Free Thinking

I Fear Nothing But Fear Itself

Epistle to Afrophobic South Africa

Epistle to Afrophobic South Africa

Sunday, 28 February 2016

Magufuli anaishi jipu ikulu

Chief Secretary Ombeni SefueKuendelea kuwa na balozi Ombeni Sefue–ambaye, kimsingi, alikuwa mshauri mkuu wa rais mstaafu Jakaya Kikwete anayedaiwa kuacha nyuma madudu kibao–ni licha ya kuchafua sifa ya serikali ya awamu ya tano, ni kuendelea na madudu yale yale bila kujua au kwa kujua jambo ambalo litaishushia hadhi serikali ya awamu ya tano bila sababu zozote za msingi. Sijui kama rais John Pombe Magufuli analijua hili. Kwa vile Magufuli ameingia na staili mpya ya utendaji, anapaswa kuwa na watu wapya pale asipolazimika kama vile kwenye uteuzi wa baraza la mawaziri.
            Mfano mdogo wa karibu ni ikulu hiyo hiyo ikiwa chini ya Kikwete na Sefue huyu huyu ni kuhusishwa kwenye kashfa ya Escrow ambapo Mnikulu wa Ikulu, Shaban Gurumo alikiri kukatiwa shilingi 80,850,000 na mtuhumiwa mkuu wa Escrow. Kuna uwezekano fedha hii ni kidogo tu inayojulikana na inaweza kuwa iliingia kwenye mikono mingi. Japo hatusemi kuwa Sefue alishiriki moja kwa moja, kama ofisi yake ilishiriki basi naye alishiriki.
Bila kupindisha maneno, Sefue atakuwa ni jipu linalopaswa kutumbuliwa kama ilivyokuwa kwa msemaji wa Kikwete Salva Rweyemamu aliyeonjeshwa ulaji akasahau kuna kesho hadi alipofurushwa hata kabla ya Magufuli kukanyaga ikulu. Hivyo, wengi wanaojua jinsi serikali zinavyofanya kazi, wanashangaa Magufuli kuendelea kuwa na Sefue kama msaidizi wake mkuu wakati alishaonyesha alivyoshirika kwenye uoza wa serikali iliyopita si kama mtu binafsi bali kwa nafasi yake.
            Kwa vile Magufuli ni mpya kwenye kazi yake, wengi wangedhani angeanza na timu mpya kama alivyopatia kwa kumteua waziri mkuu mpya asiye na doa au makamu wa rais. Hata kwa wasaidizi wake hasa katibu kiongozi lazima ateue mtu toka nje ya uoza uliopita. Maana katibu kiongozi ndiye mpishi mkuu wa sera za serikali. Na lolote lililotendwa na serikali yake lazima limkumbe. Inakuwaje Magufuli aeleze uoza alioukuta kama ulivyoachwa na mtangulizi wake ashindwe kumwajibisha Sefue. Kimsingi, kama Sefue ni mchafu hivyo–na si kwa kumpakazia hasa kutokana mapishi aliyofanya wakati wa Kikwete–uwezekano wa kumchafua Magufuli hata kuhatarisha heshima na sifa yake ni mkubwa tu. Ni suala la wakati ukweli utadhihirika na uongo utajitenga.
            Kwa hatua za hatari anazochukua Magufuli dhidi ya mafisadi wakubwa na wadogo, uwezekano wa kula na wabaya wake ni mkubwa kiasi cha kuhatarisha hata maisha yake. Kwa wanaojua uzalendo wa marehemu Edward Sokoine na alivyojikuta akipigana vita peke yake kwa kuamini kuwa aliokuwa nao walikuwa naye wakati si kweli, hawatashangaa kusoma haya na kuyafanyia kazi. Hata hivyo, tuweke bayana. Hakuna tunayemshuku zaidi ya kutaka kuonyesha umuhimu wa Magufuli kuwa na timu mpya ili aendelee na mambo yake mapya ambayo–yanawafurahisha watu wa chini–la yanawakera wakubwa ambao walizoea ufisadi kama sehemu ya kujipatia mlo wao na si mlo tu bali utajiri wa kutaka kuridhisha vichaa na uroho na roho mbaya za vitu. Maana wengine hawaibii umaskini wala uhitaji bali roho mbaya na mazoea mabaya.
            Tunafahamu kuwa ufisadi mwingi hasa mkubwa nchini huwa haufanyiki bila kuhusisha ikulu mara nyingi. Rejea kufichuka hivi karibuni kuwa mhindi aliyetorosha wanyama wetu alikuwa na vibali toka Ikulu. Hivyo, tunajua fika kuwa ufisadi mwingi unaozidi kuibuliwa lazima utaigusa ikulu kwa njia moja au nyingine na Sefue hatanusurika hasa ikizingatiwa kuwa amekaa pale kwa muda mrefu, ukiachia mbali serikali yake na Kikwete kufanya madudu mengi ambayo yanamlazimisha rais Magufuli kuchukua hatua kali kiasi cha kuwakwaza wengi waliozoea ubwete na dezo chini ya serikali hiyo. Ushahidi mwingine wa kimazingira ni ile hali ya serikali iliyopita kutowachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi na uchafu mwingine kama vile ujambazi na uuzaji mihadarati ambavyo rais mstaafu alisema alikuwa ameletewa orodha na vyombo vya usalama akaamua kuiatamia kwa sababu ajuazo. Hata hivyo, kwanini kuhangaishwa na watu wachache wakati Tanzania ina idadi ya watu inayozidi milioni 40. Kwanini kung’ang’ania viraka–na hata magamba wakati tunao watu wengi tena wenye uwezo wa kutosha wanaoweza kufanya kazi husika?
            Kuzidi kuonyesha kuwa ikulu lazima ilishiriki kwenye ufisadi mwingi chini ya utawala uliopita, rejea mfano mwingine ni kuuzwa kwa mbuga ya wanyama ya Loliondo chini ya utawala wa awamu ya pili. Nani hajui kuwa dili lote lilifanyika ikulu?
            Tumalizie kwa kumtaka ima Magufuli ateue timu mpya na katibu kiongozi mpya au Sefue mwenyewe ajing’atue ili kuendelea kulinda heshima yake iliyobaki. Akifanya hivyo, atakuwa amejijengea heshima na kuacha mzigo umuandame bosi wake kuliko yeye kung’ang’ania kukaa ikulu wakati watanzania walio wengi wanahoji: Iweje Sefue aonekane safi wakati ikulu na serikali alivyotumikia kwa muda mrefu vimeonyesha wazi kuwa vichafu? Tunaomba kutoa hoja tena kwa upole. Ni ushauri wa bure tu.
Chanzo: Mwanahalisi Feb., 29, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 19:42 No comments:

Congrats king M7 on your victory


            Dear readers and fans, greeting from the Republic of M7, sorry UG which recently concluded its charade, sorry, general elections that saw long-time demoncrat, sorry, democrat YKM7 won his 60th term in office. Boozers sent me to observe these elections in order to be able to evaluate how Danganyika has fared as far as chakachuazation is concerned.
            As I went through UG’s history, I found that M7 came to power thirty years ago when I was a teen. So, too, I discovered that M7 came to power when former president Mzee Ruksa Mwinyi was in his first year in office. Now the man is retired after Ben Tunituni Kiwila Makapi took over; and retired ten years thereafter before  Njaa Jaa Kaya taking over; and retiring last year. All three former presidents served ten years each while M7, just like Bob Jongwe in Zim is still asking for more.
            After the results were announced M7 declared a winner, I discovered another interesting thing. M7’s nemesis, Dr Ciiza Besigie was under house arrest for fear that he’d organize his buddies to take to the streets. Importantly, I’d admit. UG’s mess showed that Bongolalala aka Danganyika is a wee better comparably. However, it isn’t good to compare sick persons. What’s more, I discovered that the East African Community has broken a record when it comes to tampering with constitutions; and clinging unto ulaji. Out of five members, it is only two namely Nyayo country and Danganyika that respect term limit. As for the rest namely Urundi, Ruanda and UG, presidents have commuted themselves into democratic kings.
            After M7 came out to face the media, I posed as a journalist. Lucky me; I was one of the journos who were allowed to ask him just one question. My question was simple but complex. Before stating the question, I coughed a little and said, Mr. President-Elect, first of all congratulations on winning big. He smiled and replied, “Thank you verrry much.” I then went on, Mr. President Elect allow me to quote the words you uttered in 1986 when you first came to power.  I went on. You said. I quote, “The problem of Africa in general and Uganda in particular is not the people but leaders who want to overstay in power.” Then I dropped my bombshell as dry as it was. Mr. President-Elect, do you think your words are still relevant especially to UG?
            As usual, M7 stared in my eyes and said, “Young man, first of all thank you. Again, who sent you in the first place? Anyway, I’rr answer your question however sirry it is.” He smiled again, and went on, “In Africa term limit is not the issue. We talk about God chosen to stop LGBTs and opposition. I told UGs many times that I’d like to retire. But they said if I do, they’d commit suttee. Who wants his people to die while he's stamina? How can I leave at the time the banana republic I created is becoming ripe?”
            Given that I was accorded a chance for one question and Mr. M7 decided to ask me a question, I chipped in with another question. I said, “You’re talking about Africa while in my hunk the term limit is highly respected. Three presidents have already served two terms; and retire while you’re still at it. By the way, who appointed you to speak on behalf of Africa?”
            Before M7 answered, I found myself held up; and bundled out of the conference room. Essentially, when I pondered on what transpired in UG, I discovered that by flouting Zenj’s elections where little bird confided it to me that the big man was defeated (read this silently and tell nobody), I discovered that we tarnished our image pointlessly. My assessment is that Zenj’s imbroglio has dented even Dr Mugful a great deal more. His boil cleansing seems to be selective and one sided.
            From M7’s conference, I hit the road to Besigie’s home prison. After greetings, I wanted to know his take of his defeat. He boldly said, “My brother, do you believe in these charades whereby the dictator copied your chakachuazation thing once again? Go figure. And go tell it to the birds. M7 rigged the elections. Methinks they’d have declared him king but not democratically-elected president.” Hee Makubwa! I said and left. From Besigie’s I went to Nile Mansion hotel to meet with Gen Olushe Obasanjo former Nigerian president. He had this to say, “Once again these elections fell short of meeting key democratic benchmarks.” When I asked him to comment on Zenj, he said, "Do you think there’s any difference there? "
In a nutshell, these are greetings from UG especially going to Zenj. By the way, does Zenj’s opposition still trust Jechia who messed big time? How far sure are they that he isn’t going to do it again?
Congrats King M7 on your hot victory.
Source: Guardian, Feb., 28, 2016.




Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 08:31 No comments:

Friday, 26 February 2016

Nimemkumbuka marehemu Mashakada leo


Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 22:06 No comments:

Mlevi kumualika Obasanjo uchakachuaji Zenj


            Baada ya rafiki yangu wa zamani Jenerali Olushe Obasanjoo kuonyesha asivyo mwoga wala mnafiki kwenye uchakachuaji uliosha kwa M7, mlevi anapanga kutia timu Abeokuta kwenda kumpa shavu na kumtaka aje Zenj na kupayuka baada ya uchakachuaji unaotegemea kufanyika hivi karibuni. Jamaa hakumlazia damu mfalme M7. Alizoza wazi kuwa alichakachua na kuwaburuza wapingaji wake. Kama asemavyo Dk Kanywaji Mugful, Msemakweli ni mpenzi wa Mungu na si Mnafiki. Laiti Mugful angeamua kushughulikia unafiki wa kuchakachua kura, nadhani angeishi kwa kadri ya anachohubiri.
            Obasanjoo alikuwa mkuu wa msafara wa Jumuia ya Makoloni ya Kiingilish aliyesimamia uchakachuaji ambapo mfalme M7 alishinda kwa mara ya ishirini. Kwa vile nasi tumekuwa na Jechia Salimu Jechia ambaye alifuta matokeo ya uchaguzi uliopita bila sababu za msingi hata za kilevi, tunaamini tukipata wapayukaji kama hawa huenda wapuuzi wanaoharibu mambo wanaweza kunywea. Kwanza wanajua huyu jamaa licha ya kuwahi kuwa rahis ni mjeshi tena mwenye cheo cha jenerali kama mimi ambaye tulikutana kule kwa Aldershottukichukua mafunzo yetu ya kijeshi toka kwa mkoloni wetu kama ilivyokuwa utamanduni. Maana, wakoloni kwa kujua ujuha wetu waliamua kufundisha wajeshi wetu ili waweze kuangusha serikali ambayo hawakuwa nayo maslahi kama ilivyotokea kule Nigeria, Ghana na kwingineko.
            Nani alijua kuwa mzee Obasanjoo angemtolea nje Kagutuka M7 kuwa alishinda kwa nguvu ya mituringa ya kutumia ndata na ndutu? Kwa vile tushajua ushindi wa bao la mkono mara nyingi hutegemea ndata na masoja, lazima tuhakikishe tunawaalika washikaji wetu wenye vifua kama vile mzee Olushe waje kutupa kampani kuhakikisha hakuna jambazi wa kura anayechakachua matokeo.
            Kama siyo kufanya mambo kibongobongo nadhani walevi wa Zenj walipaswa kujua sababu ya kufutwa matokeo na nani alikuwa ameshinda kabla ya kuelekea kwenye vituo vya kupiga kura ili kuepuka kwenda kubariki uchakachuaji kama ilvyofanyika UG juzi. Maana kwa tuliofuatilia maandalizi ya uchakachuaji wa UG tulishajua mshindi hata kama ameshinda kiharamu. Ukiangalia upande wa Zenj pia, hata kama huvuti bangi na kupiga bwimbwi kama mimi unaweza kutabiri nani ataibuka mshindi hasa ikizingatiwa kuwa waliowahi kusema kuwa hawawezi kuachia ulaji kwa vijikaratasi yaani kura ya kula. Hivyo, ina maana kwa kutumia mitutu, uchakachuaji na jinai nyingine lazima itumike sayansi ya mtaalamu mmoja wa uchakachuaji aitwaye Nipe Ninaya Mapepe aliyekuja na nadharia ya bao la mkono.
            Nikiangalia wapingaji walivyoshupaa kutaka kujua kilichosababisha kufutwa matokeo Zenj huku walaji wakiminya, nagundua kuwa upande ulio kimya lazima ushinde kwa vile haulalamiki kwa vile unajua kilichofanyika kwa maslahi yake. Maana, kwa jinai aliyetenda Jechia–ambayo, bila shaka, mzee Olushe angelaani kwa kinywa kipana–hakuna mtu mwenye akili asiyenufaika nayo anaweza kuikalia kimya hata asilalamike achia mbali kutolaani. Japo wengi wanaogopa kuronga kuwa kilichotokea Zenj ni dhuluma, mlevi–kwa vile huwa hana breki–anasema wazi wazi kuwa kilichofanyika ni jinaiiiiii, dhulumaaaaaa na aibuuuuu kwa kaya yooote come what may.
            Japo mimi si tapeli anayejifanya mtabiri kama yule habith Shehena Yaya ambaye alisisha utapeli wake kwa kitegemezi chake, naweza kutabiri nani atashinda Zenj. Ni rahisi kutabiri kama ilivyo kwa kichanga kulia. Hata hivyo, hawa majipu na mabusha wanaochakachua uchaguzi wanapaswa kujua kuwa tunakokwenda wanaweza kuleta machafuko. Kwani lazima waongoze wao wakati wameishaonyesha kuchemsha kila hali tena kwa miaka nenda rudi?
            Kwa vile hawa jamaa hawataki kuacha nchezo wao, Mlevi anataka kufunga safari–tena kwa kujigharimia–kwenda kumualika mzee Olushe aje asimamie uchaguzi wa Zenj.  Baada ya kufika Abeokuta na kumwalika Olushe, nitamuomba akifika awaulize akina Jechia sababu hasa za kufuta matokeo ya uchaguzi halali na kwanini na kwa faida ya nani na walikatiwa kiasi gani na wanategemea nini huku tuendako iwapo walevi watazinduka toka ulevini na usingizini. Kuna haja ya walevi kuzinduka na kuondoa ving’ang’anizi wanaotaka kuwa wafalme kupitia sanduku la kura kama ilivyo kwa M7 ambaye ameanza kutawala UG wakati nikiwa darasa la saba na sasa mwanangu anamaliza chuo. Mijitu mingine, imezeeka hata akili lakini bado inajiona ndiyo yenye akili kuliko wengine kiasi cha kukutaka kuendelea kuwala na kuwatawala. Ishindwe na ilegee. Kwanini isiige mfano wa Olushe aliyetawala na kuwaachia wengine?
            Ngoja nimtumia ujumbe brother Olushe kupitia hapa. Kaka, kwanza nakukaribisha Bongo uje ujienjoi. Ila sitaki uje na wale jamaa almaarufu mumu wasije kuwaliza walevi wangu kwa ile kitu yao ya Kinigeria. Nakuomba sana brother uje hapa uwapayukie akina Jechia ambao inaonekana lisirikali linawatumia kuchakachua kura ili chama twawala kiendelee kula kule Zenj. Bradha Shining umeinyaka hiyo?
            Ala kumbe nimelewa!
Chanzo: Nipashe, Feb., 27, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 19:15 No comments:

Hii ni bahati mbaya au kuna namna kwenye wizi wa makontena?

KWA mujibu wa gazeti la Nipashe la leo, kampuni zifuatazo ndizo zilibainika kushiriki kupitisha makotena bandarini bila kulipa ushuru. Ukiangalia majina ya makampuni takriban yote ni ya kiarabu. Je haya makampuni yalikuwa yanatokea Uarabuni au kwingineko. Je ilikuwaje wafanyabiashara ya utoaji makontena wote wawe na majina ya kiarabu au kuna namna.
Orodha ya makampuni kama ifuatavyo:
Makampuni yalijisalimisha kulipa kati 24 kuwa ni pamoja na kampuni ya Zulea Abas Ally, Omary Hussein Badawy, Libas Fashion, Ally Awes Hamdani, Zuleha Abbas Alli na Issa Ali Salim. 
Kwa upande wa kampuni  ambayo yameshindwa kulipa kodi ni ya Said Ahmed Said, Strauss Said, Farid Abdallah Salum, Nasir Saleh Mazrui, Simbo Yona Kimaro, Ally Masoud Dama, Juma Kssem Abdul, Salum Link Tyres, Tybat Trading Co. Ltd na  Swaleh Mohamed Swalehe. 
Mengine ni Ips Roofing Co.Ltd, Rushwheel Tyre Genaral Co.Ltd, Said Ahmad Hamdan, Ahmed Saleh Tawred na Farida Abdullah Salem.
 

Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 19:14 No comments:

Tuesday, 23 February 2016

Huyu tajiri unamtathmini vipi?


Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 19:09 No comments:

Kijiwe chataka waliozima mita za mafuta nao wazimwe


            Taarifa kuwa baadhi ya wezi na wakubwa katika kaya yetu walikuwa ikiingiza mafuta bila kulipiwa ushuru kwa miaka mitano zimewaudhi wanakijiwe nusu ya kufikia kutaka kupasuka. Licha ya kulaani ujambazi huu, kijiwe kinataka hata rahis aliyepita achunguzwe na kufikishwa kwa pilato. Maana inavyoonekana huu ni mpango uliohusisha wakubwa wa juu kwenye lisirikali.
            Kapende anaingia akiwa ameramba suti leo utadhani anakwenda kurora! Kwa wasiojua kurora ni kuoa. Anakula mic, “Jamani mmesoma hii habari juu ya waduwanzi na majambazi wakubwa kufunga mita ya mafuta na kuingiza wese kayani kwa miaka mitano bila kulipa hata senti? Hivi tutaliwa hivi hadi lini?
            Mpemba anakula mic, “Mie wallahi jana hata sikula. Baada ya kupata hizi habari nilitamani nshike panga na kukata ntu kichwa wallahi.”
            Mbwamwitu anamchomkea Mpemba, “Kuchukia hakusaidii wakati wenzio wakifurahia. Tunapaswa kushinikiza wahusika nao wazimwe tena kwa miaka 500.”
            Dk Msomi Mkatatamaa anaamua kutia buti mapema tokana na uzito wa mada ya leo, “Ukisikia mara nyingi tunasema kaya ilikuwa kwenye autopilot chini ya Njaa Jaa la Kaya kwa miaka kumi ndiyo huku. Japo kusema tunaliwa kunakera na kuamsha hasira, hakuna ubishi tumeliwa kwa miaka kumi tutake tusitake. Hapa tunaongelea mafuta. Je ni mazabe mangapi hajafumliwa? Utashangaa hawa unaowaona wakitukoga kwa ukwasi wao ndiyo hao hao walioasisi na kutenda kadhia hii ambayo ni maangamizi ya kujitakia yatokanayo na upogo,  upofu na uroho wa tunaodhani ni wenzetu. Lazima hapa Dokta mwenzangu Kanywaji achukue hatua kuwafillisi na kuwazima kwa miaka 500 kama asemavyo mheshimiwa Mbwamwitu. Enough is enough.”
            Kabla ya Msomi kuendelea, Mijjinga anamchomekea na kusema, “ Sitaki kukukatisha tamaa kama jina lako. Tokana na mfumo wa hovyo tulio nao, utashangaa wahusika kufikishwa kwa pilato na kutoa chochote kitu na kuhukumiwa kusafisha hospitali kama majizi tuliyoshuhudia juzi yakipewa adhabu hii. Waarabu wa Pemba hujuana na kwa vilemba na lao ni moja na wanakula pamoja.”
            Msomi anaendelea, “Nakubaliana nawe mheshimiwa Mijjinga hasa ikizingatia kuwa ufisadi katika kaya yetu ni wa kimfumo ambao dokta mwenzaangu Kanywaji anaonekana kuukunakuna badala ya kuufumua na kuufuma upya. Bila kuja na sheria za kupiga watu shaba, tutaendelea kuumia, kulalamika na kutwanga maji kwenye kinu.”
             Msomi anakohoa kidogo na kuendelea, “Kama dokta Kanywaji amegundua hili, basi na mtangulizi wake alijua, ila kwa vile kuna namna alinufaika na ujambazi huu, aliamua kunyamaza na kupiga fedha. Wako wapi majambazio wa Escrew au EPA ambayo Njaa Jaa Kaya alituhumiwa moja kwa moja pamoja na Ben Tunituni Makapi kuasisi na kutekeleza? Sijamsikia dokta Kanywaji akiwatumbua jipu zaidi ya kuhangaika na majipu uchungu huku majipu na mabusha yenyewe akijifanya hayaoni wala kuyajua.”
            Mipawa ananyakua mic, “Hata nami sina shaka na usemayo kuwa Njaa Jaa Kaya alijua na kuwa nyuma ya kila kitu kama ilivyokuwa kwa Richmonduli aliyomtwisha Ewassa akabaki anachekelea kama kawaida yake. Lazima naye atumbuliwe jipu tena mara moja bila kumwangalia nyani usoni hata kama ni mkubwa kama sokwe.”
            Mgosi Machungi aliyekuwa anarejea kutoka msalani anaamua kula mic, “ Hapa azima tiambiane ukwei. Njaa Jaa Kaya anahusika moja kwa moja na hawezi kujinashua hapa. Nami naanza kuwa na wasi wasi na dokta Kanywaji hasa kwa ukimya na ugoigoi wake katika kushughuikia majipu na mabusha. Kwei leo nimekubai tinaiwa hata kama ni neno baya kutumia. Hata hivyo, nao akina Njaa Jaa Kaya azima waiwe watake wasitake. Kwanini tisiandamane kwenda ikuu kumshinikiza dokta Kanywaji awazime hawa mbwa miaka 5,000 ii iwe somo kwa wengine wanaodhani kaya yetu ni shamba la bibi kwa kila nyani kujiia atakavyo?”
            Kanji anaamua kutia guu kinomi, “Hata mimi roho iko uuma sana. Sasa kama jambazi yote hii nafanya witu kama hii na Jaa Jaa Kaya nakaa naangalia kwanini hapana peleke yeye pango haraka jamani?”
            Mheshimiwa Bwege anaamua kukwanyua mic, “Mimi sina imani na yoyote hasa ikizingatiwa kuwa dokta Kanywaji na Njaa Jaa Kaya wote ni watoto wa chata lilelile la kulindana, kulinda na kufanya ufisadi. Bila kunkamata Njaa Jaa Kaya na kutupa lupango, kila kitu ni sanaa na maigizo kama kawa. Haiwezekani kampuni lililofanya hujuma hili linajulikana halafu tunaendelea kupiga kelele. Bila shaka kampuni hili ni mali ya wakubwa majambazi waliowezesha upigaji huu wa hatari ambao ni jinai ya maangamizi kwa wachovu wote.”
            Mzee Maneno anakwanyua mic, “Kweli kaya yetu ni ya waliwaji. Hamkusikia vigogo wawili wakigombea nyumba ya umma waliouziana kana kwamba tuna nyumba za kutosha kwa wachovu wetu? Hamuoni dokta Kanywaji alivyowagwaya kalu na abusiii waliojazana kwenye nyumba za Msajili wakati wana majumba kibao wakipangisha kwa ma-TX? Nani anamdanganya nani? Napendekeza tujichukulie sheria mikononi kama tunavyowafanyia vibaka. Twende tukachome ofisi za hilo kampuni huku tukiwasaka majambazi wote mmoja mmoja na kuwapiga nari na; kuondoa udhia.”
            Kijiwe kikiwa kinachanganya lilipita gari la kampuni ya Oilryx; tulilikimbiza na kulipiga nari.
Chanzo: Tanzania Daima Feb., 24, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 19:07 No comments:

Sunday, 21 February 2016

Tuondoe Tanzania kwenye makucha ya vigogo

  1. [​IMG]
 Taaria kuwa katika wimbi la kukamata wanaohujumu nchi yetu limemnasa mtoto wa aliyewhi kuwa Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova aitwaye Masoud linaweza kufichua mengi. Je ni watoto wangapi wa vigogo wako kwenye ulaji wakipiga dili huku wananchi wetu wakiendelea kuteseka bila sababu zaidi ya uroho na upogo wa watawala wetu? Vyombo vya habari vilikaririwa vikiripoti, gazeti la Jamhuri (Januari 6, 2016) liliandika, “JAMHURI limepata malalamiko kutoka kwa wafanyakazi wa Bandari na watu walioko ndani ya Jeshi la Polisi wakihoji ilikuwaje mtoto wa Kova, aliyehusishwa na upotevu wa makontena amekamatwa na kupewa dhamana usiku wa Desemba 29, 2015 huku baadhi ya wakurugenzi waliokamatwa awali wakilazwa ndani.”
Sijui kama Dk Magufuli alisoma gazeti hili au watu wake na amechukua hatua gani. Hivi tunaipeleka Tanzania wapi na kwa faida ya nani tunapoendeleza mchezo mchafu wa kulindana hivi? Kukna uwezekano kuwa kukamatwa kwa mtoto wa Kova, Masoud ni sawa na tone la maji baharini, wako watoto wengi wa vigogo ambao hawajakamatwa na ndiyo sababu hadi leo suala la kauwafikisha mahakamani linakuwa la kusua sua.
Mmoja wa wasomaji aliandika yafuatayo baada ya habari hii kutoka, “Hebu fikiria mameli makubwa yanayoleta mafuta kila siku yanapaswa kulipa TPA shilingi ngapi? Sasa malipo mengi hayafiki sehemu husika maana kuna namna wanagushi kisha wanagawana na ni kikundi cha watu hao hao.”
Siyo uzushi wala siri. Watoto wa vigogo na vigogo wenyewe wanafahamika. Wako kwenye bandari zote, mipaka, viwanja vya ndege, mipakani, wizara, kwenye mabenki hasa BoT kwingineko kwenye ulaji wa haraka. Wapo mbuga za wanyama, madini, biashara hata kwenye balozi zetu nje wapo ukiachia mbali kwenye vyuo vingi vikuu vya nje walikopolekwa ima kwa scholarship za watanzania au fedha ambayo wazazi wao waliwaibia watanzania.
Lazima wakamatwe, wafilisiwe na ikiwezekana wafungwe. Kuwapata si kazi.  Ni rahisi kuwasaka na kuwafichua watoto wa vigogo au ndugu zao walioajiriwa kwa upendeleo huku vijana wetu wengi wanaomaliza vyuo hawapati kazi ukiachia mbali kuendelea kuhangaishwa na kongwa la kudaiwa mikopo waliyochukua wakati wakisoma.  Chukua orodha ya wafanyakazi wa serikali, utagundua uoza mwingi tu unaoifanya Tanzania isiwe na tofauti na Zaire ya Mobutu au Libya ya Gaddafi kuhusiana na madaraka ya kutumika kifamilia. Ilianzia ikulu hadi kwa mfagiaji ambapo kila kigogo kwa ngazi yake aliunda utawala wake wa kijambazi na kula kwa mikono na miguu tena bila kunawa. Kama mainzi, tabaka hili licha ya kula kwa miguu na mikono bila kunawa, hunya na kutapika humo humo linamolia kama mainzi. Wakati tukilalamikia umaskini –huku utawala uliopita ukisifika kwa kwenda nje kuombaomba na kujidhalilisha –tunambiwa kuwa nchi yetu inaweza kuwa na mabilionea wengi walioupata ukwasi kwa njia ya kuliibia taifa ukiachia mbali kuajiriana kwa kujuana. Mtoa habari anasema wameiba na kuwa mamilionea wenye utajiri wa kukufuru. Ndiyo, wanakula na kunya mle mle wanamolia kama mainzi.
Gazeti liliendelea kuandika tena kwa kushangaa, “Watu wanauliza mbona kuna watu wanatolewa kafara? Kuna mtoto huyu wa Kova, Masoud Suleiman Kova. Yeye ni jipu kubwa tu, na yeye ndiyo pilot kwenye mambo haya kule kwenye ICDs. Sasa jana walikamatwa, lakini kundi lake hawakuwekwa ndani, unaona ehee?”
Kama serikali ya Magufuli haitatafuta namna ya kuwabaini na kuwatia kufuli vigogo wengi waliopenyeza watoto wao kwenye sehemu nyingi za ulaji nchini, zoezi lote linaweza kuonekana kama kushughulika na wasio na washitiri wa kuwakingia kifua wahalifu wanaotuhumiwa kwa kupoteza mabilioni ya shilingi za umma. Hivyo, tuseme bila kumung’unya maneno kuwa serikali lazima itende haki katika ukamataji, ufikishaji mahakamani na ufilisi wa wezi wanaoendelea kuhangaisha taifa letu na kulifanya maskini wakati wao wakigeuka mabilionea wa kutupwa bila sababu. Kama alivyowahi kuuliza rais Magufuli: Hivi nani alituroga jamani?
Kinachoendelea kubainika ni kwamba vigogo serikalini na kwenye taasisi zake waligeuza taifa letu mali yao binafsi na watoto wao na marafiki zao. Rejea rais Mstaafu Benjamin Mkapa alivyojitwalia mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira yeye na familia yake na marafiki zake. Ajabu, umma ulipotaka awajibishwe, rais mstaafu Jakaya Kikwete–kwa kujua uoza ambao alikwisha kutenda–alisikika akiwa nchini Sweden akisema: Muache mzee Mkapa apumzike. Kwa Kikwete mapumziko ya Mkapa yalikuwa bora kuliko maslahi ya umma! Kama haitoshi, umma sasa unashuhudia vigogo wa juu kwenye idara fulani ya serikali wakigombea nyumba waliyouziana kitapeli utadhani taifa letu lina nyumba za kutosha hadi linapata za kuwauzia vigogo wake. Huu ni wizi tu hata kama unatendwa na wakubwa. Kuonyesha mfumo wetu usivyo na uadilifu wala aibu hata kidogo, wezi wa namna hii wanajianika hata mahakamani wakigombania mali ambayo kimsingi ni ya wizi. Je kuna nyumba ngapi vigogo wameuziana? Je kuna watoto wangapi wa vigogo, marafiki na makuwadi zao kwenye taasisi za umma? Kuna haja ya rais Magufuli kutumbua majipu haya ya kweli ya kimfumo badala ya kukimbizana na mwizi mmoja mmoja au kikundi huku akifumbia macho vigogo ambao kimsingi.
Chanzo: Dira, Feb., 22, 2016. 
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 19:31 No comments:

Boozer to take racism demo to Bombey


            I didn’t intend to revisit racism issue that I tackled last week. But after one bigot wrote me a provocative email, I’ve decided to revisit the same so that I can send a clear message to all those who think they’ll keep on taking us for a ride.
            One reader who goes by the name of Brave Hindi wrote me as thus: You stupid kalu son of Absii (Monkey son of Chimp in Hindi language) stop poking your nose into the issues that you don’t know. Don’t make a big deal out of nothing. Do you think your slurs can change anything God ordained? Kalu, kalu kalu kalu ad infinitum.
            After reading this stupefying message, I decided to stand my ground especially after being called monkey son of chimp.  If I were the late Chris Mtikisa, I’d have started calling these guys kalus and absiii so that they can feel the pinch Swahili feel when they’re called monkeys and chimps.
            To prove that I’m the tough gong as an old boot, I’m now planning to fly to Bombey; and demonstrate to condemn racism done by the same people whom the Caucasians call people of colour.  Firstly, before flying to Bombey, I’m intending to secure an appointment with president John Kanywaji Mugful to tell him to cleanse this boil aka jipu. I’ll tell him to issue an order to kick out all rich tenants from our National Hindi, sorry, Housing Corporation houses so that they can move to their bungalows they rent out to foreign experts. If they think we are kalus and absiii who can’t talk, they’re dead wrong. So, too, I’ll ask Mugful to rent these houses to the victims whose mbavu za mbwa were demolished in Msimbazi valley so that–for the first–time they can have a taste of their national cake.
            My demo in Bombey’ll be a one-man one aimed at showing Hindis that even Swahili are not kalu or absiii. If the authorities in Bombey fail to assure me that all this nonsense will stop, I’ll come back to Bongo and start the campaigns of calling their brethren kalu and absiii.
            Apart from seeking to end this madness resulting from mental sickness and ignorance, I’ll raise funds intended to establish the biggest university in Africa that’ll admit all Swahili that are currently facing racism in Hindi. Moreover, I’ll raise more funds to establish an ultramodern hospital that’ll admit all Swahili who waste their money going to Apollo.
            Thirdly, I’ll raise more funds to make sure that we educate boozers in commerce so that they can control their economy that–for many generations–was left in the hands of the same dudes calling us absiii pointlessly.  I’ll seek to debunk the myth that Swahili can’t run their economies while we’ve a lot of Kimaros, Mengis, chingas, kingas, and Alawas who can do business more humanly and competently than the kalus, sorry, those who call Swahili kalus and absiiis. Yes, kama mbaya mbaya. We’re tired of racism and disrespect to our boozers. Again, even Swahili should learn favouratism from these guys. You find a Swahili skipping Swahili’s shop to buy from those calling him kalus. We too have to blame. Stop your roho-ya-kwanini mentality.
            Let me take this opportunity to argue Swahili to start supporting one another instead of shying away from each other in doing business something many those calling us kalus exploit and become super rich. There’s no any magic vis-à-vis t hose calling us kalu’s success except complicity with our corrupt govt high-ranking officers who prefer to do simian biz with these guys simply because they can easily get rid of them when their scandals surface. Now look how we all are referred to as kalus.
            Given that Dr Kanywaji has decided to cleanse our hunk, I’ll meet with him to tell him to audit National Housing Houses to see if there are some that have already illegally been vended to those discriminating us and calling us kalus. If no actions are not taken back home, surely, this will prove how kalus and absiii we’re.
            These Hindis calling Africans kalus and absiiis are lucky. If the boozer would have been on the helms, Amin’s exercise would have been reenacted. So, too, from now, I urge president Mugful to make sure that all Bongolalalanders with dual or multi citizenship should choose one as they renounce others failure to which he’ll be giving those calling us kalus and absiiis bullets to finish us.
            Given that travelling to Bombey needs a lot of dosh, please, whoever that reads this iconic piece aimed at fighting racism should generously contribute so as to make my journey-cum-demo a success. My account number is 00001111a00000 Swiss Bank, Lausanne. As for those who call us kalus and absiiis, I know you’ve made a lot of dosh from exploiting those you call names. If you want me to reduce my speed of taking on you make sure you contribute a lot to show that you don’t support your brothers and sisters in Hindis who call Swahili kalus and absiiis. 
Source: Guardian, Feb., 21, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 06:00 No comments:

Saturday, 20 February 2016

What we did not about president Jacob Zuma


Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 18:12 No comments:

Mlevi agoma kusimamia uchakachuaji kwa M7


            Baada ya wajinga fulani kutaka kunigeuza juha kama wao wakitaka eti niende kwa M7 kuangalia uchakachuaji wakati nikijua kura zitaibiwa na imla atachukua na kuweka waa, niliwatolea nje kuwa siwezi kugeuzwa juha na majuha. Hata hivyo, wapo waliokubali kuwa majuha kwenda kubariki wizi wa mchana ambapo M7 alishashinda hata kabla ya kuchakachua. Sijui kama kunaweza kuwapo uchaguzi huru na wa haki zaidi ya uchakachuaji.
            Baada ya maswahiba wengi kunisihi niende, niliwazodoa kuwa wao wa Zenj umewapiga chenga, watakuwaje na uchungu wala udhu wa uchakachuaji wakati uchaguzi umewashinda kiasi cha kuendelea kuishi kwa kitatange kiasi cha kukwamisha juhudi adhimu za my friend Dk Kanywaji? Shame on them! Walidhani mimi ni mtu mzima hovyo kama jamaa yangu wa Loliyondo alivyokubali kugeuzwa bunga kwenye kubariki wizi na kuhalalisha haramu kule kwa M7.
            Kama kusimamia uchaguzi dili basi nitasimamia ule wa kwa Joji Kichaka baada ya bwana mdogo Obamiza kuachia ngazi. Kwa vile huyu dogo alikuwa mwanafunzi wangu wakati nikifundisha kwenye chuo kikubwa cha Havard, nitaenda kumpa tafu na kumpongeza kwa kumaliza ngwe bila shobo wala uchafu kama jamaa zangu wa kayani ambao sasa wamegeuka vyangu wa kudandia kila mnuso baada ya mwalimu JPM Nyerere kuwatilia ngumu kwenda ughaibuni kuzurura na kuteketeza njuluku za walevi.
            Kwa tathmini yangu ya kilevi ni kwamba hakuna uchaguzi unaoweza kufanyika kwenye eneo la maziwa makubwa kutokana na kujikita kwa udikteta na udhalilishaji wa katiba ambapo miungu watu wanataka watawale na kufia madarakani kama Jimmy Kinyatta na Kamuzi Banda ukiachia mbali M7 na mdogo wake ka-Game. Nikiangalia kilichotokea Urundi kwa Nkurumbwiza na wenzake wakamgwaya, sina imani tena na domoghasia. Hivi unategemea nini toka kwa gendaeka ambaye amezoea kuchakachua kula kwa zaidi ya miaka thelathini sasa. Muulize M7 aliingia madarakani lini. Watoto waliozaliwa akiwa maulajini nao sasa wanasimama kumpinga lakini haoni hata aibu. Ama kweli wakati mwingine mtu mzima hovyo ukiachia mbali wengine kuzeeka vibaya. Kwa mijitu iliyokosa aibu ikatawaliwa na tamaa na njaa ustaarabu ni msamiati mgumu na adimu kwao.
            Kwa mtu mzima mwenye akili sawa sawa hata kama sina soksi nisingekubali kujiingiza kwenye wizi na kejeli kama hii eti kwenda kubariki udikteta unaoitwa demokrasia. Kiakili, huwezi kwenda kusimamia jizi lililokubuhu ndani ya kaya yake ukajidanganya kuwa utalikamata.  Lazima litakuzidi akili kwa kutumia mbinu ile ile ambayo limetumia miaka nenda rudi kuendelea kuwa kwenye ulaji. Kuna dawa mbili kukomesha jizi kama hili. Mosi, ni kuliambia tena kwa shinikizo liache wizi kwa kufuata kanuni za uchaguzi badala ya viini macho. Ukiona huna mamlaka ya kuingilia mambo ya ndani ya jizi hili unaamua kulisusa na kulisusia jinai yake ili usiwe sehemu yake. Huu ndio uoni wa watu wenye bongo zinazochemka na si haya manungaembe ya kifikira yanayoendekeza tumbo na kutafuta sehemu ya kugangia njaa na kupoteza muda kama  jamaa yangu aliyedanganywa juzi kuwa atakuwa dingi wa kusuluhisha waathirika wa Kadhafi wakati waliomteua waliambiwa wazi kuwa walikuwa wakimuunga mkono habithi Kadhafi hivyo hawana maana wala uwezo wa kuhusishwa kwenye zali na Ulibyani. Kama watasha wenzao wameshindwa hawa wamakonde ndiyo watakaowapatanisha wakati watasha wenyewe wanawabagua watasha na kuwaona kama kenge wa kawaida? Huu ndiyo ukweli hata kama unauma au kuwa wa kilevi. Again, who cares if somebody has gotten another opportunity of globetrotting after Dr Kanywaji put a pin on it? My friend Njaa Kaya, upo hapo hapa kaka?
            Tukiachana na hili la kwenda UG, ngoja turejee nyumbani. Mlevi hadi sasa anajiuliza nini kitafanyika baada ya kugundua kuwa kumbe magabacholi wanawaita waswahili kalu na abisiii yani nyani au sokwe. Baada ya kulalamikia hili na kutishia kuingia Bombey kufanya kitu mbaya, naona kama wachovu wamesahau na kurejea kwenye maisha yao ya kijungu jiko. Mtaliwa sana kama tabia yenu ni hii.
            Leo nataka niwape ushauri wa bure.  Ili kuondokana na hawa nguchiro wanaotubagua huku wakija kwetu na kutanua, tuanze kuacha roho ya kwanini ambapo mlevi akianzisha biashara zake wenzake wanamkwepa kwenda kununua kwa hao hao wanawaita kalu na absiii. Kwa tabia hii ya kutojitambua kweli nyinyi si absiii hata kalu? Kuna mambo mengine hata hayataki elimu kubwa au msokoto wa bangi. Ni suala la kutumia kichwa kufikiri badala ya kutumia masaburi. Sasa mmeishaambiwa mnavyodharauliwa, kunyonywa na kubaguliwa. Kama jamii mmeamua kufanya nini kama jibu ya kadhia hii ya kishenzi na kinyama.
Chanzo: Nipashe, DWb 20, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 11:26 No comments:

Thursday, 18 February 2016

Wale wenye asili ya Sauzi bila shaka watafaidi ujumbe huu

Baba twaja mbele yako
Mungu mfalme wetu
Sikiliza sala zetu
Twakesha maporini
tukipambana na shetani
Tuma wasaidizi baba
Wawapashe watu wote
Habari zako
Ufalme wako uje
Tutakwenda mataifa kwa mataifa
Kwa jina lako (mfalme)




Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 17:18 2 comments:

Hii kali ya Zenj!


Kwa hisani ya gazeti la Mwananchi
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 10:23 No comments:

Tuesday, 16 February 2016

Serikali itangaze mgogoro na India



            Kitendo cha binti wa kitanzania kupigwa, kudhalilishwa, kuchomewa gari na kuvuliwa nguo hadharani na wananchi wenye hasira mjini Bangalore India licha ya kuwa cha kibaguzi na cha kinyama, kimedhalilisha taifa letu. Hakuna namna nyingine ya kuelezea jinai hii itokanayo na ubaguzi–tena unaofanywa na jamii ambayo tumeifuga hata baada ya kuletwa na wakoloni kutuhujumu kwa kununua mazao yetu kwa bei nafuu na kuwauzia waliowaleta–ni cha kulaaniwa kwa nguvu zote. Kitendo hiki kinaibua chuki na dharau dhidi ya waafrika kwa ujumla wao vilivyokuwa vimejificha kwenye jamii ambayo tumekuwa tukidhani ni wenzetu kumbe siyo. Huu ni ushahidi kuwa–kwa wabaguzi hawa–hata wanyama wana thamani kuliko mtu mweusi.
            Kwa mujibu wa NDTV ya India, binti mtanzania alifikwa na balaa hili baada ya kijana wa Kisudan kumgonga mama wa kihindi jambo ambalo lilihalalisha mashambulizi dhidi ya muafrika yeyote waliyemuona mbele yao. Japo wengi wanaweza kurahisisha tukio hili kama watu wenye hasira ambao wako katika kila nchi, kitendo cha kulenga mtu kwa sababu ya rangi yake–na si ushiriki wake katika kutenda kosa–kinaonyesha ubaguzi na chuki vya wazi wazi dhidi ya waafrika. Sijui kama waliotenda jinai hii ya kibaguzi wanafahamu kuwa wana ndugu zao wateule wanaoishi kwenye nchi za hao hao weusi wanaowachukia, kuwabagua, kuwadhalilisha na kuwadharau. Je kama na wahanga wa ubaguzi huu–Mungu apishie mbali–wataamua kufanya jino kwa jino, kutakalika. Ndiyo, maana hakuna mtu mwenye akili zake ataonewa, kunyanyaswa, kubaguliwa na kudharauliwa asijihami kama mtu binafsi au jamii. Hii ni hulka ya binadamu yeyote mwenye akili timamu ingawa waafrika hawana silka na hulka ya ubaguzi au ulipizazi visasi. Hata hivyo, mambo yamebadilika.
             Tuseme wazi bila uficho wala woga. Kumekuwa na unafiki na woga wa kuwaambia wenzetu kuwa mfumo wao wa kibaguzi haupaswi kuwa nafasi katika bara hili. Ni bahati mbaya kuwa ni watu wachache waliokuwa na ithibati na uthubutu wa kuliona hili na kulisemea wazi wazi wakiongozwa na marehemu mchungaji Christopher Mtikila ambaye ukali wake angalau ulipunguza makali ya ubaguzi wa wazi.
            Pamoja na ndugu zetu wa kihindi kuishi nasi kwa miaka nenda rudi, wamejitahidi kuendeleza mfumo wa kibaguzi –utokanao na jadi yao ya matabaka, caste system–nasi, kwa woga, ujinga na hata ufisadi, tumeuvumilia na kuuzoea kana kwamba ni haki. Sasa unaanza kutugeukia ambapo watu wetu hawana hata uhuru wa kwenda kwao na kuishi bila bughudha kama wanavyoishi kwetu.  Ni vizuri unapoibua hoja kuitolea ushahidi. Hebu jiulize–kwa mfano–leo utaona waswahili waliooa au kuolewa na wazungu lakini si kwa wahindi. Kwanini tena kwa jamii ambayo tumeishi nayo kwa miaka mingi kama hakuna harufu ya ubaguzi ingawa suala la nani amuoe au kuolewa na nani ni haki ya mtu binafsi? Hata hivyo, haiwezekani kwa jamii nzima yenye watu wengi wasitokee wachache wakavunja mwiko huu wa kibaguzi kama hakuna namna ya kuzuia hili kutokea.  Kimsingi, ujinga wetu umelea huu ubaguzi. Wengine wana hata mashule yao binafsi kwa kisingizio cha dini na mambo mengine ya kijinga na kibaguzi. Wanaishi kwenye maeneo yao maalumu hasa katika kati ya miji kwenye nyumba za Msajili ambazo marehemu baba wa taifa alitaifisha baada ya kugundua zilivyokuwa zimejengwa kwa fedha iliyotokana na kuwanyonya na kuwaibia waswahili.
            Waswahili ni watu wakarimu lakini si wajinga na wapumbavu kiasi cha kubaguliwa wazi wazi hivi. Sijui kama kuna mbunge Mswahili huko India ikilinganishwa na hapa. Sijui kama kuna waswahili wanapewa hata huo uraia wa India ingawa hauna faida wala thamani kwao. Rejea Waswahili wajulikanao kama Jarawa kwenye kisiwa cha Andaman huko India ambao–pamoja na kuishi karne ya ishirini na moja–bado wametengwa na kuishi kama wanyama huku wenyeji wao wakiwatumia kama kivutio cha utalii. Je wao wangefanyiwa hivyo hapa wangefurahi?
            Hata hivyo, binadamu ana nini hadi ambague mwenzie wakati akijisaidia bila kutawaza au kuishi bila kupiga mswaki ananuka kuliko hata nguruwe? Heri mbuzi na ng’ombe wangetubagua na ingeleta maana hasa ikizingatiwa kuwa huwa hawatawazi wanapojisaidia wala kupiga miswaki kila uchao lakini bado hawanuki. Kwanini serikali ya India haiwaambii ukweli watu wao kuwa nchi nyingi za kiafrika –baada ya kuua huduma zao za jamii –zinatunisha hazina yake kwa kupeleka wagonjwa na wanafunzi kule ukichia mbali kununua bidhaa feki toka kule mbali na kuwahifadhi watu wao walioletwa na wakoloni? Najua ukweli huu unauma. Ila ndiyo ukweli ambao tunapaswa kuambiana ili tuthaminiane na kuheshimiana. Nani hajui kuwa baadhi ya wabaguzi hawa huwanyonya wafanyakazi wengi wa Kiswahili huku mamlaka zetu za hovyo zisifanye kitu kana kwamba hazijui uwepo wa jinai hii ya ubaguzi?
            Tumalizie kwa kuuliza. Nani atamshughukia nani ilhali wengi wao ni wawezeshaji wa kashfa za wizi wa mabilioni wakishirikiana na wezi wazawa wenye mamlaka. Rejea kashfa za escrow na Singasinga nyuma yake, mashamba, Chavda na rada, Vithlani ukiachia mbali kashfa ya ndege ya Valambia.
Chanzo: Tanzania Daima, Feb., 14, 2016.

Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 06:58 No comments:

Sunday, 14 February 2016

Are Hindis racists?



  I can see that guy shaking his head thinking I’m making this question up. No, the question’s been adapted from Indian NDTV (4 Feb, 2016) after a Bongolalaland girl–who happens to be the daughter of my best friend–was molested, beaten and unpainted. The NDTV wrote, “Are Indians racists? The question appeared to dominate social media and prime-time TV shows in the country on Wednesday after a disturbing incident earlier this week.”
            The NDTV went on reporting that “A 21-year old Tanzanian student in the city of Bangalore in southern India told the police that a mob pulled her out of her car before setting it ablaze on Sunday night. She said the mob then beat her up, molested and stripped her, and paraded her naked.” All hell broke loose after a Sudanese student knocked down an Indian woman. Thereafter, any Swahili seen around by gabacholis was a fair game. Interestingly, despite such brutality, there’s no call in Bongo to reciprocate by attacking Hindis. Guess well what’d happen had the situation been vice versa. Ironically, when the said girl’s molested, maltreated and beaten reports had it that the cops were there just enjoying a free movie instead of taking any action. How’d they bother while a Swahili’s being taught a lesson? This reminds me of Jarawa Swahili–who are trapped in a time capsule–in the Andaman Island where gabacholis go there to view them like animals. Again, if you look at the pigments of our skins some are even dimmer than those they deem to be the darkest. I don’t know if there’s a Swahili MP in Hindiland.
            You wonder. How can somebody’s fault be punished on another? For boozers who know how Northern Sudanese who view themselves as Arabs though they’re Swahili you wonder how can a Bongolalalander be substituted by an Arab?
            Again, the history of racism goes back many years ago when it’s found in Spain before brutish British colonial rule expanded it to all corners of the world. Historically, Hindis were brought by British to serve as middlemen who’d buy produce from Swahilis at throwaway prices and sell them to their masters. They’re imported under the pretext of constructing railway.  Hence, even after those who cloned them handed over our half-baked independence–thanks to our generosity–the post-colonial govt didn’t ask the Brits to take their burden with them.
            Coincidentally, the victim who’s molested in Hindiland’s a daughter of my best friend. So, you can connect the dots and see how I’ve vested interests in this criminality.  As I went to console him he said, “To be honest, when the news broke that my daughter’s molested and brutally beaten simply because another Swahili caused an accident, I remembered two dudes, Idi Amin, former Ugandan butcher and Chris Mtikila whose outbursts reduced racist behavior among the said caste members.”
            Another one who also was there to console our friend chipped in, “Show me any Swwahili-hindi couple in the streets of Bongo I’ll give you my cow. We see Swahili-zungu couples but not them. This shows they’re racists through and through.” I’d to chip in to warn my buddies about the unfairness of painting all people with the same brush. The victim’s didn’t buy into my views. He added, “Don’t you know they discriminate against housemaids even in our own hunk and our do-nothing govts do nothing about it? You wonder seeing earthlings who run away from miseries to come and prosper in Bongo to hate and discriminate against Swahili this way.”
            His friend added, “Didn’t you know this is Danganyika! If Chavda, Vithlan, setii Singasinga and other monkeys come and rob our boozers in conjunction with our homegrown robbers do you think they can respect or care about us?” I chipped in. Whose fault’s it if our homegrown thieves invite these racists to come and help themselves? The victim’s dad replied, “how can they respect us while those supposed to protect our rights and humanity are in bed with them? Didn’t you hear Dr. Kanywaji wondering how Hindiland could become a chief tanzanite exporter while the mineral is only available in the hunk on earth? There are a lot to wonder about if you like.”
            After failing to convince my friends, I decided to imagine what’d have happen if Swahili were as stupid and racists as those who brutalized my friend’s daughter.  I consoled my friend telling him that things have changed. And soon he can get the answer to this barbarity and bigotry. Those who think they’ll always get away with murder are wasting time and endangering their future. By the way, is there anything important a human has? If goats and cows can discriminate against me, I’d be happy but not stinking bin-Adam. Look at cows and goat. When they poo, they don’t use tissues or water. When they wake up, don’t brush their teeth. Yet they’ve never been malodorous like humans. Ironically, why don’t these racists appreciate the fact that Bongo’s always filled their vaults by consuming their substandard services and goods? Remember Apollo, universities where boozers send their kids to be discriminated against after butchering their own social services.
Source: Guardian, Feb., 14, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 08:31 3 comments:
Newer Posts Older Posts Home
Subscribe to: Posts (Atom)

Cordially and unlimitedly welcome to this blog.


Writing and reading are two different processes but which share the same goal-to educate, communicate and entertain.
It is my pleasure to have you as the guest of this tablet.
I, thus, warmly and always, welcome you to share ideas.
Importantly and eminently, shall there be anything amiss or you think can advance this blog, please donate it.
Allow me to humbly and kindly welcome you once again.
Nkwazi N Mhango- A Man And a Half

When wisdom brings no profit, to be wise is to suffer. Not all thoughts are good and constructive. Others are even worse than bullets. The good thinkers are the ones that think constructively for the manumission of all bin-Adams regardless their diversity. Mwl. Nkwazi N Mhango,
Canada.


Epistle to Afrophobic South Africa

Epistle to Afrophobic South Africa

Magufulification

Magufulification

BORN NUDE

BORN NUDE

Total Pageviews

Heko Rais Magufuli

Heko Rais Magufuli

DECOLONISING EDUCATION

DECOLONISING EDUCATION

Kudos President Magufuli

Kudos President Magufuli

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

The Family Friend of Animals

The Family Friend of Animals
Children's Book

Matembezi Mbuga ya Wanyama

Matembezi Mbuga ya Wanyama
Kitabu cha Watoto

Our Heritage

Our Heritage
Children's Book

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

Perpetual Search

Perpetual Search

Africa's Best and Worst Presidents

Africa's Best and Worst Presidents

Psalm of the Oppressed

Psalm of the Oppressed
Psalm of the Oppressed

AFRICA REUNITE or PERISH

AFRICA REUNITE or PERISH
A new approach towards empowering Africa

BORN WITH VOICE

BORN WITH VOICE

Soul on Sale

Soul on Sale

Soul on Sale

Nyuma ya Pazia

Nyuma ya Pazia

We are one

We are one

SAA YA UKOMBOZI

SAA YA UKOMBOZI

Feel at home

You are always welcome to this epistle again and again time after time, ad infinitum.


Most read Posts

  • Sarkozy’s Take on African Fat Cats a Welcome Move
    At last the chicken are coming home to roost! French authorities made a groundbreaking decision by culling three most corrupt African presi...
  • Napanga kuanza kuuza mitumba na si maneno
    Ingawa mimi si mtumba, napanga kuuza mitumba. Nimechoshwa na jamii ya mitumba. Kila kitu mitumba. Mitumba, mitumba mitupu. Siasa za mitumba...
  • Better or Bitter Life for all?
    When I deeply muse on how an arrogant and brutal cabal of hoity toity (Coverted Con Men (CCM)) is tirelessly hoodwinking and dividing th...
  • Africa's Becoming more Despotic and Nepotistic
    "King of Kings" Gaddaffi The seven-day 40th anniversary of Libya strongman’s autocratic rule and charade elections in Gabon whe...
  • Kuna siku tutataifisha haya mahekalu haki ya nani
    Taarifa kuwa waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alinunua nyumba kwa zaidi ya shilingi bilioni moja licha ya kuwastua wananchi na...
  • Nyangumi mdogo akutwa amekufa ufukweni BC
    Hii ni picha iliyotolewa ya Nyangumi aina ya Humpback ambaye alikumbwa na maji na kutupwa kwenye ufukwe wa bahari ya Pasifiki kwenye eneo l...
  • Kikwete, Charity Begins at Home!
    President Jakaya Kikwete ...
  • Kweli binadamu si chochote wala lolote, wamkumbuka huyu?
    Walioko madarakani mkiabudiwa kama miungu au sanamu kumbukeni vijana hawa hata baba zao  ambao maiti zao zinaoza jangwani. Ungewaambia...
  • Pinda kulia hakutoshi, awajibike
    INGAWA kilio cha Waziri Mkuu, Mizengo Peter Kayanza Pinda, kinaonekana kuyeyusha hasira za Watanzania kwa muda, kuna haja ya kudodosa zaid...
  • Hawa si wachungaji bali ni fisi na mbwa mwitu
    KUMEZUKA mtindo mchafu na wa rejareja wa baadhi ya wachumia tumbo na matapeli kumtania hata kumtumia Mwenyezi Mungu kufanya utapeli na ujamb...

Followers

Blog Archive

  • ►  2023 (20)
    • ►  January (20)
  • ►  2022 (208)
    • ►  December (14)
    • ►  November (14)
    • ►  October (20)
    • ►  September (20)
    • ►  August (12)
    • ►  July (25)
    • ►  June (22)
    • ►  May (18)
    • ►  April (13)
    • ►  March (18)
    • ►  February (18)
    • ►  January (14)
  • ►  2021 (323)
    • ►  December (23)
    • ►  November (34)
    • ►  October (26)
    • ►  September (13)
    • ►  August (19)
    • ►  July (21)
    • ►  June (29)
    • ►  May (25)
    • ►  April (23)
    • ►  March (43)
    • ►  February (29)
    • ►  January (38)
  • ►  2020 (290)
    • ►  December (33)
    • ►  November (37)
    • ►  October (28)
    • ►  September (35)
    • ►  August (31)
    • ►  July (26)
    • ►  June (17)
    • ►  May (21)
    • ►  April (18)
    • ►  March (15)
    • ►  February (17)
    • ►  January (12)
  • ►  2019 (160)
    • ►  December (8)
    • ►  November (7)
    • ►  October (12)
    • ►  September (9)
    • ►  August (27)
    • ►  July (18)
    • ►  June (18)
    • ►  May (11)
    • ►  April (11)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (14)
  • ►  2018 (162)
    • ►  December (12)
    • ►  November (6)
    • ►  October (13)
    • ►  September (10)
    • ►  August (20)
    • ►  July (9)
    • ►  June (14)
    • ►  May (9)
    • ►  April (16)
    • ►  March (21)
    • ►  February (17)
    • ►  January (15)
  • ►  2017 (306)
    • ►  December (20)
    • ►  November (23)
    • ►  October (20)
    • ►  September (26)
    • ►  August (31)
    • ►  July (31)
    • ►  June (34)
    • ►  May (26)
    • ►  April (24)
    • ►  March (20)
    • ►  February (28)
    • ►  January (23)
  • ▼  2016 (269)
    • ►  December (22)
    • ►  November (21)
    • ►  October (22)
    • ►  September (15)
    • ►  August (12)
    • ►  July (27)
    • ►  June (24)
    • ►  May (23)
    • ►  April (29)
    • ►  March (26)
    • ▼  February (27)
      • Magufuli anaishi jipu ikulu
      • Congrats king M7 on your victory
      • Nimemkumbuka marehemu Mashakada leo
      • Mlevi kumualika Obasanjo uchakachuaji Zenj
      • Hii ni bahati mbaya au kuna namna kwenye wizi wa m...
      • Huyu tajiri unamtathmini vipi?
      • Kijiwe chataka waliozima mita za mafuta nao wazimwe
      • Tuondoe Tanzania kwenye makucha ya vigogo
      • Boozer to take racism demo to Bombey
      • What we did not about president Jacob Zuma
      • Mlevi agoma kusimamia uchakachuaji kwa M7
      • Wale wenye asili ya Sauzi bila shaka watafaidi uju...
      • Hii kali ya Zenj!
      • Serikali itangaze mgogoro na India
      • Are Hindis racists?
      • Vita ya ufisadi: CCM wanamdanganya nani?
      • Mlevi kupambana na wabaguzi wa kigabacholi
      • Laiti watanzania wanamwelewa Dk Magufuli
      • Wikendi hii natulia na Ondarata toka Okakarara Nam...
      • Kijiwe chalaani ndata kuingia kudhalilisha wahishi...
      • Hii kitu ya akina Seif na Shein imenifurahisha
      • Tulaani udhalilishaji wa wabunge
      • Magufuli atumbue na majipu mikoani na wilayani pia
      • Paying tax is better than fake aid
      • Wiki hii nilifaidi muziki toka Burkina Faso
      • Somo: Ubomoaji nyumba mabondeni
      • Mlevi kuishatiki escrew The Hague
    • ►  January (21)
  • ►  2015 (399)
    • ►  December (34)
    • ►  November (24)
    • ►  October (22)
    • ►  September (34)
    • ►  August (29)
    • ►  July (37)
    • ►  June (22)
    • ►  May (32)
    • ►  April (35)
    • ►  March (46)
    • ►  February (47)
    • ►  January (37)
  • ►  2014 (502)
    • ►  December (47)
    • ►  November (49)
    • ►  October (47)
    • ►  September (37)
    • ►  August (40)
    • ►  July (42)
    • ►  June (30)
    • ►  May (35)
    • ►  April (47)
    • ►  March (44)
    • ►  February (39)
    • ►  January (45)
  • ►  2013 (400)
    • ►  December (37)
    • ►  November (27)
    • ►  October (31)
    • ►  September (26)
    • ►  August (34)
    • ►  July (39)
    • ►  June (28)
    • ►  May (40)
    • ►  April (44)
    • ►  March (39)
    • ►  February (26)
    • ►  January (29)
  • ►  2012 (598)
    • ►  December (27)
    • ►  November (26)
    • ►  October (27)
    • ►  September (30)
    • ►  August (47)
    • ►  July (95)
    • ►  June (86)
    • ►  May (119)
    • ►  April (83)
    • ►  March (23)
    • ►  February (17)
    • ►  January (18)
  • ►  2011 (261)
    • ►  December (20)
    • ►  November (19)
    • ►  October (20)
    • ►  September (21)
    • ►  August (27)
    • ►  July (12)
    • ►  June (15)
    • ►  May (20)
    • ►  April (27)
    • ►  March (32)
    • ►  February (24)
    • ►  January (24)
  • ►  2010 (205)
    • ►  December (25)
    • ►  November (23)
    • ►  October (23)
    • ►  September (23)
    • ►  August (17)
    • ►  July (13)
    • ►  June (12)
    • ►  May (10)
    • ►  April (18)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (16)
  • ►  2009 (163)
    • ►  December (19)
    • ►  November (14)
    • ►  October (11)
    • ►  September (6)
    • ►  August (12)
    • ►  July (9)
    • ►  June (11)
    • ►  May (20)
    • ►  April (22)
    • ►  March (14)
    • ►  February (12)
    • ►  January (13)
  • ►  2008 (191)
    • ►  December (12)
    • ►  November (11)
    • ►  October (14)
    • ►  September (15)
    • ►  August (16)
    • ►  July (23)
    • ►  June (10)
    • ►  May (19)
    • ►  April (16)
    • ►  March (19)
    • ►  February (17)
    • ►  January (19)
  • ►  2007 (33)
    • ►  December (13)
    • ►  November (20)

About Me

My photo
View my complete profile

Travel theme. Powered by Blogger.