tabu sana. Siku nafatuka ile mendazake Kufuli mimi dhani kaya kuwa ya Samier siyo ya sanii. Sasa kila kitu naona sanii. Profesa sasa nayo nageuka sanii ya siasa kabisa.  Iko mingi naingia siasa. Vatu nafanya sanii kwelikweli. Nafanya sanii ya nguvu sana dugu yangu. Kama nakopa juluku, nakausa damu. Hii naona penzi ya sanii.
         Rahis naye nakuwa sanii kubwa. Napenda sana sanii na sanii napenda sana yeye. Juzi nasafiri Korea na sanii mingi kwa juluku ya sikini ya kaya. Na vana kaya nafanya chura. Hapana lalamika kwanini aache vakulima. Toto sanii. Sasa naimba stari ya rap. Hapana soma suleni. Nataka tengeneja juluku kuba harakaharaka kama Kanjibhai. Vatu kuba sasa sanii nasifia sifia Samier. Kama nachukia au nakataa sifia yeye, nakufa sikini dugu yagu. Kama veve iko sanii, nasahau Mungu, Nasifia vatu nene. Vyuo sanii. Sasa natoa honoris causae kama jugu. Sasa kaya nakuwa ya doktori sanii mingi sana. Sanii nayo nakuwa sanii ya siasa. Nagombea bungeni. Natumia vana siasa fanya sanii kwa samier. Hii kaya basi iite saniiland. Hindi nakuwa sanii. Kama naongea swahili, nabukanya. Kama nakamatwa na data, naongea swahili kuliko Zaramo. Chukuaji nayo sanii. Sasa naita wekejaji. Ile miji kubakuba sana hesimiwa. Nafanya sanii. Napata tumboni kuba na kila kitu kubakuba. Nakuwa na nyumbani dogo mingi. Nyingine nabaka toto ya chuo. Yote hii sanii ya siasa.
            Sanii sasa mali kuliko dukani. Kama nataka juluku kuba, lazima iwe sanii ya siasa. Naendesa dukani na kugombea bungeni na kupiga juluku. Sirkal kila maka nanunua sangingi. Naharibu. Nauza mnada kwa bei ya sanii na sanii kuba napata deals. Kama veve sikini nafanya kazini na nastaafu, napewa kinua gongo ya sanii. Napewa kidogo. Kikuba naweka sirkal. Natumia kama hapana akili njuri. Chovu nalalamika. Veve nanyamaza kama chura. Sirkal nafanya sanii. Nasema navekea veve juluku yako! Kama nakupa yote nakwenda lewa pombe na kufa haraka. Je kama nanyima veve juluku yako, hapana tatizo fyatua veve na kufa haraka jamani? Hii yote sanii.
         Pinjani napiga kelele sana kama kisimani ya maji. Ile chura kuba naziba sikio. Napiga juluku toto, mama, na rafiki. Vote napiga juluku. Sikini sanii nalala sikini naamka tajir.  Sasa na pinjani nayo kama nageuka chura, nani tapiga kelele ile chura kuba na nyingine napiga juluku? Kama yeye chura, basi pinjani chemsa maji naunguza chura. Kama nafanya jusi, pinjani bana lango.
            Ile vatu ya dini nayo siku hizi sanii. Naimba nyimbo ya siasa sanii. Nasifia ile chura kuba napata juluku. Nyingine nafanya sanii. Nadanganya jinga nafanya ujiza. Napata juluku kuba. Naendesa gari kuba. Nalala kwa nyumbani kuba. Ile sikini nafanyia sanii naambia omba Mungu. Nafanya sanii. Naita ujiza. Kanji iko kataa ujiza. Vajinga ndiyo valivao dugu yangu. Chunga sana sanii ya dini na sanii ya siasa. Siku hiji sanii ya dini na sanii ya siasa nalala tanda moja. Kama nataka kuwa sanii, hapana chukia witu baya. Veve sifia. Kama napigwa kofi cheka. Kama juluku yako napigwa, sema mama namwaga juluku.  
            Sanii nyingine, sirkal nakopa juluku. Natumia wibaya. Hapana taka swali howo howo. Nafanya kataba hatari. Hapana taka swali. Nauza fyatu. Hapana taka swali. Nafanya kaya kama dukani yao, Chovu na fyatu natazama tu kama chura! Chama sasa nakula kitu yote. Kama nauliza nini bana? Nasema yeye chama twavala. Natavala na kula. Hiyo ndiyo kazi ya chama tavala. Kama napinga veve, iko adui ya kaya.
            Kama nataka kwenda bungeni, lazima sifia. Kama nanyimwa radi ya jimboni yako, napiga sarakasi jengoni. Kama nabana vaziri swali gumu, chama naita veve. Kama nabisa, nenda uliza ile Lwaga Mpini. Kama naleta domo kuba, ile chura nene nasema veve itengwe. Tena iko ongeza kuwa veve laani. Nakumbuka ile Nipe Pepe Nnaiye nasema jengoni? Nasema pinjani yote laana.
Du! Kumbe naota niko Bombei na nimegeuka Napharata karanāra bin Jātivādī bin Cōra! Bhagavāna manē madada karē.
Chanzo: Mwananchi leo.

Monday 17 June 2024

Misingi na Nguzo za Ndoa (2)

Leo tunaendelea tulipoishia kuhusiana na miiko na nguzo za ndoa. Karibuni tuendelee.
Maadili
Taaluma na taasisi yoyote lazima iwe na maadili ya kufanya ifanikiwe na kuheshimika. Ndoa kadhalika, lazima iwe na maadili vinginevyo haitafanikiwa au kuimarika. Kama ilivyo masharti ya udereva au uongozi, maadili ni nyenzo zinawezesha wanandoa kujifunza nini wafanye au wasifanye na kwanini. Maadili, licha ya kuwaongoza wahusika, huwapa fursa kuona madhara yanayoweza kuwapata wanapokiuka maadili ya ndoa kama tulivyogusia hapo juu juu ya changamoto na hatari za ndoa. Kuna usemi wa kimombo unaofasiri maadili kama kujua tofauti kati ya ulicho nacho haki kutenda na kilicho sahihi kutenda (ethics is knowing the difference between what you have a right to do and what is right to do). Pia, kuna busara nyingine inasema kuwa mtu asiye na maadili ni sawa nyamamwitu aliyeachiwa kwenye dunia hii (a person without ethics is a wild beast loosed upon this world).
            Tusisitize. Kama zilivyo nguzo nyingine, maadili ni muhimu au tuseme ni mojawapo ya matofali yanayojenga ndoa. Lazima wanandoa wayazingatie.
Miiko
Pamoja na mambo mengine, taasisi yoyote, ili idumu, ifanikiwe, na kuwa salama, lazima iwe na miiko yake ambao inaoingoza katika kuendesha mambo yake. Katika ndoa, miiko ni mojawapo ya nguzo zake. Kuna vitu mfano, hamuwezi kuitana au kufanyiana. Kuna kisa cha wanandoa katika nchi moja ya Amerika ya Kusini. Katika kisa hiki, mwanandoa mmoja alichukia hadi kufikia kutishia kuvunja ndoa kwa sababu mwenzie alijamba wakiwa kitandani wanaongea kabla ya kulala. Si kwamba hawa wanandoa walikuwa hawafanyi hivyo. Kilichogomba ni kanuni. Kila aliyetoa upepo alimtaka radhi mwenzake vinginevyo awe amelala fofo hajitambui. Hivyo, mwanandoa alioachia hewa na kushindwa kuomba msamaha, alikuwa amevunja kanuni moja kubwa. Jambo hili ni dogo, kama tulivyoonyesha hapo juu ila laweza kuwa na madhara makubwa kimahusiano kwani, lilitaka kuzaa makubwa kiasi cha kutishia ndoa ya wahusika. Hivyo, kanuni mlizojiwekea lazima mzifuate hata kama ni ndogo kiasi gani.
Upekee
Kama tulivyo viumbe. Kwa mujibu wa sayansi ya vinasaba (DNA science) kila mmoja wetu ana DNA tofauti na mwenzake na wenzake. Na ndoa kadhalika. Zina DNA za kipekee. Ndiyo maana hupaswi kufunga au kuendesha ndoa yako kwa kuiga ndoa nyingine. Hivyo, jambo mojawapo la muhimu ni kutambua na kuipa upekee ndoa yenu ili iweze kufanikiwa na kupambana na changamoto zake vilivyo bila ya kuigiza au kukopa japo si vibaya kujifunza kwa wengine wenye ndoa kongwe na zilizofanikiwa kuliko zenu. Hata hivyo, lazima muangalie mazingira na sababu za kufanya hivyo.
Siri na usiri
Japo siri na usiri (secret and secrecy) vinahusiana, havina maana moja. Ni rahisi kutengeneza siri japo ni vigumu kutunza siri kama hakuna nguvu ya ziada au sababu zinazokuzuia kufanya hivyo. Katika ndoa, siri na usiri vinakwenda bega kwa bega. Ili siri iwe salama, lazima kuwae na usiri. Na ili usiri uwepo lazima kuwa na siri ya kutunzwa. Ukiachana na misingi na siri za mafanikio ya ndoa hapo juu, msingi mwingine ni siri. Ndoa ina siri zake. Wenye ndoa pekee ndiyo waumbaji, watunzaji, hata wavujishaji siri. Tumegusia umuhimu wa kulishwa kiapo kabla au wakati wa kufunga ndoa. Mbali na kuwa ishara ya kukabidhiwa majukumu, kutoka hatua moja hasa ya chini kwenda ya juu, mantiki ya kiapo ni kutunza siri. Unadhani kinachofanya askari wawe watii wasitumie vibaya nguvu na silaha zao ni nini kama siyo kiapo na usiri wa kazi yao? Bila siri, hakuna taasisi. Ndoa siyo kama chumvi muazimane na majirani na marafiki.
        Kama ilivyo kwenye siri ya mtungi, muachie kata pekee ajue siri zake. Kama mume au mkeo ni tajiri au kafanikiwa katika jambo, huna haja ya kugeuza mafanikio yenu kuwa matangazo ya biashara. Wakati mwingine mafanikio yanaweza kuwa chanzo cha maanguko kama hayatahifadhiwa na kutumika vizuri. Kuna methali ya kiingereza isemayo kuwa thamani ya siri hutugemea dhidi ya watu unaopaswa kuitunza au kuiepusha (secret's worth depends on the people from whom it must be kept). Methali nyingine inasema kuwa kutunza siri yako ni busara lakini ukitegemea wengine waituinze ni upumbavu (to keep your own secrets is wisdom but to expect others to keep them is folly).
Wivu
Kama ilivyo petroli kwenye gari au mashini yoyote, ndoa bila wivu wa pande zote si ndoa bali maigizo. Kama tulivyodokeza hapo juu, binadamu ni kiumbe mwenye wivu wa kuzaliwa nao. Je itakuwaje utakapogundua kuwa mwenzio hana wivu nawe? Je ni kweli hana wivu au anao kwa mtu mwingine mbali nawe? Kwa wanaotoka Tanga wanajua. Kuna usemi kuwa siyo wivu tu bali hata limbwata kwa mume au mkeo linafaa ili muwe pamoja. Haya ndiyo mapenzi.  Mithali 6:34 inasema wazi kuwa wivu humfanya mtu achukie kiasi cha kutoonyesha huruma siku kulipiza kisasi. Japo si wote wanaoamini katika biblia, kuna ukweli katika aya hizi ambazo wakristo na waislamu huziamini. Tunaomba kutofautisha wivu huu na husda ambayo ni dhambi kama Muslim (V. 2) anavyoonya kuwa msichukie, kuwa na husda au kugeuka.
Chanzo: Mwananchi jana.

Wednesday 12 June 2024

Waziro wako wa fedheha aka njuluku anatuhujumu na kukuhujumu


Mtukufu Dk., Dk., Dk, Dk. Dk.Rahis.  Naambwa unazo PhD tano si haba.
Sina tabia ya kupongeza. Hivyo, kwa heshima na taadhima, nakuomba usishangae. Mie ni fyatu. Si msifiaji wala chawa. Hivyo, sianzi kwa mashairi, mapambio, ngojera wala kamba. Huwa namsifu Sir God pekee na siyo masanamu ya kuchongwa na machawa ili wapate kujaza mitumbo. Si kazi yangu, maana mie siyo chawa wala kunguni wa kujipachika uchawa wala mwenye kupwaya kamaadili na kitaaluma. Ni msomi kuliko Mwambukuzi. Ni fyatu kuliko Tunda Lishe na Pita Msingua mafyatu wanaosifika kayani. 
        Leo, nakuletea skandali ya mwishiwa Madilu Lameki Nchembuz ambaye hupenda kuitwa doktari. Nadhani ishainyaka. Niseme wazi. Anakuaibisha,  kukuhujumu, kutuhujumu, kukuchonganisha, na kukuchongea kwa mafyatu wanaoshangaa kwanini kumwacha aendelee kutia aibu na hasara kaya na hata mjengo wetu mtukutu, sorry, mtukufu. Hafai kwa lolote so to speak Unadhani mwendaze aliyemfyatua aliyemuumba na kumfyatua alikosea? Juzi iliibuliwa skandali mjengoni na mheshimiwa Joji Mwanisongo Lee ikimkariri Nchembuz akijisifu uzwazwa na uzembe. Hata kama muda umekwisha kuelekea uchakachuaji, Mwanisongo Lee ni jembe. Ningekuwa wewe, ningemteua awe waziri wa njuluku maana ana uchungu na njuluku na wakulima wetu.
         Mwanisongo Lee popote ulipo, nakupa kongole fyatu wangu. Unastahiki, kwani hukuogopa mvua wala jua. Ulicheza clip mjengoni ambapo Nchembuz anajisifu kuwasikinisha mafyatu na kuwatajirishi wakwepa kodi. Hakuna kilichoniudhi hadi nikalala njaa zaidi ya kupata kanywaji kuondoa hasira kama madame Kipaza sauti aka Spiker kushindwa kuunda kamati kumchunguza hata kumuondoa madarakani Nchembuz mbali na kuamuru takokuru imfyatue. Kama mjengo kweli ungekuwa wa mafyatu au kuwawakilisha hasa ikizingatia ndiyo wanaohujumiwa kwenye skandalii hii, ingeletewa hoja kumchunguza Nchembuz liwe somo kwa wengine. Ajabu ya maajabu, hakuna aliyeona skandali hii kama tishio kwa maisha ya kaya hasa kiuchumi. Tatizo nini?
        Ajabu!!!! Nchembuzi alipotakiwa kujieleza, siyo kujitetea, alipiga siasa na skandali ikafia hapo! Je zipo skandali nyengine kama hata kubwa kuliko hizi ngapi? Je kaya imeishapoteza njuluku kiasi gani? Ni mafyatu wangapi wapiga jembe waliokwishasikinishwa? Kama ningekuwapo mjengoni, ningekamata shilingi na kuhakikisha huyu fyatu anafyatuliwa tena bila maji. Je mtukufu rahis, umeridhia mchezo huu mchafu? Fyatua bila kuangalia nonihino usoni. 
        Ushahidi upo tosha na wazi. Unamuacha ili iweje na afanye nini zaidi ya kuendelea kuboronga na kuvurunda? Je unapanga kufyatua lini japo huwa hufyatui itakiwavyo nikikumbusha skandali za akina Riz One na Janwari Joseph Marope nilizokuletea ukaminya? Je kwenye uchakachuaji ujao, utatujibu nini tutakapomkumbusha skandali hizi na nyengine kama vile Deep Weed, Ngorongoro etc.? Je mhujumu uchumi huyu analipwa mamilioni, kupewa hekalu, shangingi, na wese bure kwa kazi gani iwapo amejifunga mwenyewe kuwa anahujumu kaya? Mafyatu twataka jambo moja tu, kuwajibishwa Nchembuz as soon as possible.
        Mafyatu, hadi leo, hatujaelewa uzwazwa na majisifu hata mantiki ya kunyamaziwa kana kwamba alichofanya Nchembuz ni haki. Je ni ile hali ya maadili kugeuzwa madili na baadhi ya mafyatu kujigeuza au kugeuzwa machawa wengine miungu? Je wanaachwa kwa vile wana sifa kuu za kujisifu na kukusifia kuwa umefanya mambo makubwa kama kukopa sana na kusafiri eti kuliko hata Vasco da Gama wa Musoga. Wee! Kausha. Heri lawama za mwenye busara kuliko nyimbo za wapumbavu na wasaka tonge. Mafyatu twasema wazi. Mummy, achana na masifa na kuteua kwa sifa na ithibati. Fyatua watie akilini hawa wanaotufyatua na kupiga njuluku zetu na kutusikinisha kwa uchoyo na uroho na roho mbaya zao.
            Clip aliyocheza Mwanisongo Lee ilimvua nguo mhujumu uchumi huyu ambaye mafyatu watafurahi kama utamtema haraka maanua anatia aibu na hasara. Nchembuz, doktari wa akina Philo na Sofia, sijui alipataje hiyo PhD maana, hata akiongea huoni dalili zozote za ubukuzi. Nadhani Mwambukuzi hakosei anapowaita vilaza. Wamelaza bongo hadi njuluku za mafyatu zaibwa wakiwa wamelala. Jamaa alibanwa inakuwaje anataka kuwatoza wafa kwa ngwamba kodi ilhali matajiri wanapeta. Hakutoa jibu lolote la maana zaidi ya kukusifia na kukusingizia kama gea yake ya kuendelea kuvurunda. Wizara si mali yake ya urithi kiasi cha kuchefua na kutia kinyaa.
            Kwa vile hii ni kaya ya mafyatu na wanene mpo kwa vile mafyatu tumewakasimisha na kuwaamini maulaji, lazima tuzoze hadi umfyatue na kutuletea fyatu anayefaa tena anayeweza kuwafyatua matajiri wasiolipa kodi. Kuna fyatu mmoja wa kaya ya jirani aliwahi kusema kuwa ukiona mafyatu wenye raslimali wakijipeleka majuu kubomu na kupangwa kama wanafunzi mbele ya mkuu wa shule, ujue kuna tatizo. Kwa kaya yetu, tatizo kubwa mafyatu wanaoloona limeota sugu ni kuteuana kwa sifa za uchawa na ukunguni. Inakuwaje fyatu mwenye PhD, tena si ya kuzawadiwa, anafanya madudu kuliko hata waliosoma ngumbaru? Sasa mafyatu tunazoza tena bila kumung’unya kuwa fyatu Nchembuz atumbuliwe haraka japo huwa unaonea kinyaa majipu usiyatumbue kama mwendaze.
            Leo sirongi sana. Muhimu, nasema wazi. Mummy fyatua huyu fyatu ili mafyatu wengine chawizi watie akili. Ukimfyatua usawa huu, mafyatu tutakumwagia kura za kula hadi uzimii. Hivi leo nimekunywa gongo kiasi gani?
Chanzo: Mwananchi leo.

Sunday 9 June 2024

Misingi na nguzo kuu za ndoa

Katika makala iliyopita tuligusia misingi na miiko baadhi ya ndoa. Leo tunaendeleza tulipoishia.
Uhuru
Ndoa inapaswa kuwa huru na isiyotegemea au kuingiliwa na watu wengine katika uendeshaji wenu. Mliapishwa wawili tu na si mia mbili. Hivyo, jukumu na wajibu wa kutunza kiapo chenu ni lenu. Si la watoto wenu, marafiki, wazazi, mashoga, na wengine hata muwapende, kuwathamini, na kuwaamini vipi. Ndoa ni kama sehemu zenu za siri. Hakuna apaswaye kuziona au kuzihudumia isipokuwa wanandoa wenyewe. Nani mpambavu huanika chupi zake hadharani?  Hivyo, ndoa inapaswa kuwa taasisi huru ambapo uhuru huu ulindwa kwa wivu na tahadhari kubwa. Tutoe mfano. Jamaa mmoja alizoea kuwapa marafiki zake siri za mwenzie. Moja ya siri alizotoa ilikuwa ni ukubwa wa maumbile yake na namna alivyojua shughuli.
    Katika hao marafiki, walikuwamo wakware waliokuwa wakimmezea mate mwenzie. Hivyo, kutotunza na kulinda siri za ndoa yake kuligeuka angamizi la ndoa yenyewe hasa wahusika walipokula njama kumuandamana mhusika. Binadamu tumeumbwa na kujipenda kuliko wengine. Mafanikio yako ni yako siyo ya kuwasimulia wenzako. Kitanda usicholalia, hupaswi kujua kunguni wake.
        Japo kuna kipindi mambo huzidi kiasi cha waliotanzwa kutafuta msaada. Katika ndoa, linapotokea tatizo, ni muhimu likashughulikiwa na wahusika peke yao tena kwa usiri. Ndiyo mana tunasema siri za ndani ziishie chumbani. Zisivushwe hata kuchungulia sebuleni. Hao mnaowafuata nao wana changamoto, kasoro, na matatizo yao. Kama ikizidi sana, wahusisheni wazazi wa pande mbili japo nalo hili linataka utafiti na umakini vya hali ya juu. Mnapozoea kuwapelekea watu matatizo yenu, mnayazidisha na kuyafanya yawe magumu zaidi kuliko mkiyashughulikia wenyewe. Mlipoamua kufunga ndoa mlifanya hivyo peke yenu japo baada ya hapo, mlitoa taarifa kwao kama sehemu ya hitajio la kijamii na kisheria. Kwenye changamoto, matatizo, na migogoro ya ndoa, msiwahusishe hata wapambe au mashahidi wenu. Hakimu wa kwanza wa kushgulikia changamoto na matatizo ya ndoa ni wanandoa wenyewe na mahakama yao ni chumba cha kulala.
Ithibati
Pamoja na miiko na misingi mingine, ithibati katika ndoa ni muhimu. Ithibati huonyesha kuwa mhusika anaaminika na anajiamini. Hivyo, zinapotokea changamoto katika ndoa yako, jambo kubwa la kwanza muhimu ni kujiamini. Hii hukupa fursa ya kufikiri na hata kufanya utatifi na kulidurusu tatizo ili ulipatie ufumbuzi. Mfano, unaweza kuchunguza au kutafiti chanzo au vyanzo vya tatizo. Mara nyingi, kama tulivyosema hapo juu, adui mkubwa wa ndoa ni wanandoa. Kadhalika, chanzo au vyanzo vya changamoto ni wao pia iwe kwa bahati mbaya, kutojua, kutokusudia, au kukusudia. Hivyo, sehemu ya kwanza kutafutia changamoto ni wanandoa wenyewe.
        Pili mwitikio na namna wanandoa wanavyopokea na kushughulikia changamoto zan doa yao ni muhimu. Hapa, unaepusha kumtafuta mchafu, wa kumtwisha lawama au kuepuka lawama kwa kufanya hivyo. Changamoto za ndoa ni sawa na maladhi mwilini. Ni mwenye mwili anayeyabaini hata kabla ya daktari. Hivyo, silaha imara ya kwanza kuelekea matatizo ni kujichunguza kwa wanandoa wanaokabiliwa nazo. Hapa, kunahitajika ukweli na uwazi ili kuepuka kufukuza tatizo au kutafuta suluhu mahali ambapo si sahihi au lilipo. Mfano, ukiwa unaumwa kichwa, huwezi kutafuta tatizo kwenye mguu. Lazima ukisikilizie kichwa hata kutafuta ushauri wa daktari juu ya kichwa siyo mguu.
Kanuni
Kama zilivyo taasisi nyingine, ndoa ina kanuni zake. Nyingi za kanuni hizi hazikuandikwa popote. Zinatengenezwa na wanandoa. Mfano, ni jambo gani hupenda kufanya bila kukosa wakati wa kuamka au kulala? Ni jambo gani wanandoa wanakubaliana au kutofautiana katika ndoa? Hata hivyo, methali moja ya kimombo inasema kuwa wanandoa wanaoimba pamoja huishi pamoja.
        Tutoe mfano wetu wenyewe. Siku moja tulinunua gari jipya aina ya Chevy Equinox. Baada ya kulinua, mmoja wetu aliamua atumie gari la zamani Kia Soul. Hata hivyo, kuna wakati tulikuwa tukibadilishana magari kulingana na tulipokuwa tukienda. Nkwazi alikuwa akiendesha Chevy zaidi na Nesaa akitumia Kia Soul. Kuna kitu tulitofautiana. Baada ya kununua Chevy Equinox, Nkwazi alinunua cover ya usukani nyeusi yenye manyoya. Nesaa hakuipenda hata kidogo akisema inaweza kutunza uchafu na ni vigumu kuisafisha. Mwishowe, tulikubaliana kuweka cover ya ngozi na changamoto ikaishia hapa. Kwa kanuni zetu, hatukujiruhusu kitu kitufarakanishe zaidi ya kukubali yaishe kwa msingi wa give and take kama tuutumiavyo kwenye taaluma ya utatuzi wa migogoro na kupata win-win solution au suluhu ambamo wote mnafaidika.
Mwisho, ukiangalia ukubwa wa changamoto, unaweza kuona ni kama jambo dogo. Si dogo. Kumbuka hata mbuni alianza na yai dogo mbali na mbegu za kiume na mayai ya kike visivyoonekana kwa macho. Mbali na hili, kanuni yetu kubwa ni kwamba asiyekubali kushindwa si mshindani na mshindwa wa leo anaweza kuwa mshindi wa kesho.
    Hivyo, ni vizuri kuzingatia msingi na nguzo za ndoa sawa na unavyofanya kwa taasisi nyinginezo. 
Chanzo: Mwananchi leo.


Wednesday 5 June 2024

Mafyatu Kumkaribu Rais Kuzindua Kijiwe

 

Baada ya kuona kuwa inawezekana kumfyatua, sorry, kumchengua rahis hadi anazindua mangomangoma ya Hamnazoo, mafyatu tunakula mkakati kumkaribisha kuzindua kijiwe chetu cha ndumuu. Naona yule anatikisa kichwa kuwa rahis na vijiwe vya bangii, sorry, nimesema bangili wapi na wapi? Hamkumuona arap Rooter wa kwa njirani akijinoma na mchekeshaji kwa Joji Kichaka akiwatosa wake. Ama kweli marahis tunao. Jamaa alikodisha pipa kwa bei mbaya akajaza familia na maswahiba wakaenda zao kutanua majuu kwa kodi za mafyatu. Hamkuona vibinti vyake na vinjukuti majuu? Halafu mnashangaa kwanini Afrika siku zote haiendelei! Kwa uzwazwa huu?

            Kimsingi, baada ya urahis kuwa rahisi hasa usawa huu wanene wanavyohaha na kufyatua maigizo ya kupatia kura ya kula, wanjanja ndo wakati wa kuwatumia kirahisi. Lazima tuwarahisishe japo wamejirahisi wenyewe. Hakumsikia profedheha Muongo aliyekataa msosi hotelini eti ‘kuokoa’ njuluku za mafyatu utadhani alianza unene jana? Tuliokua zama za mzee Nchonga, haya ni makufuru yaliyovunja miiko yote kimaadili. Nakumbuka mzee Ruxa alipomkaribisha Mic Jekson. Wee, tulizoza. Hakurudia.

Turejeee inshu. Nani asiyetaka kura ya kula hata ikibidi kuvunja protokali? Kwani,waziri wa michezo hakutosha kuzindua mangomangoma ya Chingaboy aka Hamnazoo aka kijana wa maza on top of mwana wa pekee wa Arushwa na Abuduli? Wasiojua, maza ni maza wa wanangomangoma mbali na kuwa mpenzi mhifadhi, mfadhili na mchambuzi mahiri wa mambo ya mangomangoma. Soon, nitamshauri fyatu mhariri wangu ampe safu ya kuchambua mangomangoma ili mafyatu waelewe uzuri. Mwaka huu tutashuhudia mengi. Wasiojua. jiulize kwanini, maza, kwanza, alisema jamaa ni kijana wake? Pili, zile ngomangoma siyo za mafyatu bali akina maza wa kisasa na kisiasa wasio na visasi wala madenguzi.

            Nilipoitisha kikao kumkaribu mheshimika, mtukufu, mpendeka, msikivu, mchapakazi, mwelewa, doktari mwenyewe, mmwaga njuluku, fyatu mmoja alidai ninamdhalilisha. Nilimfukuza kigwenani na kumtangaza adui nambari wani wa kaya. Kama Katiba inampa kila uwezo hadi wa kimuungu wa kuweza kuumba na kufuga chawa, nani atamzuia kudhamini na kufungua kijiwe au kucheza nchiriku tena unaomsifia kamwaga njuluku tusizoziona? Kwani yeye siyo binadamu wala fyatu? Ukisikia usikivu na kujishusha­­­­––––siyo kujirahisisha––––kama mafyatu pingaji wanavyoweza kudhani––––ndiko huku. Huku ndiko kupenda mafyatu kiuchakachuaji japo kwa muda hadi kura ya kula ivunwe. Upendo au usanii? Apples and oranges.

            Mbali na hayo, siku hizi, siasa zinahitaji kiwango kikubwa cha usanii. Hivyo, si vibaya rahis kuwa msanii awatumiaye wasanii wenzake. Mmemsahau Njaa kaya kwenda kubembea kule Jomeika utadhani huku hakuna! Mmesahau? Siku hizi ikuu si kukuu tena bali playground ya wasanii? Kesho, sitashangaa kuwaona wakuu wa nkoa na wilaya wakifungua hata vigenge vya kuuzia ulabu kama siyo mmea sorry, mazao yatokanayo na mimea hata kigodoro. Tumeelewana?

            Tulikubaliana kumwalika rahis. Tumepanga tumpongeze kwa kuzindua ngoma nzuri kama hizi. Pili, tuutamtungia wimbo wa kumpongeza anavyomwaga njuluku na ni simba jike. Hamnazoo aliimba kuwa wamaza ni ngurumbili na nusu. Sisi tutaimba kuwa mamaza hasa maza mwenyewe, ni ngurumbili mia. Tatu, maza ana roho ya chuma. Nani alijua kuwa anamilki runinga binafsi? Tutamtaka ataje miradi yake yote ukiwemo ukwasi wake na namna alivyoutengeza na kuuchuma.

            Tutampongeza namna maza anavyowahusudu mafyatu maskini kama vile wauza madafu, mitumba, na udohoudoho mwingine hadi wengine wakiruhusiwa kuuzia hata pale ikuli. Nadhani umenielewa. Pia, tutamuomba mafyatu hasa Fyatu Mfyatuzi atutaje siku hiyo kama alivyowataja wasanii. Mafyatu wamenipa mbinu ya kumvutia maza ili anitaje. Lazima nianze usanii. Nitaanza kuimba mapiano na singeli na kimatress nikieleza anavyovutia kura. Nitamsifia kuwa ni goddess kama wale wa Misri zamani pia kuwakumbuka wasanii. Tutampa maza outing ya nguvu kuliko dingi anavyompa.

            Kabla ya kumaliza, lazima nimshawishi maza, atumie kipaji chake cha kujua mangomangoma na wanamangomangoma kusoma vitabu vya watunzi na waandishi wetu wa vitabu nchini waliododa na kusahaulika huku usanii  ukipewa thamani kuliko ilmu.  Tutamwambia katatizo ka kaya. Inakuwaje wasanii tena waimbao ngonongono watajirike lakini waandishi wa vitabu wafe maskini? Je tatizo ni kaya kupenda na kutukuza mambo haya? Hamjaona orodha ya short time guest houses, vilabu, na madanguro vilivyo vingi kuliko mashule hadi tunapeleka vitegemezi kwa majirani walioamua kutopenda mambo haya. Hamuoni vijigazeti vya udaku vinavyotajirisha wasanii wengi kuliko vitabu vya kiada? Mie mwenyewe niliwahi kuandika kitabu cha kiada kikauawa kwa sababu ambazo sikuambiwa.

            Tutamshauri maza, aanze kuandamana na waandishi wa vitabu badala ya wasanii.  Ikishindikana, tubadilishe shule na vyuo vyote kuwa vya sanaa huku wizara yake ikihamishiwa ikuu. Wajanja wanawekeza kwenye ilmu, sie kwenye mipasho! Sijui nani katuroga yarabi? Je tamasha la Hamnazoo kaandaa yeye au katumwa na maza aanze kampani za kampeni kabla ya kipenga? Hivi, uchaguzi, sorry, uchakachuaji ni lini? Kaeni chonjo. Nshaonya.

Chanzo: Mwananchi leo.

Tuesday 4 June 2024

Yet another baby in the house!!!!

 Yoo-hoo, Africa Is Yowling

ISBN9789956554379
Pages104
Dimensions203x127 mm
Published2024
PublisherLangaa RPCIG, Cameroon
FormatPaperback

YOO-HOO, AFRICA IS YOWLING

by Nkwazi Nkuzi Mhango

Yoo-hoo, Africa Is Yowling is an awakening chant, aiming to shed light on Africa’s losses and explore ways to reclaim its rightful place. Nkwazi Mhango critically examines the continent’s struggles with corrupt leadership, emphasizing how those in power mismanage resources. Despite Africa’s abundant potential and resources, it remains inexplicably impoverished. The central question posed by the tome is this: How can a continent so richly endowed become a dejected entity? The book challenges prevailing narratives that perpetuate Africa’s perceived poverty, urging Africans to think differently and act positively for their own development and the well-being of future generations. In its nostalgic critique, the book confronts societal ills and condemns those who hinder progress. It encourages Africans to boldly advocate for their rights, rejecting deceptive practices, defunct ideologies, and other hindrances. Ultimately, Yoo-hoo, Africa Is Yowling serves as a wake-up call – an urgent plea for Africans to rise, reclaim their agency, and shape a brighter future.

 BOOK PREVIEW
British Pound£
Paperback
£15.00 

ABOUT THE AUTHOR

Nkwazi Nkuzi Mhango

Mhango is the author of Saa ya Ukombozi, Nyuma ya Pazia, Souls on Sale, Born with Voice, Africa Reunite or Perish, Psalm of the Oppressed, Perpetual Search, Africa’s Best and Worst President: How Neocolonialism and Imperialism Maintained Venal Rules in Africa and ‘Is It Global War on Terrorism’ or Global War over Terra Africana?: The Ruse Imperial Powers Use to Occupy Africa Militarily for Economic Gains, How Africa Developed Europe: Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth and What Ought to Be Done and Known, Africa’s Dependency Syndrome: Can Africa Still Turn Things around for the Better?, Our Heritage, Family Friend of Animal and Matembezi Mbugani (Children’s book co-authored with his wife Nesaa).