The Curse for Salvation

The Curse for Salvation

Tuesday, 17 February 2026

Tufyatue Dhana ya familikrasia katika kisiasa

Leo, nazamia rubaa za kimataifa na kitafiti. Baada mtoi wa marehemu rafiki yangu kutemeshwa bungo tokana na kupata ukwasi kwa kutumia surname, leo, nazamia dhana mpya iitwayo Familikrasia, yaani unene wa kifamilia kama sehemu ya demokrasia mamboleo. 
            Nitarejea utafiti wangu wa shahada ya uzamizi, PhD kama wengi waijuavyo. Tasnifu hii ni ya kumi tena ya kubukua siyo kudukua, kununua, au kuzawadia kimagumashi kwa kukimbia umande. Ila nashauri mniite Fyatu na si daktari maana, udaktari siku hizi, umechafuka baada ya kuvamiwa na kuishiwa maana sababu mazwazwa wameunajisi na kuutumia vibaya.
            Lengo kuu ni kutaka kubaini kama familikrasia ina manufaa kikaya au kifamilia au vyote hasa baada ya kutema bungo au kufika ukomoni. Katika utafiti huu kuna matabaka makuu mawili ya ufyatuzi na ujembuzi. 
    Utafiti huu wa kidoktari na kifyatu uligundua mambo makuu yafuatayo:
        Kwanza, wahanga wanachukia familikrasia kimyakimya wakiogopa kupotezwa na kupatilizwa. Hili, limebainishwa na dhana ya Unapokula Kula Usijali Kesho Utajiju (UKUKU) ambapo wahusika hugeuka waroho, wakabila, mafisadi, na ving’ang’anizi kwenye ulaji kiasi cha demokrasia kuwa kichekesho, kikaragosi, na ghasia. Katika kufanya hivyo, hutenda makosa ambayo huwagharimu baadaye. Pia, nimegundua UKUKU ndiyo ulisababisha maanguko na vifo vya akina Kashafi na Sir Damu.
        Pili, familikrasia inachukiwa kwa sababu huhalalisha ufyatuaji mkubwa wa njuluku za mafyatu kutokana na uroho uliojificha nyuma ya UKUKU.
        Tatu, utafiti umegundua kuwa wengi, kama si wote, wa walaji hukosa vigezo vya kisomi isipokuwa ukaribu uwe wa kiukoo au kirafiki na mteuaji. Hivyo, wengi huwa mazwazwa na wasanii wa kawaida wasio na sifa yoyote hata ya kuongoza kundi la nyumbu.
        Nne, familikrasia hujihadaa na kujenga mfumo wa utukufu uchwara ambao msingi wake mkuu ni kutumia vitisho na kuzawadiana ili kuhimili vishindo vya uchakavu, ufisadi, na ulazimishi wake. Hii inapotokea, hujengeka upofu au myopia kwa kisambaa ambao nao hujenga kujisahau na kutojiamini kiasi cha kila asiyekuwamo kuonekana adui na tishio. Hivyo, huleta ukandamizi, usanii, ubabaishi, n.k. Muhimili wa familikrasia ambao ni kichwa chake hujijengea uungufyatu kiasi cha kutengeneza viini vya kujiteketeza wenyewe.
        Tano, familikrasia hulindwa kwa woga na kushuku. Hili, husababishwa na kupwaya na kutokubalika vizaavyo kutojiamini, kuaminika, na woga.
        Sita, familikrasia hubebwa na ukosefu wa aibu, udhu, ufyatu, na ukatili vya kutisha. Mfumo huu, unaweza kuua yeyote anayetaka kuuzuia, kuupinga, kuukosoa, hata kuuondosha. Hivyo, kusababisha maumivu kwa mafyatu mbali na kuwanyonya.
        Saba, familikrasia hutegemea sana matumizi mabaya ya njuluku na raslimali za mafyatu  hongo ya, ulaji, maguvu, majungu, vishawishi, ghilba, na vitisho. Kwa mtoi wa rafiki yangu, rahis wa zamani tena jobless, kilikutwa na mimamli kibao iliyotaifishwa. Je,viko vingapi duniani hii gunia?
        Nane, familikrasia hutegemea kulindana, kung'ang'ania unene ukichelea kung’olewa ambapo jinai yake hufichuka na kuishia ghaibu au lupango hata kuuawa kama ilivyotokea kwa watajwa hapo juu.
        Tisa, utafiti umeonyesha kuwa UKUKU, kwa mfano, kuna uwezekano wa wahalifu wa kiunene kunyatuliwa roho na mafyatu wenye hasira wanapouchoka na kuamua kuuangamiza usiwaangamize.
Matokeo ya utafiti
        Katika kutafiti dhana hii tata nilianzia mtaani kwangu Idodomya––––we koma!!––––na kuelekea Equatorial Guinea, kwa Tarampu. Nilimalizia kwa M7 ambako familikrasia imeota mizizi na kutamalaki kitambo sasa. Katika variables nilizotumia, kuna makundi makuu mawili yaani, kupeana ulaji kifamilia/kirafiki kwa kutegemea uhusiano wa damu au wa kindoa. Vigezo nilivyobaini ni utoi au ukweee. Mfano, kwa M7, vitegemezi na Bi Mkubwa ni sehemu ya sirkal ya Bwana Mkubwa kama sambamba na kwa Trampia ambako wakwe wanatesa katika ulaji. Kule Guinea ya Ikweta, vitegemezi vya munene vinatesa pia.
            Walaji wengi katika familikrasia wamethibitisha kuwa mifyatu mifala, milafi, yenye tamaa, na katili. Pia, mingi ya mifyatu hii ni mitoi, mikwezi, hata washirika wa bedroom hupenda ujiko kutanua ilhali upstairs ni kweupe. Haina aibu na ni michafu usipime. Ingekuwa nazo sawasawa, ingeonea aibu udandizi, wizi, na ulaji wa njuluku za mafyatu bila stahiki isipokuwa unene wa mabuda, maza, au wakweee zao.
Dokezo
Pamoja na kushauri utafiti zaidi, tunapendekeza waathirika si kuuchukia tu ufamilikrasia bali waukabili na kuuondolea mbali ili kupata HAKI na maendeleo kwa ujumla. Katika penye ufamilikrasia kunakuwapo na amani mawenge ambapo haki na usawa hutoweka kiasi cha kaya kuwa kama pango la majembuzi. Hivyo, dawa ya kuondokana na ufamilikrasia ni kuwapo na kutamalaki kwa haki, maadili, na mageuzi ya kweli kimfumo.
        Mwisho, ufamilikrasia ni jinai inayoanza kuzoeleka na kuota mizizi katika kaya nyingi za uswekeni hasa zinazojifanya kuendelea. Ushauri ni kwamba uchukiwe na kupigwa vita kulhali na na kuogopwa kama ukoma. Hii bangi, hivi niko wapi na nafanya nini yarabi!
Chanzo: Mwananchi Jtano leo.

Sunday, 15 February 2026

Letter from Canada where internet is a human right


 The heading is clear. There recently were some internet blackouts in some countries. This sacrilege can't happen in in Canada. Internet access is considered as one of the human rights everybody must enjoy. Therefore, unless otherwise stated, there’s no power whatsoever that can discretionary or out of desperation disconnect or turn internet off for whatever purposes or reasons except under certain circumstances provided for. Under Bill.C-8, the minister of Communication is strictly allowed to make an order to shutdown internet shall there be “reasonable grounds to believe that it is necessary to do so to secure the Canadian telecommunications system against any threat, including that of interference, manipulation, disruption or degradation.”

          As per the Government of Canada website, “the rights and freedoms that individuals have offline must also be protected online. Canada is committed to working with international partners to protect Internet freedom, including the rights to online freedom of expression, association and peaceful assembly, as well as to protect privacy online.” Thus, Canadians enjoy the rights of access and protection of internet.

            In Canada, it isn’t the choice or the discretion of the government or any institution to censure, disconnect, or discretionary provide internet. It’s like water and other essential amenities for Canadians. If anybody–––be it a person or a government––– denies Canadians such a right will not only be denying Canadians their rights but also committing an offence.

            Why has internet become a human right in Canada?

The answer is simple. Internet isn’t a choice or a favour. It’s an essential part and tool of life. You can measure the health of any nation by assessing its freedom of information. People use internet to do business, communicate, study, and many more. Therefore, whoever impinges on the right to access internet adversely affects the lives and the rights of millions. So, too, internet clampdown doesn’t only show how primitive and unfeeling a society that does so is but also can lead to criminal and tort liabilities.

            That said, Canadian leaders avoid such liabilities. If they don’t, they’ll foolishly lose their positions since whatever tort liabilities emanating from such a primitive act legally force the government to redress the victims. That’s because nobody is in power on her or his behalf but that of the citizens and the money paid for covering such wanton expenses comes from Canadian taxpayers. So, by committing such a crime, whoever does so, he automatically loses one of the qualities of leadership. Therefore, such a person or government can be shown the door for abuses of public funds, callousness, criminality, negligence, and others. No sane person does so or needs that. This is what is known as competent and good governance.

            That said, in my country, Tanzania, internet was shut down during chimeric elections wherein the incumbent President won by 98%! If anything, currently, this save for being one of the wonders of the world, can stand as a world record of Presidential ‘victory’ if indeed it’s won fairly and squarely, which even a little bird told me that it doubts this charade. That’s because even during the one-party dictatorship, no Tanzanian President won such a hugely convoluted and tantalising ‘victory.’

That said, such a ‘win’, in bootlicking science, is known as ‘the miracle of the miracle maker.’ Again, to connect this to internet, such a win was achieved during internet blackout. Guess what. If there wasn’t internet clampdown, it’d have interfered with the win and thereby adversely affect and endanger national security, which revolves around one demigod known as President.

            Howbeit, it’s key to know. Sometimes, in some primitive places, internet isn’t only a danger but also a deadly weapon for whoever controls it. For, hackers can use it to frustrate even destroy the win of the infallible mtukufu rais. You know what I mean. That’s the only person in a particular country who runs everything discretionary and effectively regardless of whatever flaws.

            In toto, internet is a human right that needs to be feared. For, it can make people ask for more rights or prevent young voters from voting, which can impinge on the rights of the high and the mighty. So, you know. When’ll cyberspace become a human right in Africa?
Source: Daily Nation today Sunday.

Ishini pamoja na siyo kwa pamoja


Kuna ndoa nyingi ambapo wanandoa wanaishi nyumba moja na kulala kitanda kimoja lakini hawaishi pamoja. Kimwili wako pamoja japo kiroho wako dunia tofauti.  Wanaishi kwa pamoja ila si pamoja. Tuliwahi kugusia madhara ya mitandao na rununu. Mfano, unakuta mke au mume hana haki wala mamlaka ya kujua nywila ya simu ya mwenzake achia mbali kuweza kuishika au kuitumia. Kwanini? Kwa sababu kwenye simu husika kuna mambo ambayo mwenzi hapaswi kuyaona wala kuyajua.
            Kama wanandoa, huwa tunashangaa inakuwaje? Binadamu yoyote timamu kiakili na kiumri ana siri moja inayokubalika kijamii. Nayo, ni kuficha uchi wake. Ni vichaa na watoto pekee wasioweza kufichi sehemu uhci wao. Waliobaki, hakuna kitu kigumu kufanya kama kutoka nje bila kujisitiri. Tena, husema uchi wa mnyama kwa vile ni wanyama tu wanaishi bila kuhitaji kujihifadhi. Hata nao ukiwaangalia kwa makini, hawako uchi.
            Katika ndoa, hakupaswi kuwapo siri baina ya wanandoa. Kama wanaweza kuvuliana nguo, inakuwaje kwanini wasivuliane mioyo? Kama uko kwenye ndoa kama hii, ujue. Mnaishi nyumba moja, kulala kitanda kimoja, kumilki mali na watoto pamoja lakini hamko pamoja. Dhana ya kuishi pamoja inahusisha kuwa pamoja katika kila jambo liwe kubwa au dogo. Huwezi kumficha mwenzio au kuwa na siri zako ambazo hutaki mwenzio azijue mkawa pamoja. Hapana. Kwenye baadhi ya dini, wakati wa kula kiapo cha ndoa, wanandoa huambiwa kuwa wanaacha kuwa miili tofauti na kuungana na kuwa mwili mmoja. Ni mwili gani ambao kiungo chake kimoja kikiumia, sehemu nyingine hazihisi au kushiriki yale maumivu?
            Ndoa siyo kama mashine ambayo inaweza kuwa na sehemu nyingi tofauti ambazo hazijuani wala kuwa na athari sawa.  Magari ya siku hizi yana sensor kiasi cha kuwa mwili hai. Ndoa ni sawa na mwili uwe wa mtu, mnyama hata mti. Ukichuma jani kwenye mti, mwili mzima wa mti unahisi kitendo ulichofanya. Utafiti umeonyesha kuwa miti ina hisia. Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC, 2023) ulioripotiwa na Bethany Nichols uitwao Plants Have Feelings Too miti ina hisia. Ikiguswa inajua. Utafiti huu ulionyesha kuwa miti inapata hata msongo tokana na mazingira iliyomo. Mfano, miti aina ya Arabidopsis thaliana, ikiguswa inajua. Mfano, mwaka 2014, Heidi Appel na Reginald Cocroft wa Chuo Kikuu cha Missouri walichapisha ripoti ya kushangaza. Katika utafiti wao, kwa kutumia vifaa maalumu, walichezesha sauti ya viwavi wakila majani, upepo ukivuma, wadudu chavushi wakija kuchavu na mengine. Miti ilionyesha miitikio tofauti kulingana na sauti iliyochezwa.
            Sasa tujiulize. Kama miti inaweza kuhisi, inakuwaje kwenye ndoa kuwa na siri binafsi kwenye mwili mmoja na sehemu mojawapo ya mwili isihisi au kujua?
            Hivyo, tunapoongelea dhana ya kuishi pamoja na kuishi kwenye nyumba au kitanda kimoja, tuzingatie kuwa kuna uwezekano watu wawili wakalala kitanda kimoja lakini wakaishi kwenye dunia tofauti. Jambo hili hi hatari sana kwa wanandoa. Lina gharama kubwa. Maana, hakuna gharama na usumbufu kama kulinda na kutunza siri. Hii inapotekea, licha ya kumomonyoa upendo na kuzalisha mafarakano, huwaumiza wahusika kisaikolojia kiasi cha kukumbwa na hatari na magonjwa vitokanavyo na msongo wa mawazo ambao kwa sasa ni tishio la afya ya akili duniani.
            Sasa,  nini kifanyike? Mosi, wanandoa waanze kujichunguza kama wanaishi pamoja au wanaishi kwenye nyumba pamoja. Pili, wanandoa waanze kujifunza kuishi pamoja na si kuchangia nyumba na vitanda.
            Tatu, wanaweza kuanza kwa majaribio. Matokeo watakayopata, yanaweza kuwapa la kuchagua ima kuendelea kuchangia nyumba na vitanda au kuanza kuishi pamoja.
            Nne, kwa wale wanaochangia nyumba na vitanda wafahamu kuwa hizo siri wanazoficha na kulinda kwa gharama yoyote zitakuja kufichuka siku moja na wagundue kuwa walikuwa wakihadaa wakiamini wanawahadaa wengine. Hakuna kitu hatarishi na kigumu kama kuwa na kutunza siri. Mshaambwa. Duniani hakuna siri. Kama ipo, ipo kwa muda tu ila si milele. Kama chaji ya simu imeisha, mwaweza kuaziman? Kama hamuwezi, mnaishi tofauti.
Hilo ndilo somo la leo. Kwa wenye maoni mnaweza kutufikia kwa barua pepe nesaa1977@yahoo au nkwazigatsha@yahoo.com.
Chanzo: Mwananchi Leo Jpili.

Tuesday, 10 February 2026

Fyatu kwenda Romu kuuombea Popu aombee Mafyatu

Mwenzenu napanga kwenda Vatikano kukutana na popu kumuomba na kumuombea aombee amani. Nitaadamana na baadhi ya mashehena sorry mashehu wenzangu. Tutahakikisha anaombea amani tu bila haki. Naona yule anashaangaa akadhani mibangi imenifyatua nikafyatuka na kutaka kuifyatua amani! Nina sababu nzuri tu za amani tena kwa amani. Baada ya mafyatu kuzidisha ufyatu hadi kutaka haki kwa gharama ya amani, kama mhimili mkuu wa amani Fyatuland, naanza kushindwa kuwafyatua walipofyatuka wanifyatue, na mwisho wa siku, amani itoweke.
        Sipendi niwafanyie kitu mbaya wakose amani na kunilazimisha kukimbilia kutafuta moto kwenya maji kama suluhu kama yule sulubu. Mpango mzima ni kuikomboa Fyatuland isijiangamize kwa ufyatu. Nikifika, nitamsihi sana aombe mafyatu wawe na amani katika kila jambo. Mfano, wakifyatuliwa, wawe na amani.Wakiburuzwa, wawe na amani.
            Nitamuomba na kumuombea popu aombe amani ili mafyatu, hata wakipigwa au kupigana, wafanye hivyo kwa amani, watulize boli wawe na amani. Maana, bila amani, itakuwa vigumu kuishi na kufyatuana. Amani ni uhai na uhai ni amani; haki ni vurugu iletayo machafuko itokanayo na mafyatu kutaka wapewe hata wasivyostahili kama kujua namna ninavyowafyatua.
 Najua popu atanielewa na kukubali ombi langu la kumuomba, kumuombea, aombee amani kwa amani. Nitafanya hivi kwa amani ili iwepo amani baina yetu. Nitamuomba na kumuombea aombe amani ili tuishi kwa amani bila kukwaruzana na kudaiana haki tena bila amani. Haki inaweza kuua Fyatuland kwa ukosefu amani. Uwepo wa amani utawezesha hata mvua kunyesha. Kutamalaki kwa amani kutawezesha ulaji wangu uwe na amani kiasi cha kufyatua kwa amani.
             Nitamsisitizia Bwana Mkubwa kuwa amani ni tunu ambayo niko tayari kuteka, kupoteza, hata kuua kwa ajili yake. Nataka niwe na amani ya kufyatua mafyatu ila wasiwe na haki ya kunihoji, kunituhumu, kunishitaki wala kunidai au kuwa na haki ya kuvuruga amani. Mafyatu wakiwa na amani, kila kitu kitakwenda vizuri. Hapatakuwapo madai ya kipuuzi kama vile kukinukisha, kuandamana, au kulalamika. Amani haitaki mambo haya. Nataka mafyatu wawe na amani kama kondoo. Kondoo ukimchinja kwa amani, anakufa kwa amani nawe unamla kwa amani.
             Kwa wasiojua haki na madhara yake, wanapenda sana kuomba na kuitaka. Haki ya nini wakati kuna amani hata kama ni ya imani? Haki inaweza kuleta machafuko. Nani anataka haki wakati haki haileti amani bali shari? Ukitaka kuepuka machafuko, basi omba amani tena kwa sana huku ukiikataa haki. Kama utaomba haki, basi omba haki isiwepo bila amani. Maana, bila amani, hata iwepo haki, tutavurugana na kufyatuana. Nitamuombea na kumuomba popu aombe tuwe na amani ya kuwafyatua wanaotaka haki tena kwa amani. Pia, nitamuomba aombe watakaofyatuliwa watulie kwa amani ili wasivuruge amani. Nitamsisitizia aombee Fyatuland iwe na amani na kuchukia na kuepuka haki.
Nitamshauri asiombe haki. Kwani, haki huvuruga amani. Haki huwapa haki mafyatu kuvuruga amani kwa kisingizio cha kuomba na kutaka haki. Amani ni muhimu kuliko haki. Kukitamalaki amani, kila fyatu anafanya na kufyatua kila atakacho kwa amani.
            Nitamuomba na kumuombea popu aombe amani kwa mafyatu waishi na kukubali kila jambo kwa amani. Wakifyatuana hata kuuana, wafanye hivyo kwa amani. Wakitekana au kupotezana, wafanye hivyo kwa amani. Watakaouawa au kufa, wafanye hivyo kwa amani. Wakizikana au kutopata maiti za waliofyatuliwa kwa sababu ya kiherehere cha kutafuta na kutaka haki, wafanye hivyo kwa amani.
            Mbona kuku wana amani japo hawana haki? Kama haki ni mali basi amani ni pepo. Hivyo, nawasihi mafyatu watafute amani. Haki wataikuta mbinguni. Waombe amani ili kila kitu kifanyike kwa amani. Tokana na kutokea mafyatu kama wale wa TEKI tena wanaojifanya wanamfuata popu kutaka kuvuruga amani kwa kudai haki, nitamuomba popu awaombee na kuwakataza kufanya hivyo kwa amani. Nitamshauri awaamuru wote wahubiri amani wakati wakijitenga na haki.
        Juzi, nilikwenda baa na kufanya vurugu kwa amani. Si waliitwa ndata wanidake kwa amani. Nawashukuru sana. Hawakunikamata kwa haki bali kwa amani. Walinipa kipigo cha amani hadi nikalalamika kwa amani. Baada ya hapo, walinifungulia kesi kwa amani. Sasa nangoja kuadhibiwa kwa amani.
            Najua pilato atanipiga mvua si kidogo kwa amani. Kabla ya kufanya hivyo, nitamuomba nijitetee kwa amani ili hata nikifungwa, nifungwe kwa amani. Nitamuomba pilato atoe amri kwa majamaa wa lupango wanifunge kwa amani. Hata pale pilato atakapotamka mvua nitakazokwenda kutumika lupango, nitamuomba atoe hukumu kwa amani. Nitajitetea kuwa nilipofanya vurugu, kimsingi, nilikata kalaji kwa amani nako kakanifyatua kwa amani kiasi cha kufanya vurugu kwa amani hadi nikakamatwa, kuhukumiwa, na kufungwa kwa amani. Kuanzia leo, Fyatuland itaitwa amani na itakuwa mwiko kwa fyatu yeyote kutuletea makelele haki. Du! Majinamizi mengine, acha tu! Inaonekana mgoshi Machungi keshanipiga zongo.
Chanzo: Mwananchi jtano leo.

Sunday, 8 February 2026

Letter to Muhoozi Keinerugaba, Tweet Even More Please


Muhoozi, before saying something, I must remind Ugandans of the best day the country has ever had. On 24th April 1974, Uganda and the world were blessed with and received one of the most powerful sons of presidents in the world, you. This is the time you (who avenges or revenges) came to this earth to save some of earthlings from the ennui of a long-time ruler who happens to be one of your makers. 
        It is the time your great mother gave birth to you, the great son of president who wields as much power as his father, the son who needs more power. Indeed, your arrival wasn’t a common occasion. It wasn’t like the birth of small men and women who come from poor and weak families. Yours was the birth of a saviour of some sort, especially for those who don’t believe that the more things change the more they remain the same. You know what I mean. Still, you’re a saviour for the status quo so to speak vis-a-vis Ugandan politics.
            Dear Muhoozi, a few weeks ago, you, as the most power son of the most powerful man you unveiled what Ugandans need to make do with. Yep, you started to bite at the power that your dad’s been eating on for long. Because of your significance, you openly want everybody to know and make do with you fired a tweet at the US asking it to not put its nose into Ugandan affairs. No joke. You’re not joking. 
            Did you mean business or you’re just looking the way take a bite on power and come out of the political closet. This, to me, shows your significance as the son of the most powerful man in Uganda who also is the most powerful son of the president. The twosome of–––without forgetting your mother––––are the most powerful people Uganda’s ever had. 
        Let Ugandans know that your trinity’s unshakably intact and unique since you’ve made Uganda what it’s today, although your detractors stupidly assert that Uganda was made rich for your family and poor for the rest. Let them know that you still have a lot to offer, and Ugandans must wait for more surprises from this trinity.
            Dear good General, underscoring your greatness and significance, I propose that next time you tweet, all Uganda’s media must support you by subscribing to your tweeter account. I also propose that your tweets must be made breaking news in all Ugandan media. I know those who don’t like you, dear good general, will wag tongues thinking I’m trying to get a mileage out of this assertion, or I might have been paid to say this. Nope, what I’m saying is as simple as the tweets themselves. I know those who don’t know the importance of the first family, namely you,  the mother general, and the father general, wrongly think that their lives are adversely impinged on with uncertainties your tweets cause. Go figure. Guys, who are you in Uganda? Who bewitched or cheated you not to get it?
            Dear General, when the story of your tweets warning the US surfaced in the media before you deleted them later, a friend sent me an email complaining about the uncertainties they’d cause. Also, he’s some concern about the EAC, which’s never delivered anything. I scolded him to stop being selfish, evil, and naïve since things have changed. Christians believe Jesus died for their sins though they’re told everybody to carry one’s cross. On the contrary, politicians believe that citizens must die for them and their sins. Methinks this is the genesis for many African rulers to live larger than life while their taxpayers live and lurch in penury. I told the guy to consider other related things such as the disturbances democracy’s been causing in many African countries that tried it and ended up abusing it through vote rigging and tampering with constitutions to extend their time in office.
            Dear General, methinks Ugandans––––whether they like it or not­­­­–––should brace themselves to see you becoming their leader shall anything happen to your father. This is simple to decipher. When I consider your gruff rise in the army, you can easily know what I mean. Also, if you interrogate the reason[s] behind your father’s clinging unto power, you’ll be on the same page with me. Moreover, if you consider the powers your mom has behind the curtains, you’ll agree with my hypothesis. 
            To give those who pretend to deny the truth, I want them to ask themselves as to why your tweets are leaving everybody shocked. Is the system testing the waters? Is it preparing Ugandans psychologically for what’s on the card in the upper echelons of power wherein manipulations are one of bread and butter of its mainstay? Why have you become such important this time around? Let’s get as serious as a seal instead of trying to screw over this rear up of your display. Those who don’t know your good intentions for Uganda stupidly argue that aim to achieve more power! What power is it while you already have it? Shame on them!
            Dear General, in sum, let me wish you a very spiffy tweeting mission. The Swahili sage’s it that clouds are the signs of rains. Therefore, what you’re seeing regarding your centrality is but the beginning if not the tip of the iceberg. Tweeting warning Uganda’s enemies is one leg in the waters. The sage’s it that if you can’t beat them, join them. Whether they like you or not, they need to understand Uganda’s power dynamics, especially after your dad came to power and altered everything to his advantage.  
        Look at foolish detractors. They foolishly allege that your father propped you up so quickly that way in the military. Nonsense. You’re born a soldier more of a commander. What’s wrong with you to be a presidential material? Once again, Dear General, you seem to brace yourself for big things. Big things come to big people. That’s my titbits of sagacity. Ring-a-ding-ding, nothing but.
Source: Daily Monitor today.

Tuesday, 3 February 2026

Kama miwaya inakula umeme kwanini umeme usiile miwaya?

 Juzi, nilishangaa nusura nife. Si kuna eti utafiti uliofanywa kubaini kwanini umeme unatumika haraka hata kama vifaa vyote vimezimwa! Uliona wapi zaidi ya kwa mafyatu tu? Hapa bado hujasukuti juu ya kuisha muda wa matumizi ya bando la simu. Kweli bando linaisha au linaishishwa ili kuwafyatua mafyatu waliokataa kufyatuka wakafyatua hadi wanafyatuliwa na kila jizi na zwazwa? Hamuoni wachukuaji wakiitwa wawekezaji wawekezao hila za kuwafyatua mafyatua? Ufyatuzi huu haukuanza jana wala juzi. Jikumbushe skandali ya mikataba ya kampuni jizi la Ipielo enzi za ruxa wakati jamaa wa Msonga akiwa waziri wa nishati.
        Kama haitoshi, jikumbushe kashfa ya NBC na ABSA na shemejize Ben. Pia, jikumbushe kashfa mama za Escrew, Kagoda, Mwanakaya Memetuka na nk. wakati wa jamaa wa Msonga. Ukitoka hapo, njoo wakati wa Jiwe ni ile kashfa ya Chatolite ingawa haikupigiwa upatu tokana na kumuogopa mwamba. Kwani, Chatolite ina tofauti gani na Gbadolite ya Kukungbenduwazambanga?
     Japo ya kale hayanuki, wakati mwingine hunuka. Bila kujua ya kale, inakuwa vigumu kujua ya leo yapo kwa sababu gani. Turejee ufyatuaji wa kizwazwa. Sijawahi kuelewa mfano kusikia eti miwaya inaweza kusababisha bili za umeme kupanda. Kwanini haisababishi kushuka? Nilishangaa kusikia eti miwaya isiyopaswa kubeba umeme ilibeba umeme. Kwani, umeme ni maji? Maana, hata kama miwaya ilibeba bila kutumika, umeme ungebaki pale pale. Kwani, kazi ya miwaya ni nini? Hata ukichukua hiyo miwaya ukauganisha kwenye mti, bado bili ya umeme haitaongezeka vingenevyo kuna uchawi. Hivi miwaya kweli inakula umeme au tunafyatuliwa sababu ya uzwazwa au kukosa ufyatukaji wa kuwafyatua wanaotufyatua? Kesho, bili za maji zitaongezeka. Tutaambiwa sababu ya ni aina ya mabomba yaliyotumika. Hebu tujiuize kifyatu. Nani anamilki mitandao ya miwaya inayoingiza umeme kwenye mbavu zetu za mbwa?
           Hamjasikia mafyatu wakilalamika. Mabomba hayatoi maji lakini bili zinakuja. Huenda hata taa nazo zikizimwa zinaendela kula umeme tu au umeme unakula taa. Da! Mmejua kutufyatua!
            Hii ni dharau na roho mbaya sina mfano. Mmetuletea miluku kutubana ilhali sirkal haiitumii. Hamkutosheka! Sasa mnasingizia hata miwaya! Tutajuaje kama kesho, hatutaambiwa kuwa hata matone ya mvua yakigusa miwaya au kunguru kutua juu yake vinapaisha bili? Nimekumbuka. Ndiyo maana juzi nilimuta mghoshi Machungi akiwa na manati anawinda kunguru wasitue kwenye nyaya ili wasimuongezee bili.
            Hakuna kitu huniumiza nikatamani nifyatuke na kufyatua kama namna kila tapeli tena zwazwa, awe wa ndani au nje, anavyoifyatua Fyatuliand. Yaani, mashirika mengi tunayoita ya kiwekezaji ni ya kichukuaji. Kama yanawekeza, basi ni kwa wale walioyawekeza yakawekea njuluku kwenye akaunti zao fichi. Wanachota toka kwa mafyatu na kutajirika na kuondoka na kutuachia umaskini.
            Daima, nawaza kifyatu. Mfano, inakuwaje mafyatu wanene wanatumia njuluku za mafyatu kapuku kujenga miradi halafu wanaita wachukuaji, sorry, wawekezaji waiendeshe? Inakuwaje lisrikal lijiingize kwenye biashara hii ya kichawa, sorry, kichaa? Au ni kwa vile wanene waneemeka kwa kuwafyatua mafyatu waliogoma kufyatuka wakafyatua hadi wanafyatuliwa na kila atakaye kuwafyatua?
            Sitashangaa kwenda kituo cha wese nikajaziwa hewa na kuambiwa kuwa tatizo ni aina ya mkweche ninaoendesha. Sijui itakuwaje na Bi Mkubwa akianza kunifyatua njuluku akisingizia mkoba anamoziweka. Hebu tuwe serious kidogo. Inawezekana kweli bando likaisha au kuisha muda wa matumizi wakati siyo bidhaa inayoisha? Inawekezekanaje bili kupanda bila umeme kutumika? Baya zaidi, mijizi inapanga tarehe ya kuisha bando kana kwamba ni chakula au inajua unvyotumia. Tunamfyatua nani na kwanini yarabi au tumeishiwa ubunifu wa kutengeza njuluku? Bando ni data. Siyo chakula wala dawa ifikie mwisho wa matumizi yake. Hapa Ukanadani sijawahi kusikia kitu hiki. Ukitaka kuwafyatua mafyatu wa hapa kizwazwa kama hivi, wanakufyatua, kukutoa kwenye ulaji na kukufungulia mashtaka.
            Kama hatutazuia ujambazi huu, anaweza kutokea munene akashirikiana na makampuni ya kutengeneza bidhaa kama baiskeli, magari, hata nguo na kuambiwa kuwa nazo zina mwisho wa matumizi ili kuwalazimisha mafyatu kununua bidhaa hizi. Kama bando linakuwa na mwisho wa kutumika, mbona simu hazina? Chondechonde mswambie mafyatu kuwa na watumiaji wa simu nao wana mwisho wao wa matumizi.
            Mkimaliza, mtawafyatua mafyatu. Mtadai kuwa na runinga zao zina mwisho wa matumizi! Yote fanyeni. Msijetwambia kuwa hata njuluku tulizo nazo zinaexpire. Kama vyote vinaexpire, natamani waanze hawa wanaotufyatua na kutuchezea shere kana kwamba sisi ni hamnazo kwa sababu tumegoma kufyatuka na kuwafyatua ili kuwaachisha kutufyatua tena kizwazwa.
            Natamani niandamane. Hata hivyo, naongopa ndata wasinigenzii, wasiojulikana wasiniteke, kunipoteza na kuninyotoa roho. Naonya. Ukija kuniteka, nakuteka, nakupoteza, na kukudedisha kwa vile nisipofanya hivyo, nitafanyiwa. Hii huitwa self-defense kisheria.
            Nionye. Asitokea fyatu yoyote akadai kuwa na Bi Mkubwa wangu amefikia mwisho wa matumizi. Kama hiyo inawezekana, basi kamwambia Bi Mkubwa wenu anayewaruhusu mfyatue vitu vya hovyo na kizwazwa kama hivi. Nimesemaje? Kumbe  niko Mirembe!!
Chanzo: Mwananchi Jtano leo.

Inakuwaje baadhi ya ndoa ni tegemezi?

Tunadhani wengi mmeishasikia baadhi ya wanandoa walioshindwa kuimarisha ndoa zao kwa sababu mbalimbali wakitafuta misaada. Si vibaya kutafuta misaada hata ushauri. Je, ni wapi upate vitu hivi na wakati gani na namna gani ufanye hivyo? Nini unapaswa kuzingatia na kutahadhari? Hili ndilo suala tutakalodurusu leo.Ni jambo la kawaida kusikia wanandoa wakienda kwa viongozi wa dini hasa wachungaji/mashehe kutafuta suluhu ya matatizo ya ndoa zao. Je unapofanya hivyo, huwa umechunguza ndoa zao, uadiifu, ubora, hata uhovyo wao kwanza?
                Je, ni kila mchungaji ni mchungaji au wengine ni wachunaji na hata wazizi na wezi wa kawaida wanaoweza kukutumia na kuongeza ukubwa wa tatizo badala ya kulitatu?
Mfano, unakwenda kwa padri. Vizuri. Je, padri, japo amepewa mamlaka ya kufungisha ndoa, je, mambo ya ndoa anayajuaje wakati haoi wala hajaiwahi kuishi na mke ukiachia mbali hawa wenye ndoa fichi? Unaweza kujitetea kuwa amesomea.  Hata akisomea, hawezi kuwa na ujuzi na uzoefu sawa na wanandoa. Hivyo, kwenda kwa mtu kama huyu kunaweza kuwa chanzo cha kuongeza ukubwa wa tatizo.
            Wengine huenda kwa waganga wa kienyeji ambao siku hizi wameongezeka sana. Hawa hawana cha maana cha kukupa zaidi ya kukuibia, kukudhalilisha, na kukuongezea tatizo. Huu ni upumbavu wala si ujinga. Ni sawa na wale wanaokwenda kwa waganga kutafuta utajiri. Kama waganga wangekuwa na uwezo wa kukupa utajiri, inakuwaje walio wengi ni maskini tena wa kunuka? Hawa, hawafai kabisa. Uzoefu wetu tokana na utafiti hata kusikiliza yaliyowakuta waliofanya hivi unatuambia kuwa hawa ni wa kuepuka kama ukoma hata ukimwi. Kwani, wengi ni wababaishaji, wazinzi, na wezi wa kawaida tu.
        Wengine huenda kwa mashoga au maraafiki zao. Hata hivyo, kufanya hivyo, nako, kwaweza kukuza tatizo badala ya kulitatua. Ushaambiwa ndoa ni ya wawili. Je, unaaminije kuwa hawatakuwa nyongeza ya tatizo? Je, unajua matatizo yalimo kwenye ndoa zao? Ni nini wanacho ambacho wewe huna? Nini wanaweza wewe huwezi? Jiulize zaidi. Je, wao wanakuamini au kukudharau? Je, wanaaminika au hata kujali?
        Wanandoa na watalajiwa wote wajue. Kupata changamoto au matatizo kwenye ndoa siyo mwisho wake. Ni sawa na kuwa mzima na kuugua, kupata na kukosa katika maisha. Ni mambo yanayokufikirisha na kukupa jitihada, nyenzo, ubunifu, na uvumilivu wa kuyakabili na kuyatatu. Hivyo, inapotokea, unaweza kufanya yafuatayo:
        Mosi, utulize mawazo yako ili akili yako isichanganyikiwe na kukushawishi kufanya mambo ambayo si jibu bali tatizo. Unapofanya maamuzi ukiwa na haraka, hofu, au wasi wasi, yatakuwa mabaya tu.
        Pili, kama ni lazima upate msaada, nenda kwa wazazi wako baada ya kujiridhisha wanaweza kukusaidia. Maana, si wazazi wote wanaweza. Mfano, wazazi waliotalikiana au wenye matatizo walioshindwa katika ndoa yao, hawawezi kukusaidia. Wangekuwa wanaweza, basi wengetatua matatizo yao kwanza.
Tatu, fanya utafiti kwanza ili kujua aina, chanzo, ukubwa wa tatizo ili uweze kujiandaa vilivyo. Hapa ndipo inapokuja hatua ya nne.
Nne, jisomee makala na vitabu vinavyohusiana na ndoa uone kama kuna chenye tatizo kama lao ili kujua lilipotokea, wahusika walifanya nini kulitatua.
        Tano, ikizidi ikapungua, mlilie Mungu wako badala ya kujihangaisha na watu ambao nao wanayo yao tena mengine makubwa kuliko yako.
        Sita, unaweza kupata msaada kwa mwenzako. Hapa, kama wahusika mtakuwa wakweli, mkishirikiana mtapata chanzo cha tatizo na kutafuta suluhu pamoja. Ndoa ni kama baiskeli. Kama gurudumu moja kati ya maawili litapata pancha, lililobaki haliwezi kufanya kazi yoyote. Na mara nyingi, matatizo ya ndoa huanzia kwa wanandoa wenyewe iwe kwa hiari au kwa bahati mbaya.
Mnaposhirikiana wawili, kwanza, mtajua chanzo ni nani au nini na mfanye nini. 
        Pili, mtakuwa na vichwa zaidi ya kimoja. Tatu, wote mtajiona kama mko hatarini. Hivyo, mtapambana pamoja badala ya kupambana mmoja dhidi ya mwingine.
        Hata katika kudurusu na kufanyia tatizo utafiti, mtagwana maeneo ya kushughulikia mbali na kupeana maoni na ushauri au namna mnavyolielewa, kutolielewa au kuliendea tatatizo. Kwenu, huu ni msaada mkubwa.
            Mwisho, kwa kuzingatia haya, mnajua ni wapi pa kupata msaada kama ni lazima kufanya hivyo.
Chanzo: Mwananchi Jpili juzi.

Sunday, 25 January 2026

Letter from Canada congrats Museveni

Dear President Yoweri Museveni,
I must admit. I admire your consistence, courage, and creativity. Anybody can hate or loathe you. Truth be told. You’re a master tactician who sees the future. Congrats on that. Though you’ve been in power for decades, you’ve always been ahead of time for decades. Who would think you’d easily and squarely trounce Bobi Wine without any chaos? I adore you because what transpired in my country last year has shown that you aren’t only a tactician but also a honest and a peaceful man per se.
          Now, let me say something about Canada where elections aren’t life-and-death matters. I see Canadians voting with the internet on. Canadian youths aren’t like African ones who waste time browsing and thereby abscond from voting. Methinks, for those who don’t understand why internet was turned off during elections, must know. It’s because you wanted them to go to vote instead of wasting their precious time browsing.
            I also congratulate Ugandans on peacefully voting for a visionary leader before and after elections. Tanzania must take a leaf from Uganda. For, during the voting period, you alluded to a rigging ploy, which indeed happened. Otherwise, you’d have won by 100%. I proudly applaud the Ugandan Electoral Commission on managing the exercise diligently. They made sure that you who poised to win won. I congratulate the UEC on distributing voting materials timely. There happened some glitches that didn’t adversely affect the quality of diligence, especially to an African country where punctuality and reality have never been important altogether.
I heard some ‘bad guys’ condemning your beloved son who warned them not to attempt to snatch your power. Don’t they know his name? What’d Muhoozi or the avenger do at such moment of truth? Congrats Gen. Muhoozi. Keep on tweeting. I honestly like your tweets.
             I must warn ‘Booby.’ Since you took power a few centuries, sorry, decades ago, you’ve proved to be a very truthful man. You say it as it is. Why did Booby and his hecklers easily forget how your avow of not letting power slink out of your safe pair hands? You fought for and liberated Uganda from Idi Amin. Thus, whoever seriously wants power must fight for it. You absolutely once said that you don’t work for anybody except for yourself. Ugandans understand this far too well. Remember? You said “I am not an employee. I hear some people saying that I am their servant; I am not a servant of anybody. I am a freedom fighter; that is why I do what I do. I don’t do it because I am your servant; I am not your servant. I am just a freedom fighter; I am fighting for myself” (Daily Monitor, January 27, 2017).
            In Canada, one runs for the public office to serve the people but not to serve himself or herself. What a foolish idea! You share one quality that those who run for public offices say their intentionality clearly. That said, in Canada, every public officer is an employee of the people. There’s no self-employment in Canadian politics. That’s how reckless our leaders are out here. 
            Another difference is that, in Canada, like Uganda, power comes by votes even though, in some circumstances, one must use the barrel of a gun. Why only through votes? Canada’s never been under stinking dictators like Amin whom you defeated. Like in Canada, Ugandans have truly proved. They know the type of ruler they need and why.
             I like how you’ve been clamorous and impervious throughout your rule. Uganda needs that. You consistently on countless occasions said that you’ll never allow Amin and the likes to return and destroy your gains. Who wants this? Again, those who don’t know this wrongly ask how and why Amin should return while he’s already dead. Yep. Amin died many years ago. Again, Aminism still exists. Whoever doubts this ‘truth truly said’, must ask TZs whom I heard sing Idi Amin Mama. Who know there can evolve one in Uganda?
            I recently heard Donald Trump of the US saying that he’d like Canada to be the US’ newest state after Greenland. Had Canada had a consistent person like you, this threat would have already been sorted out perpendicularly and mercilessly.
            In sum, I happily and honestly congratulate you and your family on your ‘avalanche’ victory. Museveni hoyeeee!
Source: Daily Monitor Sunday today.

Je, talaka inashangiliwa na kusherehekewa?

Japo inaweza kuonekana kama jambo la ajabu, siku hizi, kumeibuka fasheni au tuseme utaratibu wa baadhi ya watu kusherehekea talaka. Hili, kwa kizazi cha zamani, ni ajabu na jipya. Japo kusherehekea talaka kunaanza kuzoeleka baada ya kutangazwa sana mitandaoni, kiakili na kiuhalisia, kuna la kusherehekea na kushangilia katika talaka? Hili ndilo swali litakalotushughulisha leo.
Swali ambalo wengi wanaweza kujiuliza ni je, wahusika wanatuzunga kwa kutafuta umaarufu au kiki? Ni kweli wanafanya hivyo kutokana na furaha au kujiliwaza, kukomoana, hata changamoto ya afya ya akili?  Kwenye chapisho na Waite na wenzake (2002) la Does divorce make people happy?, walihitimisha kuwa kinachoitwa furaha ya kuachika si furaha bali mlinganisho wa masahibu aliyopitia mhusika na kuwa nje yake. Zimmermann na wenzake (2006) kwenye chapisho lao la Happily ever after? Cohabitation, marriage, divorce, and happiness in Germany walifanya utafiti nchini Ujerumani. Walihitimisha kuwa maisha ya ndoa huleta furaha na ridhiko na talaka ina athari hasi.
  Je, talaka, hata kwenye dini zinazoruhusu, ni jambo la furaha au huzuni? Anajibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dk Dorothy Gwajima “kikawaida ndoa ni jambo la heri na furaha, na talaka ni jambo la huzuni, ambalo haitarajiwi.”
 Je, wahusika wanakuwa na ndoa za kupanga ili zitakapovunjika wafanye sherehe na kupata wanachodhamiria? Je, zinakuwa ndoa za kweli walizoingia bila maandalizi au kwa kufuata vitu fulani ambapo wakivikosa, wanavunja ndoa na kusherehekea kujitoa kwenye kifungo cha kujitakia?
 Tukio lilotangazwa hivi karibuni nchini ni pale mama mamoja jina hatutaji, alipoarika watu kusherehekea kuachika. Hapa, pia, kuna mashaka na maswali; kwa sababu mhusika anaelezea kuwa ameachika mara tatu.
Tuzidi kudurusu. Ukitaarifiwa msiba wa ndugu ya jirani yako na ukakuta kuna sherehe na si matanga, utafanya nini? Utajenga dhana na kutoa hitimisho gani? Je, binadamu tunaanza kubadilika hadi kushabikia na kusherehekea misiba na majanga?  Kusema ukweli, ni vigumu kujua msukumo na sababu vya kufanya haya zaidi ya kutaka kiki au kukomoana kwa walioachana. Je, inawezekana wanaosherehekea, kama kweli walikuwa kwenye ndoa, ndiyo chanzo cha kuvunjika ndoa zao? Je, ni tangazo kuwa wanaotaka kuchukua mzigo wachukue au kuhalalisha mipango iliyofanyika nyuma ya pazia ambapo mtalaka hujenga mazingira ya kufanikisha kuishi na yule aliyemtaka na kusababisha kuvunja ndoa yake?
Turejee mfano wa msiba. Ukikuta mtu anashangilia na kusherehekea msiba wa ndugu yake, zaidi ya kujenga dhana kuwa ndiye muuaji, nini zaidi unaweza kudhania? Ajabu, wanaoonyesha kusherehekea talaka ni wanawake. Yupo mwanamke mkenya aliyepata umaarufu kuwa kutangaza na kueneza fasheni hii kiasi cha kuwa chanzo kizuri cha kumuingizia fedha tokana na TikTok kumlipa kwa kuwa na wafuasi wengi. Hatujaona sherehe ya kuacha iliyoandaliwa na mwanamme.
Japo bado ni mapema kutoa hukumu dhidi ya utamaduni huu mpya, tukiri. Lazima kuna tatizo fichi na kubwa. Kama jamii, tuikabili changamoto hii ili taasisi ya ndoa isibomolewe tokana na malengo na matendo ya watu wachache wenye ajenda fichi. Maana, si kawaida binadamu kupigwa akacheka badala ya kulalamika na kulia au kupata hasara akasherehehekea. 
Tumalizie na ushauri wa Dk. Gwajima aliyekaririwa akisema “wataalamu wa masuala ya ndoa, saikolojia, mahusiano, migogoro na wengine kuja na tamko baada ya kuitafiti changamoto hii ili kuepuka kuwavutia vijana wakaishia kusababisha hatari kwa ndoa zao. Kwani, bila ndoa, hata kama siku hizi watu wanaweza kuzaa nje ya ndoa, hakuna taifa. Na kama lipo hasa likitokana na utaratibu wa nje ya utaratibu uliokubalika, litakuwa ni taifa la hovyo na hatarishi.
Baadhi ya mambo ni ya kudurusu na kufikiria kwa makini na si kufuata mkumbo.
Kwa wengi, hasa wanaofunga ndoa zisizo na vipengele vya kuachana kirahisi kama wakristo, talaka haishangiliwi wala kusherehekewa. Ni msiba na bahati mbaya kwa walio wengi. Je, nini husababisha kusherehekea talaka? Mbali na utamaduni na malengo ya wahusika, si rahisi kutoa jibu moja au mawili.
Chanzo: Mwananchi J'pili leo.

Wednesday, 21 January 2026

Nisameheni mafyatu waliotekwa na kupotezwa

Kwa ndugu zangu wapendwa mliofyatuliwa,
 Nawakumbuka sana nisameheni bure. Nawakumbuka akina Ali Kibaooo, Mdudu Nyangarika, Hamp Slowslow, Saa Eight et al. Naomba mzingatie haya. Kama mko hai, mtafurahi na kufarijika kuwa bado mnakumbukwa. Kama mshafyatuliwa, wapendwa wenu watayasoma na kuyahifadhi kwa ajili yenu. Nisameheni kuchelewa kuwasiiana nanyi.
Pia, niweka wazi. Nalaani jinai, unyama, na ukatili wa kutekana, kupotezana na kuuana. Japo wapo wanaofanya hivi kwa kisingizio cha kulinda kaya, kaya hailindwi kwa baadhi ya mafyatu kuwafyatua wenzao kana kwamba wao ndiyo wana hati milki ya kaya. Jinai hii ni mbaya kuliko unyama hata ushetani. Lazima tuilaani na kupiga vita hadi tuitokomeze kabla haijaangamiza kaya.
Kwa wanaongamiza wenzao tena kulinda madhambi na tamaa vyao wanapaswa waambiwe. Nao watakufa hata kama siyo leo. Wenzetu wanatucheka na kutushangaa tulivyo makatili na hayawani. Hatuwezi kuwa kaya huru lakini baadhi wakanyang’anywa HAKI ya kuishi. Hatuwezi kuwa huru ilhali huvumilii maoni na mawazo yanayopingana na yako. Tushindane kwa hoja na si viroja na unyama jamanini.
        Kwa waliofyatuliwa, kupotezwa, na kunyotolewa roho, siku nyingi zimepita tangu mfyatuliwe baada ya kufyatua na kutishia kuwafyatu waliowafyatua na kuendelea kutufyatua mafyatu wasiofyatuka wakafyatua hadi wakawa siku zote wanafyatuliwa kirejareja tena na mazwazwa. Najua. Familia zetu zinaumia na kuteseka kwa sababu ya unyama wa mafyatu wachache wanaotenda kama vile wataishi milele. Kila kitu tunakikuta na tutakiacha. Hata uteke, upote na uue namna gani, hutamaliza mafyatu. Wengine watazaliwa na kukupinga tu. Hata ujihadae vipi, kuondoa uhai wa fyatu mwenzako utakuandamana na ukose amani na raha hata ufiche au kujifanya hayakuhusu vipi. Akina Hitler, Amin, Mussolini, Pol Pot na manyang’au wengine walifyatu mafyatu kwa mamilioni. Wako wapi?
        Kwa wahanga, msikonde. Sir God anawaona watesi wenu. Japo siku hizi HAKI ni machukizo kwa baadhi ya wenzetu, kuna siku siku HAKI itatendeke. Kama Sir God ataahirisha kuwafyatua, atatuliza tu ila si kuzuia. Zao zaja. Kwani, damu yenu itaamka na kulipiza kisasi kama si kwao, basi, kwa vizazi vyao. Kwa taaluma na uzoefu wangu kama profesa emeritus, wote waliojifyatua akili nao roho zao haziko sawa. Wanaungua bila kusema wala kunung’unika waziwazi.
        Nyuma ya pazia, wanaungua na kuumia. Kuna moto unawachoma taratibu. Mateso yao hayapimiki. Wanaishi kwa hofu na wasi wasi.
Wapendwa, hamjasahaulika wala kupuuziwa. Mko, na daima mtakuwa, mioyoni mwetu kama mashujaa. Hamtasahaulika daima. Nani chizi awasahau au kujifanya hamkufyatuliwa? Japo hawapo wanaojitoa ufahamu na kutetea vitu badala ya ufyatu, niaminini. Hawatakaa waionje hiyo amani mawenge na uchwara wasingiziayo. Nahisi hasira na uchungu ninaposikia wadudu wakitaka kuhadaa mafyatu. 
        Yupo huyu mwehu aliyeko juu aitwaye Mkumbokumbo anayetaka mafyatu wafuate mkumbo na kuamini urongo na uzwazwa wake. Anadai mafyatu wanachukiwa kwa sababu ya ukwasi wao! Ukwasi upi na tangia lini? Nani anafaidi huu ukwasi uchwara ugawiwao kwa wenye akili tena kwa hongo za peremende? 
        Wamejua kututenda. Wamelikoroga, halafu wanadai tatizo si wao japo ni wao ila maadui wa kufikirika toka ghaibu! Ni uzwazwa kiasi gani? Hao wanaoshutumiwa kuwahonga njuluku mabarubaru aka mabeberu walianza lini kuwa maadui ilhali, siku zote, wamekuwa wakifadhili mafyatu hadi tukawaita wafadhili? Wakimwga njuluku zikapigwa bila kuhoji, wanaitwa wafadhili. Kama kweli ni mabeberu, inakuwaje nasikia umbea kuwa kuna jitihada za kutafuta washawishi na wapiga chapuo wawashawishi wasamehe mipayuko yenu? Kuna haja mafyatu wazima tuache utoto. Tuamue kusema ukweli. Haiwezekani wafadhili wetu wageuke mabeberu leo siyo jana. 
        Huwa sipendi kigeugeu na urushi. Kwanini wawe wafadhili wakinyamaza? Ajabu, wakifyatuka na kustukia gemu wakahoji, tunawaita mabeberu. Nani mabeberu kati ya wao na wale warongo, wabangaizaji, na wasanii watapatapao. Kama ubeberu ni jinai, waliofyatua mafyatu wetu ndiyo mabeberu. Uzuri wa ‘mabeberu’ hawauia wala kuibia mafyatu wao. Isistoshe, sisi siyo mbuzi majike? Kwa mafyatu, mabeberu si tishio. Wakija, tunawachinja na kuwageuza kitoweo saaafi kama kweli wapo.
            Huwa nashangaa sana mabeberu wanapoiwaita washitili wao mabeberu wakati mabeberu ni wao. Kama ubeberu ni kosa, mabeberu tunao Fyatuland wakitubeberu wakisingizia mabeberu wa kufikirika. Fyatu nakataa kata kata. Beberu gani anaweza kufyatua mafyatu tena wanaofyatuliwa kwa kuishi kwa kula ugali kwa pilipili? Kazi ya beberu ni kuzalisha majike na si kuua wana mbuzi. Kama kweli kuna mabeberu, wakija, wakamateni, wachinjeni lau tuondokane na ukame wa kukosa kiteweo. Chonde chonde waonye mabeberu. Mafyatu tutawafyatua na kuwageuza kitoweo.
Kama kweli maadui wa mafyatu ni mabeberu ninaowajua, hawana haja ya kulalamika bali kuwakamata na kuwafyatua. Kama si hao bali wao hao wanaodai kuna mabeberu wakati wao ndiyo wao hao, tuache kufyatuana kirejareja. Tuambizane ukweli na kuacha kujitoa ufahamu kwa kiherehere kama yule jamaa mbayuwayu.
Chanzo: Mwananchi J'tano leo.

Sunday, 18 January 2026

Canada’s lesson to Africa’s unification

Many East Africans never actualised its profits individually and nationally. Why? Today, I’ll use Canada’s confederacy of ten provinces and three territories and its population of 41 million as one of the richest countries globally to show the lesson Africa can learn. Canada’s GDP is USD 2.3tn compared to Africa’s  GDP of USD 2.8tn with its population of 1.55 billion.
If Canada were divided into 13 countries, its economic clout would vaporise right away. It’d perilously and pointlessly give birth to trifling countries that’d burn billions of dollars on military budgets and purchasing weapons to protect themselves against their neighbours who happen to be Canadians as well. Imagine. How much the tiniest of all, Prince Edward Island with 182,657 homos, would throw away to fear-driven military expenditures just like African colonial-tailored states have always done? The upshot’s simple. If all African states could divulge their military budgets and those of their ever corrupt, extravagating, and thieving rulers, it’s obvious. They’ve what it takes to finance their own development and social services. 
        Arguably, Africa’s capable of improving our live if it can save billions of dollars burnt to colonially calculated divisions and fearmongering. This anomaly doesn’t need an ace mathematician to debunk. According to the World Bank (2020), Canada’s 2019 military expenditure stood at 1.3% of its GDP compared to ever-begging South Sudan 3.4% ; Uganda 2.1% ; Burundi 1.8%; Tanzania 1.3%; Kenya; and Rwanda 1.2%, which makes an average of 1.8% for the EAC, which 5 points higher than Canada.
        Apart from military expenditure, how many billions of dollars Africa spends on feeding its do-nothing Presidents and keeping its colonial borders safe? Surely, Africa’s what it takes to become a world economic supremo without begging as it currently is. There are those who may doubt the viability of such an anecdotal proposal due to the fear that Western countries won’t like the idea of unifying Africa. For how long will Africa feed on and internalise colonial fear?
        Rwanda’s once Francophone. After the 1994 genocide, Rwanda became Anglophone; and nobody stood in its way despite this not auguring well with France. Rwanda pressed on; and stood its ground. Again, for how long will Africans fear the West as if it’s their God? Methinks. We don’t fear God this much. We still commit sins. Let’s commit this sin of pragmatically and truly reuniting Africa commencing with the wobbly EAC. Let’s give it a try. For, we’ve nothing to lose except our shame and sufferings.
        Essentially, the fear of the unknown prevents Africa from being reunited to become stronger. Besides, our rulers’ fear, individuality, greed, and myopia are the major blockages. If Canada were divided, the democracy it enjoys would vanish. Single election would bankrupt the new countries. How much money would it burn on elections just like it’s been in slapdash and rigged elections that produce but just the same rotten and venal rulers?
        What’s more, by having their individual interests secured at the detriment of their future, African countries still blindly plot to use each other for individual interests and those of colonisers instead of working together for true emancipation. This can’t and won’t work. Commandeered in their paltry interests, African countries are comfortably divided among themselves, and their people based on rash and trivial things such as flummery and flummoxed sovereignty. That’s why countries with bigger land mass and voluminous resources have always been seen as a stumbling block to the unification of East Africa. Again, did these countries apply to be what they’re namely colonial-design structures? 
 Canada’s confederacy has big and small members. Comparably, Quebec is 62% of the East Africa but still coexists with the PEI, which is just 0.2 of the EAC just like Zanzibar that’s just 0.36 of the United Republic.
        I, for one, am an unflagging advocate of a single unitary Africa that’ll demolish faux borders and abolish divisions based on feeble and pseudo sovereignties. I’d like to see the current Presidents hitting the road to give room for one President of Africa or the EAC. If this happens, we won’t be complaining about the dictators that want to illegally die in power or suffering from their brutality and their private but public kept armies. For, without reunifying Africa to the tune of what it’s prior to 1884, all we’re cosmetically doing’s but feeding a black hole. Why’s it difficult to think as one nation instead of thinking like useless colonial-sired states we jealously protect for our peril? Call that the lesson from Canada. Hastas entonces.
Source: Daily Monitor Sunday today.