The Chant of Savant

Saturday 4 May 2013

Jipendekeze kwangu upate ukubwa



 Salva Rweyemamu na Muhingo Rweyemamu (Pichani) ni mfano wa waandishi habari waliojipendekeza kwa Kikwete na kuula.Je tuendekeze matumbo yetu na kuua taaluma au tuache njaa ituume tuokoe taaluma?
Akekho ofana no nami
Akekho ofana nami
Adekho ofana nonami
Akekho ofana nami
Hayupo afananaye nami
Hakuna afananaye nami
Hakuna hakuna kabisa
Hakuna ulaji kama wangu
Hakuna mipango kama yangu
Hiyo tafsiri inatosha mose wa lero.
Sahamba sahamba akekho akekho
Sajika sajika akekho akekho
Safuna safuna akekho akekho
Safuna safuna akekho akekho
Akekho afana naye
Naona huu wimbo wa kisauzi si mzuri. Ungefaa huu kama ningeuimba nikielekea kwenye kampuni ya kuuza ndege dezo kununua moja kwa ajili ya bi mkubwa na nyingine kwa ajili ya nyumba ndogo.
Anyways, ngoja nishuke na neema hasa ikizingatiwa kuwa karibuni nitakuwa na uwezo wa kushusha neema kwa walevi.
Tunaze kwa pamoja!
Neema neema neema imefunguliwa
Neema neema neema imewaangukia
Hata kwenye ulaji
Neema imfunguliwa
Neema imefunguliwa
Hata kwenye ushikaji,
Neema imefunguliwa
Ingawa mimi si Muumini wa dini yoyote zaidi ya ulabu, huwa napenda song la Neema imefunguliwa. Kweli, neema imefunguliwa. Ndiyo imefunguliwa.  Maana naitangaza hasa kipindi hiki ninapojiandaa kugombea ukuu wa kaya.  Kama hata wale walioishiwa wanatangaza nia kwanini mimi nisitangaze? Unadhani zama hizi urais ni big deal kama wakati wa mzee Mchonga? Thubutu! Mlevi yoyote anaweza kuwa mkuu. Kwani wao wana nini ambacho sina? Kama ni ahadi za kuukata na kuula ninazo tena magunia. Kama ni sanaa za kuwapumbaza mimi ndiyo mwenyewe. Kama ni sura na shepu ninavyo. Kama ni mitandao ninayo. Kama ni slogans za uongo na ukweli, ninazo.  Waingilishi husema I have what it takes. And surely, I am the best of all. Usikonde mshirika na msomaji. Nachonga kimombo kuonyesha kuwa sikughushi shahada zangu za ulevi na bangi.
Naanza kumwaga neema.
Waandishi makanjanja hasa wenye majina yanayoanza na herufi ‘R’ wataula iwapo watanisaidia kuwachafua wapinzani wangu na kunipamba huku wakiwaingiza nkenge walevi.
Ukubwa wa idara ya mawasiliano ya rais na ukubwa wa wilaya pia ukatibu uenezi urongo na propaganda uchwara kwenye ofisi za chama changu cha Ulaji Ngonjera na Michosho (UNM) guaranteed.  Sitajali watakaosema kuwa natumia madaraka vibaya. Kama nimeyapata vibaya kwanini nisiyatumie vibaya? Ukijipendekeza hadi kubadili jina lako kuwa Rweyebendekeza, Rwetumika, Rwetapelia, Rweyemam-ulaji nakupa ulaji aminia.
Mkakati mwingine wenye ulaji ni kuwatumia mashoga ambao lazima watachangamka kupiga kampeni kitanda kwa kitanda. Aminia lazima niwateua kuwa wahishimiwa ili nao wafaidi ulaji kwa mgongo wa shoga yao.
Makampuni ya wawekezaji yatakayonikatia mshiko wa kampeni lazima niingie nao mikataba minono.
Makanjanja watakuwa na kazi moja yaani kuandika makala safi na vitabu vyote ya uongo na ukweli kunisifia. Brother Bagendai na Silvia na Muhin-gooo Rweyependekeza mpo hapa?
Lazima waeleze umma wa wadanganyika kuwa mimi ni kijana katika umri wangu wa miaka 60.
Pia lazima wasifie uzuri na urembo wangu hasa tabia yangu ya kununa nuna kuwa inamaanisha niko serious katika kila jambo kuanzia harusi, vichekesho hadi muziki.
Marafiki na washikaji wa vitegemezi vyangu lazima wapewe ulaji kila mahali kuanzia chamani, idara zake hata kwenye ofisi zenye mishiko mizito kama vile Bandari, Banki Kubwa, Uhamiaji na TRA.
Washikaji zangu na watoto wa washikaji zangu lazima wapewe u-ambasadari kama siyo kufanya kazi kwenye konsuleiti. Sister Mwanawaiddi Maajali upo hapo? Tumia mwanangu.  Huko ndo kulipana mifwadhila bwana. Wengine watakaofanikiwa kuchaguliwa wabunge lazima niwape uwaziri. Brother Jose Ma-rope, Nchimvi, Hossein Muinyi na wengine ambao ni watoto wa washikaji zangu mpo?
Wale washikaji zangu watakaosaliti usomi wao lazima niwateua kuwa wakuu wa vyuo. Brother Pworofwesa Muggyabu’ Mkanda-raha upo hapo? Changamkia tenda hakuna haja ya kujivunga hata kama watu watasema unajipendekeza kama mtoto si riziki. siku hizi ujanja kupata regardless umepata na kupeta kihalali au kiharamu. Changamkieni ulaji wanangu. lazima serikali yangu iwe ya washikaji na wakereketwa wangu na bi mkubwa. Kwani hamjui mimi ni maarufu kuliko chama changu cha UNM.
Kwa vile urahisi ni ufalme, hata vivyele vyangu lazima wapate ulaji. Brother Seidu Mwema upo? What is wrong if Ben Dangeman Makapu did the same? Nani kasahau ile kampani ya kuitwaa Kiwila? Si vivyele waliungana na wenzao kuwaibia walevi na hakuna aliyenyea debe?
Katika kutoa ulaji sitaangalia maadili, uadilifu wala nini zaidi ya usuhuba na uwezo wa kufanikisha dili la kuupata ukuu.
Sera yangu ni simpo. Ulaji bora na mkubwa kwa sote. Tena si ulaji bora na mkubwa tu bali kwa new force, new speed na new zeal. Tafadhali ustafsiri ili tusileteane balaa watu tukaonana wabaya.
Kufanikisha ulaji, lazima kuunda mtandao wa kuhakikisha wale wote wanaoonekana kuwa tishio kwangu wanamalizwa kwa kusingiziwa kila aina ya ubaya. Tukishapeta, walevi watalia na ujinga wao wakati sisi tukitesa. Au siyo washikaji? Lazima kuchangamkia tenda maana wajinga ndio waliwao. Nyie wala msiwe na wasi wasi kutumiwa. Hapa tunatumiana. Ninawatumia nanyi mnanitumia kwa ubaya uko wapi si bora liende na riziki iingie? Au vipi washirika?
You know what? I am just kidding. Tangu lini mlevi akagombea urais? Hivyo, wale mnaoendelea kuvivuruga vyama vyenu kwa kutangaza nia za kugombea msiwe na wasi wasi sina mpango wa kuwadanganya walevi.
Seriously, waliwa na wapika kula ya kura inabidi wawe makini na mafisadi na mafisi na matapeli wenye uchu wa mali na madaraka wanaotaka kuwania urais ili wawalize kwa sana tu.  Tangu lini fisi au mbwa akachaguliwa kutunza nyama kama siyo wendawazimu? Message sent. 
Chanzo: Nipashe Jumamosi Aprili 4, 2013.

No comments: