Kuna kisa cha mwanandoa Gilombo (si jinale) tulichoshuhudia. Gilo hakujaliwa sura wala tabia nzuri. Alikuwa mzinzi wa kutisha aliyelazimisha ndoa kwa kijana handsome na mwenye nazo asiye na uzoefu. Alibahatika kupata mtoto wa kike katika ndoa ya kulazimisha iliyoduma miaka miwili tu.
Baada ya kuishi na mumewe kwa mwaka mmoja na kulazimisha kubeba mimba bila ya makubaliano, jambo ambalo lililomstua muwe, Gilo aliamini mumewe bwege asiyeweza kustuka wala kushuku. Hivyo, mazabe yake yasingefumka. Taratibu, mambo yalianza kutifuka na kufumka. Mumewe alianza kumshuku kwa kila jambo. Mfano, kuna wanaume waliokuwa wakiwatembelea aliowatambulisha kama ndugu zake. Bahati mbaya, mmojawapo alikuwa akifahamika kwa rafiki wa mumewe waliyekutana JKT. Siku moja, Gilo akiwa ametembelewa na huyu ndugu yake ambaye pia alikuwa mshikaji wake jeshini, alifika rafiki wa mumewe aliyewajua wawili hawa.
Mume aliporejea na kuwakuta wageni hawa, alimtambulisha ndugu mshikaji wa mkewe kama shemeji yake aliyekuwa amempa mtaji kuanzisha biashara. Rafiki yake alishangaa na kuchukia tokana na aliyojua. Hivyo, alishindwa kuvumilia. Wakati wakiagana, alimuomba rafiki yake awe na kifua amwambie jambo. Jamaa alipasua mbarika na kuweka kila kitu wazi. Baada ya kupita miezi kadhaa, jamaa mshikaji wa Gilo alirejea akitaka fedha zaidi toka kwa mumewe ambaye alimkatalia zamu hii. Baada ya mwizi wake kuondoka, alimbana mkewe aliyekiri kuwa na udugu na uhusiano wa kingono. Tangu siku hiyo, mapenzi yalitoweka.
Kuona kitumbua kinaingia mchanga, Gilo alianza harakati za kuhami ndoa yake. Alikwenda kwa wachungaji kuomba ushauri na kuombewa. Mambo yalizidi kuwa mabaya. Mwishowe, aliamua kwenda kwa mganga wa kienyeji aliyemwambia kuwa alikuwa na nuksi na alikuwa amerogwa via vya uzazi na shangazi yake. Hivyo, alipaswa kutumia dawa kuingiza ukeni ili kutibu nuksi. Sharti kubwa alilopewa ni kutafuta mwanaume ambaye si mumewe ajipake dawa na kumuingilia mara moja tu. Kwa kutapatapa na upumbavu, Gilo alikubaliana na sharti. Tatizo, ni nani angempata ajipake hiyo ‘dawa?’
Jibu lilikuwa rahisi. Alimwambia mganga wa kienyeji kuwa hana mtu. Mganga alimwambia kuwa kama angempa fedha, angefanya kazi hiyo. Walikubaliana na Gilo wakajifungia ndani wakafanya ngono. Baada ya kumaliza, mganga wa kienyeji aliongeza sharti jingine kuwa lazima wafanye ngono kwa wiki nzima kila jioni. Gilo alistuka lakini alikuwa ameishaingia mkenge. Alikataa katakata. Mganga kuona hivyo, aliamua kumtishia angemwambia mumewe. Gilo ilibidi akubali. Wakaendelea kufanya mapenzi. Kabla ya wiki kupita, mume alistuka na kuamua kumfuata mkewe pindipo alipoaga jioni anakwenda kwenye maombi. Kimyakimya alimfuata hadi akiingia nyumba ya kulala wageni na mganga. Alifanya harakaharaka akawafuma na kumuacha hapohapo bila hata kurusha ngumi wala tusi.
Katika kushuhudia na baadaye kudurusu sababu za kuvunjika kwa ndoa hii, tuligundua vitu kadhaa. Mosi, ndoa hailazimishwi. Pili, maisha ya kabla ya ndoa yanaaweza kuimarisha, kuyumbisha hata kuvunja ndoa. Tatu, kutokujiamini, ubabaishaji, kutafuta ushauri bila kufikiri na kutahadhari, na kuamini kila ushauri vinaweza kuvunja ndoa. Nne, kutafuta tatizo kwa kutapatapa ni hatari kwa ndoa. Wanadoa wanapaswa kuendana. Kwani, wawili hawa hwakuendana kwa sura na tabia. Japo hili si tatizo, licha ya kulazimisha ndoa, Gilo aligeuka ‘chuma ulete.’ Kwanza, baada ya kuhamia kwa kulazimisha ndoa, Gilo aliwasomba ndugu zake ukiachia kukmtoa fedha mumewe ili kuwatumia wazazi wake kwao. Pili, Gilo, licha ya kumficha mumewe ukweli kuhusiana na maisha yake yaliyosababisha alazimishe ndoa kwa, hakuwa muwazi juu ya maisha yake ya awali.
Je unajifunza nini hapa? Mosi, ndoa inataka uaminifu na ukweli. Pili, siyo kila ushauri unafaa. Tatu, ndoa haina daktari wala mchungaji isipokuwa wanandoa wenyewe. Nne, hakuna siri ya milele. Tano, usiamini kila mtu na kila kitu. Sita, ndoa inataka kujiamini. Saba, waganga wa kienyeji na wachungaji matapeli ni maadui wakubwa wa ndoa. Nane, katika ndoa, wanawake wana maadui wengi kuliko wanaume. Tisa, mchawi au mlinzi wa ndoa yako ni wewe mwenyewe. Kumi, unapopta tatizo, tumia njia sahihi ukiwa umetulia kufikiri na kufanya utatifiti ukiepuka kufanya maamuzi kwa msongo wa mawazo na hofu.
Baada ya kuishi na mumewe kwa mwaka mmoja na kulazimisha kubeba mimba bila ya makubaliano, jambo ambalo lililomstua muwe, Gilo aliamini mumewe bwege asiyeweza kustuka wala kushuku. Hivyo, mazabe yake yasingefumka. Taratibu, mambo yalianza kutifuka na kufumka. Mumewe alianza kumshuku kwa kila jambo. Mfano, kuna wanaume waliokuwa wakiwatembelea aliowatambulisha kama ndugu zake. Bahati mbaya, mmojawapo alikuwa akifahamika kwa rafiki wa mumewe waliyekutana JKT. Siku moja, Gilo akiwa ametembelewa na huyu ndugu yake ambaye pia alikuwa mshikaji wake jeshini, alifika rafiki wa mumewe aliyewajua wawili hawa.
Mume aliporejea na kuwakuta wageni hawa, alimtambulisha ndugu mshikaji wa mkewe kama shemeji yake aliyekuwa amempa mtaji kuanzisha biashara. Rafiki yake alishangaa na kuchukia tokana na aliyojua. Hivyo, alishindwa kuvumilia. Wakati wakiagana, alimuomba rafiki yake awe na kifua amwambie jambo. Jamaa alipasua mbarika na kuweka kila kitu wazi. Baada ya kupita miezi kadhaa, jamaa mshikaji wa Gilo alirejea akitaka fedha zaidi toka kwa mumewe ambaye alimkatalia zamu hii. Baada ya mwizi wake kuondoka, alimbana mkewe aliyekiri kuwa na udugu na uhusiano wa kingono. Tangu siku hiyo, mapenzi yalitoweka.
Kuona kitumbua kinaingia mchanga, Gilo alianza harakati za kuhami ndoa yake. Alikwenda kwa wachungaji kuomba ushauri na kuombewa. Mambo yalizidi kuwa mabaya. Mwishowe, aliamua kwenda kwa mganga wa kienyeji aliyemwambia kuwa alikuwa na nuksi na alikuwa amerogwa via vya uzazi na shangazi yake. Hivyo, alipaswa kutumia dawa kuingiza ukeni ili kutibu nuksi. Sharti kubwa alilopewa ni kutafuta mwanaume ambaye si mumewe ajipake dawa na kumuingilia mara moja tu. Kwa kutapatapa na upumbavu, Gilo alikubaliana na sharti. Tatizo, ni nani angempata ajipake hiyo ‘dawa?’
Jibu lilikuwa rahisi. Alimwambia mganga wa kienyeji kuwa hana mtu. Mganga alimwambia kuwa kama angempa fedha, angefanya kazi hiyo. Walikubaliana na Gilo wakajifungia ndani wakafanya ngono. Baada ya kumaliza, mganga wa kienyeji aliongeza sharti jingine kuwa lazima wafanye ngono kwa wiki nzima kila jioni. Gilo alistuka lakini alikuwa ameishaingia mkenge. Alikataa katakata. Mganga kuona hivyo, aliamua kumtishia angemwambia mumewe. Gilo ilibidi akubali. Wakaendelea kufanya mapenzi. Kabla ya wiki kupita, mume alistuka na kuamua kumfuata mkewe pindipo alipoaga jioni anakwenda kwenye maombi. Kimyakimya alimfuata hadi akiingia nyumba ya kulala wageni na mganga. Alifanya harakaharaka akawafuma na kumuacha hapohapo bila hata kurusha ngumi wala tusi.
Katika kushuhudia na baadaye kudurusu sababu za kuvunjika kwa ndoa hii, tuligundua vitu kadhaa. Mosi, ndoa hailazimishwi. Pili, maisha ya kabla ya ndoa yanaaweza kuimarisha, kuyumbisha hata kuvunja ndoa. Tatu, kutokujiamini, ubabaishaji, kutafuta ushauri bila kufikiri na kutahadhari, na kuamini kila ushauri vinaweza kuvunja ndoa. Nne, kutafuta tatizo kwa kutapatapa ni hatari kwa ndoa. Wanadoa wanapaswa kuendana. Kwani, wawili hawa hwakuendana kwa sura na tabia. Japo hili si tatizo, licha ya kulazimisha ndoa, Gilo aligeuka ‘chuma ulete.’ Kwanza, baada ya kuhamia kwa kulazimisha ndoa, Gilo aliwasomba ndugu zake ukiachia kukmtoa fedha mumewe ili kuwatumia wazazi wake kwao. Pili, Gilo, licha ya kumficha mumewe ukweli kuhusiana na maisha yake yaliyosababisha alazimishe ndoa kwa, hakuwa muwazi juu ya maisha yake ya awali.
Je unajifunza nini hapa? Mosi, ndoa inataka uaminifu na ukweli. Pili, siyo kila ushauri unafaa. Tatu, ndoa haina daktari wala mchungaji isipokuwa wanandoa wenyewe. Nne, hakuna siri ya milele. Tano, usiamini kila mtu na kila kitu. Sita, ndoa inataka kujiamini. Saba, waganga wa kienyeji na wachungaji matapeli ni maadui wakubwa wa ndoa. Nane, katika ndoa, wanawake wana maadui wengi kuliko wanaume. Tisa, mchawi au mlinzi wa ndoa yako ni wewe mwenyewe. Kumi, unapopta tatizo, tumia njia sahihi ukiwa umetulia kufikiri na kufanya utatifiti ukiepuka kufanya maamuzi kwa msongo wa mawazo na hofu.
Chanzo: Mwananchi leo.