Juzi, nilifyatuka nusu kufyatua mkumbaff mmoja. Si nilisikia mfugo–––tena mkubwa tu–––unaopayuka kuliko hata aliyeufuga. Ulidai eti mafyatu wanaoishi ghaibu wanafugwa kama wenyewe. Nani, vipi, na kwanini? Huko, hawali dezo kama huu. Hawapigi, hawababaishi, wala kuongopa. Hakuna usanii, uchawa, ufunza, au ukunguni. Unawaita mafyatu waanimo kwa vile wewe ni muanimo? Nani afugwe iwe home au kisiasa?
Ughaibuni, mafyatu wanabeba maboksi, kulipa kodi, kutuma dolari home. Hawapigi kodi za mafyatu. Hawakopikopi wala kubomubomu wala kupiga wapewacho. Hawashirikiani na wachukuaji waitwao wawekaji. Pia, hawana uchumi wanaoukalia kama mifugo inayowashutumu kuwa mifugo wakati si mifugo wa yeyote kama hii inayoibia mafyatu na kuwatumia kubomu na kupiga.
Ughaibuni, hakuna ulevi wa maulaji ya dezo. Kule kuna uchapakazi na uwajibikaji. Hakuna mifugo, wadudu, wala ulevi zaidi ya kupiga mzigo. Kama mafyatu wa ughaibuni ni mifugo, mbona wanawafuga mafyatu wa kayani hadi hao wanaoshiba na kunonihino kwa midomo wanawashawishi wawekeze kaya? Tangu lini aliyefugwa akafuga mbwa? Kuweni na aibu jamani.
Kaya jirani, mafyatu wa ughaibuni wanaenziwa kama kuku watagao mayai ya dhahabu. Kwani, wanaingiza mamilioni ya dolari kwa kuwekeza au kuwatumia jamaa zao. Fyatuland, wanachukiwa hadi kuitwa mifugo ilhali wanaogopewa wasichukue fursa za walevi wa maulaji wasio na ubunifu wala ithibati na kujiamini kupambana nao kishua. Kwani, hatujui?
Ughaibuni, hakuna ulevi wa maulaji ya dezo. Kule kuna uchapakazi na uwajibikaji. Hakuna mifugo, wadudu, wala ulevi zaidi ya kupiga mzigo. Kama mafyatu wa ughaibuni ni mifugo, mbona wanawafuga mafyatu wa kayani hadi hao wanaoshiba na kunonihino kwa midomo wanawashawishi wawekeze kaya? Tangu lini aliyefugwa akafuga mbwa? Kuweni na aibu jamani.
Kaya jirani, mafyatu wa ughaibuni wanaenziwa kama kuku watagao mayai ya dhahabu. Kwani, wanaingiza mamilioni ya dolari kwa kuwekeza au kuwatumia jamaa zao. Fyatuland, wanachukiwa hadi kuitwa mifugo ilhali wanaogopewa wasichukue fursa za walevi wa maulaji wasio na ubunifu wala ithibati na kujiamini kupambana nao kishua. Kwani, hatujui?
Unapoongea na mafyatu, ujikumbushe au kukumbushwa kuwa wana akili tena timamu na kubwa kuliko hata zako. Wengine ni wabukuzi wa kweli na mahiri kuliko hawa wa kuungaunga. Ughaibuni usishangae kuona mzoa taka akitinga kibaruani na ndinga kama mnene wa uswekini. Huko, kazi ni kazi si kuchagua kazi. Pia, hakuna ving’ora uchwara vya kujipendelea.
Huwashangaa sana mafyatu wa hovyo wafugwao. Ukimpa doshi, anakuita mafadhili. Ukimfyatua ukamkosoa anavyofyatua na kutumia vibaya msaada ulichompa, anakuita beberu! Ebo! Tujitofautishe na mbuzi jike? Ukifugwa, usijidanganye kudhani wenzio wanafugwa. Ukiwa zwazwa, usidhani wenzio mazwazwa. Kama siyo Tunda Lishe, wengine sijui hata kama wangekanyaga hapo wanapopanonihino na kukufuria wasijue kacheo ni dhamana au koti mwilini.
Heri mafyatu waishio ughaibuni wanaoweza kulisha mafyatu wa kayani kuliko wapigaji waishio kwenye mabega, migongo yao, wakiwatumia kubomubomu. Ukiwauliza kwanini wanaishi bure wakati wanaowatukana ndiyo wanaowalipia kuanzia kula, home, michuma, mishahara, marupurupu, na hata hizo nguo wanazovaa, hawana jibu. Watakuita majina mabaya.
Huwashangaa sana mafyatu wa hovyo wafugwao. Ukimpa doshi, anakuita mafadhili. Ukimfyatua ukamkosoa anavyofyatua na kutumia vibaya msaada ulichompa, anakuita beberu! Ebo! Tujitofautishe na mbuzi jike? Ukifugwa, usijidanganye kudhani wenzio wanafugwa. Ukiwa zwazwa, usidhani wenzio mazwazwa. Kama siyo Tunda Lishe, wengine sijui hata kama wangekanyaga hapo wanapopanonihino na kukufuria wasijue kacheo ni dhamana au koti mwilini.
Heri mafyatu waishio ughaibuni wanaoweza kulisha mafyatu wa kayani kuliko wapigaji waishio kwenye mabega, migongo yao, wakiwatumia kubomubomu. Ukiwauliza kwanini wanaishi bure wakati wanaowatukana ndiyo wanaowalipia kuanzia kula, home, michuma, mishahara, marupurupu, na hata hizo nguo wanazovaa, hawana jibu. Watakuita majina mabaya.
Hakuna kilichonisitisha na kunifyatua hadi kufyatuka kama kugundua kuwa huyu zwazwa mkubwa aliyefyatua haya eti aitwa mbukuzi. Kabukua nini? Fyatu lenyewe tena lililoghushi linawatukana mafyatu wetu mashujaa wanaotuwakilisha ghaibuni? Kwani, mafisi na mafisadi wote wanaishi aka kufugwa wako ughaibu? Mbukuzi gani anayejumuisha mambo badala ya kuwa sceintific and specific? Tumuiteje zaidi ya zwazwa?!!
Kisa tajwa kilinikumbusha namna mafyatu walivyonizodoa nikajiona zwazwa tena mfugo. Si waliishiwa ma-water. Nami, kutaka kuwafunga kamba si nikafyatuka na kupayuka kuwa tatizo ni tabia kaya. Baada ya Fyatuland kukumbwa na ukame, si, kwa uzwazwa na ubukuzi wa kuungaunga, nikafyatuka na kupayuka kuwa hili ni tatizo la dunia nzima. Kabla ya kuendelea, bi mkubwa mama Mfyatuko, alinijongelea na kuniuma sikio “dear, mbona Asia kuna mafuriko au na Fyatuland iko huko?” Lol. Si niliaibika. Kama fyatu zwazwa tajwa hapo juu, nami niliwalaumu mifugo kwa kufuga na kufunga akili zangu hadi nikapayuka kizwazwa. Mwenzenu niliaibika japo nilijitoa ufahamu na kujifanya hamnazo na kuendelea kuronga.
Nimegundua kitu. Kumbe na ulaji wa dezo unalevya na kufyatua hadi fyatu mzima unafyatuka kama chizi au shehetani wa kufyatua vichwa! Juzi, fyatu mmoja kaniomba lift. Kwa kujiamini, nilimuuliza inakuwaje hana ndinga wakati zimejaa barabarani. Uzuri, huyu fyatu hakunifyatukia wala kujibu kifyatu wala kilevi kama huu mfugo. Alinidharau na kuuchuna.
Siku nyingine, mafyatu walilalamikia ufyatuaji wangu na wafyatuaji wenzangu. Badala ya kuwapa majibu yanayoingia akilini si niliwaambia kuwa huu ni mchezo uliokuwa umeandaliwa na kuchezwa ghaibu! Wakati nifyatuka hivi, si fyatu mmoja akafyatuka na kunitolea uvivu na kuuliza “hivi mkuu huwa kinywa na mlomo wako vina mawasiliano au ugomvi?” Nilimuuliza alikuwa akimaanisha nini. Alijibu kuwa, kila nikironga huwa anaona kama kuna mgongano baina ya viungo hivi vya mwili mmoja.
Kuna mwanafalsa mmoja maarufu aliyetangulia mbele ya haki. Alituasa kuwa unapochonga, ubakize akiba kwa vile hujui ya kesho. Tuliwaona mafyatu wangapi wenye vichwa na vifua tena vya haja? Walikuwapo akina Mkwavinyika Muyigumba Wamuyinga almaaruf Mkwawa, Mtyela Kasanda aka Milambo, Nyungu ya Mawe, mzee Nchonga, Jiwe, na wengine. Wako wapi?
Nimalize kwa kuwasihi wote.
Kisa tajwa kilinikumbusha namna mafyatu walivyonizodoa nikajiona zwazwa tena mfugo. Si waliishiwa ma-water. Nami, kutaka kuwafunga kamba si nikafyatuka na kupayuka kuwa tatizo ni tabia kaya. Baada ya Fyatuland kukumbwa na ukame, si, kwa uzwazwa na ubukuzi wa kuungaunga, nikafyatuka na kupayuka kuwa hili ni tatizo la dunia nzima. Kabla ya kuendelea, bi mkubwa mama Mfyatuko, alinijongelea na kuniuma sikio “dear, mbona Asia kuna mafuriko au na Fyatuland iko huko?” Lol. Si niliaibika. Kama fyatu zwazwa tajwa hapo juu, nami niliwalaumu mifugo kwa kufuga na kufunga akili zangu hadi nikapayuka kizwazwa. Mwenzenu niliaibika japo nilijitoa ufahamu na kujifanya hamnazo na kuendelea kuronga.
Nimegundua kitu. Kumbe na ulaji wa dezo unalevya na kufyatua hadi fyatu mzima unafyatuka kama chizi au shehetani wa kufyatua vichwa! Juzi, fyatu mmoja kaniomba lift. Kwa kujiamini, nilimuuliza inakuwaje hana ndinga wakati zimejaa barabarani. Uzuri, huyu fyatu hakunifyatukia wala kujibu kifyatu wala kilevi kama huu mfugo. Alinidharau na kuuchuna.
Siku nyingine, mafyatu walilalamikia ufyatuaji wangu na wafyatuaji wenzangu. Badala ya kuwapa majibu yanayoingia akilini si niliwaambia kuwa huu ni mchezo uliokuwa umeandaliwa na kuchezwa ghaibu! Wakati nifyatuka hivi, si fyatu mmoja akafyatuka na kunitolea uvivu na kuuliza “hivi mkuu huwa kinywa na mlomo wako vina mawasiliano au ugomvi?” Nilimuuliza alikuwa akimaanisha nini. Alijibu kuwa, kila nikironga huwa anaona kama kuna mgongano baina ya viungo hivi vya mwili mmoja.
Kuna mwanafalsa mmoja maarufu aliyetangulia mbele ya haki. Alituasa kuwa unapochonga, ubakize akiba kwa vile hujui ya kesho. Tuliwaona mafyatu wangapi wenye vichwa na vifua tena vya haja? Walikuwapo akina Mkwavinyika Muyigumba Wamuyinga almaaruf Mkwawa, Mtyela Kasanda aka Milambo, Nyungu ya Mawe, mzee Nchonga, Jiwe, na wengine. Wako wapi?
Nimalize kwa kuwasihi wote.
Tuache madharau. Fikiri na jisikilize kabla ya kupayuka. Mbona tunajitoa ufahamu na kuwa na kiherere wakati ni jana tu tulikuwa na Mwamba Jiwe. Yuko wapi? Ama kweli, simba akifa, usishangae panya kula ngozi yake au walevi kukojolea makaburi ya watakatifu. Ulevi si kanywaji tu. Hata msosi, tena wa dezo, unalewesha. Kweli, hujafa, hujaumbika. Nani alitegemea wala kuwazia kuyashuhudia haya? Kuna haja ya kuheshimiana. Kwani, hewala si utumwa.
Chanzo: Mwananchi J'tano leo.
Chanzo: Mwananchi J'tano leo.