The Chant of Savant

Sunday 13 March 2011

Unamjua Bilionea asiye na nyumba wala gari?

Je ungekuwa wewe ungefanyaje?

Chuck Feeney angekuwa mtanzania au mkenya angeambiwa ni chizi. Ni bilionea ambaye ameupata ukwasi wake bila kuibia serikali wala kudhulumu bali kuchapa kazi. Ni bilionea ambaye ameishatoa msaada tena akitaka asijulikane wa yapata $ 4,000,000,000. Ni mtu wa ajabu kwa viwango vya kawaida. Maana hana makuu wala hana gari na hupenda kusafiri kwa usafiri wa kawaida wa umma. Laiti tungepata mtu kama huyu kuwekeza kwenye ikulu yetu ningempigia debe bila kuombwa.

Wakati nguli huyu mkwasi anaishi kama binadamu wa kawaida, tuna wezi na majambazi wanaonenepeshwa na jasho letu kupitia kodi wanaofanya makufuru kama alivyofanya hivi karibuni waziri Lazaro Nyalandu mbunge maskini na limbukeni wa Singida aliyetaka watanzania kutumia usafiri wa anga waendapo mikoani asijue kwa walio wengi kula yao ni shida tupu.
Bofya usome zaidi habari za bilionea Feeney Pia kwa habari zaidi Bonyeza hapa
Ukitaka kumjua Biionea mdogo kuliko wote soma hapa

No comments: