The Chant of Savant

Thursday 8 December 2011

Wanaopenda kupeleka watoto kusoma Kenya na Uganda mmeliwa na soma hapa

Utafiti uliofanyika hivi karibuni umeonyesha kuwa mfumo wa elimu wa Tanzania si mbaya kama wengi wetu wanavyoamini. Katika utafiti uliofanywa kwenye nchi za Afrika Mashariki na Kusini umegundua kuwa Mauritius inaongoza na kufuatiwa na Kenya kwenye Hisabati lakini inazidiwa kwenye kusoma na nchi za Tanzania, Seychelles, Mauritius na Swaziland mtawalia kwenye sanaa za usomaji.
Hivyo, wale wanaofuja watoto na pesa zao kuwapeleka watoto wao Kenya na Uganda wajue wameliwa haswa. Katika utafiti huu nchi za Zambia, Malawi, Namibia, Lesotho na Uganda mtawalia, zimeonyesha kufanya vibaya katika nyanja zote.
Hivyo, tunaweza kuhitimisha tukiwashauri wenye imani mfu kuwa elimu yetu ni mbaya na inazidiwa na ile ya Kenya na Uganda kufikiri upya.
Tuliwahi kuandika kuwa wakenya wengi hupeleka watoto wao Uganda huku watanzania wakipeleka kote Kenya na Uganda. Sasa wahusika mnataka nini zaidi? Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA.

No comments: