Kwanza, nawasalimia kabla kuwafyatua lau mfyatuke muwafyatue waliofyatua hadi mkakufyatuliwa na shida mkakimbilia kwa Tarampu aliyefyatuka na kuwafyatua. Nilimwandikia barua. Hajanijibu. Pili, niwajuze. Fyatu niko poa. Najua. Wengi wameniandikia barua mapepe kwa mapepe wakinisikitikia kuwa nitarejea na pingu miguuni na mikononi baada ya Tarampu kufyatuka na kufyatua. Wapo pia wanaoomba nirejeshwe lau wanikoge hasa wale walionibomu nikawachunia. Kadhalika, wapo wanaonionea huruma kuwa nikifyatuliwa na kutua na nitafyatuliwa na ukapuku na mifupo jizi nisiyozoea. Hawa ni nilikuwa nikiwatumia njuluku kidogo mbali na kuwapa moyo kuwa kuna siku ningewasukia waje majuu kutesa wasijue unaweza kuja ukaishia kuteseka.
Tatu, wapo niliowafyatua hasa wanene wanaotamani nishuke kwenye pipa na pingu nao wanifyatue kuelekea lupango. Hafyatuliwi fyatu vinginevyo nitake. Kwanza, siishi kwa Joji Kichaka mbali na kuwa, hata nikipewa green card, nitaichana. Nani aishi kwenye kaya inayofyatuliwa na kichaa mbaguzi japo ana pwenti?
Tatu, wapo niliowafyatua hasa wanene wanaotamani nishuke kwenye pipa na pingu nao wanifyatue kuelekea lupango. Hafyatuliwi fyatu vinginevyo nitake. Kwanza, siishi kwa Joji Kichaka mbali na kuwa, hata nikipewa green card, nitaichana. Nani aishi kwenye kaya inayofyatuliwa na kichaa mbaguzi japo ana pwenti?
Nije kwenye inshu. Kwanza, nawashauri watakaofyatuliwa na kurejeshwa na pingu wasikonde na kusononeka. Afrika ina fursa bwererere. Kwa yeyote aliyeishi ughaibuni, kama hazioni, ajue anajifyatua au kujifyatulisha mwenyewe. Najua mifumo yetu ya kikale na kirushwa. Ukikomaa unatoboa. Hivyo, nendeni mkachafyatukie fursa ilmradi msijiingize kwenye siasa za majitaka mkaambiwa mna uraia pacha japo hamna. Pili, nawashauri. Mkishafyatuliwa na kurejea home, fyatueni wanaowafyatua. Anzeni mandingo kuonyesha namna exposure yenu ilivyowakomaza hadi mkang’ang’ania ughaibuni.
Tatu, nawashauri msirudie kosa kudhani kuwa ughaibuni kuna barabara za dhahabu na pepo. Nne, mbali na ubaguzi aliionyesha Tarampu na wengine kama yeye wanaozidi kuchepuka huko Ulaya, mjue adui yenu yuko home siyo ughaibuni.
Tano, mjiulize hasa wale waliokimbia ukapuku, ilikuwaje mfyatuliwa na kugeuka makapuku kwenye bara lenye utajiri chekwa? Je tatizo ni wanaowafyatua mlowatengeza wenyewe mkashindwa kuwafyatua au nyinyi? Je mmejipanga vipi kuwaelimisha mafyatu juu ya kuwafyatua mafyatu wanene wanaofyatua hadi ukapuku ukawafyatua mkakimbilia ughaibuni bila kuwafyatua?
Sita, hakuna kitu hunichanganya kama sirkal kuhangaika na namna ya kufyatua njuluku toka ughaibuni wakati haina mpango wowote wa kuwasaidia mnapofyatuliwa kama kaya nyingine zilivyofanya kwa mafyatu wao waliofyatuliwa na Tarampu. Sijui hata kama wanajua idadi yenu na mahali mlipo.
Saba, mjue, njuluku zinazotafutwa na sirkal husaidia mafyatu wezi wanene kuzifyatua na kupoza machungu yenu kiasi cha kushindwa kuwafyatua. Hivyo, husaidia wawafyatue kirahisi. Sasa Tarampu kafyatuka na kufyatua. Mafyatu fyatukeni mfyatue na kudai haki zenu badala ya kutegemea kukimbilia ughaibuni. Hisani huanzia home mafyatu wangu. Hata Tarampu angewajaza madolari na kumkatuma home, wezi wanene wangeyafyatua mkaendelea kuwa makapuku pamoja na kubeba moboksi usiku na mchana.
Kwa wale kama mimi wasio na wasi wasi wa kufyatuliwa wala kulazimika kuchukua uraia kwa sababu uraia pacha ni dhambi kayani, nendeni shule mkafyatue mambo ya maana ili mkirejea lau muwe na nyenzo za kufyatua njuluku kihalali. Mnadhani nisingefyatua shule ningepewa na kuaminiwa uga wa kufyatua ninayo fyatua tena kifyatu bila kuogopa hata mhariri wangu. Sorry. Nimesemaje? Mezea hiyo kama nimekukwaza bosi wangu. Nilizidisha kanywaji na chigala kubwa.
Najua. Wengi hawatapenda ufyatuzi huu hasa wale wanaowafyatua mafyatu waliogoma kuwafyatuka na kuwafyatua. Kimsingi, Tarampu anatufundisha somo la kujitegemea, kufyatuana, kutokuwa wavivu, kujiheshimu, kutenda na kutendeana haki, na uwajibikaji wa pamoja kama mafyatu tuwe wakubwa hata wadogo. Kwa wanaomkumbuka jembe Joni Kanywaji, alitufundisha kuwa tukifyatuka na kuamua kufyatua mambo, tunaweza. Japo fyatu huyu alikuwa na madhaifu yake, angalau alikuwa na uthubutu wa kifyatu.
Hivyo, badala ya kumchukia na kumshutumu Tarampu, tumshukuru kwa kutukumbusha kuwa mikono na vichwa vyetu si mapambo. Licha ya kutufundisha kwa masimango, Tarampu ameonyesha asivyo mnafiki wala muongo kama wengi waliomtangulia waliokuwa wakitumia misaada ya kuacha mafyatu wetu ughaibuni kama njia ya kutufyatua ili tuwe tegemezi na kufyatuliwa. Ametufundisha kufagia nyumba zetu ili tuwe wasafi japo kiuchumi.
Mnajua siri ya ughaibuni kutuzidi katika kila kitu? Simpo. Kila fyatu huku ni fyatu kweli kweli anayefyatuka na kufyatua bila kuruhusu kufyatuliwa na fyatu yoyote awe na madaraka au la. Huku, mfano, huwezi kufunga rodi kupisha walaji wengi wao wasiolipa kodi bali kuifyatua mbali na kaya kapuku kutoa misaada ukiachia mbali kuingia uwekezaji uliogeuka uchukuaji na ufyatuaji mali na njuluku za mafyatu.
Mwisho, kwa mafyatu walionusurika kufyatuliwa, popote mlipo, gomeni kutuma njuluku hadi mjue haki zenu home. Mfano, muwambie wanaotaka kufyatua au kutegemea njuluku zenu wajenge mazingira yaliyowezesha kaya kama pale kwa jirani kuingiza mabilioni ya dolari. Lazima mjue mna usalama gani mkiwekeza badala ya kufyatuliwa na hadhi sijui maalumu. Nimesemaje? Ngoja nikajifiche wasininyake wakanitia pingu na kunipakiza kwenye pipa bure!
Chanzo: Mwananchi leo.
No comments:
Post a Comment