The Chant of Savant

Wednesday 22 April 2015

Hii comment ya msomaji imenifurahisha sana

Anonymous said...
Mwalimu Mhango,Bwana Mola azidi kukulinda kwani kalmu yako imekua ni silaha ya kuwatetetea wanyonge daima,lakini tatizo kubwa ni ni kuingiliana kwa maradhi sugu katika jamii ya ulimwengu watu hususa Sub Sahara Afrika ambapo kila aina ya maradhi ya kumfanya mwanadamu adumae kiakili yanazidi kujizatiti nakusudia hapa UMASIKINI na UJINGA na kama ujuavyo umasikini na ujinga ndio mama wa mabalaa yote ya maradhi ya kijamii katika jamii yoyote ile ile duniani na wakati mwingine uwezi kuamini kwa vile maradhi haya yamejikita basi hata wale wenye elimu ya aina moja au nyingine utakutwa wamedhurika na maradhi hayo ebu angalia hawa waumini ambao wanaowatajirisha hawa mbwa mwitu ambao wamevaa ngozi ya kondoo,utawakuta ni wenye elimu zao na vyeo vyao katika serikali na sekta binafsi ambao wanakuja na mavazi ya fahari,magari makubwa makubwa ya fahari na hata michango yao ni mikubwa mikubwa wakiamini kwamba watakuwa na sehemu kubwa katika maisha ya mbinguni.
Kama tulikoloniwa kwa sababu ya ujinga wetu,umasikini wetu na ukarimu wetu leo hii tnakoloniwa na hawa matapeli wanaodai wana miujiza ya kuwafanyia waumini wao ambao wengi wao ni masikini kuliko maelezo.
Mwalimu Mhango tuna safari ndefu sana ya kuweza kupambana na maradhi haya ya kijamii na watu wa aina hii ambao wametoa makucha yao na bila ya huruma kuwaparura wafuasi wao bila ya kujali muda wa kudumu tu wao wanafaidika na wanazidi kufaidika.
NI kweli kabisa kama ulivyoandika kwamba..."Hakuna miujiza katika kufanikiwa au kutatua matatizo yoyote yawayo"maelezo yako haya ni ya kielimu(sayansi) lakini katika jamii ambayo imetawaliwa na ujinga,umasikini na uchawi maelezo haya yanakosa maana kabisa.kwa nini wajanja hawa wategemee katika mahubiri yao au dini yao miiujiza?kwa nini wasiende makaburini kuwafufua wafu arudi duniani na kwenda makanisani mwao ili kuwahakikishia waumini kwamba haya wanayohubiri hawa matapeli ni ukweli mtupu?Bwana Yesu alikuwa anafufua wafu.Kwa nini wasiende katika hospitali za ukoma wakawaponya watagonjwa kama alivyokuwa akifanya Bwana Yesu?kwa nini wasiende shule za vipofu viziwi na mabubu wakawafanye miujiza huko kama alivyokuwa akifanya Bwana yesu?Bwana Yesu alikuwa asubiri kuifanya miujiza yake katika kanisa japo yeye alikua akihubiri na kusali katika nyumba ya kiibada ya kiyahudi (synagogue)Bwana Yesu popote pale ilpohitajika au kuhitajika kufanya miujiza yeye aliwajibika tu bila ya lkusita,lakini hawa matapeli na utapeli wao upo wazi wanafanya miujiza yao makanisani mwao kwa kutumia uchawi,kupanga watu ambao wanakula na kanisa na viini macho.
Mwalimu Mhango sisi bado tupo katika stage ya jamii ya ki primitive na mihimili muhimu ya jamii hiyo ni uchawi,wachawi makuhani,na watu wa dini na kwa bahati mbaya hali hiyo bado inaendelea na itaendelea afrika mpaka dunia kwisha.
Msemo wa Karl Marx hapa una uzito wake "Religion is the opium of the masses."
Mwalimu Mhango ni serikali gani hiyo ambayo unayoikusudia kuwachukulia hatua watu wapuuzi kama hawa?ikiwa serikali inashindwa au inakataa kwa makusudi kuwachukulia hatua viongozi ambao wamebobea katika machafu ya ufisadi unaonuka kaya nzima leo itawachukulia hatua matapeli wa kiroho?Unajua nini nachoongea hapa Mwalimu Mhango.
22 April 2015 at 06:53

No comments: