The Chant of Savant

Tuesday 28 May 2013

Tufanye mpango Kikwete aende kutalii mwezini

Picha kwa hisani ya Michuzi blog


Wapo waliomheshimu na kumwita Vasco da Gama wakimaanisha yule jambazi wa kireno aliyezunguka dunia akitafuta pa kupora. Wasio na muda wa kufichaficha walimwita mzururaji huku wale wanaomheshimu walimwita mtalii. Wengine wanamwita msanii kutokana na tabia yake ya kufanya mambo kisanii. Yote amefanya hili la kuizunguka dunia limemkaa. Rais anazurura utadhani waziri wa mambo ya nchi za nje! Kwa vile Kikwete na mkewe walishaizunguka dunia nzima, napendekeza afanyiwe mpango aende kutalii anga za juu kupitia mradi wa sasa wa kupeleka watalii kule unaofanywa na vyombo vya anga binafsi.

3 comments:

Jaribu said...

Tunaweza tukafanya hiyo safari one way tu?

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Jaribu, why one way? Don't you want them to return and enjoy their yum-yum stolen from us? So be it!

uswazi said...

Labda ameshakwenda, kalimbikiza/ kaficha mali zake huko....