The Chant of Savant

Thursday 31 January 2008

CCM,kufilisika,kufa mafisadi na saa ya Ukombozi.

Kwanza nilicheka kwa huzuni; niliposoma habari kuwa CCM imepora hoja ya ufisadi wa BoT iliyoibuliwa na waandishi wa habari kwa kuipenyeza kwa kambi ya upinzani. Nilicheka na kuhuzuni sana kutokana na ukweli kuwa ni upuuzi, urushi na kutapatapa kwa CCM kutoa madai ya kitoto kama haya bila aibu.

Nilicheka zaidi niliposoma kuwa CCM inasema mafisadi wafilisiwe! Nilicheka kwa sababu tuendako CCM haiwezi kukwepa kuhusika na ufisadi uliotikisa taifa letu. Kwa mujibu wa taarifa zilizomkariri John Chiligati, Katibu wa Uenezi wa CCM, kamati kuu ya chama eti imetaka wote watakaobainika kuwa walipora pesa BoT wafilisiwe! Kwanza ifahamike kuwa CCM inajua kuwa watakaopatikana ni mbuzi wa shughuli na vidagaa wachache; watakaobeba msalaba wa vigogo wa CCM na serikali. Mbona vyombo vya habari vimeishafichua njama hii? Rejea lead story ya gazeti la Raia Mwema la Januari 31, kuwa, mashahidi watakaojitokeza mbele ya tume ya rais ya kuchunguza kadhia hii wasiwataje vigogo wa chama na serikali.

Hivi CCM inadhani watanzania wana mafyongo na upogo kiasi cha kutoona zengwe linalotembezwa? Nani hajui kuwa kashfa hii inashughulikiwa kinamna namna kwa kutafuta ku-buy time na kuwahadaa wananchi? Kwanini serikali ya CCM imeshindwa hata kuiomba rasmi Marekani kumrejesha nchini Ballali? Rejea taarifa ya balozi, Mark Green, wa Marekani kwa wanahabari siku chache kabla ya CCM kuja na usanii huu? Mbona rais anapata kigugumizi kuomba Ballali arejeshwe haraka? Badala yake, serikali imepata kisingizio kwa kupigia upatu ujio wa rais George Bush wa Marekani utadhani ni big deal!

Nina sababu mahsusi kwa hili.

Kwanza, CCM ndiyo inayounda serikali zote tangu uhuru. Ukiondoa serikali ya awamu ya kwanza na ya kidogo, awamu ya pili, serikali zilizobaki ni uoza mtupu. Je hapa CCM itakwepaje kuwajibika kwa uchafu wa serikali na watendaji wake? Anayebishia hili ajikumbushe kashfa zinazomkabili rais mstaafu, Benjamin Mkapa, mkewe, watoto wake na marafiki zake huku mwenyekiti wa CCM hii hii akimkingia kifua kuwa hawezi kuchunguzwa. Tulishasema kinga ya urais inatumiwa vibaya kulinda wezi. Tulishahoji kutochukuliwa hatua kwa Anna Mkapa, Nicholaus Mkapa na Daniel Yona ambao ni washiriki wakuu wa Mkapa. Je nao walikuwa marais nyuma ya pazia?

Pili, CCM -na serikali zake- ndiyo iliyoasisi na kuneemesha mfumo mfu wa watawala kujiibia watakavyo. Hapa napo CCM haiwezi kukwepa lawama na kuwajibika. Hebu rejea kuendelea kufichwa kwa kigogo wa serikali anayejulikana kuwa nyuma ya kashfa ya Richmond. Rejea kuendelea kulipwa pesa kwa kampuni kama IPTL, Richmond na nyingine nyingi hewa kama Deep Green.

Tatu, CCM kwa kutumia wingi wa wabunge wake bungeni ilidiriki hata kuzuia bunge kujadili ufisadi wa BoT hadi upinzani uliposimama kidete na kuiibua upya kupitia majukwaani. Kwanini CCM inasahau iliyosema jana? Mbona CCM na serikali, mwanzoni zilizisema: madai ya ufisadi yaliyokuwa yakitolewa na wapinzani ulikuwa umbea na uongo mtupu? Yaani CCM ilivyotembezwa zengwe hadi mhusika mkuu, mbuzi wa kafara Dk. Daudi Ballali akawaita waandishi wa habari na kuwaambia, "Sina wasi wasi na morale ya kazi iko juu."!? CCM mara imeishasahau yote haya!!!

Nne, CCM ndicho chama tajiri barani Afrika; kikimilki mali nyingi za wizi kama viwanja vya wazi vya umma vitumikavyo kama maegesho ya magari ukiachia mbali viwanja vya michezo kama vile CCM- Kirumba.

CCM haishii hapa. inamiliki miradi iliyojengwa kwa fedha ya umma kama makao makuu Dodoma, Chuo cha CCM Kivukoni na mali nyingine nyingi.

Tano, CCM ndiyo inayotajwa sana kunufaika na chumo la wizi la Benki kuu lililotumbukizwa kwenye uchaguzi aghali kwa viwango vyote. Ukitaka kujua namaanisha nini, hebu jaribu kujumlisha gharama za kununulia Khanga, vibandiko, T-shirts, mabango, matangazo, nauli za kuzunguka nchi nzima, pesa ya malazi mahotelini, per diems zilizolipwa kwa wajumbe na wapiga kampeni wa CCM nchi nzima, magari na vikorombwezo vingine halafu ulinganishe na pato halali la CCM. Utapata pesa kubwa kiasi cha kutisha. Hii maana yake ni kwamba ufisadi unaoongelewa ni mkubwa kuliko huu kiduchu tunaopewa.

Hapo bado hatujaangalia mali za vigogo wa serikali wanaoishi kama wafalme kwenye bahari ya umaskini wa kutupwa. Hapa bado hujagusia ile pesa inayotoroshewa nje na wageni wa CCM na serikali zake yaani akina Chavda, Patel na makanyabwoya wengine.

CCM kwa kutoa madai ya kipuuzi kama haya inaonekana bado ina mawazo kuwa watanzania ni wajinga wa miaka ya 60 ambapo wangeweza kukaa na kubishania milioni moja ina sufuri ngapi! Imesahau: watanzania sasa ni mabingwa wa kutumia teknolojia ya kisasa ya mawasiliano ya internet kiasi cha kuwa taifa la kwanza duniani kuutumia mtandao kufichua kashfa kubwa ya kifedha kuliko zote nchini!

Sasa tuangalie taarifa kuwa kuna baadhi ya wana CCM safi wenye uchungu na nchi yao wanaotaka mafisadi wote watajwe bila kuangalia sura zao. Hawa wakishikiria msimamo huu wanaweza kurejesha chama chao kwa wanachama toka mikononi mwa wezi na wasaka ngawira. Kabla ya kifo chake, mwanzilishi wa CCM, mwalimu Julius Nyerere, aliwahi kutishia hata kujitoa kwenye chama alichosema siyo mama yake. Hii ni baada ya chama kuporwa na wachuuzi wa roho na miili ya watu walioua azimio la Arusha kwa kuanzisha la Zanzibar.

Hadi Nyerere anafariki, alikuwa mtu aliyekata tamaa na kuchukia sana. Rejea maneno yake, "Nawaombea watanzania wangu’" Hii licha ya kuwa laana ni kauli ya kukata tamaa. Tunamshukuru Mungu: maneno ya gwiji hili yamedhihirika hata kabla ya kuoza. Rejea aibu na kihoro vinavyompata rais mstaafu Mkapa ambaye licha ya kumvua nguo Nyerere aliyemuwezesha kuwa rais asijue alikuwa bomu, ameifuja nchi yake na misingi yote aliyoiweka akaipigania na kuifia.

Na bado. Mkapa anaweza kukwepa kifungo leo kwa sababu Kikwete -kwa sababu anazojua mwenyewe- amemkingia kifua. Lakini ajue nchi hii siyo ya Kikwete wala Kikwete hataishi milele akiwa rais wa nchi. Na isitoshe, yeye akiponyoka hawa wengine arobaini yao itafika.

Huenda utabiri wa Nyerere kuwa CCM itakuja kufa --kama haitaacha kuwakumbatia matajiri kwa kuwatelekeza wanyonge-- ndiyo inatimia. Nani haoni wafanyabiashara wachoyo waliojipenyeza kwenye chama na kupata vyeo wanavyoipeleka CCM kuzimu?

Ukitaka kujua hatari hii, chunguza ni wabunge wangapi wako bungeni kulinda himaya zao za biashara kwa mgongo wa CCM --ambayo kama fala-- nayo imewapokea na kuwapa madaraka makubwa isijue; lao ni matumbo yao; na siyo taifa; kama ilivyokuwa agenda ya kuanzishwa kwa CCM.

Hivyo, wana-CCM wenye uchungu na nchi hii wanaweza kushirikiana na upinzani na vyombo vya habari kuwafichua manyang’au waliomo chamani walioshiriki kwenye uchafu wa BoT ili umma uwape adhabu wanayostahili. Kama mwalimu Nyerere, wasichelee lolote. Kwani CCM siyo mama zao wala Mungu wao.

Kuna haja ya kuanza kuchimba kaburi la CCM. Maana kaka na dada zake iliozaliwa nao wote wameishakufa kuanzia Ghana, Kenya, Zambia, Malawi, Senegal, Uganda, Nigeria na kwingineko. Umefika wakati wa ama CCM kuuawa na mafisadi au wana-CCM wazalendo na wasafi kuinyakua CCM toka kwenye pango la wezi wanaoichuuza yenyewe na watu wake.

Tuhitimishe. Kama CCM inataka mafisadi wafilisiwe, wa kwanza kama haki itatendeka itakuwa CCM yenyewe.

Nihitimishe na kituko. Rais Jakaya Kikwete amekaririwa akiwataka mawaziri na wabunge ama kuchagua biashara au siasa ili kuondoa mgongano wa kimaslahi. Nina maswali madogo. Kwanini angoje wawe matajiri ndipo aseme? Mbona anakatalia kutaja mali zake na wenzake?Je hii nayo ni kamba nyingine? Je waliokwishaneemeka na jinai hii wafanywe nini na ni wangapi? Je umefika wakati wa kuinusuru CCM toka kwa wafanyabiashara? Mwisho atatoa lini ombi kwa Marekani kumrudisha Ballali? Na je ataanza lini kuwashughulikia mafisadi, mabaroni wa unga, wala rushwa bila kusahau nyumba zetu?

Mungu ibariki Tanzania.
Iepushe na mafisadi,
Iondoe kwenye mizengwe na usanii.

Wednesday 30 January 2008

HIV/AIDS: The Africa – Canada Experience.

HIV/AIDS exists in Canada save that it is not much publicized as in Africa. Despite being a danger, how an individual protects him or herself against HIV, remains personal. Nobody makes noise to anybody about it. Media ads on HIV/AIDS and its dangers are not as traumatizing, cultural destructive or monotonous as in Africa. This is because Canada has no donors to attract by blowing the issue out of proportion.



In many African countries, sadly, pornographic adverts are aired without underscoring the truth and danger that this may cause. They end up being catalysts for promiscuous and related acts, turning our kids and youth into experimental guinea pigs.



Many NGOs and governments know this danger too well. But due to their greed for donor funds, they ignore the truth. Figures are cooked and inflated. In Tanzania for example, nobody knows the exact number of HIV/AIDs victims. Every NGO has its own figures and statistics based on creating fear and attracting donors!



Many medical trials are carelessly conducted on Africans! Authorities condone this under the pretext of fighting HIV/AIDS! How do we trust the same guys behind the creation of the malady? We give them our secrets and statistics so as to be vulnerable! If anything, this lust for money has become another danger which is bigger than HIV/AIDS itself.



I have neither seen condoms being advertised here nor adverts which cross the line being pumped to the media as it is back home. Do we know that pumping dirty adverts cause many miseries to our young ones that we condemn for cultural erosion?



Much money is spent on these adverts and money-making seminars and conferences whilst the victims are dying without any help. Hither is where I concur with those agitating for stamping out poverty and corruption, the vices enhanced by donors who support and give money to corrupt regimes.



In Tanzania, TACAIDS, the commission responsible for HIV/AIDS-like the government of the day alleged to squander money on expensive oil guzzlers whilst the victims are dying of lack of simple drugs for elongating life! Super scale salaries are paid to do nothing but make money for TACAIDS officials!



In Canada, due to advanced and reliable medical facilities-cum services, you can not feel the presence of HIV/AIDS. This does not imply that the scourge is absent. It exists, but the figures are not known. This is because under Canadian Law, private information is protected.



One incident in Montreal late last year unearthed a very gloomy reality. It was discovered that som people in the country do not know HIV/AIDS! This happened when one doctor discovered that some secondary school students were infected with AIDS. But to his shock, they did not know what AIDS was! These findings forced the doctor to alert the people of such reality. And the media was urged to put more efforts to educate the general public. The doctor again found that at least three cases are discovered at his hospital everyday.



HIV/AIDS is a menace. But like in Canada, Africa needs to address it in a transparent, decent and humanistic way in lieu of commercial rust aimed at vending the souls and bodies of the victims as it has always been the case of governments of Africa when it comes to attend their citizenry.



The fight against HIV/AIDS in Africa has become a means of minting money. Take a leaf guys else we shall perish unnecessarily.

Source: The African Executive Magazine January 30, 2008.


By Nkwazi Mhango
Mhango is a Tanzanian living in Canada. He is a Journalist, Poet, Teacher, Human Rights activist and member of the Writers' Alliance of New Foundland and Labrador (WANL)

Kwanini kila ufisadi wa kaya hii yumo Gabacholi?

NIMEJILAWA leo. Nautafakari unafiki wa wakubwa. Nimechukizwa na baadhi ya wachumia tumbo waliojaa kwenye majoho wakivichafua vitabu na nyumba za Mungu. Wapo wengi. Wanaojifanya wanakipenda kijiwe, ilhali ni mbweha wa kawaida.

Yupo mbweha mmoja, aliyedai tumsaidie mkuu wa kaya kupambana na ufisadi wakati kufanya hivyo ni kupambana na yeye mwenyewe.

Leo nina mada: Kwanini kaya na kijiwe chetu vimegeuka nyumba ndogo ya magabacholi? Na kwanini tunaridhika na uongo wa Cheka cheka kumlinda kibaka Tunituni na genge lake?

Nikiwa nimejiinamia, nasikia salamu toka kwa Mpemba.

Anasalimia: "Salaamaaleko jamia."

Mzee Kidevu anamjibu haraka huku akipokea kipisi cha sigara toka kwa mzee Ndomo.

Mara Msomi anaingia akiwa anabofya ki-Nokia chake. Akiwa anatafuta mahali pa kukaa, Mkurupukaji anaingia na gazeti. Kichwa cha habari ni, 'Yule mwizi wa pesa ya rada kumbe bado anatanua!'

Utadhani kamwaga jivu kwenye siafu!

Mgosi Machungi analamba mic. "Jamani hali hii inatishangaza. Yaani kia wizi wapo magabachoi! Hivi huu ndiyo ubinafsishaji hata kaya?"

Akiwa anashangaashangaa, Mkurupukaji analamba mic. "Mgosi hujui kwanini kaya hii imewekwa kimada na magabacholi? Hujui baada ya kuondoka Mchonga ziliingia sirikali za kijiweni zinazotumiwa na magabacholi kujineemesha huku sisi tukiteketea?"

Kabla ya kujibu, kwa mara ya kwanza, gabacholi Kanji anayeishi mtaa jirani, anatia timu kupata gahawa. Inaonekana katumwa na wenzake baada ya kusoma habari za kijiwe hiki mama wa siasa kutuchunguza.

Mzee Kidevu anaamua kumchokoza. Anauliza swali la nyodo. "Jamani kaya hii hivi ni ya Wadanganyika au ya magabacholi?"

Kanji kapata upenyo! Analamba mic bila kutoa hata taarifa. "Swahili napenda laumu Hindi. Kwanini silaumu ongozi yenu? Sisi nakuja na fuko tupu natoka na fuko jaa kwenda Bombay."

Kabla ya kuendelea Mbwamwitu anakwanyua mic kwa hasira. "Kanji acha kututia madole machoni. Yaani huna aibu unatutukana, tena kwenye kijiwe chetu!"

Kanji halazi damu. "Wewe toka. Iko na jiwe wapi we jusi? Sisi taka ondoa mbea yenu naweza honga city, kazi kwisa. Kama taka salama acha sisi. Nyinyi iko na lengo dogo dio maana ongozi yenu natumia sisi kuibia nyinyi. Kwanza nyinyi haiko na secret. Kama nakamatwa nasema siri yote. Lakini sisi nakimbilia London, Canada au Bombay. Pia sisi haiko na bibi nyingi. Sisi nazaa kama panya, lakini hapana lala na jumba dogo."

"Kanji acha nyodo, huo ni wizi hata kama mnashirikiana na baadhi ya wachumia tumbo wetu, mna lawama. Kwanza mmekujaje hapa kama siyo kuletwa na malkia mkoloni?" anauliza Makengeza kwa hasira.

Kanji halazi damu, anajitetea. "Hata kama letwa na Queen sisi iko raia sasa. Nenda laumu ongozi yenu kutumia pesa jumbani dogo."

Kabla ya kuendelea, Mbwa mwitu anamzodoa Kanji. "Nyie raia au kunguru! Angalia wenzenu walivyoitelekeza Kenya baada ya kuanza vagi. Nyie ni raia wa karatasi sawa na chui wa karatasi, hamna sera, ni wezi watupu, rudini kwenu mkafe kwa umaskini uliotamalaki."

Kanji anajibu. "Hiyo dua ya kuku haipati mewe dugu yangu. Wewe sida nini? Kwanini siseme sisi jumuia yetu kachangia wewe pesa kidogo ya kula na mama toto yako?"

Kapende anapandwa ghadhabu. Anamkwida shati Kanji ampe dispilini.

Anasema. "Kawatie madole akina Tunituni na Cheka cheka siyo sisi. Unapata wapi jeuri kutunyea tena hadharani mbwa we!"

Kapende anamtembezea kichapo Kanji hadi tunaanza kumuonea huruma.

Mzee mzima naingilia kati kuwaachanisha huku Kapende akitweta na Kanji akitetemeka utadhani kiama chake! Maana bila kufanya hivyo polisi wetu waabudiao magabacholi wakitukuta tunampa displini ponjoro watatutia ndani na kutubambikizia kesi za bange hata mada.

Mzee Maneno anaingilia kuokoa jahazi. "Kapende unamuonea Kanji bure. Hawa ni kama inzi, hawawezi kuacha kidonda bila kuchokonolewa. Hapa wa kulaumu ni vyangudoa wetu anaoongelea mzee. Huko nyuma walikuwa hawatumiwi hovyo hivi." Anamtazama Mkurupukaji.

Kanji hana imani na kijiwe tena. Anaamua kutimka mbio kwenda zake asipate kichapo.

Kijiwe kinamzomea hadi wapita njia wanashangaa.

"Huyo gabacholi. Huyo!" Yanasikika makelele.

Msomi anaamua kuingilia. "Wazee, japo hakuna mzinzi mmoja bali awe na mzinzi mwenzie, Kanji mmemuonea. Tumeshindwa kuwatia adabu vyangudoa wetu tunawaandama malaya wenzao! Hebu muangalie Tunituni. Eti bado anaalikwa akasuluhishe akina Kibaka wakati naye zigo la ufisadi linamlemea."

Anavuta kombe lake la kahawa na kupiga funda na kuendelea kutoa mapwenti.

"Mie nina wasiwasi na usomi wetu. Hivi inakuwaje afisa tena mzima kama Tunituni bwana kujua anaingizwa mjini na tapeli kama Jitu au Shaileshi Visirani?"

Kabla ya kuendelea, Makengeza anamjibu. "Msomi usishangae. Hukusikia vizuri maneno ya Kanji? Jamaa wanawatumia magabacholi kuficha siri zao. Huoni wanavyohangaika na Ballaliii kutaka kumnyotoa roho ili awafichie siri? Usishangae kuona tunaowalilia watende haki ndiyo wezi wenyewe."

"Du!" Anasema Msomi Mkatatamaa na kuendelea. "Mzee umenifumbua macho. Kumbe ndiyo maana Chekacheka kaamua kututoa kafara kumlinda Tunituni! Hakika kaya hii si huru, ina maadui aina mbili; magabacholi na vyangudoa wetu wachumia tumbo. Angalia mabaki ya nyumba za Mchonga, viwanda, maduka, mabenki, maduka ya kubadilisha na kutoroshea pesa na sasa kimebakia kijiwe kama pango la wezi kama alivyoonya Mchonga. Kwanini tusianzishe chama cha kudai uhuru upya?"

Akiwa anajiandaa kukomelea pointi nyingine, Mpemba anadandia. "Yakhe, hawa dawa yao kupigwa mawe. Adhabu ya mzinzi yeyote kupigwa mawe hadi kufa bila kujali nasaba wala cheo. Hivi naye Ntikila kaishia wapi? Maana naona magobacholi wazidi sasa hadi waingia kwenye mjengo wetu Idodompya!"

Msomi anaendelea. "Ami umesema vyema. Tumewekwa mabaya hadi kuruhusu kunguru wa mzee Karumekenge watutawale na kutuibia. Napata taabu kuamini hata bidhaa wanazotengeneza kwenye viwanda vyao. Kama wanaweza kuwa na influence kiasi hiki kwanini wasitulishe sumu, uchafu na bidhaa zilizopo chini ya kiwango? Nani atawakamata iwapo hata kijiwe ni chao? Anayebishia hili arejee utawala uliopita wa mfanyabiashara Tunituni na mkewe mama moneybags."

Kabla ya kuendelea simu yake inalia. Anaipokea na kuongea kwa kifupi na kuendelea na lecture.

"Hawa jamaa si bure. Wanapata jeuri kutokana na kuibeba sirikali iliyomo mifukoni mwao tokana na tamaa, upofu na nyongea ya jamaa zetu. Hata chama kimeishaingiliwa muda mrefu. Ogopa kiama cha walaji kinachopata ruzuku isikitoshe kikaamua hata kuwachuuza watu wake. Chama ilikuwa zama za Mchonga sasa ni kiama chetu.

"Ni genge la wachumia tumbo. Hakuna aliye safi wala mwenye nafuu. Hata hawa mnaowadhania ndio siyo. Juzi jamaa wa intelligence alinitonya, kama ukweli wa ufisadi wote kijiweni na kayani ukiwekwa hadharani, wa kwanza kuadhirika na kuathirika kama Wadanganyika wataamka ni kiama chao cha walaji. Wa pili ni mkuu wa kijiwe mwenyewe. Huoni kila uchao anakuja na mazingaombwe! Kwanini hawakamati Tunituni na magabacholi wake?

"Anafahamu akiwakamata nao watamkamatisha. Laiti kijiwe kingekuwa na watu wenye akili, dawa hapa ilikuwa kumkoma nyani bila kuangaliana usoni. Maana kijiwe kimewashinda kiasi cha kuwaachia magabacholi wakichezee wanavyotaka. Kama alivyobainisha Kanji, usishangae siku moja tukawa na mkuu wa kijiwe gabacholi kama alivyowahi kuotea mbweha mmoja gabacholi kule Zenji. Mnamkumbuka ya Zenji? Hakina wataalamu hii huiita Gabacholization of Kaya and Kijiwe."

Alipokuwa akijiandaa kuendelea, mara ndata walivamia kama upupu ili watunase kwa kumtia adabu mteule gabacholi Kanji. Mie nilitimkia zangu Ilala kwenye ofisi ya DP ya Ntikila.



Source: Tanzania Daima Januari 30, 2008.

Tuesday 29 January 2008

Mkapa and Meghji, the ball is in your court.

Today’s pointblank is to pore on two or more prominent and controversial figures in our country that are supposed to expediently and reasonably rejuvenate their honour or their tarnished names -as politicians would put it.


Anybody conversant with accountability as means of proving innocence of anybody will agree with us: Zakhia Meghji, minister for finance’s resignation is long over due. On the same footing, even the former president, Benjamin Mkapa is duty bound -as per the norm and constitution- to break his silence with regards to all allegations surrounding him.

Will the duo of the trio embark on the fulmination to suing all tongue wagers agitating they be brought to books? Nay! This can’t be let alone helping them. For those who opted for this derangement ended up in shame -tail in legs. Doing this will add more valour and vigour to Dr. Slaa who seems to be hell bent to knock sense in some bumpkins.


Anybody well versed with legal matters will agree with us once again: what Meghji did -by admitting- she was cheated by former Governor of BoT, Daudi Ballali so as to illegally consent to payment to ghost companies like , Kagoda, Jeetu Patel’s and other Peculators, is nothing but self incrimination or self-inculpating in legalese.

In law, objecting to making an admission can be taken as refuting allegations. This is the way Mkapa chose. But again, in the court of the people, the rules are totally different. The "judges" in this court are not learned brothers and sisters. Thus technical legalese does not apply; even lacunae may sound different.

This being this, truly, Meghji has no reasons whatsoever to remain in the office of the minister. How can she whilst she consented to the firm that peculated our money? How can she whilst she lunged our economy in lumping danger?


This aspect of things does not affect Meghji alone. It applies even to President whose silence and consent with regards to ufisadi is creating dismay and make many chafe the country over. This state of silence and denial is transcendental. Mkapa sought not to answer to all-seem-to-be-real-and-plain-true allegations against him. Will this solve the problem and avert him the danger he eminently faces? Is Mkapa embarking on the art of a wise monkey that sees nothing and says nothing? Contemporary thinkers have Mkapa as an expounder and extemporizer of the doctrine of lazy thinking in ruling, running and ruining a state. Will Mkapa, his wife, kids and other consigliore survive in the future shall we have a new responsible person on the helm?


I vividly still remember Mkapa, the firebrand, leathery and doyen in calling names. Had what is alleged been wrong and inaccurate, he’d not fall short of calling --those egging on him to come clean or face auto-da-fe-- freebooters, love children, putains even the like of merry-andrew. It seems. Mkapa, who used to call us names, was unaware of satirizing the other Mkapa behind the curtains we know now! What a faux pas!

On Meghji with her lugubrious job, one can lucubrate: she must go before being told to do so. This is but most honorable way to show sense of accountability and responsibility in the first place. As for President, his silence and obscurantism are seen by other quarters --especially opposition-- as condoning corruption! Does he cognize this?


Will Meghji wait for President to lug her out? How does she take this lusus naturae so openly known by every eye? Will President extend his powers of clemency to Meghji as he did to Mkapa et al? Shall this happen, isn’t another abuse of powers in the first place?

Meghji stay is nothing but flouting the office she has already upbraided. Will President macerate towards this chicane?

As for Mkapa, though we’re told not to disturb the old man who is supposed to enjoy his yum-yum and chapattis in his world of merry-go-round with his wife, the pains and twangs of our money still forces us not to.

How can we swallow our pride to stomach this whilst we are cascading into abject poverty? How can we let him swim in profusion and opulence whilst we are sunk in impecuniosities?

This reminds me of King Lear in Shakespeare and Oedipus in Sophocles. Mkapa’s coming clean and Meghji’s resignation will "turn all these pains and outrages, the cruelties and atrocities into a means of sell-liberation, thus giving us an inner solace which can not be attained by any other way."

If anything, this forces me into re-mourning for Edward Sokoine especially when I recall how he sternly dealt with economic saboteurs and the likes. Of all this sends me back to crying for Mwalimu Julius Nyerere who died a pauper but protuberant and saintly as far as economic shames are concerned.



So it should be noted. The contumely of the trio namely Mkapa, Meghji and president among others will never do them good but otherwise. The wisdom here is to hark and heed vox populi vox dei in that the voice of the mass is the voice of God. For by and large and in the main, the ball is indeed in their court come what may.

Let us face it point blank and faute de mieux. Ada ya mja kunena.

OFF THE CUFFS: I read of the denial by CCM treasurer, Rostam Aziz which in the sense is an admission that his party swindled our money though by then he was not a treasurer. The damage has already been done though. What is CCM waiting for?
Guys, what are you waiting for? What do I know?

Monday 28 January 2008

Mkapa, Kikwete, ufisadi na mainzi.



Jikumbushe makele ya Mainzi wanapokuwa kwenye mzoga halafu akaja Mbweha au Mbwa hata Kicheche kuushambulia mzoga wake. Mainzi uhanikiza na kupiga makelele kama silaha pekee yaliyo nayo.

Hakika makelele ya mainzi huwa hayamzuii mvamizi kula mzoga atakavyo hata wakati mwingine kuyala mainzi yenyewe na yasifanye kitu! Hawa ni hayawani isitoshe wadogo wasio na misuli na vikumbo kuweza kupambana na mvamizi.

Jaribu mfano mwingine wa Vyura pale Tembo avamiapo bwawa kunywa kuoga na kuyachafua Maji. Vyura, kama Mainzi, nao hupiga kelele hadi Mswahili akawazodoa: kelele za Vyura hazimzuii Tembo kunywa maji.

Mswahili huyu huyu bingwa wa falsafa hata mafumbo haishii hapo. Husema: kelele za mMango hazimnyimi Mpangaji usingizi.

Ukiangalia mazingaombwe, usanii, ujambazi na kila hadaa vinavyofanyika "kuwanusuru" watuhumiwa wizi wa mabilioni ya pesa kwenye akaunti ya madeni ya nje (EPA), bila shaka, unaijiwa na picha hizi tatu. Ni somo gani unapata hapa?


Kwanza, ni uhovyo wa mainzi, vyura hata mlango. Pia ni uonevu wa tembo na mbweha, mbwa, vicheche (mvamizi).


Pili ni hekima: tusifanye mambo kama hayawani. Tusiridhike na makalele ilhali "wabaya wetu" wakiendelea kuukatua mzoga, kuchafua na kunywa maji au kuuchapa usingizi. Je nasi tumekuwa wa hovyo kama wao? Je tumekuwa katili kwa vizazi vijavyo kwa kuendekeza woga na makelele ilhali mambo yanazidi kuharibika?

Kujibu maswali haya vizuri, jiulize, mbali na makelele na ngebe, watanzania wamefanya nini kuzuia mzoga wao kushambuliwa na wanyama tajwa wanaojulikana kwa uchoyo na ulafu wao? Wamefanya nini pale waliyemtegemea atende haki kwa kumkabidhi ofisi na zana zote za dola ameamua kuzitumia dhidi yao kuwalinda Mafisadi?

Je kwa msimamo wa rais Jakaya Kikwete kwa mfano kusema wazi hatamchunguza mtangulizi wake, Benjamin Mkapa, siyo kuusaliti umma na viapo vyake vya ofisi? Maaana, wahenga husema: asiyevuta kamba nasi si mwenzetu ilhali waingereza wakisema: show me your friend I shall tell you who you are ama nionyeshe marafiki zako nikwambie wewe ni nani? Je katika hili Kikwete ni nani? Sitaki nimjibie.

Taarifa za vyombo vya habari kuwa uchunguzi wa kashfa ya BoT, jina la rais mstaafu linajitokeza mara nyingi si za kuacha kama taarifa tu bali onyo kuwa watanzania hawajiandaa kupambana na ufisadi wala kurejesha mali zao zilizomo mikononi mwa mafisadi ambao kwa bahati mbaya wengine bado wamo kwenye ofisi za umma wakiharibu ushahidi na kulindana!

Inashangaza udhati wa Kikwete kuweza kulala usingizi hata kujitahidi kuwaridhisha wananchi; atapambana na ufisadi wakati ukweli ni kwamba kinachofanyika na kinachosemwa ni tofauti kama usiku na mchana hata mbingu na ardhi! Je umma haujaona mchezo mzima?

Niliwahi kuuliza: kama Mkapa ana kinga na mkewe, mwanae na washirika kwenye makampuni yao nao wana kinga? Mbona hawakuwa marais hata kwa sekunde moja? Au ni yale yale ya ufalme wa mlango wa nyuma? Au tuseme: ni yale yale; waarabu wa Pemba?

Kwanini hatutaki kuwaambia watawala: hii ni nchi yetu na siyo yao wala mama zao? Kwanini tunaogopa hata kuchukia kama tumeshindwa kuondosha kwa mkono?

Leo ufisadi wa BoT umebebwa na Daudi Ballali, gavana wa BoT wa zamani utadhani alikuwa peke yake! Kwanini tunachezewa mahepe mchana kama watoto wadogo nasi tunaupwakia uongo na matusi haya?

Tuliwahi kuuliza na kudodosa alipopata na alivyopata mali zinazosikika kuwa za Mkapa kama vile majumba ya Lushoto, Upanga na mengine ambayo bado hayajajulikana. Tulidhani umma ungetumia hojaji zetu kudai haki kwanza na kama madai hayasikilizwi basi uchukue mali zake au hatua mujarabu. Lakini wapi?

Tuliwahi kuhoji: nani anamfanya nani bwege? Tulihoji: kazi ya rais ni nini na ipi iwapo anatuzodoa tena hadharani; hawezi kumchunguza Mkapa achilia mbali kumfikisha mbele ya haki? Je hatujawa mainzi tena mafu? Ajabu ya nchi yetu; tuko tayari kuandamana hata kupambana na FFU kwa mambo madogo kama kashfa za kidini na mengine lakini hatuna mshipa wa kusimamia haki zetu zitendeke na kulindwa?

Je rais na watendaji wake wanajua uhovyo wetu kiasi cha kututendea mambo ya hovyo hivi? Je kwa kutenda hivi wahusika nao hawajawa wa hovyo kiasi cha kuwa na nchi hata jamii ya hovyo? Je mwelekeo wa hali hii ni nini kama siyo miaka mitano ijayo kushuhudia makubwa kuliko hata haya ya Mkapa? Je hatujawa kichwa cha mwendawazimu kama alivyowahi kuonya mzee Ruksa? Hatujawa mainzi mafu?


Ajabu ya maajabu, vijana wetu wengi wamegeukia jinai kama ujambazi hata uchangudoa ambayo kimsingi vinaweza kuondoa uhai wao ilhali kudai haki halali kumetelekezwa! Kiongozi na shujaa wa Mau Mau kule Kenya, Dedan Kimathi aliwahi kusema; heri kufa umesimama kuliko kuishi umepiga magoti. Tuko wapi sasa?

Nchi jirani ya Ethiopia kuna kabila la Oromo ambalo kwenye lugha yake ya Oromia kuna methali isemayo: heri kuishi siku moja kama simba kuliko miaka mia kama kondoo. Je sisi hatujawa kondoo tena wa shughuli ya fisi?

Kuna haja ya kuwatolea uvivi Kikwete na swahiba yake Mkapa na kuwaambia: Tanzania siyo yao peke yao:ni yetu sote kwa sawa. Badala ya kunung’unika na hata kumlilia marehemu Mwalimu Nyerere au kuotea; atakuja malaika kutukomboa, tuamke na kurejesha nchi yetu mikononi mwetu.

Inashangaza na vyombo vya dola vyenye watendaji makapuku kama Polisi na idara nyingine vimeridhia uhovyo na uinzi huu!

Kama Kikwete alituahidi kututumikia na siyo kututumia kama ilivyo, basi atutumikie. Kama ameshindwa kwanini tusitafute mwingine ambaye yuko tayari na mwenye uwezo wa kufanya hivyo badala ya kuishi kwenye uinzi?

Tumekuwa tukimuogopa Kikwete hata waziri wake mkuu. Tunawaandika kwa kuzungusha. Tunatumia lugha za kinafiki za mheshimiwa rais angefanya hivi au vile. Jamani, tumwambie hata kama atachukia kuwa anakotupeleka na anavyotuswaga sivyo tulivyokubaliana. Tulimchagua awe mtumishi wetu siyo Bwana wetu kama ilivyo. Anayebishia hili aangalie utendaji mbovu wa serikali ya awamu ya nne tangu iingie madarakani.

Ajiulize ni mangapi tuliyokubaliana yametimizwa zaidi ya dana dana na mazingaombwe kama wengine wayaitavyo. Je kwa Mkapa kuendelea kutuchezea na kutudharau haimaanishi bado anatawala kwa mlango wa nyuma? Je nani anapenda kuwa na hali ya ukatuni (Caricuture). Nani anautaka u-Joice wowowo! Mkumbukeni Joyce Wowowo akinengua baada ya achezeshaye kutia madole kwenye kijisanduku naye akamwaga burudani lakini kwa mikatiko ya matusi. Je tumekuwa wa hovyo kushabikia matusi haya? Namshukuru Mhariri wa Tanzania Daima kwa tahariri yake ya jumapili 26 Januari aliyemtaka Mkapa avunje ukimya. Je atafanya hivyo? Je kama Mkapa na Kikwete wataendelea mchezo huu, utabiri wa mawe kusema kwa namna tofauti na mainzi ya kwenye mzoga unatimia taratibu?

Kwanini Mkapa anaonekana kuwa na kiburi? Je ni kwa kujua uinzi wetu au ukubwa wa kinga ya Kikwete? Je kwanini Kikwete naye anaridhia kadhia hii kama hana mpango wa kuitenda hata zaidi ya hii? Siku njema huonekana asubuhi na siyo jioni. Imetimu miaka zaidi ya miwili tangu Kikwete akabidhiwe nchi. Je kuna ishara gani tokana na matendo ya awamu yake?


Kikwete asijesema nampakazia. Akinipa sababu zenye siha hata mbili za kwanini Mkapa asishughulikiwe na yeye hana mpango wa kuwa Mkapa mwingine miaka ijayo, nitaacha kuuliza swali langu kuu:kwanini Kikwete na Mkapa lao lisiwe moja.

Muda umeisha. Tuachane na uinzi tuuvae usimba tuikomboe nchi yetu toka mikononi mwa akina Mkapa na wenzake ambao wanatucheka badala ya kuomboleza. Yote hii inatokana na makelele ya maizi ilhali mzogo unatafunwa na mbweha.
mpayukaji@yahoo.com

Wednesday 23 January 2008

Kondoo wanapogeuka mbuzi kwa mafisadi

HABARI kuwa wananchi wenye hasira walivamia shamba la aliyekuwa gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Daudi Ballali, haziwezi kupita bila kujadiliwa.

Januari 20, mwaka huu, tulishuhudia wananchi wenye hasira kwenye eneo la Mbweni-Maputo, Kinondoni, Dar es Salaam, wakivamia shamba la Ballali na kuanza kuligawana.

Walifanya hivyo, kwa kudai kuwa lile shamba lilipatikana kutokana na pesa yao iliyoibwa na wachache wakishirikiana na watendaji wa serikali akiwamo Ballali.

Hakika huu ni mwamko mpya licha ya kuwaonya mafisadi kuwa muda wao wa kutanua unaanza kuwatupa mkono.

Ni kauli na kitendo cha ukombozi cha kuukataa ukondoo na urambaji wa viatu vya wakubwa wasio na ukubwa wowote, isipokuwa ukubwa wa ovyo.

Kama wezi wetu wamebakiwa na ukubwa, basi si ukubwa chochote, bali ukubwa wa dume la nyani ambalo licha ya kuwa na maguvu, halina akili ya kulima bali kuongoza kushambulia mashamba ya binadamu.

Katika sakata hili, binadamu wameamua kwa dhati kupambana na manyani watu, waliovamia rasilimali na asasi zao hata serikali kwa ujumla.

Hili laweza kuonekana kama jambo dogo. Lakini ifahamike umma hauna dogo unapoamua. Hata kuchoma vibaka moto kulianza na watu wachache.

Tumekuwa tukiwahimiza wananchi waachane na kuwaua vibaka huku wakiwanyenyekea wanaotafuna mabilioni yetu na kusababisha ongezeko la vibaka.

Sasa wakati wa wananchi kuwasaka wabadhirifu umewadia.

Pamoja na sheria kuwa wazi, hakuna anayeruhusiwa kujitwalia mali halali ya mwenzake, sheria hiyo hiyo iko kimya kuhusiana na mali haramu kama hii ya Ballali.

Kilichofanyika ni somo kwa serikali, ikamate mali za watuhumiwa haraka kabla hakujatokea vurugu hata umwagikaji wa damu. Watawala wetu walizoea kutukoga na kututuliza kwa pesa zetu wenyewe.

Wamezoea kumkaanga samaki kwa mafuta yake. Sasa samaki ameshtuka. Ukiingia majini kwake anakugeuza asusa.

Hakuna nchi ambayo mafisadi wana jeuri kama Tanzania. Ni watuhumiwa wangapi wa ujambazi tunawajua sasa ni waheshimiwa?

Ni wangapi wameghushi nyaraka na vyeti na sasa ni waheshimiwa huku wakikingiwa vifua na serikali hiyo hiyo tuliyodhani ni yetu?

Inashangaza kuona mali zinazodaiwa kupatikana kwa dhuluma kama za kina Kagoda, Jeetu Patel, Tanpower, ANBEN (Anna and Benjamin Mkapa), na Fosnik (Foster and Nicholas Mkapa) na nyingine nyingi bado zimo mikononi mwa watuhumiwa!

Ni majumba mangapi na viwanja vya ubadhirifu vingapi vinaendelea kuwa mikononi mwa wamiliki kinyume cha sheria? Je, hii ndiyo siri ya serikali kusuasua kukamata na kufilisi watuhumiwa wanaojulikana, tena wakubwa?

Ziko wapi nyumba zetu zilizouzwa na Serikali ya Awamu ya Tatu? Je, serikali itaendelea kuwalinda wahalifu hawa dhidi ya wananchi ambao inaonekana kuwaacha kila mtu ajitafutie haki yake ajuavyo?

Ingawa tumekuwa tukiaminishwa na watawala wetu kuwa nchi yetu ni ya amani. Ijulikane wazi kuwa amani haiwezi kuwapo bila haki na uwajibikaji.

Ikiwepo imani ya amani na si amani kwa maana yake. Ikiwepo ni kejeli (mockery) kwa amani na wananchi kwa ujumla. Ni uongo wa mchana kusema kuna amani iwapo umma unaibiwa kila uchao, tena na wale watu uliowaamini kuwapa ofisi zake.

Sasa ndiyo wakati muafaka wa wananchi kuukiuka mwiko wa kugeuzwa nepi za kufutia uchafu wa watawala. Ni wakati muafaka kwa wananchi kuachana na kugeuzwa vichaka na mihuri ya kufichia mali za wizi zitokanazo nao.

Ni mara ngapi rais amekumbushwa kutaja mali na wenzake? Je, wananchi wataendelea kuwa ‘wajinga’ na kuruhusu watawala waendelee kufanya ubadhirifu kwenye fedha zao?

Serikali inayoficha mali za watumishi wake inaweza kujiepusha na shutuma za ubadhirifu? Hata chama kinachounda serikali hii si chama cha ubadhirifu?

Kama kuna wilaya imeonyesha mwamko wa kifikra, si nyingine bali Kinondoni, Dar es Salaam, ambayo ninaipongeza.

Tukio la kukamatwa mali ya Ballali si la kwanza. Nani amesahau mkuu wa wilaya hiyo aliponusurika kipigo baada ya kutaka kuwageuza wananchi kuwa ‘wajinga’ kusimamia ubadhirifu wa mali zao?

Ilitokea Wazo Hill, Kijiji cha Chasimba. Imeingia kwenye vitabu vya historia, wananchi wameukataa utawala usiowajali wala kuwafanyia lolote isipokuwa kuingia mikataba mibovu kama ilivyodaiwa kwenye sakata la Richmond, IPTL, ubinafsishaji na uuzwaji wa NBC.

Huu ni mwaka wa wananchi kujinasua kutoka mikononi mwa mafisadi hata kama watakuwa wanalindwa na serikali.

Tulionya kuwa serikali inaweza kufurushwa na wananchi wakijua kuyatumia vizuri madaraka yao kama ilivyotokea kwenye mifano hii miwili.

Hakika hata wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu wanaoendelea kuzungushwa na kudhalilishwa na wamangi meza wachache nao wataamua kuamka usingizini na kudai hata kuchukua kilicho chao.

Hatua hii ya ukombozi itaondoa uongo na unafiki wa baadhi ya watawala kuwa wanaongoza kwa ajili ya wananchi, wakati ukweli ni kwamba wanatawala na kufanya ubadhirifu kwa ajili yao binafsi na marafiki zao.

Ingawa serikali imeshikilia ripoti ya ukaguzi ya Ernst and Young, ukweli ni kwamba kashfa nzima ya BoT haijawekwa ugani kama ilivyo. Tulicholetewa ni majani.

Bado shina na mizizi ya gogo zima liitwalo kashfa ya BoT, nani ataridhika na mbuzi wa shughuli (Ballali) wakati wenye shughuli wenyewe bado hawajaguswa? Je, rais anajua kuwa wananchi wanamfahamu zaidi ya anavyodhania?

Anayo habari kuwa wana hasira kuliko anavyojiridhisha au watapiga kelele halafu watanyamaza?

Kwa upande wa wananchi nao inabidi waongeze kasi. Maana inashangaza kuona walipigia kelele kulanguliwa umeme halafu taratibu wanaletewa kesi ya Ballali, nao kama ‘mbwa’ aitikiaye miito mingi, wanauingia mkenge wananyamazia kadhia na jinai ya kulanguliwa umeme, ilhali serikali ndiye mlimbikizaji mkuu wa madeni, ukiachilia mbali kuwa nyuma ya Tanesco.

Hata kama mbinu chafu za kuleta picha mpya kila inapozuka picha yenye kuweza kuwaamsha wananchi inainusuru serikali, ukweli unabaki pale pale kuwa wananchi wanaita mazingaombwe ya Rais Jakaya Kikwete na timu ya mawaziri wake waliotajwa kwenye ufisadi.

Leo, watu wangetaka kuona mawaziri kama Basil Mramba, Juma Ngasongwa, Andrew Chenge, Edward Lowassa, Zakhia Meghji, Ibrahim Msabaha na wengine wengineo, wanaotuhumiwa kuiingiza nchi kwenye matatizo ya kiuchumi wakichukuliwa hatua za kisheria.

Hakika kilichotokea kwenye shamba la Ballali ni ukweli kuwa kondoo wameanza kugeuka kuwa mbuzi dhidi ya mafisadi wanaowasumbua.



Source: Tanzania Daima Januari 23, 2008.

Vigogo mnangoja nini kijiweni?

LEO mzee mzima napayuka na kupayuka na kupayuka si kwa sababu ya ulabu kama kawaida yangu.

Nimelewa hasira na njaa kusema ukweli. Jana niliichapa pombe kiasi cha kuamka na hangover. Nimeishazoea, kuutundika ili nao mbu nikirejea wanitundike kabla ya mshirika wa bedroom naye kunitundika kwa kuniibia akiba ya mama.

Zamani wezi walikuwa wanaume, hasa walevi kama Mpayukaji ambao bila kuzamisha chupa iwe ya boa ulanzi au mataputapu mengine, siku haiendi.

Mambo yameenda yakibadilika siku hizi. Hata akina mama nao wamo kwenye kukwanyua njuluku hasa za kaya!

Hebu chukulia mfano huyu Iron Lady utadhani ameumbika kwa chuma. Juzi ameamua kukiri kwamba alishauriwa vibaya na Ballaa Dadi Dalaliii wa Band of Thugs ambayo kwa kuifupisha waweza kuiita BoT.

Zamani vibaka walikuwa vijana wasio na mbele wala nyuma, juu wala chini. Siku hizi ni watu wazima na nafasi zao, tena za kupewa na umma wanaouuma kwa uma utadhani hatujui!

Nani angelidhani waziri mzima, tena wa njuluku angejikurupukia kama ndugu yangu na mwana kijiwe mwenzangu Mkurupukaji na kuidhinisha malipo yasiyostahiki kwa Kampuni ya Kagoda? Sasa kama Kagoda kamemuingiza mjini akaukwaa mkenge, kitakapokuja kigoda si atamaliza njuluku za Kaya? Sijui naye anangoja nini?

Ajabu ya maajabu hata Mkuu wa Kaya ya Kijiwe naye ameuchuna utadhani maneno ya kujinyonga ya Iron Lady ni muziki. Au ni kwa vile Iron Lady na mkuu hawakusomea sheria kiasi cha kutoimanya? Mbona wanasheria huita hali hii ‘self-inculpatory evidence’ au ‘admission’ kwa lugha rahisi?

Je, Mkuu wa Kijiwe anangoja wapingaji wahanikize kumtaka amtimue huyu mama ambaye kama Hill Clint-on wa kule kwa Joji Kichaka Pori anavyobabaika kwenye kutoa maamuzi? Aliunga mkono majeshi ya Kichaka na Diki Chini kumvamia na kumfurusha Saadaam Husseinii eti kwa kuwa na silaha hewa za maangamizi ya umma (Weapons of Mass Destruction). Mara kwenye kampeni ya kutaka kukaa kwenye jumba jeupe lisilo jeupe bali jeupe kisera, anajikanyaga kiasi cha akina Obamaaa kumbamiza na kumkanyaga kanyaga!

We mama unangoja nini iwapo mkono wako ulibariki maasi yaliyosababisha kuangamia kwa pesa ya umma? Huoni kuwa maamuzi yako nayo ni Weapons of Money Destruction kwa Wadanganyika? Je, unangoja nini?

Ngoja nikutolee uvivu nipayuke zaidi tena bila woga wala kupinda maneno. ZM au Iron Lady pack and hit the road. Siku hizi nimesoma na naumanya ung’eng’e. Nasema mama kitoe huna dili wala sera hata kama una dola pamoja na akina Kagoda, ANBEN, Fosnik, Tanpower na wengine.

Leo nimeamua kutoa dozi tena kwa mapozi. Ngoja niwashukie wakubwa tu wanaojifanya hatujui chafu yao. Nanyi mna kosa la kigaidi la kuwa na zana za maangamizi ya njuluku au Weapons of Money Destruction.

Yupo huyu Eddie Lu-washa ambaye alikiri mwenyewe kwamba alikurupuka kuipa ulaji Richmond iliyopata mimba na kuzaa Dowans kama ilivyo mitandao ya nambari wani inavyopata mimba hovyo hovyo na kuzaa mitandao mingine midogo ya kumalizana. Hayo tuyaache. Acha nipayuke.

Eddie, una habari kitendo chako cha kukiri baada ya kuitetea Richmond kama walivyofanya wale watu wa rushwa wa TUKUKURA, ni kosa sawa na alilokiri huyo mama juu niliyempa vipande vyake?

Juzi nilipokea tuhuma kuwa binti yako naye kumbe yumo BoT akikamua na kutanua. Je, analinda hisa zako au ndiyo hayo kuwa mtoto wa nyoka ni nyoka?

Eddie Lu-washa, hata kama mkuu wa kijiwe ni swahiba yako ujue una udhaifu kwa kukurupuka kama Iron Lady halafu ukasimama kwenye kijiwe cha Idodomya ukautetea huu uoza na baadaye ukakiri ulilazimika kutokana na uhitaji wa nishati. Kaka jiondoe maana huna sera kwa sasa.

Yupo kaka Basi Shilingimbili. Wewe hata kama umekula kobisi na jiwe, tunakujua ulivyosuka dili la akina Bangue of Tanzanie. Je, kaka nawe unangoja nini? Kitoe. Tumechoka na michosho.

Leo nimeamua kupayuka tena kwa herufi kubwa na kinywa kipana. Acha nipayuke kabla hamjanikolimba au kunibenea na kunigambwage kwa tindikali. Ila mjue hilo si jibu wala suluhu bali kuchokoza hasira za umma mnaouuma mkidhani ni maamuma.

Leo sijautwika. Nina mapwenti kama Mchonga na usongo kama Sokoine na Lyatonga.

Siogopi vigogo wala Wagogo. Hata vikwea na Wakwere siwaogopi. Mie natoa dozi kama kazi wala sitaki upuuzi hata ujambazi.

Kaka Ibra M7ha nawe unangoja nini iwapo, kama Iron Lady, uliridhia Richmond? Nawe kitoe hata kama unatoka eneo moja na mkuu wa kijiwe.

Siwezi kumaliza mipayuko yangu bila kumpa salamu rafiki yangu Enderea Chenga. Wewe ulishirikiana na Tunituni kuiingiza kaya kwenye balaa la mikataba mibomu ya madini. Japo uliwalamba chenga akina Tunituni na Chekacheka, jua hutaulamba chenga zako umma ambao uliishakustukia. Ujue mie naongea kwa niaba ya umma.

Tena umma wenyewe si wa kuuma bali wa kuzomea na baadaye kutoa kichapo. Wewe ni loya.

Ohoo! Nilitaka kusahau salamu za swahiba zangu wawili Niziro Kadamage na Rostitamu Aziz. Nyie nanyi yenu twayajua hata kama mnazo, lakini si za wizi kama za yule jamaa yetu ponjoro Jitu Patili? Kumbe tulidhani madingi na wazito kumbe wakwanyua njuluku za umma. Angalia Kadamage alivyoshikwa pabaya kule Landani kwenye hoteli ya… Oh! Nimesahau jina.

Rostitamu Aziz tunaambiwa ndiyo unaendesha kijiwe kwa kutumia mitandao na mitandio ya chama! Jamani, yaani hii kaya kweli hovyo! Jitu linatoka sijui wapi huko linakuwa na say kwenye kaya yetu!

Hivi Mdanganyika anaweza kwenda umangani au uhindini akafanya chafu kama hii bila kulipuliwa kama Benazir Bhutto? Je, tatizo ni sisi au hawa kunguru? Where is the problem ya matatizo jamani?

We naona unacheka. Usicheke. Hii si habari njema. Don’t cheka wakati unaliwa, you must lia na kuomboleza. Usichekecheke kinafiki kama Cheka Cheka anayechenga chenga na kudana dana kwa kutumia vicheko.

Naona na yule anashangaa maneno haya. Mbona hushangai urithi wako kugeuzwa sadaka ya vyangudoa wa nje na ndani? Mbona hushangai jamii ya makondoo na kuku? Acha uvivu wa kufikiri kama Tunituni aliyeishiwa fikra, kwa uvivu akanenepa kiasi cha kiuno na shingo kulingana huku akiwabeua wenzie kwamba ni wavivu wa kufikiri!

Acheni uvivu wa kufikiri nyie. Msijidanganye, mambo hayatabadilika au umma kuwabadilikia kama mlivyoubadilikia. Acheni kudhani wataendelea kuwa kondoo. Wanaweza kugeuka chui kama Daktari Silaha wakageuza kibao. Shauri yenu! Kalagabaho.

Nimegukie Mkuu wa Kijiwe. Bro, bado unachekea chekea matatizo haya! Bado unawavumilia magaidi wenye Weapons of Money Destruction! Una habari zamani Osamaa alikuwa best wa akina Kichaka? Alipoamua kuwa gaidi kama wao wakamtolea uvivu. Hata Saadamu alikuwa best wao pia. Alipojiingiza kwenye Weapons of Mass Destruction, walim-destroy.

Nawe mshirika huna jinsi. Achana na uswahiba na magaidi wa njuluku ya umma. Wafanyie kweli. Kwa vile wewe ni mswahili huna historia ya kujilipua, basi watimue urejeshe confidence ya wanakijiwe waliokupa kula kama Tsunami wasijue Tsunami kweli!

Nihitimishe kukumbusha. Wafuatao lazima mwaka huu watimke.

Iron Lady Zakhiya Mengi-Jii, Eddie, Enderea Chenga, Basi Shilingi mbili, Ibra M7ha, Niziro Kadamage, Rostitamu Aziz et al.

Loo! Kumbe napayuka tu! Acha nitimke kusaka pesa ya kula. Sijui ya kuishi nitaisaka lini?

Msomaji usijali, naongea peke yangu baada ya kusikia taarifa kuwa mama wa njuluku amekiri kuingizwa mjini na Dalaliii. Sijui wote hawa wanangoja nini? Mkuu naye sijui anangoja nini!

mpayukaji@yahoo.com

Source:Tanzania Daima ya Januari 23, 2008.

Wednesday 16 January 2008

Kijiwe chalaani kufukuzwa Ballali peke yake

BAADA ya mkuu kuwaingiza mkenge Wadanganyika, kijiwe kimefanya kikao na kuja na azimio la ghafla kulaani kutupiwa changa la macho. Bila hofu tunatoa shinikizo BoT isafishwe pamoja na taasisi nyingine.

Mzee mzima nimewahi na kumkuta muuza kahawa peke yake akilalamikia maudhi ya mkewe. Analalamika tangu mafisadi waupeleke uchumi wetu ICU, mkewe anatishia kuondoka. Amechoka kulishwa mbwanda na bichwa la kambare.

Nikiwa nimechoka kusikiliza umbea wa muuza kahawa, mara Mgosi Machungi anatia timu akiwa anatafuna ubani.

Anaanza. "Mgosi umesikia ushanii wa Mkuu wa Kaya ya Kijiwe? Eti anamtimua Baai na kuwaacha wezi wengine, tena pae pae Benki Kuu! Mbona wae watoto wa vigogo hajagusia? Hii Kaya sina hamu Mgosi."

Wakati najiandaa kujibu naona na Mpemba anaingia akiwa anavuta tasbihi yake. Inaonekana hili la Dalaliii halimshughulishi kama Mgosi.

"Salaamaleko jamia," anasalimia Mpemba.

Tunajibu na Mgosi anaona kama wazo lake linapuuziwa. Anaamua kurejea ugani. "Ami naona unashughuika na mengine waa la Baai halikuhangaishi! Hawa makafii sijui walitilisha nini?"

Mpemba anajibu. "Weye waongelea usanii wa kutengua ulaji! Mie banki kuu nshaaitoa maana. Ile banki kuu au ya vigogo na watoto wao? Hata kule Zanzibar wevi watupu."

Wakati tukisukuti maneno ya Mgosi na Mpemba, Mbwa Mwitu anatia timu akiwa anaimba wimbo wake sijui kaunyaka wapi?

"Pokea chako kibomu,
Mkuu ninakutumia,
Hata ukinilaumu,
Siri zenu twazijua.

Kazi zao ufisadi
Jeuri ngebe na nongwa,
Baraka ya ukaidi,
Ukali ka’ embe gwagwa"
Mshenzi huyu hajali wala hasalimii anaendelea.

"Dalaliiii alijigamba
Kuwa morale i juu,
Sasa panga amelambwa,
Kakimbilia majuu"

Mara Kijiwe hakina hamu kwa umahiri wake wa kushusha mistari!

Makengeza anaamua kumkatisha kwa kumpa kipisi cha sigara ndipo anatuguna mic. "Wazee tusichukulie suala hili kijuujuu. Kwanza tujiulize kama kutengua au kufukuzwa kwa Dalaliii ndiyo jibu au ni kukwepa matatizo na kusogeza muda."


Kabla hajaendelea, Kapende anachomekea. "Huu ni ujanja hata kama wanakijiwe wameukwaa mkenge kiasi cha kumpongeza mkuu wa kijiwe ilhali naye na Dalaliii lao moja. Kwanini alichelewa na kuacha mambo yaharibike ndipo achukue hatua uchwara za kimazingaombwe?”

Akiwa anajiandaa kuendelea kutoa mapwenti, mara Mbwa Mwitu kamtimulia moshi sikioni kiasi cha kulikoroga.

"Jamani tulishasema hizi bange zitakuja kuwaweka pabaya. Inaonekana moshi wa bange zenu umeathiri wanakijiwe wote. Vinginevyo wasingekubali dhihaka na matusi haya. Ajabu wamehanikiza kama vyura kumpongeza!"

Mkurupukaji hangoji aendelee kutanua. Naye ana usongo. "Nyie mnajidanganya na hizi sanaa! Kwanza hata hao wakaguzi hawajagusa lolote zaidi ya kuja na dili ya kumtafutia Mkuu upenyo wa kujificha na kuwaficha wenzake. Hii Kaya bwana ni ya wajanja na walaji watupu kuanzia juu hadi chini."

Mzee Maneno hangoji. Anatia timu kavu kavu. "Kijana wajanja na walaji ni ndugu zako. Acheni kutukana watu mwajidai mna uchungu na kaya. Kama mnao mbona tunaishia kusema sema vijiweni bila kufanya kweli?"

Mkurupukaji hakubali kushindwa. Anaamua kumjibu mzee Maneno. "Mzee hata ukane na kuchukia, kaya yetu ni ya wajanja na walaji. Kama siyo basi sasa hivi tulianzishe uone kama hutakuwa wa kwanza kuufyata."

Mzee Maneno naye hakubali kushindwa. "Kulianzisha si tatizo hata ukitaka tuanze sasa hivi. Tatizo ni baadhi ya wenzetu kutusaliti. Chukulia mfano wazee wa virungu. Wao huamrishwa kama mbwa na kushambulia wasijue wanaowashambulia ni wenzao wanaoteseka kama wao!"

Baada ya kuona mjadala unaanza kupoteza mwelekeo, Msomi Mkatatamaa anaamua kuokoa jahazi.

Kutokana na mapwenti na kisomo chake, wahusika kuona anaanza kutia timu, wanaufyata.

Anasema. "Wazee hamna haja ya kutiana madole wala kutoana macho. Tukubaliane; wanakaya wana sehemu kubwa ya lawama kwa ukondoo wao. Hayo tuyaache."

Anakohoa na kuendelea. "Nitaongelea hili la usanii wa kijiwe chetu. Je, mbona ame-concentrate kwenye bilioni 133 ilhali zilizoporwa ni ziadi ya hizo? Mbona majina ya vigogo na makampuni yao hayatajwi badala yake tunatajiwa vikampuni vya misheni town?

“Mbona Chama Cha Namba One kilichonufaika na chumo hili la wizi hakitajwi au ni ule usanii wa wanufaika kuwatimua waliowanufaisha? Kufukuza Dalaliii siyo suluhu iwapo watoto wa vigogo wanaendelea kuiba." Anainua kombe lake la kahawa na kulipiga busu na kuendelea.

"Ukitaka kujua zimeibiwa ngapi jumlisha zote zilizotolewa kwenye takrima, zilizojenga mahekalu na zilizotoroshewa India na kwingineko ndiyo utajua Bongo inaibiwa kiasi gani.

“Zilizoibiwa ni zaidi ya upuuzi huu wa bilioni 133. Kwani siri? Ajabu wanakijiwe wanashikilia kumpongeza Mkuu bila kuangalia athari za kiuchumi na kijamii kutokana na ufisadi huu wa kitaasisi na kimfumo.

“Dokta Silaha aliturahisishia kazi kuwataja wahusika. Ametaja list of shame. Ametaja Deep Green Finance. Ametaja wahusika ambao bado wanazidi kutesa. Kwanza niwaulize. Zile kesi tulizosikia zingefunguliwa dhidi yake zimefia wapi? Je, huu siyo ushahidi kuwa wahusika ni mafisadi hata kama ni waheshimiwa?"

Akiwa anajiandaa kuendelea, Mzee Ndomo anauliza swali. "Msomi unataka kusema pesa iliyoibiwa ni kubwa kuliko tunayoambiwa, na wahusika ni zaidi ya hawa?"

Msomi anajibu. "Naam mzee wangu. Hebu jiulize takrima zilizotembezwa mwaka 2005 zilitoka wapi kama siyo huko? Je, tatizo la uchumi wetu ni Benki Kuu tu? Mbona wale wanaojulikana kusaini mikataba ya mabomu katika uwekezaji hawafanyiwi kama Dalaliii?

“Je, Dalaliii alikuwa peke yake? Mbona mwanzoni tuliambiwa wapingaji ni waongo na wasemayo ni uongo? Je, hapa muongo, tena mkubwa ni nani? Je, tutaendelea kuwaamini waongo hata kama ni wakubwa?

“Naona suluhu siyo kutengua bali kufukuza, kukamata, kutaifisha na kushitaki. Na siyo Dalaliii tu, bali wote wanaojulikana wakijijua kuwa ni mafisadi wakubwa hata kama ndiyo wanaojifanya askari wa kuwakamata mafisadi."

Mara mate yanampalia, anapiga chafya. Mara Mbwa Mwitu anachomekea kiutani. "Angalia mzee wasikukolimbe na kukumwagia tindikali. Maana kwa Bagamoyo si unawajua?"

Msomi ameishakuwa gado anaendelea. "Hapa hakuna cha Bagamoyo bali wanakijiwe kuondokana na ukondoo. Tutaendelea kuwa ngazi za mbweha na mafisi kupandia ilhali tunaumia?

“Kinachofanyika ni kudhalilishwa tena na wale tuliowapa dhamana zao. Suluhu si kukuna kipele bali kutumbua jipu. Je, Mkuu hakushiriki? Mbona nyumbani kwake wamejaa mapapa na manyangumi tu? Hata wasaidizi wake wote si safi hata kama ni marafiki zake.

“Hebu angalia Richmond, Buzwagi, AIPITIELO, mbona kila kitu hadharani? Mkuu asitutie madole machoni naye hafai ndiyo maana Babu wa Kuchonga alimkataa.

“Kwanza amrejeshe Dalaliii tumsulubu au anaogopa asitoboe siri na mzee mzima akaumbuka?"

Kijiwe kikiwa ndiyo kimenoga mara alikatiza kibaka aliyekuwa anafukuzwa na watu wenye hasira na umasikini, tukajiunga nao kumtia adabu kibaka huyooo.





Source: Tanzania Daima Jan, 16, 2008

Kenyans must save Kenya.

On 9 January, the media reported that some retired African presidents were congregating in Kenya to try "straightening things up." Heavyweights like Kenneth Kaunda, Festus Mogae and Joachim Chissano gathered in Kenya aiming at arresting the situation. These three have good records: thus a force to reckon with. But again, who thinks an African ruler with a dictatorial constitution under his disposal like Kibaki will listen to such former presidents despite their noble records?



Another tainted former president Benjamin Mkapa of Tanzania (awkward and untrustworthy by all standards) minus Bakili Muluzi (Malawi), also weighed in! Mkapa, like Muluzi, Chiluba and Moi, arrogantly supported or dubiously ran all-time-corrupt and undemocratic forces-cum regimes in his country when he was in power. Mkapa faces charges of being one of the corrupt rulers in Africa. He owns illegal conduits such as ANBEN, Fosnik and Tanpower outfits which acquired some lucrative projects in Tanzania. His Chama Cha Mapinduzi (CCM) is renowned for rigging and being undemocratic altogether. Muluzi, on the other hand, attempted and failed what Kibaki successfully did by rigging. I don’t know why Rwandan Pasteur Bizimungu was excluded. Is it just because the dictator in Rwanda does not like it?



Bringing back calm and normalcy in Kenya is noble and desired. But who has such moral authority to do the same? Jakaya Kikwete of Tanzania and Mkapa should not be accepted in whatever talks on Kenya. Their governments and parties have a known philosophy. Mere pieces of paper (ballots) can not take away power from their grip. So is their murky image. Dictators like Yoweri Museveni and Paul Kagame are products of foul play. Will these doyens really hold water as far as the volatile situation in Kenya is concerned? Can Kenyans really trust such emissaries?



What did they achieve in Zimbabwe? What did they do when Fredrick Chiluba (Zambia) and Bakili Muluzi (Malawi) respectively attempted this sin? What did regional rulers do when Yoweri Museveni tampered with the constitution and ultimately rigged election and got away with it? Don’t forget Paul Kagame who heinously overthrew and degraded Bizimungu.



African rulers share one nexus: they sympathize with those with powers and vindicate those without. African politics is about hypocrisy and time wasting. Thus Kenyans should never be deceived by these fire-extinguishing or coke like efforts. In the end, the winner takes it all.



Africans under the yolk of bovine politics need to borrow a leaf from countries like Iran, South Africa, and Romania. Changes in those countries were not enhanced by international efforts but those of the citizenry themselves.



If regional rulers are all rotten, should we turn to the international community? As fate may have it, chances of putting the genie back to the bottle this way are also slim.



Like Dictator Pervez Musharraf in Pakistan, Kibaki knows too well how the police of the world --the US that is currently white washing-- is unable to nibble him. You know what? Kibaki knows what Al-Qaeda threat in Somalia means and poses to the US. He thus knows: the US needs his services; and he’s already offered much. To know what this means refer to the dictator of Ethiopia Meles Zenawi. He can kill and torture his opponents without any worry given that Delilah is in bed with the Samson of the world.



As for the UN and AU, forget. What can toothless dogs do? So who is to solve this puzzle? Kenyans and only Kenyans can. Go back to the drawing board: and give the heck to Kibaki’s illegal regime. Stick on people power: boycott and demonstrate against it. This will suffocate it as it breaks its backbone. Ultimately Kibaki will succumb let go the presidency. Otherwise all this hocus pocus and flibbertigibbets by rulers, be they African or otherwise, is but buying time so as to let the people goof and forget. Importantly Kenyans must learn from Zimbabwe.


By Nkwazi Mhango
Mhango is a Tanzanian living in Canada. He is a Journalist, Teacher, Human Rights activist and member of the Writers' Alliance of New Foundland and Labrador (WANL)


Source: The African Executive no. 143

Saturday 12 January 2008

Hapa kuna nchi kweli au mabaki?

Attention please!

Belly of Tembo. Kama uchafu wenyewe unanuka kiasi hiki, jamani, nani amkamate nani? Hapa ni BoT. Je NIC,Harbours, Immigration, TRA na kila penye ulaji wapo wapi, wangapi na wenye sura zipi? Kweli Tanzania au Danganyika siyo ya wadanganyika bali genge lijiitalo Watuwala.

1. Pamella Lowassa, Mtoto wa waziri mkuu wa sasa kinara wa kikundi cha Mafia kinachoiuza Tanzania mwili na roho.
2. Filbert Frederick Sumaye, Mtoto wa waziri mkuu wa zamani aliyesifika kwa kupenda mali na kujilimbikizia na bingwa wa kuboronga.
3. Zalia Kawawa, Mtoto wa waziri mkuu wa zamani.
4. Harieth Lumbanga,Mtoto wa Katibu wa ofisi ya rais wa zamani.
5. Salama Ally Mwinyi,Mtoto wa rais wa zamani!
6. Rachael Muganda, Mtoto wa hawara wa gavana wa benki kuu wa zamani.
7. Sylvia Omari Mahita,Mtoto wa mkuu wa polisi wa zamani!
8. Justina James Mungai, Mtoto wa waziri mzee wa zamani.
9. Kenneth John Nchimbi, Mtoto wa mzito wa CCM wa zamani.
10. Blassia Blassius William Mkapa, Mtoto wa ndugu wa rais wa zamani!!
11. Violeth Phillemon Luhanjo,Mtoto wa katibu mkuu ofisi ya rais wa sasa!
12. Liku Irene Katte Kamba, Mtoto wa naibu spika wa sasa na waziri wa zamani.
13. Thomas Mongella, Mtoto wa waziri wa zamani
14. Jabir Abdallah Kigoda..................... Mtoto wa waziri wa zamani kinara wa kuibamiza nchi mkenge kwenye uwekezaji na ujambazi!

KUMBE TULIIBIWA ZAMANI TENA ZAMANI SANA KWA MBINU NA HILA ZA KIZAMANI NA GENGE LA WEZI LA ZAMANI? wezi waliisharithishana zamani gani!

Friday 11 January 2008

Nenda Balali. Bado Kikwete na genge lake.

Ingawa hatimaye, rais Jakaya Kikwete amekumbuka blanketi asubuhi baada ya kutosikia la mkuu, kumfukuza kazi gavana wa zamani wa Benki Kuu, Daudi Balali na kumteua Profesa Benno Ndulu, hakuwezi kupita bila kujadiliwa.

Kwanza je ni kweli Balali amefukuzwa kazi au ni dili? Je aliyemrithi ni safi? Mbona anaonekana kuwa na sifa kama za Balali? Maana kama Balali naye anatokea huko huko Washington kunakopikwa kila upuuzi unaoutuumiza.

Je atakuwa na jipya zaidi ya kuzidi kuvuruga ushahidi muhimu ambao haujafikiwa na wakaguzi? Je mfumo uliomtengeneza na kumneemesha Balali na wenzake umerekebishwa?

Je matokeo ya "kazi’ ya Balali kwa uchumi na sarafu yetu ni yapi? Maana tumekuwa tukipewa takwimu chafu na za kubuni toka kwa akina Balali ili kulinda uchafu wao.

Je mbali na Balali na kundi lake, wanufaika wa uchafu huu wengine ni wapi? Je kama kwa kuthibitika kuwa madai ya wapinzani ni ya kweli, rais haoni kuwa naye anahusika hasa ikizingatiwa kuwa alitajwa kwenye list of shame? Je watanzania kwa mara nyingine watakubaliana na usanii huu? Je wanajua kinachofanyika na kuwapaka mafuta kwa mgongo wa chupa? Maana tatizo letu siyo BoT na Balali bali serikali nzima na taasisi zake zote na karibu watendaji wake wote kuanzia Kikwete mwenyewe.


Kimsingi Kikwete alipaswa kufanya yafuatayo haraka na kwa uwazi kama ana nia ya kulisaidia taifa analoongoza kuelekea kwenye maangamizi:


Angepaswa ajiuzulu na serikali yake. Lakini kwa vile kitu kama hiki kwenye nchi zenye demokrasia maneno kama Tanzania hakiwezekani basi angalau rais angefanya yafuatayo:

Kwanza awaombe msamaha wananchi kwa kichwa ngumu yake na kuchelewa kuchukua hatua huku akipuuzia na kuwadharau waliompa ushauri huu.

Pili aiombe msamaha kambi ya upinzani iliyoibua uoza huu. Na si kuomba msamaha tu bali afanyie kazi mapendekezo yake.

Kwa mfano ahakikishe Balali na wote waliohusika wanakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria ili sheria ichukue mkondo wake tena bila kuingiliwa na serikali kwa namna yoyote.

Pili akamate mali zao wakati kesi zao zikiendelea. Maana wanajulikana hivyo na mali zao zinajulikana.

Tatu awawajibishe wote waliohusika na uchafu huu mara moja bila kuangalia sura au ukaribu wa mtu kwake au wakubwa wenzake.

Wednesday 9 January 2008

Msimamo wa Kijiwe kuhusu Mwali Kibaka

BAADA ya kumtwanga salamu za onyo Mkuu wa Kijiwe kwenye ujio wa Mwaka Mpya, tumeonelea tutoea salamu kama hizo kwa mwenzao mzee aliyetia aibu ya mwaka, Emilio Stanley Githinji Mwai Kibaki.

Tukiwa tunashuhudia utitiri wa maponjoro wanaokimbia Kenya , ilibidi tuitishe kikao cha haraka ili kuelezea msimamo wa Kijiwe.

Kwanza tunalaani ujambazi wa kujifanya wananchi yakitokea machafuko unaikimbia nchi! Ni mpuuzi gani awezaye kuikimbia nyumba yake ikishika moto badala ya kuuzima!

Machungi ndiye analianzisha. "Ami yae yaiyowatokea kue Pemba sasa yako Kenya. Kwei Afiika imelaaniwa kuwa na watawaa michosho kama Mwali Kibaka wa Kenya! Tazama mzee mzima anavyojitia aibu na kuitia nchi yake matatani kwa sababu ya uchoyo utadhani ni mwanachama wa nambai wani!"

Kabla ya kuendelea Mpemba anadakia. "Yakhe usinkumbushe Wallahi. Kumbe wanasiasa wote mzazi wao mmoja! Nani alitarajia shehe kama Kibaki kufanya utwahuti namna hii Yarabi? Ajabu ya maajabu eti Mkuu wa Kijiwe aihadaa dunia enda suluhisha wakati ya Pemba yanshinda!"

"Nyie mnaongelea utumbo wa Kibaka Mwai, mbona hamuongelei la Maponjoro kukimbia nchi ilhali wao ndiyo wanaofaidi uchumi wa nchi ile? Namanga, Arusha,Tanga hata Musoma wamejazana wakingoja hali itulie wende kuchuma! Kweli Afrika imelaaniwa kama alivyosema Mgosi pale!" Anachomekea Makengeza.

Kapende anaongezea msumari. "Afrika hatuna viongozi bali manyang'au wanaotuchuuza kwa unafiki, uroho, roho mbaya na urongo. Nakumbuka Kibaka alivyotoa mpya aliposema kwenye hotuba ya kubariki ujambazi wake. Acha niseme tena kwa herufi kubwa; Kibaka toka ukacheze na wajukuu". Anawageukia Mbwa na Mzee Maneno waliokuwa wakinong'ona.

Anaendelea. "Acheni hizo. Hamkusikia akiwadhihaki wakenya: eti nipo hapa kwa utiifu kuwashukuru kunichagua tena! Nani alimchagua zaidi ya tume ya uchafuzi? Na la Msanii wetu nalo kinyaa. Mara utasikia maafriti kama M7 na Kagame nao wakija na zao. Ama kweli kwa unafiki Afrika inaongoza!"

Mkurupukaji anakurupuka. "We unashangaa utiifu! Mbona hushangai aliposema anaipenda Kenya na yuko tayari kuitumikia kwa moyo mmoja utadhani hata kuua watu ndiyo mapenzi! Wezi wetu wako hivyo. Wanajidai wanatupenda wakati wanapenda mafisadi na wizi wao wa kura na pesa ya umma".

Mbwa Mwitu anakurupuka na kuchomekea. "Unashangaa kusema utiifu! Mbona alisema tena "mapenzi ya hali ya juu"! Wenzenu wanajua jinsi ya kuwaingiza mjini majuha kwa kuwapaka mafuta kwa mgongo wa chupa! Kama anawadanganya nanyi mnaupwakia urongo kwanini asiwatie madole?"

Mzee Maneno anaamua kupiga ngumi kubwa zaidi. "Jamaa wanatupenda kweli. Nyie hamjui. Damu na jasho letu ni vitamu kweli kweli. Hata biashara ya kutuuza kwa wawekezaji na walaji wengine inawalipa vilivyo. Nani aliwahi kumwambia ng'ombe au kuku wake anamchukia? Tunapendwa ila ni kwa faida yao hasara yetu uhai wao msiba wetu"

"Usemayo ni kweli tupu". Anadandia Mzee Ndomo. "Huoni mapenzi ya Mkuu kutumia njuluku ya Makapuku kujirusha na malkia wake Majuu! Ama kweli wamejua kutupenda wadudu hawa! Kumbe hata funza huupenda mzoga hadi akauozesha! Kweli mapenzi ya wadudu!"

Mgosi anakatua mic tena. "Tiambizane ukwei. Kama haya ni mapenzi basi ni ya changudoa ya kuambukizana miwaya! Au ndiyo ushanii tinaobambikwa kia siku?"

Msomi alikuwa amejiinamia utadhani yu alala kumbe alikuwa ndiyo akisikiliza kwa majonzi makubwa.

Alianza. "Afrika ilie sana. Lia sana mama Afrika. Huu ndiyo wimbo pekee unaoweza kukufaa. Nani alijua kuwa wale tuliowaingiza kwa mbeleko ya demokrasia wangegeuka kuwa madikteta wa kutupwa? Kibaki si wa kwanza wala wa mwisho.

Anakatua andazi lake na kutamia tangawizi na kuendelea.

"Mmesahau upuuzi aliojaribu Bakili Muluzi na Frederick Chiluba. Heri yao walishindwa. Huyu Kibaka sijui Kibaki katia fora! Kwanza jitu lenyewe limeisha expire achia mbali kufaa"

Kabla ya kuendelea kumsiliba Kibaka, Makengeza anachomekea. "Asha-ekispaya au ameishakufa! Mijitu mingine bwana, inataka ifie madarakani ili midhambi yake isijulikane. Hata Tunituni angejua yangemfika yaliyomfika hata kama Chekacheka kamkingia kifua si haba angefanya mambo"

Kabla ya kuendelea Mbwa Mwitu anaingilia. "Kwani hakufanya kweli kwa kula dili na jamaa yake na alivyorahisisha ujambazi pale BoT?"

"Jamani acheni Msomi atambae" Anashauri Kapende akiwa anamtolea macho Mbwa Mwitu.

Msomi akiwa anatabasamu kwa kutetewa anaendelea kumwaga sumu.

"Kibaka is a rigger not a winner" Kabla ya kuendelea anagundua kosa lake anarekebisha lugha. "Huyu si mshindi bali mwizi wa kura wa kawaida sawa na kule kwa akina yakhe." Anamgeukia Mpemba ambaye naye anatingisha kichwa kumuunga mkono huku akitabasamu.

Anaendelea. " Hata hivyo Kibaka anaonekana ni mchovu kifikira. Kipigo kilichopata chama chake cha Panua Kibaka apite (PANU) kilimtosha kutia akilini.

Kinachomsaidia hana mpango wala sera ya kutawalia vinginevyo kwa kutokuwa na wingi wa wabunge kungemgharimu. Lakini kwa vile wingi wa wabunge mara nyingi kwa serikali za kijambazi ni chanzo cha ruzuku na kupitishia uchafu wake, Kibaka anaweza kuiba na kuacha wabunge wagomee kila upuuzi au awahonge na kuhamia kwenye genge lake la PANU."

Anainua kombe lake na kukwapua tama mbili tatu na kuendelea. "Nikija kwa hili la mkuu wetu wa kaya kuombwa afanye mazungumzo, sina la kusema zaidi ya kulaani unafiki huu.

Unawezaje kuona punje kwenye jicho la mwenzio wakati lako limejaa tumbawe? Lakini jamaa hajakosea.

Kama umaarufu umeshuka Kijiweni kwanini asiusake nje ya Kijiwe? Isitoshe anaweza kuambulia safari na njuruku za per diem na siku zikaenda.

Kama wakenya watakuwa wakweli kwa nafsi zao, hawahitaji msaada wowote toka Kijiwe chetu.

Kwa kilichotokea Kenya wale mbweha wetu wa genge la Chagua Chizi Mkome au CCM (si Chama Cha Mapinduzi), wanashangilia kilichotokea.

Kwani katika uchafuzi ujao watapa mbinu ya kufanyia uchafu wao. Kilichotokea wataalamu wa makufuru hukiita wanachukua, wanaweka waaa! Au unamlamba mtu goli la kisigino. Hii ndiyo lugha ya kijambazi inayotumiwa na majambazi kama Kibaka kuhalalisha uchafu na ujambazi wao. Kwani hamjui!"

Akiwa anajiandaa kumwaga lazi, mara tulisikia kuwa Kibaka amepata shinikizo la roho kutokana na uzee na kuzidi kubanwa. Hivyo tulitawanyika haraka kwenda kusikiliza radio zetu na wenye kwenda internet, walikwenda.


Source: Tanzania Daima Januari 9, 2008

Suluhu Kenya: Ni ama Kibaki ang'oke au uchaguzi mpya

NANI alijua: mzee msomi na mtu aliyepigiwa upatu kuwa mwanamageuzi na mvumilivu kama rais-tata Mwai Kibaki wa Kenya angefanya madudu kama tuliyoshuhudia nchini humo?

Nani alishuku: nchi iliyoitwa jiko la uchumi katika Afrika Mashariki ingetumbukizwa kwenye maanguko ya kiuchumi kirahisi hivi? Yametokea na tumeyashuhudia.

Genge la manyang'au na mipapa ya kiuchumi imo vitani huku mwananchi wa kawaida asiye na hatia akipoteza hata uhai na mstakabali wake kisa alitimiza haki yake kwa nchi yake!

Mchukulie Kibaki utakavvyo. Ukweli unabaki pale pale: amegeuka aibu na machukizo kwa nchi na bara zima la Afrika. Kama akili ya kawaida haitapewa nafasi, yaliyotokea Kenya yamemvua nguo Kibaki na genge lake wapambe wasasi ngawira wanaoona damu ya binadamu kama kamasi hata imwagike sawa ilmradi lao litimie!

Kilichotokea ni machukizo kwa misingi na maana yote ya demokrasia na ubinadamu. Hizi ndizo wataalamu wanazoziita siasa za king'ombe-bovine politics.

Kwa upande mmoja tunaye king'ang'anizi Kibaki na genge lake wakitaka kuihadaa dunia kuwa alichaguliwa wakati alitangazwa na Samuel Kivuitu kwa hila na ghilba za kisiasa! Kenya inabakwa na kunajisiwa na genge hili lisilosikia la muadhini wala mchota maji! Kwao hata damu zikimwagika sawa!

Kwa upande wa pili tunaye Raila Amolo Odinga anayechukuliwa kama mshindi. Huyu anaonekana kuwa na hoja kiasi cha kuwashawishi wakenya kumchagua hata kuwa tayari kumfia.

Japo uhasama baina ya mafahali wawili umefunika hata maslahi ya kitaifa, ukweli unabaki kuwa wananchi walitaka mageuzi baada ya Kibaki, mzee, mgonjwa na asiye na jipya kuwachosha.

Ajabu huyu anayeng'ang'ania aliingia kwa njia hiyo hiyo anayoiharamisha alipomshinda mgombea wa Kanu Uhuru Kenyatta! Kibaki kwa afya na umri wake hafai kuongoza nchi kwenye karne ya 21 yenye kila aina ya mikiki inayotaka nguvu na akili.

Isingekuwa roho mbaya, uroho, upofu na ukosefu wa visheni, Kibaki hakuwa na haki wala sababu ya kung'ang'ania madaraka wala kuridhia umwagaji damu kama tulivyoshuhudia.

Huwezi kujua yaliyoko nyuma ya pazia. Huenda anataka afie madarakani ili afe na siri za uchafu wake utokanao na ufisadi. Na huu umekuwa ndiyo mchezo wa watawala wetu vidhabi Afrika.

Kinachokera zaidi ni kwa mtu yule yule aliyeamuru mbwa na polisi kuwaua na kuwatesa wananchi anayedai anataka maridhiano na umoja wa kitaifa! Umoja upi iwapo ushaupiga mapanga kwa tamaa zako?

Nani amesahau kejeli, kefule na machukizo ya Kibaki aliposimama eti kuwashukuru Wakenya kwa kumchagua kwa mara ya pili utadhani walimchagua wakati alipitishwa kiwizi na tume yake ya uchaguzi? Maridhiano na umoja wa kitaifa ni kwa Kibaki kuondoka na kwenda kucheza na wajukuu zake kule Othaya.

Hapa ndipo wanasiasa wanapotenda kama machangudoa wakiwa mabingwa wa kusema lolote wasitende chochote!

Huapa kwa jina la Mungu kuwatumikia watu ilhali moyoni wana lao kuwatumia watu kujineemesha wao na wapambe wao, walamba viatu hata mbwa wao! anayebishia hili ajiulize Afrika tuko wapi na katika hali gani?

Acha ukweli usemwe: inahitaji roho ya mwendawazimu kuwahadaa wananchi kuwa unawapenda wakati ukweli wewe ndiyo chanzo cha mateso na vifo vyao kama ilivyotokea kwa Kenya na Kibaki wake. Kibaki ondoka. Ndivyo wasemavyo wakenya tena kwa umoja na sauti kuu.

Inatisha mtu kuwa tayari kufia madaraka kwa njia ya kuwaua wengine kufikia lengo hili chafu!

Inahitaji ulimi wa nyoka aliyemdanganya Eva kuwaambia wananchi nawapenda achia mbali kuwashawishi wakati ukweli unachopenda ni madaraka na marupurupu yake ya kiwizi!

Utawapendaje iwapo unachopenda ni Ikulu ili uibe na wenzio wasasi wa ngawira? Utawapendaje ilhali wewe ni Mungu mtu tena mwenye tamaa kama za Nebkadnezza?

Hakika inahitajika uwe chongo kuona mstakabali wa taifa linaloelekea kwenye mauaji ya mbari kama ilivyo nchini Kenya. Mwenye kusema na kuona haya lazima awe na sifa moja. Nayo ni kama inzi - kukosa aibu!

Huwezi kujizungushia wasasi ngawira na madikteta na mafisadi wenzako wengine hata kama ni wakuu wa mataifa ya kigeni kudai maridhiano wakati huridhiki wala kuheshimu maamuzi ya umma.

Ajabu mpangaji huyu king'ang'anizi wa Ikulu anawaita wenzake eti wajadiliane kubariki jinai yake! Nao kwa unafiki wao wanaitika! Wataachaje ilhali wote ni wale wale?

Kinachostua zaidi na kutia mashaka ni ukweli kuwa nyuma ya "zoezi la kuleta suluhu na maridhiano" wapo watu wenye kutia kila aina ya mashaka.

Tanzania kama jirani yake tunataka kuingia kutafuta suluhu nchini Kenya . Inatia shaka kama tutaweza iwapo hali kama hiyo ndani ya nyumba yetu umetushinda!

Rejea mauaji yanayodaiwa kutokana na wizi wa kura kule Zanzibar vilivyozaa kinachoitwa mtafaruku uliotushinda kwa miongo sasa.

Ajabu na madikteta kama Yoweri Museveni, Paul Kagame nao wanahanikiza wasuluhishe wakati wao ndiyo wanahitaji kusuluhishwa na wananchi wao waliowaua na kuwadhulumu!

Ila ijulikane katika usanii huu, wanaoumia ni wapiga kura na walipa kodi wa Kenya. Je, Wakenya watakubali kugeuzwa wajinga na damu yao kumwagika bure huku kura zao zikiishia kuwa upuuzi?

Japo tunahitaji amani na utangamano Kenya lakini siyo kwa njia ya usanii kama unavyoanza kufanywa na mabingwa wa sanaa katika eneo hili.

Suluhu kwa Kenya ni Kibaki kusikia sauti ya umma na kuachia madaraka anayoyamiliki kwa wizi uliosababisha madhira makubwa kwa nchi na watu wake.

Hakuna suluhu nyingine ya kudumu zaidi ya hii. Ama aachie ngazi au arudie uchaguzi ulio huru na haki vinginevyo kinachoendelea ni matusi kwa wakenya na demokrasia kwa ujumla. Wale wote wanaoipenda Kenya na Kibaki wamwambie Kibaki ukweli: Kibaki ondoka. Ni hilo tu.

Acha Kibaki aondoke utangamano na amani viingie. Kwa nini taifa liangamie eti kwa sababu wachumia tumbo wachache wanataka kulinda maslahi yao ya jinai?

Kama hatutakwepa ukweli Kibaki kama ataendelea na njama zake na ung'ang'anizi wake ataipasua Kenya kiasi cha kuiingiza kwenye machafuko ya kudumu.

Hapa ni busara inayohitajika siyo kingine. Tuweke utani kando. Kinachoendelea Kenya kinanikumbusha machozi ya mamba ya mchawi amliliaye kichanga aliyemuua mwenyewe. Kibaki ni sehemu ya tatizo hawezi kuwa au kuleta suluhu akiwa bado ni Rais wa Kenya kwa urais alioupata kimizengwe.

Umefika wakati muafaka kwa Kibaki kuondoka hata wale wanaofanana naye. Afrika imechoka. Kibaki 'has to go and he must go now'. 'Kibaki go!'


Source: Tanzania Daima Januari 9,2008

Monday 7 January 2008

Kuwauwa waandishi si jibu bali balaa kwa taifa.

Vyombo vya habari vimeripoti kumwangiwa tindikali na kukatwa mapanga waandishi Saed Kubenea na Ndimara Tegambwage. Kuna kundi la manyang’au na gwagu wanawatishia maisha waandishi wote wasioridhika na ufisadi nchini mwetu. Wanataka tunyamaze ili waendelee na uchafu wao. Mtaweza kuwadhuru hao waliomo nchini. Je sisi tulio nje mtafanyaje?

Hakika wapuuzi hawa wanapoteza muda. Wanaweza kuwanyamazisha waandishi hata kuwaua. Watafanikiwa kuua mwili lakini siyo roho wala kile tunachosimamia. Edward Modlane, Steve Biko, Ernesto Che Guevarra, Mtwa Mkwawa na wengine wengi waliuawa. Lakini kile walichosimamia na kupigania hakikufa. Msumbiji, Afrika Kusini, Bolivia,Tanzania na nchi nyingine ziko huru.

Inatia kinyaa kuwa zamani mashujaa wetu waliuawa wakidai uhuru na haki ambavyo sasa vinahujumiwa na ndugu zetu wenyewe huku wakitutishia maisha! Hawa ni wabaya kuliko hata wakoloni. Maana hatukuwa nao nasaba. Serikali na CCM inabidi zilaani na kujitenga na kundi hili. Yenyewe ndiyo mtuhumiwa mkuu wa ufisadi. Maana kama ni ugomvi wa wandishi hata wananchi ni dhidi ya yeyote awe mtu binafsi,chama au kikundi cha watu anayewahujumu.

Je CCM kwa kuendelea kukaa kimya haioni kuwa inajitia kitanzi na sifa mbaya kuwa sasa imeishiwa kiasi cha kugeuka dude linalotaka kuangamiza watu wake kwa sababu ya kulikumbusha kutenda haki na kuachana na unyangau? Je hawa wanaotishia watu maisha wamekodiwa na CCM? Je hawa ni aina nyingine ya waharifu walioamua kujiajiri kwenye kutenda na kulinda jinai?

Waueni waandishi hata kuwafunga hata kuwalazimisha wakimbie nchi. Lakini mtaua wangapi? Je hilo ndiyo jibu na suluhu wanavyotaka wananchi? Je ni njia muafaka na ya kistaarabu. Umma inabidi uiambie serikali na watuhumiwa kuwa kama waandishi hata wanasiasa wanaopinga dhuluma ya serikali watauawa nao wajiandae kulipia. Maana wabaya wa waandishi wanajulikana. Ni wale wote wanaotuhumiwa kulihujumu taifa kwa kupokea rushwa, kujilimbikizia mali, kupeana vyeo kwa rushwa na kujuana, kusaini mikataba feki na upuuzi mwingine kama huo. Hakuna mtuhumiwa mwingine katika hili.

Yaani nchi yetu imekuwa ya hovyo kiasi cha kuanza kuuana kwa sababu za kulinda uoza na jinai? Hiki ndicho walichofia akina Mkwawa, Mirambo na wengine? Hiki ndicho walichopigania akina mwalimu Nyerere? Hakika hii ni aibu kwa taifa.

Leo madai ya watanzania yako wazi. Hata kunguru wanajua kuwa watanzania wanataka haki yao siyo kuiomba wala kutishwa ili manyang’au wachache na familia zao waendelee kuneemeka migongoni mwao.

Vijana wameishatoa tangazo wazi. Kinachopingwa ni zaidi ya kile anachosema wapinzani. waandishi wajumbe na watoa habari tu. Akina Kubenea wako wengi hata kama hawajitokezi kwenye majukwaa au bungeni na magazetini. Wapo mashuleni,viwandani, majeshini, mashuleni, vyuoni safarini, misikitini,makanisani,mitaani kote wamejaa.

Wanaona watu wanavyoingia siasa wakiwa maskini na kuibuka matajiri wa kupindukia huku umma ukitopea kwenye ufukara. Wanaona na wanajua. Huu ni ukweli usiopingika. Kupingana nao ni kupoteza muda na nguvu. Anajua zinapotoka "Neema" za ghafla na waneemeka wanawajua hata kwa sura na majina hata wanakoishi na wanachofanya.


Wamekuwapo muda mrefu ila wakati wa kusema ulikuwa bado. Hata akina Mpayukaji, Ansbert Ngurumo, Freddy Macha na wengine wako wengi hata kama hawaandiki kwenye magazeti wala kutangaza kwenye matelevisheni.

kwa lugha nyepesi ni kwamba vijana wamestuka wanaulizia kazi 500,000 walizoahidiwa kwenye uchaguzi siyo vibarua. Hakuna aliyewalazimisha kuahidi.

Wanapinga "wakubwa" kujilimbikizia mali na madaraka. Serikali lazima itoe ufafanuzi na mipango inayoingia akili juu ya kuwapatia vijana ajira na kupambana na wakimbizi wa kiuchumi waliojazana nchini mwetu.

Leo wanahoji kesho wanaweza kuchukua hatua.
Leo ni watazamaji. Kesho ni wachezaji.
Wanapinga uchoyo, roho mbaya, usanii, ufisadi,kujuana, ufisi, uchangudoa na ubinafsi vinavyooonekana wazi.

Wanapinga maneno matupu bila vitendo.Wameamua kuwakabili wahusika baada ya wazee kuwaangusha kwa kuridhika na mateso wanayopewa.
Wanatangaza azimio lililowazi kama maandalizi ya kujikomboa. Waandishi wanafikisha ujumbe kwa niaba ya wananchi. Wao ni sauti ya wasio na sauti-voice of voiceless. Mnawaonea bure na ukweli huwa na tabia kuu moja. Unaweza kuzimwa lakini hauuawi hata kidogo.

Kwa mtu anayejua vikundi vya mbwa koko walamba matapishi na wachokora majalala yawe ya jinai, kisiasa na ya uchafu walioivamia CCM, ni rahisi kuwabaini wanaomtishia waandishi maisha. Ni rahisi kujua wanalipwa na nani. Bahati nzuri mahabithi hawa ni woga. Si kosa lao bali ulafu, njaa na utapiamlo wa mawazo. Hawa maskini hawajui kesho wala vizazi vijavyo! Kama nyangumi, uhai wao ni matumboni mwao. Utawajua kwa kazi zao. Wamejazana magazetini wakiimba nyimbo za kuusifia ufisadi kwa vile unawalisha na kuwavisha. Hawana tofauti na vyangudoa wauzao miili yao. Heri hata ya vyangu huuza mwili siyo roho zao hata za mama zao.

Wapo wengi. Kuna wauaji. Waandishi wa habari nyemelezi wapendao kusifia uoza. Wapambe wa wakubwa na makuadi wao. Wafanyabiashara ambao Mungu wao ni pesa. Wako tayari hata kuwauza mama zao mradi wajaze matumbo. Wapo viongozi wa vyama vya kijamii wanaowasaliti watu wao. Wapo viongozi wa dini wanaoshindwa kukemea ufisadi kwa sababu nao ni mafisadi kwenye majoho yao. Wanalipa fadhila, serikali inajua wizi wao. Inawavumilia. Wanaivumilia. Lao moja.
Kuna haja ya kujiandaa kuwahami. Wanapambana nao bega kwa bega. Zamani tulikuwa tukiwacheka wakenya kwa kumalizana wao kwa wao ili kulinda ufisadi. Tuliwacheka walipouawa akina Tom Mboya, Josiah Mwangi Kariuki, Robert Auko na wengine wengi waliopinga ujambazi wa watawala.

Tuliwacheka sana. Leo na wao karibu wataanza kutuzomea watakapogundua unafiki wetu kufanya walichokuwa wakikifanya wakati wa kiza. Karne ya 21 ni ya maendeleo ya kisayansi na kisiasa kwa watu waliobahatika kuuona mwanga.

Wanaomtishia maisha Kubenea wanapata wapi jeuri? Wanadhani watanzania ni kondoo wa kushuhudia mwenzao akichinjwa? CCM na serikali yake sharti watueleze. Serikali sharti iwajibike. Ni jukumu la serikali kulinda watu na mali zao hata kama wanaipinga. Yasirudiwe ya Stan Katabaro aliyeuawa na mbweha waliouza Loliondo. Yasirudiwe ya Edward Sokoine aliyeuawa na walafi na wapendao kujilimbikizia mali ambao sasa wamebakia kuishi wa misaada ya kujikomba kwa wakubwa maana hawana bao tena.

Yasirudiwe ya Horace Kolimba aliyewapa ushauri nasaha kwa upumbavu wao wakamkolimba wakidhani watakolimba wote waliosikia alichosema. Wakati wa kushuhudia wenzetu wakiuawa na majambazi yawe ya kisiasa au kitumwa umepita.

Kwa kadri umma unavyowashangilia wapinzani kwa kufichua uchafu wa wale wanaotunafiki kuwa ni wasafi wakati wameoza iwe hivyo hivyo katika kulipiza kisasi kama mmoja wao atadhurika. Walatini walisema sauti ya wengi ni sauti ya Mungu (Vox populi vox Dei). Nani anaweza kushindana na Mungu? Wananchi tubadilike. Tusitegemee ukombozi toka kwa malaika bali sisi wenyewe. Wabaya wetu tunawajua. Tuwataarifu kuwa watakapoanza kutuua kwa risasi, mapanga, tindikali au sumu baada ya kushindwa kutumaliza kwa umaskini, ujinga, maradhi, dhuluma nasi tutajihami kwa kuwavamia popote walipo.

Wasijidanganye kuwa hatuwajui. Hawa malaika wa kifo- messangers and agents of death- wanajulikana kirahisi. Ni sawa na majambazi wa kawaida. Utawaona maisha yao yakibadilika baada ya kujiunga na kundi la wezi wetu. Kwa vile wanapenda sifa na kujikomba kwa mabwana wao, tuwaweke alama kwa kuambiana. Tusome makala zao na upuuzi wao halafu tuweke kumbukumbu. Siku likitokea la kutokea tuwatafute mmoja baada ya mwingine tuwalipizie kwa kadri walivyotenda. Huu ndiyo ukombozi.

Dhana ya amani itatoweka kama mbinu za porini zitatumika kutatua sakata zima la kashfa za ufisadi.

Kwa mtu anayejua watu wanaosingiziwa, atasema wazi kuwa wahusika kama hawalaani njama hizi hata waende wapi hawataonekana wasafi. Kwanini shutuma zao ziamshe wauaji? Je ni wao waliowakodisha?
nkwazigatsha@yahoo.com


Ifuatayo ni taarifa ya Reporters Sans Frontiers- Paris baada ya kutaarifiwa tukio hili na Nkwazi Nkuzi Mhango hapo tarehe 7 Januari, 2008

Machete and acid attack on two journalists inside their newspaper

Reporters Without Borders condemns an attack with machetes and acid on Saeed Kubenea, the publisher of the weekly Mwanahalisi, and Ndimara Tegambwage, its editor, by thugs who forced their way into the newspaper’s office in the Dar es Salaam suburb of Kinondoni on the evening of 5 January.

“This barbaric attack is especially disturbing in a country where it is not customary to use physical violence to try to silence journalists,” the press freedom organisation said. “We note that an investigation is under way and we urge the authorities to do everything possible to ensure that those responsible are identified and receive an appropriate punishment.”

Armed with machetes and acid, the assailants stormed into Mwanahalisi’s offices at around 9 p.m., ordered Kubenea and Tegambwage to lie down, gave them a severe beating, threw acid on them and dealt Tegambwage several machete blows to the head.

“They fell on us with iron bars,” Kubenea later said from a hospital bed. “They hit me about the head and threw a burning liquid in my face. My colleague, who tried to resist, was also beaten and sprayed before the assailants stole his mobile phone.” The two journalists were taken to Muhimbili National Hospital the next day.

It seems the attack was prepared with care as witness say they saw suspicious individuals hanging around outside the newspaper’s premises earlier in the evening. Kubenea said the attack was the culmination of a series of threats against him that began in mid-2007.

He said that his car was recently the target of an arson attack and that he often received telephone threats as a result of articles published in the newspaper. “I was warned that I would be killed if I did not stop meddling in people’s business,” he said.

Confirming that an investigation was under way, regional police chief Jamal Rwambow said he thought the attack was an attempt to silence journalists who had helped to uncover scandals.