The Chant of Savant

Tuesday 28 April 2015

Mauaji ya albino tuige mfano wa Malawi


        Hivi karibuni serikali nchini Malawi imetangaza hatua za kimapinduzi dhidi ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi. Baada ya kukamatwa wahalifu wenye viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi, serikali imeamuru jeshi la polisi nchini mle kuwapiga risasi watakaokutwa na viungo vya binadamu. Japa wengi wanaweza kuona kuwa hatua hii ni ukiukwaji mkubwa wa haki za bindamu, inabidi wajiulize. Ni binadamu yupi anastahili haki za binadamu kati ya wahanga na wahalifu wanaowawinda na kuwaua watu wenye ulemavu wa ngozi.
Kimsingi, mtu anayewinda, kuua, kumilki, kusafirisha, kuuza na kununua viungo vya binadamu mwenzake si binadamu tena. Hivyo, jinai hii inamuondolea haki za binadamu kutokana na kutenda kinyume na ubinadamu. Siku zote haki huandamana na wajibu. Yeyote anaposhindwa kutimiza wajibu wa kibinadamu, anaondokewa na haki ya kuwa au kufaidi haki za binadamu.
Tatizo la mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini Malawi si kubwa kama ilivyo Tanzania ambayo inasifika kuwa chanzo cha kadhia hii ya kishenzi na kinyama. Pamoja na udogo wa tatizo, mamlaka nchini Malawi zimeonyesha nia na utashi wa kupambana na tatizo hili hasa kulikomesha. Hii maana yake ni kwamba sisi Tanzania tumezembea. Je kwanini Malawi wamechukua hatua hii ambayo kwa serikali huwa mara nyingi si rahisi kuichukua tena ndani ya muda mfupi?
Kwanza, wanajali haki za binadamu ambapo uhai ni haki kubwa ya binadamu kuliko zote. Pili, wanawajali raia wao kiasi cha kuwa tayari kujiweka kwenye nafasi ya kulaumiwa kwa kuchukua hatua kali hivyo. Tatu wanajua madhara kwa watu binafsi na taifa yatokanayo na mauaji haya ya kinyama na kishenzi yatokanayo na ujinga, roho mbaya, ushirikina na tamaa ya utajiri wa haraka tena bila kutumia maarifa wala kufanya kazi halali. Nne, wanajua madhara ya kadhia hii kwa sifa ya taifa. Malawi ina mottoisemayo kuwa Malawi is warm heart of Africa. hawapendi sifa hii ichafuliwe na yeyote. Na anayejaribu kuichafua havumiliki na serikali itatumia mbinu na sheria yoyote kuhakikisha hili halifanyiki. Je Tanzania sisi motto yetu ni ipi? Kusema ukweli sijui kama tuna kauli mbiu au motto ya kutangaza taifa letu ambalo limegeuka kusanyiko la watu wa hovyo, mafisadi, wezi, majambazi, wauaji, waongo, wanafiki na wababaishaji.
Maana ukiangalia tangu mauaji haya yaanze na hatua ambazo serikali ya Tanzania imechukua, unagundua uhovyo na ukatili wetu kitaifa na sasa kimataifa kutokana na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi kusambaa nchi jirani. Malawi ni taifa la pili jinai kukumbwa na kashfa hii ya “kitanzania”. Nchini Burundi vimewahi kuripotiwa vitendo vya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi. Shirika la habari la Reuters likikariri taarifa ya Umoja wa mataifa limeripoti kuwa watu wapatao 15 ima wameuawa au kushambuliwa ndani ya  mitatu katika nchi za Burundi, Malawi na Tanzania. Hii si idadi ndogo hata kama ingekuwa ya faru au tembo. Hii si idadi ya watu tu bali watu waliopoteza maisha kwenye mikono ya wanyama waitwao binadamu wenye tamaa ya kutajirika hata kwa kukatiza uhai wa wenzao bila hatia. Malawi imeamua kupambana na tatizo bila kusita wala kificho kwa kuutangazia ulimwengu kuwa itawapiga risasi watakaokutikana na hatia hii ya kuua, kumilki, kusafirisha, kuuuza na kununua viungu vya binadamu. Mkuu wa jeshi la polisi nchini Malawi, Lexen Kachama alikaririwa akitoa amri kuwa askari, “wapige risasi, wahalifu hatari watakapobainika kuwateka watu wenye ulemavu wa ngozi.” Reuters inaripoti kuwa tangu mwaka huu kuanza, watu wenye ulemavu wa ngozi wapatao 10 wameishauawa nchini Malawi. Kachama aliongeza kusema, “Hatuwezi kuangalia tu wakati rafiki zetu wenye ulemavu wa ngozi wakiuawa. Tumegudua kuwa wahalifu hawa ni katili na hawana huruma hivyo washughulikiwe hivyo hivyo.” Kwa maana nyingine, Malawi imeamua kutumia sheria ya jino kwa jino na dawa ya moto ni moto. Wakati mwingine tunahitaji kukabili baadhi ya matatizo kulingana na uhalisia wake. Waingereza husema, “Extraordinary problems need extraordinary solutions” yaani matatizo yasiyo ya kawaida uhitaji suluhu zisizo za kawaida.
Kama tutakuwa makini na wakweli kama taifa, basi mauaji katili na ya kinyama ya ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi yanapaswa kushughulikiwa bila huruma kama ilivyotangazwa nchini Malawi. Hatua iliyochukuliwa na Malawi –pamoja na utata wake kwenye macho ya watetezi wa haki za binadamu –ni ya kuigwa hasa ikizingatiwa kuwa wauawaji wa watu wenye ulemavu wa ngozi ni katili na wasio na utu. Hivyo, tunapowashughulikia tunapaswa kuweka utu pembeni.
Tumalizie kwa kuitaka serikali ya Tanzania ichukue hatua kama hizi ambazo zinaonekana na kuingia akilini badala ya siasa na usanii wa kuwaita viongozi wa watu wenye ulemavu wa ngozi ikulu na kupiga picha nao huku wakiendelea kuangamia. Mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi yanahitaji ujasiri na utashi wa hali ya juu unaozingatia thamani na haki za binadamu. Tanzania isipobadili mbinu yake ya kupambana na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi, basi wana harakati za haki za binadamu waifungulie mashtaka kwenye mahakama ya jinai ya kimataifa ili iweze kuwajibishwa iwalinde raia wake dhidi ya wauaji wasio na huruma wala utu.
 chanzo: Tanzania Daima Aprili 29, 2015.

Kijiwe chaasa wachovu kuchukia na kufanya mabadiliko


          Tukiwa tunahuzunika tokana na ajali za barabarani zilizosababishwa na ufisadi na utawala mbovu si tukazinyaka kuwa kuna majambazi makubwa yameingia kaya mkengeni kwa kupiga mabilioni. Inshu yenyewe ni kwamba washenzi hawa wenye roho za kinyama waliagiza mabehewa mabovu wakapandisha bei yake na kudai ni mapya wakati si kweli. Tulistuka kusikia kuwa waziri Sam Sixx amewasimamisha kazi badala ya kuwatupa lupango wakingojea kunyongwa.
Mgosi Machungi anaingia akiwa amekunja ndita kana kwamba atapiga mtu zongo. Anafungua moyo na kuronga, “Jamani mimesikia huu ujambazi wa bandaiini ambapo majambazi yamepiga njuuku kwa kununua mabehewa mikangafu na kudai ni mapya?” Kabla ya kuendelea anachomoa gazeti mkobani na kutupa tusome wenyewe nyuzi zenyewe.
Mipawa anadakia hata bila kusoma gazeti, “Huyu Sixx naye ni msanii. Kwanini asiwatupe lupango kwanza huku mali zao zote zikikamatwa ili kuchunguzwa wakiwa wanapoa lupango?”
Kapende anadakia, “Lupango ni kwa wezi wa kuku na vidokozi wadogo wadogo na vidagaa lakini si kwa mapapa.”
Msomi Mkatatamaa anadakia, “Ni kweli kaya imeibiwa jumla ya madafu bilioni 230 ukiachia mbali mabehewa husika kuletwa kutupwa kayani ambayo licha ya kupata hasara imegeuzwa dampo la taka hizi hatari. Nakubaliana na wachangiaji wanaotaka wahusika watupe lupango hata kunyongwa bila kungoja kupoteza muda kwa ndata kufungua kesi potofu na kuwapa mwanya majambazi hawa kushinda na kudai fidia.”
Kabla ya kuendelea, mheshimiwa Bwege anakatua mic, “Usemayo Msomi ni kweli. Kesho utasikia wamefikishwa mahakamani kama akina Idd Lion waliofilisi UdA na kuitwaa kwa kuwaweka vidhabi wachovu kujifanya ndiyo wamilki wakati wamilki wanajulikana kuwa ni akina Riz na wanene wengine.”
Anakoho kidogo baada ya kashata kumkwama na kuendelea, “Hapa hafungwi wala kushitakiwa mtu hasa ikizingatiwa kuwa ujambazi huu unawahusisha wakubwa wenyewe wanaojifanya kuushupalia.”
“Yakhe nasikia presha yanpanda Wallahi. Yaani wajalaana wajiibia kana kwamba hii kaya haina mwenyewe! Waleta mabehewa 150 kudampu hapa huku wakituibia na njuluku kana kwamba sie vichaa!” Mpemba analalama
Sofia Lion aka Kanungaembe anaamua kukwanyua mic, “Jamani nyie mmeingiliwa na nini? Yaani hamngoji sheria ichukue mkondo wake? Kwanza, mna ushahidi gani kuwa hayo mabehewa ni mikangafu kama si kuzuazua?”
Kabla ya kuendelea Mgosi anamchomekea Sofi, “Da Sofi ngoja nikuchomekee. Kwei wewe ni wa kutiambia kuwa timeiingiwa na nini?”
Sofi hangoji, anakatua mic, “Halo Halo! Mmesahau ambavyo mmekuwa mkiniambia nimeingiliwa na nini siyo? Ama kweli mkuki kwa nguruwe!” anaangua kicheko huku akimtazama Mgosi anayeonekana kuudhika dhahiri.
Kanji anaamua kutia guu, “Kwanini Swahili penda tafsiri witu tofauti?  Mimi siku yote sikia ingiliwa ingiliwa. Sasa tatizo nini?”
“Kweli Kanji huwezi kuona ubaya hasa ikizingatiwa kuwa hii mikangafu imenunuliwa toka Bombei. Yaani kaya hii imegeuka shamba la bibi la magabacholi kupiga njuluku watakavyo.” Analalamika Mchunguliaji anayesoma gazeti kwa makini utadhani anatafuta majibu.
Mpemba anarejea, “Yakhe mie nshangaa sana. Yaani kaya imegeuzwa dampo la India. Mabehewa feki India. Madawa feki, India. Wawekezaji feki, India, vyangudoa wa kuja kwa kisingizio cha kucheza nziki bhangra na banjan nao watoka huko huko. Hata kunguru nao watoka huko huko kunani jamani?”
Kanji anastuka kusika Mpemba anavyotaja mitindo ya miziki ya kigabacholi. Anauliza, “Kumbe veve Pemba jua myuziki ya India! Iko veve ongea hindi?”
 Mpemba anajibu kwa kihindi, “Tame mari sathe dance karso yaani unataka kucheza muziki nami?”
Kanji anajibu, “dhanvaad yaani asante.”
Mpemba anajibu tena, “Tamaarūṃ svaagata cha yaani shukrani nawe.”
Kijiwe chote kimepigwa butwaa na jinsi Mpemba anavyokirudi kigujaraati.
Msomi baada ya kuona lugha gongana zinataka kupoteza mada anaamua kula mic,, “ Ami na Kanji tunawashukuru kwa kugonganisha lugha ingawa bado hamjaleta suluhu ya mada iliyoko mezani.” Anamgeukia Kanji na kusema kwa kigabacholi, “manne maaf karo yaani samahani na kuendelea. Nami nakimanya japo si sana ila hili si muhimu kwa leo. Turejee kwenye mada kwa kutoa shinikizo kwa lisirikali jizi liwashughulikie hawa majambazi wake vinginevyo tuingia mitaani au vipi?
Mipawa anakula mic, “Mie sidhani kama hawa mapapa watafungwa. Nani awafunge wakati wote lao moja? Jiulize akina Rugemalaya na Seti Singasinga wa wa escrew wako wapi zaidi ya kuwa mitaani wakipiga dili nyingine za kuiba kutumia bandari ya kule kwa akina waja leo waondoka leo?”
Mgosi anadandia, “Usiniumize ndugu yangu. Hata mimi sitegemei wezi wa HEPA wawashughuikie wenzao wa escrew. Nakubaina nawe lao moja.”
Mzee Maneno anachomekea, “Mie bado namuamini mzee Sam Sixx kwa vile ni mtu wa viwango.”
“Viwango ilikuwa zamani. Leo naye keshaingia kwenye maji taka. Mara hii umesahau alivyoua katiba ya mzee Jose Waryuba ya wachovu? Naye ni fisadi kama wenzake kwenye genge lao. Kwangu mle hakuna msafi hata mmoja bali unafiki na usanii mtupu.” Anajibu Kapende huku akikamua kahawa yake.

Kijiwe kikiwa kinaendelea si tukasikia king’ora cha treni ya kuelekea bara. Tuliamua kwenda kusimama relini kupinga hiyo mikangafu isitumike hadi kieleweke.
Chanzo: Tanzania Daima Aprili 29, 2015.

Hawa ndiyo wanaojua kupambana na wauza unga

Monday 27 April 2015

Kufungwa mtoto wa rais somo kwa marais watoto

  • Abdoulaye Wade y Karim Wade
    Rais wa zamani wa Senegal Abdulaye Wade na Mwanae Karim wakati akiwa madarakani
   Kupatikana na hatia ya wizi wa fedha za umma na kuhukumiwa kifungo kwa mtoto wa rais wa zamani wa Senegal, Karim Abdulaye Wade kuna mafunzo mengi.
Kwanza, kila kitu kina mwisho chini ya jua. Maana jinsi Karim na baba yake walipokuwa madarakani walionywa mara nyingi wala hawakusikia cha muadhini wala mteka maji kwa vile madaraka mara nyingi hulevya. Hawakuamini kuwa madaraka yangefikia kikomo siku moja.
Pili, cheo ni dhamana. Hili liko wazi sema watu wengi wanapoyapata hulewa na kujisahau. Badala ya wengi kutimiza dhamana waliyopewa na umma huutumia umma kujineemesha wasijue wengine wanaweza hata huo utajiri waliouchuma kwa kuuibia umma wanaweza wasiufaidi kama ilivyotokea Libya.
Tatu, Afrika inahjumiwa na waafrika wenyewe hasa wanaotumia madaraka vibaya pamoja na wake, watoto, marafiki na waramba viatu wao.
Nne, wakati mwingine usomi wa mtu hauondoi ujinga wake. Rais wa zamani Wade ni profesa tena wa sheria lakini aliyeivuja na kuivunja sheria vibaya. Rejea maprofesa wetu hapa nchini walioboronga hadi wengine kuondolewa kwa kashfa za upokeaji vijisenti na kusimamia wizi wa fedha za umma.
Karim, kama Seif al Islam Gaddafi, alikuwa akiandaliwa kumrithi baba yake. Alipewa uwaziri kwenye serikali ya baba yake.  Alifika pale alipofika si kwa sababu ya sifa nyingine zaidi ya kuwa mtoto wa rais. Je Afrika inao akina Karim wangapi ambao hawajahukumiwa lau kupata stahiki ya jinai walizotenda? Je ni wangapi wamejifunza tokana na anguko hili takatifu?
Baada ya kuondoka wakoloni weupe wakawaachia mamlaka wakoloni weusi, kuwa rais Afrika maana yake ni kwamba ukoo wote unakuwa marais kwa namna wawezayo. Wake za viongozi japo si wote wanaunda kampuni almaaruf NGO na kujipatia utajiri wa ghafla kwa kutumia mgongo wa ikulu. Kulipana fadhila na udugu, kujuana na kulindana vinachukua nafasi kiasi cha kushindwa kutofauti kati yao na genge la wezi. Wengi wa marais wameruhusu wake au watoto au marafiki zao kuwa karibu kila ufisadi unaotendeka kwenye mataifa yao. Mtoto wa rais Congo Denis-Christel Sassou Ngweso anasifika kujihusisha na karibu kila kashfa inayohusisha mabilioni ya dola nchini humo. Mtoto wa rais wa Afrika Kusini, Duduzane Zuma anasifika kwa kushirikiana na familia ya kihindi ya akina Gupta kujipatia utajiri wa kutisha. Ilifikia mahali hata akaruhusu ndege binafsi ya wahindi hawa iliyobeba maharusi kutua kwenye kituo cha kijeshi kinyume cha sheria na hakuna kilichofanyika. Binti wa Zuma, Thuthukile (25) alipewa kazi ya ukuu wa watumishi kwenye Wizara ya Posta na Mawasiliano nafasi ambayo hajawahi kupata mtu kwenye umri huu bila uzoefu wala elimu ya kutosha. Kama haitoshi, mpwa wake Zuma aitwaye Khuhulubuse Zuma anakabiliwa na tuhuma za kufilisi shirika la umma la Aurora ambapo alikuwa ameteuliwa na ndugu yake kuwa mwenyekiti.
 Bado dunia inakumbuka jinsi watoto wa rais wa zamani wa Kenya Moi walivyojitajirisha kwa vile baba yao alikuwa rais.
Karim sasa ni mfungwa baada ya kupatikana na hatia na kuhukumiwa kwenda jela miaka sita. Mwezi Machi umekuwa mbaya kwa watawala wa kiafrika. Kwani mke wa rais wa zamani wa Ivory Cost, Dr. Simone Gbagbo alihukumiwa kwenda jela miaka 20 wiki moja kabla ya Karim.
Hata hivyo haya matukio yanatukumbusha kitu kimoja kikubwa kuwa bara la Afrika mara nyingini ni maskini si kutokana na ukosefu wa raslimali wala wachapakazi bali usimamizi na utawala bora. Viongozi wengi wa kiafrika wameruhusu ndugu na marafiki zao kuzihujumu nchi zao kwa kupewa vijirushwa kidogo wakati wanaowatumia wakijiingizia mabilioni ya dola na kuyatoroshea nje huku wakiliacha bara maskini huku watawala wake wakisifika kwa kuombaomba na kukopakopa. Wengine hata hicho wanachoomba hakifikishwi nyumbani zaidi ya kuachwa huko huko ughaibuni kwenye mabenki almaarufu kwa kuficha fedha.
Somo jingine unaloweza kupata kutokana na kufungwa kwa Karim ni kwamba upinzani unaposhinda na kuingia madarakani, uwezekano wa kubadili mambo ni mkubwa ingawa hili siyo mia kwa mia. Nchini Kenya, upinzani ulipoingia haukuwachukulia hatua Moi na watoto wake. Tofauti, nchini Zambia, Fredrick Chiluba na mkewe walichukuliwa hatua za kisheria hadi bi mkubwa kuonja jela. Nchini Malawi mambo yamekuwa nusu kwa nusu kuhusiana na tuhuma zilizomkabili rais wa zamani Bakili Muluzi.
 Tuhitimishe kwa kushauri wahusika watie akili wakijua fika kuwa hakuna kisichobalika chini ya jua. Leo wanakula kwa kujidai wengine hata bila kunawa. Wanatanua kwa msemo wa kisasa, wajue fika mwisho ukifika wanaweza kuishia pakanga. Pia wafahamu kuwa upogo na uroho wao ndicho chanzo cha bara letu kuwa maskini, kukosa usalama na maendeleo. Kuna maisha baada ya kuondoka madarakani. Pia tuwasihi wananchi kuanza kuchukia huu utawala wa kifalme wa kisiasa unaorejeshwa kwa mlango wa nyuma.
Chanzo: Dira.

Sunday 26 April 2015

Is ours a criminal hunk?


          Don’t think I’m writing this because of kanywaji and ganja. Nay, I've strong and healthy reasons to embark on becoming a big criminal aka a big thug, you may call it. I reached this stance after discovering that in our hunk is crime friendly. Steal ducks and chickens, you’ll end up rotting behind bars. Ironically, if you steal billions, you become mhishimiwa in your own light. Ask nshomiles Rugemalayers, Anna Kajuamlo, Sauce pie Muongo, and Andy Chenge, Rost Tamu l’Aziz of Kagoda, Jake Kiq’ette, A Liar Maswiswi and singanga Seti. They made a killing out of the blue; and they’re now honourable dining and enjoying their loots with kings as boozers gasp with throes. Mince no words. Mmeigeuza kaya ya wahalifu pointlessly!
That I’m smart, I’m pondering about becoming a big thug so that I can rob big bucks and get away with it in the hunk of criminals. What’d I fear if everything is ruksa? If it were under mzee Mchonga, I’d not think of becoming a big thug. How’d I while the Mchonga used to employ spies to check on how many beers swallowers were able to buy? Spies used to spend much time in the watering holes counting corks of the beer one’d swallowed. Thereafter, they’d squeeze the guy to know how he made his dosh. Failure to substantiate, firstly, his loot’s taken –and then –he’d rot in the cage for sabotaging the hunk. Currently, one can steal, rob, and plunder as wishes without getting in troubles. Currently, criminal do kill people with albinism to meet the requirements of the conmen who order them to do so promising them to hit the jackpot. Those foolish and illiterate conmen are duping you. Stop it. Mtamaliza mazeruzeru bure and you won’t become rich. Work diligently, wisely and hard or rob the govt. Why are you turning our hunk into the den of adulterous and criminals wantonly?
I know. Doubting Thomases will doubt my project thinking it is the result of hangover and ganja. I tell them point blank to go and see those folks mentioned above. Robbing the hunk does pay. All paupers you evidenced suffering before their god came to ulaji are now stinking billionaires thanks to this crime of robbing the hoi polloi of this God-forsaken hunk aka Danganyika aka Bongolalaland aka Bongo-Bongo.
Those doubting that criminality does not pay in this criminal hunk should go and ask the bigwigs who forged their academic credentials. Some are shamelessly and undeservedly referred to as doctors while they’re but quacks and forgers. Makorongo Muhanga, Marry Nyagu, Bill Luku-vii, Emmy Nchimvi, Diodolorous Kamala, Addymu Malima and Saaaada Mkuyati know this too well.  The other day I read the CVs of Mkuyati and Malima how they got their Master’s degree after completing form four and ended up drinking like a fish to calm my anger. You know. We, morani feed on kiroriti. So, when our angers swell, we just get kanywaji to avoid taking jambia and slash somebody’s head in broad daylight.
 Remember Ukafiri Dar si Salama aka UdA. Do you know that some criminals took it despite the parliament opposition to this theft? Nobody’s ever pooped in the bucket at Ukonga or Segerea. Instead, criminals behind this holdup are minting and printing dosh using the same UdA.  Little bird confided me that there’s a bigwig or his son behind UdA graft.  See? Doesn't criminality pay in our hunk? Go to local govts, airports, border points, harbours, immigration, TrA, Bunch of Thieves (BoT) littered with vigogo’s children and everywhere dosh’s made quickly and see how the paupers of yesterday are the billionaires of today wantonly. Those unsatisfied can go ask the putas selling fake drugs such as Rama Madabidabi and others what happened to them after their dirty linens were put on the agora. Nothing, they’re still importing even bigger quantities of the poisonous and sell it to boozers they kill like people with albinism. Thanks to their greed and heartlessness.
If you still can’t believe, go to the dungeons and interview those behind bars. Most of them are chicken thieves, petty offenders and those jailed on fabricated cases which cops know how to do too well.
Guess what. Did you just recently hear that some connected criminals working in the Tanzia Harbour Authorities bought old wagons they called new and advanced? Don’t ask me what befell them for committing such sacrilege. I read somewhere that the minister responsible suspended them. Suspend them! Why not slit their necks so that other can get the message? Again, who is to reprimand who while they all are in the frenzy of eating almost in every office? Do you remember the MPigs sorry MPs implicated in the scam of asking for kickbacks from local govt officials so that they can pass their audit reports? One of them was ironically appointed a mini minister before the hand of God chipped in. Grrrr, this is but a criminal state!
Source: Guardian April 25, 2015.

Saturday 25 April 2015

Mlevi kuanzisha kanisa ili anunue Boieng


          Baada ya kugundua kuwa jina la bwana God linalipa, basi mzee mzima nasukuti kuanzisha kanisa la Upendo, Furaha, Uzima Fanaka na Utajirisho, Kupitia Ombi (UFUFUKO). Katika kuhakikisha napata njuluku toka kwa walevi na wachovu waliokata tamaa kiasi cha kuamini kila anayewaingiza mkenge kwa kisingizio cha kutatua matatizo yao, nitahubiri utajirisho wa chap chap bila kulazimika kuingia kwenye jinai kama EPA, Richmonduli, escrow an MWAPORC inayonukia kule kwa akina waja leo waondoka leo Mwambani.
Ili kupata njuluku ya kutosha, nitawalenga akina mama ambao bila shaka ni wengi kayani. Nitahubiri jinsi ya kuimarisha ndoa, kupata mtoto na kupendwa na waume zao ili wawachune vizuri. Si utani. Kama huzai au umechelewa kuzaa we njoo kwangu utapata mapacha idadi unayotaka hata kama ni kuzaa kumi kwa mpigo. Hakuna lisilowezekana kwangu.
Kama haitoshi, nitauza CDs zangu zenye mahubiri yangu ya urongo na ukweli bila kusahau maji upako, vitambaa vya baraka na kanda zangu za video nikihubiri. Nitawaingiza mkenge watakaopwakia huduma sorry hujuma yangu kuwa ninafanya miujiza ambayo haijawahi kufanywa na yeyote.
Naona yule anatikisa kichwa akidhani hii ni mipango ya bangi asijue wapo wengi ambao wameishaula kirahisi kama marais kwa kujificha nyuma ya neno la bwana. Nani mara hii amesahau kuwa kidhabu mmoja kule Nigeria aitwaye TB Joshi sasa ni bilionea wa kutupwa tokana na kuwaingia mkenge wajingawanjinga wasiojiamini? Pale Kenya yupo rafiki yangu Vickie Kanyare anayehubiri radioni na kwenye runinga huku akipanga matapeli kutoa ushuhuda wa uongo radioni na kwenye runinga ili kuwavutia wajinga? Kwani hapa Bongo hawapo? Mbona wengi tena wengine walitumia huu usanii hata kuupata uheshimiwa. My friend Get Rwakatarehe hupo hapa? Wengine wameula hadi wakanunua hata vyelikopta na kuishi kwenye mahekalu huku wachovu makapuku na wajinga wanaowachuna wakitembea hadi kanda mbili kuwakatikia wakingojea miujiza uchwara. Hapa my friend Jose Gwaijimama utakuwa unanipata vilivyo au vipi?
 Kwa vile kaya hii ni ya walevi mazezeta na washirikina, lazima utumie ujinga wao kupiga njuluku au vipi? Najua mwezi wa kumi lazima nitaukata kama sina akili mbaya hasa pale nitakapoanza kuhubiri kutenda miujiza ya kisiasa ambayo inawabadili wapiga kura kukupigia kura ya kula hata kama hawakupendi. Ukija kwangu utapendwa hata na ndege watake nao kukupigia kura ili ule dezo kama wengine ukiachia mbali kuitwa mhishimiwa hata kama u muishiwa au MPig kama wawaitavyo jamaa zangu wa kaya ya Nyayo pale jirani. Nilishasema tangu zamani. Huna haja ya kwenda Bwagamoyo au Sumbawanga wakati mtume mwenyewe wa walevi nipo na nimepata ufunuo toka kwa mwenyewe top. Usiende huko unakotakiwa uwapelekee mifupa ya wenye ulemavu wa ngozi na ndevu za bibi yako na mkojo wa kuku. Kwangu ni rahisi kupata hata urahisi, uhishimiwa hata kuteuliwa ukuu wa mkoa na wilaya. Huna haja ya kufanya kazi chafu kama vile kuwashambulia akina mzee Jose Waryuba ndiyo uteuliwe ukuu wa wilaya. Uhitaji kupoteza njuluku kwa makanjanja wajifanyao diaper aka nepi kujikomba kwa wakubwa wakiwatungia vitabu vya kipuuzi vya kuwasifia au kuandika makala za kuwasifu magazetini wakisaliti taaluma yako na kuzika heshima na utu wao. Njoo kwangu uokoe njuluku yako na kashfa na aibu ya kulipa fadhila baada ya kuupata ukuu kwa njia haramu kama yule jamaa yangu Jambazi Kuu (JK). Uhitaji akina Makondokonda wala Rweyependekezamu na matapeli wengine kama hawa. Uhitaji akina Bagendagenda wakutungie vitabu ambavyo hata ndege akisoma anajua ni njaa kujikomba na utapeli.
Kwa wanasiasa habari hii ni njema kuliko zote. Kama una mshiko wako unaweza kutumia jina langu kununua chopa ya kupigia kampeni zako.  Wafanyabiashara wanene wanene njoo kwangu niongeze utajiri wenu. Nafanya miujiza kweli. Guess what. Ni simple. Kwa vile dhehebu langu litakuwa linapewa misamaha ya kodi kwa vitu nitakavyoingiza kayani, basi njoo kwangu tuongee. Dili lenyewe liko hivi, unatumia jina langu kuagiza mali zako. Zinapita bila kutozwa kodi. Wewe unanikatia cha juu unatajirika nami natajirika. Kwani kuna mbaya kuibia kaya ya mazoba?  Je huu si muujiza kweli? Huna haya ya kusumbuana na kutolewa upepo na maafisa wa TrA wakitaka chao. Mie nakutoza kidogo tena nakuombea biashara zako ziongezeke kama mchanga wa bahari. Njoo upate muujiza wako.
Wanafunzi mashuleni na vyuoni hamna haja ya kuteswa na walimu na maprof uchwara. Wala wazazi hamna haja ya kununua pepa feki kama walivyofanya magabacholi huko Ugabacholini hivi karibuni kiasi cha kuwa kivutio kwenye mtandao. Njooni kwangu nitawaombea mshinde mitihani yenu. Wazito vihiyo wanaotaka waonekane wasomi hamna haja ya kuhonga vyuo viwape shahada za dezo wala kuingizwa mkenge na vyuo feki vya ughaibuni. Njoo kwangu niwapige dua mpate shahada zenu kimiujiza.
Kwa vile ulimwengu wa sasa ni wa sayansi na teknolojia, huna haja ya kuja kanisani kwangu kutoa fedha. Wewe tumia M-pesa tu na fedha ikishaingia nipigie simu nianze kukuombea uondokane na matatizo yako. Wale wala rushwa na mafisadi wanaoogopwa kutolewa upepo na Takokuru, njoo kwangu nitawadhibiti Takokuru. Kama wameishapata habari zako za kukwepa kodi au kula rushwa nitakuombea dua wakusahau na wakikuona wakupende uendelee kupeta na kutesa. Wauza bwimbwi, hamja haja ya kutolewa upepo uwanja wa ndege. Njoo kwangu niwapige na dua ya kuwafumba macho hao mafisi wa uwanjani waliotajirika kishenzi kwa kuwatoa upepo. Lo! Kumbe muda umekwisha hivi!
Wajinga ndiyo waliwao. Nisipowala mimi mjanja wataliwa na matapeli uchwara na wajinga wenzao. This is a man eats man country of No Brainland.
Tumalizie na yetu uliye mbinguni kwa kizulu baba :
  Baba wethu osezulwini
 Maliphathwe ngobungcwele igama lakho.
 Umbuso wakho mawufike.
 Intando yakho mayenziwe emhlabeni njengasezulwini.
 Awusiphe namhla isinkwa sethu semihla ngemihla.
 Usithethelele izono zethu
 Njengoba nathi sibathethelela abasonayo.
 Ungasingenisi ekulingweni
 Kodwa usisindise kokubi.
Chanzo: Nipashe April 25, 2015.

Wednesday 22 April 2015

Hii comment ya msomaji imenifurahisha sana

Anonymous said...
Mwalimu Mhango,Bwana Mola azidi kukulinda kwani kalmu yako imekua ni silaha ya kuwatetetea wanyonge daima,lakini tatizo kubwa ni ni kuingiliana kwa maradhi sugu katika jamii ya ulimwengu watu hususa Sub Sahara Afrika ambapo kila aina ya maradhi ya kumfanya mwanadamu adumae kiakili yanazidi kujizatiti nakusudia hapa UMASIKINI na UJINGA na kama ujuavyo umasikini na ujinga ndio mama wa mabalaa yote ya maradhi ya kijamii katika jamii yoyote ile ile duniani na wakati mwingine uwezi kuamini kwa vile maradhi haya yamejikita basi hata wale wenye elimu ya aina moja au nyingine utakutwa wamedhurika na maradhi hayo ebu angalia hawa waumini ambao wanaowatajirisha hawa mbwa mwitu ambao wamevaa ngozi ya kondoo,utawakuta ni wenye elimu zao na vyeo vyao katika serikali na sekta binafsi ambao wanakuja na mavazi ya fahari,magari makubwa makubwa ya fahari na hata michango yao ni mikubwa mikubwa wakiamini kwamba watakuwa na sehemu kubwa katika maisha ya mbinguni.
Kama tulikoloniwa kwa sababu ya ujinga wetu,umasikini wetu na ukarimu wetu leo hii tnakoloniwa na hawa matapeli wanaodai wana miujiza ya kuwafanyia waumini wao ambao wengi wao ni masikini kuliko maelezo.
Mwalimu Mhango tuna safari ndefu sana ya kuweza kupambana na maradhi haya ya kijamii na watu wa aina hii ambao wametoa makucha yao na bila ya huruma kuwaparura wafuasi wao bila ya kujali muda wa kudumu tu wao wanafaidika na wanazidi kufaidika.
NI kweli kabisa kama ulivyoandika kwamba..."Hakuna miujiza katika kufanikiwa au kutatua matatizo yoyote yawayo"maelezo yako haya ni ya kielimu(sayansi) lakini katika jamii ambayo imetawaliwa na ujinga,umasikini na uchawi maelezo haya yanakosa maana kabisa.kwa nini wajanja hawa wategemee katika mahubiri yao au dini yao miiujiza?kwa nini wasiende makaburini kuwafufua wafu arudi duniani na kwenda makanisani mwao ili kuwahakikishia waumini kwamba haya wanayohubiri hawa matapeli ni ukweli mtupu?Bwana Yesu alikuwa anafufua wafu.Kwa nini wasiende katika hospitali za ukoma wakawaponya watagonjwa kama alivyokuwa akifanya Bwana Yesu?kwa nini wasiende shule za vipofu viziwi na mabubu wakawafanye miujiza huko kama alivyokuwa akifanya Bwana yesu?Bwana Yesu alikuwa asubiri kuifanya miujiza yake katika kanisa japo yeye alikua akihubiri na kusali katika nyumba ya kiibada ya kiyahudi (synagogue)Bwana Yesu popote pale ilpohitajika au kuhitajika kufanya miujiza yeye aliwajibika tu bila ya lkusita,lakini hawa matapeli na utapeli wao upo wazi wanafanya miujiza yao makanisani mwao kwa kutumia uchawi,kupanga watu ambao wanakula na kanisa na viini macho.
Mwalimu Mhango sisi bado tupo katika stage ya jamii ya ki primitive na mihimili muhimu ya jamii hiyo ni uchawi,wachawi makuhani,na watu wa dini na kwa bahati mbaya hali hiyo bado inaendelea na itaendelea afrika mpaka dunia kwisha.
Msemo wa Karl Marx hapa una uzito wake "Religion is the opium of the masses."
Mwalimu Mhango ni serikali gani hiyo ambayo unayoikusudia kuwachukulia hatua watu wapuuzi kama hawa?ikiwa serikali inashindwa au inakataa kwa makusudi kuwachukulia hatua viongozi ambao wamebobea katika machafu ya ufisadi unaonuka kaya nzima leo itawachukulia hatua matapeli wa kiroho?Unajua nini nachoongea hapa Mwalimu Mhango.
22 April 2015 at 06:53

Tuesday 21 April 2015

Xenophobia: The Oppressed Become Oppressors

Recently, Media reported barbaric and xenophobic attacks on foreigners in South Africa. Such attacks resulted from a wrong perception that foreigners–who in this case are Africans–caused the miseries especially poverty and unemployment they are facing. Shops and businesses owned by foreign Africans have been facing a spate of attacks whereby the attackers ransack them thinking that such a criminal act would solve their problems.
Again, such attacks have one lesson: South Africans seem to have learned nothing from their history of being persecuted, exploited and discriminated against by Boers. The victims of yesterday are now becoming the perpetrators of the same crime they were fighting against yesterday. South Africans are reiterating exactly the same by attacking foreigners, especially, Africans. Before South African xenophobic eyes, foreigners are Africans from just neighbouring countries but not others such as Indians, Chinese or even Caucasians coming from afar! If anything, xenophobic attacks seem to have all hallmarks of racism.
Xenophobia is stinking racism that embarrasses not only South Africa but also Africa. The difference from racism we’re used to, is that the current one is perpetrated by Africans against themselves. Ironically, Africans are discriminating against Africans and spare non-Africans in South Africa. If the issue forcing South Africans to attack foreigners is an economic one, they need to know and confront the real problems by dealing with those who own their economy especially land that’s grabbed from their ancestors.
Xenophobic attacks in South Africa, if they work, are at the detriment of the same South Africans perpetrating them. Such attacks will frighten other Africans, especially, small scale traders who operate shops that employ many poor South Africans apart from adding to the government revenues. For, instead of confronting the real problem, they’re missing the opportunity to address their real problems by creating pretext and scapegoatism.  Those Africans South Africans are attacking are just innocent and poor people escaping miseries back home. Through their resilience and creativity, they are able to open small business so that they can survive. Their presence can’t be an impediment to their poor colleagues –Africans in South Africans. 
Everybody knows that the South African economy is in the hands of a few whites who used to be favoured by the former criminal apartheid rule before being dismantled in May 1994. Unemployment among blacks is high just like in any other African countries due to being ruled by corrupt and thuggish rulers. The freedom that new South Africa got in 1994 seems to be more political than economic. The big chunk of the majority blacks is still suffering from unemployment, ignorance, diseases and poverty while the minority whites seem to do better comparably.
The solution to poverty and unemployment does not lie in attacking foreigners struggling to make ends meet. Instead, South Africans need to take on their government and urge it to create jobs and educate the people to truly address their problems in right ways instead of attacking others wantonly. Singling Africans out is not only racism but also a misguided move that will not solve the problems but exacerbate them.
Shall such xenophobic attacks go on without South African authorities reigning in to stop them; African countries – whose citizens are targeted – should cut ties with South Africa as a means of forcing the authorities to take decisive actions against such criminality. Jonathan Crush in his article, The dark side of democracy: migration, xenophobia and human rights in South Africa 2001, argues that “South Africa prides itself in having one of the most progressive constitutions in the world. A Bill of Rights guarantees a host of political, cultural and socio-economic rights “to all who are resident in the country.” This means security is a human right for every person residing in South Africa.
This is why we urge African countries whose citizens are attacked and discriminated against to take on the authorities in South Africa reminding them to fulfill their obligations under their own constitution. Why have South Africans forgotten so easily this way? It is only yesterday almost all African countries were sacrificing their economies to support them to achieve independence. Now they’re independent yet they act like Boers who used to discriminate against them. Even the nationality they are fighting for and taking pride in was created by the colonizers in Berlin in 1884 during the scramble for and partition of Africa whereby current African states were curved out at that conference.
According to African sociologist Mike Neocosmos (2008), the recent violence was a manifestation not so much of the xenophobic attitudes of the poor at the bottom of society as of a xenophobic discourse that starts at the top, at the highest levels of the ANC-led state, and is prevalent among the elites – the rising black elite as well as the established white elite – whose interests are the state’s main concern.

If anything, this is where the nexus of xenophobic attack is whereby African elites act like neo-nazis, malanites and Kuyperians. South African should stop whitewashing and witch hunting that have resulted into ignoring xenophobic attacks that have culminated in death and loss of property for innocent people whose sin is being black Africans in a black African country known as South Africa. It shocks and pains beyond comparison to find that some South Africans are dueting with the fathers of apartheid. There must be a rim between black South Africans attacking other blacks and criminals and architects of apartheid such as Abraham Kuyper, Nico Diederichs, Piet Meyer, Geoff Cronje, H.F.Verwoerd and Dr. Daniel François Malan (The Prime Minister who officiated apartheid in 1948).The country of Mandela can’t keep on committing such sacrilege.
Source: African executive Magazine  22.4.2014.

Kama mali za Gwajima ni halali, anahofu nini?

          Askofu wa kujipachika Josephat Gwajima amevutia vyombo vya habari kwa siku za karibuni. Ni baada ya kwanza, kushutumiwa kumchukua mwimbaji wa nyimbo za injili Flora Mbasha ambaye mumewe wa zamani Emanuel Mbasha anamtuhumu Gwajima kumwiba mkewe. Kabla ya hili kupoa lilizuka jingine la Gwajima kumrushia matusi Askofu mkuu wa Jimbo la Dar es Salaam Polycarp Pengo kiasi cha kuitwa polisi kutoa maelezo. Kana kwamba hii haitoshi, Gwajima alipofika polisi akitegemea kutoa maelezo juu ya kashfa na matusi, alijikuta akitakiwa kueleza alivyochuma utajiri wake wenye kutia shaka na wa haraka.
Tokana na na kutakiwa kueleza utajiri wake alivyoupata, Gwajima anaona kama anaonewa wivu tu akidai yeye ni “maskini” ingawa si maskini wa kawaida. Alikaririwa hivi karibuni akisema, “Wanaodai mimi ni tajiri wana wivu tu na wananionea, mimi si tajiri, bali ni masikini kama walivyo masikini wengine. Natarajia kutajirika hapo baadaye waumini wangu wakiwa matajiri, siwezi kutajirika kama waumini wangu bado ni masikini, nitatajirika pamoja nao.”
Je ni kweli kuwa Gwajima si tajiri kwa kiwango chochote hata kwa nchi tajiri duniani kama Marekani? Jibu linapatikana tokana na utajiri anaosema ni umaskini alio nao Gwajima. Alikaririwa akisema, “Wanaodai mimi ni tajiri wana wivu tu na wananionea, mimi si tajiri, bali ni masikini kama walivyo masikini wengine. Natarajia kutajirika hapo baadaye waumini wangu wakiwa matajiri, siwezi kutajirika kama waumini wangu bado ni masikini, nitatajirika pamoja nao.”
Je mtu mwenye kuweza kuwanunulia wenzake magari yapatayo 40 kweli ni maskini huyu? Je kama ameweza kuwanunulia wenzake magari yeye amejibakizia utajiri kiasi gani na ameupata vipi na kwa muda gani? Jibu utalipata tokana na utajiri wa Gwajima ambao umetajwa kuwa ni majumba, magari ya starehe na juu ya yote helkopta. Kwa Tanzania na afrika, kwa mtu mwenye kumilki helkopta si tajiri tu bali tajiri wa kutisha. Kuwa tajiri si dhambi kama mhusika amepata utajiri wake kihalali. Hata hivyo, inatia shaka tokana na kazi anayofanya Gwajima ambayo kimsingi, si ya kuzalisha bali kutoa huduma. Hata yule anayesema kumhubiri, Yesu Kristo hakuwa tajiri na aliuchukia utajiri. Methali 28:20 imeweka wazi kukwa “Mtu mwaminifu atapata baraka tele, lakini mwenye pupa ya kuwa tajiri hataepa adhabu.” Je utajiri wa Gwajima ameupata baada ya muda gani na kwa kufanya nini? Na kwanini anapoulizwa siri ya utajiri wake anang’aka kama hakuna namna? Ni muhimu kumshauri Gwajima kuwa asipoteze muda kutunishiana misuli na serikali hadi kumpa shinikizo rais kuwazuia polisi kufanya kazi yao. Mtu wa namna hii anaonekana kutojua afanyacho hasa ikizingatiwa kuwa, japo serikali imemnyazia kwa muda mrefu, si kwamba haijui mchezo wake.
Kwa mtu ambaye hana wasi wasi na utajiri wake na jinsi ulivyopatikana, alipoitwa na polisi alipaswa kutoa maelezo na vielelezo na kuruhusiwa kwenda nyumbani badala ya kusimama mimbarini na kuanza kutishia na kulaumu watu wanaotekeleza wajibu wao. Tanzania haiwezi kuendelea kuwa shamba la bibi ambapo wachumia tumbo wachache wanawaibia watu wetu kwa kuwadanganya na miujizi na ujinga mwingine. Serikali inapaswa kuwachukulia wote wanaotia shaka hasa wachungaji na maaskofu wa kujipachika vyeo ili kuwaibia wajinga na maskini kama ilivyoanza kuzoeleka. Hatuwezi kuendelea na jinai kama hii. Huu nao ni ufisadi wa kutumia dini kuwaibia wajinga na maskini waliokata tamaa nchini. Serikali inapaswa kuingilia kati kupambana na wachungaji wachunaji ambao hawana tofauti na matapeli na waganga wa kienyeji wanaopotosha na kuiibia jamii. Hakuna miujiza katika kufanikiwa au kutatua matatizo yoyote yawayo. Ni wajinga waliokata tamaa wanaoweza kuendelea kugeuzwa mabunga kwa kushawishika kutoa kidogo walicho nacho kuwapa matapeli wanaochezea akili zao. Kazi ya serikali ni kuhakikisha hakuna mtu anayemnyonya mwenzie hata kama mnyonywaji ameihiari tokana na ujinga na kukata tamaa kwake.
Kuna haja ya kuwachunguza hawa viongozi wa kiroho wanaojipachika vyeo vikubwa kama askofu, mitume na wachungaji wakati hawana sifa zaidi ya kusaka fedha. Mwishoni mwa mwaka jana nchini Kenya aligundulika tapeli wa namna hii aliyejipa uchungaji, uaskofu, utume na udaktari aitwaye Victor Kanyari ambaye alikuwa akitumia radio na runinga kulaghai watu kuwa anatenda miujiza wakati waliokuwa wakitoa ushuhuda walikuwa matapeli wenzake wa kupanga. Hali imekithiri nchini Nigeria na hata Zimbabwe ambapo matapeli wenye majoho wameweza kuwaibia waumini wao huku wakikwepa kulipa kodi na kutokea kuwa matajiri wa kutisha ndani ya muda mfupi. Hii ni aina mpya ya wizi inayoshika kasi barani Afrika ambapo watu wengi licha ya kuwa wajinga, wamekata tamaa kiasi cha kupwakia kila uongo kwa imani kuwa wanaweza kuboresha maisha yao.
Tumalizie kwa kuzitaka mamlaka kumbana Gwajima aeleze alivyopata utajiri wake kwa haraka hivi. Si yeye tu bali wote wenye utajiri wa kutia shaka ilmradi wasifanye hivyo kumkomesha kwa sababu za kisiasa. Akishindwa kufanya hivyo, ataifishwe na kuchukuliwa hatua za kisheria ili liwe somo kwa wengine wanaotumia ujinga na umaskini wa watu wetu kujitajirisha kinyume cha sheria.
Chanzo: Tanzania Daima Aprili 22, 2015.

Ajali za Barabani: Kijiwe Chaishukia Sirikali


          Baada ya mheshimiwa Bwege kupoteza ndugu zake kwenye ajali iliyotokea huko Rufiji hivi karibuni, Kijiwe kimekaa kama kamati kutoa shinikizo kwa lisirikali likomeshe jinai hii ya kizembe na ya kujitakia kama jamii.
          Mheshimiwa Bwege baada ya kupokea salamu na michango ya rambirambi toka kwa wanakijiwe analianzisha, “Jamani, hali ya ajali za kujitakia za barabarani zitokanazo na mfumo wa kishenzi na wa kifisadi zitatumaliza tusipochukua hatua. Ni juzi tu nimepoteza ndugu zangu watano kwenye ajali ya barabarani. Mwaka jana mke wangu alipoteza ndugu watatu kwenye ushenzi huu huu. Jamani tufanyeje ili tunusurike?”
          Mbwamwitu anaamua kujibu haraka, “Tumuulize Pombe Makufuri anayejinadi kwa kuchapa kazi wakati ni wale wale. Hapa waziri hawezi kunusurika. Maana anajua chanzo cha ajali za mara kwa mara lakini hataki kuchukua hatua.”
          Sofia Lion aka Kanungaembe anadakia, “Acheni uvuvi wa kufikiri jamani. Sasa waziri anahusikaje na ajali kama siyo uzushi na kukosa la kusema ukiachia mbali kutaka kuwabebesha wengine lawama?”
          Msomi Mkata Tamaa aliyekuwa akisoma gazeti lililokuwa likizungumzia ajali ya kutisha ya mabasi, analiweka pembeni na kutia guu, “Dada yangu Sofi inapaswa uelewe kuwa waziri ndiye anahusika na sera na sheria za barabarani. Asemayo Mbwamwitu ni kweli. Maana waziri anajua kuwa chanzo cha ajali za barabarani hapa kayani ni barabara zenyewe. Nakumbuka, alishaambiwa kuwa barabara nyingi zimepungjwa ukubwa ili mafisadi wapata chao. Je nani unataka ashughulikie kadhia hii kama si waziri anayehusika na ujenzi wa barabara?”
Mijjinga aliyekuwa akisoma gazeti baada ya Msomi kuliweka mezani, analiweka pembeni na kubusu mic, “Sofi una matatizo ajuaye ni Mungu. Yaani unashindwa kuona vitu rahisi kama hivi au unajifanya tu?”
Kabla ya kuendelea Mbwamwitu anadakia, “Mpe vipande vyake. Amezidi kujifanya na kujitia tia wakati hajui kitu. Anajifanya msemaji na mtetezi wa lisirikali chovu na ovu linalonuka utadhani kuna kitu anapewa au kulipwa.”
Mijjinga anaendelea, “ Hapa hakuna cha kutwisha watu lawama. Wanazistahili. Hata hivyo, wana bahati. Maana, kaya hii isingekuwa ya wachovu na woga waziri kama huyu angepigwa chini haraka sana ili wenye uwezo wachukue nafasi yake na kufanya kazi vilivyo.”
Mpemba anaramba mic, “Yakhe msemayo ya kweli ati. Hivi, hawa waniotaka tusilaumu sirikali wataka tunlaumu nani?” Anamgeukia Sofia na kusema, “Dadangu sasa naanza amini kuna kitu kimekuingilia wallahi. Maana sikutegemea kama ungeweza tetea waovu tena wakati huu tunipoomboleza vifo vya ndugu zake ndugu yetu Mheshimiwa Bweeege. Hivi hawa walopoteza maisha wangekuwa nduguzo ungewezayasema haya uniyosema?”
“Mpe vipande vyake. Hebu yakhe mpe dozi huenda atatosheka aache mapenzi ya kibubusa.” Anachomekea Mipawa.
Mgosi Machungi anakula mic, “Tinamishangaa dada Sofi. Japo shiwezi kusema kuwa ameiingiwa na kitu fulani, sasa naanza kuamini. Si bue. Naona timuuize da Sofi yeye anadhani suuhu ya tatizo la ajai ni nini?” anamgeukia Sofi ambaye anaonekana kuudhika wazi.
Kanji anaamua kumuokoa mshikaji wake Sofi. Anakwanyua mic, “Dugu zangu samehe yeye hapana jua ile natetea.” Anamgeukia Sofia na kusema, “Dada yangu nini naingilia veve dugu yangu? Mbona nyuma haikuwa hivyo dada yangu Sofi? Nini napewa tamu hivyo na sirkali mpaka natetea kila kitu?”
Kijiwe hakina mbavu jinsi Kanji anavyoongea maneno yanayotafsiriwa tofauti na alichokusudia.
Kapende aliyekuwa akitikisa kichwa anaamua kutia buti, “Ndugu zangu, msimshangae Sofi. Wapo wengi kama yeye wenye mapenzi ya kibubusa kiasi cha kushabikia maafa ya wenzao. Kama alivyouliza Ami, hivi hawa wahanga wangekuwa nduguzo ungeyasema haya unayosema au ni kwa vile hawakuhusu? Kama hawakuhusu sisi wanatuhusu na isitoshe leo hawa kesho hujui atakuwa nani hasa ikizingatiwa kuwa sisi wachovu hatusafiri kwa madege kama wao wanaosimamia maafa yetu.”
Msomi anarejea, “Nadhani tuachane na Sofi na kumtumia salamu waziri mhusika kuwa arekebishe uoza wa kupunguza upana wa barabara na kuzijenga chini ya kiwango. Nadhani kaya yetu ndiyo yenye barabara finyu kama vijia vya panya duniani kutokana na kutawaliwa na walaji, walafi, mafisi na mafisadi. Mbona hatusikii hizi ajali kaya jirani kama si ukweli?”
    "Yakhe hawa watu wajue sana hili tatizo. Maana wakisafiri wao hufunga barabara ili wasikutane na vichaa wendao kasi wakawanyotoa roho," Anachomekea Mpemba.
Mijjinga anakatua mic, “Nadhani tatizo jingine ni wenye mikangafu kutoihudumia ukiachia mbali kuwafanyisha kazi madereva kwa muda mrefu bila mapumziko. “
“Kaka umesahau wazee wa mabao yaani wale nyangenyange wa barabarani. Wanawatoa watu upepo na kuacha wapakie abiria wengi watakavyo badala ya kuangalia uwezo wa magari.” Anachomekea Mipawa.
Mgosi anarejea, “Usemayo ni kwei tupu. Juzi nikitoka Ushoto niishuhudia taafiki akipokea bahasha toka kwa konda wa basi aiyekuwa amepakia abiia kupita kiasi. Kwei hawa nao ni chanzo cha ajai.”
Kapende anampoka Mgosi mic na kuongeza, “Chanzo kingine ni mwendo kasi. Tatizo na suka wetu wengi wanadhani kukimbiza magari ndiyo ufundi. Juzi nilishuhudia abiria wakimshangilia muuaji aliyekuwa akikimbiza gari utadhani alitaka lipae. Hawa nao ni wa kutupiwa jicho.”

Kijiwe kikiwa kinanoga si vipanya (daladala) viwili vikavaana katika kuwahi kugombea abiria. Ilibidi tuwahi kuokoa majeruhi hasa baada ya kuona gari likianza kutema moshi. “Ama kweli ajali zitamaliza wengi tusipowajibisha wakubwa wanaohujumu miundo mbinu.” Aljisemea Mzee Maneno.
Chanzo: Tanzania Daima Aprili 22, 2015.

Sunday 19 April 2015

My comment of the year

  • Around 300 immigrants aboard a small fishing boat were intercepted by ...

After reading many irresponsible comments on the sinking of the boat carrying at about 700 migrants in the Mediterranean sea, I chipped in by provoking even many writing:-
I fully support this exodus. When Europeans invaded Africa and colonized it didn't know that Africans will one day pay back coming the same way, without passports and visas. The difference however is that Africans are not going there to colonize Europe but seek employments. They are not going there to rob or exploit as Europeans did in the seventeenth and eighteenth centuries. Again, if western countries are not going to stop exploiting Africa by supporting their stooges in power, they must get prepared to be exiled to Americas and Australia for fear of African Arabs and Indians invading them to pay them back for their colonialism and perpetual exploitation. This is historical tit for tat that Europe should accommodate the same her colonial agents were accommodated in Africa and other places she colonized.


Saturday 18 April 2015

Kiquette: True, presidency is a “tough” job


When some news breaks leaves your heart broken. The other day I was at our eatery at Uwanja wa Hyena devouring some visceral and trimmings expecting to go for kanywaji and ganja aka msokoto. I can see that fella laughing especially after reading my menu of offal. Do you think I’m alone in this business of insanity? Wait.
Sometimes you wonder about the world boozers live in.  We swiggers wonder if politicians live in this world we all live in. They say things that need the courage of the mad. I don’t mean they tell lies even if they do. This is why politics is called usanii or abracadabra. The other day Jake Kiquette bumfuzzled me alleging that Bongolalanland’s presidency is a tough, rough and sucking job. Really?! Yeah. Sucking others is not cool for them.
Jake knew how to choose his spot. For, he said that presidency –for him –was a tough job when he’s in the country of Joji Kichaka at Woodrow Wilson International Centre for Scholars. Interestingly an unscholarly doc speaks to scholars! He knew too well. If he said this in Bongo, he’d be booed and cooed. He said eti presidency –especially of Bongolalaland –is a hard job. Hey folks, giddyap. There’s nothing easy like ruling uncomplaining and unsuspecting Bongolalanders. First, they forget easily. Refer to scams that left them screwed up like escrow and other mega ones involving the high and the mighty. Remember how the draft constitution was slain merciless and stupidly? One boozer whom we call Snake Andrew used to call Bongo the land of the  insane,the  blind and the  forgetful.
Again, was Jake right or wrong to say that ulaji is a heck of a thing? Surely, eating for free with hands and legs without even washing them is not that easy. You’re always guilty so as to ensconce yourself amidst body guards and bouncers. Do you know why these folks are always overprotected? Now you know. Keep this info till Election Day and use it well to decide whom you’ll want to piggyback on your resources and tax come next season for appointing a chief eater.
Just imagine. Once you become head you make sure that your wife, friends and courtier, and you crisscross the world to enjoy as tax payers pick up the tab. You globetrot till some folks baptize you Vasco da Gama to signify that you can win the prize of globetrotting. Is this tough really? Indeed, eating with both hands and legs without washing them after taking a dip in a gravy train is a tough job especially competing with the richest first raider, sorry rider, sorry lady who used to be a pauper before you got to power.
If presidency were a tough job, goons and freaks like Joseph Desire Mobutu, Idd Amin, Sani Abacha and Jean-Bedel Bokassa and other crooks would not have stayed in power even for a single day. See, everybody can become president and eat free and unaccountably just like others who try to put a spin on this naked truth claiming that the job is tough while it is as easy as ABC.
Again, Jake is not the first eater to say that eating is a tough job. Ben Dugong aka Nkapa said the same after lapsing his brutal phase. An interesting thing about these folks is their detachment with time and reality thinking they know more than others. Methinks, only one person deserves to say that presidency is a tough job. This is none other than iconic mzee Mchonga who used his presidency to make other eat instead of eating them as it currently is. Mchonga’s presidency’s tough, holy and ever demanding especially, laying the foundation for whatever laughing hyenas are now wolfing. By then ikulu was the holy of the holy not now it’s become “a den of robbers” where hyenas, wolves and all bête noirs congregate to do their monkey business.
Under Mchonga, the president was a leader not a ruler. He’d to shape the vision of the nation. The president was the father of the hunk but not a thug of it as it currently is. Guess what. Under Mchonga corruption was a crime not a rewarding thing as it currently is whereby escrow thugs are in bed with the high and the mighty. Say not I’m making this up. If they’re not in the same bed, do you think they’d been free making more killings? Again, this is Bongolalaland of the blind, insanity, and stupid where the high priests of graft go scot-free.
Presidency becomes even easier for people without conscience and vision. Myopic and greedy as they’re, they use their intestines to think in lieu of brains. Can you expect any true and sensible thing from them while they actually use their bums to think in lieu of heads? Being a kind of boozers of Bongolalaland has nary been a demanding job. This position gives you the power of making all sorts of errors as you commit as many crimes as possible without being brought to books or being thrown behind bars.
Source: Guardian April 19, 2015.