How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do

How the Berlin Conference Clung on Africa: What Africa Must Do

Sunday 21 July 2024

Watufilisio wamefilisi, tumefilisika wamefilisika!

“Kufilisika kubaya. Jamanini kufilisika kubaya. Heri ufilisike mali kuliko akili. Heri ung’atwe na dogi kuliko kung’ata dogi.” Hayo ni maneno ya wimbo nilioutunga zamani nikakosa vifaa ukaishia kwenye makabrasha. Tuachane na mistari ya dhahabu ya zama za dhahabu. Naami mafyatu wote mnajua maana ya kufilisika. Niwasaidia wasiojua. Ni kuishiwa kitu chochote iwe akili au njuluku hata sera. Leo nitaongelea namna mafyatu wanavyofilisiwa na wanaowafilisi wanaopaswa kuwafilisi ili sote tufilisike na watufilisio wakiwamo ngoma droo ili kutenda haki.
Kunyaka mantiki ya somo, nitafudisha kupitia maswali kama ifuatavyo:
Mosi, je unapoteua cahawa kuwa mlongaji wa chata lako huligeuzi chata kuwa Chata cha Machawa (CcM)? Niliwaonya tusifanye mchezo na waharifu mafyatu wakadharau. Yako wapi sasa? Si tuliweka kikaragosi kikafyatufyatuka kikitaka kutubomoa eti kwa kujijenga baadaye eti kichukue ulaji wangu kama rahis wa mafyatu. Yametukuta mafyatu. Juzi katika kijiwe chetu cha uongozi si tukapendekeza fyatu mmoja aliyewahi kupatikana jinai ya kuteka na kuua mafyatu wenzake. Jamaa huyu chawa na changu kisiasa alijipenyeza, akapenya, na tukapenyeka tukamteua kuwa mlongaji wa Chama Cha Mafyatu (CCM). Naomba msichanganye CCM letu na nambari one ya twawala. Huko sipo. 
        Kufilisika nifundishao hauwahusu hao, kwani, walifilisika zamani machawa yalipowanyonya hadi wakaonda hata upstairs hadi wakawa wanalindwa na mbwa aliyekonda utadhani makondakonda sorry makandokando ya mikweche ya akina Daodi, Alubati, na Buushit.
Pili, unapofungulia mbwa, tena mwenye kichaa cha dog akawang’ate mafyatu usijue anaweza kukung’ata hata wewe, unategemea nini? Je hapa hujafilisika kisiasa? Je ulishajiuliza itakuwaje dogii akiamua kufilisika kama mwenyewe na kukung’ata wewe umfugaye? Hii huitwa mbwa kula mbwa kwani mbwai mbwai. Je unajua kuwa hizi ni baadhi ya dalili za kufilisika pale mwenye mbwa unapotegemea mbwa akulinde na kukuhakikishia usalama hata kukubalika kwako kwa mabavu wakati mbwa ni mbwa atabwabwaja na kufanya uumbwa? 
        Je unaambua nini kwenye ushauri huu wa bure toka kwa gwiji Dk, Profesa, Alhaji, Mhashamu, His Excellency, His Eminence, HH etc. Fyatu Mfyatuzi bin Mfyatuaji bin Mfyatukage wa Mfyatulizi mwana wa Mfyatukizi mjukuu wa Fyatuafyatua mwana wa Mfyatuizi? Naona yule anashangaa na kutikisa kichwa. Hujui naweza kutaja majina elfu na ushei ya kizazi changu kama kilivyoandikwa kwenye vitabu vitakatifu ingawa lilibadilishwa likawekwa la ka jamaa toka Mashariki ya nonihino? 
        Tatu, wewe unayeendelea kufanya makosa kuendekeza mbwa ukidhani atakuletea amani na usalama hata kwa kuwang’ata wachapakazi wako? Huku ndiko kufilisika kunakoongelewa hapa. 
        Nne, unapompa bangi mbwa mwenye kichaa tayari kung’ata wabaya au wapingaji wako  kwa sababu ana uzoefu wa kung’ata, kwanini nao wasijitoe akili wakamng’ata ikawa habari halafu wakakufyatua nawe na jibwa lako fyatu? Huku ndiko kufilisika kunakotufilisi kwa kufilisiwa na hawa waliofilisika wakatufilisi nasi.
        Tano, ili kuonyesha hawajafilisika, kwanini mafyatu wasinyongelee mbali hili jibwa ili wasing’atwe na kuendekeza madogiii? Huu si wakati wa madogii kutuchezea na kutung’ata kama kipindi kile walipokuwa wakibweka na kung’ata huku aliyewafuga akizidi kuchekelea na kuwanenepesha tena kwa njuluku na mamlaka ya mafyatu wafyatuliwa na kufilisiwa.
        Sita, mafyatu walipoona wanene tumempitisha huyu dogi, walisema wazi kuwa kipindi hiki ang’atwi fyatu hata mmoja. Badala yake mafyatu watang’ata hata mbwa mng’ataji. Hivi unapowaletea mafyatu mbwa, ina maana mafyatu wamekwisha au ni ile hali ya kuzidiwa na kunyonywa na chawa au kufilisika?
Saba, hivi inawezekanaje mbwa kuwazidi akili mafyatu tena wakubwa kiumri na kimaulaji? Je hapa mbwa na fyatu ni yupi au mmebalishana baada ya kufyatuka na kufilisika hadi mkaruhusu mbwa awafyatue na kuwafilisi? Je mfupa uliomshinda fisi nyinyi mtauweza?
Nane, inakuwaje mbwa anaendekezwa ili ang’ate mafyatu waliokwishafyatuka wakati tunao wanyama kibao na mabaki kibao kwa wale wanene wanaokula nyama? Kwanini wasimtupie mabaki ya milo yao badala ya kutaka awang’ate mafyatu wasio na noma na yeyote?
Baada ya kumaliza kuuliza maswali ambayo sitegemei kuletewa majibu ili yachapishwe kwa vile fyatu anayenihariri na kuruhusu hii kitu itoke hewani mafyatu wasome hataruhusu. Naye kuna siku nitamfyatua. We acha tu. Ukisoma hii, soma kimya asisikie akanifyatua nikashindwa kuwafyatua mafyatu wanaotufyatulia mimba itufyatue wasijue usawa huu, tutaifyatua kama mbaya, mbaya. Kwani mbwai mbwai kwa kimombo.
        Je tuko tayari kuendelea kung’atishwa majibwa tena yaliyochoka baada ya kujaribu hata kuwang’ata waliowakota majalalani? Inakuwaje mbwa koko anaendekezwa kiasi cha kuwazidi mafyatu wakati ananenepa kwa njuluku zao? Je kinachoendelea ni mbwa kugeuka chawa au chawa kula akanenepa na kugeuka mbwa?
Nimalizie. Kweli wametulifisi mali nao wakafilisika mawazo! Du! Kwani niko wapi?
Chanzo: Mwananchi Jumatano iliyopita.

No comments: