The Chant of Savant

Wednesday 16 November 2011

Heri nife njaa, ushoga hapana

JUZI nilitaka kuua mtu hivi hivi. Kwanza niwataarifu. Siku hizi nimebadili jina. Naitwa Nkwazi Mhango. Why? Nitawaambia next time.

Si ilitoka habari kuwa Watasha wanataka kutupa misaada kwenye kijiwe lakini kwanza tushikiane ukuta wenyewe kwa wenyewe kijiweni. Kweli akutukanaye, hakuchagulii tusi!

Kwanza mghoshi Machungi aliapa kuua mtu. Maana zilipotoka habari nilimsikia mwenyewe akiongea kisambaa akisema, “Ho tate nane, Mghoshi ndie andose ntambidiza.” (Tafsiri, mie lazima nimmalize atakayenifuata).

Kila mtu alisema lake. Maana kama ni ukoloni huu wa midume kuonana wenyewe kwa wenyewe kisa misaada yao, hapana, tuwaache waendelee wao.

Tukiwa tunatafakari si Mbwamwitu naye katoa mpya eti waziri mkubwa wa Utasha aliyetoa pendekezo la ushoga kumbe naye ni shoga ndiyo maana jina lake anaitwa Davida Kinyonga. Anavaa suti kumbe ni kinyonga ambaye nyuma ya pazia ni shoga la kawaida.

Baada ya habari hii kuibuka, ilizua taharuki na mitafaruko kibao. Msomi Mkatatamaa anasema eti habari hiyo ilifika kijijini kwake ikiwa imechakachuliwa kiasi cha wanakijiwe kuitafsiri eti wameambiwa kuwa wazungu wamemwambia mkuu kuwa wasiporuhusu ndoa za mashoga, hawatapewa misaada.

Mpemba mshenzi kweli. Si alikwenda mbali na kusema, “Wajua, nasikia kuna rahisi wa nchi fulani alikwenda kuomba msaada, akaambiwa ati ashike ukuta.”

Kachokoza nyuki! Kujikomba mwana kijiwe mpya mshabiki wa Chata la Mafisadi alidhani anarushiwa yeye hilo dongo. Alisema, “Uongo mkubwa. Washenzi wakubwa nyie.” Hata kama mkuu wetu wa kijiwe ni ombaomba, nisiwasikie mkisema eti alitaka kuolewa. Laanatullillahi.

“Hivi hawa watasha wana akili kweli?” alihoji mzee Ndevu na kuendelea, “Kwanini wanapenda sana mambo ya kishoga shoga?”

Mzee Maneno alidaki, “Sasa kijiwe kimeazimia kuwasusia. Kuanzia leo hatutaongea kitasha ambacho wajinga wengi hukichukulia kama lugha ya usomi.

Hii ni hatua moja ya kuwasusia hadi watuombe msamaha. Kama wataendelea, basi tutawatuma vijana wetu waende huko huko wamzomee na kumtaka Kinyonga aende akaishi Mombosa, akafanye ushenzi wake aone.” Kijiwe hakina mbavu.

Anaendelea, “ Kama wanadhani huo ni mchezo mwema si watoe wao kwanza waone cha moto kama wanaona mchezo huu mwema, lakini hapa kwenye kaya yetu hapana, tena wakome.

Yaani sipati picha kaya nzima watu wachakachuane kimasomaso kweli? Hii siyo kutengeneza Sodoma na Gomora nyingine?” alimalizia.

Mzee mzima nami nakula mic, “Hata juzi mwanae alipokuja Bongo kuwahadaa wabongo akiwa na kimada wake nilimtokea na kama si polisi kunizuia huenda ningepata kesi kwa kumnasa mtu mbanta.

Anayedhani namfunga kamba ajue siyo. Maana wakati Chaz alipokuwa akitaka kuvuka kwenda zake Kigamboni kushangaa kwanini shilingi inazama na meli inaelea nilikuwa kwenye pantoni ya kwenda Kigamboni.

Baada ya kumuona haraka haraka niliwahamasisha wananchi wamshit. Hata alipopunga mkono wake hakuna aliyejibu. Uliza kama unadhani nadanganya. Nidanganye ili iweje. Nilikuwa nimechukia siku hiyo na kama si jamaa zangu kwenye feri kunikamata ningekufa maji au ningemtia mbanta na kuishia kufungwa.

Najua ningefungwa. Maana pamoja na kuwatukana watu wetu bado baadhi ya wenzetu wenye masilahi naye walimkaribisha kwa bashasha kana kwamba kweli wao si watoto riziki kama alivyowadhania!

Laiti ningekuwa mkuu wa kaya mbona ningemsusa na hata nisingeruhusu dege lake kutua wala kumpa viza ya kuingia nchini. Dhiki nyingine mnaziendekeza hadi kujidhalilisha.

Huu nao ni ushoga wa kisiasa na kimsimamo na mkakati. Chaz alikuwa na jipya gani zaidi yakuja kutalii kwa bei nafuu na kupima maji kuhusiana na kushauriwa tuwape ulaji mashoga kisheria?” Naongea bila kituo ili asitokee mtu akanipoka mic.

Wakati kijiwe kikiwa kimehanikiza kulaani hizi kampeni za kueneza ushoga si Mchunguliaji aliingia na kutufunga macho?

Yeye alisema kuwa amependa sana tusi hili kwa vile wanene wetu wamezidi kuombaomba kiasi cha kutakiwa kulipa eti kwa njia hiyo!

Mchunguliaji alikuwa na furaha utadhani naye alikuwa shoga! Kumbe alikuwa akishangilia jamaa kuumbuliwa kutokana na u-Matonya wao.

Alisikika akisema, “Kaya ina midini kama haina akili nzuri. Mnagawa midini kwa wachukuaji halafu mnakwenda kujidhalilisha kwa kuomba.

Acha wawaombe nanihino mkome.” Pamoja na lugha yake kuwa ya maudhi, kila mtu alishikilia mbavu zake kwa kicheko kiasi cha kuyeyusha hasira iliyokuwa imetawala kijiweni.

Mchunguliaji alikuwa seriyasi kweli. Aliendelea. “ Watasha si wapumbavu kama nyinyi. Wamekuwa wakiwatukana na kugundua kuwa hamstuki. Sasa wameamua kutukana mitusi mizito ili mtie akilini.”

Alikatua kashata yake na kuendelea, “Baada ya kuwatukana tusi la kupamba na miwaya kwa kutangaza ngono mkidhani mnaizuia nanyi kama mataahira mkalishabikia na kuhujumu mila zenu, sasa wameona wawashike pabaya ili mstuke. Maana ukitaka kumpata Mswahili muite shoga.”

Alikunywa kahawa kidogo na kuendelea. “ Hata kama yuko shimoni au darini atatoka na kuja juu hata kama ni shoga kweli.”

Mchunguliaji aliendelea, “Nyie mlishaliwa na kuchakachuliwa sana sema hamjitambui.” Mghoshi aliamka na kutaka kumnasa kibao Mchunguliaji ambaye naye alijitetea. “Mgosi huna haja ya kupandisha ingawa najua wewe bado hujashikishwa ukuta.”

Mgosi alijibu, “Hapo umenena mghoshi. Yaani unatiambia eti wametufanyia ushoga!”

Mchunguliaji hana mbavu anaendelea, “Tuseme ukweli. Tushaliwa sana na kuchakachuliwa sasa wanataka tuchakachuane wenyewe kwa wenyewe tena kiza na hiki we acha tu.”

Mzee mzima nilikuwa nacheka na kuhuzunika kwa pamoja. Niliamua kukwanyua mic na kuwatuliza wanakijiwe.

“Msemayo ni kweli hata kama yanauma. Kaya imechakachuliwa kila kitu. Umeme, kura, madawa, mafuta, bei za vitu, ulaji, hata na nyinyi wenyewe.”

Kikao kilivunjika baada ya jamaa kutaka kuninyotoa kwa kusema eti waliliwa zamani na kuchakachuliwa.
Naona dege la Kameruni linatua. Acha niwahi kumzomea japo kiduchu. Kwa heri!


Chanzo: Tanzania Daima Novemba 15, 2011.

No comments: