The Chant of Savant

Thursday 31 March 2011

Je mwanzo wa mwisho wa Gbagbo umefika?


Gen Mangou katikati akiwa na wasaidizi wake kabla ya kukimbia

Laurent "Badboy" Gbagbo
Habari toka Abidjan Ivory Coast zimelipoti kuwapo mapambano makali baina ya wafuasi wa rais halali wa nchi hiyo Alasane Ouattara na mwizi wa urais Laurent "Badboy" Gbagbo.
Pigo la pili kwa Gbagbo ni mkuu wake wa majeshi Gen. Phillippe Mangou, mkewe na watoto wao watano kutafuta na kupata hifadhi kwenye nyumba ya balozi wa Afrika Kusini nchini humo.

Habari ambazo hazijathibitisha ni kwamba wafuasi wa Ouattara wameishateka Televisheni ya Taifa RTI ambayo imetoweka hewani tangu Jana. Pia wafuasi wa Ouattara kwa sasa wanadhibiti zaidi ya 80% ya nchi.

Baada ya Ouattara kuona Gbagbo anaendelea kung'ang'ania ameamrisha majeshi yake kupambana na wafuasi wake huku akitanga kufunga mipaka yote ya Ivory Coast na hali ya hatari.Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA

No comments: