The Chant of Savant

Saturday 31 May 2014

Mlevi amshangaa mheshimiwa bwege

Mbunge wa Kilwa Kusini Selemani Ally Bungara aka Bwege
         Hivi karibuni mlevi ataingia kwenye majarida ya uvumbuzi ya kaya kwa kuwa msomi wa kwanza kugundua chanzo cha mipasho mjengoni. Nisingekuwa nimeishapata PhDs zangu ningefanya uvumbuzi huu kuwa thesis au tasnifa ya andiko langu.
Jamani sizushi. Msidhani hangovers za gongo na “hangunders” za bangi vinanisumbua hadi kuwakosea hishima waishiwa wahishimiwa wasio na hishima. Hakuna kitu kilikuwa kinanisumbua kama kitendo cha kutamalaki mipasho matusi hata vijembe na taarabu mjengoni kuanzia mjengo mkuu hadi ule wa Katiba na constitution ya constipation.
Katika utafiti wangu niligundua kuwa kumbe nilikuwa nakosea katika kuangalia watafitiwa wangu vizuri kwa kuogopa kuvunja kile ambacho watafiti huita Nuremberg Code ambapo mfanya utafiti anabanwa asimfiche wala kumfanyia upepelezi mtafitiwa au kumtenza kama kitu au mnyama. Mambo ya kitafiti na kisomi tuyaache. Maana huwa yaboa tu.
 Hivyo, juhudi zangu za kujua ni kwanini mijengo yetu imegeuka vijiwe vya mipasho na upuuzi mwingine ziligonga mwamba hasa kuogopa kuwapeleleza waishiwa wahishimiwa.  Hata hivyo, bwege mmoja alinisaidia kugundua kuwa kumbe ubwege ni sababu mojawapo. Kwa lugha ya kawaida ni kwamba kuna mabwege wengi mijengoni kiasi cha kutamalaki mambo ya hovyo ambavyo, mara nyingi, huthibitisha ubwege wa wahusika. Msidhani natukana. Ninachofanya hapa ni kutoa uchambuzi wa kitaalamu na kilevi ili waathirika wagundue chanzo cha masahibu yao kiasi cha kuishia kushuhudia maigizo runingani huku waigizaji wakiwa mabwege mjengoni.
Punde si punde nilipata clue nyingine toka kwa naibu microphone Jobless Nduguy alipodai kuwa mjengoni kuna waishiwa wanavuta mibangi na kubwia mibwimbwi. Hiyo ni clue ya kwanza tena toka kwa mwenzao na kiongozi wao.
Juzi nilipata lead nyingine toka mjengoni kwenye kile ambacho wamasai huita from the horse’s mouth. Nilimsikia mwenyewe mjengoni muishiwa mhishimiwa mmoja kutoka kusi tena kisiwani akimtishia waziri maji. Du nimesahau! Naibu kipaza sauti si alimuuliza jina lake. Naye akaijibu, “Mimi naitwa Sele Seydou Ali Bunga’ Bwegee!” Alijibu hivyo mara tatu kuonyesha kuwa hatanii.  Baada ya kusikia hivyo nilisikia mkota mmoja akisema, “La haula wala quwata illa billah! Si heri mngejaza walevi na wavuta bangi mjengoni kuliko mabwege.”
Baada ya bwege kukiri kuwa ni bwege tena maarufu, Mlevi niligundua kuwa kumbe kuna mabwege wengi. Wapo mabwege wanaotishia kwenda mwituni wakati wanasifika kwa kuuchapa usingizi mjengoni tena kibwegebwege huku midomo ikiwa wazi na udenda ukiwatoka. Wapo tena mabwege wanaotishia walevi kuwa wasipokubaliana na upuuzi wao ndutu zitachukua kaya.
Pia wapo mabwege wanaosifika kutoroka vikao mjengoni huku wakijidai wanawawakilisha walevi. Kama si ubwege nini kwa mwakilishi kukosekana pale anapopaswa kuwa kuwawakilisha anaodai kuwawawakilisha? Mabwege wengine ni wale wanaounga mkono kila upuuzi simply because sirikali inayotawala ni ya chata lao. Mabwege wa namna hii wanashindwa kuchagua baina ya wale waliowapa kura ya kula na hicho kijichama.
Orodha ya mabwege ni kubwa tu. Wapo mabwege wanaolilia kuitwa wahishimiwa hata kama wanayofanya hayastahili hishima.  Mkinichagua mie kwenda kuwawakilisha mjengoni kitu cha kwanza nitakataa kuitwa mhishimiwa. Nitapenda niitwe ndugu kwa vile mimi ni ndugu yenu wala si mkoloni wala mpenda sifa wala bwege. Mie ni mlevi, finish. Mabwege wengine ni wale wanaocheza makidamakida mjengoni kwa kuwaita wenzao Boko Haram. Sijui wanafanya hivyo kwa sababu wanaongozwa na makidamakida au wasanii?
Mabwege wengine ni wale waliostukiwa hivi juzi kuwa wameghushi vyeti vya kitaaluma. Ni ubwege kiasi gani kwa mtu kuogopa umande halafu akajiita msomi wakati usomi wenyewe ni wa kughushi. Mabwege hawa wana bahati. Kwani kuna mabwege wakubwa wanaowakingia kifua pamoja na kutuhumiwa miaka mingi iliyopita.
Aina nyingine ya mabwege ni ile iliyoingia mjengoni kwa njia haramu kama vile kupata umaarufu kutokana na ukoo au madhehebu yake ya mfukoni. Ni ubwege kiasi gani, kwa mfano, kuchanganya dini na siasa au udugu na kazi za umma? Je hatunao mabwege waliomo mjengoni simply because ni watoto wa wakubwa fulani au waliongia kwa mchongo fulani?
Mabwege wengine ni wale waliosimikwa pale kufanya kazi moja tu, kutetea fisadi kama dada yangu Annae cheza Makidamakida aliyesimikwa na mafisadi baada ya kumwengua rafiki yangu Sam Sixx baada ya kumsulubu Eddie Luwasha na Richmonduli yake.
Mabwege wengine ni wale wanaokaa upande mwingine wakatoa majibu ya kipuuzi kwa maswali muhimu ya waishiwa mjengoni. Bwege mmojawapo ni Sossie Muongo aliyelipuliwa na David Kafulia kuwa yeye na wenzake waliiba njuluku za walevi halafu badala ya kujibu tuhuma akaanza kudai eti wabaya wake wanazua ili kumng’oa. Prof mzima anakuwa muongo kiasi cha kujikuta kwenye kundi la mabwege mjengoni!
Makala hii haiwezi kuisha bila kuwataja mabwege wanaoongea kiswangilish mjengoni wakati hawajui chochote si kitasha wala kiswazi bali usanii mtupu. Hivi ni ubwege kiasi gani kwa mtu anayedai kuwawakilisha awawakilishao kutumia lugha wasiyoelewa? Anadhani nao ni mabwege kama yeye washobokee lugha za watu?
 Napiga picha nikiitwa na kipaza sauti au naibu wake akiuliza jina langu nami najibu profesa Mlevi mkuu kutoka Ukanadani. Naona yule anatikisa kichwa kudhani kuwa sifai kuwa mjengoni kwa vile ninaishi kwa mibangi gongo na madude mengine yanayowanyotoa roho walevi. Heri walevi wanaolewa kama komba kuliko mabwegwe wanaobwabwaja na kufanya mambo kibwegebwege kama kupashana na kutukanana au kuuchapa usingizi.
Sikuamini mjengoni kunaweza kuwa na bwege hata mabwege wengi tu. Sijui mna mabwege wangapi mjengoni hasa nikiangalia mambo ya kibwegebwege yanayoendelea humo?
Tumalizie kwa kuwasihi mabwege wanaochagua mabwege kuacha ubwege wa kuchagua mabwege ili wakafanye mambo ya kibwege kiasi cha kaya yetu kuonekana kaya ya mabwege au kila mwandishi mmoja aliita pepo ya mabwege.
CHANZO: NIPASHE 

Thursday 29 May 2014

Uchumi mnao ila mnaukalia


       Marehemu baba wa taifa mwl Julius Nyerere aliwahi kusema kuwa Tanzania uchumi tunao ila tunaukalia. Wapo waliomwelewa.  Pia wapo ambao hawakumuelewa kiasi cha kumtafsiri walivyojua na walivyotaka. Habari kuwa Tanzania inapoteza dola za kimarekani bilioni 1.8 kwa mwaka tokana na utawala na usimamizi mbovu wa raslimali za nchi ni ushahid wa usemi huu. Nia ajabu zilipotangazwa viongozi wetu hawakukereka wala kuona lau aibu. Wameendelea na upuuzi ule ule kudai wapo kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wakati ni unafiki mtupu.
Hukuna kuzungusha. Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndiyo imetufikisha hapa. Ajabu wakati ikitusaliti na kutuuza mchana kweupe walevi wake wa madaraka wanapoteza pesa na muda wetu kutwambia nani anafaa kutuongoza kwa kuwakandia wapinzani wakati wa kuambiwa hawafai ni hao hao walimu wetu wa nani atuongoze na mfumo upi ututawale. Ajabu hawa wanaoshindwa kusimamia raslimali zetu wanajisifia ubingwa wa kuombaomba na kukopa kopa wasijue wanazidi kuzamisha taifa! Wengine wamestaafu na kujiingiza kwenye magendo na uchuuzi.
          Sikumbuki kumsikia katibu mkuu wa CCM Abdulrahaman Kinana wala katibu wa uenezi, Nape Nnauye wakiongolea uchafu huu zaidi ya kuendelea na wimbo ule ule wa jogoo. Lau kutokana na chuki za kibinafsi na ukweli wa hali halisi ya mparaganyiko wa serikali Nape amerudia kuwaita wenzake mizigo japo naye ni mzigo huo huo. Huu ni ushahidi kuwa tusingekuwa na viongozi na watendaji mizigo, kwa raslimali tulizojaliwa Tanzania haipaswi kuwa maskini. Sana sana ilipaswa kushindana na Singapore na Korea ya Kusini nchi  ilizokuwa ikizipiku kiuchumi wakati wa kupata uhuru.
 Bahati nzuri habari hii ilitoka wakati wa ziara yao mkoani Tabora. Watu wa Tabora walitumia fursa hii kumtumia salamu rais Jakaya Kikwete kupitia kwa Kinana wakitaka atimize ahadi yake ya kujenga bomba la maji toka ziwa Nyanza. Nadhani wangemwendea angesema hakuna fedha ya kufanya hivyo wakati serikali yake ikisifika kwa upuuzi wa kuacha wageni waje wachote na kwenda kujitajirisha wao na nchi zao wakati watu wetu na taifa letu wakiendelea kutopea kwenye umaskini wa kutengenezwa na watawala wavivu wa kufikiri kama aliyeanzisha msemo huu. Kujitoa kimasomaso na kukwepa uwajibikaji, Kinana aliwarushia lawama viongozi wa afya akisema, “Viongozi hawa ni wazembe, wamangimeza na warasimu wanaokwamisha maendeleo ya wananchi. Nakwenda kushikana nao mashati ni lazima wasajili zahanati hizo.”  Ama kweli nyani haoni nonihino lake! Kuna wazembe kama viongozi wa juu wa taifa wanaoruhusu uchumi wetu kunufaisha majambazi wa kimataifa wanaoshirikiana nao? Sikutegemea lolote toka kwa Kikwete kwa kujua fika yeye ndiye mzizi wa balaa hili.
          Hakuna kilichokera kama kugundua kuwa deni la taifa limeumka huku tukipoteza pesa ambayo ingeweza hata kulilipa tena pesa yenyewe tuliyopoteza ndani ya miaka kumi tu. Japo Nyerere alisema: Uchumi tunao tumeukalia, unaweza kuongeza: Akili tunazo lakini hatuzitumii na kama tunazitumia basi ni vibaya na mbaya.
          Kuna viongozi wababaishaji na wasanii wanaotoa ahadi wasizitekeleze ukiachia mbali wanaodandia mambo ya kuwarushia lawama wengine wakati wa kulaumiwa ni wao kama tulivyoonyesha hapo juu. Kuna viongozi manunda na manyang’au wenye uroho na roho mbaya. Hata uwaseme vipi wanajifanya hawasikii wala hawaoni na kuendelea na jinai yao ya kuhujumu taifa letu. Juzi mbunge wa Kigoma Kusini kwa mfano amewatuhumu maafisa wakubwa wa serikali kwa wizi wa shilingi bilioni 200 toka Benki Kuu. Ajabu ya maajabu hakuna anayewashinikiza wawajibishwe na kuchunguzwa hata kuchukuliwa hatua za kisheria. Nani amwambie nani wakati wote lao ni moja? Ni bahati mbaya kuwa na wananchi wetu nao wamekuwa kama kondoo wanaojirahisi kuelekea machinjioni. Hwafurukuti wala kuonyesha hasira zao. Imefikia mahali habari kama hizi zenye kuchusha na kukera zinaonekana kama udaku na burudani kwa waathirika maskini wa nchi hii. Uchumi yaani akili wanazo lakini wanaukalia. Uchumi yaani umoja na nguvu wanavyo lakini wanavikalia huku wakalia kulia na kulalamika bila kuchukua hatua. Wanaliwa lakini hawastuki. Je tatizo ni nini? Woga, au ukosefu wa uaminifu na uzalendo kwa watu binafsi?
          Jiulize ni kiasi gani cha madini tunapoteza kila mwaka ukiachia mbali pesa ya kodi ambayo imefikia hizo dola za kimarekani takribani bilioni mbili? Je ni watalii kiasi gani wanaingizwa kinyemela kutokea nchi jirani ukiachia mbali wanyama wanaouawa kwenye ujangili hadi kuweza kusafirishwa wakiwa hai bila mamlaka kufanya lolote? Tanzania ingekuwa na watu makini na wenye kupenda taifa lao bila shaka serikali ya rais Kikwete ingeishatimuliwa miaka mingi iliyopita. Lakini nani wa kumwajibisha nani iwapo hata watu binafsi hawako tayari kuwajibika kwa nafasi yao kwa kulikomboa taifa lao toka mikononi mwa wababaishaji na matapeli wa kisiasa?
          Jiulize taifa linapoteza mabilioni kiasi gani kwa kulipa wafanyakazi hewa, walioghushi wasiofanya kazi bali kubabaisha na matumizi mengi ya kipumbavu kama ilivyogundulika hivi karibuni ambapo tiketi za ndege za wakubwa kwenda kutanulia nje zililanguliwa mara 16 na serikali ikaendelea na wimbo wake wa kuleta maendeleo kwa watanzania? Mnaleta maendeleao au maangamio?
          Jiulize ni wahalifu kiasi gani toka Asia na kwingineko wamegeuza Tanzania kichaka cha kufanyia uovu wao. Mmojawapo wa hivi karibuni ni yule anayejidai kununua IPTL wakati ni mwizi wa kawaida.
          Imefikia mahali mtu akikutajia jina Tanzania kinachokuja akilini haraka haraka ni utapeli, usanii, uzembe, ubabaishaji na maangamizi ya kujitakia. Kuna kipindi watu walilalamikia ujenzi wa viwanja vya ndege binafsi kwenye machimbo ya madini ambavyo vinatumika kutorosha madini. Ajabu watanzania wameendelea na mambo yao kama kawaida kana kwamba kadhia hii imeshughulikiwa. Kwa kujua udhaifu wao serikali wala huwa ahangaiki na kutatua kero yoyote zaidi ya kuongeza spidi ya kula na kufanya madudu.
           Wakati wa kuwataka watanzania watumie uchumi wao uwe raslimali, akili, urathi wa utulivu na nyingine nyingi kujikomboa badala ya kuendelea kushikwa matekwa na genge la wahalifu ni huu. Hakika, uchumi mnao ila mmeukalia tu.
Chanzo: Dira Mei 2014.

Wednesday 28 May 2014

Bongo’s rich save’s poor bongo

 
When news came out that Bongolalaland loses zillions of dosh thanks to insane admin, boozers pinned down the cause of this entire spooky and creepy situation. However boozers have been quick to blame their monarchs, we need to know who sustain those guys? If anything, the worst injury a society can inflict to itself is nothing but the culture of carelessness and complaining without taking actions. If you allow them to screw you up why don’t they do so? Kick their ass and see if there’ll be such megalomania. You too are to blame except me who tells the right thing to do.
Look at what’s been going on in Dom where some jet-set-smoothies are eating boozers’ dosh under the pretext of writing a new constitution that’s become a new constipation. What have swiggers done to arrest and foil such blatant theft by consent? Interestingly, thieves, sometimes, laugh at boozers simply because they are always downed so as to be robbed. Who’s the right to laugh at another? Nyani haoni nonihinole! Again, looking at begging pilfers while they allow other foreign thieves to rob them and the boozers, you wonder. The amount so stolen by crooks that conspire with ultra-greedy and egoistic official is not only staggering but also jaw-dropping. I am told that for only ten years almost 20 trillion Dollars have been siphoned from the hunk.
More of stolen dosh, one fyatu tried to put in perspective what the hunk loses annually saying that such humongous dosh can build 374 ultra-modern dispensaries at the cost of $5 million (approx. 8 bn dafus) each or refurbish the dilapidated Central Railway Line.
This whooping sum would enable the hunk supply water to at least a half of boozers in the hunk. If it spent on kanywaji, it can make all boozers happy for almost a year. If spent on education though it is not a spiffy idea, for it can wake up boozers, such amount would enable all university students to study comfortably and get their degree instead of forging. If this humongous amount would be spent on vehicles for boozers, quarter of all boozers would get mikangafu.
So too, alternatively, the amount could enable obsolete BongoAir to purchase at least 30 Airbus A320 passenger jets at the cost $60 million each.
Jokes aside, Global Financial Integrity (GFI), the US-based international financial overseer, says in its latest report that from 2002 up till 2011 Bongo lost $18.73 billion.
True, the hanky panky of losing zillions proves my belief that Bongo’s richer save that it’s poor bongo or brain. If boozers can get a soul to man their affairs with just common sense to think and act sanely chances of forging ahead are big. Looking at how much boozers lose annually, I found that for just ten years they lost more than their internal and external debts put together at the time the current cabal of eaters came to clout. I won't wonder to hear that Bongo’s contributing to the economies of India, Singapore and Switzerland hugely. While this simian biz goes on, boozers’ head is always globetrotting under the pretext of begging. It is only recently boozers discovered that their man doesn't aim at begging but soliciting per diem. Had they had a sane head, he'd have manned the hunk wisely and pay himself even bigger sums than the peanut he gets from per diem. Given that there’s a lack of common sense; boozers are making less important things important as important ones are made less important. This reminds us of the epic foolish monitor that used to run to the lake to avoid shower or the foolish fish that used to beg for water while it lives in the lake. All the same, wonder not. When you see a guy in an expensive suit kow tow before donors begging while he allows more dosh than he begs to be stashed abroad know something’s wrong upstairs.
 So, when I say there’s a vacuum or absence of common sense I don't mean to abuse or belittle anybody save to tell the naked truth.
If you wake me up in the middle of the night and ask why Bongo’s a begging hunk, I’ll look in your eyes straight and tell you to go to hell or to go and tell it to the birds. Bongo is not supposed to languish in begging. Methinks the reason’s what mzee Ben Makapi’d call being lazy at thinking something he’s good at though he did see it on others. He sold everything at a throwaway price. What followed is disaster so to speak. Other crooks came in and finished his job of ruining the hunk. Evidently, you can see it on how all types of criminals, thieves and thugs, dope peddlers and drug barons became tycoons overnight and nobody’s questioning them. How many rich thieves do you know that screwed the hunk up to become billionaires?         
Rib cracker: India this year won a trophy of open defecation not to “dig medicine” or chimba dawa but just downloading in the bush. India’s 600 million defecators compared to Africa that has more cellphones than toilets. For the first time, Africa’s beaten in this mess. What development in underdevelopment! I can’t imagine seeing a boozer doing his things in a bush while talking on phone!
Source: Guardian May 25, 2014.

Tuesday 27 May 2014

Banda Reaping What She Sowed

It’s obvious that outgoing Malawi president, Joyce Hilda Mtila Banda’s poised to lose. However, when Banda took the reins of power after the death of her forerunner, Bingu wa Mutharika, as a woman, she received a lot of palms not just as a hard worker but just as a woman. Before Banda and her Liberian counterpart, Ellen Johnson Sirleaf, came to power, there’s a mystical-cum-mythical belief that female presidents are less corrupt, thus, having one on the helms might save the country she mans from corruption. Again, after the duo displayed their true selves and the way they run state affairs, the belief slowly dissipated. Banda, just like Sirleaf, didn't bring in any fresh air. For, the duo proved beyond doubts that corruption knows no sexual characteristics.
Now it is an open secret that Banda will go down as Malawi’s only-two-year president. However, Banda won’t throw in the towel easily. After sensing  defeat, she decided to annul the elections though in vain. She’s quoted as saying, “As president I have used the powers conferred upon me from the constitution to declare the elections null and void.” After such an announcement, Malawi Election Commission (MEC) went to court and obtained an injunction that allowed it to go on counting votes.
 True, Banda did deservedly reap what she sowed. If there’s anything, if anything, Malawians weren't ready and able to forgive and forget is nothing but cashgate, the scam that sealed Banda’s fate as far as presidency is concerned. Malawians waited for the opportunity to show Banda that they’re not mugus or big idiots as Nigerian scammers call their dupes. The anguish became so big that Banda wouldn’t  have survived. How’d she survive amid such a mega scandal that added more pangs and twangs to the already frustrated Malawians? Ironically, it seems that Banda and her advise-givers didn't see this danger coming.
Eight months in power Nyasa Times had this to write, “Eight months, the majority of those getting government contracts have political connections to the ruling People’s Party (PP).” PP is Banda’s party. Essentially, Banda authored her own downfall. She completed the feat of self-destruction when she ordered her portraits reprinted after being awarded a controversial honorary PhD by South Korean University of Jeoju so as to have  Dr, initials on her name. Banda didn’t know that such a move would present her as a self-seeker and controversial character apart from consuming highly needed money pointlessly especially for a cash-strapped country.
Apart from cashgate that saw over $ 30 million being embezzled under Banda’s watch whereby some of her consigliore were implicated, another reason for Banda’s downfall is nothing but her style of leadership based on settling of scores, witch-hunt and whitewash. For instance, when she took power, after Mutharika’s kitchen cabinet unsuccessfully tried to prevent her from taking over, Banda made sure that her nemeses were smoke out and subdued. She, too, saw to it that whatever she did aimed at winning the hearts and minds of Malawians for her personal gains even if such a move would harm the nation in the future. Banda tried to pay the Malawians back for their support when a cabal of Mutharika’s confidants tried to oust her. Nothing sacrilegious Banda committed like devaluing Malawi kwacha by almost 50%. If anything, among many reasons for the loss of Banda, deflation had deeper and wider economic, political and social blowback to Malawi and the general wellbeing of the people. It caused hardship and sufferings for them pointlessly something voters used to punish Banda mercilessly.
Nonetheless, Banda’s been accusing her archrival for rigging and hacking the Malawi Election Commission’s computers, the real reason basically is people’s pent-up anger thanks to the results of devaluation of Malawi currency. No country’s ever devalued her currency and looked good to her people. Devaluation, especially for African countries, has always been proposed by rich countries and the Breton Woods to avoid loss in their transactions between them and poor countries. The story was the same in Malawi. After Banda took over she easily allowed the devaluation of kwacha contrary to her predecessor who's at loggerheads with donors for refusing to do so.
It is sad. Banda didn't learn from her predecessor who in 2011 devalued Kwacha by 10% and caused increase of price in the prices of goods and services. If 10% caused such an upsurge, what did 50%  cause? It was next to a miracle for Banda to win the elections. African Outlook report had this to say about Malawi under Banda, “The country has continued to face macroeconomic pressures. These include inflation, exchange rate volatility and excessive government domestic borrowing.” This shows how deeper and wider the effects of devaluing Kwacha were.
Another fact that Banda needs to underscore is that it is her government that convoked and crewed the whole elections. How come the opposition rigged without supervising the said elections? Allegations of rigging from Banda might be genuine and worthwhile. This shows Banda’s own poor management. It is true there were some irregularities. Who’s behind such irregularities and who is to blame?
In sum, Banda needs to come to an understanding that her defeat in recent general elections in Malawi's authored by Banda herself. For the time she spent in office, it was harder for her to win given that after ascending to power she performed differently from what she's expected of.
Source: African Executive Magazine May 28, 2014.

Kikwete ananufaikaje na walioghushi?



JAPO vyombo vya habari vimekuwa mstari wa mbele kuwaumbua na kuwashupalia wazito walioghushi, serikali imekuwa mstari wa mbele kuwakingia kifua kwa sababu izijuazo.Baadhi ya wanaharakati wa haki za binadamu wamefikia hata kuandika vitabu kuwafichua wakubwa walioghushi vyeti vya kitaaluma. Mmoja wa wanaharakati aliyeweka uovu huu wa kiakili kwenye maandishi ni Keinerugaba Msemakweli ambaye ameishaandika vitabu viwili kuhusiana na kadhia hii akiwataja mawaziri William Lukuvu, Mary Nagu, Makongoro Mahanga na Mathayo Mathayo.
Wengine waliotajwa ni mawaziri wa zamani Emmanuel Nchimbi na Deodorus Kamala ambaye baada ya hapo aliteuliwa Balozi nchini Ubelgiji anakoendelea kufanya kazi licha ya kutuhumiwa kutenda kosa la jinai.
Pia wamo wabunge Victor Mwambalaswa, Samuel Chitalilo, Raphael Chegeni kutaja kwa uchache.
Mbunge wa Ole, Rajabu Mohamed Mbarouk (CUF) ndiye aliyemtoa paka kwenye fuko alipoliambia Bunge, “Suala la vyeti feki ambalo Baraza la Mitihani la Taifa ndilo lenye dhamana na jukumu la kuhakikisha halitokei katika taifa limeonekana kama suala la kawaida. Vyeti feki ni vingi kiasi kwamba linasababisha kuajiriwa kwa watendaji ambao ni feki na mawaziri mizigo.”
Japo alichosema mbunge si kipya, inafurahisha kuona kuwa hata wabunge japo si wote wameanza kukerwa na kadhia hii.
Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa (CHADEMA) aliyejipatia umaarufu kwa kuukabili uoza vilivyo alikuwa na haya ya kusema, “Hawa watu tuko nao humu ndani hawajakanusha, ndiyo maana tuna mawaziri mizigo kwa sababu wana vyeti feki. Serikali isiwe na kigugumizi hawa watu waonekane hapa hadharani.”
Msigwa licha ya kuwashukia walioghushi, anafahamika jinsi alivyomshukia hata anayewalinda, yaani Rais Jakaya Kikwete, ambaye kimsingi amewakingia kifua kwa kuendelea kuwa nao kwenye baraza lake la mawaziri licha ya kutuhumiwa kughushi.
Hivi karibuni Msigwa alikaririwa akiliambia Bunge kuwa wengi wa majangili ni marafiki wa Kikwete. Sasa ameongeza na majangili wengine wa kielimu.
Kama haitoshi, mbunge mwingine, Moses Machali (NCCR-Mageuzi) Kasulu, aliongeza moto kwenye sakata hili la wale wanaoitwa waheshimiwa kufanya mambo yasiyostahili heshima aliposema, “Kama inafika wakati watu wanataja ni mawaziri na wabunge wana vyeti feki halafu Bunge lako bado linakaa kimya tutegemee watu wataenda kupiga dili huko la vyeti feki.”
Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho kimsingi ndicho chenye watuhumiwa wengi hakikukaa kimya. Kada wake ambaye pia ni waziri wa wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa (Tamisemi), Hawa Ghasia aliamua kutetea uoza huu kwa sababu anazojua mwenye.
Alikaririwa akisema, “Baadhi yetu si ajabu mnatengeneza vyeti feki. Hata wabunge wapo. Na kambi ya CHADEMA mnaye mbunge ambaye ana cheti feki cha kidato cha nne.”
Ni aibu na hatari kiasi gani kwa waziri mkubwa kama Ghasia kutetea uoza kwa sababu tu unatendwa na wote, yaani chama tawala na wapinzani?
Kwa vile ufisadi na jinai vinaanza kuhalalishwa nchini, waziri hana haja ya kuona aibu. Maana kama kungekuwa na serikali inayowajibika vilivyo Ghasia sawa na wale anaowatetea walipaswa kuwa nje ya Bunge na baraza la mawaziri huku wakikabiliwa na kesi mahakamani.
Lakini hili haliwezekani, hasa ikizingatiwa kuwa Serikali ya Kikwete imejizoelea umaarufu kwa kuwalinda wahalifu kama hawa walioghushi vyeti ambao wamekuwa wakirejeshwa kwenye baraza la mawaziri na wengine kuzawadiwa uwaziri.
Kimsingi, maneno ya waheshimiwa wabunge ni ushahidi kuwa serikali inajua kila kitu haitaki kuwajibika. Je, serikali inanufaika vipi na jinai hii? Ushahidi kuwa serikali haishughulikii kadhia ya kughushi ni kuwepo kwa mawaziri na wabunge wanaojulikana wazi kughushi.
Pia kitendo cha polisi kubaini watu 212 walioghushi vyeti na kuwaachia kwa kuwafukuza badala ya kuwafikisha mahakamani ni ushahidi tosha kuwa wanaoghushi wako kitanda kimoja na serikali. Je, uzembe huu unalisaidia nini taifa?
Ukiachia mbali mawaziri waliotajwa na Msemakweli, wapo wengine ambao hakuwataja. Hawa ni Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum ambaye maelezo yake kwenye sifa za kuwa mbunge yana mushikeli.
Pia Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima, naye kama bosi wake, maelezo yake yanatia shaka sana.
Mfano, wasifu wa Mkuya unasomeka hivi: Alisomea Shahada ya Master of Finance kuanzia mwaka 2008 hadi 2010 bila kutaja chuo alikosomea.
Alisomea Business Study ngazi ya Advanced Diploma mwaka 1997 hadi 1999, kama ada hataji chuo alikosomea.
Unaendelea kudai kuwa Mkuya alisomea shahada nyingine ya biashara yaani Master mwaka 2000 hadi 2000 bila kutaja chuo. Si hilo tu. Wasifu unasema kuwa badala ya kupata shahada alipata cheti! Pia wasifu wa Mkuya hauonyeshi kama ana shahada yoyote ya kwanza.
Wasifu wa Malima nao ni mauzauza matupu kama bosi wake. Unasema, alimaliza kidato cha nne mwaka 1982. Baada ya hapo yaani mwaka 1983 alikwenda Cuba kusomea shahada ya pili bila kuwa na hata cheti cha High School au shahada ya kwanza. Vipi?
Hakuna nchi duniani inaweza kuruhusu mtu aliyemaliza kidato cha nne kusomea shahada ya pili hasa nchi yenyewe inapokuwa na utaratibu wa kusoma kidato cha tano na sita. Hata kwenye nchi ambapo mtu humaliza kidato cha nne na kuingia chuo hazina utaratibu wa kuruhusu wanaomaliza kidato cha nne kusomea shahada ya pili.
Je, Malima alitumia miujiza au mbinu gani kuvunja kanuni hii? Anatokea Tanzania nchi ambayo elimu yake iko ICU kama walivyosema waheshimiwa wabunge hivi karibuni.
Wakati umefika wa kumwambia Rais Kikwete aache kuigeuza nchi yetu chaka la uovu. Awawajibishe watu wake wanaotuhumiwa kughushi hata kama ni marafiki na washirika au watoto wa rafiki zake.
Kwanini rais amejiruhusu kuwa mhimili wa maovu kuanzia ujangili, kughushi, ufisadi, mihadarati, ujambazi na mengine mengi?
Chanzo: Tanzania Daima Mei 28, 2014.

Kijiwe chalaani umafia wa EWULA

BAADA ya kunyaka habari za kunyotoana roho kunakofanywa na wanaotuibia, Kijiwe kimekaa kutoa tamko.
Msomi Mkatatamaa ndiye anayelianzisha baada ya kuingia. “Waheshimiwa mnaona na kushuhudia yale ambayo nimekuwa nikionya mara kwa mara?”
Mpemba anadakia, “Wamaanishani; mbona ushaonya juu ya mengi msomi?”
“Yakhe naongelea haya madudu yaliyofichuliwa na CAG pamoja na mauaji ya jamaa wa EWULA alipotaka kuonyesha wenzake wanavyoula wakaamua kumnyotoa roho ili waendelee kuula.”
“Kumbe unaongelea huyu mugabo aliyenyotolewa roho na kudaiwa alijinyotoa? Hapo nimekupata mkuu.” Anachomekea Mijjinga ambaye kama kawa ameulamba ile mbaya.
Kanji anachomekea, “Veve pata somi vapi bona tusi yeye bwana?”
“Kanji usikonde hata nami nimempata aliyosema. Hivyo, achana na hiyo tusonge mbele na mada ya leo au vipi?”
Mipawa aliyekuwa anavuta sigara kali yake anaamua kuisigina na kula mic, “Kama anavyosema Msomi, tuachane na kupatana na mambo madogo kama hayo. Badala yake tujadili huu umafia unaoanza kushamiri ambapo watu wananyotoana roho ili kuficha madhambi yao.”
Mgosi Machungi anakatua mic, “Wakiuana wao kwa wao fit. Wamekuwa wakitinyonga kwa kutiibia kuna kosa gani wakitoana oho? Kinachogomba hapa ni kwamba unajengeka umafia. Kama wananyongana wao ukiwaona kuwastukia si wanakuua na ukoo wako.”
Msomi anakamata mic, “You are dead right Mgosi. Hapa kinachofanyika ni kujenga mazingira ya kuweza kuficha madhambi yao ima kwa kuwaua na kuwanyamazisha washirika zao au whistleblowers. Nadhani tusipobadili mfumo wa kijambazi tutaangamiza kaya.”
Kabla ya kuendelea Kapende anakatua mic, “Naungana nawe Msomi. Ulimsikia mheshimiwa Nunduu alivyosema kuwa wahalifu wachache wenye madaraka wanasamehe kodi za mabilioni kwa kuhongwa vijijumba?”
“Huyo naye mnafiki mkubwa. Kuonyesha lao lilivyo moja alishindwa kuwataja kwa kuogopa naye kutajwa kama ilivyokuwa kwenye sakata la waheshimiwa waishiwa kughushi vyeti huku mkuu akiangalia tu kana kwamba naye ameghushi.” Anajibu Mijjinga haraka.
Sofi Lion aka Kanungaemba anaamua kudema, “Nyinyi mlitaka amtaje nani wakati alikuwa akitoa matamshi ya kisiasa? Hata hawa mnaowasingizia kuuana mnawaonea hasa ikizingatiwa kuwa uchunguzi unaonyesha marehemu alijinyonga.”
“Go tell it to the birds Sofi. Siku zote nashangaa nini kimekuingilia kiasi cha kushabikia uovu hata kama unatendwa na chama chako. Kujinyonga gani iwapo wanasema walikuta dimbwi la damu na kwanini baada ya kuhojiwa na waheshimiwa? Hata kuku wanajua kilichofanyika. Hapa tatizo kama alivyosema Mgosi kuwa unajengeka umafia na janja ya kuwanyamazisha whistleblowers au kuwatisha washirika wao katika jinai hii. Mara hii mmesahau Aminia Chifwupa alivyokolimbwa kwa kuingilia dili za unga?”
“Mie hakuna waheshimiwa waliponiacha hoi kama kuambiana kuwa kwenye mjengo wamejazana walioghushi.” Mbwa Mwitu anadakia.
“Unashangaa nini wakati Pita Msigua alishasema kuwa majangili na walioghushi ni maswahiba wa rahisi na rahisi mwenyewe asikanushe? Unategemea nini au nini kifanyike iwapo walioghushi na vihiyo wote ni marafiki wa mkuu?” Anakatua mic Mipawa.
Mpemba naye anajikusuru na kula mic, “Huyu Nsigwa ankuna wallahi. Maana mojawapo wa hao vihiiyo ni Bill Lukuvii toka huko huko. Waloghushi kweli wana dhiki kiroho. Tulivowaghasi lau wangejibu.”
“Kaka wajibu nini wakati ni ukweli wengi ni madaktari feki? Ngoja niwataje tena ili msiwasahau. Yupo Merry Naguu, Makorongo Muhanga, Emmy Nchimbii, Diddie Massaburii, Vicky Mwambalashwa, Matthew Mataayo, Dorolos Kamalaa, Raph Chengeni na wengine ambao nitawataja wiki ijayo.” Anazoza Msomi.
Kabla ya kuendelea Sofi anakatua mic, “Unao ushahidi wa tuhuma hizi kwa waheshimiwa?” Msomi hajibu. Badala yake anampa kitabu cha Keineruga Msemakweli.
Waswazi wasivyopenda kusoma, Sofi anatoa mimacho kama gabacholi aliyekamatwa na bwimbwi.
Kuona hivyo Kanji ananyakua mic, “Veve zani hii Semakweli semakweli au politics? Mimi ona iko siasa ya maji taka.”
“Kanji unaambiwa kilichoandika cha milele halafu unatia shaka? Kweli hizi ni siasa za maji taka ambapo sirikali inaundwa na wahalifu tena vihiyo. Hukuona yule kihiyo mwingine Hawa wana Gasia alivyosiama kuwatetea majambazi wenzake akisema kuwa na upinzani nao unao vihiyo walioghushi?” Anachomekea mzee Maneno.
Mijjinga anazidi kukandia, “Nilitamani waanze kutajana ili tuongeze orodha ya walioghushi ambapo watu kama Jan Makambaa, Saadaa Mkuyati yule wa Njuluku na naibu wake Adamu Kagoma Milima waongezewe kwa kujidai wana masters wakati hata bachelor hawana. Bahati nzuri wote nawafahamu ndani na nje.”
“Mijjinga unaua. Yaani unawafahamu ndani na nje?” Anatania Mbwa Mwitu.
“Hata mie nanfahamu huyu Mkuyati. Hana hiyo master wala bachelor. Sijui hata hiyo diploma alo nayo kama ya ukweli. Si hawa twawaita maamum kumaanisha vihiyo kama huku msemavo.” Anazidi kukandia Mpemba.
Baada ya kugundua kuwa mada imehama toka EWULA na kwenda kwenye kughushi, Msomi anaamua kuirejesha. “Msemayo ni kweli. Baada ya jamaa kuona kughushi na kutuibia kiasi cha kuwa mizigo kama alivyosema shujaa Msigua, wameamua kuanza kunyotoa roho yeyote anayefichua dhambi zao hata awe mwenzao. Maskini kijana wa watu amepotea bure.”
Mipawa hakubaliana na Msomi. “Hajapotea bure hasa ikizingatiwa kuwa alikuwa akila nao. Tusiporejesha sheria za maadili na kutaka kila mtu kutaja mali zake tutaangamia kama kaya.”
Kapende anadandia, “Hiyo sahau. Unaona mkuu anamaliza ngwe mbili na hataji unadhani kuna atakayetaja? Wengine wakitaja tutakufa kwa shinikizo la moyo kwa walivyo matajiri tena wana wa maskini wa kunuka.”
Mchunguliaji anakamua mic, “Dokta Kapende usemacho ni kweli. Hukumsikia yule Nshomile Jemus Rugemaliiira kuwadi wa kawaida anasema eti bilioni 120 ni vijisenti vya ugoro? Mijizi mingine bwana. Kama ni vijisenti hiyo bia ya Mabi-bo alikojificha anauza ya nini kama ni tajiri? Hawa walipaswa kunyongwa.”
“Hoo Tate nane uzanitonesha! Kwei hawa na wae waiogushi wanapaswa kunyongwa. Siku akija mkuu mwenye akiii na udhu wataumia wengi kama si kuuawa.” Mgosi anazoza.
Kijiwe kikiwe kinanoga si likapita shangingi la mkuu wa EWULA. Tulilikimbiza kwa hasira ili tumkamate tumnyotoe roho halafu tuseme amejinyonga mwenyewe lakini wapi!
Chanzo: Tanzania Daima Mei 28, 2014.

Sunday 25 May 2014

Complicity and impunity will deck the hunk

           The report by Controller and Audit General (CAG) whose findings cause heart attacks to boozers left me morally injured.  Though CAG’s job was done and dusted, it was supposed to be the beginning for boozers’ task to question and possibly punish the villains. I sadly this didn't happen. Since the said report came out I feel like dying with anger and desire to drink the blood of a criminal. Since then, of course, things have calmed down as if nothing impious did happen. Boozers have already forgotten. They’re back into their hand-to-mouth struggles as usual while the eaters are eating even more. I’d state from the outset. When I look at the future of our hunk, I see doom and gloom thanks to economic and political morass. I’m worried God knows. How’d I stop worrying while everything is eaten? It is but an eating frenzy. As one Brit envoi to one East African hunk put it: Like houseflies, they eat vomit and poop in the container they eat from.  What a mess are we in!
Folks, I mean it. When I say dudes eat I mean it seriously. They eat and suck blood in a broad daylight. To make it worse, they've invited even their vitegemezi to eat with them. Now our hunk’s just like their private estate to abuse as pleased. Lucky dogs, those who’d take on them are completely dead mentally and morally.  I evidenced it just the same way CAG did. It is as if we’re becoming the society of termites that can gnaw and gnash everything put in front of them! No, we’re the society of egoistic, ruthless and blind monsters. Sadly, there’s no sane person one can tell to take on this calamity. Big and small, white, black and green eaters are just eating. What makes things worse and lugubrious is the truth that we’ve become man-eat-man humanity. Our future as a hunk’s drab and lurid due to impunity and complicity. Since we turned rapaciousness to be our credo as a hunk, surely our future’s nothing to be proud of or optimistic about shall we not change. Boozers hide nothing. They say it categorically and loudly that we've become the hunk of crooks, androids and fiends except themselves.
Who’d believe that exhibits would be stolen from cop’s stations in the first place? It did happen and it has been happening for years. CAG unearthed such stinking criminality in the ranks. We’re told that in Kilwa, cops mugged their own station and got away with tusks they intercepted. Again, in such crime race which criminal deserves heavy punishment between the one we pay and the poacher? While others are using gun to poach our animals others are using our offices. So we need to improve the dictionary with regard to the meaning of poaching. We used to believe that poaching is the act of entering restricted areas where animals live and kill them and take their products. Now, we’d add that poaching can be done out of the games and national parks. It can be committed in cop stations.
Another crime CAG revealed is hiking. The champions in this rolly making aka making a killing were the office of the biggie himself and many ministries whose officers hiked their air tickets they purchase in their globetrotting missions to inspect their offshore accounts on the expense of those they rob wantonly. What do you call the act of hiking a ticket at sixteen folds? If nobody can see this thuggery thereby says we’re attacking the high and the mighty pointless, such a person must be either sick or an abettor to this megalomania in the hunk. If there those among us who still think that things are spiffy, they need to have their heads checked. Indeed, if anything, this is the testament of how some of us can miscast things and take things easily for our peril. Many people are asking: Is this Better Life for all our corporate plants looking for deals promised or just better life for those wonks who take us for a ride?
Turns out that those we wrongly trusted still take us of goons and silly guys they can abuse as pleased.
When the report came out one boozer who like to call himself a patrician summarized it as thus, “Bongolalaland is the hunk of powerful criminals known as watuwala and weak zombies known as watuwaliwa. It is only in Bongo where this psychosis can be committed and tolerated. Take it from me. Nobody will face the music. Instead, wait for the coming year to discover that more dosh has been stolen.”
Another chipped in: If they rob us why don’t we rob them back by nationalizing their loots? Another sipper pared in asking, “Who’ll tell the king that he’s naked if all are in the same bed doing the same monkey biz? Sadly though, when you see a fool axing the branch is on, cry and holler.” Knowing the league of rulers we've, I just told him to his face: Guy, this is not Mzee Mchonga’s time. Unatawaliwa na vibaka na mibaka.
Source: ThisDay May 26, 20145.

This is purely institutionalized racism

 Naturally, racist regimes discriminate against people who don’t belong to them especially those regarded as aliens or intruders. We evidenced it under Nazi Germany whereby Adolf Hitler butchered Jews simply because they’re not Germans. Under Apartheid, Boers discriminated Africans for what they called self-preservation. Again, racism is a crime. However, those above mentioned stinking racists had a justification.
Today we’re delving into what seems to be institutionalized racism in our own doorstep. The difference is that this racism is done at the peril of our people. Our system either purposely or otherwise does discriminate indigenous as it favours foreigners. This, for long, has been the case save our rulers have tried to get away with it making boozers believe that everything is spiffy while it isn't.
Our take on this long-standing racism’s triggered by what happened in Arusha recently where remandees decided to strip naked protesting the release of two folks, Dharam Patel (26) and Nivan Patel (20) charged with drug-related crimes. It is sacrilegious to note that such crime’s committed by crime stoppers.
To prove our point, apart from using what transpired in Arusha recently, we’ll adduce more examples to show how racism’s been covertly and overtly institutionalized. Refer to tax holidays many foreign investors enjoy in a begging hunk.  The minister responsible for revenues has more discretion than he or she needs as if this hunk’s his or her mother’s. I've nary heard anywhere the minister of dosh offering any tax reprieve to hoi polloi. What’s going on? Does it mean that these overprotected investors are in bed with our biggies so as to be allowed to exploit us and get away with it? Those thinking I’m fabricating this should refer to the now-famous tendency whereby investors change the names of their biz after every five years in order to get more tax holidays. You can refer to oft-name changers such as Sheraton, Movenpick, Kempinski and many more. 
As this goes on, our paupers are overtaxed so as to feel the pinch as it recently occurred in Kibaigwa where coolies decided to square it with their Member of Parliament, Job Nduguy, whom we’re told narrowly survived a beating from them. So too, you can refer to how our Matching guys aka wamachinga are brutalized by City militia in Dar and other cities and town. While this is going on particularly in Dar, Indian dukawallahs enjoy maximum protection. They pose in their National Housing houses and laugh at the exercise of humiliating our jobless youths. Why harassing Chingas while we’re the ones who created their unnecessary predicaments? Chingas’ situation's doom and gloom so to speak. What adds up to Chingas’ pangs and twangs is the mantra of saying that our govt’s there to deliver Better Life for All. Who’s this all if our Matching guys are always crucified as if they’re aliens in their hunk? Isn't this divide and rule or Lugardism as it used to be known at colonial times?
I, for one, see no freedom or the state of being free for boozers who can be maltreated in their own hunk while aliens are protected. Jobless people are not free especially when they try to make ends meet and meet with mgambos and their beatings and robberies. This can’t be the life of a guy who’s been independent for over five decades. While this goes on, Idd Simba, former Trade Minister, tells us that the economy of the hunk is in the hands of just ten Indian businessmen and we treat this just as a normal thing! Are we okay really? I’m trying to imagine. If such’s the situation in India, what’d happen? I’m asking this not out of ignorance. Nay, when I look at how Africans known as Jarawa are maltreated in Indian Andaman Island where they’re used for tourism just like beasts, I feel that such revelations would cause a blood spill. Yes, let’s face it. Our systems are discriminating against boozers. Refer to what’s been going on for decades vis a vis National Housing houses. In areas like Kariakoo and Posta, almost all occupants of these houses are from Asia. Why? Isn't this racism?
There are yet more examples. Most of humongous dealings in Dar are run by the same people not to mention the same people being behind many mega deals and corruption involving our top dogs in the upper echelons of power. Refer to Vithlani, a criminal behind the hike of fake and defective radar and presidential jet. Refer to Chavda’s scam of billions of shillings and the just recent scandal of illegally exporting over 130 live animals via KIA by Kamran Ahmed whom we’re told was granted bail and jumped it. Was he alone? Nope. One Ladislausie Komba, former permanent secretary in the ministry responsible was mentioned to be in cohorts with Kamran. Do you know what happened? Mr. President appointed him ambassador. And that was the end of the chess.
The space doesn't allow a missive. In sum, I sense that we’re institutionalizing racism against our own brethren as we favour Martians.
Source: The Guardian May 25, 2014.

Saturday 24 May 2014

Mnapojaza mabwege bungeni mtegemee nini?

Hebu msomaji chukua sekunde thelathini umsikie bwege mbunge ambaye anakiri kuwa yeye ni bwege tena bwege kweli kweli. Je bunge limejaa mabwege kiasi gani kuanzia wale wanaotumia mabilioni kwenye sherehe za muungano huku wakiomba kujazia bajeti yao ya mwaka? Ama kweli tunaongozwa na mabwege kama huyu bwege!

Sera ya Mlevi sasa ni kububujikwa michozi

        Baada ya kuinyaka kuwa Katibu mkuu wa Chama Twawala Abduli Kinamna alibubujikwa michozi kule kwa akina Mwanawetu, Mwanawima, Mzindakaya na wengine wengine wengi, akiwalilia wakulima wanaonyonywa, mlevi amependa staili hii ya kukwepa kuwajibika kwa kumwaga michozi ya mamba.  Ukisikia usanii uliotukuka ndiyo huu.  Jamaa anafaa kupewa nishani ya kuweka walevi sawa. Haiwezekani mtu mwenye mamlaka ajilizelize tena akishindwa kuwawajibisha watu wadogo wa chini yake kusiwe na namna. Hata hivyo, ni rahisi mtu na staili ya namna hii kustukia. Cheats never prosper walisema waswahili.
Hawa jamaa kama walioingizwa mkenge kwa machozi ya mamba kama si kuendekeza huruma si wangemtwanga angalau juju. Sijui nini mantiki ya kushindwa kusumbawanga lau akashika adabu mjivuni huyu? Nisingekuwa bize, nilitamani niende kule kulikoungua jembe ukabaki mpini nimzodoe Kinamna kuwa uongozi si uongo na kulialia bali kutatua matatizo ya walevi. Hivyo, walevi wasimwamini bali wamzomee hata kumtia adabu kama aliyotia jamaa yangu Njaa Kaya kule kipindi fulani kule kwa akina Twambombo Tununu waliompenda hadi wakamrushia mawe ya upendo.
Kwa vile Mlevi amekuwa akiwaibia na kuwatapeli walevi hasa wanapompa ofa au kumkopesha asirudishe njuluku, basi ataanza kuangua kilio kila akikutana na anayemdai. Badala ya kumlipa fweza unamlipa fedheha ya michozi kama Kinamna. Badala ya kutatua tatizo ambao kwa mlevi ni deni au kutoa huduma kwa Kinamna na sirikali ya rafiki yake, unamwaga chozi na wajinga na walevi wanakuamini kuwa unawamaindi wakati unawa-fool. You better fool them before they fool you for if they fool you without fooling them you’ll end up in trouble like Muamar Gaddafi they fooled that they used to love while they actually loved to hate him up till they butchered him like Kibaka the way they wish they should treat you the one they love to hate and fool that they love. Kwa unyambilisi wangu hili sitafsiri otherwise mniahidi kuwa mtaacha ukondoo na unjiwa na ukijiko na uupawa.
Kijicho huchota chakula lakini huwa hakili sawa na upawa. Kondoo hujifanya mtiifu hata kwa mchinjaji wake huku njiwa akijifanya hayamhusu wakati yanamhusu. Hata hivyo, hivi ni vitu na hayawani si walevi wanadamu kama nyinyi. Ni matusi ya nguoni mwanadamu kutenzwa kama kitu au hayawani.
Usishangae kuandika sentensi ndefu namna hii. Nina uwezo wa kuandika sentensi moja ikajaza ukurasa mzima. Mie sijagushi ati. Nimesoma tena ughaibuni mnakozimikia kuanzia shahada ya kwanza hadi ya mwisho. Hayo tuyaache. Sitaki nionekane najidai au kujipigia debe kama akina Kinamna na Nipe Mapepe Nnauyee Ninaye walioishiwa hadi wanaanza kukamatana uchawi kwa kuita wenzao mizigo. Japo ni kweli wale walioitwa mizigo ni mizigo kweli kweli hata waliowaita mizigo nao ni mizigo ile mbaya au siyo. Hebu tuachane na akina Kinanae na mapepe yao yasiyo na maana.
“Heri kufa nimesimama kuliko kuishi nimepiga magoti,” alivyosema Field Marshal Dedan Kimathi wa Kenya ambaye tulizoea kupata kanywaji pamoja kabla ya wenzake hawajamsaliti na kumnyotoa roho halafu wakamwaga michozi kama Kinamna ilhali ni michozi ya mamba aliyeshiba “anayemlilia” aliyemuua na kumgeuza kitoweo.
Si juzi nilituhumiwa kuwa nauza bwimbwi na pembe za ndovu kana kwamba mimi ni ndata. Kama Kinamna, baada ya kutuhumiwa badala ya kutoa maelezo, nilimwaga michozi hadi ndata wakanichangia uchache kwa kunionea huruma wasijue tuhuma zenyewe ni kweli. Hata jamaa yangu alipotuhumiwa kusafirisha vipusa, si alimwaga chozi hadi Njaa Kaya akaingia mkenge na kumpa ulaji anaoutumia kupiga fweza kwa njia ya kumwaga michozi. Michozi, kama mipasho na mitusi kule Idodomya inalipa.
Kwa vile michozi inalipa,ningeshauri hata wale mafwisadi papa waliotuhumiwa hivi karibuni kujichotea bilioni 200 kwenye akaunti ya Scrow iliyogeuka screw wamwage michozi walevi watawaonea huruma waendelea kutesa na kupiga njuluku nyingine kama hawana akili nzuri. Hata yule karasinga gabacholi anayejifanya kuinunua IpTl wakati ni tapeli wa kawaida akistukiwa anaweza kumwaga chozi na mambo yakaisha au vipi?
Ndugu zangu akina Sossie Muongo, Benny Ndururu, Elyakim Maswi, Saada Mkuyati na Freddie We-rema mpo? Yaani mmeamua kufuata nyayo za akina Basiri Mlamba na David Balalii kwa kuchonga EPA nyingine siyo? Huwa najiuliza sipati jibu. Sijui kamana walevi wote na wadaganyika huwa wanajiuliza swali hili. Kwani njuluku huwa zinaibwa karibu na kuelekea uchaguzi wa uchafuzi wa uchakachuaji kama hakuna mkono wa nambari wahedi na madingi wake majizi? It is too boring to evidence such megalomia every year. Nawashauri mkipata jukwaa la kujieleza mmwage michozi kama Kinamna ili wale mnaowaibia wawaonee huruma na kudhani hamna hatia. Mara hii mmesahau akina Yuda Iskarioti walivyomwaga chozi wakati ndiyo hao waliomsaliti mwana wa Adamu siyo? Mwanikumbusha mlevi mmoja aliyefumwa na bi wa mwenyewe tena amekumbatia akamwaga michozi na kudai walikuwa wakionyesha mshikamano!
Najua wengi wasiojua faida za kanywaji na bangi huwa wanapenda kunikosoa na kuniona kama hamnazo. Nawashaurini, tena kwa upole, msihangaike na mimi nisemaye bali yale nisemayo. Mie ni mtume, sawa na yule Paulo aliyekuwa akiuwa wanafunzi wa Yesu. Alipoona ngoma inakuwa nzito aliamua kujisalimisha. Fikiria. Kama waliweza kumwamini muuaji, kwanini wasiniamini mlevi na mvuta ganja ambaye wala simkwazi mtu zaidi ya kumpa vipande ili angalau aamke na kudai kilicho chake mapema kabla akina Chukua Chao Mapema hawajamaliza kila kitu? Hawa jamaa wanaweza kumaliza kila kitu sitishii kama akina Joni Kombakombo na Bill Lukuvie au Njaa Kaya Kiquette. Jamaa wana roho mbaya na wanaweza kufanya kweli.
Salamu maalumu kwa walevi na wavuta bangi wote wanaofia ukweli bila woga. Heri kufa mmesimama kuliko kuishi mmepiga magoti au siyo?
Chanzo:  Nipashe Mei 24, 2014.

Zuma: Mkombozi au mroho tu wa kawaida


Hapa chini ni makazi ya kifahari ya rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ambaye ameapishwa leo kwa kipindi kingine cha pili na cha mwisho kama rais. Ameahidi mengi kubwa ni kuboresha maisha ya wananchi wa Afrika Kusini. Kujua kama kweli Zuma anamaanisha anachosema, tumeweka hiyo picha ya makazi yake ya kifahari yaliyozamisha mamilioni ya rand huku jirani yake kukiwa na  kibanda cha wale anaosema ataboresha maisha yao. Je kama alishindwa kufanya hivyo miaka mitano iliyopita ataweza kwenye kipindi hiki cha lala salama?Je ni yale yale ya Maisha Bora kwa Wote wote waliolengwa wakiwa ni familia na marafiki na waramba viatu wa rais? Hakika yetu macho kungoja kuona Zuma atakavyowakomboa au kuendelea kuwanyonya na kuwazamisha wananchi.

Thursday 22 May 2014

Ujenzi kweli au usanii

Hapa anaonekana akila na mafisadi

Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahaman Kinana ni mtu asiyeishiwa vituko. Kwa nje ni mtu anayejionyesha kama mpenda maendeleo hasa ya watu maskini. Kwa ndani ni mtu wa kuogopwa kama ukoma. Ni Kinana huyu huyu aliyetuhumiwa kutumia kampuni yake kusafirisha nyara za taifa nje anayejifanya kuwajali hawa anaotuhumiwa kuwahujumu. Wapo wanaosema kuwa anautupia jicho urais japo wanaomjua wanaona kama urais umeishiwa maana. 
Hapa anajionyesha kama mtu wa kawaida ila akishaukwaa humuoni
Rais wa Tanzania anapaswa  kutumiza sharti moja kuu kati ya mengi. Awe amezaliwa Tanzania na mtanzania ambaye wazazi wake walizaliwa Tanzania. Wenye kujua historia ya Kinana watupe ili tutafute jinsi ya kumdurusu kuona kama ana sifa za kuwa rais ingawa hili la kujihusisha na ujangili linamtoa nje ya ulingo. Siku hizi ametokea kuwa mtu wa kuikosoa serikali ya Kikwete hasa baadhi ya mawaziri na kujionyesha kama mpenda kusaidia watu wa vijiji na mtu wa watu wakati si kweli. Je anachofanya kwanini anakifanya leo na siyo miaka mingi iliyopita?