The Chant of Savant

Monday 29 April 2013

Makinda: Nakuzimikia (You're my heroine)









Mpendwa Anna,
Kwanza, nisamehe. Sitakuita Anne kama unavyopenda kuitwa. Tunaokujua twajua wewe ni Anna na si Anne. Enzi za Mchonga na zile za alikwina uliitwa Anna. Anne inasound kisomi kuliko Anna. Umenikumbusha Musa Nnauye aliyejipachika Moses. Tuyaache.
Pili, nikufamishe.  Huwa nazimia vitu vyako hasa kuburuza--- sorry--- kuongoza Mjengo. Napenda unavyokomesha wapingaji. Wewe ni shujaa kwenye chama chako. Hawajui wewe ni kada nambari wani wa nambari wani? Walidhani utaruhusu wavuruge ulaji wenu? Imekula kwao!
 Nakupongeza, naibu wako Jobless Nduguy na fyatu Pita Sheukamba aka mzee wa f*ck you. Wamesahau Job alisema: Waishiwa wanakula bwimbwi? Je Pita alitoka kupata bwimbwiz au hajui maana ya fwaki you?  Tungejuaje anajua kimombo tena cha mitusi? Kazi kwa waliofanya makosa kumchagua wasijue anawakilisha tumbo na bangi zake? Siku hizi mitusi na sanaa ni sera ati. Ukisikia mheshimiwa kuishiwa na kuwa muishiwa ndiyo huku.
Naandika kukushukuru.  Staili yako ya kuwakomesha wapingaji imenisaidia kuwakomesha walevi kijiweni. Kama si kuiga mfano wako waingereza wauitao bulldozing or maumauing, ningeshapigwa chini zamani. Believe me. Ubabe wako uliniokoa na kusaidia kuendelea na ulaji wangu Kijiweni aka Mjengoni.  Hakuna kitu kinanikera kama wapingaji kujidanganya kuwa wana haki ya kufaidi demokrasia wasijue yenu ni domoghasia yenye wenyewe ambao ni nambari wani.
Acha nikupe ushauri wa chee. Akiamka mpingaji kutoa hoja hata kama ina mashiko bamiza. Akiinuka mwenzenu, hata kama anatoa pumba na kutukana fwaki you, minya aendelee kuwapa vipande vyao. Hawajui ulisimikwa hapo baada ya mzee Sam Sixx kukaanga chata pale aliposababisha kutoswa kwa Eddie Ewassa na baadaye mawaziri wengine?
Juzi nilisikia wapingaji wakilalamika kuwa unawaburuza na kupendelea chama chko. Noma ni nini? Hakuna kitu kiliniudhi nusu nijinyotoe roho kama wapingaji eti kutaka kuja na hoja ya kukuwajibisha wewe na Jobless ambaye wanamtuhumu kuongea bila kufikiri. Hii ilinitokea Mjengoni kwangu hivi karibuni. Si walevi walitaka kuni-impeach wakidai ninaiba pesa yao na kuwaburuza! Kama kawa, nilitumia mbinu yako ya kuwatoa nje ya Mjengo na kupeta kama ulivyowafanyia akina Tundul Issu.
Kwa vile mimi ni mpenzi na shabiki wako, kijiweni kwetu wananiita Makinda na majina mengi mengine ya hovyo. Hakuna waliponikera kama kusema eti mzee Sam Sixx kweli alikuwa kiongozi wa kupigiwa mfano tofauti na wewe na mimi wanaotuona kama kanyabwoya na mawakala wa mafisadi.
Baada ya walevi kuzidiwa kete si waliamua kufuatilia mambo yangu ya ndani kama vile ndoa na nyumba zangu ndogo! Walipojua sijaoa walikuja na mambo ya kijinga kutaka mkuu wa Mjengo wetu lazima awe ameoa au kuolewa! Pia wapo waliosema eti mkuu wa Mjengo lazima awe amesomea sheria na awe msomi kweli tofauti na wewe wanayesema eti una elimu ya kuungaunga. Kwa vile mimi ni msomi mwenye shahada magunia, waliamua kukutumia kujiridhisha. Baada ya kuona wamezidi niliwapa live na kuwaambia: You can go to hell kama Joni Malisela alivyowapa akina Agwe zama zile. Hata hivyo, wana bahati. Angekuwa fyatu Pita Sheukamba angewaambia fwaki you all.
Una habari? Yeyote aliyefanyiwa nchezo huo hudhani wote wanafanyiwa hivyo! Kuna mlevi alituacha hoi alipouliza, “Huyu anayewowa na kufwaki watu anapata wapi jeuri? ashukuru. Zingekuwa enzi za Mchonga anayewambia wenzie fagi you angefwagiwa yeye ajikute hana kazi.” Alisema atakwenda Mwisho wa Reli kuwatafsiria mitusi waliokuchagua fyatu Pita ili wasimchague tena kuwaangusha watu wastaarabu kama wao. Yupo aliyesema kuwa Pita alitukana wana kaya wote, wewe hata mkuu maana Mjengo ni sehemu takatifu.
Walevi ni viumbe wa ajabu! Kweli walevi ni walevi katika kila kitu! Hawakosi la kusema utadhani wanasiasa! Si juzi walisema eti huna lako.  Eti kila ufanyalo sharti uwe remote controlled na mafisadi waliokusimika kulinda uoza wao! Laillah illallah! Niliposikia matusi haya nilirusha ngumi na kuwajeruhi kadhaa ndipo waliamua kutoka unyoya na kikao kwisha bila maridhiano. Sikuona haja ya kuendelea kuwatoa nje wakati wenzao wakibakia na kuendeleza libeneke ya kutuacha uchi.
Hata hivyo, kabla ya ngumi kufumka niliwapa laivu wanaokuchukia kuwa mwenye wivu ajinyonge.  Kama ulisimikwa na mafisadi kwanini nao inawauma nini?
Kuhusu la elimu niliwapa wazi kuwa kwenye kaya yetu elimu nzuri au uzoefu kwa wanaojuana chini ya dhana ya kulindana na kulipana fadhili, elimu na uzoefu si muhimu. Kama mawaziri walighushi wazi na wanaendelea kutesa kwanini nawe usitese, kupeta na kupetuka? Hata hivyo, nashauri. Badala ya kuendelea kusumbuliwa na madai kuwa hukubukua ningeshauri uongee na chuo kimoja feki ndani au hata ng’ambo wakuzawadie PhD kama yule rais wa Unyasani alivyofanyiwa hivi karibuni akafikia hata kutumia pesa ya walevi kubadili picha zake ili ziwe na neno Dk.
Isitoshe, hautakuwa peke yako. Huoni akina Dk Emmy Nchimvi na Dororas Kamala ambao walizoea kuitwa madaktari wakati walikuwa kanjanja hadi juzi niliposikia kuwa wamehitimu shahada za udaktari? Hata hivyo, nina wasi wasi kama wamehitimu zaidi ya kuhitimishwa. Kama walishindwa mwanzo kutambua umuhimu wa kubukua hadi wakaghushi kwanini wasiendeleze libeneke yao hasa ikizingatiwa kuwa hata mkuu anakubaliana na jinai yao?
Nilipowabana walevi watoe ushahidi kama ambavyo huwa unawafanyia wapingaji mjengoni, walisema kuwa zilipotolewa shutuma kuwa ulikuwa umeandaliwa na kusimikwa na mafisadi hukupinga wala huwa hutaki kujadili suala hili. Niliwauliza: So what? You can go to hell. Hata hivyo, hawa jamaa ni wapumbavu wa kutupa. Walitaka ujibu shutuma ili ziibuke nyingine nyingi ambazo hazijulikani siyo? By the way, ule mjengo wako wa Sinza Uzuri umeishakamilika? Naomba unialike kwenye ufunguzi wake. Vipi ile barabara ya Mto wa Ng’ombe uliyokuwa umefunga ushaifungua?
Sista Anna,
Acha nimalizie kwa kukupongeza kwa kulinda amani ya kaya yetu kwa kuwakomesha wapingaji. Napendekeza waishiwa wa chama chako wawe wanaingia Mjengoni na kamusi za mitusi ili kuwakomesha wapingaji. Pia Pita Sheukamba achaguliwe mwenyekiti wa kamati ya mitusi akisaidiwa na Mwehuhuyu Michembe kuwakomesha wanaosumbua ulaji wenu.
Nisalimie Pita, Job na Lameck Michembe. Wambie nazimia vitu vyao pia.
“Blessed be.”
Chanzo: Nipashe Jumamosi Aprili 27, 2013.

Nani ataibuka mshindi kati ya watumishi hawa wa mafisadi?


Hakuna ubishi. Kuna mgogoro unarindima ndani ya Chama Cha Mapiduzi tangu lilipoporomoka jengo la ghorofa 16 kwenye mtaa wa Indira Gandhi jijini Dar ambapo makundi ya kifisadi yanagombea maslahi binafsi. Kwa anayejua jinsi wafanyabiashara fisadi na hatari wa kihindi wanavyowatumia watawala wetu kama nepi, atajua ninachomaanisha hapa. 
Hakuna jambo limenishangaza kama kusoma taarifa kuwa mkuu wa mkoa wa Dar Said Mecky Sadik anangojea matokeo ya tume ya uchunguzi wa kuporomoka wa jengo hasa baada ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, kutoa agizo jengo jingine kama lile karibu na lile liloporomoka yote yakimilkiwa na mpuuzi mmoja. Kwanini kungoja ripoti ya tume ilhali chanzo cha mkasa huu kinafahamika? Yaani mara hii wamesahau hata maneno ya mlinzi jirani na eneo lile aliyewaambia wajenzi baada ya kushuhudia wakifanya vitu vya kipuuzi kuwa walivyokuwa wakifanya siyo? Hivi inahitaji tume na ripoti kujua kuwa mejengo husika yalijengwa kinyume cha sheria viwango na taratibu? Je kinachofanyika hapa si ufisadi mwingine wa kuokoa mwingine ni nini? Je Sadik anadhani watanzania wote ni mataahira kama yeye anavyetumiwa kama nepi? Je katika kipute hiki nani ataibuka mshindi kati ya hawa watumishi wawili wa mafisadi ambapo mmoja anatumikia wahindi na mwingine serikali fisadi? Kwa habari zaidi BOFYA hapa.

Alex Massawe: Matajiri Uchwara, siasa za kijambazi na jinai


Taarifa za kukamatwa kwa mfanyabiashara mashuhuri lakini mwenye kutia mashaka nchini zinatufungua macho. Habari zilizokaririwa na vyombo vya habari ni kwamba Massawe alikamatwa nchini Afrika Kusini kutokana na makosa ambayo polisi wa Tanzania hawakuwa wazi kuyaeleza.
Massawe mwenye mrorongo wa biashara alisifika sana alipoakamatwa miaka ya karibuni akihusishwa na kufadhili ujambazi mbali mbali nchini. Tokana na ukweli kuwa Massawe ni mmojawapo wa wafadhili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kesi na kashfa hii ya aina yake ilizimwa kinamna ingawa wachambuzi tulishapata ukweli. Kukamatwa kwa Massawe na majambazi wengine wakubwa kulitokea baada ya rais Jakaya Kikwete kujigamba kuwa anawajua majambazi wakubwa wote, wauza unga, wezi bandarini, mafisadi na wengine kutokana na kuwa na orodha yao. Wengi wasiojua mchezo mzima wanaendelea kuuuliza: Kama Kikwete hanufaiki na utajiri huu uchwara utokanao na jinai anakuwaje mgumu kuwakamata wahusika? Wanaouliza swali hili wanasahau kuwa bila ujambazi wa EPA na ule wa kuwachafua wengine huenda Kikwete asingekuwa madarakani! Hapa sijui ni jambazi gani amkamate nani. Mungu siku zote hamfichi mnafiki. Baada ya kulindana kwenye ujambazi wao sasa wanaanza kuuana wao kwa wao kutokana na laana ya kuwaibia watanzania maskini. Hata polisi washikwe kigugumizi juu ya maendeleo haya mapya ya  kuumbuka kwa majambazi, umma utajua tu. Kwa habari zaidi BOFYA hapa.

Sunday 28 April 2013

Who’s Kibanda? Vs who’s Wasira?













Today we're interrogating the bunkum of who’s who especially in doing fatuous stuff of pointlessly self-dressing down. Nothing left me cheesed off like the Minister of State in the Presider’s Office Steve Wassira’s irresponsibly turbo- charged hoo-ha. He’s quoted recently defending the ever-tarnished Taifa Institute of Sabotage and Setbacks (TISS) after being alleged to have abducted and tortured Absalom Kibanda the Chair of TEF and Managing Editor of Habari Corporation (200) on March 5.
Out of the ordinary, Wassira went ballistic averring that Kibanda’s too small for TISS to abduct and torture. Kumbaya! He added that it’d have crossed his mind had those abducted and tortured been CHADEMA chair Freeman Mbowe or General Secretary Dr. Wilbrod Slaa. It is all-out disconcerting to note that a minister in the top office doesn't know that no institution in the hunk’s the mandate of torturing or harming anybody; be he small or big. Such careless and frozen remarks left many dismayed. No sane mind would risk thinking such a minister would ridiculously jabber that way. We’re still baffled.  How can  Wassira fail to know that all human beings are equal and are entitled to living without any harassment leave alone torture and abduction?
Wassira’s boneheadedness made many analysts draw a single conclusion that TISS does abduct and torture people save that it deals with bigwigs. Given that we've over four famous leaders whose deaths have remained a mystery, we now know who’s likely to be behind their demise. There’s a big secret Wassira knows that we don’t know.  Does Wassira know who killed former PM Edward Sokoine who died in April 12, 1984?
Is TISS behind a sudden but suspicious death of Horace Kolimba in March 13, 1997? What of the death of then TISS Tsar, Lt Gen. Imran Kombe in June 30, 1996? Were those police alleged to have killed Kombe TISS’s agents or just flamed to save face? What of the death of Zakayo Wangwe in July 20, 2008? Wassira, if squeezed, may unravel the mysteries of those deaths.
Again, let’s answer the major question of who’s Wasira.  He’s but a former NCCR-Mageuzi’s wizard of Oz currently a good cadre of CCM after returning from hibernation to NCCR-Mageuzi to do away from political cold. So too, Wasira’s a wino whose mouth lost touch with brain and reality. There’s no border between him and Pita Sheukamba aka Mr.Screw you aka F*ck you and Andulrahman Kinamna who said that opposition doesn’t like development while he’s accused of smuggling our animals and their products to Asia. Furthermore, Wasira’s a toff that sleeps Mjengoni and lies that it is because of medication. The other day another political wino, Jobless Nduguy, said that some heshimiwas do sniff bwimbwiz.
Indeed, Wassira’s a gruff dude known as Tyson who wrongly thinks is better than others especially by pointlessly accusing others of the scandals he himself commits.
As for Kibanda, is he a small person by Bongo’s standards? Don’t get me wrong. I don’t intend to create classes among Bongolalalanders however they’re always there. If Kibanda is small, nobody and useless as Wasira would like us to believe, why his boss, Jakaya Kikwete, went to Milpark Hospital in South Africa to wish him well? Kibanda might look small in the eyes of Wassira. In the eyes of our constitution, every citizen’s somebody. Apart from that, Kibanda’s an innocent person who earns his bread legally. He’s a professional whose works speak volume. So too, Kibanda, as a senior journalist, is a voice of voiceless. Above all, Kibanda nary proved to be stupid or crazy just like those vuvuzelas and dashers that blindly belittling him have time and again proved to be. I know Kibanda. He didn't live depending on lies like fake and double-faced politicians who can jump from one party to another not simply because they’re enjoying their constitutional rights but due to looking for green pastures. It is sad to hear Wassira condemning the same opposition that received him at the time he’s desperate after CCM refused him to stand for Member of Parliament in 1995. Kweli shukrani ya punda! Who knows? Given that Wassira can easily change, maybe in 2015 he’ll attack the same CCM the same way he’s currently attacking the opposition. If I were president Kikwete, I’d sack Wassira forthwith for embarrassing my government and me altogether.
Another bankrupt ‘do-gooder’ acting like a macaroni that left me stitched is Mad  Moody Safe Khatib who said that Chadema’s laden with adulterous who should not go to Ikulu which he said is sacred. Is Kikwete safe hither?  Isn't this better than thou?  True, a baboon does not see its ass!  If anything, this is the art of speaking without bothering to think. The mouth says this while the brain says that. Wameishiwa hawa.
Mbowe and Slaa shouldn't take Wassira’s utterance lightly but rightly.  Who knows? Was Wasira trying to preempt what’s to come for them if not to intimidate them? Maybe, just maybe, Wassira still believe that TISS can torture even kill these leaders and get away with it as it is in the cases of Kibanda and Ulimboka or other mysterious deaths of Sokoine, Kolimba, Komba and Wangwe to mention but a few.
Today’s wisdom is a double quote. “Scarecrow: I haven't got a brain... only straw,” The wizard of Oz.
“How can you talk if you haven't got a brain? I don't know, but some people without brains do an awful lot of talking,” L. Frank Baum, the Wonderful Wizard of Oz.
Source: Thisday April 29, 2013.

Wapenzi wa anga angalia hiii


Friday 26 April 2013

Tuingie weekend na unyenyekevu


Nimeamua kuwakaribisha kwenye tafakari wakati tukianza weekend hii. Ingawa sitatoa tafsiri ili kila mtu atafsiri kivyake, nawakaribisheni kwenye kujumuika pamoja. Sikiliza wimbo huu toka Busokololo Kabwe Zambia wakati ukitafakari. BOFYA hapa.

Tunaadhimisha siku ya kuzaliwa Muungano au Mgongano?


Imetimu miaka 49 tangu mataifa ya Tanganyika na Zanzibar kuungana na kuzaa Tanzania. Hakika miaka 49 si haba. Je tunasherehekea Muungano au Mgongano? Je watanzania bado wana hamu na hamasa na Muungano? Je nani anafaidi Muungano ukiondoa watawala wa pande zote mbili? Maana ukisikia manung'uniko toka pande zote unashangaa mantiki ya kuendelea na kuwa na Muungano wenye kila aina ya migongano miongoni mwa wananchi wa pande mbili. Ilifikia mahali watu wa visiwani wakahisi kama watu wa bara wanawanyonya ingawa hawana cha kunyonya. Ilifikia mahali tukaanza kuitana majina ya machogo na upuuzi mwingine hata kusingiziana jinai.Kwa vile watanzania wanaanza kujitambua, kuna haja ya kuwasihi wauangalie upya Muungano ambao umegeuka kero. Blog hii ni shabiki wa umoja wa Afrika. Tofauti ni kwamba Umoja huu ujengwe na waafrika wenyewe badala ya watawala. Huwa nashangaa kuona Tanzania inavyopoteza muda na raslimali kujiingiza kwenye Jumuia ya Afrika Mashariki wakati huo huo ikishindwa kutatua kero za Muungano wake. Je watanzania tutaendelea kufanyiwa majaribio hadi lini? Wakati tukitafakari hali ya Muungano wetu, majibu tutakayopata yatusaidie kupinga kuingia kichwa kichwa kwenye Jumuia hasara ya Afrika Mashariki ambayo inatumiwa na nchi wanachama kutaka kutuibia ardhi na raslimali zetu. Haiingii akilini kwa nchi yenye ardhi nzuri na kubwa na raslimali kuungana na vijiinchi visivyo na lolote bali mzigo wa ongozeko la watu na watu wasio na ardhi.
KILA LA HERI NA TAFAKARINI.

Thursday 25 April 2013

Doping even in animals!


We used to hear doping  that used to involve humans who wanted to win and make more money. Nobody would risk thinking that animals would dope just like humans. We still remember the famous doping scandal involving cyclist Lance Armstrong.  Recent reports have it that it came to light that in UK horses were introduced to drugs in order to win horse races. For more information CLICK here.

Angalia watawala wetu wanavyotula


Kuna taarifa kuwa viongozi wastaafu wanatengewa pesa nyingi kuliko baadhi ya wizara. Hii imefichuliwa na vyombo vya habari hivi karibuni. Wengi huwa tunajiuliza, kwanini watumishi wengine wa umma wanaostaafu wanaachwa wajifie huku viongozi na wake zao wakiendelea kutunyonya na kutanua huku sisi tukiteseka? Huu licha ya kuwa uroho na roho mbaya, ni ujambazi wa wazi unaofanywa na wanajiita wenye madaraka. Je ufisadi huu wa kimfumo ambao umegeuka ukoloni mamboleo ukitekelezwa na wakoloni weusi utakomeshwa na nani na lini kama siyo sisi na sasa? Je umma unaridhika na wizi huu wa mchana chini ya dhana ya viongozi wastaafu? Inashangaza na kusikitisha zaidi kukuta kwenye orodha ya viongozi wastaafu kuna watu kama Edward Lowassa ambaye aliachia madaraka bila kufikia muda unaopaswa kisheria ukiachia mbali kuondoka kwa kashfa iliyolisababisha taifa hasara ya mabilioni ya fedha. Inaumiza kukuta mijitu kama Benjamin Mkapa anayejulika wazi kujitwalia Machimbo ya Makaa ya Mawe ya Kiwira na mkewe aliyeliibia taifa kuendelea kuongezewa pesa itokanayo na kodi ya mlipa kodi maskini waliyemwibia. Je tumegeuka taifa la hovyo na kuridhika na hali hii? Tafakarini.
Kwa habari zaidi BOFYA hapa.

Wednesday 24 April 2013

Tuwaunge mkono wakulima wa korosho walioamua kujikomboa


Si siri tena kuwa kondoo ameamka kiasi cha kumtembezea fisi mateke! Ingawa wakulima wa Tanzania wamekuwa wakitumika kama mtaji mkubwa wa kukiweka Chama Cha Mafisadi (CCM) madarakani, upepo umeanza kubadili. Hivi karibuni huko mkoani Lindi wakuliwa wa korosho waliamua liwalo na liwe. Waliamua kusema kwa herufu kubwa ENOUGH IS ENOUGH. Vurugu zilitokea na nyumba kuchomwa moto huku serikali ikikirika kuwakamata iliowaita wachochezi wakati ni wapigania haki na ukombozi wa kweli. Hakika yale niliyoandika kwenye kitabu changu ambacho hata hivyo hakijapokelewa vizuri na watawala cha SAA YA UKOMBOZI yanaanza kutumia nikiwa kijana bado. Namshukuru Mungu na kuzidi kuhanikiza nikiwataka watanzania kusimama kidete na kidedea kuhakikisha tunawaondoa hawa nunda wala watu na manyang'au walitukalia kooni kwa muda mrefu. Inafurahisha kuwa habari hii sasa inaanza kupiga hodi kwenye vyombo vya kimataifa. SAA YA UKOMBOZI IMEWADIA TUSIMAME NA KUJIKOMBOA.
Kwa habari zaidi BOFYA hapa.

Open Letter to M23



I must admit. My observation of the conflict between M23 and the authorities in the Democratic Republic of Congo (DRC) is of an outsider. So too, I must clearly say that I heard or read a letter you sent to heads of states and citizens of Malawi, South Africa, and Tanzania, warning them about the danger sending their troops in DRC poses.
To a Conflict Resolution Studies professional, your message served two or more purposes. First, it is a true warning due to the fact that a war has no eyes. Second, it creates and inflicts fear, and if possible, acts as a drive to encourage peace talks.  To me, this is but an olive branch to new forces coming into the big picture to pick and tell Kinshasa to talk under certain favourable conditions for you. Third, it alienates and intimidates your enemy so that you can easily take him down. Fourth, it asserts your authority and the zeal of seeing to it that what you want is achieved by all means. Generally, what you did is a PR strategy that your enemy has always embarked on.
Looking at our geopolitical stance, no side will win in this imbroglio. What’s been going on is but wastage of life and property knowing that there won’t be a winner. The conflict in DRC is not a two-person zero-sum game kind of equation.  It is lose-lose situation shall the war go on. Again, it can be turned around and become a win-win situation.
Being under unipolar command currently, the dynamics of ‘wars of liberation’ have changed. Under the Cold War, it was easy to get backing from two antagonistic sides. Currently, the world is under one order. So too, you need to underscore that even the emerging powers especially China are talking to those with powers in their hands. It is cheap to do business with a government in power than supporting a group to take up power. Their interests are second to none. You can kindly refer to what’s going on in North Korea whereby China is openly siding with the international community thanks to safeguarding its interest and extending its tentacles.  Also, the world is facing an economic crisis. It thus needs a break from war.
Even a few avenues of support especially from business interested sides and arms dealers does not suffice to make things look good on your side. Seeking peace is pivotal and the only way out of the impasse in DRC and the whole region at large.
I understand you’d like to paint your enemy with your own brush. Likewise, your enemy would like to do the same. Nobody has a soft spot in the heart for the other. This is what has oiled the cogs of your killing machines. Again, looking at the recent ‘self-handing over’ of your former enemy-turned ally, Bosco Ntaganda aka Terminator, chances are that he is going to spill the beans. This won’t do you good.
The sure means of getting out of this conflict safely is  by means of round-table talks. You can take this to the bank - once you decide to sit down and discuss, support will come even from those you didn’t expect. At this level and time you’ll be able to achieve what many failed to achieve - everlasting peace as a means of developing your mineral-rich country.
I am saying this after looking at the history of conflicts in Africa. When I look at people like Charles Taylor, Laurent Gbagbo, Lubanga, Jean Pierre Bemba and others, I find that peace talks stand as the only viable and reliable means.
Sadly though, clinging to the barrel of the gun means committing more atrocities and tarnishing your already tarnished image more. The world is seeing your atrocities more vividly than the other side. Looking at how Eastern DRC is traumatized, methinks. You have the land but not the population. How can you have the people to support your legitimacy whilst what the people in the area have known is war and trauma, atrocities and poverty?
This conflict is sucking in many more players who obviously sympathize and cooperate with authorities in Kinshasa. Given that the UN has already authorized the take on you, believe you me, think about talking instead of fighting.
Let me wind up by inviting you to face the reality; and, if possible, seek conciliators out of political and diplomatic circles. Academics can do a good job to see to it that they bring three players namely authorities in Kinshasa, the International Community and M23. If you need that, just let me know so that I can shop around and put forth some proposals about who fits to take the task. I believe this is another hunch.
Source: The African Executive Magazine April 24, 2013.

Kibanda ni nani? Wassira ni nani?


HAKUNA kauli imekera na kuhuzunisha wengi kama ile iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Steven Wassira aliyeuliza kwa kebehi kuwa ‘Kibanda ni nani?’
Kauli hii itokanayo na upogo na ulevi wa madaraka iliwakilisha mawazo ya serikali.
Maana tangu Wassira aliporopoka, serikali haikumkana wala kumkaripia. Hii maana yake ni kwamba kauli yake ni kauli ya serikali.
Wassira alikaririwa akiwa bungeni hivi karibuni akisema kuwa haamini wala haiingii akilini kuwa Usalama wa Taifa (TISS) wanaotuhumiwa wanaweza kumteka na kumtesa Mhariri Mtendaji wa Habari Corporation (2006) na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Absalom Kibanda Machi 5 kwa vile ni mtu mdogo.
Yaani si saizi ya TISS. Kumbe Watanzania tunatathimiana na kuthaminiana kwa matabaka!
Kukoleza kejeli na matusi yake ya nguoni kwa Watanzania, Wassira alisema kama wangekuwa wameteswa Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe au Katibu Mkuu Dk. Willibrod Slaa ingeingia akilini! Je, kauli ya Wassira ilimaanisha nini? Je, kuna mpango wa kuwateka na kuwatesa Mbowe na Slaa? Je, kama TISS ‘wanashughulika’ na wazito ina maana Wassira anaweza kuwajua waliowaua watu maarufu kama vile Edward Sokoine (Aprili 12, 1984), Horace Kolimba (Machi 13, 1997), Lt Gen. Imran Kombe (Juni 30, 1996) na Zakayo Wangwe (Julai 20, 2008)?
Maana kauli ya Wassira kwa wachambuzi na wajuzi wa mambo inatoa hitimisho moja kuwa TISS ina jukumu la kuwateka na kuwatesa hata kuwaua wazito kama tuliowataja hapo.
Ni ajabu TISS hawakujitokeza kupinga wala kumkaripia. Je, walimtuma aseme aliyosema? Muhimu Mbowe na Slaa wawe makini wakijua fika wanatafutwa. Maana lisemwalo lipo kama halipo laja. Wassira hata kama ni mropokaji si mwendawazimu.
Laiti Jeshi la Polisi lisingekuwa linatumika kisiasa, lilipaswa kumbana aeleze anachojua kuhusiana na Kibanda.
Inasikitisha na kutisha kuona waziri mwenye hadhi ya Wassira kutojua hata haki za binadamu wala ukweli kuwa hakuna taasisi yoyote hata iwe kubwa namna gani yenye mamlaka ya kumtesa au kumdhuru raia hata kama ni msukuma mkokoteni.
Inasikitisha na kuudhi kuona waziri mzima hajui kuwa Watanzania wote ni sawa na wanapaswa kulindwa na serikali yao. Ni uzembe na mawazo mgando kiasi gani? Nitashangaa sana kama Rais Jakaya Kikwete hatamwajibisha kwa kumuaibisha na kumwangusha ukiachia mbali kumtukana na kumuonyesha kama kiongozi wa wenye mamlaka.
Hata hivyo, tumshukuru sana Wassira kwa kutoa mwanga kuhusiana na matukio yaliyotokea huko nyuma maana yalikuwa kitendawili kabla ya kutujuza haya.
Sasa tuangalie swali la Wassira ni nani? Kwa wanaomjua, Wassira ni mmojawapo wa wanasiasa wenye utata na wapenda madaraka.
Ni Wassira huyu huyu aliyekihama Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujiunga na NCCR-Mageuzi pale alipokosa nafasi ya kugombea ubunge mwaka 1995.
Ni ajabu kuwa Wassira huyu huyu anausakama upinzani uliomhifadhi kipindi kile alipokuwa amepigwa teke na CCM anayoitetea.
Kilichofanyika alipohama Wassira si kufaidi haki ya kikatiba ya kuhama toka chama kimoja kwenda kingine bali uchu wa kutaka kuwa mbunge alioupata kabla ya kuvuliwa mwaka 1996 na baadaye kuadhirika na kujirejesha CCM akijikomba na kupewa ulaji alionao sasa ukimlewesha na kujiongelea hata bila kufikiri.
Wassira ni kati ya wanasiasa ambao vinywa vyao vilishakata mawasiliano na vichwa. Hana tofauti na Peter Serukamba aliyetukana matusi mazito bungeni asichukuliwe hatua.
Wassira ni mbunge anayesifika kwa kusema hovyo na kulala bungeni akisingizia madawa bila kutoa uthibitisho.
Pia Wassira ni mwanasiasa mbabe na kichwa ngumu ambaye amethibitisha sifa hizi kwa kujiita ‘Tyson’ ambaye kila mtu anamjua alivyokuwa akijidhalilisha ulingoni hadi kufikia kumng’ata mwenzie sikio kama ishara ya kushindwa kuzuia hasira zake.
Wassira pia husifika kwa kuwatupia wenzake madongo hata juu ya madhambi anayotenda kama alivyowahi kusema kuwa wapinzani wanawaita wake za watu vyumbani wakati ndani ya CCM wapo wanaotuhumiwa kwa hili na wasijibu.
Je, Kibanda ni nani? Kibanda ni mwanataaluma ya uandishi wa habari na mwandishi wa habari mwandamizi na Mtanzania anayeishi kwa jasho lake na si posho za makalio ambazo upinzani umekuwa ukipigana ziondolewe.
Kibanda ni Mtanzania kama mwingine asiye na makuu wala asiyejisahau kama Wassira.
Ingawa Wassira anamuona Kibanda kama mtu mdogo asiyepaswa kuwa na thamani, kitendo hiki ni tusi kwa bosi wake yaani Rais Jakaya Kikwete ambaye alikwenda Afrika Kusini anakotibiwa Kibanda kumjulia hali.
Je, Wassira ana maana Kikwete alikwenda kule kumsanifu Kibanda au alikwenda kule kwa dhati? Kibanda anaweza kuonekana mdogo mbele ya Wassira lakini si mbele ya katiba ya nchi yenye jukumu la kuwalinda Watanzania bila kujali vyeo, kipato, rangi, dini, itikadi na mengine kama hayo.
Kwa ufupi ni kwamba Kibanda ni mtu mwadilifu asiye na hatia ambaye ni sauti ya wasio na sauti kutokana na taaluma yake ambayo anaitumikia kwa ufanisi mkubwa kiasi cha kuwatia hofu akina Wassira.
Kibanda si mwanasiasa nyemelezi na aliyefilisika kimawazo kama wale wanaouliza kuwa Kibanda ni nani?
Nadhani tofauti ya Kibanda na Wassira ni kwamba Kibanda si mropokaji, mjivuni wala mlevi wa madaraka.
Bila kusema mengi, tumalizie kwa kuwataka Watanzania wachukue tahadhari na watu kama Wassira na Taasisi ya Usalama wa Taifa ambayo imekuwa ikituhumiwa kuhusika na jinai mbalimbali kama vile kuteka na kutesa watu na kuwalinda mafisadi.
Ila ni vizuri Wassira na TISS wakajua kuwa wapo hapo walipo wakifaidi vinono hadi kulewa na kupayuka hovyo kutokana na madaraka na pesa ya Watanzania.
Hakika Mungu hamfichi mnafiki. Wassira amejifunua, kazi kwetu kumsoma na kufanyia kazi kauli zake.
Aliyosema Wassira yangesemwa na mbunge wa upinzani angekuwa ndani akisota. Kila kitu kina mwisho. Tumalizie na nukuu hii. “Sina ubongo… bali mrija.”
Chanzo: Tanzania Daima Aprili 24, 2013.

Ghorofa laporomoka Bangladesh na kuua zaidi ya 80


Wakati watanzania wakionekana kusahau na kusuasua juu ya kuporomoka kwa ghorofa la mtaa wa Indira Gandhi, huko bara Hindi mambo yanazidi kuwa magumu. Mjini Dhakar nchini Bangladeshi limeporomoka na kuua zaidi ya watu 80. Blogu hii iliwahi kuuliza uhusiano wa kuporomoka kwa ghorofa la Dar es Salaam na yale ya India. Ukiangalia mmilki wa ghorofa lililoanguka na lile linalopaswa kubomolewa anatoka huko huko. Je Tanzania na Afrika kwa ujumla inaanza kuingiza ustaarabu wa kishenzi wa ujenzi hatari kama ilivyo huko bara Hindi? Kwa habari zaidi BONYEZA hapa.

Tuesday 23 April 2013

Nimemkumbuka Leonard Dembo "Musoro we Nyoka"

Wapenzi wa Sungura hebu tujumuike pamoja kwenye kitu shiri ya  Kangwara Toka kwa Marehemu  Kwangwari Gwaindepi au Leonard Dembo mwanamuziki ambaye viatu vyake havijawahi kuvaliwa na yeyote nchini Zimba.

Monday 22 April 2013

Is Museveni becoming another Gaddafi?

President Yoweri Museveni holding a bag of money

News that Ugandan Strong man Yoweri Museveni doled out money to youths left many baffled.  Again, Museveni behaviour of dish thousands of Dollars out to those he chooses is not new to Ugandans who are used to it. To them, Museveni is president Moneybag like former Libyans strong man Muamar Gaddafi who used to do the same wherever he toured. While Gaddafi was offering big sums, some of his citizens were living in abject poverty just like Museveni's. Recently, Museveni offered a sackful of money to Busoga Youth Group which observers say it was $ 100,000. Does it mean that Museveni does not keep his money in bank? Does Museveni keep money like former Malawi president Bingu wa Mutharika in whose room police discovered bags of dollars and other denominations after is death?
 Again, how did Museveni make this money? Is he donating the monies as president or as Museveni and individual? Is this the right way to contribute to Youths' development or  just the other way of bribing them? For more information CLICK here.

Minister and MPs arraigned for extortion in a foreign country

A Ugandan  Minister and two Members of Parliament were arrested by Indian police when they attempted to extort over $ 20,000,000 from an investor in Mumbai. Uganda authorities have kept mum saying that the issue must be resolved in India where the offence was allegedly committed. This happens a few weeks after Uganda strong man Yoweri Museveni asserting that he abhors impunity. Museveni was quoted as saying he abhors impunity during the swearing-in of Kenya's president Uhuru Kenyatta. What happened shows that many African leaders are used to such malpractices and this is why many bogus investors have been coming to Africa and getting away with a lot of wealth without doing anything and if they do, they just offer substandard services. Currently, Tanzania's  many investors in communication sectors especially telephone. Again they're duping and ripping Tanzanians off while the authorities are just watching. Maybe, this is being tolerated due to the true that the said investors have already dined and wined the biggies in the upper echelons of power. For more information CLICK here.

Sunday 21 April 2013

Hekalu la Rwakatare lazidi kuitesa serikali

 Hekalu hili la bei mbaya lilipozinduliwa na Getrude Rwakatare aliyejipachika uchungaji wanaojua jinsi dini zinavyotumika ima kuwaibia maskini au kuficha biashara haramu walihoji. Baadaye zilitoka habari kuwa limejengwa kwenye eneo lisiloruhusiwa kisheria hivyo kupaswa kuvunjwa sawa na wengine waliokuwa wamejenga kwenye eneo husika ambalo ni mkondo wa bahari. Hivi karibuni sakata hili limeibukia bungeni ambako mbunge wa viti maalumu Esther Bulaya (CCM) aliamua kulivalia njuga. Wenye kufuatilia tunangojea kuona hili suala litapigwa dana dana hadi lini. Sambamba na hili tunangojea kuona lile jengo la gharofa 16 la Mtaa wa Indira Gandhi lililoamriwa na waziri Anna Tibaijuka kubomolewa litabomolewa lini. Kwa habari zaidi BOFYA hapa.

What Bongo boondoggle-cum- Bongo bondage!


In Bongo where brain’s used criminally, any doodle can get away with it. In this part of screwed up world, one may say: Self-help and boondoggling on public offices is the only thing venal creatures living there know.  In doing so, sadly tough, the majority ---wishing would be a part of robbing party--- is perishing in bondage thanks to the activities of a cabal of boods.
No research no right to chonga. Tell me. Aren't kleptos behind Kagodamn, EPA and other thuggery a criminal-turned politicians? What’s up Roast-tamu Aziz, Eddy Lowasa, Endru Chenge and Jake Kikwete?
The other day I heard the economy was growing. I wonder. How could the economy grow at the tune of 8% while our foreign debt does the same at 400% (according to CHADEMA)? In such a situation, is there any true growth or bookish and cooked one? How can there be any growth amid corruption and drug peddling as Kangi Lugola (CCM) put it that some ministers and other bigwigs are good cheapjacks of be it mihadarati or drugs stolen from public hospitals, dispensaries and whatnot? Other badasses forged even their academic credentials.
As I wondered, there came this ad infinitum sacriligo involving robbing the public dosh in almost all ministries, departments, local governments and whatnot as the report of Comptroller and Audit General (CAG) unearths every year.
Logically, I see no rationale in having CAG’s office whose reports are sat on years in, years out. We always hear of CAG reports with all damning implications.   No single bin-Adam’s ever been charged or being punished all the more.
Always, in our gaffe-and-flaw-prone hunk the question is: Why could the government dress itself down by fearing and protecting drug barons, tax evaders and other criminals? Does it mean that these killers are the part of it or a government in its own light? If not, why’s it buffed them? Lao moja nini?   This country bwana, trust no boondoggler. Those thought to be clean aren’t.  Those thought would bring changes are changed themselves. Tamaa Bwana. Everybody wants to get rich by all and any means!
Guess what. When Kikwete said he knows all drugs dealers, thugs, corrupt officials and whatnot, I thought he’d take on them in lieu of ending up being soft on them. Seven years down the line, nothing’s ever come forth. Methinks this was another sanaa.
 The other day one geezer said that Kikwete’ll deal with all criminals he knows after retiring.
Bongo’s always funny in its own ways. It’s the only hunk on earth whose kit and caboodle of doodles can dubiously congregate and divide public houses among themselves without being whacked. Funny enough, the same criminals still holler that whatever they do is in the interest of people! To make things worse, when they congregate to ruin the hunk, receive fat perks called sitting allowances! Who’d believe that sitting on us pays this way? Fat perks for just farting around!   Indeed, Bongo with it boondoggles, is where crimes pay and criminals are heroes and heroines.
I don’t want to sound alarmist.  Again, didn't you hear of thugs that used to godfather and midwife Chama Cha Maulaji (CCM)? They’re arrested temporarily.  Thence, nothing’s ever been heard. Unacheza na pesa?
I’m waiting to hear government’s responses regarding its bigwigs especially Emmy Nchimbi, Mwilugu Mchembe and Taifa’s Institute of Sabotage  and Setbacks (TISS aka Uhasama wa Kaya) allegedly to be involved in gunk guff of sabotaging opposition using terrorist methods. Shame on them! Can this tell why Nchimbi’s forgery scandals have nary been dealt with? Mchembe, too, is said to have used somebody’s name in school. As for Riz Kiquette, ‘hanging’ on his dad’s back’s become monotonously sickening. Huu ni ukupe per se.
Bongo’s second to none in terms of plundering and stealing from paupers. Investors, especially fake ones, and most criminals can come and conspire with corrupt government officials and make away with billions of dosh. It has reached a point at which some government officials would conspire with corrupt politicians to rob the central bank and those responsible are waheshimiwa all the more! These bêtes noires have turned the Garden of Eden into a dungeon unnecessarily thanks to their myopia and greed. They preach water and drink wine!
Bongo’s the only hunk on earth where lies are turned into policies without the public waking up and stand up against it! Do you remember the say that Bongo’s an island of peace? Do people with albinism, elderly and retirees-especially those of the defunct East African Community- enjoy this ersatz peace? True, in Bongo, if you’re not a good freeloader, you’re as good as dead. Your rights will be vended to tarts by political mongrels.
Ours is the hunk in which a few rump-fed ronyons can mercilessly amass wealth while the majority cascades in abject poverty. Sadly, the same will still stomach calling this good life for all! Ironically, they refer to an all-you-can-deem-doom business of vending the people.
Ours is the hunk in which you can sleep Mjengoni and such shameful act is rewarded by being paid allowances. Though this can be seen as being naïve, blimpish or even giddy, I’m comfortable to submit that I see as Bongo Boondoggle Bongo-cum- Bondage thanks to Bongolalalanders’ sheepishness.
Source: Thisday April 22-28, 2013

Saturday 20 April 2013

Natafuta mjenzi Bongo atakayenijengea ngoma hii


Nilialikwa kuapishwa Uhuru Kenyatta

Naona yule anacheka akidhani ni kamba. Soma ujue ilikuwaje. Kuarikwa Kenya unastuka ingekuwa kwa Obama si ungekata roho! Kenya ukiuliza imekuwaje, wanajibu ishakua. Seriously, nilialikwa na kushiriki kuapishwa rais wa mpya ambaye si mpya wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Wengi hawajui uhusiano wangu na Kenyatta wala Moi Kibaki. Hiyo siri yangu na personal issue.
Wengi walishangaa kusikia nikitambulishwa kabla ya marais waliohudhuria. MC, kwa manjonjo, alisema, “Namleta kwenu rais asiyetambulika na kukubalika wa walevi wote duniani mstahiki mtukufu Nkwazi Mhango. Wengi walipigwa na kihoro wasijue nami ni rais tena ninayejulikana.
Ghafla Kenyatta alinitania akisema, “Wali ku mutongolya wa njohi, yaani ulikuwa wapi kiongozi wa pombe?” Bila kujivunga nilimjibu, “Lehe kanjohi ka uthamaki wa forori ya Muratina na Mwomboko.”
Nilimtania kuwa urais umevuka tena mto Chania na kurejea Kiambuu toka Nyeri. Alicheka sana na kushangaa ninavyojua utani wao wa asili baina ya watu wa Kiambuu, Kiambaa, Gatundu na hata Kangema na wa Nyeri, Othaya, Tetu, Githakwa na Ithekahuno.
Muda ulikuwa hautoshi. Aliniomba niwe mshauri wake mkuu kuhusiana na kilevi. Sikukubali wala kukataa. Nilimwambia kuwa nitafikiria. Siwezi kukueleza yote tuliyoongea.
Maana mambo mengine ni yetu wakubwa si makapuku wala walevi wa kawaida kama wewe msomaji wangu.
Tulicheka sana na kukumbatiana kwa furaha hasa baada ya kutoonana kwa muda mrefu. Mara ya kwanza tulionana nchini kwa Joji Kichaka akisoma wakati ule nikiwa visiting professor wa falsafa. Nilimsaidia sana huyu dogo kiasi kwamba hawezi kunisahau. Mara ya mwisho tulionana mitaa ya Muthangari na Gigiri tulipokuwa tukipata kanywaji pamoja na washirika zetu wengine ambao nisingependa niwataje hapa. Dogo alishangaa kufahamu kuwa nafahamiana na jaji mkuu aliyemwapisha Dk. Willy Mutunga. Hayo tuyaache.
Hakuna kilichonivutia kama ahadi ya Uhuru Kenyatta ya kulinda raslimali, mazingira na maslahi ya Kenya. Dogo alisema bila kumung’unya kuwa atahakikisha analinda raslimali za Kenya na mazingira kwa ajili ya vizazi vijavyo
Pia aliahidi pesa yote itakayopatikana toka kwenye raslimali husika itatumiwa kwa adabu na nidhamu
Maneno ya Kenyatta yaliniacha na maumivu sana kuona Tanzanite inavyoibiwa huku wachukuaji wakija na kuchimba madini na kujiondokea na mifweza huku wakituachia mishimo na mabalaa ya kimazingira. Hivi nani alituroga yarabi?
Hakuna aliponiacha hoi kama pale aliposema kuwa atahakikisha uhusiano na majirani zake hasa Bongolalaland unadumu ili aweze kujipatia ardhi aongezee kwenye ile aliyo nayo ambayo ina ukubwa sawa na mkoa wa Arusha. Pia alisema atahakikisha anaunganisha Kenya na nchi jirani ili kuwawezesha watu wake wasio na ardhi waende kule na kujitwalia ardhi madini na raslimali kutokana na wajinga fulani kuchezea vitu hivi.
Kwa tunaomjua alikuwa akirusha kijembe kwa majuha wanaochezea raslimali na uchumi wa mataifa yao. Aliporusha hili dongo nilimuona jamaa yangu mmoja toka Bongo ambaye kwa leo simtaji akikenua meno wakati roho ikimuuma. Nilijisemea moyoni kuwa kumbe kimwana cia Kamau wa Ngengi ni noma!
Baada ya kuongea na Uhuru nilikwenda kuongea na mzee Daniel arap Mwai ambaye alifurahi sana na kuniambia kwa Kiswahili chake kibovu, “My friend ukuje tubulahi pamoja my project has won at last.” Baada ya kukumbatiana na kuamkuana na mzee Nyayo niliamua kumuasa amwambie dogo abadili baadhi ya ahadi zake.
Kwa mfano aliahidi kutoa laptop kwa kila mwanafunzi wa shule ya msingi bila kujua kuwa Kenya yote haina umeme na kwamba watoto wa maskwata hawana chakula wala viatu.
Hivyo laptops alizoahidi wangeziuza kwa watoto wa mafisadi kwenda kununua unga. Tulikubaliana na kuagana ndipo nikajikunja kwenye laptop yangu kumwandikia email agwambo Raila Odinga ambaye alikuwa Sauzi kumjulia hali Mandela na kuepuka kukirihishwa kushuhudia ulaji wake akipewa mtu mwingine.
Alinijibu haraka kuwa kwake Mandela was better than anything except God alone. Nilimpa pole ya kuzidiwa kete kwenye kile alichoona ni uchakachuaji na uchafuzi wa uchaguzi. Anyways, siasa wakati mwingine ni mchezo mchafu.
Hakuna mtu alitia aibu na kuchefua watu kama jamaa yangu M7 aliyechemsha kwa kuishambulia ICC akidhani anamsaidia dogo. Alijigamba kuwa anachukua ufisadi wakati ndicho chakula na hewa yake. Nilitaka niamke nimzabe mabao ila niliacha kwa vile bodigadi wake wakijitia kujua nkawaumiza.
Mna habari kuwa nilitambulishwa kwa habithi wa Sudan anayejiita mwarabu wakati ni mmakonde tena mwenye machale nikakataa? Mie sio kama wajinga wanjinga wanaoendekeza nakuchekacheka na kushikana mikono na maadui na kila habithi kwa vile nao wameficha uhabithi wao.
Wajua kuwa baada ya sherehe ya kuapa nilifanya kitu ambacho kililetea kaya yangu heshima kubwa? Ilikuwa ni pale makamu wa Kenyatta alipopotosha historian a ukweli kusema eti mabaki ya mtu wa kwanza yaligunduliwa Kenya wakati ni Bongo tena Odivai Gorge. Niliudhika nusu ya kunasa mtu mabao hadi Kenyatta akashangaa.
Hata hivyo Rutuo aliniandikia SMS akiniomba msamaha kwa vile alisema kuwa alikuwa amehemkwa nilimsamehe na kuelekeza hasira zangu kwa majuha walioshindwa kuitetea Bongolalaland yangu. Nilishangaa kuona ujumbe wa Bongolalaland ukikenua macho badala ya kudai afute kauli yake maana hii ilikuwa ni kutuibia haki yetu ukiachia mbali kutudhalilisha.
Hii imenikumbusha kisa ambapo mzee Mchonga alitaka kufungulia jeshi baada ya hawa jamaa kudai mlima Kilimanjaro uko kwao. Baada ya hapo wanadai karibu kila kitu kuanzia Kiswahili, Serengeti hata Tanzanite viko kwao huku jamaa zangu wanaopaswa kuwatolea uvivu wakichekelea kama vile hawana akili! Hayo tuyaache.
Baada ya kumaliza shughuli nilianza kuwaza mantiki ya kumzawadia Moi Kibaki jumba la mabilioni ya shilingi na mshahara na marupurupu bila kufanya kazi ni nini kama si wizi wa siasa za kijambazi za Kiswahili za kuwaibia makapuku.
Jitu lina mijumba kama serikali halafu linaongezwa mengine wakati wananchi wakilala njaa! Nilijionea huruma. Nikistaafu urais wa walevi nitapewa michupa ya gongo na misokoto ya bangi. Kweli wanajua kututenda!
By the way, if I attended the inauguration or not, if I was invited or not and if what I’ve said is true or not what’s it to do with you? Think twice. Again, I’m just kidding. Tafsiri nyepesi:Kama nilihudhuria kuapishwa huko au la, kama nilialikwa au la na ni vipi kama nilichosema ni kweli au siyo, inakuhusu? Fikiria mara mbili. Ninatania
Walevi wa Roundabout shule ya Uhuru mpo! Smile!
Chanzo: Nipashe Jumamosi Aprili 20, 2013.

Friday 19 April 2013

Polisi wakamata rais wa zamani



Kiongozi wa zamani wa Pakistan Parvez Musharraf alikamatwa jana  usiku nyumbani kwake nje kidogo ya mji mkuu Karachi. Musharraf anakabiliwa na mashitaka ya uhaini yaotkanayo na kusimamisha katiba ya nchi alipochukua madaraka kwa njia ya kupindua serikali mwaka 2001. Alitawala hadi 2008 kabla ya kuachia madaraka kukimbilia Uingereza ambako alikaa uhamishoni hadi aliporejea hivi karibuni akitaka kurejea kwenye siasa bila mafanikio. Kwa mwaka huu Musharraf anakuwa rais wa pili kukamatwa na polisi na kufunguliwa mashitaka baada ya rais wa zamani wa Zambia Rupiah Banda ambaye hivi karibuni alikamatwa na kufunguliwa mashtaka ya ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka. Kukamatwa kwa watawala hawa wa zamani ni somo kwa watawala wa sasa wanaotumia madaraka vibaya bila kujua kuwa kuna siku yatawaponyoka na wataonja joto ya jiwe. Kwa habari zaidi BOFYA hapa.

Tuesday 16 April 2013

ICC and Kenya: Museveni Got it Wrong



The Hague
I will be shocked if the legal fraternity in Kenya and East Africa in general won’t react towards recent salvos leveled by Ugandan Strongman Yoweri Museveni. Museveni’s recent attacks on the International Criminal Court (ICC) must be condemned. During the swearing-in of Kenya’s new president Uhuru Kenyatta, Museveni saluted “… Kenyan voters on...the rejection of the blackmail by the International Criminal Court (ICC) and those who seek to abuse this institution for their own agenda." Museveni’s remarks, which amount to the contempt of court, reveal that most likely, he does not respect the courts in Uganda.
Kenyans did not vote for President Kenyatta and his Deputy, William Ruto, based on indictment. They voted on the basis of the belief that the duo would govern Kenya well. So too, Kenyan elections were not about rejecting or endorsing the ICC; they were about getting a new leadership after the one that was in power lapsed its constitutional term in office. Simple! I don’t know how the victims of the 2007- 08 Post-Election Violence felt when they heard Museveni’s remarks.
Museveni attacked the ICC pointlessly. The ICC has nary been an ambulance chaser. Whatever issue that is brought before the ICC is brought by the way of application from individuals or countries looking for legal settlement. This is what happened regarding Kenya’s ICC case. Kenya went before the ICC seeking its intervention in trying PEV. What is wrong here? Why didn't Museveni wait for the ICC to reach its verdict and say whatever he wants to?
Is Museveni saying what he is saying just because his file on alleged atrocities in DR Congo has not been opened? It is still early Mr. Museveni! Even Charles Taylor once daydreamed that his crimes would not be brought before the light.
"I was one of those that supported the ICC because I abhor impunity," Mr. Museveni says. If this is true, why haven’t his consigliore implicated in multi-million scandals been brought to book? Why was he forced to reimburse donor money using public coffers?
"I am confirming that we have paid the Irish [and] we shall pay the others (donors) who want their money back…We are making a lot of progress on that front,”  Says Museveni’s deputy secretary of Treasury, Keith Muhanikizi. If Museveni ‘abhors’ impunity as he’d like everybody to believe, why did he pay the monies back by even committing another crime of breaking into the treasury instead of letting the implicated personalities in the scandal to face  the judicial process? Is this the way Museveni abhors impunity - by blessing it?
Media in Uganda reported of massive theft involving donor money. At least $22.2 million meant for recovery and development activities in northern Uganda and Karamoja was allegedly swindled, infuriating donors who, in a meeting with President Museveni, demanded for a refund of their stolen cash.
Kenya’s ICC indictees are innocent until the ICC rules otherwise. Kenyans know what is going on. They don’t need any tutor to teach them what it is. I urge all those who wrongly think like Museveni to respect the ICC and the intelligence of Kenyans.
In sum, Kenyans did not vote along the lines of who was indicted or not but they voted for those they wanted, believing these would stir and man their nation. Saying that Kenyans voted for Kenyatta and Ruto simply because they’re indicted is to belittle them so to speak. This should not be accepted.
Source: The African Executive Magazine April 17, 2013.

Wajue maadui wakubwa wa taifa la Tanzania


Hivi karibuni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kiliamua kuwaanika magaidi wa kitanzania wanaolindwa na serikali ambayo nayo inaonekana kuwa ya kigaidi. Hii ni baada ya CCM ikishirikiana na Usalama wa Taifa ambao umegeuka kuwa Uhasama na Zahama ya Taifa kutengeneza video iliyolenga kukionyesha CHADEMA kama chama cha kigaidi. Ni bahati nzuri kuwa CHADEMA walistukia mchezo mzima na kuamua kuanika ukweli. Kitendo cha CHADEMA licha ya kuwa cha kizalendo, kimeufungua macho umma wa watanzania wanaojali kuwa kumbe wanatawaliwa na genge la waharifu na magaidi wanaojificha nyuma ya madaraka ya umma. Kwa mfano, tumejua ni kwanini shutuma za kughushi zinazowakabili baadhi ya mawaziri, wabunge na mabalozi hazishughulikiwi.
Vinara wa ugaidi huu ni waziri wa Mambo ya Ndani Emanuel Nchimbi anayedaiwa kughushi shahada ya udaktari na Naibu Katibu mkuu wa CCM, Mwigulu Nchemba anayetuhumiwa kutumia jina la mtu mwingine kuweza kusoma sekondari. Je watanzania wataendelea na ukondoo wa kujifanya hayawahusu wakati yanawaumiza vibaya?Kwa habari zaidi BOFYA hapa uone na kusikia mkanda mzima kama ulivyoanikwa na CHADEMA.

Mtoto wa rais wa zamani Wade akamatwa



Mamlaka nchini Senegal yanamshikilia mtoto wa rais wa zamani wa nchi hiyo Karim Abdulaye Wade kwa makosa mbali mbali yahusianayo na ufisadi, wizi wa fedha za umma na kujilimibikizia mali kinyume cha sheria. Karim ambaye anakadiriwa kuwa na utajiri wa zaidi ya dola za kimarekani bilioni moja, alikuwa akipigiwa upatu kuweza kumrithi baba yake kabla ya kushindwa kwenye uchaguzi. Karim alikuwa waziri mwandamizi kwenye serikali ya baba yake. Karim anaendelea kukanusha shutuma dhidi yake. Mchezo wa watoto wa marais kuibia nchi zao kwa mgongo wa baba zao umegeuka kuwa sehemu ya utawala wa kifisadi wa kiafrika. Kwa habari zaidi BOFYA hapa.

Monday 15 April 2013

Mkapa, are you seriously or what?


Former presider Benny Mkapa sickened boozers when he chided Jake Kikwete’s government to adhere to Nyerere’s legacy--- accountability, responsibility, vision and fighting graft among many.  Mkapa derided the government for not keeping up with the principles Nyerere laid down. Those in the know thought he’s taking a dig at President Kikwete.  When those in the know don’t know boozers know and ask. Are things falling apart or what? How come that Mkapa is seeing the light late? Is there anything new we see today that Mkapa did not do or cause?
Mkapa, who’s a chief guest, launched his missiles from Bukoba during the installation of Bishop Desdelius Rwoma recently. He’s quoted as saying that current leadership can’t take us anywhere in protecting the existing peace. Therefore, future leaders need to follow the principles that Mwalimu Nyerere left to protect peace in the country.”  Mkapa erred.  To put it bluntly, doesn’t he see how we’re going backward that’s somewhere?
Swahili sage’s it: A baboon doesn't see its ass. It laughs at and sees the asses of others.  It is true Mwalimu left a peaceful country Mkapa violated favouring investors as opposed to boozers. Mkapa’s rule was a Tophet to the Bongolalalanders he used to say they’re lazy at thinking little knowing he too was! Mkapa enhanced and protected peace by embarking on Zanzibar massacres of 2001 whereby, for the first time, Tanzania produce refugees.
Jokes aside, can Kikwete beat Mkapa in violating Nyerere’s principles? Does Mkapa remember how Nyerere died heartbroken after knowing a true Mkapa he didn’t know before? He breathed his last crying for Tanzanians after learning that he put them in wrong hands of Mkapa.  Doesn’t Mkapa remember this too? Somebody needs to remind him of this reality.
 One can ask: Why didn’t Mkapa abide by the principles he’s advocating now? Is it better than thou or hypocrisy?  If Kikwete is rotten Mkapa too is. Doesn't Mkapa know that Kikwete’s style of ruling is his carryover if not a prolongation?  They all are members of venal CCM. Does Mkapa support the opposition that’s always maintained that CCM has become bankrupt and moribund politically? If so, well done Ben! For even Nyerere once averred that CCM’s neither his mother nor his father.
I don’t want Mkapa’s assertion to force me think he’s a liar if not seeking cheap popularity.  How come Mkapa’s easily, and within a short time, forgotten how he created unnecessary classes of investors, members of CCM and opposition in Tanzania? Has he forgotten his role in EPA scam whose money’s used to bribe voters?
 Let’s remind Mkapa: Current high level of poverty and corruption picked up after he sold our parastatals at a throwaway price.  Has Mkapa forgotten how he sabotaged the National Bank of Commerce (NBC) and Tanzania National Electric Supply Company Limited (TANESCO) when he allowed his brothers- in- law to bring Net Group Solution that made away with our dosh?
One of Nyerere’s legacies is the promotion and protection of public property. What of Mkapa? Dishing them out to real and bogus investors! To crown it all, Mkapa took Kiwira coalfield.
Mkapa doesn’t need to make a dig on others using Nyerere he failed miserably. He’s no moral ground whatsoever. Again, those who know Mkapa are not shocked to hear his noises. Nyerere’s blamed for superimposing Mkapa on Tanzanians who later let him down. I still remember how Nyerere went to China to find investors who later saved Urafiki from Mkapa’s fangs. Has Mkapa forgotten how Kikwete saved him after wananchi wanted him prosecuted for corruption, doing business while in power and abuses of the office?
Mkapa dwelt on peace referring to the current religious misunderstandings and enmity. Again, how can peace exist without justice? Mkapa failed to underscore the fact that what he calls religious hatred is nothing but people’s disillusionment resulting from lack of protection which forced them to rely on whatever cabals. Has Mkapa forgotten how he allowed his wife to use a dubious NGO to mint and print dosh? Where is EOTF today? No donor wants to see it given that it can’t reciprocate by enabling him to land lucrative deals in the government. All donors have now turned their backs. They’re in bed with WAMA that’ll be avoided after Jake hits the road in 2015.
I still remember how Mkapa reprimanded the media for telling him the truth regarding how corrupt his regime was. He fired back saying that those accusing his regime were so too corrupt. He wanted to know where they got monies to establish their business. For Mkapa nothing would be done without involving corruption.
I still remember how he nullified Jenerali Ulimwengu’s citizenship after becoming a thorn in a shoe.
Only one person can help Mkapa. This is Freddie Sumaye who recently was quoted as saying, “Remember what happened in Mtwara (Mkapa’s home region), people torched houses even those of long time Members of Parliament simply because one motorist was ran on, although he did not die, all this resulted from pent-up anger and thoughts that they (people) are so treated because of their poverty.”
Suffice it to say, everybody can accuse the current government but not Mkapa. “To forget one's purpose is the commonest form of stupidity,” Friedrich Nietzsche.
Source: Thisday April15, 2013.

Sunday 14 April 2013

Tanzania imebakwa na CCM na vikaragozi na vinyamkera wake

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimewashika pabaya baadhi ya vigogo wa serikali, Chama Cha Mapinduzi (CCM) na vikaragosi vyao wanavyotumia toka Usalama wa Taifa (TISS) ambayo imegeuzwa nyumba ndogo ya CCM kiasi cha kutumiwa kufanya karibu kila uchafu wa kuhujumu upinzani. Katika kashfa hii itokanayo na kutekwa na kuumizwa kwa mhariri wa magazeti ya Habari Corporation (2006) na mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF) Absalom Kibanda wamo wengi usiotegemea kama waziri wa mambo ya ndani, mtoto wa rais na mahabithi wengine wanaojificha nyuma ya kazi mbali mbali kama kupiga picha Ikulu na upuuzi mwingine. Moja ya jambo ambalo limetufungua macho ni kugundua ni kwanini waziri wa  mambo ya ndani Emanuel Nchimbi anayetuhumiwa na kosa  la kughushi vyeti vya kitaaluma hafukuzwi wala kuwajibishwa. Kwa ufupi ni kwamba taifa letu limebakwa na vinyamkera wasioangalia kesho kutatokea nini. Kwa habari zaidi BOFYA hapa.

Are Air travelers safe and what is the answer?

How did you feel when you read news that anybody can easily hacker into plane computer and set it even on the collision course? Firstly, I thought it was a prank little knowing it was true! I am trying to imagine. If no protective measures are taken what will happen to air travelers especially at this time terrorism is an in-thing? Are we still safer or are just waiting to be toasted?
For more info please CLICK here.

Eti anatafuta mchinjaji wa kitimoto!


Kuna watu wachokozi na wabishi duniani sina mfano! Hayo hapo juu si maneno yangu bali mlevi mmoja anayejiita mwana falsafa wa kizazi hiki. Bwana huyu, licha ya kuwa mlevi, huibua hoja zenye kufikirisha hata wakati mwingine kukera. Naamua kuwasilisha ‘vitu vyake’ kama vilivyo---bila kuyachuja wala kuchakachua. Sina tabia ya kuzuia watu kufikiri hata kama wanavyofikiri vinaweza kuwa kero. Hata hivyo, ukitaka kuepuka kero duniani, jifanye kama haupo wala huna thamani kuliko wengine. Ukijitia kimbelembele cha kujiona ni bora na sahihi kuliko wengine, hao wengine watakuudhi utamani kujinyotoa roho. Mie humo simo wala sitakuwamo. Mie si fala hivyo ati!
Kwanza, niseme mapema ili tusijelaumiana bila sababu ya msingi. Sina dini zaidi ya ulabu. Seriously, wakati wengine wakiapa kwa misahafu yao mie naapa na chupa ya gongo na msokoto wa ganja. Kwani dini ni nini zaidi ya imani? Hakuna imani inayoweza kushinda imani nyingine kama tutaondoa mawenge na makengeza. Hakuna imani inayoweza kukuonyesha kitu kwa uhalisia wake zaidi ya kutumia mifano na hadithi, ngano visa na heakaya. Hayo tuyaache.  Naheshimu dini zote kwa sharti kwamba ziheshimu dini yangu. Kama dini yako inapiga vita ulabu ujue unavunja na kupinga sheria za walevi.
Juzi kwenye kikao chetu tukikamata kanywaji ilitokea mpya. Baada ya mlevi mmoja kusikia habari za ugomvi juu ya nani achinje au kutochinja, alikuja na mpya. Alidai eti ana nguruwe wake na angependa yeyote mwenye kuruhusiwa kuchinja akamchijie ili kuepuka kuingia mtafaruko. Wakati jamaa akisema haya kulikuwa kumetokea mapambano na minyukano huko Mwanza na Tunduma wakigombea kuchinja.  Hii ilitokea wakati tukishangaa: Inakuwaje watu wagombee vitu vidogo na vya kibinafsi hivi kana kwamba hawana vitu vya maana vya kufanya?
Baada ya mlevi kuja na hoja yake, nilimpa laivu kuwa sina ugomvi na hilo. Akichinja mchinjaji au asiyemchinjaji mie natwanga tu. Mie hata ukitwanga nyundo au kunyonga naramba tu. Kwani tumboni kuna sheria zaidi ya njaa? Ukila haramu halali kibudu au whatever mwisho wa yote unaishia kudownload chooni. Ingekuwa amri yangu kuna vyakula hasa aina ya samaki ningeharamisha. Maana kuna mifish ina sura mbaya sina mfano. Mingine inanuka sina mfano! Anyways hayo tuyaache.
Pia nilimuonya mlevi kuwa atajiingiza kwenye mzozo na mjadala wa kipuuzi wa nani achinje na nani asichinje. Msimamo wangu simpo. Kama mzee Ruksa, kula kitu roho inataka ilmradi kisinitapishe wala kuniletea madhara. Kwangu, ugomvi ungekuwa kwenye uhalali na uharamu wa nani kafuga lakini si nani achinje ingeniingia akilini hata kama nafikiri kilevi.
Sasa nisaidie nimsaidie mlevi mwenzangu.  Anasema alipewa zawadi ya kitomoto na wakwe zake na ana usongo na kitu ile. Anasema,hachagui dini bali usongo wake ni kutaka kutafuna kitu ile. Je amuite nani amchinjie kitu hii? Maana, sisi walevi hatutaki shari na yeyote.  We are the bin-Adams of peace and only peace. So whenever you read this, please take seriously and sincerely. Lo! Ulabu nao! Yaani sijavuta bangi zangu naongea kikameruni hivi. Je nikishaliweka itakuwa mbwai? Forgive me for my ukameruni.
Tuache utani. Kumbe kila kitu duniani ni darasa. Kabla ya mlevi kuja na wazo la kutafuta mchinjaji wa kitimoto yake sikuwa nimeangalia utata huu. Naona utata ambao unahitaji wana falsafa kama mimi kuutatua.  Naona hatari mbele ya safari. Kuna siku watataokea watu kutupangia nini tule, tupike, tunywe hata wapi tutembelee na kutembea kwa staili ipi. Hivyo, kwa sisi walevi kuona hatari hii, tunaamua kutoa mapwenti na mawazo ya kuwasaidia wachovu waepuke kuingia mkenge huu. Nadhani tangu tuliponyaka Uhuru wetu wa hovyo, tulikubaliana kuwa kila mtu ana uhuru wa kufanya atakavyo ilmradi asivunje sheria.
Juzi nilisoma sehemu kuwa katika kaya hii hakuna sheria inayomzuia au kumruhusu mtu kuchinja. Kila mmoja anaweza kuchinja ilmradi asimchinje binadamu mwenzake kama wale washenzi wanaochinja na kuua mazeruzeru. Nakubaliana na busara hii ikizingatiwa kuwa kuchinja si kazi sawa na kufuga au kununua hicho kichinjwacho. Haiingii akilini nifuge au kununua mnyama wangu halafu mtu baki eti anipangie jinsi ya kumchinja. Huu ni ukoloni tena ubeberu so to speak. Kama dini, ni suala la mtu binafsi ati.
Hebu niwamegee kidogo mjadala wa kuchinja ulivyokuwa. Alikuja mlevi mmoja aitwaye Shebby Machungi. Huyu bwana anasifika kwa kupenda sana nyama. Machungi ni mwenyeji wa Mashindei, Lushoto. Yeye huiita Ushoto. Kwanza, alipokuja alikuwa na mpango wa kunifundisha ngoma za kwao ili nikiwa narejea kutoka kupiga ulabu nijiimbie. Badala ya kuendelea na kufundishana ngoma alileta wazo la kimasaburi la kugombea kuchinja.
Siku moja kabla tulikuwa tukiongolea ngoma ya Kidembwa na mdumange ambazo nilitokea kuzizimia. Hii ilitokea baada ya kumsimulia safari yangu ‘nchini’ mwake ambapo nilitembelea maeneo kama Nyasa, Kwembago, Shashui, Magira, Mbelei,Kwesime, Baga,Mgwashi,Kongoi, Bumbui, Mazumbai, Malimbwi, Kwemakame, Kwekanga, Kwai (msichanganye na River Kwai kule Uthailandini), Kwenkwazi, Kwenkuzi, Lukozi, Kongei, Kizelui, Kweshashi, Kwenesaa na Kwemachungi, Kwemlazi,Kwemtonto, Kwezumi,Kwemdoe, Kishewa,Kwemtonga, Kwekitui, Makanka.  Ukiondoa KweNkwazi na KweNkuzi yaliyobaki majina ya ajabu ajabu kama dawa za kienyeji!
Kilichomuua Machungi ni kugundua kuwa nayanyaka majina yote hapo juu kichwani tu bila kusoma popote. Alishangaa kipaji hiki. Nilimwambia kuwa hayo ni madogo. Maana ninajua karibu majina ya nusu ya miji yote duniani bila kutazama kwenye kitabu. Hayo tuyaache.
Kuhusu nani achinje, kesho utasikia ndugu zangu akina njomba nao wakiuliza nani anaruhusiwa kunchinja chamaki nchanga. Nashukuru: Kule kwa akina Mwauka bwanji na muli bwanji hakuna kamchezo haka ka kugombea kuchinja. Maana wanavyochinja mbewa na kugombea mbewa zanga ingekuwa noma kama siyo so. Kwa wasiojua nimaanishacho ni kwamba ukivuka mpaka wa Kasumulu pale Mbeya ukaingia nchi ya Maravi usishangae kuona panya wamebanikwa na kutembezwa mitaani kama pweza na ngisi. Kwa ufupi ni kwamba hawa jamaa wakiamua kugombea kuchinja, sijui nani atakuwa tayari kuwachinja hawa jamaa wapenda karanga? It is indeed a challenge and wakeup call that not all that grimmer are diamond. Wakati mwingine tunaweza kugombea vitu tusivyojua au tukivijua vikazuka ambavyo hatukutegemea.
Du yule manzi ana masaburi makubwa hayo! Sijui huyu naye anapaswa kuchinja. Sorry, nilipotea mawazo kiasi cha kubwabwaja. Hi kwa walevi wasomaji wangu wote popote mlipo.
Khalas kweisi.
Chanzo: Nipashe Jumamosi April 13.2013.