The Chant of Savant

Wednesday 23 June 2010

Kabila Must Expose Chibeya's Assassins


June has been a very sad month for Human Rights activists. In this month, DRC’s champion of Human Rights Floribert Chibeya Bahizire (chair of Voix des Sans-Voix [Voice of the Voiceless]) was grisly felled. In June, professor Peter Erlinder was arrested in Rwanda where he had gone to defend Victoire Ingabire, leader of opposition. His arrest proved beyond doubt that Ingabire has already been convicted without being heard. This is a blow and shame to Rwanda.

The family of Human Rights activists the world over is in tears over the untimely and brutal death of Chibeya and his driver on Wednesday 2 June 2010. Preliminary reports had it that the late Chibeya was asked to meet DRC’s National Police Commissioner General John Numbi (Kabila’s kingpin-cum-link with the Rwandan regime and close associate of renegade general Laurent Nkunda). He was required to do so a day before his demise.

Other reports have it that one, Colonel Daniel Mukalay (the head of the police intelligence unit DRGSS) confessed to have killed Chibeya without intent! Unfortunately, the reports do not disclose the circumstances behind Mukalay killing Chibeya without intent. There’s something fishy here.

Doesn’t this show that the exhibits found alongside the body of Chibeya namely condoms and Viagra must have been planted by the security agents who- by looking at the personalities involved- were ordered by the top to finish up this provocateur in a brutal and degrading way? If they wanted us to believe that Chibeya died as a result of Viagra overdose, what of his driver?

International figures have urged DRC’s authorities to bring Chibeya’s killers to book. But is this enough? Given that the circumstances of Chibeya’s death direct to the high and mighty in the current regime, why shouldn’t the whole government be held responsible?

Reports had it recently that DRC was due to enjoy the cancellation of about $ 8,000,000,000 of its debt to the international community. Why should such a reward be given to a blood-spurting regime? Why shouldn’t the donors squeeze it to see to it that the butchers of Chibeya face the music? Shall donors commit this silent conspiracy, they’re but blessing the assassinations and intimidation of human rights activists hence defeating their stance on restoration and promotion of true democracy.

“We are concerned about the killing of human rights defenders in DRC in recent years, and note that the Congolese human rights groups remain particularly vulnerable to arbitrary arrests and detention and other abuses by security forces,” says the US State Department. Concern only does not address or arrest this chronic anathema. We need actions, not sweet words.

When Dr Robert Ouko, former Kenyan foreign minister died mysteriously, the high and mighty in then president Daniel arap Moi's government were water-tightly implicated. Thanks to Moi’s protectionism, the suspects are still free to vie even for political posts. Another example is the suspicious death of General James Kazini in neighbouring Uganda on 11 November 2009. Apart from the arrest of pawns, who has ever been brought to book? Who is squeezing the authorities to deliver justice? Many living examples abound. The most controversial and laughable is the felling of Tanzania's former prime minister Edward Sokoine in 1984.

Chibeya's case should not end up as happened in Kenya, Uganda and Tanzania. Kabila and his men must tell us who killed Chibeya and why!
Source: The African Executive Magazine June 23, 2010.

Tusikwepe ukweli, huu ni urais wa kununua

WATANZANIA ni watu wa ajabu kidogo. Si kwamba wana macho nyuma au wana sura za ajabu ajabu kama Barney wa kwenye katuni za kitoto. Wala hawana uajabu wowote kimaumbile bali kiakili na kitabia.

Hakuna kitu kilichonishangaza kama jina lao kutumika kuendeleza wizi wa pesa za umma na hongo ukiachia mbali ufisadi wa kunuka.

Bado ni jina lao hili hili linalotumiwa na ombaomba wa masuti kwenda kwa wafadhili kupewa pesa ya kuja kufisidi! Nao kwa bahati mbaya wamekubali kujirahisisha na kujikomba kwa kundi la watesi wao kiasi cha kushangilia na kushabikia maafa yao.

Je, hawa wana tofauti na nondo mdudu ambaye huona mwanga na kuchachawa kiasi cha kuishia kuunguzwa na moto utoao mwanga huu?

Je, hawa wana tofauti na mbwa ambaye huwinda na kuishia kupewa kwato na mapupu huku nyama safi ikifaidiwa na amfugaye?

Ukiangalia Chama Cha Mapinduzi (CCM) “kinavyochangisha” pesa kwa ajili ya uchaguzi, utajua ninachomaanisha kwa kusema Watanzania ni watu wa ajabu.

Ni wa ajabu kutokana na kusahau kuwa ni CCM hii hii iliyotuhumiwa kuchota pesa toka Benki Kuu mwaka 2005 toka kwenye fuko la pesa ya malipo ya madeni ya nje (EPA). Wamesahau kuwa ni CCM hii hii iliyotuhumiwa kuiba pesa ya umma kwa kutumia kampuni lake la Deep Green Finance.

Wamesahau kuwa ni CCM hii hii iliyotuhumiwa kutumia kampuni la Meremeta kuiba pesa ya umma kwa ajili ya uchaguzi unaodaiwa kuwa ulimwingiza Rais Jakaya Kikwete madarakani kwa njia ya kuchafuana na rushwa!

Ni Watanzania hawa hawa wamesahau kuwa ni CCM hii hii iliyotuhumiwa kutumia wafanyabiashara wezi na mafisadi wakuu kuifadhili na kuiba pesa husika katika kashfa hizo tajwa!

Ajabu wamesahau kuwa katikati ya hujuma hizi kuna CCM na Kikwete ambao kwa pamoja hakuna aliyewahi kukanusha tuhuma tajwa hapo juu!

Wamesahau kuwa ni Kikwete huyu huyu ambaye amelipa fadhila kwa kuwanyamazia watuhumiwa wote wakiwamo chama chake hata yeye mwenyewe!

Ni mpumbavu ang’atwaye na nyoka kwenye shimo moja mara mbili. Ni maafa ya kutisha hili linapofanywa na nchi.

Tutafakari na kujiuliza. Je, Kikwete ni maskini wa kuhitaji kuchangiwa hata pesa ya kuchukulia fomu?

Je, wanaofanya hivyo licha ya kulea ufisadi na kuathirika na ufisadi wa kiakili hawajikombi, kujihujumu, kujidhalilisha na kugeuka tishio kwa mustakabali wa taifa?

Hakuna umaskini na ufisadi mbaya kama wa kiakili. Tujihoji na kujisuta. Kikwete amefanya nini cha mno kuwatajirisha Watanzania kiasi cha kumpenda hadi kumchangia ukiachia mbali kujikomba na mapenzi ya mshumaa?

Je, mke wa Kikwete chini ya Kampuni yake ya WAMA inayoingiza mamilioni kila uchao kwa mgongo wa ikulu wamekosa pesa ya kumchangia Kikwete kama kweli ni mchovu kiasi hiki?

Mchezo huu mchafu wa kujikomba ulianzia Bukoba ambapo umoja wa vijana wa CCM huko ulimchangia shilingi milioni moja kwa ajili ya kuchukulia fomu hapo Juni mwaka jana.

Je, vijana wa namna hii wanaojikomba na kujigeuza vifaa vya kutumiwa wanaweza kulifaa taifa?

Je, hawa si aibu kwa taifa hata wazazi wao na kwao wenyewe? Je, hawa wana tofauti na nepi ambayo hukumba kila uchafu? Ajabu vijana hawa wanaojifanya kuwa na uchungu na Kikwete ni wale wale wanaoathiriwa na ukosefu wa ajira na mikopo kwa ajili ya elimu ya juu, ukiachia mbali matatizo mengine mengi!

Je, kweli waliochanga hii pesa ni vijana au wametumiwa na wafadhili wa Kikwete ambao hawataki kujulikana?

Tunaambiwa CCM imeishachangisha kiasi cha shilingi bilioni 50 kwa ajili ya kumwezesha Kikwete kushinda.

Je, huku ni kumwezesha kushinda au kununua urais? Je, urais wa kununua unatufaa na unaweza kutuvusha kwenye karne hii?

Mbona wapambe uchwara wa Kikwete wanasema: yu maarufu kuliko chama na ametenda mengi ukiachia mbali kuwa chaguo la Mungu? Ni chaguo gani la Mungu hata watu, linahitaji mabilioni kuweza ‘kushinda?’

Sisi ni watu wa ajabu kweli kweli. Tuna uwezo wa kuchangisha bilioni 50.

Hapo hapo tunakwenda kwa wafadhili kujidhalilisha kuomba za kugharimia uchaguzi!

Tuna jeuri na ubavu wa kuchangisha mabilioni kwa ajili ya mtu mmoja. Tunakosa za kuchapishia vitambulisho vya taifa, kununulia madawa mahospitalini ambapo wagonjwa wetu wanalala wanne kitanda kimoja! Huyu atokanaye na bilioni 50 si rais wetu bali wa wale waliomchangia (waliomnunua).

Hii ni biashara ikulu ambayo Baba wa Taifa alituasa kuiogopa kama ukoma. Huu licha ya kuwa wizi na ufisadi ni uhaini-kwani tunaifanyia uhuni katiba yetu inayosema rais wa Tanzania atapatikana kwa uchaguzi huru na wa haki.

Ajabu huyu tunayemchangia utamsikia akitoa somo la uwajibikaji, uzalendo na usafi! Huyu ni mbinafsi na mchoyo, taka usitake japo hataki kukubali hili. Heri tutangaze ufalme tunusuru nchi.

Hivi pesa hii ingetumika kununulia vifaa mashuleni tungeboresha elimu yetu kwa kiasi gani?

Kweli Watanzania ni watu wa ajabu. Ajabu ya maajabu hata Kikwete mwenyewe ameridhia mchezo huu mchafu wa rushwa na ufisadi!

Nani amesahau kuridhia kwake kwa kitochi (takrima) ambayo bila shaka ataitoa kutokana na hizo bilioni hamsini! Je, mtu wa namna hii licha ya kuvurunda anatufaa kweli?

Juzi nilisikia Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, ambaye mwanae anakabiliwa na kashfa ya kutumia madaraka yake kusaka ubunge akisema kuwa CCM ilishindwa Moshi Mjini kutokana na njaa ya wanachama wake. Anajigamba kuwa mwaka huu watairejesha Moshi Mjini kwa vile wana mabilioni ya kumwaga.

Kinachothibitisha uajabu wa Watanzania ni pale mtu atakapoiba au kununua kura wazi wazi halafu wakimtangaza wanasema ameshinda kwa kishindo wakati si kushinda bali kuiba kwa kishindo. Huu ni uchafu.

Watanzania wataendeleza rekodi yao ya kuwa watu wa ajabu watakapokubali kuchezewa mchezo mchafu tena kwenye uchaguzi mwakani.

Na hali ilivyo wameisha halalisha uchafu huu. Kwa kukubali chama kichangishe mabilioni, tena kutoka kwa vyanzo vyenye kutia mashaka, ni ushahidi wazi kuwa wameishakubali kuibiwa haki kwa mara ya pili na chama kile kile na mtu yule yule ambaye utawala wake umeweka rekodi ya kuwa na kashfa kuliko tawala zilizopita zikiwekwa pamoja.

Swali linalojitokeza kila mara ni je, Watanzania wanamchangia rais kwa utajiri gani walio nao na umaskini gani rais alionao?

Je, wanaomchangia kweli ni Watanzania au wezi wachache waliovumiliwa na Watanzania?

Hapa hatujaongelea utawala wa kifalme uliojengwa na Kikwete ambapo wake, watoto na marafiki za rais wanaifuja nchi kwa mgongo wake.

Tuache upumbavu na kujikomba kwa watesi wetu. Tusimame tuhoji mantiki na vyanzo vya pesa hii chafu. Tuhoji na kukumbushia maadili ambapo hata huyu mnayemchangia amegoma kutaja mali zake na bado mnaendelea kumwamini na kumuabudia kwa njaa zenu vichwani. Atawajibikaji kwenu atakaowahonga badala ya wale waliomuwezesha kuwanunua? Hapa ndipo jibu la swali la Baba wa Taifa kuwa wanakimbilia nini ikulu wakati hakuna biashara utalipata barabara.

Laiti angekuwa hai akalisikia mwenyewe! Angekufa kwa mshtuko kuona wanaotarajiwa wawe wasomi pale Dodoma kujikomba na kumchangia sh 1,200,000 mtu anayewabana mikopo. Kama usomi ni huu, heri kuitwa kihiyo.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 23, 2010.

Kiherehere cha vibinti, vibaba au watuwala?

MASAAMU Masaamu daktari daktari
Masamu wajile tutakuroreninde?

Masamu y’ egetonto
Muntu musaja muntu mukungu
Ni kiwe we niki musubati niki mukungu?

Omonene tataaa ehee
Tindi kuzurate x 2.

Huu ni wimbo mzuri lakini wa kilugha, acha niimbe wa Kiswahili. Mura Alex Msama upo hapo?

Kiherehere wee kiherehere wee
Wanafunzi acha kiherehere
Wanasiasa acha kiherehere
Walimu nanyi acha kiherehere
Maprofesa acha kiherehere
Siri-kali ache kiherehere
Rai… wee acha kiherehere
Wauza chips acha kiherehere weee kiherehere wee
Umeogelea kwenye mwamba? Eee
sorry sana.


Baada ya rafiki yangu mkuu kupata ugonjwa kama wangu (kupayuka) akapayuka, nilijikuta nikikumbuka huu wimbo tuliozoea kuuimba kipindi fulani mambo yalipo kuwa si mambo. Uzee mwingine unaanza vibaya hasa ukichanganyikana na ulevi wa maulaji.

Siku moja nilimuimbia shangingi mmoja wa kinshomile aitwaye Silvia Rweyependekeza wimbo huu nusu aninyotoe roho. Hayo tuyaache.

Si juzi tu bwana Nkubwa alipopatwa na kashfa ya kuvitukana vishikaji-sorry vibinti vyake kuwa vinadungwa mimba na wakwale wa kiume kwa vile vina kiherehere! Waliouliza yeye anaumwa ugonjwa gani kama si kiherehere hadi awapayukie wafanywa kazi na siku chache baadaye awakashfu wanafunzi?

Je, huyu hajampa mtaji yule mwalimu wa kisukusi anayeoa madenti wake ukiachia mbali wale wanafunzi wanaodunga mimba wenzao na kuwalaza mahospitalini wakati wao wanakula book?

Hebu ninukuu msidhani umbea. “kila anayepata ukimwi anautafuta mwenyewe na wengine ni viherehere vyao; kwa mfano watoto wa shule.” !!!!!!!!!!!!!. Mwanawitu!! Kama huu ndiyo msimamo wa mkuu tumeliwa na tumekwisha.

Mbona kama wao si viherehere wanaogopa kupima ukimwi achia mbali ukiwanyotoa wanavyosingizia mashinikizo ya blood?

Kwanza, kama mzazi siwezi kupata ubavu wa kupayuka hivi hata kama nina ugonjwa huu. Sina ubavu wala hicho kiherehere kuyatamka makufuru haya kusema ule ukweli.

Pia ukiangalia umbali toka Ng’wanza alipoyatamkia na Kishapu na kwingineko kwa akina chagulaga, ni kama ametoa baraka kuwa sasa vibinti vyetu vitolewe kafara hasa na wale wazazi wanaoabudia ng’ombe na fweza.

Japo tunalaani ukeketaji wa viungo, huu wa kiakili ni hatari zaidi hasa unapoungwa mkono na mkuu mwenyewe.

Badala ya kuamuru wanaodunga mimba vitoto vya shule wachapwe bakora na kufungwa, mnawachapa bakora walimu! Ama kweli hii ndiyo Kanani yenyewe ya waharifu na mafisadi!

Sitaki nionekane namshambulia mkuu hata kama tuna ugomvi wa kisiasa. Alichosema waarabu huitaa sharaabiin al nukhama tafsiri sitoi.

Leo najikumbusha enzi zangu nikifundisha kwenye chuo kikuu cha Havard. Zama zile Ziro alikuwa mwanafunzi wangu. Hivyo nitatoa lecture kuonyesha kuwa mimba mashuleni si kiherehere cha wanafunzi bali wanasiasa.

Hivi unategemea nini unapofanya maisha ya wanakaya kuwa magumu kwa kuruhusu mfumko holela wa bei huku ukitanua majuu kwa njuluku hiyo hiyo?

Je, kupenda mialiko pekee si kiherehere kinachosumbua wana siasia wetu? Je kupenda ‘per diem’ ambazo hupatikana kwa kuhudhuria washa, semina na makongamano ya ulaji si kiherehere kingine?

Je, serikali kuridhia nyumba za kufanyia ngono chapu chapu au maarufu kama guest houses zisizo na wageni si kiherehere? Hebu jikumbushe nionayo mtaani kwangu pale Tabata Liwiti. Kila kona ni grosari na kibanda cha chips. Ajabu upuuzi huu umezunguka kila shule na kila sehemu hata misikiti na makanisa. Je, kiherehere cha kisera kama hiki si balaa la wanyonge mkuu?

Kaya yenye sera kama hizi haikosi kihorohoro cha maisha kiasi cha watu kujiuza hasa pale nchi inapouzwa kwa wachukuaji waitwao wawekezaji.

Huyu anauza madini, yule mkoa wake na wengine hata miili yao. Wakati hawa wakiwa na kiherehere cha kupayuka wale wana cha kuuza miili yao na wengine kughushi hata vyeti vya kitaaluma na kuzaliwa mradi kila mtu anakula kwa kiherehere chake.

Hapa hujagusia kiherehere mama wa viherehere, yaani ufisadi wa kuhongana kitochi hadi mnaibiana kula ya kura katika uchafuzi ujao kwa uchaguzi.

Je, kutowashughulikia kina Kagoda and your company si kiherehere ukiachia mbali kuiba majumba ya kaya? Kwanini hii kaya isiwe ya viherehere kiasi cha kushindwa kujua ni kiherehere gani anamsema gani?

Kuna ukweli katika hili. Kweli wanafunzi si viherehere hasa wale wanaochangia wanasiasa wakati sera zao zinawabinya wao?

Nenda pale Udom kaulize juzi walifanya nini kwa kumchangia nani wakati nijuavyo kama profesa mzoefu maisha ya vyuoni ni ya dhiki sana. Ajabu ya maajabu ni pale maji yanapokimbia toka jangwani kwenda baharini! Siasa na elimu wapi na wapi?

Nenda pale Mabibo Hostel hata Milimani complex ujue kuwa viherehere si wasichana tu bali hata wababa watu wazima na heshima zao.

Kabla ya kampeni za mwaka 2005 kuna kiherehere mmoja namjua alikuwa akienda pale Mlimani kutafuta wasichana viherehere wa kufanya kiherehere chake nao.

Tujiulize kwanini vibinti vyetu vimekuwa na kiherehere. Je, ni cha kurithi au kuambukizwa nasi wazazi viherehere wa kila kitu kuanzia siasa hadi maadili na madili?

Hivi wazazi wanaozaa hovyo hovyo nje ya ndoa si viherehere? Nani mara hii amemsahau yule mheshimiwa toka Zenj alokuwa kaoa mwanafunzi na serikali haikumchukulia hatua?

Hata ukienda kwenye vyuo vikubwa, utakuta walimu wakiwataka wanafunzi wa kike ngono lau wawape hizi shahada za mavazi ya ndani. Lisirikali limefanya nini kuwabaini hawa na kuwatimua hata kuwafunga? Ajabu hata ajira nono nono serikalini hata siasani siku hizi zina dalili za kamchezo haka.

Najua wabaya wangu watapakaza kuwa nampakazia jamaa kwa sababu nimepania kuingia ikulu mwaka huu. No. Kwanza mimi ni mzazi ninayeheshimika sana hom kwangu na nina mabinti wengi. Pili, nimeokoka baada ya kuwa na ugonjwa wa kiherehere kiasi cha kuwa na nyumba ndogo kila mtaa ukiachia mbali idadi ya watoto wangu kushindana na swahiba yangu Jacob Zuma ambaye bi mkubwa wake ameamua kurivenji siku zilizopita kiasi cha kuiacha dunia kinywa wazi. Zuma akifanya kiherehere ruksa. Lakini Nompumelelo akijibu mapigo kwa kiherehere hiki nongwa siyo?

Hakuna kitu kimenistua na kunifurahisha kama kufichuka kwa usanii wa shirika moja la kikubwa lenye kujidai linatetea vitoto vya kike na akina mama la MAWAWA.

Baada ya daddy kupayuka na kuchafua hewa ajabu halikujitokeza kumpinga lau kwa upole! Huu ni ushahidi kuwa MAWAWA ipo kutafuta mtaji kifedha na kisiasa kwa kuwahadaa walengwa nao waingie kiherehere chake cha kutafuta ngawira.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 23, 2010.

Thursday 17 June 2010

Why Africa Should Support ICC

Africans have been blamed for not being able to emancipate themselves from thuggish and corrupt rule. However, the international Criminal Court (ICC) seems hell bent to pull a rabbit out of many a hat. The just ended ICC Review conference on the provisions of Rome statute in Munyonyo Uganda is the way forward.

Many analysts are still puzzled why ICC chose Uganda to host the same. Is it a warning to Ugandan strong man and others who came to power by means of manipulation and rigging? Why did ICC chose, among others, Tanzania’s president Jakaya Kikwete whose government came to power by means of the same vice to give a keynote speech? We have all reasons to support this mighty court of revolution which seeks to define some of the Rome statutes.

The proposed amendment has put weight on the act of aggression that can birth chaos and mayhem. After this is adopted, we need to see embezzlement and corruption by those in high offices termed as aggression that is triable by the ICC. This should be done under proprio motu, namely the volition of the prosecutor in lieu of depending on UN-backed resolutions.

African leaders need to be warned. Things have changed tremendously. Who, for example in the 60s, would think that communism in Russia would be something historical not to mention the reunification of Germany?

In this judicial revolution in the making, Tanzania, whose treasury was robbed by the current regime in order to bribe voters, will see justice. Uganda, struggling under the weight of one first family will see justice. Kenyans will see their warlords arraigned in court or foiled from pursuing any more political ambitions.

The beneficiaries of corruption - those in high places- would like to make us believe that ICC is an imperialist tool for fostering the will of rich countries. If this “imperialist tool” can usher positive changes in, so be it. If an “imperialist tool” can prosecute those that committed genocide and other atrocities, let’s fully support it. Why should we support “patriotic regimes” that plunder and ruin our nations?

When you look at how the leaders of rich countries are held accountable by their voters, you see no logic in opposing this bold and revolutionary take by ICC. Apart from emancipating and stabilizing poor countries, it will bring more development based on accountability and merit.

Though Africa has lagged behind for many reasons, one of the main killer is having corrupt and inept rulers who man their countries like their private property. ICC intends to checkmate this. With the coming of this legal revolution, our thieves are caught between the devil and the deep blue sea.
Source: The African Executive Magazine June 16, 2010.

Tusiidhalilishe taasisi ya urais kwa udoho udoho

Japo mimi si mshauri wa rais Jakaya Kikwete, kama mwananchi, nataka nijipe fursa hii japo kwa mara moja. Juzi niliona picha nyingi kwenye mitandao zikimwonyesha rais akipokea misaada toka kwa balozi wa China yenye thamani ya shilingi 51,000,000 ambazo ni sawa na takribani dola 42,000 na ushei. Kwa cheo cha rais na ratiba yake finyu, kuhusika kwenye kupokea udoho kama huu ni kupoteza muda na kumdhalilisha.

Na hii si mara ya kwanza kwa rais kutumiwa vibaya. Aliwahi kuonekana akipokea misaada uchwara toka kwa wahindi fulani. Aliwahi kuonekana akiongea na Didier Drogba mwanasoka wa Ivory Coast anayecheza mpira wa kulipwa Ulaya. Pia aliwahi kuonekana akipewa jezi ya mchezaji Ronaldo wa Real Madrid ya Hispania. Ajabu aliipokea kwa shangwe bila roho kumsuta kuwa ukiona vyaelea vyaundwa. Yeye ametengeneza akina Ronaldo wangapi tangu aingie madarakani? Naye meya wa jiji alishabikia dharau hii kana kwamba hakuna vitu vingine vya maana vya kumpa! Kweli wazungu wanajua kutuchezea akili!

Kwa wanaojua hadhi ya rais, kupokea upuuzi kama baiskeli, pikipiki na viatu si sehemu yake. Rais anapaswa awapokee wageni wa hadhi yake. Kama ni kufuata itifaki, rais hapaswi hata kumpokea waziri mkuu vinginevyo awe ndiye mkuu wa nchi kama ilivyo kwa India, Kanada na nchi nyingine.

Juzi rais alionekana akipeana mikono na wachezaji wa timu ya Brazil jambo ambalo lilipaswa kufanywa na waziri wa michezo hata mwenyekiti wa TFF.
Baada ya hapo ratiba ya ziara yake mkoani Kilimanjaro alipokumbwa na aibu ya magari yake kujazwa mafuta machafu, alipangiwa kufunga tawi la Benki ya Biashara ya Kenya (KCB). Kwa wenye akili hili lilipaswa liwe suto kwa sera yake ya ubinafsishaji wa kiwendawazimu na kijambazi. Je Tanzania ina mradi gani wa maana Kenya zaidi ya kulilisha taifa hili kiasi cha kuweza kuuza hata Sudan ya Kusini. Hata katika biashara hii wafanyabiashara wa kitanzania hawanufaiki. Kwani wakenya hugoma kununua kutoka kwao na hivyo kulazimika kulanguliwa nao tayari kupata soko zuri Sudan. Kwanini Kenya waweze sisi tushindwe? Aibu.

Na hii imekuwa tabia inayoota sugu ambapo rais ameanza kutumiwa na hata wafanyabiashara wenye kutia mashaka kufanya shughuli ambazo si saizi yake.
Kama sikosei, udhalili huu umeanzia kule. Rais amekuwa akitumiwa vibaya. Anavunjiwa hadhi. Sijui kwanini washauri wake hawalioni kama hata yeye halioni?

Hebu piga picha rais anakwenda kupokea msaada wa shilling milioni hamsini tena hafla yake kufanyika ikulu. Je hafla hiyo imetumia shilingi ngapi? Maana siku zote wageni wanapomtembelea rais ikulu lazima awakirimu. Si ajabu ukakuta pesa iliyotumika ukichanganya na muda wa rais ni zaidi ya msaada uliotolewa. Ndiyo. Maana hesabu za watawala wetu zina utata. Wanatumia pesa nyingi kwenda nje kuomba pesa kidogo. Na hii ndiyo maana inafanya iwe rahisi kuwatuhumu kwenda kwenye shopping na kukagua miradi yao au hata kujilisha upepo.

Kuna hata kwa rais kugeuzwa bidhaa rahisi kwa wafanya biashara na watafutaji umaarufu wa shilingi mbili. Licha ya kupoteza heshima na muda wa umma, kuna hata hii tabia ya rais kutumiwa kwenye shughuli zisizoendana na hadhi na hata sheria. Rejea kwa mfano rais kufungua hoteli Arusha na baada ya muda mfupi ikabomolewa sehemu zake kutokana na kuvunja sheria. Rais na hoteli tena ya mtu binafsi wapi na wapi?

Marehemu baba wa taifa Mwl. Julius Nyerere hakuwahi kuhudhuria harusi za wafanyabiashara au kufungua biashara zao. Alijua fika wafanyabishara wangetumia picha yake na wao hata kukwepa kodi na kuwatisha maafisa wa chini kama ambavyo iliwahi kudaiwa kufanywa na baadhi ya wafanyabiashara wachafu nchini hasa wenye asili ya kigeni. Huu mchezo upo ingawa hatutaki kukubali. Nenda kwenye baadhi ya maduka ya wahindi. Utakuta wametundika picha zao na rais ukutani. Ili iweje? Wawatishe watu wa kodi hata kuvutia wafanyabiashara wanaotafuta dili.

Tusishangae siku moja rais kualikwa kwenda kwenye ngoma ya dogoli.

Kinachokera ni ukweli kuwa rais anapata muda wa kupokea misaada ambayo ingepokelewa hata na mnikulu au katibu kiongozi lakini anakosa muda wa kusoma miswaada anayosaini kama ilivyotokea kwenye mswaada wa uchaguzi ambao uliingizwa vifungu kinyume cha sheria bila ridhaa wala taarifa ya bunge.

Afadhali hata muda huu anaotumia kufanya vitu visivyoligana na hadhi yake angeutumia hata kujisomea na hatimaye kuandika hata kitabu kimoja. Maana baada ya marais wa kizazi cha uhuru waliofuata ni wavivu wa kusoma na kuandika vitabu ukiachia mbali kutojua mambo mengi wanayopaswa kuyajua. Urais umegeuzwa kuwa kama u-master of ceremony.

Hata ukiangalia hotuba zinazotolewa na marais wa kizazi hiki ukilinganisha na kilichopita utagundua kuwa ni nyepesi. Ikija kwenye kuwajibika ndiyo usiseme. Rais anamaliza muda wake bila kutangaza mali zake nasi tunaendelea kuaminishwa kuwa anafaa!

Nisingependa Kikwete ahitimishe utabiri wa mwalimu Nyerere kuwa ikulu imegeuka sehemu ya wafanyabiashara chafu. Ingawa balozi wa China anawakilisha taifa lake, siamini kama anaweza kumshauri rais wake apoteze muda wa umma kupokea vitu vidogo kama baiskeli na viatu vya shilingi milioni 51.

Japo tunaweza kuwalaumu washauri wa rais kwa kutomshauri vizuri, kuna upande wa pili. Kutokana na rais kupenda kuendelea kuwa mdarakani, anahitaji kila tukio linaloweza kumjenga awepo. Atapokea baiskeli ambazo zimetolewa na wachina. Lakini zikifikishwa kwa walengwa utasikia baiskeli za Kikwete. Wapambe wake watafanya hivyo naye akijua kuwa ni kinyume. Lakini kwa vile zinamuongezea mileage atanyamaza ilmradi wapiga kura wamepata taarifa na kushawishika. Hii nayo inaweza kuwa rushwa. Maana tangu uchaguzi ukaribie utasikia rais katoa saruji kwa shule fulani. Unashangaa rais anapopata hii pesa ya kutoa misaada hii. Mfano kwa karibuni ni kufichuka kwa taarifa kuwa kulikuwa na kasheshe wilayani Pangani mkoani Tanga kutokana na kutumiwa vibaya mifuko 500 ya saruji iliyotolewa na rais kwa ajili ya ujenzi wa bweni kwenye shule ya Bushiri.

Kuhusu hili mkuu wa mkoa Said Kalembo alikaririwa akisema: “Hivi rais akija hapa tutamuambia kitu gani kuhusiana na mifuko ya saruji aliyoipatia wilaya kwa jili ya ujenzi wa mabweni ya Sekondari ya Bushiri kwa kuwa hamna kilichofanyika? Hii ni aibu.”

Kutokana na rais kujiingiza kwenye biashara isiyomhusu hata watendaji wadogo mikoani na wilayani wanajua udhaifu wake kiasi cha kutotekeleza maagizo yake. Wanajua udhaifu wake kuwa anasahau. Anasema mengi na kukumbuka machache. Wanalijua hili fika. Wanajua kuwa anapata muda wa kutosha wa kusafiri na kukutana na akina Drogba lakini hana muda wa kushughulikia masuala muhimu na makubwa ya kitaifa kama kutoa dira ya taifa.

Hivi siku tukiletewa kibonzo kikimuonyesha rais na suti yake akisakata mchiriku au mpira tutaanza kulaumu anadhalilishwa?

Hii ni kwa refa-mchezaji Joni Tenda

LEO niseme wazi. Sitapayuka bali kueleza kilio changu. Nalia na kuomboleza kiasi cha kupanga kwenda The Hague nimshitaki refa-mchezaji, audhubillahi minaa shaitwan rajiim, Joni Tenda, ambaye amenitenda mambo mabaya baada ya kupewa tenda ya kutuhujumu ili adui yangu mkuu apete asipopaswa.

Taarifa kwa umma ni kwamba siridhiki na jinsi mchezo (mchafu) navyochezeshwa na refa mchezaji niliyemtaja hapo juu. Naamini nawe unamjua na kujua mchezo mchafu na rafu anaotuchezea tena kwa kulipwa kodi zetu.

Unajua kuwa anatumwa na bwana wake, kiasi cha kujidhalilisha kila uchao kumridhisha huyu mshitiri wake kibaka mkuu.

Tuache kuzungusha. Juzi nilijifaragua kwenda kusajili Chama changu Cha Jeuri (CCJ).

Kwanza nilifanya kosa kubwa kuamini kuwa refa mchezaji na rafiki mkubwa wa jamaa yangu, audhubillahi mina shaitwan rajiim, Njaa Kaya ambaye simfichi. Ni Tenda. Sikujua kuwa nilikuwa napeleka kesi ya ngedere kwa nyani anifanyie unyani nyani na ungedere mchana kweupe bila hata chembe ya aibu! Niliamini kuwa katiba viraka ya kaya inazuia makocha, majaji, mapolisi na watumishi wengine wa kaya kuwa wanachama wa timu yoyote.

Hii imewekwa makusudi kuzuia ushikaji, hujuma, upendeleo, kujipendekeza na mambo mengine kama haya.

Hii ililenga kuzuia vurugu zinazoweza kusababishwa na waamuzi baada ya kulishwa takrima na kuonjeshwa kitochi.

Inatia aibu na kinyaa kukuta watumishi wa umma nao wana kadi fichi za vyama tena wakizitumia kuonea timu nyingine bila wasiwasi wowote kana kwamba wanachofanya ni kwa mujibu wa sheria!

Kwani hamuwajui majaji, wakuu wa majeshi hata mahakimu wenye kadi za chama kinachowala? Kama huwajui basi nakutajia mmojawapo yaani Tenda ambaye tenda yake ni kuhakikisha vyama vingine vinakufa ili chama chake cha maulaji kipete milele.

Anayebishia hili ajiulize wale majaji na wakuu wa majeshi wastaafu waliotaka kuwania urais na ubunge chini ya chama fulani chenye kutia mashaka walikuwa wamepata wapi kadi kama si kuwa wanachama hata walipokuwa kwenye ofisi za umma!

Nani zaidi ya mimi anayeshinikiza wafikishwe mbele ya haki ingawa na haki yenyewe siku hizi ni bidhaa sokoni? Je, hawa si wahalifu wa kawaida hata kama ni waheshimika?

Je hawa si matapeli wanaoweza hata kughushi vyeti vya taaluma hata vya kuzaliwa?

Ni juzi tu jamaa yangu alianzisha sera yake haramu ya kitochi ili kuweza kupeta bila kustahiki. Hayawi hayawi sasa yamekuwa!

Nilipoanzisha Chama changu Cha Jeuri, mafisadi wa Chama Cha Maulaji walianza kuchachawa na kuchanganyikiwa wakijua kiama chao kilikuwa hatimaye kimefika nisijue watatembeza takrima na kunijeruhi!

Ni juzi tu wamechangisha pesa chafu na haramu ili kuwahonga wapiga kula hatukusema. Sasa wametafsiri kimya chetu kama woga kiasi cha kumtumia huyu gendaeka Tenda kuendelea kujeruhi vyama vingine! Kaya hii ya walevi inapelekeshwa wapi na kwa spidi hii?

Niseme wazi. Ni upuuzi kwa refa kuwa mchezaji. Ni jinai sina mfano kuona jitu linalopaswa kuheshimika na kufanya mambo ya heshima kufanya upuuzi. Kama unapenda kucheza si uunde timu yako au ujiunge rasmi na timu nayoipenda na kuipendelea kwa kutuumiza wengine. Kinachonikera nusu ya kujinyotoa roho ni ile hali kuwa hili jamaa linalipwa mamilioni ya pesa ya madafu toka kwenye kodi yangu na walevi wengine.

Kwanini Tenda asiachane na kujidhalilisha akaunda chama chake na kujaribu kukisajili akajua machungu tupatayo hata akajiwajibisha na kutangaza kushiriki siasa kihalali badala ya kufua nepi za chama cha maulaji? Kujificha nyuma ya vyeo vya kupewa ni mojawapo ya woga na ujuha ukiachia mbali upakacha.

Pakacha huwa halina ubongo wala halichagui cha kubebeshwa. Huku ni kujigeuza mtu mzima hovyo kwa makusudi mazima kiasi cha kuishi kutegemea uchangudoa wa kisiasa ambalo si jambo jema kwa mja.

Niliamini refa huyu angekuwa huru na mstaarabu na si mleta fujo na mambo mengine ya hatari kwa kijiwe kama ambavyo siku zote amejinadi. Kumbe refa mwenyewe fisadi na fisi!

Kwa umri na cheo chake ni aibu isiyo kifani kufanya mambo ya kitoto.

Tutakuja kuchenjiana kama jamaa hataacha upuuzi wake au hata kuweka kando ili wenye udhu watuhudumie kwa mujibu wa katiba.

Nani angeamini kuwa mtu mwenye akili tena na cheo kikubwa kama cha refa huyu angeweza kutoa kadi nyekundu hata kabla ya kabumbu lenyewe kuanza? Wote mu mashahidi. Mmeona alivyoifanyia mtimanyongo timu yangu, tena changa.

Zamani nilikuwa nikishangaa wachezaji wanaoanzisha zilzali baada ya kuonewa na waamuzi vicheche kama Tenda mtenda mabaya.

Ingawa sina mpango wa kuanzisha vurugu, siwalaumu tena wanaofanya vurugu baada ya kuhujumiwa kama nilivyofanyiwa. Hata hivyo nitaanzisha vurugu gani iwapo Tenda keshaianzisha kwa sababu anazojua yeye ambazo bila shaka hata wewe unazijua-rushwa, takrima, ufisadi na ufisi.

Tufikie mahali tuachane na mambo ya kizamani, yaani kudhani kila mtu ni juha kama wewe kwa vile unaweza kufanya uhalifu na wahalifu wenzio wakakulinda kwa vile uliwafanyia kazi yao chafu.

Ni fikra mgando kudhani kuwa umma utaendelea kunyamazia matendo haya machafu ambayo ni uchokozi na hatari kwao na kaya yao.

Ajabu ya maajabu zee zima halioni hata aibu. Utaliona kwenye runinga likijidai kutenda haki wakati linaihujumu. Hili linafaa kuchapwa bakora.

Hata wale linaowabeba utawaona wakicheka cheka na kujisifu eti wameleta mema wakati wameleta zahama. kusuru wote.

Nyie ni majizi hata kama mtajificha nyuma ya utukufu usio mbele wala nyuma. Siku zenu zinazidi kuhesabika. Kuna siku tutawapeleka Segerea mkanyee mitondoo. Siku hiyo ikifika hakutakuwa na cha msalie mtume wala nini bali kufanya kweli.

Nimalizie kwa kumshauri Tenda aende milimani kwao akauze nyanya kama urefa na kutumia akili vimemshinda. Usidhani namshambulia. Thatha nifanyeje kama jitu lenyewe linatia kinyaa na aibu kiasi hiki tena kwa umri huu?

Acha nianze kuchapa mguu. Maana hata magari nayo siku hizi yananichukia kiasi cha kunigomea nisiyapande.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 16, 2010.

Thursday 10 June 2010

Why is AU doing Bashir’s dirty laundry?




This is none than African Union (AU) Chief Jean Ping. This gentleman originates from Gabon, the country that suffered a great deal more thanks to be manned and ruined by one dictator, that was succeeded by his son after his death. Thus, he’s suffering from this experience of being timid and an instrument of the dictatorship.

I firstly reprimanded Mr Ping in January this year when he equated South Sudanese freedom with sitting on a powder keg. Many sane people thought the AU would shut up, put up or pack up after it openly supported Sudanese strongman Omar Bashir when, on 04 March 2009, The International Criminal Court ( ICC) issued an arrest warrant in conjunction with the genocide he committed in Darfur. So too many thought the same would at least feel ignominy thanks to keeping mum for good twenty-one years as Bashir felled thousands of innocent people in South Sudan not to mention his apartheid system of discrimination against them.

No doubt. Mr Ping must have the courage of the mad to cry such hooey of such proportions. How can he add salt to the injury caused by Bashir for long while his outfit took a pew aside and laughed and still take himself as doing the right thing? Is this fair really?

If this puerile way of thinking is the typical replica of the mindset we have, then “cry for Africa”. It is even sad to note that such cheap and dangerous propaganda are promulgated by such organ that has always been a let down for Africa. AU is always hellbent to mercilessly shoot down or zap the desire for South Sudan to realize her autonomy and honour. AU that has nary united any part of Africa should however nary worry. For the new nation of South Sudan is welcome to the bubbly East African community where it feels more secured and at home than Khartoum. This is where it naturally belongs.

Let us look at his backward looking argument clinically. Mr Ping was quoted recently as saying: “From the outset we’ve argued in favour one of the options, making (Sudan’s) unity attractive.” Sadly, Mr Ping uttered the same during the events of marking African Day.

It shocks to find that such a so-regarded as senior diplomat, can’t understand or even respect the democratic rights of the people of South Sudan to decide for themselves what they want. Even the butcher he is trying to defend, Bashir, recently admitted that shall South choose to go solo, he will support and honour their decision.

Mr. Ping is worried. He added: “That’s a major problem for all African countries which could be confronted by similar situations, that’s what concerns us.” He was referring to the fact that South Sudanese seem stay put to see to it that she goes solo from apartheid Sudan, which has for long been perpetrated by pro-Arab black Africans regarding themselves Arab, whilst they actually are not.

He added his fears when he said: “Such a decision could lead us again to a number of major difficulties, including war.” One thing is imminent. South Sudanese desire to be free can only be stopped and foiled by a miracle but not human machinations. It is too late to urge South Sudan to cool her jet.

Why doesn’t AU want to face the truth that wars in Africa have always been caused by dictatorship, corruption, incompetency, impotency, lunacy, duplicity, greed and what not as far as manning Africa is concerned? Our wildcat diplomats are always horsing around attending shoptalks in the name of Africa as they leave us conned and robbed. Fault them. They will come with huffing and puffing stuff all aimed at getting away with it. They will pummel lies and threats as Mr Ping is trying to do.

Importantly, it must be clearly understood that Africa can nary return her mojo back when she’ll get and have reasonable, accountable, responsible, visionary, reasonable and civilized leaders. Not plundering dictators and Johnny-come-late things in power as it currently has.

Therefore, shall individuals or states keep on supporting such bloodletting regimes as they plunder and commit genocide like it happened in Sudan. We must introduce new laws dealing with all those with genocide philosophy or those that abet with those that committed and their criminal solidarity. Dirty laundry already done for Bashir is enough. In simple parlance, shall individual or states keep on supporting Bashir, they must be indicted by ICC. This is the only way out of this megalomania.
Source: Afro Spear June 6, 2010.

Je yawezekana kumsafisha Lowassa akatakata?

Rafiki yangu alinipigia simu kwa mshangao toka Arusha. Alikuwa akinifahamisha siasa chafu zinazoendelea mkoani Arusha na Manyara.

Tangu mgogoro huu anze baada ya waziri mkuu aliyetimuliwa Edward Lowassa kutolewa kafara kuiokoa serikali ya swahiba yake rais Jakaya Kikwete, kumekuwako na majeruhi wengi mmojawapo maarufu akiwa mbunge wa Simanjiro Christopher ole Sendeka aliyefunguliwa kesi mbili zilizobainika kuwa za kutunga.

Je kesi za Sendekeza zinahusianaje na Lowassa? Simpo. Ni kutokana na waliokuwa nyuma ya kesi hizi kuwa wapambe na maswahiba wa Lowassa ambao alianza kuwatumia kuonyesha makucha yake pindi alipoteuliwa kwa utata kuwa waziri mkuu katika serikali ya swahiba yake kabla ya kuvurunda na kutolewa kafara ili kuinusuru serikali ambayo kama si uoni mfupi wa watanzania ilikuwa itimuliwe kutokana na ufisadi wa wazi.

Siasa za kuhasimiana hazipo Arusha na Manyara tu. Ziko Tanzania nzima hasa baada ya Chama Cha Mapinduzi kumeguka kwenye makundi mengi makuu yakiwa yale ya wanaopinga ufisadi na wanaonufaika na ufisadi. Haya yalipewa jina la mitandao hasa kipindi kile cha kuelekea uchaguzi mkuu wa 2005.

Japo mitandao ni sehemu ya makundi haya mawili, ilikuwa mingi kulingana na wana-CCM walioonyesha kuwa na kiu na nguvu ya kuwania urais baada ya kwisha muda wa rais mstaafu Benjamin Mkapa ambaye ugombea wake ulizua mitandao lakini ikauawa na ushawishi wa baba wa taifa marehemu Mwl. Julius Nyerere aliyemuunga mkono wazi wazi na kumwingiza madarakani.

Japo kuna mitandao mingi, leo tutaongelea kundi moja kubwa lenye ushawishi serikalini la Lowassa-Rostam-Kikwete. Ingawa wachambuzi hawalitaji wazi wazi kama lilivyo, kundi hili linawakilisha wale wanaonufaika na ufisadi kutokana na kuwa na watuhumiwa wengi wa ufisadi ambao serikali imeshindwa kuwashughulikia. Badala yake inashughulikia wale wanaotaka washughulikiwe.

Kundi la pili ni la Sitta-Mwakyembe. Hili kundi linapata jina lake kutokana na spika wa Bunge Samuel Sitta kuridhia bunge kuunda tume teule kuchunguza kashfa ya Richmond. Tume hii iliongozwa na mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe hivyo kuwa kinara wa kundi ambalo linasakamwa kwa kila gharama na kundi la kwanza kutokana na kuhofia kuweza kusababisha litimliwe madarakani.

Hatutaeleza ushiriki wa kila kinara ingawa mbunge wa Igunga Rostam Aziz anafahamika alivyo swahiba wa Lowassa na Kikwete hasa baada ya kutuhumiwa kuwa nyuma ya sakata la Richmond. Alianza kujulikana pale alipotajwa na waziri wa zamani wa nishati na madini aliyetimuliwa na kashfa ya Richmond Dk Ibrahim Msabaha pale aliposema kuwa yeye alikuwa Bangusilo kwa kikwao akimaanisha kuwa mbuzi wa kafara-kwa vile mradi mzima wa Richmond ulikwa wa serikali ukishinikizwa na Lowassa kwa niaba ya bosi wake Kikwete huku akishinikizwa na aliyetajwa kama mwarabu wake yaani Rostam. Historia ya genge hili ni ndefu.

Tuje kwa mhusika mkuu wa makala hii, Edward Lowassa mbunge wa Monduli. Huyu baada ya kujeruhiwa na marehemu baba wa taifa kuelekea kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 1995-akishutumiwa kuwa amejilimbikiza mali nyingi zisizo na maelezo, hakukata tamaa. Kwa kujua hatari iliyokuwa ikimkabili baadaye, alijiunga na Jakaya Kikwete aliyeonekana kushinda kinyang’anyiro cha kubeba bendera ya CCM lakini akakataliwa na Nyerere akidai hakuwa amekomaa kisiasa- hivyo kutostahili kuongoza taifa wakati ule.

Wazungu husema a good politician is a schemer yaani mwanasiasa mzuri lazima awe mwenye mbinu. Hivyo Lowassa baada ya kugundua hili, aliamua kuweka dau lake kwenye farasi aliyeonyesha kushinda yaani Kikwete.

Wapo wanaosema kuwa Lowassa licha ya kujua kuwa Kikwete alikuwa turufu pia alijua udhaifu wake-ulegelege. Hivyo alijua ushindi wa Kikwete ungemuwezesha kuwa kingmaker au mtengenezaji wa wafalme ambaye baada ya Kikwete angejitengeneza. Hivyo kuwa rais.

Wanasiasa mara nyingi hawakati tamaa. Wana subira ya fisi. Baada ya Lowassa kuteuliwa kuwa waziri mkuu na akaanza kuonyesha cheche zake akitenda karibu kila jambo huku Kikwete akiwa kama kaenda likizo, wengi wenye kutaka urais walianza kustuka na kufikiria la kufanya.

Bahati mzuri kwa kundi hili, mtu aliyeonekana kuwa tishio lake alianza kujimaliza kwa kuanza kuingia deal zilizommaliza hatimaye kubwa ikiwa Richmond. Hapa inabidi ieleweke kuwa Richmond haukuwa mradi wa Lowassa pekee bali Kikwete na Rostam na serikali nzima.

Je ni kwanini msalaba ulimuangukia Lowassa? Kwanza alikuwa waziri mkuu ambaye kimsingi ni mtendaji mkuu wa rais. Hapa ndipo dhana nzima kuwa kupatikana na hatia kwa Lowassa kulitosha kuiangusha serikali nzima ya Kikwete kama si watanzania kuwa na muono mfupi na ushabiki wa kijinga. Ila kama Lowassa, kutokana na jina baya alilokwishapewa na marehemu Nyerere, alikuwa ni mtu muafaka kubebeshwa zigo ili amuokoe rafiki yake na serikali yake.

Sababu nyingine ya kubebeshwa msalaba kwa Lowassa ni ukweli kuwa aliingia mkenge wa Richmond kwa pupa kutokana na chumo binafsi ambalo lingepatikana. Naye hakuwa wa kwanza kuwekeza kwenye jinai hii. Rejea rais mstaafu alivyoingia kwenye kashfa ya kujitwalia mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira na kuilazimisha Tanesco kununua nishati toka kwake kwa mwendo wa kuruka. Hivyo huu ni utamaduni mchafu ulionza kuota mizigo kiasi cha kuacha nchi yenye raslimali ikiomba omba. Anayebishia hili arejee tukio dogo la hivi karibuni ambapo afisa tawala mkoa wa Kilimanjaro Hilda Gondwe alijiuzia gari aina ya Toyota Land Cruiser VX (shangingi) lenye thamani ya shilingi 155,000,000 kwa bei ya kijambazi ya shilingi 6,000,000.

Kwenye nchi iliyotawaliwa na upanya na ufisi, hili ni jambo la kawaida na kila mbuzi anakula kwa urefu wa kamba yake.

Sasa si siri wala fununu. Lowassa ni majeruhi kisiasa. Yupo chumba cha wagonjwa mahututi. Wale madaktari mzungusho au spinning doctors-wenzake na mbwa wao yaani walamba viatu na makanjanja wako mbioni kutaka kumsafisha ili hapo baadaye awe rais. Je hili litafanikiwa bila muujiza? Tuazime maneno ya spika wa bunge akimpiga kijembe alipouliza: je yawezekana maji taka yakamsafisha mtu akatakata? Anayetilia shaka hili ajiulize ni vyombo vingapi vya habari vimeishaingia kazini kwa ujira wa pipi kumjenga huku vikiwabomoa wapinzani wake.

Ila wale wanaoota mchana kumsafishia njia Lowassa inabidi wajiulize maswali makuu muhimu.
Je anasafishika Je madhambi yake watayaficha wapi? Je watanzania watakuwa wasahaulifu na majuha kiasi hiki? Je anafaa baada ya kuonyesha uroho na uhovyo usio kifani? Je hatalipiza visasi tena kwa watu wasio na hatia bali kuwa wakweli? Je hatuna watu wengine wenye udhu kutuongoza? Je tuko tayari kurudia madudu tuliyo nayo? Maswali ni mengi kuliko majibu.
Chanzo: Dira Juni 2010.

Mgomo wa wafanyakazi ungelikomboa taifa

KWA mara ya kwanza kwenye historia ya taifa letu, serikali na chama tawala hawakukaribishwa kwenye kilele cha sherehe za wafanyakazi maarufu kama Mei Mosi. Tunaambiwa. Wafanyakazi walikataa kumwalika rais kutokana na waziri wake kuwadharau na kuwahadaa.

Walikaririwa wakisema kuwa hata hivyo hawana ugomvi na rais bali waziri wake! “Hatuna ugomvi wala chuki na Rais Kikwete, tumeshindwa kumwalika katika maadhimisho ya kesho (leo) kwa sababu TUCTA haikutaka baadhi ya viongozi wa serikali wahudhurie katika sherehe zetu. Wao ndio kikwazo cha sisi kutotimiziwa mahitaji yetu.” Alikaririwa Naibu Katibu Mkuu wa TUCTA, Nicholaus Mgaya akisema.

Tamko la namna hii ama linalenga kuzidi kumpa kichwa rais ili wafanyakazi wamuumize au ni kupigwa siasa kirahisi ukiachia mbali kujidhalilisha na kujikomba kwa serikali.

Kama tamko hili ni mawazo binafsi ya msemaji aonywe na kuanza kuangaliwa kwa makini kama ni msimamo wa wafanyakazi, basi ni tatizo kubwa tu.

Hii ni ajabu kidogo! Huwezi kumchukia waziri anayeshughulikia wafanyakazi ukampenda aliyemteua na kumbakiza madarakani hata baada ya kuvurunda. Kufanya hivyo ni kujidanganya, danganya, kujenga mazingira kwa rais kukudanganya. Ni kumpa rais sifa asiyostahili.

Kimsingi, serikali ambayo kwa muda mrefu imekandamiza wafanyakazi na kuwanyonya ni ya rais si ya waziri. Wafanyakazi walipaswa kulielewa hili na kulizingatia.

Maana hata huyo waziri hana mamlaka yoyote kufanya lolote bila kuidhinishwa na kikao cha baraza la mawaziri. Hii ni sawa na kupenda boga ukachukia ua lake au kumpenda mama ukamchukia mtoto wakati wote ni wamoja.

Kadhalika kuna dhana nzima ya uwajibikaji wa pamoja kwa serikali katika kila jambo, liwe baya au zuri.

Rais na serikali yake wanaweza kukwepa na kumtumia waziri mhusika katika sehemu nyingine lakini si katika uwajibikaji wa pamoja.

Je, ni kwanini serikali imefikia kushikwa pabaya wakati huu mbaya wa kuelekea uchaguzi? Jibu ni rahisi. Watawala wamezoea kutawala watakavyo wakidhani Watanzania wa sasa ni sawa na wale wa mwaka 47, ambapo hakukuwa na utandawazi na kupanuka kwa haki za kiraia na upinzani.

Ingawa tuko kwenye mfumo wa vyama vingi, serikali imo kwenye usingizi wa chama kimoja! Ni bahati mbaya sana kuwa na utawala wa namna hii.

Mgomo ungefanikiwa ungeweza, kwa mara ya kwanza, kuiwajibisha serikali baada ya upinzani kupoteza nafasi wakati wa kashfa ya Richmond ambapo serikali ilimtoa kafara waziri mkuu ili isianguke.

Kama mgomo huu ungefanikiwa, licha ya kuwa hatua muhimu kuelekea ukombozi kamili wa taifa, ungeweza kuwa ukurasa mpya wa kufikia ukombozi mapema na kwa njia ya kistaarabu na si umwagaji damu.

Sababu nyingine inayoipa kiburi serikali kuwahadaa na kuwadharau wafanyakazi ni ile hali ya kuua upinzani. Hivyo, serikali bado ina mazoea kuwa hakuna awezaye kuitia kashi kashi.

Wafanyakazi walipoteza nafasi adhimu na muhimu. Tunasahau kuwa mapinduzi ya Ufaransa yaliletwa na wafanyakazi. Tunasahau hata historia ya juzi nchini Poland ambako Chama cha wafanyakazi cha Solidarity kikiongozwa na Lech Walesa kilivyoporomosha tawala zandiki kule.

Ni rahisi kuuminya hata kuua upinzani lakini si sauti na mshikamano wa wafanyakazi. Ingawa serikali inaangalia tishio la mgomo kama suala la wafanyakazi na serikali kwa upande mmoja, ukweli ni kwamba ni mtafaruku wa kitaifa.

Kama wafanyakazi wangeacha woga na ujinga wakatimiza azima yao ya kugoma, na wakulima ambao nao ni wafanyakazi tukiondoa majina ya kisiasa, wangejiunga na mgomo ule.

Walaji kadhalika wangekuwa sehemu ya mgomo. Watu kama wanafunzi wasingebaki nyuma. Mgomo ungesimamisha shughuli zote kiasi cha kuathiri maisha ya kila mmoja-wanaopinga na wanaounga mkono mgomo.

Tunajua kuwa waajiri wengi ambao wengi ni wageni hawakuunga mkono mgomo huu kutokana na wao kuwa wanufaika wa unyonyaji wa wafanyakazi. Rejea taarifa kuwa uchumi wa Tanzania unamilikiwa na wageni kwa asilimia 90.

Je, ni kwanini serikali ilifanikiwa kutumia vitisho kuepuka kutofanyika mgomo kwa kutumia ujanja ujanja kama ambayo imekuwa ikifanya?

Wafanyakazi sawa na Watanzania wengine wamedanganywa sana na serikali ya sasa ambayo inasifika kwa matumizi mabaya na kulea ufisadi kutokana na kuwa tunda lake.

Je, tumejifunza nini au kujiandaa kuchukua hatua gani? Hili ndilo swali kuu tunalopaswa kulijibu ili tuweze kujikomboa.

Serikali haiwezi kuendelea kuwaambia wafanyakazi kuwa haina pesa wakati kila siku unaripotiwa ufisadi wa mabilioni ambayo yangeweza kuendesha nchi kwa mwaka mzima bila kuomba au kukopa.

Serikali haiwezi kuendelea kuwaambia wafanyakazi haina pesa wakati ikipandisha mishahara ya wazito kila uchao ukiachia mbali matumizi ya hovyo kama ununuzi wa magari ya bei mbaya, kulipana posho kubwa bila kufanya kitu, ziara za mara kwa mara za watawala ndani na nje na matumizi mengi ya kutia shaka ukiachia mbali kusamehe kodi.

Serikali ya sasa imekuwa ikiwahadaa Watanzania kila mwaka. Yako wapi matunda ya kasi mpya, ari mpya na nguvu mpya? Iko wapi safari ya Kanaani au ni kwa vile wakubwa walishafika na kuishi huko huku umma wa ukiishi motoni?

Iko wapi mipango na sera zinazoingia akilini ukiachia mbali hizi zinazotumika za kujinufaisha baada ya zile tulizoambiwa ambazo rais mstaafu Benjamin Mkapa alisema hazitekelezeki?

Ajabu CCM bado inategemea sera hizo hizo zisizotekelezeka kuwashawishi wapiga kura waichague! Wakifanya hivyo watakuwa wamejivika kitanzi wenyewe.

Tuwahimize wafanyakazi kuanza kufikiri upya juu ya kugoma wakijua wazi kuwa kufanikiwa kwa mgomo wao ni ukombozi si kwao tu bali taifa zima. Na wajue.

Ndiyo njia ya kistaarabu na kisasa ya kuondosha mfumo fisadi na ovu uliopo ambao unawabinafsisha waajiri yaani serikali na wawekezaji kwa gharama ya wafanyakazi na wakulima wa taifa hili.

Wafanyakazi wakiweka zana chini hata hao wanaojiona wakubwa watamomonyoka kama kipande cha theruji kwa siku moja. Maana hakuna aishie bila kupanda mgongoni mwa wafanyakazi ajue au asijue.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 9, 2010.

ICC adui yangu namba moja

HEBU piga picha. No. fikiria. Mtu umekwanyua vijisenti vya wanuka njaa na umaskini ili uvitumie kuwahonga upate ukuu ambao ni ulaji wa dezo kwako familia na marafiki zako halafu jitu linataka kutia kichumvi.

Hebu jaribu kufikiria. Unajipinda na kutengeneza dili kama HEPA, Richmonduli hata Kagoda halafu jitu lililoko huko Uropa linakuja na wazo kuwa ufungwe spidi gavana na kupelekwa The Hague ukanyee debe.

Je, namna hii ni wakuu wangapi katika bara hili la mwanga liitwalo la giza tutapona kama kweli hii itakuwa kweli na si geresha bwege? Msidhani natania. Kuna balaa linaundwa huko Uropa ili kuvuruga mavituz yetu.

Kwaza lazima niseme tena kwa kinywa kipana. Wazungu ni waoga, waongo na wanafiki. Kwanini wangoje Joji Kichaka amalize ngwe zake? Au ni kwa vile alikuwa akitawala taifa dume duniani? Kwani wanadhani tumesahau alivyoiba kura?

Mbona haya mazungu hayaendi kumshitaki malkia wa Uingrishi ambaye huwa anatanua tena bila ya kuandaa uchaguzi kiini macho hata angalau kwa kuiba hizo kura? Jamani eleweni. Huu ni ubaguzi wa rangi usio na mfano nasema.

Rafiki yangu Moi Kibaka juzi kanitonya.

Anasema tuwe macho na tukae chonjo lolote laweza kutokea hasa kwetu sie tulioweka tukachukua waa. Kibaka hafichi. Akiangalia yanayojiri kwenye kaya yake anasema wazi wakuu tutaumbuka. Anayebishia hili ajikumbushe Charles Taylor alifanywa nini?

Shujaa mzima yuko ananyea debe huku shujaa mwingie Omari Bashiri akitafutwa naye akanyee debe. Hawa jamaa hawana adabu. Nasikia kuwa Karumekenge na Madevu nao walionywa na EU na ICC kuwa kama watarudia upuuzi na madudu yao watanyea debe.

Hii ndiyo siri ya jamaa yangu kuuogopa ulaji kama ukoma huku Madevu akisilimishwa na kuongelea matambuano na amani wakati aliishaapa asingemtambua mtu wala malaika hadi yeye akalie kiti! Hamuoni alivyoingia ndoa ya mkeka kichwa kichwa akidhani ataukwaa ukuu ale dezo na kupunyua kama jamaa yake na shoga yake mpya Karumekenge?

Kuna jamaa moja limeniudhi nusu nijinyotoe roho. Si lilisema kuwa eti itungwe sheria ya kuwabana hata bibi wakubwa zetu kutokana na wao kutumia migongo yetu kufanya biashara ya kimachinga kama kuanzisha NGOs za uongo na ukweli ili mradi wachume.

Haya majuha kweli kweli. Si lipo jingine lililosema eti bi Nkubwa wangu ni muongo na mnafiki kutokana na kusema kuwa aliwahi kunyanyaswa alipokuwa akijifungua.

Lilisema eti hizi zilikuwa longo longo na kamba za kuwafungia walevi kuwa anawajali kiasi cha kuongopa. Linataka aeleze ni lini, wapi na nani alifanya kitendo hiki kwenye kaya ambapo wakubwa na miungu watu wasioweza kuguswa na vinyangarika waitwao manesi.

Sasa kama ni kamba au longo longo wewe inakuhusu nini. Si uache walevi waukwae mkenge wadhani bi nkubwa anawapenda wakati ukweli ni kwamba anawaponda kwa ulevi na ujuha wao.

Turejee kwa hili li ICC au International Criminals’ Court. yaani mahakama la wahalifu. Kuna jamaa lenye midevu kama Osama liitwalo Okampu Mreno. Hili jamaa linanikera na nalichukia kuliko hata huo ukoma.

Linasema kwa nyodo kuwa litatukomesha utadhani limewahi kukalia kiti cha enzi! Si lingejaribu kuutafuta ukuu lijue siri ya mchezo kuliko kupayuka hovyo.

Kwanza najua. Hili jamaa ni li-reno. Linatokea Ureno, taifa ambalo liliwatesa na kuwaua wanamapinduzi wengi. Wako wapi kina Eduardo Mondlane, Samora Machel, Louis Amircal Cabral, Augustino Neto na wengine wengi ambao waliuawa kwa njama za Wareno?

Mbona sijasikia hili likimshughulisha huyu Mreno uchwara? Anatufanya wote mabwege siyo? Hivi jamaa hili lilitaka tule polisi siyo?

Kwanza niseme wazi tena kwa kinywa kipana: Mreno hanitishi wala hatampata mtu. Lazima tupinge ukoloni huu mamboleo wa kutaka kuingilia madaraka yetu na kuvuruga amani na mshikamano. Sijui yanapata wapi mshipa wa kuhoji mamlaka yatokayo kwa Mungu.

Hivi hawa hawajui sisi ni chaguo la Mungu? Yaelekea hawa jamaa ni makafiri wasiosoma neno la Mungu lisemalo kuwa kila mamlaka hutoka kwa Mungu.

Mie nalishauli hili li-Mreno liseme shida yake ili likatiwe kitu kidogo kama akina Alex Stewart badala ya kuingilia ulaji wa watu. Kwanza pesa ya walevi inaliuma nini iwapo si yake?

Kisheria Mreno ni mhaini anayetaka kupindua serikali za wananchi tena wenye jamhuri zao.

Jamani tuache mchezo. Hali inatisha. Juzi nilimsikia rafiki yangu M7 akiwalaani wafadhili akitaka washughulike na ujenzi wa barabara badala ya kujisumbua kutaka kuingilia chafuzi zetu.

Kuna jamaa alimzodoa kuwa ameishiwa. Maana anataka wafadhili watoe mchicha wa kujengea barabara halafu wana siasia waukwibe na kutumia kuwahongea walevi.

Hawa jamaa si mabwege kama tunavyoweza kujidanganya kama jamaa yangu waliyempunguzia njuluku akajitia sizitaki mbichi hizi wakati hata pupi anayovaa na bi nkubwa wake imenunuliwa kwa njuluku za wafadhili hao hao anaojidai kuwatishia nyau.

M7 ameshtuka baada ya kaya yake kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano huu wa ICC wa kuharibu ulaji wetu.

Hata ukiona walioufungua ni wale wale wezi wa kula ambao nao kama M7 nadhani wamepewa onyo kuwa zao zinahesabika.

Je, walevi wanalipokeaje hili? Je, ni suto kwao kuwa wameshindwa kujikomboa hivyo Wazungu wameona wawakomboe ili waache kuwategemea kwa kuwabomu na kukopa kila uchao?

Mie mwenzenu niko nawaza la kufanya. Kama si wapambe wangu ningependa niachane na ukuu kabla sijalikoroga nikashindwa kulinywa.

Maana mambo yangu yanajulikana nilivyotembeza njuluku nilizoiba kijiweni kuwahonga walevi walionichagua wakidhani nitawakomboa wasijue nitawaangamiza.

Halafu kuna jambo jingine nasikia li-Mreno linataka kupendekeza. Linasema eti ambaye atachaguliwa kuwa mkuu asipotangaza mali zake au kumdhibiti bi nkubwa wake naye afikishwe The Hague.

Baada ya hili kujulikana nilisikia mimbea fulani ikisema eti hata walioghushi vyeti vya elimu na kuzaliwa nao wafikishwe The Hague.

Wengine wanataka hata Kagoda na Richmonduli nao wafikishwe The Hague kwa vile walitenda makosa ya ukatili dhidi ya mifuko ya binadamu.

Mie ningependekeza hata wale wanaochoma mibaka wakiabudia mibaka nao wafikishwe The Hague bila kusahau wauza unga maarufu wanaofadhili vyama na serikali.

Hata wale walioiba nyumba za walevi nao wangefikishwa huko ili wanyee debe kama Taylor au wafie huko kama Slobodan Milosevic.

Nasikia kuna mijitu inataka orodha ya waharifu wa kufikishwa The Hague iongezwe kiasi cha kuhusisha hata wezi kama mzee wa Vijsenti aliyeficha mabilioni ya madafu kule kwa Maza visiwani Jersey baada ya jamaa yake kumkingia kifua kutokana na kumsaidia kutengeneza Mahepe ya HEPA.

Kwa vile mie si mwoga na sina mpango wa kutengeneza HEPA tena, nilimpigia simu Mreno angoje kidogo nimalize kufanya vitu vyangu ndiyo awabane majuha wengine isipokuwa mimi.

Kuonyesha nisivyo mwoga na aibu niliunga mkono ukoloni huu nilipoitwa kutoa nasaha ingawa rohoni nilikuwa na unywanywa sina mfano.

Kwa vile mambo yanaanza kubadilika na kuharibika, nimewataarifu kina Mbwamwitu, Kanji Rosttamu na Ewassa kila mtu abebe furushi lake na tusilaumiane.

Ingawa walevi wameonekana kushabikia ujinga huu, kuna siku hawa wakoloni wanaoongozwa na Mreno kudai tutaje hata nyumba zetu ndogo na watoto wetu wa nje ya ndoa. Sijue nani atapona hapa?

Wakati natafakari huu upuuzi wa Mreno, roho inaniuma kuona nimeishachangisha vibilioni kidogo kwa ajili ya kitochi, vingi vikitoka kwa watu wachafu. Lakini nitaongea na wanasheria wangu wajenge hoja kuwa ukarimu au takrima si tendo baya linalopaswa kuchukuliwa kama kosa la jinai.

Lazima sheria hata kama ni za kimataifa zitambue kuwa ukarimu ni jadi yetu.

Pia nitashauri wahoji ni kwanini watu wanataka kutumia sheria kuvuruga mshikamano na amani tulivyorithi toka kwa mashujaa wetu?

Naona dege la Mreno linakaribia kutua airport ngoja nikitoe lisije likanikamata na kunisukumiza The Hague nikanyee debe.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 9, 2010.

Saturday 5 June 2010

Masauni, ubaguzi na uonevu wa CCM

BABA wa Taifa, marehemu Mwalimu Julius Nyerere, alituachia urithi bora japo tunaufuja kwa ujuha na upogo wetu. Hakuwa mnafiki wala kigeugeu. Alichukia ubaguzi, ufisadi, uroho, ubinafsi, ubepari, ufisi na mambo mengine kwa namna ya pekee.

Hakuna dhambi iliyomuumiza kichwa kiasi cha kukamua hazina yetu kama ubaguzi. Rejea mchango wa Tanzania kwenye kuikomboa Afrika ya Kusini. Bado tunakumbuka wimbi la wakimbizi waliopewa hifadhi na fursa toka Afrika ya Kusini.

Watu wa Mazimbu ilipokuwa kambi maarufu ya wakimbizi hawa ya Solomon Mahlangu, wanakumbuka vizuri.

Nyerere alilaani ubaguzi na kupigana nao kwa matendo.

Aliishi na kulitimiza hili kwa kiwango cha juu. Sijui wanaojua hili wanajisikiaje wanapoona Watanzania wanaanza kubaguana kwa misingi ya mitandao, vyama, dini hata makabila vitu vinavyopingana na dhamira ya mwanzilishi wa taifa hili?

Uonevu na ubaguzi wa hivi karibuni dhidi ya mwenyekiti wa zamani wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Hamad Yusuf Masauni, ndio umenisukuma kudurusu hali halisi kuhusiana na jinai hii iliyohalalishwa hivi karibuni nchini mwetu.

Kuna madai kuwa Masauni alighushi cheti cha kuzaliwa, hatua iliyomwezesha kuchaguliwa kushika wadhifa huu adhimu chamani. Wadhifa huu ni muhimu hasa wakati huu wa kuelekea kwenye uchaguzi mkuu kutona na vijana kuwa kundi kubwa nchini.

Kama Masauni alighushi au la hilo ni suala la polisi na mahakama kuchunguza na kuamua ingawa kutokana na vigogo walioko nyuma ya sakata hili ukweli ni kwamba Masauni keshahukumiwa tu.

Je, Masauni ni wa kwanza kutuhumiwa kughushi? Jibu ni hapana. Alianza kutuhumiwa Mbunge wa Buchosa, Samuel Chitalilo. Wakati tuhuma hizi zikitolewa, Rais Jakaya Kikwete wakati ule akiwa mgombea alimtetea kwa kusema kelele za mlango hazimzuii mpangaji kulala, kwa maana kelele za wapiga kura hazimzuii mbunge kufanya vitu vyake.

Wengi wanashangaa. Kwanini Kikwete ambaye mtoto wake Ridhiwan anatuhumiwa kuwa nyuma ya sakata la Masauni- hakusema kelele za mlango? Au ni yale ya uchungu wa mwana? Wengi wanajiuliza. Je, huu si ubaguzi wa wazi tena utendwao na wale tuliowaamini madaraka na ofisi za umma.

Pia sakata la Masauni limeuvua nguo utawala wa Kikwete na kuuonyesha kama usio makini.

Kwani ndiye aliyempitisha kuwa mwenyekiti bila kuwa na uhakika na historia yake. Je, wako wangapi kama Masauni waliopitishwa na utawala huu ilhali hawafai?

Baada ya hapo mwanaharakati Keinerugaba Msemakweli aliwatuhumu vigogo wengine wa CCM kwa kosa hilo hilo.

Waliotuhumiwa tena kwa kutungiwa kitabu ni ni mawaziri na wabunge Dk. Makongoro Mahanga (Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana), Dk. Mary Nagu (Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko), Dk. Diodurus Kamala (Waziri wa Afrika Mashariki) na Dk. Emmanuel Nchimbi (Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa).

Wengine ni Mbunge wa Ismani ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (William Lukuvi), Victor Mwambalaswa (Lupa-CCM) na Dk. Rafael Chegeni (Busega-CCM).

Baada ya kuzuka madai na manung’uniko kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, alimlazimisha Masauni kujiuzulu Mei 18, kwa shinikizo la chama, Makamba alijitetea na kusema kuwa jukumu la kushughulikia tuhuma za Masauni limo mikononi mwa polisi.

Wengi wanaamini Masauni ametimuliwa baada ya kugusa masilahi ya wakubwa fulani. Wanajiuliza mantiki ya tuhuma za Masauni kukimbiziwa polisi ilhali tuhuma za Chitalilo zilishughulikiwa na polisi hao hao zikawekwa chini ya busati. Wanashangaa kwanini Masauni aachishwe uongozi wakati watuhumiwa waliotajwa hapo juu hawakuwajibishwa ukiachia mbali kutoshughulikiwa na polisi?

Katika kukwepa aibu, hivi karibuni vyombo vya habari vilimkariri Naibu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai nchini, Naibu Kamshna wa Polisi, Peter Kivuyo, akisema suala hilo linafuatiliwa na polisi kwa karibu.

Kivuyo alisema “Kuhusu mawaziri kughushi vyeti polisi imeanza uchunguzi na hatua kali zitachuliwa kwa wahusika iwapo watabainika kufanya makosa hayo ili iwe fundisho kwa wengine.”

Ahadi ya hatua kali kuchukuliwa imeishakuwa wimbo wa jogoo. Kwanini wasiwajibishwe kwanza ndipo hatua zifuate kama kweli kuna utashi wa kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria?

Suala la Masauni linachunguzwa na polisi wakati la vigogo waliotajwa muda mrefu na rais akawanyamazia linafuatiliwa siyo linachunguzwa!

Hapa unaweza ukaona ubaguzi na kulindana kwa dhahiri. Tunakwenda wapi iwapo vyombo vya dola vinaanza kutumika kama asasi za watu binafsi kulindana na kupeana kinga?

Hapa tunapigwa changa la macho. Anayebisha ajiulize tuhuma zenye kila aina ya ushahidi za kughushi zinazomkabili Mbunge Chitalilo ziliishia wapi baada ya Kikwete kumkingia kifua kuwa kelele za mlango haziwezi kumzuia mpangaji kulala?

Je, kiongozi wa namna hii anayetenda kwa upendeleo anaweza kutuvusha au kutuzamisha?

Hii maana yake ni kwamba anatawala kifamilia na ushikaji. Hivyo watu wake wa karibu wakiguswa sheria itapindwa na kuwahami.

Wako wapi kina Kagoda, Deep Green Finance, Meremeta na wezi wengine wa EPA, CIS, rada, ndege ya rais na wengine wengi walio karibu na wakubwa?

Swali ambalo litaiandama CCM ni mantiki ya kumwajibisha Masauni ambaye ni dagaa huku mapapa wakiendelea kukata mawimbi.

Kituko na kufichuka kwa unafiki wa CCM ni ukweli kuwa ilimpitisha Masauni ikijua madhambi yake. Kosa hapa kwa CCM si kughushi vyeti vya kuzaliwa bali kugusa masilahi ya wakubwa fulani.

Maana kama kughushi kungekuwa kosa kwenye macho ya CCM watuhumiwa vigogo wangekuwa wameishawajibishwa zamani gani!

Je, wako wangapi walioghushi lakini wakaendelea kuwa kwenye ofisi za umma kwa kinga ya kujikomba kwa na kulinda masilahi haramu ya CCM?

Je, kuna ufisadi na ujambazi kuliko huu? Je, hapa mfumo wetu haujaoza kiasi cha kugeuka kansa?

CCM, polisi na umma tutende haki. Wananchi tuwashinikize wahusika kuacha mchezo mchafu wa kutumia sheria kibaguzi. Na wahusika watuhumiwa na washitiri wao wajue fika. Mambo yameanza kubadilika.

Kuendelea na jinai hii mtaamsha hasira za umma kiasi cha kuleta vurugu. Jinai ya CCM. Polisi na Masauni na vigogo walioghushi iwe somo kwetu. Amkeni tuibadili jamii yetu kwa faida yetu.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 2, 2010.

Ijue sinema ya BoT na ufalme wa majizi

HATIMAYE ile sinema maarufu ijulikanayo kama Bunch of Thieves (BoT) imekwisha! Sinema hii maarufu yenye kila ukatili, ujambazi, upofu, ufisi, ufisadi, utaahira, uhujumu na kila aina ya jinai ilitungwa na Benny (Hyena) M. Kappy.

Katika sinema hii Jackal (Mbwamwitu) Kwetty anakabiliwa na mtihani mkubwa wa kusaka ufalme katika nchi ya Thugsland.

Watu wa Thugsland hupenda sana kuitana majina ya wanyama. Hivyo msishangae kuona majina ya wafalme hawa wawili ambayo kimsingi yanawasilisha tabia na hulka zao.

Kwetty hana pesa wala sera zaidi ya sanaa na longo longo katika azma yake ya kukalia kiti cha enzi cha ufalme. Hana ajenda wala mpango wowote zaidi ya kukamia kukwapua kama hana akili nzuri. Anautaka ufalme kwa udi na uvumba ingawa hana lolote la kuwafanyia wananchi zaidi ya kuwaingiza kwenye matatizo.

Katika kampeni zake za kuusaka ufalme, anaahidi pepo itakayogeuka jehanamu huku akiwahonga waandishi wa habari, wanajeshi, polisi na wengine wenye nafasi anaowapa vyeo kama fadhila jambo ambalo baadaye linakuwa tatizo sugu na hatari kwake.

Katika kufanikisha hili, maskini Kappy anaamuru hazina ya nchi iibiwe ili kupata pesa ya kuendeshea mipango ya kuupata ufalme kwa Kwetty, ambaye baadaye atalipa fadhila kwa kumkingia kifua mfalme.

Kappy kutokana naye kuhomola kama hana akili nzuri hasa akiongozwa na bi mkubwa wake Anatamaa. Kwa kujua alivyomesi, anaamua kuingia mkataba wa siri ili kuepuka kunyea debe baada ya kukabidhi taji la ufalme. Mpango huu mchafu unaratibiwa na jizi maarufu liitwalo Devil Lally akisaidiwa na jizi jingine liitwalo Matus Yumby.

Majizi haya yanafanikisha ujambazi huu kwa ujuha na ukatili sana kiasi cha wananchi wa nchi ya Thugsland kuachwa midomo wazi hasa pale Kwetty anapomfikisha mbele ya makuhani wajulikanao kama maruhani, Yumby.

Kinachowakera ni ukweli kuwa Yumby hafikishwi mahakamani ili haki kutendeka bali kuwahadaa wananchi na kuichezea shere mahakama inayotumika kama kikaragosi cha kubariki ujambazi na jinai za watawala!

Wakati Yumby akifikishwa mbele ya makuhani, Lally anayeyuka kinamna na kuacha zigo lote kwa Yumby. Anatokomea ughaibuni na hajulikani alipo.

Mchezo huu mchafu unapewa jina la EPA yaani Enabling Profiligacy Action. Chini ya mpango huu, yanaundwa makampuni hewa na kwenda benki na kukwanyua njuluku zinazowekwa kwenye akaunti mbali mbali za Chama Cha Maulaji (CCM) siyo chama cha mapinduzi chonde chonde) ambacho baaadaye kinawahonga wananchi na kunyakua taji la ufalme.

Mchezo mzima unaishia mbele ya baraza la makuhani linalokaa kwenye mji wa Kisooty na kufanya kile ambacho kila mmoja alikitegemea kutokana na mazoea ya kulindana na kufugana kwenye bahari ya mapapa wa ufisadi.

Pesa inatembezwa na siku ya siku Yumby anayewakilisha watawala wezi anashinda kesi kwa kupewa adhabu ya kifungo cha siku mbili. Umma wa wananchi unamwaga machozi na vilio kutawala wakililia hazina yao iliyobunguliwa huku makuhani na wakuu wakichekelea kwa ushindi ambao ni dhahiri, utaiangamiza nchi ya Thugsland.

Pamoja na ushindi huu bado wananchi wanajua kilichofanyika na kama si woga walikuwa na kila sababu ya kuwatia adabu mafisadi hawa wanaotumia sheria kama karatasi za chooni.

Baada ya makuhani kupinda na kunyea sheria, wananchi wengi wanasikika wakilaani sheria chafu na makuhani wachafu walioamua kuitumia sheria kujinufaisha kwa kuwaletea nakama umma.

Wakati hitimisho la sinema hii yenye kusikitisha na kuamsha hasira likifikiwa, mambo mengi ya ajabu yanaonekana. Mfalme bado anajipiga kifua kuwa ameweza kuleta haki ilhali ameipora na kuitukana. Amevunja na kutumia sheria vibaya. Lakini bado anajipa matumaini kuwa anatawala kwa sheria na haki wakati ukweli ni kwamba anatawala kwa vurugu na ujambazi.

Kinachokera zaidi ni kusikia walamba viatu na wapiga filimbi wa mfalme wakimsifia upumbavu badala ya kumwambia ukweli kuwa haki haijatendeka.

Katika sinema hii kuna kibaraka mmoja aitwaye Bogus Lemar. Huyu bwana amekuwa changudoa wa mfalme hakuna. Ameuza kichwa chake na mwili wake kiasi cha kusifia kila uchafu wa mfalme kiasi cha wananchi kuongeza jina Bogus yaani hovyo kwenye jina lake.

Msomi mmoja aitwaye Wheelbarrow Weapon, ambaye ndiye aliyefichua uchafu wa wafalme hawa bazazi anasikika akisema, “tumeliwa”. Je, nani atamsikiliza iwapo matumbo yameteka vichwa kiasi cha makamasi kutumika badala ya ubongo? Hii ndiyo hali ya kusikitisha ya nchi ya Thugsland.

Pamoja na kelele na vilio vyote, mfalme ameziba masikio na kuendeleza uharibifu wake. Hakuna alichowahi kufanikiwa tangu anyakue taji zaidi ya kuliangamiza taifa.

Anatumia na kuponda atakavyo huku wananchi wakipondwa na umaskini na mateso makubwa. Yeye na ukoo wake wanafaidi ufalme ukiachia mbali walamba viatu na wadandizi kila aina wanaoimba utukufu wa mfalme katikati ya maangamizi.

Badala ya kuwa mfalme wa watu wote, mfalme amegeuka mfalme wa wezi na fisi wachache aliojizungushia bila kujali kinachoendelea nje ya genge hili hatari kwa mustakabali wa taifa!

Kuna kitu kimoja kimejidhihirisha vilivyo kwenye filamu hii. Ni ile hali ya mfalme kuwa kipofu kiasi cha kutumiwa na wachumia tumbo wenye hata uwezo mdogo wa kufikiri kiasi cha yeye kujijengea mazingira magumu siku taji likimtoka.

Na yote hii imesababishwa na mfalme kutawala kwa kuangalia nyuma badala ya mbele. Amejijengea sifa za ajabu na umaarufu wa kipuuzi kiasi cha kushindwa kusoma alama za nyakati! Anaalika vurugu asijue kwenye vurugu hizi muathirika wa kwanza anaweza kuwa yeye. Tumewaona wangapi tena wenye akili zao.

Hata hivyo inatia faraja kugundua usemi maarufu kuwa muonee huruma msomi aliyepotezwa na mjinga, sawa na mfalme aliyepotoshwa na walamba viatu vyake au hata mkewe na mashoga zake kama Samson aliyepotoshwa na Delilah.

Japo mfalme anajifanya kutosikia, ameishaonyesha wazi kutikisika kiasi cha kuishi kwa wasi wasi.

Hata akisikia mlipuko wa pancha anahaha akidhani wananchi wamekuja kumpa haki yake kwa kuwafanyia mambo mabaya. Ana furaha usoni. Moyoni keshaoza kwa huzuni, majuto na ghadhabu.

Kitambo kidogo kabla ya sinema kuisha, mfalme anasikika akipayuka kuliko hata Mpayukaji mwenyewe. Anaonyesha kukata tamaa na kutokuwa na matumaini ingawa anajipa matumaini kwa kuwapa matumaini hewa wananchi ambao nao wameishamshtukia na kumchoka.

Loh, ngoja nipige mguu mapema. Maana hawachagui pa kupiga. Tukutane wiki ijayo.
Chanzo: Tanzania Daima Juni 2, 2010.