The Chant of Savant

Saturday 3 December 2011

Picha za karne kwa Blog hii


Laiti walioko kwenye foleni ya kumfuata Gbagbo wangeangalia picha hii mara kwa mara na kutafakari mara kwa mara. Ni upuuzi kiasi gani kufikiri kama Gbagbo aliyetawaliwa na mkewe asijue anapotoshwa. Nyerere aliwahi kuonya juu ya marais kutawaliwa na wake zao. Yuko wapi mr Clean Ben Mkapa aliyeishia kuwa mr Filth?

Naye mwendazake Muammar Gaddafi alipoambiwa ya Misri na Tunisia yaja alicheka sana na kusema, "Hii ni Libya." Alimaanisha haya hayawezi kumkuta asijue yatamkuta tena baada ya muda mfupi na kwa namna ya kutia aibu na kusikitisha. Tieni akilini wakati tukimaliza mwaka huu.

No comments: