Free Thinking

I Fear Nothing But Fear Itself

Epistle to Afrophobic South Africa

Epistle to Afrophobic South Africa

Wednesday, 30 March 2016

Kijiwe chapanga kutembelea Zenj


            Japo kijiwe hakikushiriki kwenye uangalizi wa uchakachuaji wa marudio kule Zenj–kwa  kutoridhika na jinsi mambo yalivyokwenda ndivyo sivyo–mjumbe wake, alhaj Mpema, alikuwako kule kuangalia si kupiga kula jinsi mambo yalivyokuwa yakienda ili atuletee taarifa ambazo ameziwasilisha leo.
            Baada ya kuamkua huku akiwa anaonyesha wazi kuchukia, Mpemba anakwanyua mic, “Yakhe najua kila mmoja atakajua kiliochotokelezea Zenj hasa kuhusiana na huu uchakachuaji uliomalizika. Taarifa ni kwamba kilichotokelezea kule ni wizi wa kula wa kawaida tokana na wapika kula wengi kutopika.”
            “Unataka kuniambia hizi sherehe za kupongezana na kuapishana ilikuwa ni danganya toto tofauti na ukweli wenyewe? Kama ni hivyo basi rais Joni Kanywaji Makufuli amejichagua kuushiriki ukiachia mbali kula jiwe muda wote ambapo mambo yalikuwa yakifukuta kule Zenj utadhani yeye si rais wake.” Anauliza Mijjinga huku akimkazia macho Mpemba.
            Kabla ya Mpemba kujibu Mgosi Machungi anaamua kumchomekea Mijjinga, “Kwanza yue njomba angu wa madevu yuko wapi mbona hatimsikii akitoa tamko au naye ameamua kukata pua na kuunga wajihi ii apate tena umakamu?”
            Mpemba anajibu, “Kusema ule ukweli wa Mungu kule Pemba hakuna ntu hata mmoja alopiga kula. Kama wapo waliopiga basi ni wale mamluki, mapandikizi au mazombi kama siyo maruhani walozoea kuwatumia hasa kwa kuengeza idadi ya wapiga kura wakati siyo. Hilo la bwana nkubwa kushiriki au kutoshiriki dhulma hii ni juu yake kupima na kuchagua. Hata hivo atajitofautishaje wakati chama chake ndo kinioshikilia usukani kikifanikisha kila jinai huku Zenj? Mie njuavo hapa hakuna haki ilotendeka bali dhulumaa.”
            Kabla ya Mpemba kuendelea, Kapenda anauliza, “Una maana kuwa huyu bwana hakushaini na anatawala upande mmoja kama mwenzie Kanywaji aliyeonyesha kufanya hivyo wakati wa gogoro hili?”
            Kabla ya kujibu Mpemba anatikisa kichwa na kusema, “Yakhe hilo li wazi kuwa huyu jamaa ataendelea kutawala kimabavu kama yule bazazi alojiita Komandoo wakati hakuwa chochote wala lolote. Ukimuona leo huweziamini kuwa huyu ndo alowahi jiita komandoo wakati sasa yu kama kondoo na si komandoo.”
            Baada ya kuona zinaingizwa inshu zisizoendana na mada Msomi Mkatatamaa anaamua kula mic, “Kutokana na taarifa aliyoleta alhaj Mpemba ni kwamba Zenj hakuna aliyeshinda bali kushindishwa. Kama mnakumbuka niliwaambia kuwa huyu wa kushaini atashindishwa hasa baada ya kufuta uchaguzi bila kutoa sababu za kufanya hivyo. Nadhani huko aliko Jechia Dhwalimu Jechia anachekelea kwa kufanikisha ulaji wake. Kitaalamu naweza kusema kuwa mgogoro ambao Nambari Wani wamejidanganya wameuua au kuuepuka ndiyo unaanza. Wataweza kufanikiwa kama watamshawishi Madevu na kumpa ulaji kama walivyofanya mwanzoni pamoja na mkakati huu kuwa na mashaka na matatizo yake. Je wanakaya waliogoma kushiriki uchakachuaji watakubali mtu wao kuwa kitanda kimoja na watesi wao?”
            Mpemba anakula mic tena, “Wallahi nakuaapia. Kama kuna ntu adhani anawezawatumia watu kulinda ulaji wake binafsi aota huyu. Nijuavo mimi ni kwamba wale waliogomea uchakachuaji hawatakubali lolote isipokuwa kusomewa matokeo ya uchaguzi halali wa kwanza uliovurugwa na huyu Jechia Dhwalimu Jechia. Vinginevo hapa hakuna atondanganya yoyote awe ni wa upingaji au wale wanaotula sasa.”
            Kanji aliyekuwa akisikiliza kwa makini anaamua kutia guu, “Dugu yangu Pemba kama nasema iko kweli basi iko sida kuba sana Zaainzibaa. Kwanini sasa gagania laji kama vatu ingine hapa kuwa na tumboni ya kula?”
            Kapende anaamua kutoa jibu, “Kwani mafisadi wanaotuhangaisha wawe wa kiuchumi au kisiasa unadhani hawajui kuwa nasi tuna matumbo kama wao? Wanajua ila wanajiona kuwa wao ndio wanaofaa kula na wengine waliwe tu kana kwamba wao si watu. Huyu bwana hana cha kupoteza hata kama wachovu wakiamua kuchenchiana. Mambo yakiwa magumu atatumiwa ndata na ndutu toka Barani na watamlinda kwa kuwaumiza wapingaji kama alivyofanyiwa komandoo na mchezo unaishia pale.”
            Kabla ya Kapende kuendelea Da Sofia Lion aka Kanungaembe anamchomekea, “Mie tangu nigundue kuwa kumbe siasa ni mchezo mchafu hasa baada ya mjomba wangu kubomolewa nyumba yake sina hamu na wanasiasa. Sishangai kuona kinachoendelea Zenj. Iwavyo vyovyote Madevu anaweza kupewa chake kama alivyofanyiwa swahiba yake wa zamani Hamad Rashid Mood akatulia na wachovu wakaendelea kusota kama kawa kwani hii ni mara ya kwanza hii kufanyika?”
            Mipawa anamchomekea Sofi, “Da Safi, sorry, Sofi usemayo ni kweli tupu. Je kulalamika tu kunatosha au lazima tufanye mageuzi lau ili tuweze kuleta mabadiliko yenye manufaa kwa jamii yote?”
             Kabla ya da Sofi kuendelea Mbwamwitu anachomekea, “Bwana Mipawa si useme tu kuwa kuna kitu unataka kwa Sofi hadi unamwita safi au vipi?”
             Sofi anaamua kujijibia, “Kaka hayo yako. Sisi watu wazima ati. Kama kuna anachotoka kwani kuna ulazima gani wa kuzunguka au kukuogopa wewe? Tunajadili mambo muhimu kwa kaya wewe unaleta utani. Ndiyo maana mnaliwa na hawa mafisadi tokana na kutokuwa serious.”
            Mbwamwitu anaamua kumkaba da Sofi ili amtie adabu kwa kumwambia analiwa.
Kuona hivyo tunaamua kuingilia kati. Tunawaachanisha na kila mmoja anatawanyika!
 chanzo: Tanzania Daima, Machi 30, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 07:41 No comments:

Monday, 28 March 2016

Barua ya wazi kwa waziri mkuu Majaliwa


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.             Mheshimiwa waziri mkuu,
Kwanza nakupongeza kwa kuteuliwa kuwa waziri mkuu. Pili, nakupongeza kwa juhudi unazofanya kupambana na uovu kuanzia bandarini hadi kwenye sekta ya ardhi.
Ndugu waziri mkuu, hivi karibuni ukiwa mkoani Kagera, ulifanya maamuzi magumu ambayo ni kuwanyang’anya ardhi mafisadi wa ardhi walioipata na kuihodhi kinyume cha sheria na wasiiendeleze katika wilaya ya Ngara. Hili ni jambo la kupigiwa mfano kama juhudi zako zitalenga kuwabaini na kuwashughulikia wote waliojilimbikizia ardhi.
Ndugu waziri mkuu, hivi karibuni waziri wa Ardhi, William Lukuvi alitoa madai kuwa kuna wafanyabiashara wawili waliohodhi ardhi kwenye eneo la Kigamboni waliotaka kumhonga shilingi bilioni tano ili awawezesha kuiuzia serikali ardhi waliyoipata kwa bei ya kutupwa baada ya kuwarubuni na kuwadhulumu wananchi. Lukuvi alikaririwa akisema kuwa wafanyabiashara wakubwa wawili walikuwa na jumla ya ekari 700 walizonunua kwa shilingi milioni tano kwa heka huku wakitaka kuiuzia serikali kwa shilingi 141 kwa heka.
            Ndugu waziri mkuu, baada ya Lukuvi kutoa madai haya –ambayo bila shaka yaliacha mashaka na maswali mengi bila majibu–wengi tulishangaa ni kwanini hakuwataarifu Tume ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) au polisi ili kuweka mtego na kuwakamata wahalifu hawa. Kama haitoshi, Lukuvi alificha majina ya wahusika kiasi cha kujenga shaka juu ya ukweli wa madai na usafi wake. Kwa kuonyeza uzembe wa wazi, wengi wanamuona Lukuvi kama jipu linalopaswa kutumbuliwa na kuondolewa kwenye serikali ya awamu ya tano. Maana, ameonyesha uzembe wa wazi wazi na kutojua wajibu wake kama waziri na mtanzania kwa kushindwa kuripoti tukio la jinai. Wengi walidhani kwa mtu wa kada ya Lukuvi, angechukua hatua mujarabu na kuonyesha kwa vitendo anavyochukia na kupiga vita rushwa. Sijui kama hata rais ameuona huu udhaifu wa Lukuvi ambao tungetaka nawe uupige darubini na kumshauri rais nini cha kufanya dhidi ya waziri kama huyu ili liwe somo kwa wengine wanaofanyia kazi mazoea badala ya kufuata taratibu na kanuni.
             Ndugu waziri mkuu, tukirejea kwenye maamuzi yako ya wilayani Ngara ambapo hati za kumilki jumla ya ekari 7,700 zilifutwa, tunakutaka uchukue hatua hiyo dhidi ya wamilki aliowataja Lukuvi huku ukibaini wengine ambao wameishafanya mchezo huo au wanapanga kuufanya. Pia tungeshauri sheria ya uuzaji na umilkishaji ardhi wawekezaji irejewe na kurekebishwa ili kuziba mianya ambayo waroho wachache wenye madaraka na fedha wamekuwa wakitumia kuhujumu taifa huku wao wakitajirika wakati taifa linazidi kuwa maskini wakati lina raslimali lukuki. Kwa mfano, tunashangaa serikali–ambayo kisheria ndiyo mmilki wa ardhi nchini–kulanguliwa ardhi yake wakati ina mamlaka ya kufuta hati milki husika na kuchunguza namna hawa walanguzi wa ardhi walivyopata hodhi ya ardhi husika. Hili halitasaidia tu kupambana na hawa wanaojulikana. Pia, litasaidia kubaini mitandao yao iliyojazana kwenye ofisi za umma. Waziri Lukuvi alisema kuwa kumekuwapo wafanyabiashara hasa wawekezaji kuja Tanzania na kununua ardhi bila kuiendeleza huku wakienda kwenye mabenki na kuchukua mikopo kwenda kuanzisha miradi kwenye miji ya Dubai na London jambo ambalo licha ya kuhujumu taifa linawanyima watanzania ajira na huduma. Tungeomba umuite Lukuvi kwenye ofisi yako na kumtaka atoe maelezo ya kufanikisha kuwakamata wahalifu hawa pia ukimtaka aeleze kwanini–kama ni kweli alitaka kuhongwa–hakutaarifu vyombo husika viweke mtego wa kuwanasa? Pia umtake waziri Lukuvi akupe majina ya wahusika ili kubaini ukubwa wa tatizo na kulishughulikia.
            Ndugu waziri mkuu, pia tunakushauri uchunguze kujua hawa wawekezaji, wawe wa ndani au wa kigeni walipataje kununua na kuhodhi ardhi husika na nani aliwaambia kuwa Kigamboni ingekuwa na soko kubwa baadaye wakati miradi ya serikali ni siri?  Hili litasaidia kubaini watumishi wasio waaminifu wa serikali wanaovujisha siri za serikali na kuzitumia kuhujumu watanzania bila sababu zaidi ya uroho na ufisadi.
             Ndugu waziri mkuu, Lukuvi alikwenda mbele na kudai kuwa kuna baadhi ya viongozi waliojilimbikizia ardhi. Tungeshauri na hili Lukuvi aitwe na kulitolea maelezo ili uchunguzi ufanyike na kubaini wahusika walipataje ardhi husika na hatua zichukuliwe ilil kukomesha mchezo huu unaotokana na ubinafsi na ufisadi wa kutumia madaraka ya umma kwa kujinufaisha binafsi kwa baadhi ya maafisa wa serikali.
            Kwa vile umeonyesha umakini na juhudi kubwa katika kutatua matatizo ya wananchi, tunategemea hutaacha tuhuma na kashfa kama hizi zifutikwe chini ya busati jambo ambalo litaionyesha serikali yako kama yenye kupendelea na kugwaya baadhi ya wahalifu. Tusingependa dhana potufu kama hii iruhusiwe kujengeka ingawa kuizuia kutatokana na namna utakavyofanyia kazi madai kama haya.
            Tumalizie kwa kusema wazi kuwa tunaitikia wito wa rais John Pombe Magufuli wa kutaka watanzania wamsaidie kubaini na kupambana na ufisadi mambo ambayo yameikwamisha nchi yetu kimaendeleo ukiachia mbali kuigeuz shamba la bibi na kuiletea hasara na aibu. Wakati wa kufanya kazi kwa mazoea unapaswa kukomeshwa na kujenga uchapakazi unazingatia sheria, taaluma na maadili.
Ndugu waziri mkuu, tunaomba tuishie hapa kwa kutoa hoja.
Wasalaam.
Chanzo: Tanzania Daima, Machi 27, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 11:56 No comments:

Lukuvi whom are you trying to dupe

Image result for photos of lukuvi
           
Soil Minister, Bill Lukuvi, left boozers shocked and infuriated. He’s recently quoted alleging that he turned down a cool Tsh5 billion bribe that two tycoons wanted to offer him so that he’d allow them to hike their parcels of land to the govt. Lukuvi’s quoted as saying,
 “If you are greedy you can’t do the job you were sent to do. Sometimes, there came two big businessmen and wanted to give me Sh5 billion so that I pass there project worth of billions and they announced to my friends that they would give me the money, but it is impossible here.” Doesn’t Lukuvi see that his negligence, apart from setting these criminal free, portrays him as inept and unfaithful person?
For the boozers whose brains are as sharp as a razor, despite being sloshed all times, Lukuvi’s hoo-has left many more questions than answers. All such questions portray Lukuvi as a boil that president Joni Kanywaji Mugful must cleanse as soon as possible. Though Lukuvi wanted to portray himself as a clean chap, he failed miserably so as to end up inculpating himself. Maybe, he thought that boozers are tabula rasa that can’t weigh and analyze things.  Kaka, you can’t take us for the raid and get away with murder. Lukuvi’s allegations are wanting; and have a lot of holes.
First of all, he is neither serious nor trustworthy. His allegations are ambiguous; and they show the dearth of truth.
Secondly, boozers are asking a couple of questions as to why Lukuvi didn’t alert the Prevention and Combating Corruption Bureau (PCCB) to set a trap and catch these criminals. For any sane person, this would have been the first step to take to net such criminals who sabotage our hunk. Why didn’t he do that if there wasn’t any foul play; that Lukuvi doesn’t want to divulge? Lukuvi needs to tell us.
Thirdly, Lukuvi’s allegations lack evidence. If he thought that by revealing such criminality without taking any actions was something that’d depict him as an incorruptible dude, he ended up opening Pandora’s Box pointlessly. For, such allegations render Lukuvi as an irresponsible person who lost such a golden chance to nip such criminals in the bud.
Fourth, boozers think: Lukuvi didn’t tell the whole truth; and if he did, he just told a half-baked one. Although Lukuvi aimed at creating a good image that he is incorruptible, he ended up messing even more. The law is clear that whenever anybody comes across anybody attempting or committing crime, that person is duty bound to inform the authorities. This is the procedure that even boozers–despite being blotto all the time–know. Again, Lukuvi alleged that some big criminals have been using our land to solicit dosh from various financial institutions; and invest in Dubai and London. Are these freebooters the citizens or foreigners who have turned our hunk into shamba la bibi the president was complaining about the other day? After becoming aware of such criminality, what is Lukuvi going to do to take on them and stop them altogether? How did they know that Kigamboni will become a hot cake so as to amass such huge chunks of boozers’ land? Aren’t these criminals a government within a government? How many are out there and how many are there in public offices? These are simple questions any sane person even if he or she was boozers was supposed to ask and find answer to.  Look at how stupid, sometimes; some of our officials tend to be. The punk is spending just five million on a plot; and sells it to the same that owns the land at the tune of 141 million shillings by simply catching the ferry and go to Kigamboni to conclude a deal! What monkey business.
If Lukuvi were competent and patriotic enough, he’d have told us the number of freebooters that have been benefiting from this theft. So, too, aren’t such criminals along with Lukuvi boils that President Mugful is supposed to cleanse as urgently as possible? Again, whom does Lukuvi want to deceive while everything is clear that he slept at the wheel? Which measures does Lukuvi intend to take to arrest this criminality?
In sum, boozers want Lukuvi to tell the whole truth and show cause why he shouldn’t be cleansed just like other jipus. For, his negligence–apart setting these criminals free–Lukuvi sabotaged our hunk for not taking actions. What is behind the curtain that Lukuvi doesn’t want to be put on the agora? With my bhang and Kanywaji, I can conclude that Lukuvi hid a lot of information that would have helped us to put these criminals where they are deservedly supposed to be, behind bars. So, too, had Lukuvi did his homework, we’d have been able to attack their already amassed wealth as we squeeze them to divulge their accomplices especially in the positions of power. Lukuvi, go tell it to the birds. Whom do you want to fool and cheat?
Source: Guardian, March 27, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 08:24 No comments:

Saturday, 26 March 2016

Mlevi astukia 'ugesishaji' kaya

Tangu alipoingia kwenye ulaji baada ya kuchukua ukanda toka kwa Njaa Kaya aliyeonekana kuwa kilaza kiutawala kiasi cha kuigeuza kaya shamba la bibi kama alivyodai rahis hivi karibuni, nilitokezea kumzimikia rahis Dk John Kanywaji Makufuli. Nilichetuliwa na kasi na namna yake ya kuwasaka na kuwatumbua majipu wagonjwa wa ufisadi. Hata hivyo, tangu juzi alipotangaza timu yake ya wakubwa wa mikoa, badala ya kumzimikia, natamani nimuwakie kama si kumbwatukia. Maana, ametoa rungu kwa machizani ili watuumize tena watakavyo ukiachia mbali kuwaangiza watembeze undavandava hata kama ni kwa makosa ilmradi baadaye warekebishe.
Hakuna kauli iliyonkata na kunifanya nivute na kunywa kama sina akili nzuri kama kuwapa ulaji wageshi wastaafu wakati kuna vijana wengi–tena waliobukua mambo ya siasa na ma-political sciences na madude mengine magumu yahusuyo utawala–wanaoweza kutawala hiyo mikoa bila kulazimisha wala kutoa maamuzi bora maamuzi ili warekebishe baadaye kama alivyowaagiza. Kikatiba, wageshi hawapaswi kujiingiza kwenye siasa hata kama wamestaafu isitoshe siasa zenyewe zinapokuwa za majitaka na kupeana fadhila. Hii maana yake ni kwamba hawa jamaa walikuwa na kadi za nambari wani kibindoni jambo ambalo ni kosa la jinai. Ina maana walikuwa wakifanya kazi ya umma na kulipwa njuluku wakati wamevunja sheria ukiachia mbali upendeleo na kupokea amri za kijinga kama kusimamia uchakachuaji wa kura. Ndiyo maana jamaa amewaamini na kuwaachia kila kitu wafanye watakavyo. Nadhani hapa kamchezo kachafu ka kulipana fadhila karudufiwa. Katika kuwafunda na kuwaagiza, rahis Makufuli alisikika akisema ni heri wafanya maamuzi hata kama ni mabaya watarekebisha baadaye kuliko kutofanya maamuzi. Je kinachotakiwa hapa ni kufanya maamuzi au kuchukua maamuzi ya maana? Kwa walevi, heri mtawala asiyefanya maamuzi ya hovyo ili arekebishe baadaye kuliko anayechukua maamuzi ya kijinga na kutegemea kufanya maamuzi mazuri baadaye. Kwani kazi ya ukubwa wa mikoa ni ya majaribio ya kufanya au kuchukua maamuzi au namna ya kuwafundisha wageshi wastaafu mambo ya utawala?
Kama haikutosha, jamaa aliwaambia wakamate walevi na kusweka ndani hasa wale akina sie tunaoshinda vijiweni kutokana na kutokuwa na ajira. Hebu fikiri. Wachizani kama jamaa yangu Po Makondakonda ambaye alishasweka ndani wahishimiwa na watumishi wengine wa halmashauri atatumiaje rungu hili? Kwani kaya yetu ni ya kigeshi au vipi? Tuambizane kabla ya kuchenchiana bwana. Mbona akina Jimmy Rugemalayer, Roastatamu Kagoda, Singansinga Sethii na mzee wa Vijisenti na majambazi wengi waliosababisha umaskini na ukosefu wa ajira hawakamatwi kama hapa siyo usanii wa Ki-SISIEM?
Simuwakii wala kumbwatukia rahis Makufuli. Badala yake nampa ushauri wa bure. Kama anaamini kuwa wageshi ndiyo wanaweza kukomesha matatizo ya kaya bila kufumua mfumo na kuufuma upya anajidanganya ten asana. Mara hii amesahau tulivyoambiwa kuwa Njaa Kaya alikuwa mgeshi. Hivyo angeweza kuinyoosha kaya akaishia kuiharibu hadi kumpa ujiko Makufuli? Kinachotakiwa si ugeshi wala utishi bali kufuata sheria na kubadili mfumo mfu na muovu ulioanzishwa baada ya kung’atuka mzee Mchonga wa Burito. Hata ukitumia bangi na kanywaji, huwezi kutoa amri za kutatua matatizo ya miaka zaidi ya thelathini ndani ya siku 15. It is impossible sir.
Kitu kingine kinachonifanya nitamani kumuwakia Makufuli ni ile kutoa maagizo ya kihasara hasara kama vile kuwaambia wakubwa wa mikoa na wale wa Banki kubwa kuwa wafute majina ya wafanyakazi hewa ili kuanza upya. Tutaanzaje upya bila kuwakamata na kuwashughulikia walioajiri wafanyakazi hewa na kupiga njuluku kwa miaka nenda rudi?
Nijuavyo aina mpya ya utawala unaoanza kuota mizizi wa kumridhisha Dk Kanywaji, wahusika watakwenda kuumiza walevi bila sababu ili kumridhisha bosi wao. Tushawaona wengi hasa kwenye jiji la Bongo ambako jamaa yangu Makondakta alifanya kila vituko kwa kuvunja kila sheria kitabuni kuhakikisha anamuingiza mkenge Makufuli na kuishia kupewa rungu zaidi ili avurunde zaidi. Siku moja ataniambia kama si kukumbuka haya ninayochora hapa. Angajua usanii wa huyu dogo wala asingejivunjia heshima kumpigia debe wazi wazi. Atajuta baadaye baada ya malalamiko kuzidi juu ya tabia yake ya umungumtu itakapoanza kujitokeza na kuumiza wale anaodai analenga kuwaondolea kero. Sijui kama kuruhusu wakubwa wa mikoa kufanya watakavyo kama ni kuwasaidia walevi. Ni kama ametangaza utawala wa kigeshi kwa mlango wa nyuma asijue madhara yake. Walevi tunapinga kukamatwa na kuswekwa ndani au kuburuzwa simply because wahusika wanataka wajijenge na kumfurahisha muungumtu wao aliyewaumba. Huwezi kuendesha kaya kwa amri ya mtu badala ya kanuni zilizotugwa na kukubaliwa na wanakaya wenyewe. Huu ni uimla hata kama tunaambwa una nia nzuri.
Nimalizie kwa kuwamba wahusika warejeshe kaya yetu kwenye utawala wa kiraia badala ya kuigesisha kwa mlango wa nyuma. Hii kaya ni ya walevi wote bila kujali kazi wala vyeo vyao. Natamani nimuwakie jamaa niliyemzimikia sasa anaanza kuniangusha.
Chanzo: Nipashe, Machi 26, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 06:15 No comments:

Friday, 25 March 2016

Kwa ndugu zetu mnaoamini kwenye dini za kigeni


Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 16:17 2 comments:

SHUKRANI YA PUNDA


Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 10:04 No comments:

Wednesday, 23 March 2016

Kijiwe kupinga amri za Dk Kanywaji


            Amri za rahis Joni Kanywaji Makomeo zimekichefua kijiwe kiasi cha kupanga kwenda kwa pilato kuzipinga. Haiwezekani turejeshewe utawala wa kindavandava wakati twaambiwa sisi ni kaya ya kidemokrasia.
            Mpemba ndiye anaanzisha mada kuhusiana na amri hatari za Dk Kanywaji ambaye Kijiwe kilikuwa kimetokezea kumwaminia. Anachonga, “Jamani mmezisikia hizo amri alozitoa rahis Kanywaji hivi karibuni baada ya kuapisha geshi lake la wakubwa wa mikoa? Wallahi mie zankata kweli kweli.”
            Mgosi Machungi anakatua mic, “Hata mimi simielewi huyu jamaa hasa pae aipoamua kuajiii wageshi wastaafu kuwa wakubwa wa mikoa huku akiwaamuu watiweke ndani hasa sisi tinaoshinda Kijiweni baada ya kukosa ajia.”
            Mipawa anaamua kumchomekea, “Kumbe ulikuwa hujui kuwa huu mchezo wa kuajiri wageshi ni wa zamani tangu zama za mzee Mchonga? Kwa nijuavyo mimi, tumekuwa tukitawaliwa kigeshi kwa mlango wa nyuma. Hivyo, alichofanya Dk Kanywaji ni kuwa muwazi tofauti na waliomtangulia.”
            Msomi Mkatatamaa leo anaingia mapema. Anakwapua mic, “Hii ndiyo hatari na kasoro za kutokuwa na sera za kutawalia. Kimsingi, wanashindwa kitu kidogo yaani kufumua mfumo mfu tuliourithi toka kwa wakoloni na kuufuma upya. Kaya haiwezi kuondokana na matatizo iliyomo kwa nguvu ya zima moto. Ningeshauri waka chini wafanye utafiti na kubaini chanzo cha matatizo yetu ambacho kimsingi si kingine bali kuondokana na maadili ya utumishi wa umma. Wanakula umma wakidai wanautumikia wakati wanautumia.”
            Kabla ya kuendelea Mijjinga anachomekea, “Usemayo Msomi ni kweli. Bila kubadili mfumo wanajisumbua. Hukumsikia Dk Kanywaji akiwaambia wakubwa wake wa mikoa kuwa ndani ya siku 15 wafute majina ya wafanyakazi misukule? Ajabu ya maajabu, wengi tulidhani mojawapo ya maagizo ya rahis yangekuwa kuwakamata wote walioajiri misikule na kujipatia njuluku na kuwasweka lupango then wapelekwe kwa pilato. Lakini jamaa hili halikumhangaisha. Mie naona anatoa maagizo kana kwamba kaya yetu ni shamba lake binafsi.”
            “Yote tisa, mie aliniacha hoi alipowapa ulaji wageshi ndata waliostaafu jana tu. Hakuwapa hata nafasi ya kwenda uraiani wakajifunze jinsi ya kuishi kama wastaafu. Sijui kaya yetu inapelekwa wapi? Unawezaje kuwapa madaraka makubwa watu wasio na uzoefu tena waliostaafu jana kana kwamba kaya haina wachovu wengine wanaoweza kuwatawala wenzao?” anachomekea Kapende huku akibofya kiSumsung Galaxy 6 chake.
            Mheshimiwa Bwege anakatua mic, “Mie hata sishangai. Kinachonishangaza ni ile hali ya kuua muungano kwa kuwagawia watu wake mikoa yao wakajifanyie watakavyo. Hamkumsikia akiwaagiza wafanye maamuzi hata kama ni ya kipuuzi ili warekebishe baadaye badala ya kuogopa kufanya maamuzi? Huu ni nini kama siyo uimla unaorejeshwa kwa mlango wa nyuma kwa kisingizio cha kutatua matatizo ya wachovu? Nadhani, badala ya kuwasaidia wachovu, watawakwaza zaidi. Unawezaje kupiga marufuku vijiwe wakati wenzetu wanakutana Idodomya, wanaitwa wahishimiwa na kupewa mshiko kwa kupiga gumzo mjengoni? Kama ni hivyo basi na spika wa mjengo awa mgeshi. Nani anaongelea kuwashughulikia mafisadi papa kama vile Kagoda, EPA, Escrew au Kiwira? Who wants to fool another here?”
            Mzee Maneno anamchomekea Mheshimiwa Bwege, “Mheshimiwa huna haja ya kulalamika. Hao unaotaka washughulikiwe hawatashughulikiwa. Kinachoendelea hapa ni kutumbua vijipu uchungu huku majipu yenyewe yakiendelea kuzaliana. Unaweza kunieleza ni kwanini–kwa mfano–wadokozi wa bandarini waliswekwa lupango ilhali wale wafanyabiashara wakubwa waliokuwa wakishirikiana nao wakipewa muda wa kurejesha fedha waliyoihujumu kaya? Ama kweli Chama Cha Maulaji (CCM) ni chuo cha sanaa!”
            Kanji hataki kubaki nyuma. Anakatua mic, “Mimi sangaa sana witu nafanya Dokta Kanyaji. Yeye ikosema kuwa geshi takamosha valo vote naharibu amani hasa kwenye koa ya pakani. Kama vatu nakaa kule nakaribisha geni tena jambazi nayokuja na bunduki nategemea nini?”
            “Wallahi Kanji hapa wankata. Wankumbusha yule ngeni aliyepewa ardhi awekeze kule Kagera akaamua lima bange na asiguswa na ntu. Je wako wangapi wanofanya mambo ya hovyo kama haya na waitwa wafanyabiashara tena mashuhuri wakati ni wezi mashuhuri? Je huyu Singasinga wa Escrew ana tofauti gani na wale waniochukua bunduki wakafanya ujambazi unaoleteleza matatizo huko mikoani? Wankamate kwanza ndipo ntajua kuwa wataka sasa fanya kweli vinginevo yote hii danganya toto nawaambia.”
            Da Sofia Lion aka Kanungaembe anaamua kutia timu, “Mie jamaa amenichefua hasa pale alipoamua kuteua warume tu huku akiwatia akina mama kiduchu katika hilo jeshi lake la wakubwa wa mikoa. tunataka uwiano wa kijinsia bwana.”
            Mgosi anarejea, “Mie hakuna aipontisha kama kumpa ungu Makondakta. Napanga kuejea Ushoto ii kuepuka kunyanyaswa na huyu dogo ambaye aiwahi kuwatia ndani wahishimiwa na wafanyakazi wengine wa haimashaui ya Kinondo. Hapa azima titegemee utawaa wa kigeshigeshi, na kindavandava kama siyo uimua.”
            Msomi anarejea, “Hapa lazima tutegemee vurugu zisizo na sababu. Kwa mtu mwenye nia njema na Kaya, alipaswa kuwaasa wasifanye mambo hovyo ili kumfurahisha yeye badala ya wachovu.”
            Akiwa anataka kuendelea mara shumbwengu la Makondakta lilitia breki Kijiweni. Jamaa alishuka na kuanza kutuuliza tunafanya nini kijiweni badala ya kwenda kuchapa mzigo. Acha tumzomee. Kama siyo kuwahi na kujongomea kwenye mchuma wake huenda historia ingekuwa nyininge!
Chanzo: Tanzania Daima, Machi 23, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 06:02 No comments:

Tuesday, 22 March 2016

How do you view and assess this stuff?

Source: Daily Nation
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 06:33 No comments:

Friday, 18 March 2016

Makufuli mtumbue jipu Lukuviii


            
Baada ya muishiwa waziri wa Udongo Bill Lukuviii kuja na mpya kiasi cha kumlewesha Mlevi hata bila kanywaji na tubangi, imebidi lau niseme ili wote na yeye wajue kuwa sikuingizwa mkenge. Hii itasaidia na wengine wasiingizwe mkenge katika msako huu wa umaarufu wa shilingi mbili.
            Bila hata chembe ya aibu, Bill alikaririwa na wambea akijisifu kuwa alikataa mshiko wa bilioni tano. Hebu nirudie. Five billions doughs! Ngai, Zumbe na Ambuye! Kwa vile mlevi ni mtaalamu wa masuala ya jinai hasa kusema uongo, ilibidi nirejee kwenye maktaba yangu na kufungua makabrasha na shajala zote lau nipate pa kuweka uongo huu. Kwa lugha ya kisambaa hii huitwa cheap popularity ambapo mhusika hujitahidi kujipigia debe kama yule jamaa mbaguzi wa kwa Joji Kichaka aitwaye Don Drumpf. Mhusika hujikweza hata kujikweza kwenyewe kukiishia kwenye maanguko kama ilivyotokea kwa Bill ambaye leo namrarua bila huruma.
            Kwa vile mlevi ni bonge la gwiji la sheria, nitajaribu kutoa sababu za kutokubaliana na madai ya Lukuvii.
            Mosi, Lukuviii alificha majina ya wahalifu–aliowataja kama wafanyabiashara wakubwa–waliotaka kumshikisha mabilioni haya. Hawa ni wafanyabiashara wakubwa au wezi na wahalifu wakubwa tu? Je ni kwanini alificha majina ya majambazi kama hana lolote la kuficha? Je kuficha kwake na kutoboa vinatusaidia nini iwapi watuhumiwa wamefanywa kuwa top secret?
            Pili, kwanini hakuitaarifu ile kampuni ya umma ya kulinda na kupamba–sorry–kupambana na rushua (Takokuru) kama hakuna namna. Ina maana–pamoja na nafasi yake kubwa na nyeti kama hiyo–Lukuviii hajui kuwa sheria inamtaka kila mwanakaya anayekuta mtu anatenda au kujaribu kutenda kosa la jinai anapaswa–kisheria–kutoa taarifa kwa vyombo husika? Je Bill hakuwa na imani na Takokuru? Kama ni hivyo, kwanini hakuwatonya ndata lau wakaweka mtego na kuwanyaka hawa wanahizaya wanaoharibu kaya yetu?
            Tatu, Lukuviii alidai kuwa kuna mtandao wa matapeli tena aliwaowaita wawekezaji wanaolangua ardhi yetu na kwenda kufungua mabiashara makubwa Dubai na London. Je hawa ni wabongo au maabsii na makalu? Je hawa ni wawekezaji au wachukuaji? Je walipataje taarifa za siri ya sirikali kuwa Kigamboni kungekuwa dili kama nao siyo kuwa na sirikali yao ndani ya sirikali na siri kali ambayo Bill amejitahidi kuitunza? Pia, Lukuviii alidai kuwa kuna wakubwa waliojilimbikizia ardhi. Je Bill kama waziri mhusika, kwanini hakutaja majina yao na kueleza mikakati aliyo nayo ya kuhakikisha wanatumbuliwa jipu na kurejesha ardhi yetu? Je sheria ya kuzuia kuuzia wageni ardhi ilibatilishwa au kubadilishwa lini? Je kwa uzembe wote huu hapa Bill kajijenga au kujibomoa na kuonekana muongo na mzembe?
            Nne, Lukuviii–wa uzembe na habari zisizo na ukweli kama hizi–hajawa jipu linalopaswa kutumbuliwa mapema na Dk John Kanywaji Makufuli? Katika maajabu ninayongojea ni mawili. Mosi, Lukuviii kuendelea kuwa kwenye ulaji bila kutumbuliwa jipu na kutupwa nje kama Sifui. Na pili, kama Lukuviii hatajibu maswali yangu tena kwa majibu yanayoingia akilini. Asipofanya hivyo, nitatia guu ikulu mwenyewe kushinikiza atumbuliwe jipu na kuwataja hao waliotaka kumhonga. Atafichaje majina ya wahalifu waliotaka kutuibia walevi? Anadhani hii kaya ni mali yake peke yake kiasi cha kufanya jinai kama hii suala la binafsi?
            Tano, kwanini Lukuviii hakueleza uhusiano wake na hawa “wafanyabiashara wakubwa” ambao hadi sasa ni kitendawili anachoweza kutegua yeye mwenyewe?
            Sita, kama mtu mzima na kiongozi, je Lukuviii anaona alichofanya ni haki na sawa sawa? Je hawa jamaa wangekuwa wanapanga kuvunja nyumba yake au kumkaba bi nkubwa angeficha majina yao bila kuita ndata kuwashikisha adabu?
            Saba, je kwa kuwaficha, Lukuviii haoni kuwa amewasaidia na kuwapa hifadhi kiasi cha kusaidia uhalifu uendelee kutendeka? Je uhusiano na biashara ya Lukuviii na hao wenzake inaishia hapo au kuna mengi yamefichwa na kwanini na ili iweje na kwa faida ya nani?
            Nane, je Lukuviii–kuondoa ubishi na shaka–yuko tayari kutaja majina ya hao wezi wakubwa aliowapa sifa ya ufanyabiashara mkubwa?
            Tisa, je Lukuviii yuko tayari kueleza ni kwanini asitumbuliwe jipu kutokana na kushirikiana na wahalifu kwa kuficha majina yao?
            Je Lukuviii anajua madhara atakayoisababishia kaya kwa kushindwa kuwaitia Takokuru au ndata wakawatia mbaroni? Je anafahamu kuwa na Dk Kanywaji–licha ya kuaibishwa na kutiwa majaribuni–amechukia uzembe huu wa mchana tena bila sababu na kama zipo ziko nyuma ya pazia?
            Tumalizie kwa kumpongeza Lukuviii kwa angalau kusema. Maana, alipotuhumiwa kughushi sifa za kitaaluma na yule gwiji wa kuwaumbua vihiyo Keinerugaba Msematruth. Kwa nondo ninazomwaga hapa wala Lukuviii asipoteze muda kutishia watu. Kwani ninalo tabu lote la Keinerugaba liitwalo Orodha ya Mafisadi wa Elimu. Ni bahati nzuri, wote waliotajwa humo akiwamo Bill tena wakati ule akiwa mkuu wa mkoa wa Bongo walifyata bila kwenda mahakamani. Sambamba na kumpongeza, ningetaka ajitokeze lau kimasomaso akanushe madai ya Msematruth ambayo ameyaweka kwenye maandishi. Ama kweli madai ya Lukuviii yanaacha maswali mengi kuliko majibu! Kazi kwa Dk Makufuli kumsefue ili liwe onyo kwa wengine.
Chanzo: Nipashe, Machi 19, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 20:46 No comments:

Tuesday, 15 March 2016

Kijiwe chastukia sanaa za Lukuvi


            Hivi karibuni Kijiwe kilibaki kinywa wazi na maswali mia kidogo baada ya mjivuni mmoja kuja na mpya kuwa alikataa rushua ya madafu bilioni tano. Kukataa au kupokea si issue. Kinachogomba ni kutotoa ushahidi hata kiduchu. Issue hii aliinyaka Mijjinga ambaye anaileta kijiweni ili tuidurusu.
            Baada ya Mijjinga kuingia kwa madoido na mbwebwe anaamkua na kumwaga stori. Yeye hataki kusema mengi. Anabwaga gazeti la Danganyika Daima mezani na kuanza kutoa stori. Anakatua mic, “Hebu jionee wenyewe baadhi ya wajivuni wanavyotugeuza majuha na hamnazo.”
            Kabla ya kuendelea Mpemba ambaye alikuwa akivuta uradi anaamua kumuuuliza, “Yakhe mbona mie sikuelewi? Wamaanishani na nani huyu anayetaka kuwafanya hamnazo na majuha na kwanini?”
            Mijjinga anampoka gazeti Mchunguliaji ambaye alikuwa ameishalinyaka na kuanza kusoma. Anasoma kichwa cha habari, “Bill Lukuvi akataa rushua ya bilioni tano.”
            Kabla ya kuzama kwenye habari kamili, Mgosi Machungi anadakia, “Kumbe unaongelea hizi Sanaa za kutaka kumridhisha Dk Kanywaji ambaye anaonekana naye kupenda sifa kiasi cha kuanza kuvurunda? Umeona uteuzi wake wa wakubwa wa mikoa? Kuna sura ambazo hazikufaa hata kuwa wakubwa wa kijiji achia mbali mikoa.”
            “Bila kujipendekeza usawa huu hupati ulaji,” anachomekea Mbwamwitu huku akicheka.
            Msomi haridhishwi na mada ya Mpemba inavyopelekwa ndivyo sivyo. Anakula mic, “Hii stori kwanza haikubalanced. Mwandishi aliyemhoji Bill alikuwa kama anamfagilia. Nashangaa hakumuuliza kwanini hakuwaita Takokuru wawanyake hawa watoa rushwa au kuna kitu hataki kijulikana kama si kutaka umaarufu wa shilingi mbili.” Anakohoa kidogo na kuendelea, “Hata kwenye maelezo yake marefu hajaeleza atafanya nini kukomesha mchezo huu na wale ambao wamekuwa wakiushiriki atawafanya nini.”
            Kabla ya kuendelea Mipawa anampoka mic na kusema, “Huyu jamaa sijui anatuona sisi hamnazo au vipi. Umeona alivyoficha majina ya hao wenzake ukiachia mbali kupoteza fursa adimu ya kuwatia adabu. Maana sheria iko wazi. Kama ukikuta mtu anatenda kosa la jinai au yuko kwenye harakati za kulitenda, unatoa taarifa kwa vyombo husika.  Je huyu–kama si kutaka sifa za shilingi mbili kama ulivyosema Dk Msomi–alishindwa nini kuweka mtego na kuwakamata wanaharamu hawa? Cha kushangaza utakuta wanaofanya hujuma hii kwa kaya ni ima raia wa karatasi au wachukuaji uchwara wanaoshirikiana na akina Bill hao hao wanaojifanya kuwageuka. Si waseme kuwa dili halikuwaiva.”
            Mgosi Machungi naye anapoka mic na kuronga, “Hebu tifanye anaisis kidogo hapa. Kwanza, kwanini Bii ameficha majina ya hawa jamaa kama si washiika wake? Pii, imekuwaje hakutaka kuwakamata ii afichue mtandao wote wa wanaoibia kaya? Je inakuwaje seikai iuziwe aidhi yake yenyewe kama hakna namna? Je hawa jamaa waijuaje kuwa Kigamboni kutakuwa mai au nao wana siikai yao ndani ya siikai? Tiambie tiewe bwana Bii popote uiko.Vinginevyo huu ni uongo wa kawaida kama si usanii tu. Go tell it to the birds Bill humpati mtu hapa.”
            Msomi anaendelea, “Mimi hakuna aliponiacha hoi Bill kama kusema eti kuna wakubwa wamejilimbikizia ardhi lakini asiwateje wala kusema atawachukulia hatua gani. Ni ajabu kuwa na watu wanaofanya vitu kana kwamba hawakwenda shule. Unawezaje kuja na madai ya kitoto kama haya usichelee kuumbuliwa na wasomi kama sisi? Nadhani–kama rahis Kanywaji asingekuwa anendesha kaya kama mali yake binafsi kwa kujizungushia marafiki na waramba viatu–Bill alipaswa kutumbuliwa jipu mara moja. Maana hafai hata kidogo.”
            Mheshimiwa Bwege anaamua kula mic, “Nyie kumbe hamfahamu hizi Sanaa? Kwani hapa kuna utumbuaji majibu au vipele na vijipu uchungu? Huwezi kutumbua majipu ukawa na watu kama Bill au Muongo wanaokumbwa na kashfa kama vile kughushi na Escrew. Mie sitaki nionekane mwanga. Huyu jamaa atachemsha muda si mrefu. Mliona alivyokwenda banki kubwa kwa pupa na kutoa maagizo kuwa wafanyakazi hewa wafutwe badala ya kuagiza waliowaajiri wapelekwe kwa pilato? Huku ndiyo kutumbua majipu au kuyafuga. Yeye anatoa amri ya kufutwa majina badala ya kuyatumia kama ushahidi kama nani? Kwani hii kaya ni mali ya mama yake? Kama yeye anafanya hivyo, kwanini wapambe na waramba viatu wanaotaka kumuingiza mkenge wasifanye mambo ya hovyo kama Bill kutoa habari za uongo?”
            Kanji aliyekuwa anateta jambo na mshikaji wake Sofia Lion aka Kanungaemba anakula mic, “Hata mimi hii iko changanya mimi sana. Sasa kama yeye shinda kamata hii jambazi natangaza nini kama si ongo tupu? Kwanza mimi hapana ami kama swahili naweza pewa feza kuba kama hii natakataa wakati sahara yake dogo sana.”
            Sofi anamuunga mkono Kanji, “Kuna uwezekano mkubwa kuna ukweli uliofichwa. Maana, ukiangalia usawa huu, na namna habari yenyewe ilivyoparaganyika na kuacha maswali mengi, unashindwa kuelewa lengo la Bill. Kama ni kutaka umaarufu nadhani hapa amepiga chini. Naungana mkono na wanaotaka atumbuliwe haraka. Maana, naye ni jip utu.”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si likapita shankupe la Bill. Acha tuliotoa mkuku tukitaka tumtumbue jipu kama bosi wake anamgwaya au kumkingia kifua!
Chanzo: Tanzania Daima, Machi 16, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 18:45 No comments:

Magufuli usitegemee kuombewa uchukue hatua

            Akiwa mkoani Arusha baada ya kuweka jiwe na msingi la ujenzi wa barabara ya inayoelekea Nchini Kenya yenye urefu wa Km 234.3 hadi Holili rais John Pombe Magufuli aliwaambia wananchi kuwa Tanzania ilikuwa imegeuzwa shamba la bibi. Pia aliwaomba wamuombee ili aweze kufanya kazi ngumu ya kuisafisha nchi na kuirejesha kwenye mstari, kazi ambayo ni hatari na ngumu. Magufuli aliyasema haya huko Tengeru.
            Kwanza ni kweli kuwa Tanzania tangu baada ya kung’atuka kwa baba wa taifa Mwl Julius Nyerere mwaka 1985 hadi Magufuli anaapishwa, ilikuwa si shamba la bibi tu bali chaka la wezi waroho na wenye roho mbaya. Kimsingi, tawala zote ukiondoa wa awamu ya kwanza, ziliongozwa na viongozi wasio na visheni wala uchungu na taifa. Ili tusionekane tunawapunja marais wastaafu, tutatoa mifano. Nani mara hii amesahau kuwa serikali ya awamu ya pili iliyosifika kwa falsafa ya hovyo ya ruksa iliasisi ufisadi? Rejea kashfa ya uuzwaji wa mbuga ya wanyama ya Loliondo, vimemo vya mikopo ya daladala na utoaji wa viwanja. Awamu ya pili iliyofuata ya Benjamin Mkapa ya kauli mbiu ya Ukweli na Uwazi vilivyokuwa kinyume imeondoka na kashfa nyingi kuliko ya awamu ya pili ya Ali Hassan Mwinyi. Kwani, hadi anaondoka madarakani, Mkapa alikuwa ameasisi kashfa za EPA ambayo iliasisiwa kumsaidia mgombea aliyeshinda na kumrithi Mkapa, Rada, Ndege mbovu ya rais, uuzwaji wa iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Ubinafsishaji wa kijambazi, uzururaji uliofanywa na rais na washikaji zake, na mwisho wa yote utwaliwaji wa Machimbo ya Makaa ya Mawe ya Kiwira kati ya mengine bila kusahau NGO ya ulaji ya mkewe ufisadi uliorithiwa na mke wa aliyemrithi. Hadi sasa Magufuli ameuepa mtego huu. Kwani, hatujasikia NGO ya mkewe.
            Baada ya Mkapa kuondoka madarakani, iliingia awamu ya nne ambayo imevunja rekodi kwa uchafu.ilifikia mahali watu wakasema nchi ilikuwa ikijiendesha. Wengine walisema ilikuwa kama ndege au meli iliyoko kwenye autopilot–hawa kwa kiasi fulani waliipendelea. Rais wa awamu hii Jakaya Kikwete alisifika kwa kupenda kuzurura nje hadi akaitwa Vasco da Gama, yule jambazi wa kireno aliyezunguka dunia akitafuta makoloni na sehemu za kuiba. Kikwete atakumbukwa kwa kuwa na serikali kubwa isiyofanya kitu (a big and do-nothing government) iliyoundwa ima na marafiki zake wa karibu, waramba makalio na wengine wengi. Kikwete hakuachia hapo–kama alivyodai waziri wake mmoja January Makamba kuwa serikali ya Kikwete ilijaa kulindana na kuoneana aibu–aliruhusu mafisadi kila aina wajiibie watakavyo kiasi cha kugeuka hiki anachosema rais Magufuli–shamba la bibi.
            Historia ya uovo wa serikali za awamu za pili, tatu na nne ni ndefu. Kwa vile Magufuli amegundua huu uhovyo, ugumu na hatari ya kazi yenyewe na jinsi waliozoea kunufaika na upuuzi huu wanavyotaka kumkwamisha, anapaswa kuchukua hatua madhubuti za–ikiwezekana–kuwakamata kwanza akasema baadaye badala ya kusema kabla hajawaweka sehemu salama. Nadhani alipoua Edward Sokoine alikuwa shule. Hata hivyo, anajua kilichotokea. Hivyo, tunamkumbusha, awe msiri kama chui. Akamate kwanza atangaze baadaye. Hana haja ya kulalamika wala kueleza mipango yake zaidi ya kukamata kwanza akatangaza baadaye. Anapaswa awe simba mwenda kimya badala ya kuwapa faida wabaya zake ambao ni wabaya wa wananchi.
            Tokana na ugumu na hatari ya kazi anayofanya Magufuli alisikika akiomba wananchi wamuombee. Kuomba si jibu wala siyo kile anachopaswa kufanya. Wananchi watamwombea. Ila ajua maombi mengine huwa hayajibiwi au hujibiwa baada ya muda mrefu hasa ikizingatiwa shaka ya usafi wa wanaomwombea ambao wanaweza kuhongwa udohodoho au hata wengi wao kutamani wapate fursa waibe. Hao hao anaotaka wamwombee wengi wao ndiyo wanaokula na hao anaotaka kuwatumbua majipu. Unaweza kuona jinsi ulivyoibuka utitiri wa makanisa, makundi na viongozi wa kiroho kujifanya wanaliombea taifa kana kwamba lilipokuwa likigeuzwa shamba la bibi hawakuwapo. Hawa wanaomba kweli au wanatafuta ukaribu na ulaji? Tanzania–nilishaandika mara nyingi tu–ahitaji kuombewa bali kuambiwa na kukombolewa na watu wasio na mchezo na nyani. Hata Magufuli ahitaji kuombewa bali kusadiwa na kushirikiana naye kufichua maovu.
            Hivyo basi, tumalizie kwa kumshauri Magufuli aachane na matangazo, malalamiko wala maombi. Badala yake akamate majibu na kuyakamua kimya kimya halafu atangaze. Akiendelea na staili hii, atakwamishwa kweli kweli hata na wale anaodhani ni wenzake wakati ni maadui zake. Wapo wengi waliomuunga mkono wanaojuta kwa kufanya kosa kubwa tu. Kama alivyowaambia viongozi wa Jumuia ya Afrika Mashariki, awahakikishie waovu hawa kuwa walifanya kosa kubwa kumuunga mkono na kumpitisha wakati wao ni wachafu kama nguruwe hata wawe wakubwa kiasi gani.  Kama Magufuli anataka kuikomboa Tanzania basi aanze kuwatumbua hawa waliosababisha iwe shamba la bibi. Kwani walizembea kwenye majukumu yao. Anawajua; tunawajua; na wanajijua.
Chanzo: Tanzania Daima, Machi 13, 2016.
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 18:44 No comments:

Janga la taifa: Vyuo vikuu vinapoeneza ujinga

St. Joseph University In Tanzania Logo.png
            Kashfa ya hivi karibuni iliyokikumba Chuo Kikuu cha St Joseph inapaswa kulifumbua taifa macho. Baada ya kuingia kwenye sera mbovu za kiliberali mamboleo za kubinafsisha kila kitu, nchi nyingi za kiafrika–ikiwamo Tanzania–zilipwakia kila aina ya takataka na ujinga. Tuliambiwa kuwa ubinafsishaji ndiyo chachu ya maendeleo ingawa maendeleo yenye hatujayaona. Badala ya uwekezaji kuleta maendeleo, umeleta maanguko katika nyanja nyingi ikiwemo elimu.
            Nyanja ya elimu nchini ni mojawapo ya maeneo yanayoonekana kuathiriwa na sera za hovyo za uhuria ambao umegeuka uholela. Hivi karibuni kulifumka kashfa ambapo St. Joseph kilifungwa kutokana na:
            Mosi, kutoa elimu chini ya kiwango ambayo matokeo yake ni wahitimu kuondoka chuoni wakiwa wamesheheni ujinga kiasi cha kutofanana na elimu wanayodai kuwa nayo ukiachia mbali kutoajiri. Hali hii ina athari kama vile kupoteza wahitimu muda ukiachia mbali kuwanyima hali ya kujiamini na kutoweza kuajirika kirahisi.
            Pili, licha ya kutoa elimu chini ya viwango, iligundulika kuwa chuo hiki kilikuwa kikiwalangua, kuwahadaa, kuwatapeli na kuwaibia wanafunzi kwa kuwajaza ujinga. Je viko vyuo vingapi kanywabwoya kama hivi nchini na vimeishaibia na kuwahadaa ukiachia mbali kuwajaza ujinga wangapi?
            Tatu, kuajiri wakufunzi wasio na ujuzi wa kutosha wala kukidhi viwango wa ufundishaji kwenye vyuo vikuu. Tunadhani kuwa kufungia chuo si jibu. Kwani  chuo husika licha ya kufuja dhamana yake kimetenda makosa mengi ya jinai kama vile kutoa elimu na huduma mbovu, kulangua wanafunzi, kuharibu maisha ya wanafunzi, kuwaibia na pia kukiuka taratibu za uendeshaji taasisi ya elimu ya juu. Hivyo, chuo husika kinapaswa kuchuliwa hatua mojawapo zikiwa, kurejesha fedha za waathirika, kuwaomba msamaha, kuwalipa fidia wahusika na yote katika yote, kupigwa marufuku kutoa huduma yoyote ya kielimu nchini ili liwe soma kwa wengine wenye mawazo ya kuligeuza taifa letu shamba la bibi.
            Mapungufu hayo matatu ni kati ya mengi ambayo hayakuwekwa wazi. Hata hivyo, malalamiko ya wanafunzi yaliyokaririwa na vyombo vya habari ni kwamba chuo kilikuwa kikiwatapeli kwa kuwapa alama za juu wakati wahusika hawakuwa na ujuzi wowote. Hali inakuwa mbaya hasa pale ukosefu wa ujuzi uliotarajiwa unapobainiwa na mwanafunzi mwenyewe na si muajiri wala mtu mwingine.
            Je kwanini tumefika hapa? Nitaazima maneno ya rais John Pombe Magufuli aliyekaririwa akisema kuwa Tanzania ilikuwa imegeuzwa shamba la bibi na tawala mbovu na hovyo zilizopita ambapo kila kitu kilikuwa kikijiendea kana kwamba hapakuwapo na serikali. Kwa hiviyo basi, madhara ya ukosefu wa uongozi wenye visheni na mapenzi mwa taifa uliathiri kila idara na mahali nchini. Rejea jinsi umma ulivyomlalamikia waziri wa elimu na ufundi wa zamani Dk Shukuru Kawambwa kwa kuharibu elimu na rais ambaye alikuwa rafiki yake asimchukulie hatua.
Tokana na uoza huu uliokithiri nchini, tunashauri wizara inayohusika na Vyuo Vikuu ifanye yafuatayo:
Mosi, ihakikishe inatunga sheria na kupanga utaratibu wa kuwa na waangalizi na wakaguzi wake ndani ya vyuo vikuu vyote nchini.
Pili, ajira zote za walimu wa vyuo vikuu zisifanyike bila kuwasiliana na sheria ili kuangalia kama wanaojaliwa wanakidhi viwango vyote kuanzia elimu hata tabia kama vile rekodi za jinai, kwa wageni vibali vya kuishi na kufanya kazi nchini.
Tatu, kuwepo na utaratibu wa wizara husika na vyuo vyenyewe kutumia mfumo huria unaotumika sana vyuo vya nje wa wanafunzi kuwafanyia tathmini walimu wao kila baada ya kumaliza muhula. Katika utaratibu huu, wanafunzi hupewa fomu za tathmini ambazo huzijaza bila kuandika majina yao (Anonymous) ili kuepuka kuwajengea woga au kuchelea kupatilizwa na watathminiwa. Mfumo huu huwajengea kuthaminiana, kuheshimiana na kutendeana haki wadau yaani walimu na wanafunzi wao. Huu ni mfumo unaojenga demokrasia kitaaluma, kujali, kuchapa kazi na ufanisi wa hali ya juu katika vyuo vingi katika nchi za magharibi. Maana, kila mdau anamtathmini mwenzake vilivyo. Kimsingi, elimu yetu inatolewa kwenye mazingira kandamizi ya kikale ambapo baadhi ya maprofesa hujigeuza miungu watu kiasi cha kuwaumiza wanafunzi badala ya kuwasaidia. Wengine hutumia udhaifu huu hata kujiingiza kwenye rushwa za ngono ambalo ni janga kwa vyuo vyetu nchini. Ni dhahiri, hakuna namna ya kujua ufanisi au vinginevyo vya walimu kama hakuna mfumo wa kupata taarifa na tathmini ya wanafunzi. Mfumo huu huondoa ubabe na ujinga wa baadhi ya walimu kuwaonea wanafunzi na kujiona kama miungu. Pia mfumo huu huondoa utegaji na ubabaishaji.
Nne baada ya serikali ya Magufuli kuthibitisha kuwa nchi yetu si maskini, kuna haja ya kuangalia namna ya kuwezesha kila mkoa kuwa na chuo kikuu angalau kimoja cha umma. Maana, unapokuwa na vyuo vingi vya umma, unapunguza uhitaji na uhaba wa vyuo kiasi cha kuondoa motisha wa majambazi yanayotumia elimu kuwajaza ujinga watu wetu.
Eneo jingine linalotaka uangalizi, ni kupambana na kughushi sifa za kielimu ambako husaidia na kuwezesha watu wasio na ujuzi kughushi na kuishia kuajiriwa kama walimu na wataalamu wakati si chochote si lolote.
Tumalizie kwa kuishauri serikali ikichukulie chuo husika hatua kali huku ikivisaka vyuo vingine hewa kama hivi ili kuepuka kulanguliwa na kuchezewa watu wetu. Unapochezea elimu, unaharibu mstakabali wa taifa kwa ujumla. Hivyo, suala hili lipewe uzito usio wa kawaida ili kuepuka kuendelea kuchezewa watu wetu  na nchi yao.
Chanzo: Dira
Posted by Ndugu Nkwazi N Mhango at 08:29 2 comments:
Newer Posts Older Posts Home
Subscribe to: Posts (Atom)

Cordially and unlimitedly welcome to this blog.


Writing and reading are two different processes but which share the same goal-to educate, communicate and entertain.
It is my pleasure to have you as the guest of this tablet.
I, thus, warmly and always, welcome you to share ideas.
Importantly and eminently, shall there be anything amiss or you think can advance this blog, please donate it.
Allow me to humbly and kindly welcome you once again.
Nkwazi N Mhango- A Man And a Half

When wisdom brings no profit, to be wise is to suffer. Not all thoughts are good and constructive. Others are even worse than bullets. The good thinkers are the ones that think constructively for the manumission of all bin-Adams regardless their diversity. Mwl. Nkwazi N Mhango,
Canada.


Epistle to Afrophobic South Africa

Epistle to Afrophobic South Africa

Magufulification

Magufulification

BORN NUDE

BORN NUDE

Total Pageviews

Heko Rais Magufuli

Heko Rais Magufuli

DECOLONISING EDUCATION

DECOLONISING EDUCATION

Kudos President Magufuli

Kudos President Magufuli

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

JOKEY HORSE-JOCKEY NORTH-SOUTH RAPPORT Diagnostic-cum-Prognostic-Academic Perspectives on Who Truly

The Family Friend of Animals

The Family Friend of Animals
Children's Book

Matembezi Mbuga ya Wanyama

Matembezi Mbuga ya Wanyama
Kitabu cha Watoto

Our Heritage

Our Heritage
Children's Book

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

How Africa Developed Europe:Deconstructing the His-story of Africa, Excavating Untold Truth...

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

Africa's Dependency Syndrome: Can Africa Turn Things around for the Better?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

'Is It Global War on Terror' or Global War on Terra Africana?

Perpetual Search

Perpetual Search

Africa's Best and Worst Presidents

Africa's Best and Worst Presidents

Psalm of the Oppressed

Psalm of the Oppressed
Psalm of the Oppressed

AFRICA REUNITE or PERISH

AFRICA REUNITE or PERISH
A new approach towards empowering Africa

BORN WITH VOICE

BORN WITH VOICE

Soul on Sale

Soul on Sale

Soul on Sale

Nyuma ya Pazia

Nyuma ya Pazia

We are one

We are one

SAA YA UKOMBOZI

SAA YA UKOMBOZI

Feel at home

You are always welcome to this epistle again and again time after time, ad infinitum.


Most read Posts

  • Sarkozy’s Take on African Fat Cats a Welcome Move
    At last the chicken are coming home to roost! French authorities made a groundbreaking decision by culling three most corrupt African presi...
  • Napanga kuanza kuuza mitumba na si maneno
    Ingawa mimi si mtumba, napanga kuuza mitumba. Nimechoshwa na jamii ya mitumba. Kila kitu mitumba. Mitumba, mitumba mitupu. Siasa za mitumba...
  • Better or Bitter Life for all?
    When I deeply muse on how an arrogant and brutal cabal of hoity toity (Coverted Con Men (CCM)) is tirelessly hoodwinking and dividing th...
  • Africa's Becoming more Despotic and Nepotistic
    "King of Kings" Gaddaffi The seven-day 40th anniversary of Libya strongman’s autocratic rule and charade elections in Gabon whe...
  • Kuna siku tutataifisha haya mahekalu haki ya nani
    Taarifa kuwa waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alinunua nyumba kwa zaidi ya shilingi bilioni moja licha ya kuwastua wananchi na...
  • Nyangumi mdogo akutwa amekufa ufukweni BC
    Hii ni picha iliyotolewa ya Nyangumi aina ya Humpback ambaye alikumbwa na maji na kutupwa kwenye ufukwe wa bahari ya Pasifiki kwenye eneo l...
  • Kikwete, Charity Begins at Home!
    President Jakaya Kikwete ...
  • Kweli binadamu si chochote wala lolote, wamkumbuka huyu?
    Walioko madarakani mkiabudiwa kama miungu au sanamu kumbukeni vijana hawa hata baba zao  ambao maiti zao zinaoza jangwani. Ungewaambia...
  • Pinda kulia hakutoshi, awajibike
    INGAWA kilio cha Waziri Mkuu, Mizengo Peter Kayanza Pinda, kinaonekana kuyeyusha hasira za Watanzania kwa muda, kuna haja ya kudodosa zaid...
  • Hawa si wachungaji bali ni fisi na mbwa mwitu
    KUMEZUKA mtindo mchafu na wa rejareja wa baadhi ya wachumia tumbo na matapeli kumtania hata kumtumia Mwenyezi Mungu kufanya utapeli na ujamb...

Followers

Blog Archive

  • ►  2023 (20)
    • ►  January (20)
  • ►  2022 (208)
    • ►  December (14)
    • ►  November (14)
    • ►  October (20)
    • ►  September (20)
    • ►  August (12)
    • ►  July (25)
    • ►  June (22)
    • ►  May (18)
    • ►  April (13)
    • ►  March (18)
    • ►  February (18)
    • ►  January (14)
  • ►  2021 (323)
    • ►  December (23)
    • ►  November (34)
    • ►  October (26)
    • ►  September (13)
    • ►  August (19)
    • ►  July (21)
    • ►  June (29)
    • ►  May (25)
    • ►  April (23)
    • ►  March (43)
    • ►  February (29)
    • ►  January (38)
  • ►  2020 (290)
    • ►  December (33)
    • ►  November (37)
    • ►  October (28)
    • ►  September (35)
    • ►  August (31)
    • ►  July (26)
    • ►  June (17)
    • ►  May (21)
    • ►  April (18)
    • ►  March (15)
    • ►  February (17)
    • ►  January (12)
  • ►  2019 (160)
    • ►  December (8)
    • ►  November (7)
    • ►  October (12)
    • ►  September (9)
    • ►  August (27)
    • ►  July (18)
    • ►  June (18)
    • ►  May (11)
    • ►  April (11)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (14)
  • ►  2018 (162)
    • ►  December (12)
    • ►  November (6)
    • ►  October (13)
    • ►  September (10)
    • ►  August (20)
    • ►  July (9)
    • ►  June (14)
    • ►  May (9)
    • ►  April (16)
    • ►  March (21)
    • ►  February (17)
    • ►  January (15)
  • ►  2017 (306)
    • ►  December (20)
    • ►  November (23)
    • ►  October (20)
    • ►  September (26)
    • ►  August (31)
    • ►  July (31)
    • ►  June (34)
    • ►  May (26)
    • ►  April (24)
    • ►  March (20)
    • ►  February (28)
    • ►  January (23)
  • ▼  2016 (269)
    • ►  December (22)
    • ►  November (21)
    • ►  October (22)
    • ►  September (15)
    • ►  August (12)
    • ►  July (27)
    • ►  June (24)
    • ►  May (23)
    • ►  April (29)
    • ▼  March (26)
      • Kijiwe chapanga kutembelea Zenj
      • Barua ya wazi kwa waziri mkuu Majaliwa
      • Lukuvi whom are you trying to dupe
      • Mlevi astukia 'ugesishaji' kaya
      • Kwa ndugu zetu mnaoamini kwenye dini za kigeni
      • SHUKRANI YA PUNDA
      • Kijiwe kupinga amri za Dk Kanywaji
      • How do you view and assess this stuff?
      • Makufuli mtumbue jipu Lukuviii
      • Kijiwe chastukia sanaa za Lukuvi
      • Magufuli usitegemee kuombewa uchukue hatua
      • Janga la taifa: Vyuo vikuu vinapoeneza ujinga
      • Leo natoka na Wanda Boys na vimbwanga vyao
      • Wakuu "wapya" wa mikoa, Magufuli achemsha
      • Boozer won’t pray for Mugful
      • Mlevi amtumbulisha jipu Sifui
      • Sijui kama wanaong'ang'ania madaraka walijifunza k...
      • Reunite East Africa instead of integrating it
      • Haya ni maombi au utapeli na ubangaizaji
      • Kijiwe: Makonda acha kudhalilisha walimu
      • Breaking news Sefue chini Ikulu
      • Cronyism, nepotism and nihilism: Hooray Makamba
      • Kwa wanandoa au watarajiwa
      • Mlevi kuwa wakili wa kujitolea kesi za mafisadi
      • Kijiwe chataka Kiquette ajitumbue kwanza
      • AFRICA REUNITE or PERISH chaanza kufundishwa chuoni
    • ►  February (27)
    • ►  January (21)
  • ►  2015 (399)
    • ►  December (34)
    • ►  November (24)
    • ►  October (22)
    • ►  September (34)
    • ►  August (29)
    • ►  July (37)
    • ►  June (22)
    • ►  May (32)
    • ►  April (35)
    • ►  March (46)
    • ►  February (47)
    • ►  January (37)
  • ►  2014 (502)
    • ►  December (47)
    • ►  November (49)
    • ►  October (47)
    • ►  September (37)
    • ►  August (40)
    • ►  July (42)
    • ►  June (30)
    • ►  May (35)
    • ►  April (47)
    • ►  March (44)
    • ►  February (39)
    • ►  January (45)
  • ►  2013 (400)
    • ►  December (37)
    • ►  November (27)
    • ►  October (31)
    • ►  September (26)
    • ►  August (34)
    • ►  July (39)
    • ►  June (28)
    • ►  May (40)
    • ►  April (44)
    • ►  March (39)
    • ►  February (26)
    • ►  January (29)
  • ►  2012 (598)
    • ►  December (27)
    • ►  November (26)
    • ►  October (27)
    • ►  September (30)
    • ►  August (47)
    • ►  July (95)
    • ►  June (86)
    • ►  May (119)
    • ►  April (83)
    • ►  March (23)
    • ►  February (17)
    • ►  January (18)
  • ►  2011 (261)
    • ►  December (20)
    • ►  November (19)
    • ►  October (20)
    • ►  September (21)
    • ►  August (27)
    • ►  July (12)
    • ►  June (15)
    • ►  May (20)
    • ►  April (27)
    • ►  March (32)
    • ►  February (24)
    • ►  January (24)
  • ►  2010 (205)
    • ►  December (25)
    • ►  November (23)
    • ►  October (23)
    • ►  September (23)
    • ►  August (17)
    • ►  July (13)
    • ►  June (12)
    • ►  May (10)
    • ►  April (18)
    • ►  March (9)
    • ►  February (16)
    • ►  January (16)
  • ►  2009 (163)
    • ►  December (19)
    • ►  November (14)
    • ►  October (11)
    • ►  September (6)
    • ►  August (12)
    • ►  July (9)
    • ►  June (11)
    • ►  May (20)
    • ►  April (22)
    • ►  March (14)
    • ►  February (12)
    • ►  January (13)
  • ►  2008 (191)
    • ►  December (12)
    • ►  November (11)
    • ►  October (14)
    • ►  September (15)
    • ►  August (16)
    • ►  July (23)
    • ►  June (10)
    • ►  May (19)
    • ►  April (16)
    • ►  March (19)
    • ►  February (17)
    • ►  January (19)
  • ►  2007 (33)
    • ►  December (13)
    • ►  November (20)

About Me

My photo
View my complete profile

Travel theme. Powered by Blogger.