Kwa ndugu zangu wapendwa mliofyatuliwa,
Nawakumbuka sana nisameheni bure. Nawakumbuka akina Ali Kibaooo, Mdudu Nyangarika, Hamp Slowslow, Saa Eight et al. Naomba mzingatie haya. Kama mko hai, mtafurahi na kufarijika kuwa bado mnakumbukwa. Kama mshafyatuliwa, wapendwa wenu watayasoma na kuyahifadhi kwa ajili yenu. Nisameheni kuchelewa kuwasiiana nanyi.
Pia, niweka wazi. Nalaani jinai, unyama, na ukatili wa kutekana, kupotezana na kuuana. Japo wapo wanaofanya hivi kwa kisingizio cha kulinda kaya, kaya hailindwi kwa baadhi ya mafyatu kuwafyatua wenzao kana kwamba wao ndiyo wana hati milki ya kaya. Jinai hii ni mbaya kuliko unyama hata ushetani. Lazima tuilaani na kupiga vita hadi tuitokomeze kabla haijaangamiza kaya.
Kwa wanaongamiza wenzao tena kulinda madhambi na tamaa vyao wanapaswa waambiwe. Nao watakufa hata kama siyo leo. Wenzetu wanatucheka na kutushangaa tulivyo makatili na hayawani. Hatuwezi kuwa kaya huru lakini baadhi wakanyang’anywa HAKI ya kuishi. Hatuwezi kuwa huru ilhali huvumilii maoni na mawazo yanayopingana na yako. Tushindane kwa hoja na si viroja na unyama jamanini.
Kwa waliofyatuliwa, kupotezwa, na kunyotolewa roho, siku nyingi zimepita tangu mfyatuliwe baada ya kufyatua na kutishia kuwafyatu waliowafyatua na kuendelea kutufyatua mafyatu wasiofyatuka wakafyatua hadi wakawa siku zote wanafyatuliwa kirejareja tena na mazwazwa. Najua. Familia zetu zinaumia na kuteseka kwa sababu ya unyama wa mafyatu wachache wanaotenda kama vile wataishi milele. Kila kitu tunakikuta na tutakiacha. Hata uteke, upote na uue namna gani, hutamaliza mafyatu. Wengine watazaliwa na kukupinga tu. Hata ujihadae vipi, kuondoa uhai wa fyatu mwenzako utakuandamana na ukose amani na raha hata ufiche au kujifanya hayakuhusu vipi. Akina Hitler, Amin, Mussolini, Pol Pot na manyang’au wengine walifyatu mafyatu kwa mamilioni. Wako wapi?
Kwa wahanga, msikonde. Sir God anawaona watesi wenu. Japo siku hizi HAKI ni machukizo kwa baadhi ya wenzetu, kuna siku siku HAKI itatendeke. Kama Sir God ataahirisha kuwafyatua, atatuliza tu ila si kuzuia. Zao zaja. Kwani, damu yenu itaamka na kulipiza kisasi kama si kwao, basi, kwa vizazi vyao. Kwa taaluma na uzoefu wangu kama profesa emeritus, wote waliojifyatua akili nao roho zao haziko sawa. Wanaungua bila kusema wala kunung’unika waziwazi.
Nawakumbuka sana nisameheni bure. Nawakumbuka akina Ali Kibaooo, Mdudu Nyangarika, Hamp Slowslow, Saa Eight et al. Naomba mzingatie haya. Kama mko hai, mtafurahi na kufarijika kuwa bado mnakumbukwa. Kama mshafyatuliwa, wapendwa wenu watayasoma na kuyahifadhi kwa ajili yenu. Nisameheni kuchelewa kuwasiiana nanyi.
Pia, niweka wazi. Nalaani jinai, unyama, na ukatili wa kutekana, kupotezana na kuuana. Japo wapo wanaofanya hivi kwa kisingizio cha kulinda kaya, kaya hailindwi kwa baadhi ya mafyatu kuwafyatua wenzao kana kwamba wao ndiyo wana hati milki ya kaya. Jinai hii ni mbaya kuliko unyama hata ushetani. Lazima tuilaani na kupiga vita hadi tuitokomeze kabla haijaangamiza kaya.
Kwa wanaongamiza wenzao tena kulinda madhambi na tamaa vyao wanapaswa waambiwe. Nao watakufa hata kama siyo leo. Wenzetu wanatucheka na kutushangaa tulivyo makatili na hayawani. Hatuwezi kuwa kaya huru lakini baadhi wakanyang’anywa HAKI ya kuishi. Hatuwezi kuwa huru ilhali huvumilii maoni na mawazo yanayopingana na yako. Tushindane kwa hoja na si viroja na unyama jamanini.
Kwa waliofyatuliwa, kupotezwa, na kunyotolewa roho, siku nyingi zimepita tangu mfyatuliwe baada ya kufyatua na kutishia kuwafyatu waliowafyatua na kuendelea kutufyatua mafyatu wasiofyatuka wakafyatua hadi wakawa siku zote wanafyatuliwa kirejareja tena na mazwazwa. Najua. Familia zetu zinaumia na kuteseka kwa sababu ya unyama wa mafyatu wachache wanaotenda kama vile wataishi milele. Kila kitu tunakikuta na tutakiacha. Hata uteke, upote na uue namna gani, hutamaliza mafyatu. Wengine watazaliwa na kukupinga tu. Hata ujihadae vipi, kuondoa uhai wa fyatu mwenzako utakuandamana na ukose amani na raha hata ufiche au kujifanya hayakuhusu vipi. Akina Hitler, Amin, Mussolini, Pol Pot na manyang’au wengine walifyatu mafyatu kwa mamilioni. Wako wapi?
Kwa wahanga, msikonde. Sir God anawaona watesi wenu. Japo siku hizi HAKI ni machukizo kwa baadhi ya wenzetu, kuna siku siku HAKI itatendeke. Kama Sir God ataahirisha kuwafyatua, atatuliza tu ila si kuzuia. Zao zaja. Kwani, damu yenu itaamka na kulipiza kisasi kama si kwao, basi, kwa vizazi vyao. Kwa taaluma na uzoefu wangu kama profesa emeritus, wote waliojifyatua akili nao roho zao haziko sawa. Wanaungua bila kusema wala kunung’unika waziwazi.
Nyuma ya pazia, wanaungua na kuumia. Kuna moto unawachoma taratibu. Mateso yao hayapimiki. Wanaishi kwa hofu na wasi wasi.
Wapendwa, hamjasahaulika wala kupuuziwa. Mko, na daima mtakuwa, mioyoni mwetu kama mashujaa. Hamtasahaulika daima. Nani chizi awasahau au kujifanya hamkufyatuliwa? Japo hawapo wanaojitoa ufahamu na kutetea vitu badala ya ufyatu, niaminini. Hawatakaa waionje hiyo amani mawenge na uchwara wasingiziayo. Nahisi hasira na uchungu ninaposikia wadudu wakitaka kuhadaa mafyatu.
Yupo huyu mwehu aliyeko juu aitwaye Mkumbokumbo anayetaka mafyatu wafuate mkumbo na kuamini urongo na uzwazwa wake. Anadai mafyatu wanachukiwa kwa sababu ya ukwasi wao! Ukwasi upi na tangia lini? Nani anafaidi huu ukwasi uchwara ugawiwao kwa wenye akili tena kwa hongo za peremende?
Wamejua kututenda. Wamelikoroga, halafu wanadai tatizo si wao japo ni wao ila maadui wa kufikirika toka ghaibu! Ni uzwazwa kiasi gani? Hao wanaoshutumiwa kuwahonga njuluku mabarubaru aka mabeberu walianza lini kuwa maadui ilhali, siku zote, wamekuwa wakifadhili mafyatu hadi tukawaita wafadhili? Wakimwga njuluku zikapigwa bila kuhoji, wanaitwa wafadhili. Kama kweli ni mabeberu, inakuwaje nasikia umbea kuwa kuna jitihada za kutafuta washawishi na wapiga chapuo wawashawishi wasamehe mipayuko yenu? Kuna haja mafyatu wazima tuache utoto. Tuamue kusema ukweli. Haiwezekani wafadhili wetu wageuke mabeberu leo siyo jana.
Huwa sipendi kigeugeu na urushi. Kwanini wawe wafadhili wakinyamaza? Ajabu, wakifyatuka na kustukia gemu wakahoji, tunawaita mabeberu. Nani mabeberu kati ya wao na wale warongo, wabangaizaji, na wasanii watapatapao. Kama ubeberu ni jinai, waliofyatua mafyatu wetu ndiyo mabeberu. Uzuri wa ‘mabeberu’ hawauia wala kuibia mafyatu wao. Isistoshe, sisi siyo mbuzi majike? Kwa mafyatu, mabeberu si tishio. Wakija, tunawachinja na kuwageuza kitoweo saaafi kama kweli wapo.
Huwa nashangaa sana mabeberu wanapoiwaita washitili wao mabeberu wakati mabeberu ni wao. Kama ubeberu ni kosa, mabeberu tunao Fyatuland wakitubeberu wakisingizia mabeberu wa kufikirika. Fyatu nakataa kata kata. Beberu gani anaweza kufyatua mafyatu tena wanaofyatuliwa kwa kuishi kwa kula ugali kwa pilipili? Kazi ya beberu ni kuzalisha majike na si kuua wana mbuzi. Kama kweli kuna mabeberu, wakija, wakamateni, wachinjeni lau tuondokane na ukame wa kukosa kiteweo. Chonde chonde waonye mabeberu. Mafyatu tutawafyatua na kuwageuza kitoweo.
Kama kweli maadui wa mafyatu ni mabeberu ninaowajua, hawana haja ya kulalamika bali kuwakamata na kuwafyatua. Kama si hao bali wao hao wanaodai kuna mabeberu wakati wao ndiyo wao hao, tuache kufyatuana kirejareja. Tuambizane ukweli na kuacha kujitoa ufahamu kwa kiherehere kama yule jamaa mbayuwayu.
Wapendwa, hamjasahaulika wala kupuuziwa. Mko, na daima mtakuwa, mioyoni mwetu kama mashujaa. Hamtasahaulika daima. Nani chizi awasahau au kujifanya hamkufyatuliwa? Japo hawapo wanaojitoa ufahamu na kutetea vitu badala ya ufyatu, niaminini. Hawatakaa waionje hiyo amani mawenge na uchwara wasingiziayo. Nahisi hasira na uchungu ninaposikia wadudu wakitaka kuhadaa mafyatu.
Yupo huyu mwehu aliyeko juu aitwaye Mkumbokumbo anayetaka mafyatu wafuate mkumbo na kuamini urongo na uzwazwa wake. Anadai mafyatu wanachukiwa kwa sababu ya ukwasi wao! Ukwasi upi na tangia lini? Nani anafaidi huu ukwasi uchwara ugawiwao kwa wenye akili tena kwa hongo za peremende?
Wamejua kututenda. Wamelikoroga, halafu wanadai tatizo si wao japo ni wao ila maadui wa kufikirika toka ghaibu! Ni uzwazwa kiasi gani? Hao wanaoshutumiwa kuwahonga njuluku mabarubaru aka mabeberu walianza lini kuwa maadui ilhali, siku zote, wamekuwa wakifadhili mafyatu hadi tukawaita wafadhili? Wakimwga njuluku zikapigwa bila kuhoji, wanaitwa wafadhili. Kama kweli ni mabeberu, inakuwaje nasikia umbea kuwa kuna jitihada za kutafuta washawishi na wapiga chapuo wawashawishi wasamehe mipayuko yenu? Kuna haja mafyatu wazima tuache utoto. Tuamue kusema ukweli. Haiwezekani wafadhili wetu wageuke mabeberu leo siyo jana.
Huwa sipendi kigeugeu na urushi. Kwanini wawe wafadhili wakinyamaza? Ajabu, wakifyatuka na kustukia gemu wakahoji, tunawaita mabeberu. Nani mabeberu kati ya wao na wale warongo, wabangaizaji, na wasanii watapatapao. Kama ubeberu ni jinai, waliofyatua mafyatu wetu ndiyo mabeberu. Uzuri wa ‘mabeberu’ hawauia wala kuibia mafyatu wao. Isistoshe, sisi siyo mbuzi majike? Kwa mafyatu, mabeberu si tishio. Wakija, tunawachinja na kuwageuza kitoweo saaafi kama kweli wapo.
Huwa nashangaa sana mabeberu wanapoiwaita washitili wao mabeberu wakati mabeberu ni wao. Kama ubeberu ni kosa, mabeberu tunao Fyatuland wakitubeberu wakisingizia mabeberu wa kufikirika. Fyatu nakataa kata kata. Beberu gani anaweza kufyatua mafyatu tena wanaofyatuliwa kwa kuishi kwa kula ugali kwa pilipili? Kazi ya beberu ni kuzalisha majike na si kuua wana mbuzi. Kama kweli kuna mabeberu, wakija, wakamateni, wachinjeni lau tuondokane na ukame wa kukosa kiteweo. Chonde chonde waonye mabeberu. Mafyatu tutawafyatua na kuwageuza kitoweo.
Kama kweli maadui wa mafyatu ni mabeberu ninaowajua, hawana haja ya kulalamika bali kuwakamata na kuwafyatua. Kama si hao bali wao hao wanaodai kuna mabeberu wakati wao ndiyo wao hao, tuache kufyatuana kirejareja. Tuambizane ukweli na kuacha kujitoa ufahamu kwa kiherehere kama yule jamaa mbayuwayu.
Chanzo: Mwananchi J'tano leo.
No comments:
Post a Comment