Tunaamini wengi wa wasomaji wetu wanaijua maabala. Maabala ni mahali ambapo hufanyika majaribio ili kupata nyenzo na ujuzi wa kufaa katika maisha. Japo si maabala zote, mara nyingi, maabala zimalizapo kazi zake au hata kutoleta matunda au kufikia malengo yaliyotarajiwa hufungwa. Ni maabala za taasisi za kielimu za kisayansi ambazo daima huendelea kuwepo.
Kama ada yetu, leo, tutadurusu na kuongelea ndoa na wanandoa. Tutakita kwenye namna wanaofanya kosa kubwa na kukubali kujigeuza au kugeuzwa maabala. Kwa watu wa Pwani wanajua neno chuo au vyuo. Kuna baadhi ya makabila ambayo ndoa zao ni kama maabala. Mama au baba anaingia kwenye ndoa na kuivunja na kudandia nyingine. Hapa, ndipo dhana ya chuo inapoanzia. Utamsikia mama akiulizwa “chuo changapi hiki? bimaana ni ndoa ya ngapi.
Pamoja na kuwa mila iliyokubalika kuoa na kuolewa na kuachika, si jambo jema kwa binadamu. Lina madhara mengi kibinafsi, kijamii, kimwili, kiakili, kiuchumi hata kimaisha Je, hii husababishwa na nini? Hatuna jibu moja wala jibu rahisi. Yapo mengi yanayosababisha umaabala huu. Moja, yaweza kuwa kuingia kwenye ndoa bila kufanya utafiti na kuielewa mila na shurti zake.
Pili, ni tabia ya wahusika. Wapo wanaokwapukia na kupwakia ndoa bila kujiandaa au kuandaliwa. Zamani, kulikuwa na taasisi za Kiafrika za kuwaandaa watarajiwa kuingia kwenye ndoa. Ziliitwa jando kwa wanaume na unyago kwa wanawake. Taasisi hizi zilitofautiana baina ya makabila. Tofauti hii ilitokana na utofauti wa mazingira na mila za jamii husika. Hata hivyo, zilifanana kwa kitu kimoja kikuu. Vijana wa kike na kiume walipelekwa sehemu maalumu na kufunzwa na kufundwa na makungwi namna ya kuishi katika ndoa.
Katika jando na unyago, yapo makabila ambayo yalitahiri vijana wa kiume na mengine hata wa kike. Kutahiri wanawake, kuna madhara makubwa kimwili na kiakili. Hivyo, zama hizi, mila hii imepitwa na wakati.
Kwa ufupi, katika jando na unyago, wahusika walifunzwa na kufundwa juu ya namna ya kuwa watu wazima wake na waume. Walifundishwa miiko ya ndoa na mambo mengine muhimu ili kuwasaidia kuishi maisha ya ndoa kwa furaha na ufanisi. Hata hivyo, siku hizi vijana wanafundwa na mitandao ambapo mambo mengi ya hovyo na uongo hufundishwa na wale wanaotaka kupata wafuasi ili wapate fedha.
Hata hivyo, baada ya ujio wa dini za kigeni, taasisi hii adhimu na muhimu iliuawa na kudharaulika kiasi cha kusababisha madhara makubwa kwa taasisi ya ndoa. Ni bahati mbaya. Si wengi wanashuku wala kuhoji uvamizi huu wa kimila ambao kimsingi, si chochote bali ukoloni kama ukoloni mwingine wenye lengo la kuwabadilisha wahusika ili kuwatawala na kuwanyonya.
Tatu, ni msukumo wa jamii iliyoacha maadili yake na kupwakia maadili ya kigeni bila kuyajua vizuri na athari zake hasi kwa walengwa. Mfano, siku hizi mabinti wengi hawajifunzi kunga za nyumba kama vile heshima, mapishi, usafi, uvumilivu, usiri, na mengine mengi ambayo zamani, yalithaminiwa sana.
Nne, kukua kwa teknolojia. Tangu kuibuka kwa matumizi ya mtandao, mabinti wengi hawana nafasi ya kujifunza stadi za maisha. Mfano, wapo wasiojua kupika kabisa. Wanachofanya ni kwenda kwenye mitandao na kutafuta recipes za mapishi au mapishi, hatuna Kiswahili chake.
Kama tujuavyo, japo binadamu ana uwezo mkubwa wa kujifunza, si mara zote huelewa anachofundishwa. Huweza kuelewa anachofundishwa kupitia kurudiarudia ndiposa huelewa na kukubuhu. Mapishi yatokanayo na kujifunza pindipo mhusika atakapo kupika hayamuweki kwenye nafasi nzuri ya kuyamudu. Kuna usemi kuwa njia ya kuingia kwenye moyo wa mwanaume hupitia tumboni. Hivyo, chakula kina nafasi kubwa katika kuimarisha au kudhoofisha ndoa.
Hata hivyo, tokana na usasa, stadi za mapishi zinaonekana kama jambo la zamani. Hapa, ndipo umaabala unapoanzia na kutamalaki. Pia, tunashauri jamii ianze kurejea mila na utamaduni vya zamani vinavyofaa na kuacha visivyofaa. Hii itasaidia kuepusha ndoa na wanandoa kuishia kuwa maabala na kujenga jamii ya kimaabala ambayo haidumu.
Kama ada yetu, leo, tutadurusu na kuongelea ndoa na wanandoa. Tutakita kwenye namna wanaofanya kosa kubwa na kukubali kujigeuza au kugeuzwa maabala. Kwa watu wa Pwani wanajua neno chuo au vyuo. Kuna baadhi ya makabila ambayo ndoa zao ni kama maabala. Mama au baba anaingia kwenye ndoa na kuivunja na kudandia nyingine. Hapa, ndipo dhana ya chuo inapoanzia. Utamsikia mama akiulizwa “chuo changapi hiki? bimaana ni ndoa ya ngapi.
Pamoja na kuwa mila iliyokubalika kuoa na kuolewa na kuachika, si jambo jema kwa binadamu. Lina madhara mengi kibinafsi, kijamii, kimwili, kiakili, kiuchumi hata kimaisha Je, hii husababishwa na nini? Hatuna jibu moja wala jibu rahisi. Yapo mengi yanayosababisha umaabala huu. Moja, yaweza kuwa kuingia kwenye ndoa bila kufanya utafiti na kuielewa mila na shurti zake.
Pili, ni tabia ya wahusika. Wapo wanaokwapukia na kupwakia ndoa bila kujiandaa au kuandaliwa. Zamani, kulikuwa na taasisi za Kiafrika za kuwaandaa watarajiwa kuingia kwenye ndoa. Ziliitwa jando kwa wanaume na unyago kwa wanawake. Taasisi hizi zilitofautiana baina ya makabila. Tofauti hii ilitokana na utofauti wa mazingira na mila za jamii husika. Hata hivyo, zilifanana kwa kitu kimoja kikuu. Vijana wa kike na kiume walipelekwa sehemu maalumu na kufunzwa na kufundwa na makungwi namna ya kuishi katika ndoa.
Katika jando na unyago, yapo makabila ambayo yalitahiri vijana wa kiume na mengine hata wa kike. Kutahiri wanawake, kuna madhara makubwa kimwili na kiakili. Hivyo, zama hizi, mila hii imepitwa na wakati.
Kwa ufupi, katika jando na unyago, wahusika walifunzwa na kufundwa juu ya namna ya kuwa watu wazima wake na waume. Walifundishwa miiko ya ndoa na mambo mengine muhimu ili kuwasaidia kuishi maisha ya ndoa kwa furaha na ufanisi. Hata hivyo, siku hizi vijana wanafundwa na mitandao ambapo mambo mengi ya hovyo na uongo hufundishwa na wale wanaotaka kupata wafuasi ili wapate fedha.
Hata hivyo, baada ya ujio wa dini za kigeni, taasisi hii adhimu na muhimu iliuawa na kudharaulika kiasi cha kusababisha madhara makubwa kwa taasisi ya ndoa. Ni bahati mbaya. Si wengi wanashuku wala kuhoji uvamizi huu wa kimila ambao kimsingi, si chochote bali ukoloni kama ukoloni mwingine wenye lengo la kuwabadilisha wahusika ili kuwatawala na kuwanyonya.
Tatu, ni msukumo wa jamii iliyoacha maadili yake na kupwakia maadili ya kigeni bila kuyajua vizuri na athari zake hasi kwa walengwa. Mfano, siku hizi mabinti wengi hawajifunzi kunga za nyumba kama vile heshima, mapishi, usafi, uvumilivu, usiri, na mengine mengi ambayo zamani, yalithaminiwa sana.
Nne, kukua kwa teknolojia. Tangu kuibuka kwa matumizi ya mtandao, mabinti wengi hawana nafasi ya kujifunza stadi za maisha. Mfano, wapo wasiojua kupika kabisa. Wanachofanya ni kwenda kwenye mitandao na kutafuta recipes za mapishi au mapishi, hatuna Kiswahili chake.
Kama tujuavyo, japo binadamu ana uwezo mkubwa wa kujifunza, si mara zote huelewa anachofundishwa. Huweza kuelewa anachofundishwa kupitia kurudiarudia ndiposa huelewa na kukubuhu. Mapishi yatokanayo na kujifunza pindipo mhusika atakapo kupika hayamuweki kwenye nafasi nzuri ya kuyamudu. Kuna usemi kuwa njia ya kuingia kwenye moyo wa mwanaume hupitia tumboni. Hivyo, chakula kina nafasi kubwa katika kuimarisha au kudhoofisha ndoa.
Hata hivyo, tokana na usasa, stadi za mapishi zinaonekana kama jambo la zamani. Hapa, ndipo umaabala unapoanzia na kutamalaki. Pia, tunashauri jamii ianze kurejea mila na utamaduni vya zamani vinavyofaa na kuacha visivyofaa. Hii itasaidia kuepusha ndoa na wanandoa kuishia kuwa maabala na kujenga jamii ya kimaabala ambayo haidumu.
Chanzo: Mewananchi Jpili leo.