The Chant of Savant

Friday 24 July 2015

Raisa wa Tanzania anapotembelea Malaysia



Utawala wa rais Jakaya Kikwete utaingia kwenye vitabu vya historia kama utawala wa hovyo uliowahi kuwapo nchini. Kwa kisingizio cha kuaga ughaibuni Kikwete amekuwa akipoteza mamilioni ya shilingi eti kwenda kuaga nje utadhani ndiyo waliomchagua. Anaondoka kesho kuelekea Australia kuaga baada ya kurejea juzi toka Uswizi alikokwenda kuaga. Kama haitoshi na mkewe yupo Malaysia sijui naye anakwenda kuaga au ndiyo hiyo tabia ya kuzurura waliyojizoesha.

Ngoja watoke madarakani tuone kama watazurura kama walivyozoea. Kuna haja ya kubadili katiba kuzuia upuuzi huu wa kuzurura na kuacha kazi zikilala nyumbani. Kwa miaka kumi Kikwete ametuibia tu ukiachia mbali kulea na kushiriki ufisadi.

No comments: